Sina Mgogoro na CHADEMA

Sina Mgogoro na CHADEMA

Attention seekers...ile dhambi itawatafuna mno. Insanity si lazima kuokota makopo!

Ukikataliwa na jamii ya watu wenye akili nawe ukajijua kuwa umekataliwa na hukubaliki tena, huwezi kuendelea kubakia mentally alright.

Watu wa psychology wanakuelewa upo katika wakati gani. Chademaphobia haikumalizi wewe peke yako, hata Mkuu wenu inamhangaisha kweli kweli.

Hili nalo neno Tumaini Makene.
 
Pasco unaweza kuja hapa na kunijuza ni kwanini huyu bwana hataki kufuata ushauri wako uliompa hapo juzi?

Hivi ni kwanini ktk siku za hivi karibuni amekuwa na matamko mbalimbali kupitia JF akikihusisha Chadema na vijimambo vyake anavyoviandika kila uchao humu ndani? Kubwa ni kujaribu kuwaaminisha watu hapa ndani kwamba yeye bado ni mwanachama wa Chadema na kwamba anamapenzi makubwa na chama hicho?

Kuna ninu kiko nyuma ya Pazia juu ya haya matamko yake kwa chama? Tukumbuke huyu anajamaa mwenzake anaitwa Deus nani sijui...? Aliwahi kuja hapa jamvini na kuanzisha uzi unaosema "WAKATI WA MIMI KUSEMA UMEFIKA"....

Sasa mkuu Pasco naamni kwa namna flani ni fundi wa kusoma Saikolojia za watu unaweza kuniambia lolote juu ya haya yanayopangiliwa na hawa watu dhidi ya Chadema??

BACK TANGANYIKA
 
Last edited by a moderator:
Yaani hata hujafukuzwa walijua we ni mwehe sasa wakufukuze nini mpaka unaanza kupiga kelele wakusikie,huna kipya acha kelele zako
 
mwenzako machange alijipendekeza CCM baada ya kujichangan ya kwenye ishu ya mwangosi CCM wakamwambia chizi wewe kaa pembeni

naona unapoelekea na wewe kibarua kitaota nyasi maana CCM hawafanyi kazi na vichaa au watu wenye upungu wa akili maana ueleweki sana nachokiona kwako ni kama mtu aliye[poteza uelekeo wa maisha
 
LUDOVICK..Speak sense sometimes jamani...!!otherwise ur drunk,go and sleep.!!
 
Hivi ni kwanini unafanya wahaya wote tunaonekana wapumbafu na wasaliti...?sio hulka yetu mkuu ludo.
 
Jiulize kwanini mahasimu wa Chadema humu ndani wanasapoti sana uandikayo hapa?

Jiulize kwanini mpaka sasa hivi hawajaja kukusapoti?(najua wanaiona thread).

Majibu ni kwamba hata wao wameanza kukuchoka sasa.


Swali LA Mwisho: Kwanini kila uandikacho na usemacho wana CHADEMA wanaki-Crush?

Mwalimu umeshauriwa sana humu ndani na wengi wenye mapenzi mema, fuata ushauri, Lay low for a while.
 
Wakuu,
kwa siku kadhaa nimekuwa nikiandika ushauri na maoni yangu huru kwa chama changu CHADEMA. Yote yamefanyika kwa nia njema na mapenzi makubwa niliyo nayo kwa chama changu. na hakika hata yote mengine yanayotajwa dhidi yangu, yamefanywa nami kwa sababu ya mapenzi na kukilinda chama changu. Sasa wapo baadhi ya watu wameshindwa kuelewa maana ya ushauri na maoni yangu hayo na kwa makosa wameishia kunishambulia tu kiujumla bila kuainisha makosa kwenye hoja zangu. baadhi yao,licha ya kuona ukweli kwenye maoni yangu, wakadhani kuna motive behind ambayo ni mbaya, wengine wakaniona nimekuwa insane, wakielezea ninavyojichimbia kaburi. hawa kwa kinyume wanasema kitu cha hatari zaidi kwa chadema kuwa inaweza hata kukolimba, kuchacha watu nk,na wengine baadhi wakiendeleza mitazamo "makengeza" ya kuona kila anayekosoa na kushauri chadema basi ni mamluki na anatumiwa na CCM.

Wapo wengine ambao bila kufuata urari wa hoja wala kufahamu ninachokiongelea wametukana matusi,ama kuchepuka kwenye mada husika na kuingiza mada tofauti kabisa ili kupunguza makali ya ukweli katika maoni yangu. Tena wapo ambao kwa haki kabisa na kwa weledimkubwa wameona mantiki na ukweli wa yale ninayoyaeleza na nia njema niliyo nayo, na mwisho kuna wanaodhani ninatoa maoni na ushauri huu kwa sababu nina mgogoro na chadema.

