Simulizi ya kijasusi: Shattered Evil: Light And Shadow

Simulizi ya kijasusi: Shattered Evil: Light And Shadow

kailojonhjo

Member
Joined
Jun 7, 2025
Posts
6
Reaction score
5
SHATTERED EVIL:LIGHT AND SHADOW

MTUNZI:KAILOJONHJO.


 UTANGULIZI
SHATTERED EVIL: LIGHT AND SHADOW Ni simulizi inayochanganya ,mystery, fantasy,mapenzi, ujasusi
Miaka ya zamani watu walisifika sana kua na nguvu iyo ilitokana na kua na upeo mkubwa wa akili mpaka kuweza kuamsha nguvu za kichawi na hatimae kufikia levo za juu kulikua na mbinu mbalimali za kuamsha nguvu hizo yote hayo yaliwezekana ila baada ya miaka mingi kupita mambo hayo yote yalibaki kama Nadhalia tu na hadithi za kufikilikika hivyo kupelekea watu wenye nguvu huishi kwa siri kubwa

Katika miaka ya sasa Miaka kumi na sita iliyopita, mtoto mdogo alipotea katika mazingira ya kutatanisha, katikati ya mchana kweupe, akiwa ndani ya shule ya msingi jijini Dar es Salaam. Hakuacha alama. Hakukuwa na ushahidi. Hakukuwa na majibu. Taifa lilishtuka. Serikali ilituma vikosi. Kamera zilichunguzwa. Lakini mtoto huyo alimezwa na giza lisiloeleweka.

Watu wengine walisema labda ni uchawi

Alipelekwa mahali palipo nje ya uelewa wa binadamu—ulimwengu wa siri uliojaa nguvu zisizosemwa, mafunzo ya hatari, na maamuzi ambayo yangebadili maisha yake milele. Alirudi akiwa mtu mwingine. Si mtoto tena—bali mwanaume mwenye nguvu, aliyejificha kwenye kivuli cha jina la Liam jina lake jipya ambalo alipewa na mmoja wa master wake

Sehemu alio pelekwa Liam ni nje kabisa ya uelewa wa kidunia si kila mtu anaweza kufika kuingia kwake kuna kifaa malumu ambavyo ndio hutumika kama funguo

Katika kurudi kwake kuitafuta familia aliyosahau, hatima inamtupa katikati ya jiji lenye kelele, uongo, na siasa chafu—na hapo ndipo anapokutana na , binti tajiri mwenye ushawishi mkubwa Ni baridi. Ni mwenye akili. Na ni mgumu kumpenda mtu asiye na historia inayoeleweka.

Lakini moyo haujui mantiki.

Na vivuli vya zamani vinamfuata liam—wakati majibu ya ukweli juu ya kutoweka kwake yanaanza kujifungua taratibu.

Usikose kuifatilia simulizi hii:itakua inatoka kila jump 5
********

SEHEMU YA 1
Katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere Internation airport, Dar es Salam

Saa 9:30 mchana

Nguvu za injini ga Qatar Airways zilitulia polepole mlango wa ndege ukafunguli wa na kushaku ka talatibu Abılıa to kuanza

Miongo ni ma Abilia hao alioneka na mwanaume mmoja wa takribani miaka 24 ad 26 akishuka talatıbu alikua amevaa Shatı jeusı la mikono mirefu lililo fungwa shingoni Suluarı ya cargo ya kijivu na buti nene za ngozi begi dogo klikninginia upande wa kushoto wa bega

Sauti ya afsa wauhamiajı yenye upole lakını ya kazı lışıkıka

Kalibu Sana Tanzania ndugu Paspot tafadhali

kijanana (Alitoa kimya kimya mach bado kwenye dari la jengo)

"Hll hapa." Alimkabidhi afisa huyo paspot

Afisa alitazama pasipoti jina lililo andikwa lilimfanya agande kwa Sekunde kadhaa

: Liam..... Liam Carter umetoka wap?" Afisa alimuuliza mwanaume huyo ambae anafaamika kwa jina la Liam Carter kama paspot yake ilivyo andikwa

"Thailand. Alijibu mwanaumehuyo anaefahamika kwa jina la Liam. Afisa alimtazama kwa muda mfupi, akatabasamu kwa tahadhari. Kisha akampigia muhuri pasipoti na kumrudishia.

"Karibu Sana Tanzania, kaka liam

Asante (Liam alijibu kisha Akatembea mbele bila kuuliza lolote.)

Aliingia kwenye ukanda wa kuchukua mizigo, lakini hakusubiri -- hakuwa na mizigo mkubwa zaidi ya begi lake dogo. Alivuka sehemu ya ukaguzi, akaingia sehemu ya mapokezi. Uwanja ulikuwa na watu wengi, baadhi wakikimbia kuwakumbatia ndugu zao, wengine wakisubiri kwa macho yenye hamu. liam alisimama kwa sekunde chache. Hakukuwa na yeyote aliyemsubiri. Hakukuwa na hata bango la jina lake.

