Sina Mgogoro na CHADEMA

Sina Mgogoro na CHADEMA

Joseph Ludovick

JF-Expert Member
Joined
Aug 11, 2013
Posts
382
Reaction score
506
Wakuu,

kwa siku kadhaa nimekuwa nikiandika ushauri na maoni yangu huru kwa chama changu CHADEMA. Yote yamefanyika kwa nia njema na mapenzi makubwa niliyo nayo kwa chama changu. na hakika hata yote mengine yanayotajwa dhidi yangu, yamefanywa nami kwa sababu ya mapenzi na kukilinda chama changu. Sasa wapo baadhi ya watu wameshindwa kuelewa maana ya ushauri na maoni yangu hayo na kwa makosa wameishia kunishambulia tu kiujumla bila kuainisha makosa kwenye hoja zangu.

Baadhi yao, licha ya kuona ukweli kwenye maoni yangu, wakadhani kuna motive behind ambayo ni mbaya, wengine wakaniona nimekuwa insane, wakielezea ninavyojichimbia kaburi. hawa kwa kinyume wanasema kitu cha hatari zaidi kwa chadema kuwa inaweza hata kukolimba, kuchacha watu nk,na wengine baadhi wakiendeleza mitazamo "makengeza" ya kuona kila anayekosoa na kushauri chadema basi ni mamluki na anatumiwa na CCM.

Wapo wengine ambao bila kufuata urari wa hoja wala kufahamu ninachokiongelea wametukana matusi,ama kuchepuka kwenye mada husika na kuingiza mada tofauti kabisa ili kupunguza makali ya ukweli katika maoni yangu. Tena wapo ambao kwa haki kabisa na kwa weledimkubwa wameona mantiki na ukweli wa yale ninayoyaeleza na nia njema niliyo nayo, na mwisho kuna wanaodhani ninatoa maoni na ushauri huu kwa sababu nina mgogoro na chadema.

Kwa kweli WOTE nawashukuru kila mmoja kwa nafasi yake. Niseme tena hapa hadharani kuwa mimi sijawahi kuwa na mgogoro na chadema, na wala sina kinyongo na chama as such.(hii as such, ni muhimu kueleweka vema, kwani ni ontological concept). Na kwa kweli sijawahi kufanya jambo lolote kinyume na katiba,maadili na miongozo ya chama. kwa sababu hiyo, mimi sijawahi kuonywa,wala kupewa karipio wala barua yoyote na chama, sijawahi kupewa adhabu walakusimamishwa/kufutwa uanachama.

Bado ninayo kadi yangu na ninailipia na muhimu zaidi bado naishi misingi na falsafa za chadema. Kwa kuwa viongozi wetu wameongoza maasi ya misingi hii kiasi cha kutoeleweka tena kwa wanachama wetu, hadi chama chetu kuwa sawa na CCM, Nikumbushe tu kwa uchache kuwa tunaamini katika nguvu ya umma, kuchukia ufisadi, uwazi na demokrasia, na kwa kweli tunaamini katika mabadiliko.

Tunapaswa kusema kweli daima hata kama ukweli huo utatuweka matatani. ndivyo hapo kale ilivyokuwa kwa dokta Slaa na Zitto kule bungeni na mwembeyanga tulipotaja orodha ya aibu. tunapaswa kuuchukia ufisadi hata kama unafanyika na viongozi wetu ama chama chetu. mambo kama kufoji risiti za mafuta ili kuiba hela kwenye fungu la mafuta ya magari kama ifanyikavyo na baadhi ya wakurugenzi wetu makao makuu ya chama, ama vitendo kama kujiuzia jengo la mabaraza ya chama na chama kulipa kodi kwa mmiliki ambaye ni afisa wa chama makao makuu, ni ufisadi kama ufisadi mwingine na unapaswa kusemwa bila kujali eti msemaji anakidhalilisha chama, na haya ni kwa uchache.

