#SimuliziZa116: Baba Neema Atoa Taarifa ya Mimba za Utotoni

#SimuliziZa116: Baba Neema Atoa Taarifa ya Mimba za Utotoni

Sema Tanzania

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2016
Posts
251
Reaction score
466
Baba Neema alitupigia simu #116 baada ya kugundua mwanae kwa jina Neema, mwenye umri wa miaka 16 ni mjamzito na hivyo hatoweza kuendelea na masomo. Mwanzoni, Neema alisita kumtaja aliyempa ujauzito, lakini baadae alimueleza baba yake kuwa alibakwa na Askari Polisi na kupata ujauzito huo. Askari huyo alimtishia Neema baada ya kumbaka hivyo aliogopa kumueleza mtu yeyote.

Baba Neema alipopiga 116 kuomba msaada alisema, “Inasikitisha kuona kwamba watu tunaowaamini na kuwapa dhamana ya kulinda jamii zetu ndiyo hao hao wanaotuumiza.” Alikuwa amekwishafungua kesi lakini alihitaji tumsaidie kufuatilia na kuhakikisha haki inatendeka.

Tuliwasiliana na Kituo cha Polisi ambako mshukiwa wa tukio hilo alikuwa anafanya kazi na OCS alitujuza kuwa, afisa huyo alishasimamishwa kazi na uchunguzi unaendelea.
 
Sometimes sisi walevi tunaonekana hatuna akili tunafanya mambo ya hovyo kumbe kinyume chake watu wazima wenye dhamana na wanaojielewa wanafanya mambo ya hovyo
 
Umri wa mtu mzima urudi miaka 15, hawa mnaoita watoto- wana vijimambo maana wanajua sheria haiwagusi.
 
Sometimes sisi walevi tunaonekana hatuna akili tunafanya mambo ya hovyo kumbe kinyume chake watu wazima wenye dhamana na wanaojielewa wanafanya mambo ya hovyo
Sasa ndugu yangu wewe unafikiri hizo dhamana ndio zinaondoa aspect za mtu alizo nazo? Kama mtu ni nyang'au atabakia kuwa nyang'au tu.
 
Back
Top Bottom