Alitembea kuelekea mlango mkuu wa kutoka. Gharika ya jua kali na joto ikampiga uso wake mara tu alipovuka mlango wa kioo. Akika ni kama nilivyo sikia nchi hii inajoto sana

Alitazama kulia na kushoto baada ya kuona taksi na kuanza kuzisogelea

Dereva mmoja wa Teksi baada ya kumuona akamsogelea haraka):

“Vipi bro! Tunaenda wapi leo? Masaki? Mikocheni? Sinza? Gari iko poa, AC iko full!”

Liam alitazama macho ya dereva kwa muda mfupi):

“Masaki. Kwenye. Hotel yoyote yenye utulivu.”

Dereva (akiwa amefurahi):

“Ah, sawa! Karibu kaka, twende basi! Bei ni rafiki -- elfu hamsini tu.”

Liam (akitikisa kichwa na kukubali

“Dah, fresh kabisa bwana. Karibu Dar es Salaam!”

Gari ilikuwa Toyota Crown ya rangi ya silver. Dereva alifungua mlango wa nyuma kwa haraka, liam akaingia kimya. Akatupia begi pembeni na kuangalia dirishani. Na safari ikaanza Jiji lilianza kufunguka mbele yake -- magari, foleni, bajaji zilizopambwa, milango ya maduka ya Mlimani City, matangazo ya kampuni kubwa, harufu ya jua juu ya lami.

Dereva (akajaribu kuanzisha mazungumzo):

“Unaonekana mpya kabisa. Mara ya kwanza kufika Bongo?”

Liam (bila kugeuka):

“Sio mara ya kwanza… lakini ni kama mara ya kwanza.”

Dereva (akiwa anacheka):

“Heh! Hiyo sasa ni deep. Ulikuwa nje miaka mingi nini?”

“Niliwahi kuishi hapa nikiwa mtoto. Kisha niliondoka…”

Gari likakaa kimya. Dereva hakuliza zaidi. Aliangalia kupitia kioo cha nyuma lakini macho ya liam yalikuwa mbali sana -- kana kwamba alikuwa anatazama mahali palipo nje ya dunia hii.

Toyota Crown ya rangi ya fedha ilipinda kona ya mwisho kuingia Masaki. Jua la mchana liling’ara juu ya mtaa wa Chole, na upepo wa baharini ulivuma taratibu. Gari ilipunguza mwendo mbele ya jengo lenye maandishi meusi yaliyong’aa: Lush Bay Hotel.

Dereva akatazama kupitia kioo cha nyuma):

“Bro, tumefika. Hii hapa Lush Bay, ni nzuri na ina utulivu wa maana kabisa. Internet ipo, AC kali, na chakula fresh.”

Liam akavuta pumzi kwa kina

“Nzuri. Ahsante.”

Alitoa noti ya dola 100 na kumpa bila kuongeza neno

Dereva akapokea kwa bashasha

“Karibu Dar kaka! Ukihitaji gari tena sema tu, naitwa Hashim hii ni business cad

Liam alipokea business cad kisha akashuka taratibu, akanyoosha viungo kama mtu aliyekaa muda mrefu. Alibeba begi begani na kutazama juu ya jengo kwa muda mfupi — macho yake hayakutoa maelezo, lakini ni kama alikuwa anajaribu kukumbuka kitu. Mlango wa hoteli ulifunguka kiotomatiki alivyokaribia.

Ndani ya mapokezi, msichana mrefu mwenye sare ya kijivu aliketi nyuma ya kaunta. Jina lake liliandikwa kifuani: Edna. Tabasamu lake lilikuwa la kawaida, lakini lilivutia.

Edna kwa sauti ya kitaalamu):

“Karibu Lush Bay Hotel. Umefanya reservation?”

Liam akamtazama dada huyo kwa sekunde kadha kama kam chunguza kisha akajibu kwa sauti ya utulivu

“Hapana. Nahitaji chumba — tulivu, chenye dirisha, na bila usumbufu.”

Edna (akitazama kwenye skrini ya kompyuta):

“Tuna Executive Single na Private Balcony Deluxe. Deluxe ina view nzuri ya bahari.”

“Deluxe. Nachukua kwa siku saba. Alisema liam


Edna akainua macho kwa mshangao kidogo

“Ooh, fresh. Utalipa kwa kadi au cash?”

Liam alitoa pochi ya ngozi, akamkabidhi kadi ya Visa:

“Kadi.”

Baada ya malipo kukamilika, Edna alimkabidhi kadi ya chumba, nambari 408.