Kuna wanaopanua midomo humu kuwa chama kilikwisha nitimua,ama kuwa nilishapuuzwa kwa sababu ya matendo niliyofanya. bahati nzuri watu hao ni ama wafagiaji tu wa makao makuu, ama wachumia tumbo waliojazana pale makao makuu, ama ni hawa mashabiki wasioijua chadema kwa ndani lakini wakikariri kila kisemwacho huko bila kuhoji kiasi cha kudhaniwa na watani zetu kuwa tunakunywa viroba au zaidi kwamba sisi ni misukule.

kama chama (as such-ni muhimu kuelewa maana ya neno hili) kimefanya maamuzi tofauti na ufahamu wangu huu, nifahamishwe na watu rasmi ambao tunao humu, na namba zangu za simu wanazo kwani viongozi wa chadema makao makuu, tunawasiliana kila siku, ila huwa hawasemi.iko siku tutaonyesha mawasiliano yetu ya mara kwa mara ili kunyamazishwa wabwekaji wa humu.

Hatimaye, nitaendelea kuipenda chadema kama mwanzo, kuitetea na wapuuzi wote, na kuitenga na kusingiziwa ujinga wowote. nitatumia uwezo na nguvu zangu zote, hadi dakika ya mwisho.ili ikiwa nikiwa hai ama nimekufa historia inikumbuke kama mzalendo wa kweli kwa taifa langu na chama changu. njia hii ni ngumu na wengi wa "vuvuzela" wa chadema licha ya kutoielewa, hawawezi hata kuifuata. kwa sasa waendelee kuniita msaliti, na mamluki.

Baadaye kama taifa letu litaondokana na ukoloni wa CCM, na kama CHADEMA kitaleta kweli utawala wa haki, basi tutakuja kufurahi na kuinuliwa na CHADEMA yenyewe na hawa "Vuvuzela" wa chadema wataimba nyimbo za kutusifu na kusema hatukujua. hofu yangu ni kuwa CHADEMA kinaweza kuja kuwa chama kibaya kuwahi kutawala Afrika. Dalili tumekwishaziona.

Mwl. Ludovick
 
Ludo uko sawa kweli mdogo wangu? Tafuta utulivu na wataalam wa ushauri nasaha wakushauri. Sio kawaida kwa mtu uliyekumbwa na masaibu yote yale umetoka gerezani majuzi na kashafa kibao unakuwa so outgoing. Tuliza akili kwanza ndio ukirudi ukisema unaipenda sijui chadema,sijui unaikosoa ndio utaeleweka. Unalazimisha kuwa somebody wakati we ni nobody na huna madhara yoyote. Nakuonea huruma sana unavyohangaika mara sijui unawasiliana na makao makuu kila siku. Na wasiwasi uchizi unaanza kukuingia. Unajua hata km hayo unayosema unashauri ni kweli sio muda wake kwa sasa kutokana na mazingira yanayokuzunguka. Na hakuna atakayekuchukulia serious hata maadui wa chadema watakupuuza tu. Chama hakina habari na wewe huku unalazimisha kushauri! Tulia kwanza urudi upya polepole. Utakufa kwa kihoro bure. Kwa sasa you are nothing!
 
Hongera kwa ushauri mwanachama mtiifu wa chadema lakini ni kwanini ung'ang'anie kuwa mwana-chadema ili hali wanachadema wenzako kwa matendo na kauli zao hawakutaki.....!
 
Nakushauri wahi Mirembe,kama unabisha rudia kusoma x3!!

Taaluma yako ni Ualimu,Mwalimu gani huwezi hata kupanga haya na mantiki??!! Hata walimu wa voda faster hawapo hivyo,no wonder shule za watoto wa maskini zinazidi kufelisha!!
 