Kwa kweli WOTE nawashukuru kila mmoja kwa nafasi yake.
Niseme tena hapa hadharani kuwa mimi sijawahi kuwa na mgogoro na chadema, na wala sina kinyongo na chama as such.(hii as such, ni muhimu kueleweka vema, kwani ni ontological concept). Na kwa kweli sijawahi kufanya jambo lolote kinyume na katiba,maadili na miongozo ya chama. kwa sababu hiyo, mimi sijawahi kuonywa,wala kupewa karipio wala barua yoyote na chama, sijawahi kupewa adhabu wala kusimamishwa/kufutwa uanachama. Bado ninayo kadi yangu na ninailipia na muhimu zaidi bado naishi misingi na falsafa za chadema. Kwa kuwa viongozi wetu wameongoza maasi ya misingi hii kiasi cha kutoeleweka tena kwa wanachama wetu, hadi chama chetu kuwa sawa na CCM, Nikumbushe tu kwa uchache kuwa tunaamini katika nguvu ya umma, kuchukia ufisadi, uwazi na demokrasia, na kwa kweli tunaamini katika mabadiliko.

Tunapaswa kusema kweli daima hata kama ukweli huo utatuweka matatani. ndivyo hapo kale ilivyokuwa kwa dokta Slaa na Zitto kule bungeni na mwembeyanga tulipotaja orodha ya aibu. tunapaswa kuuchukia ufisadi hata kama unafanyika na viongozi wetu ama chama chetu. mambo kama kufoji risiti za mafuta ili kuiba hela kwenye fungu la mafuta ya magari kama ifanyikavyo na baadhi ya wakurugenzi wetu makao makuu ya chama, ama vitendo kama kujiuzia jengo la mabaraza ya chama na chama kulipa kodi kwa mmiliki ambaye ni afisa wa chama makao makuu, ni ufisadi kama ufisadi mwingine na unapaswa kusemwa bila kujali eti msemaji anakidhalilisha chama, na haya ni kwa uchache.

Kuna wanaopanua midomo humu kuwa chama kilikwisha nitimua,ama kuwa nilishapuuzwa kwa sababu ya matendo niliyofanya. bahati nzuri watu hao ni ama wafagiaji tu wa makao makuu, ama wachumia tumbo waliojazana pale makao makuu, ama ni hawa mashabiki wasioijua chadema kwa ndani lakini wakikariri kila kisemwacho huko bila kuhoji kiasi cha kudhaniwa na watani zetu kuwa tunakunywa viroba au zaidi kwamba sisi ni misukule.
kama chama (as such-ni muhimu kuelewa maana ya neno hili) kimefanya maamuzi tofauti na ufahamu wangu huu, nifahamishwe na watu rasmi ambao tunao humu, na namba zangu za simu wanazo kwani viongozi wa chadema makao makuu, tunawasiliana kila siku, ila huwa hawasemi.iko siku tutaonyesha mawasiliano yetu ya mara kwa mara ili kunyamazishwa wabwekaji wa humu.

Hatimaye, nitaendelea kuipenda chadema kama mwanzo, kuitetea na wapuuzi wote, na kuitenga na kusingiziwa ujinga wowote. nitatumia uwezo na nguvu zangu zote, hadi dakika ya mwisho.ili ikiwa nikiwa hai ama nimekufa historia inikumbuke kama mzalendo wa kweli kwa taifa langu na chama changu. njia hii ni ngumu na wengi wa "vuvuzela" wa chadema licha ya kutoielewa, hawawezi hata kuifuata. kwa sasa waendelee kuniita msaliti, na mamluki. baadaye kama taifa letu litaondokana na ukoloni wa CCM, na kama CHADEMA kitaleta kweli utawala wa haki, basi tutakuja kufurahi na kuinuliwa na CHADEMA yenyewe na hawa "Vuvuzela" wa chadema wataimba nyimbo za kutusifu na kusema hatukujua. hofu yangu ni kuwa CHADEMA kinaweza kuja kuwa chama kibaya kuwahi kutawala Afrika. Dalili tumekwishaziona.

Mwl.Ludovick
Ikiwa ni kweli unawasiliana na wakubwa wako hapo makao makui kila siku kwanini usiwaambie huo unaouita ushauri? Lakini ndugu yangu yote uliyofanya kuhujumu Chadema na unayoyafanya sasa bado unasema unaipenda Chadema? Come on Ludo unatuona wooote wajinga ila wewe tu ndio kichwa??? Kuna jamaangu alinambia Wahaya hujiona wao wanajua kuliko wengine na wengine wote wajinga tu, lakini nimegundua sio wote bali wachache style ya Ludo wamo. Ulipata ajali kwenye gari la uenezi la ACT ukiwa kwenye harakati na wenzako wa ACT, unaenezaje chama usichokuwa mwanachama? Kama ni mwanachama mbona hutoi ushauri huko bali chama ulichotoka?
 
Back
Top Bottom