“Chumba 408, ghorofa ya nne. Lifti iko upande wa kulia. Ukiwa na swali lolote, piga namba hii.”

Liam alitikisa kichwa taratibu

“Sawa.” kisha alienda kwenye lifti kwa hatua tulivu. Ukimya wake uligusika, kama hewa nzito. Mlango wa lifti ulifunguka, akaingia peke yake. Ndani ya lifti, Liam alitazama uso wake kwenye kioo. Alishika kifua chake na kuhisi mapigo ya moyo wake.

Liam alijinong’oneza

“Nimeanza. Sura ya mama... ndiyo pekee niliyonayo.”


Mlango ulifunguka kwenye ghorofa ya nne. Liam alitembea kwenye korido yenye mwanga wa manjano laini, akiangalia namba za milango. Alisimama mbele ya 408. Akaingiza kadi na mlango ukafunguka. Chumba kilipiga harufu ya sabuni safi na maua ya vanilla. Alifungua pazia — mbele yake, bahari ya Hindi iling’ara chini ya jua.


Alitupa begi juu ya kitanda, akaketi kwenye kochi karibu na dirisha. Mikono yake ilishikilia kichwa, macho yake yakiwa yamekwama kwenye upeo wa macho. Fikra zake hazikuwa baharini — zilikuwa mbali, gizani, ndani ya mahali pasipoelezeka.


Alisimama taratibu. Akachukua simu yake, akaishika mkononi bila kuifungua.


Liam kwa sauti ya chini, akajinong’oneza


“Tayari niko nchini nini kinafata


Liam alionekana ana vitu vingi sana kichwani vinavyo mtatiza alitafakali kwa sekunde kadhaa kisha akaamua kujipunzisha

*****

Flashback: Miaka 17 nyuma Jua la asubuhi lilikuwa na joto la upole. Ndege walikuwa wanapita anga la Buguruni, wakiimba nyimbo za kila siku. Ilikuwa ni siku ya Jumatano, shule ya msingi Mtoni Mchangani ilikuwa imejaa sauti za watoto, kicheko, na kelele za walimu waliokuwa wakijitahidi kuweka nidhamu.

Kulikua na mtoto, akiwa na miaka 8 tu, aliketi darasani kwenye dawati la tatu upande wa kushoto. Alikuwa mtoto mtulivu kupita kawaida, mwepesi kuelewa, na mwenye sura ya kuvutia iliyojaa utulivu wa kipekee. Wakati mwalimu wao, Bi Zena, alipokuwa anaandika kwenye ubao, macho ya mtoto huyo yalitazama dirishani — kama alikuwa anasikia kitu fulani, tofauti.

“Michael! Tazama ubao, si dirisha.” mwalimu zena alimwambia mtoto uyo ambae aliitwa Michael

Michael (kwa sauti ya upole):

“Samahani mwalimu... lakini... kuna mtu... ananiangalia kule nje.”

Wanafunzi wengine waligeuka. Dirishani kulikuwa wazi, ila hakuna mtu aliyemwona. Mwalimu alifika karibu, akatizama nje. Hakukuwa na mtu.

“Hakuna mtu. Rudi kwenye daftari lako na utazame ubaoni alisema mwalim zena

Dakika chache baadaye, kengele ya saa nne ililia — muda wa mapumziko. Wanafunzi walimiminika uwanjani. Michael naye alichukua kipande cha mkate wa siagi mama yake aliyomwekea, akaelekea kivulini chini ya mti wa mkungu karibu na uzio wa shule. Hapo ndipo aliposimama.

Upande wa pili wa uzio, kulikuwa na mzee mmoja. Alivaa joho jeusi lenye maandishi ya dhahabu, na macho yake yalikuwa ya kijani kibichi. Alikuwa na tabasamu la ajabu, si la kirafiki, lakini pia si la tishio — bali la kuvuta mtu bila sababu.

Mzee huyo (kwa sauti ya ajabu, kama hewa):

“Michael... unakumbuka wimbo wa nyota tano?

Michael alitikisa kichwa. Ndiyo, ulikuwa wimbo mama yake alimfundisha akiwa mdogo.

“Ndiyo. Mama yangu hua ananiimbia nikitaka kulala.”

“Basi njoo, tukaendelee kuimba pamoja.” alisema mzee huyo

Ni hapo ndipo Liam alipoanza kutembea, taratibu, kana kwamba alikuwa kwenye usingizi wa macho. Aliingia kichakani kupitia uwazi uliokatwa kwenye uzio — njia ambayo haikuwa hapo siku zilizopita.

Walimu hawakumwona, walinzi wa shule hawakumwona, na hata wanafunzi wenzake walifikiri bado yupo chini ya ule mti.

