Wakuu,
Haya mambo ya dini yapo wazi sana. Mimi huwa nasikiliza redio Imani kila siku. Redio hii waziwazi wanamshambulia Dk. Slaa si kwa ubaya wake, bali kwa dini yake! Wanasema kabisa kwamba yule atawaumiza waislam!
Siku moja allitwa shehe Mwaipopo na mwenzakwe mmoja na wakakumbushia mambo ya Mwembechai na kusema ulikuwa mkakati wa wakristo kuumiza waislamu. Wakaenda mbali zaidi kwa kusema , pamoja na kwamba Raisi alikuwa ni Hassan Mwinyi (muislamu), bado si yeye aliyekosa, bali alikuwa ni Augustino Mrema ( Mkristu), kwani yeye ndo alikuwa Waziri wa mambo ya ndani na akamdanganya Mwinyi hivyo Mwinyi kuingia mkenge kwa kuua Waislamu wenzake!
Bila kumung'unya maneno wakadai kwamba waislamu wasimchague Mkatoliki, kwani huo utakuwa mwanzo wa kutawaliwa na Vatican!
Lakini cha ajabu wamesahau kwamba, Omar Mahita (Muislamu) ndiye aliye watwanga risasi wapemba wale ambao ni Waislamu wenzao. Wamesahau kwamba wakati huo Raisi wa Zanzibar alikuwa ni musilamu!
Tatizo ni kwamba, wanaohubiri siasa za chuki ya dini kwenye hiyo misikiti ni watu wanaofaidika na uongozi wa kifisadi uliopo CCM. Si waislamu wote wanapenda hizi chokochoko, ila wengi wanaamini hayo yasemwayo na mashehe kiasi kwamba wamejenga chuki ya wazi kabisa.
Kuna rafiki yangu sasa hatuongei, kisa tu nilimwambia JK ameshindwa kufanya maamuzi mazito...yeye badala ya kunisikiliza aling'aka "kwa hiyo tumchague mkatoliki?"
Nikajiuliza, swala la Mkatoliki linakujaje wakati tunajadili uongozi?
Radio imani inaeneza ujumbe hatari sana, na nashangaa kwanini serikari inainyamazia. Ina dalili zote ya kwamba ni redio ya vigogo wa CCM walioko Morogoro na sehemu nyingine za nchi. Magazeti yanyosomwa pale ni yale ya RA (Mtanzaia etc) , na yale ya kiislamu, ya CCM (Uhuru) na ya serikali (Habari leo). Pia Mwananchi huwa wanalisoma, pale tu lisipokuwa na habari za DK Slaa!
Kuna ujumbe amboa kila siku unatolewa wakisema " Waisilamu wananyanyaswa sana kote ulimwenguni, na waislamu wanateswa, wanachinjwa na wana uawa kwa sababu tu ya kuwa waislamu"!
Muda Mwngi pia huutumia kushambulia Marekani kwamba ni adui wa Uislamu! Cha ajabu Raisi wetu wa JMT Mh. DK Jakaya Kikwete ni muislamu safi na ambaye ameikumbatia Marekani kama baba na mama yetu! Je kwanini basi wasimkemee JK badala yake wanawadanganya waislamu wasio jua hila za hawa viongiozi wa kidini, kwamba Marekanioni adui huku JK akionyesha waziwazi mapenzi yake kwa Bush?
Haya mambo ya dini yapo wazi sana. Mimi huwa nasikiliza redio Imani kila siku. Redio hii waziwazi wanamshambulia Dk. Slaa si kwa ubaya wake, bali kwa dini yake! Wanasema kabisa kwamba yule atawaumiza waislam!
Siku moja allitwa shehe Mwaipopo na mwenzakwe mmoja na wakakumbushia mambo ya Mwembechai na kusema ulikuwa mkakati wa wakristo kuumiza waislamu. Wakaenda mbali zaidi kwa kusema , pamoja na kwamba Raisi alikuwa ni Hassan Mwinyi (muislamu), bado si yeye aliyekosa, bali alikuwa ni Augustino Mrema ( Mkristu), kwani yeye ndo alikuwa Waziri wa mambo ya ndani na akamdanganya Mwinyi hivyo Mwinyi kuingia mkenge kwa kuua Waislamu wenzake!
Bila kumung'unya maneno wakadai kwamba waislamu wasimchague Mkatoliki, kwani huo utakuwa mwanzo wa kutawaliwa na Vatican!
Lakini cha ajabu wamesahau kwamba, Omar Mahita (Muislamu) ndiye aliye watwanga risasi wapemba wale ambao ni Waislamu wenzao. Wamesahau kwamba wakati huo Raisi wa Zanzibar alikuwa ni musilamu!
Tatizo ni kwamba, wanaohubiri siasa za chuki ya dini kwenye hiyo misikiti ni watu wanaofaidika na uongozi wa kifisadi uliopo CCM. Si waislamu wote wanapenda hizi chokochoko, ila wengi wanaamini hayo yasemwayo na mashehe kiasi kwamba wamejenga chuki ya wazi kabisa.
Kuna rafiki yangu sasa hatuongei, kisa tu nilimwambia JK ameshindwa kufanya maamuzi mazito...yeye badala ya kunisikiliza aling'aka "kwa hiyo tumchague mkatoliki?"
Nikajiuliza, swala la Mkatoliki linakujaje wakati tunajadili uongozi?
Radio imani inaeneza ujumbe hatari sana, na nashangaa kwanini serikari inainyamazia. Ina dalili zote ya kwamba ni redio ya vigogo wa CCM walioko Morogoro na sehemu nyingine za nchi. Magazeti yanyosomwa pale ni yale ya RA (Mtanzaia etc) , na yale ya kiislamu, ya CCM (Uhuru) na ya serikali (Habari leo). Pia Mwananchi huwa wanalisoma, pale tu lisipokuwa na habari za DK Slaa!
Kuna ujumbe amboa kila siku unatolewa wakisema " Waisilamu wananyanyaswa sana kote ulimwenguni, na waislamu wanateswa, wanachinjwa na wana uawa kwa sababu tu ya kuwa waislamu"!
Muda Mwngi pia huutumia kushambulia Marekani kwamba ni adui wa Uislamu! Cha ajabu Raisi wetu wa JMT Mh. DK Jakaya Kikwete ni muislamu safi na ambaye ameikumbatia Marekani kama baba na mama yetu! Je kwanini basi wasimkemee JK badala yake wanawadanganya waislamu wasio jua hila za hawa viongiozi wa kidini, kwamba Marekanioni adui huku JK akionyesha waziwazi mapenzi yake kwa Bush?