Wakuu,
kwa siku kadhaa nimekuwa nikiandika ushauri na maoni yangu huru kwa chama changu CHADEMA. Yote yamefanyika kwa nia njema na mapenzi makubwa niliyo nayo kwa chama changu. na hakika hata yote mengine yanayotajwa dhidi yangu, yamefanywa nami kwa sababu ya mapenzi na kukilinda chama changu. Sasa wapo baadhi ya watu wameshindwa kuelewa maana ya ushauri na maoni yangu hayo na kwa makosa wameishia kunishambulia tu kiujumla bila kuainisha makosa kwenye hoja zangu. baadhi yao,licha ya kuona ukweli kwenye maoni yangu, wakadhani kuna motive behind ambayo ni mbaya, wengine wakaniona nimekuwa insane, wakielezea ninavyojichimbia kaburi. hawa kwa kinyume wanasema kitu cha hatari zaidi kwa chadema kuwa inaweza hata kukolimba, kuchacha watu nk,na wengine baadhi wakiendeleza mitazamo "makengeza" ya kuona kila anayekosoa na kushauri chadema basi ni mamluki na anatumiwa na CCM.
Wapo wengine ambao bila kufuata urari wa hoja wala kufahamu ninachokiongelea wametukana matusi,ama kuchepuka kwenye mada husika na kuingiza mada tofauti kabisa ili kupunguza makali ya ukweli katika maoni yangu. Tena wapo ambao kwa haki kabisa na kwa weledimkubwa wameona mantiki na ukweli wa yale ninayoyaeleza na nia njema niliyo nayo, na mwisho kuna wanaodhani ninatoa maoni na ushauri huu kwa sababu nina mgogoro na chadema.
Kwa kweli WOTE nawashukuru kila mmoja kwa nafasi yake.
Niseme tena hapa hadharani kuwa mimi sijawahi kuwa na mgogoro na chadema, na wala sina kinyongo na chama as such.(hii as such, ni muhimu kueleweka vema, kwani ni ontological concept). Na kwa kweli sijawahi kufanya jambo lolote kinyume na katiba,maadili na miongozo ya chama. kwa sababu hiyo, mimi sijawahi kuonywa,wala kupewa karipio wala barua yoyote na chama, sijawahi kupewa adhabu wala kusimamishwa/kufutwa uanachama. Bado ninayo kadi yangu na ninailipia na muhimu zaidi bado naishi misingi na falsafa za chadema. Kwa kuwa viongozi wetu wameongoza maasi ya misingi hii kiasi cha kutoeleweka tena kwa wanachama wetu, hadi chama chetu kuwa sawa na CCM, Nikumbushe tu kwa uchache kuwa tunaamini katika nguvu ya umma, kuchukia ufisadi, uwazi na demokrasia, na kwa kweli tunaamini katika mabadiliko.
Tunapaswa kusema kweli daima hata kama ukweli huo utatuweka matatani. ndivyo hapo kale ilivyokuwa kwa dokta Slaa na Zitto kule bungeni na mwembeyanga tulipotaja orodha ya aibu. tunapaswa kuuchukia ufisadi hata kama unafanyika na viongozi wetu ama chama chetu. mambo kama kufoji risiti za mafuta ili kuiba hela kwenye fungu la mafuta ya magari kama ifanyikavyo na baadhi ya wakurugenzi wetu makao makuu ya chama, ama vitendo kama kujiuzia jengo la mabaraza ya chama na chama kulipa kodi kwa mmiliki ambaye ni afisa wa chama makao makuu, ni ufisadi kama ufisadi mwingine na unapaswa kusemwa bila kujali eti msemaji anakidhalilisha chama, na haya ni kwa uchache.
Kuna wanaopanua midomo humu kuwa chama kilikwisha nitimua,ama kuwa nilishapuuzwa kwa sababu ya matendo niliyofanya. bahati nzuri watu hao ni ama wafagiaji tu wa makao makuu, ama wachumia tumbo waliojazana pale makao makuu, ama ni hawa mashabiki wasioijua chadema kwa ndani lakini wakikariri kila kisemwacho huko bila kuhoji kiasi cha kudhaniwa na watani zetu kuwa tunakunywa viroba au zaidi kwamba sisi ni misukule.
kama chama (as such-ni muhimu kuelewa maana ya neno hili) kimefanya maamuzi tofauti na ufahamu wangu huu, nifahamishwe na watu rasmi ambao tunao humu, na namba zangu za simu wanazo kwani viongozi wa chadema makao makuu, tunawasiliana kila siku, ila huwa hawasemi.iko siku tutaonyesha mawasiliano yetu ya mara kwa mara ili kunyamazishwa wabwekaji wa humu.
Hatimaye, nitaendelea kuipenda chadema kama mwanzo, kuitetea na wapuuzi wote, na kuitenga na kusingiziwa ujinga wowote. nitatumia uwezo na nguvu zangu zote, hadi dakika ya mwisho.ili ikiwa nikiwa hai ama nimekufa historia inikumbuke kama mzalendo wa kweli kwa taifa langu na chama changu. njia hii ni ngumu na wengi wa "vuvuzela" wa chadema licha ya kutoielewa, hawawezi hata kuifuata. kwa sasa waendelee kuniita msaliti, na mamluki. baadaye kama taifa letu litaondokana na ukoloni wa CCM, na kama CHADEMA kitaleta kweli utawala wa haki, basi tutakuja kufurahi na kuinuliwa na CHADEMA yenyewe na hawa "Vuvuzela" wa chadema wataimba nyimbo za kutusifu na kusema hatukujua. hofu yangu ni kuwa CHADEMA kinaweza kuja kuwa chama kibaya kuwahi kutawala Afrika. Dalili tumekwishaziona.
Mwl.Ludovick
Unayaleta humu ! Kwani JF ni tawi la CDM?. Mwl gani hujui taratibu za chama chako unashinda kwenye social network ukielezea mambo ambayo ulipaswa uyaelezee ndani ya chama chako!
 