Dakika ishirini baadaye, mtoto huyo anaye fahamika kwa jina la Michael hakuwepo. Uwanja wa shule ukazizima. hii ilifahamika kuwa mtoto mmoja hayupo mala bada wa kuludi daladani na kukosekana kwa mtoto huyo

Ilibidi walimu waanze wakishilikiana na mlinzi kumuuliza labda mtoto huyo alitoka lakini mlizi alijibu kua hakuna mtoto yoyote alietoka waliendelea kumtafuta nje ya madalasa kwa kuzani labda huenda alikua bado nje lakini mpaka yanatimia masaa 4 hakukua na dalili yoyote ilio onesha kupatkana kwa mtoto

Ilibidi waitwe police wakaja. Upelelezi ukaanza.

Askari wa Kituo cha Polisi Buguruni – CPL Mwita:

“Mliona mtu yeyote akichukua mtoto?” aliuliza afisa wa jeshi la polisi

“Hapana afande. Hii shule imezungukwa na ukuta. Na hakuna mlango mwingine zaidi ya wa mbele.” alijibu mlinzi wa shule

“Alikuwa na mkate wake. Alikaa tu kivulini kama kawaida. Halafu... alipotea. Kama upepo maana huna alie muona alisema mwalimu mkuu -Bi faidha

Ilibidi wawasiline na Wazazi wa Michael walipokuja, vilio vilitanda. Dada zake walilia kwa uchungu. Kakake mkubwa aliapa kutomcheka tena kama alivyozoea.

Tukio hilo liliingia kwenye vyombo vya habari. Magazeti kama Mwananchi, Majira, na Nipashe yaliandika vichwa kama:

"Mtoto Apotea Buguruni: Alimezwa na Hewa?"

"Tukio la Kimaajabu: " akika tukio hilo lilikua ni la kustaajabisha

Jeshi la Polisi liliunda kikosi maalum. Maafisa wa usalama wa Taifa wakaja. Lakini hakuna aliyepata ushahidi wa kamera, wala alama ya viatu, wala njia ya mtego.Ilikuwa ni kana kwamba Michael alitoweka kutoka dunia hii

*****

Saa ilikuwa 6:00 jion. Hoteli ya Lush Bay, iliyoko Masaki karibu na bahari, ilikuwa tulivu, joto la jiji likianza kushuka polepole. Liam alikaa kwenye kiti cha ngozi chenye mvuto wa kifahari, miguu yake ikiwa imekunjwa kidogo, mikono yake ikiwa nyuma ya shingo.

Dirisha la chumba namba 408 lilifunguliwa nusu, likimuonesha barabara ya Chole Road na baadhi ya paa za majumba ya kifahari yaliyo jirani. Vioo vya dirisha viliakisi macho yake ya samawati yenye kina

Simu ya mezani ikaanza kuita

“Trriiiiii... Trriiiiii...”

Akastuka kidogo, kisha akaiinua taratibu.kwa sauti ya taratibu): “Hallo...?” alisema liam

Sauti ya mapokezi: “Habari za jioni, bwana Liam. Tumepokea mzigo wako wa mkoba uliobaki airport. Je, tukuletee chumbani?”

: “Ndio, tafadhali. Ahsante.” alisema liam

Baada ya kutata simu, akasimama na kutembea taratibu kuelekea bafuni. Kioo cha bafuni kilimuonesha sura yake — sura ile ile, lakini ikiwa , na ukimya mzito. Akaushika uso wake kwa mikono miwili, macho yake yalionekana kama yanapambana na kivuli kisichoeleweka

Liam alijinong’oneza atimae leo niko Tanzania…”

Alihisi kama sauti ndani yake inamwambia kuna kitu kinamkaribia. Lakini bado hakijajulikana ni nini.

Mara mlango wa chumba ukagongwa.

“Pppppp!”

Liam akasogelea mlango na kuufungua. Kijana mhudumu wa hoteli, mwenye tabasamu dogo usoni, anasimama mlangoni.

Huu hapa mzigo wako. Alisema muhudumu na kumkabidhi mkoba ule liam

Ahsante sana. Alisema liam

Akapokea mzigo wake na kuufunga mlango. Akakaa kitandani, na kufungua zipu wa begi lake. Ndani kuna koti lake la ngozi jeusi, pochi ndogo ya pesa, na kijikaratasi kimoja cha zamani — kilichokunjwa mara nyingi sana.

Akakikunjua na kukitazama. ilikua Ni picha ya mwanamke mwenye sura laini, macho ya huruma, na tabasamu la mama. Ilionekana ni picha ya zamani sana na ilio chakaa lakini bado inasimulia hadithi.

(Liam kwa sauti ya upole sana): “Mama… bado nakukumbuka. Lakini... uko wapi? Alisema liam

Papo hapo, dirishani upepo ulianza avuma na matazia yalipepepelushwa na upepo kwa sekunde chache. Liam akanyanyuka taratibu, na kufunga dirisha. Lakini moyo wake haukutulia

Anahisi kuna mtu anamwangalia. Au kuna jambo linamvuta kutoka mbali — kitu cha zamani, kitu cha hatari.

Akaamua kupoteza mawazo na kuagiza chakula akipendacho kwa maana hakua amepata chchote kangu alipo ingia nchini alipiga mapokezi na baada ya muda aliletewa

Baada kumaliza kupata chakula muda ulikua umesha enda ilikua ni mida ya kwenye saa3 za usiku hivyo Akaamua kujilazaa juu ya kitanda, hakua na mpango wa kutoka ukizingatia ni mgeni macho yakitazama dari. lakini gafla tu aliamka na kushuka kwenye kitanda hii ni mala baada ya kuhisi atali iko kalibu nae

Mwili wake wote ulisisimka. Ilikuwa kama umeme mdogo ulivyopita mgongoni

ITAENDELEA
 
SEHEMU 2
Liam baada ya kusimama aliskilizia kwa sekunde kadhaa aliudii kitandani na kujisemea ndio kwanza hajamaliza hata siku moja lakini tayari kuna watu wamesha tumwa kushugulika nae

Mlango wa chumba 408 ukafunguliwa kimya kimya, kwa kutumia kifaa maalum. Wanaume watatu waliingia, wakiongozana na mmoja alie onekana kua kaitika umli wa miaka 40 adi 50 alionekana kua ndio kiongozi wao wengine walikua ni vijana tu ambao dam zao bado zinachemka na walikua na maumbo yaliyo jazia misuri wote walivalia suti uku shingoni wakininginiza vitambulisho walionekana

Liam baada ya kuwaona vizuri watu hao aliweza tutambua hisia zake hazikua sawa kwani kutoka na na uzoefu wake aliamini moja kwa moja watuao watakua ni wana usalama

Wewe ndio liam. Alisema mtu yule alie onekana kua kiongozi

Liam. Alinyanyua mkono wa kushoto, akawapungia hewani kama mtu anayewasalimia watoto wa nursery.

“hey mna shida gani mbona mnaingia bila ata hodi nikisema mmenivamia nitakua nakosea. Alisema liam

Bwana alie kua anaonekana ndio kiongozi aliwageuzia macho wenzake na kuludisha umakini kwa liam na kusogea mbele. Alikuwa mweusi wa asili, mwenye macho makali kama mchora ramani wa roho.

“Jina langu ni Inspector DCI Evans Mshindo. Tuko hapa kwa magizo ya kukuchukua kwa mahojiano hii ni kwasababu za kiusalama. Kila kitu kiko kisheria. Hivyo tuna kira haki za kukukamata hivyo usifanye mambo kua magumu vinginevyo tutalazimika kutumia nguvu

Liam kusikia hivyo aligeuka taratibu, akakaa pembeni mwa kitanda, akatikisa kichwa na kusema

“kishindo? Ndio jina lako? Duuh... linatisha. Ila si tishio. Sawa, nimeelewa. Naona nimeanza kuwashtua mapema.”

OK Inspector kishindo unaonaje unikiacha nikapumzika kwanza alaf kukikusha ndio uendelee na zoezi la kunikamata kwa maana ni usiku saiv ata maswali mnayo taka kuniuliza ntashidwa kuwapa majibu mazuli. Alisema liam uku akitabasamu

Sisi Tunafata maagizo hivyo unatakiwa kutii vinginevyo atutakua na jinsi zaidi ya kutumia nguvu. Alisema inpecta kishido

Capten unambembeleza sana alaf anaonekana kutudhalau kama vipi tumshkishe adabu. Alisema bwana mmoja miongoni mwa watu alio kuja nao inpecta Mshindo na kuanza kupiga atua kumsogolea liam.

Lakini kabla hajamsogolea zaidi liam alizuiwa na inpecta mshindo kujiamini kwa liam kulimfanya inpecta Mshindo kua na tahadhari kwani kwa uzoefu wake wa zaidi ya miaka 25 hakuwahi kwenda kumkamata mtuhumiwa na mtuhumiwa kuto onyesha hofu yoyote hali hiyo ilimfanya kua makini na Liam.

Lakini kwa muonekano wa liam aliamini hana kitu chochote cha ziada cha kumhofia aliona labda kujiamini kwa liam anaweza kua anatoka katika familia ya kitajir au yenye wazfa flan uko nje ya nch maana alikua na taalifa kua mtu kuyu ni leo hii ndio ameingia Tanzania hivyo alijiambia kama ni hivyo ilimladi amli ya kumkamata imetoka kwa mkubwa wake hatokua na kosa kama mambo yatakwenda ndivyo sivyo

Hey bwana mdogo usifanye mambo kua magubu tafadhali ongozana na sisi. Alisema inpecta Mshindo

Liam alijisemea kimoyo moyo nisiku yake ya kwanzatu alipanga kuitumia kwa kupumzika lakini watu hawa wamekuja kumuhalibia usingizi wake. Ata hivyo aliona acha tu akubali kuondoka nao ukizingatia ndio kwanza qmeingia nchini

Liam Akasimama, akavaa t-shirt aliyokuwa ameitelekeza kwenye sofa.