Kama watu wanakusema vibaya kwa uliyofanya,na kwamba haya wakusemeao watu uliyafanya kwa nia njema juu ya chadema,sasa;
1.Wanasema umehusika kumteka Kibanda,je,hili lingekisaidiaje chama unachodai ni chako?
2.Wanasema ulihongwa na Mwigulu iliumrekodi na baadae kutengeneza video ili chama kihusishwe na ugaidi na baadae kifutwe,je,na hili lingekisaidiaje chama ulichokula njama ili kifutwe kwa video ya kutengenezwa?
Jibu hayo kwanza mkuu mwalimu
 
You are talking too much, thats why you are likely to spat something foolish later.....




For Now you are insane...
 
Attention seekers...ile dhambi itawatafuna mno. Insanity si lazima kuokota makopo!

Ukikataliwa na jamii ya watu wenye akili nawe ukajijua kuwa umekataliwa na hukubaliki tena, huwezi kuendelea kubakia mentally alright.

Watu wa psychology wanakuelewa upo katika wakati gani. Chademaphobia haikumalizi wewe peke yako, hata Mkuu wenu inamhangaisha kweli kweli.
 
Kama watu wanakusema vibaya kwa uliyofanya,na kwamba haya wakusemeao watu uliyafanya kwa nia njema juu ya chadema,sasa;
1.Wanasema umehusika kumteka Kibanda,je,hili lingekisaidiaje chama unachodai ni chako?
2.Wanasema ulihongwa na Mwigulu iliumrekodi na baadae kutengeneza video ili chama kihusishwe na ugaidi na baadae kifutwe,je,na hili lingekisaidiaje chama ulichokula njama ili kifutwe kwa video ya kutengenezwa?
Jibu hayo kwanza mkuu mwalimu

Majibu timilifu ya haya maswali hayawezekani kwa sababu ya kesi iliyoko mahakamani.
 
Watu kumi mkifanya kosa moja au linaloelekeana, wale tisa wakaonya au kufukuzwa na wewe usiambiwe chochote jua umedharauliwa kuliko wowote!
Huna impact, huna funzo kwa wengine!
Ni wewe kubaki au kusepa!#Ludo
 
Attention seekers...ile dhambi itawatafuna mno. Insanity si lazima kuokota makopo!

Ukikataliwa na jamii ya watu wenye akili nawe ukajijua kuwa umekataliwa na hukubaliki tena, huwezi kuendelea kubakia mentally alright.

Watu wa psychology wanakuelewa upo katika wakati gani. Chademaphobia haikumalizi wewe peke yako, hata Mkuu wenu inamhangaisha kweli kweli.
Huyu Bwana ni msemaji rasmi wa chama chetu na nadhani amesoma post yangu yote. silence means YES.
 
Kama watu wanakusema vibaya kwa uliyofanya,na kwamba haya wakusemeao watu uliyafanya kwa nia njema juu ya chadema,sasa;
1.Wanasema umehusika kumteka Kibanda,je,hili lingekisaidiaje chama unachodai ni chako?
2.Wanasema ulihongwa na Mwigulu iliumrekodi na baadae kutengeneza video ili chama kihusishwe na ugaidi na baadae kifutwe,je,na hili lingekisaidiaje chama ulichokula njama ili kifutwe kwa video ya kutengenezwa?
Jibu hayo kwanza mkuu mwalimu

akiJIBU MASWALI YAKO NAJITOA JF .
 
Huyu anahitaji tiba mbadala sio mzima.
 
Busara ya kawaida ingekutaka ukae kimya. kuendelea kusema ni kuthibitisha uovu unaotuhumiwa nao
 
Back
Top Bottom