Watu wale walikaa kimya. Walimchunguza kwa macho. Kuona aanataka kufanya nini Hakukuwa na dalili ya uoga — si kwa sura, si kwa sauti, si kwa miili.

Liam Aliinama kuchukua simu, kisha akawatazama.

“Oke Twende basii.” alisema liam uku akitabasam na kuanza kuongoza njia na watu wale walimuweka katikati kama kumlinda

Wakiwa kwenye lifti, Evans Mshindo alimtazama kwa pembeni.

“Unajua kwanini tumekukamata ,?”

Liam akashtua bega lake kidogo kwa kebehi.

“afande sasa mimi ntajuaje. Alisema liam na kumfanya afande au inpecta Mshindo kukaa kimya

Walipofika chini, gari jeusi aina ya Prado lilikuwa tayari likisubiri. Mlango ukafunguliwa, Liam akaingia kwanza, kama anaalikwa kwenye cocktail ya Waziri wa Mambo ya Ndani. Askar wawili waliingia pia nyuma na kumuweka liam kati kati

Liam Akaangalia wale maofisa, kisha akawauliza:

“By the way... mnaonaje tukisha fika mniagizie budget ya kahawa? Alisema liam uku akitabasam

Askari wale kusikia hivyo Mmoja akacheka kimya kimya. Evans Mshindo hakusema kitu. Lakini alijua moja:

Mtu huyu si wa kawaida. Kutokana na uzoefu alio kua nao

Baada ya dakika kadhaa gari lilisimama mbele ya jengo la ghorofa lenye ulinzi mkali. Ilikuwa ni moja kati ya vituo vya siri vya usalama vilivyojificha katikati ya jiji ambapo ni ngumu kudhania kua jengo hilo ni la usalama,

Walipomshusha, Liam alishuka taratibu kana kwamba alikuwa anashuka kwenye zulia jekundu la Golden Globes. Akaangalia jengo, akakunja uso kisha akasema:

“Aise hii ni mala yangu ya kwanza kukamatwa na akari duu nakupa hongela sana bana kishindo. Alisema liam huku akitabasamu liam alikua akifanya makusuki kumuita afande huyo kishindo ili kumkela tu lakini bwana huyo alionekana kua mtulivu

Waliingia naye ndani kimya kimya. Baada ya kuingia walikutana ka kordo ndefu walitembea kidogo na kukunja kushoto wakatembea hatua kadhaa na kukutana na mlango waliingia na kutokea seemu iliyo onekana kua ni mapokezi

Na upande wakulia wa mapokezi kulukua na lift na walitembea kuisogelea na walimuamulu Liam kua wa kwanza kuingia na wao walifata lift ilianza kushuka chini na kitendo kile kilinfanya Liam kushanga kwake yeye alitalajia wangepanda juu lakini ilikua ndivyo sivyo

Baada ya lifti kufunguka walitoka n walikutana na korgo nyingina ilikua ndefu na pembeni kulikua na milango ya vyumba walitembea mpaka mlango wa mwisho na walimuingiza liam liam kulikua na meza ilio tenganisha viti viwili

Adande Mshindo alimuamulu liamu kukaa kwenye kiti moja wapo alikaa nai wakamfunga pingu kwa kuunganisha na meza kisha walitoka na kumuacha liam pekeake

Liam alijiwazia walishindiwa nini kumfunga ping tangu wakiwa hotelin na kuishia kusikitika aliangaza huku na kuku na kuona camera ilio kua ikimmurika

Muda mfupi baadaye, mlango ulifunguliwa na afisa aliyevaa suti ya kijivu aliyekuwa na uso mkali na macho yasiyo na wasiwasi wa aina yoyote

"Jina lako kamili tafadhali." Alisema kwa sauti ya amri.

"Liam Carter," Alisema Liam kwa utulivu huku akiegemea kwenye kiti. "Lakini wengine huniita 'Tatizo lisilopimika'."

Afisa hakutabasamu. Alichukua daftari lake na kuanza kuuliza maswali.

"Ulikuwa ukifanya nini Lush Bay Hotel usiku huu?" Alisema kwa ukali.

"Nilikuwa nikijaribu kupumzika baada ya safari ndefu ya maisha." Alisema Liam kwa kejeli.

"Unafanya kazi gani hasa?" Alisema afisa mwingine aliyekuwa nyuma ya kamera.

"Mimi ni mpelelezi wa ndoto zangu." Alijibu Liam huku akitikisa kichwa, "Na ninafanya kazi kwa niaba ya amani ya ndani."

Afisa wa kwanza aligonga meza kwa hasira. "Huu sio mchezo, Carter. Tuna taarifa zako. Tumeona hakuna rekodi zako zozote zaidi ya kua ulizaliwa Tanzania na uliondoka hujulikani ulikua wapi na unafanya nini alisema afisa kwa kufoka

"Liam aliamua kua siliazi Basi mtafute taarifa zangu vizuri zaidi. Huenda Kuna watu katika serikalini yenu watakua na access zaidi ya ninyi." Alisema Liam kwa saut ya mkazo.

Kwa muda wa zaidi ya saa moja walijitahidi kumvuta Liam azungumze kitu cha maana, lakini kila jibu lake lilikuwa limejaa mzaha, kejeli au utulivu uliowachanganya. Hawakutaka kutumia nguvu kutokana na kuto kua vizibitisho vya moja kwa moja amri

Nyinyi mnacho fanya apa ni kua na makisio tu wala hamna ushaidi mnacho fanya ni kama kutaka mimi nikili kua muhalifu wakanti mimi laia mwema na nilicho afanya ni kuludi kwenye nchi yangu kama hali itaendelea hivi mnaonaje nikishilikisha mwanashelia mwangu. Alisema liam

Lakini kabla hajajibu, afisa mmoja aliingia haraka akiwa na bahasha mkononi. Alimsogelea mwenzake na kunong'ona nae kwa haraka.

Wakamwangalia Liam kwa mashaka.

"Vipi tena?" Alisema Liam huku akiinama mbele kidogo,

Afisa wa pili aliufungua mdomo kwa shingo upande. "Bwana liam.. Inaonekana hakuna ushahidi wa kutosha wa kukushikilia. Lakini nikupe angalizo kila atua unayo piga tuko nyuma yako

"Asante sana ma afande" Alisema Liam kwa furaha ya dhihaka, "Ningetaka chai lakini sasa muda umeisha."

Alifunguliwa pingu na kuiinuka kutoka kwenye kiti, kisha walimuongozo kuelekea mlangoni.

"Tutakuwa tunakufuatilia nyendo zako hivyo kua makini." Aliongeza afisa wa yule

"Oka afande nawatakia kazi njema Fuatilieni kwa makini.

Ilikua ni majila ya saa7 usiku ndio muda ambao liam Alipotoka nje, aliangaza anga la jiji lililokuwa na mwanga hafifu ulio sababishwa na taa zilizo kua zikiwaka. Akavuta pumzi ndefu, macho yake yakitulia alitembea mdogo mdogo hakua akijua mtaa aliopo kutokana na kua sio mzoefu sana wa jiji baada ya ya kutembea kwa umbali kadhaa aliweza kuona taksi alisimanisha na kuingia

 
Baada ya muda aliweza kufika hotelini alikua amechoka sa mizunguko na pulikushani zilizo tokea siku hiyo hakuitaji kufanya jambo lolote zaidi ya kujipumzisha



Ilikua ni Asabuh aliangalia saa ilikua ni mida ya saa5 asubuh Hakuwa na mawasiliano mapya. Simu yake ilikuwa kimya kama hakukua na mtu alie mtafuta. Lakini sasa, hakuhisi kukasirika wala kukosa subira.



Alibofya kitufe cha simu ya mezani, akapiga huduma ya chumba.



“Naomba kuletewa kifungua kinywa



Dakika kumi baadaye, mhudumu akaleta. Liam akatapa kifungua kinywa polepole huku akitazama bahari kupitia dirisha. Baada ya kula, alihema kidogo kwa furaha,



“Baada ya kumaliza aliona kuendelea kuka ndani ataboeka ivyo alifikilia angepata ata mtu wa kumpa kampani



Mara moja akamkumbuka yule msichana wa mapokezi – mwenye tabasamu la dhahabu, macho makubwa ya kuvutia na sauti tamu yenye vionjo vya pwani. Edina.



“Why not?” Alinong’ona kwa sauti ya kicheko, akajipiga kiganja begani na kutoka chumbani akiwa na shati la mikono mifupi na suruali ya khaki nyepesi.



Alifika mapokezi na alipo angaza aliweza kumuona Edina aliekua akimtafuta mwanamke huyo hakua akiudumia hivyo alitombea kumsogelea mrembo huyo



“Hey, Mrombo Edina... unanikumbuka?”



Edina alitabasamu kwa aibu kidogo, lakini akajibu kwa haraka.“Yaa siwezi kukusahau,.”



Liam alicheka.



“Ok mi nimngeni aapa nchini Nilihitaji tu... ah, ulafiki. Unaweza kua rafiki yangu?” alisema liam



“sawa hakuna shida ivi ulisema unaitwa nan vile?” Alisema Edina kwa ucheshi.



Jina langu ni liam. Alijibu uku akitabasam



Vip tunaweza kutembea tembea kidogo . Aliuliza Liam



kutokana na zamu yake ilikua imeisha na likua huru hivyo alikubali mara moja



Walitoka nje ya mapokezi, wakakaa kwenye bustani ya hoteli, pembeni ya mwanga mdogo wa taa. Edina akiwa na sare yake ya kazi, Liam akiwa kama vile anatoka kwenye onyesho la mitindo ya jioni.



“Wewe ni mzuri kupita kiasi kuwa mapokezi tu, Edina. Hakika mtu atakayekupoteza atakua kipofu wa moyo.” Alisema Liam huku akimtazama kwa jicho la dharau ya kupendeza.



“Wewe ndio mgeni pekee ambaye anaongea kama mwanasiasa wa mapenzi.” Alijibu Edina huku akicheka.



“Usinibebe vibaya, Edina... mimi ni mtu wa ukweli. Nimezunguka dunia, lakini tabasamu lako linaweza kufanya mtu asahau hata nywila ya benki.”



Edina alijigeuza kidogo, akajifunika uso kwa mikono yake.



“Usinifanye nicheke ka sauti kali, manager ataniona kama nimechanganyikiwa.”



Mazungumzo yao yaliendelea kwa dakika zaidi ya arobaini. Waliongea kuhusu Dar es Salaam, vyakula, vichekesho vya wateja, na hata tofauti ya chai ya Tanganyika na kahawa ya Colombia.



Ilionekana kama marafiki wa zamani waliokutana baada ya miaka mingi.



Mazungumzo yalichukua muda mrefu kidogo, Liam alisimama na kusema:



“Sikujua Dar ina watu wa dhahabu... mpaka nikakuona. Nashukuru sana kwa muda wako, Edina. Leo nimeinjoy sana compani yako... alisema liam”



“Nami nimefurahi kukujua zaidi.” Alisema Edina kwa tabasamu.



“Ni mwanzo tu... nina mengi ya kushangaza.” Alijibu Liam.



Waliagana kwa tabasamu. Edina akarudi kazini, Liam akarudi ghorofani.



Ni takribani wiki ilipita tangu Liam aweze kuingia nchini Tanzania na katika wiki yote mtu ambae alikua kama mwenyeji wake alikua ni edina dada wa mapokezi wiki hiyo liam aliitumia kujipa uzoefu na kutembelea baadhi ya maeneo ili kuuzoea mji



Ilikua ni usiku wa juma tano mwajila ya saa2 usiku



Liam aliamua kutoka hotelini, akahisi kuchoka na mpangilio wa kawaida. Hakutaka kwenda klabu wala baa; alitaka kutembea na kufikiri. Liam alikua mtaa wa Mwenge, karibu na sehemu za viwanda ambazo huwa tulivu usiku.



Alikuwa amevaa sweta nyepesi ya kijivu na kaptura ndefu. Aliingia katika mtaa mmoja wenye giza hafifu, taa chache zikipepesa pepesa mithili ya roho zinazokufa.



Wakati alipoanza kukata kona ya pili, hewa ilibadilika.



Haikuwa hewa ya kawaida.



Ilikuwa nzito—kama mvuke wa barafu unaopanda juu ya ngozi na kuchoma mishipa.



Akasimama. Hakuhitaji kuambiwa. Alihisi uwepo wao. Ilikua ni muda tangu alipo isi anafuatwa na watu walio kua wanamfata walikua si wa kawaida uwepo wao aliuhisi muda ndio maana akaamua kuchakua uelekeo ambao ni tulivu na hauna watu



Kutoka gizani, watu wanne walijitokeza, wote wakiwa wamevalia mavazi meusi, vinyago vya ajabu vinavyong’aa kwenye paji la uso, na macho yao yakimetameta mithili ya moto wa bluu. Haikueleweka walikua ni watu wa bala lipi kutokana na mavazi yayo yalikua yamewafunika mwili mzima ila watu wale waliongea kiswahili fasaha



“Liam Carter,” mmoja wao alisema kwa sauti ya kina na baridi. Tume pata taalifa kua wewe ndio mtu unae miliki Luminark hivyo kwa usalama wako tupatie nasi tunaadi kuacha hai vinginevyo usije kutulaumu



Liam alitabasamu kidogo, kisha akavuta pumzi ndefu.



“Luminark? Kwa hiyo nyie ndo mmefuata hicho kitu?”kwani hiyo Luminark ni nin maana ndio mala ya kwanza nasikia kutoka kwenu liam aliongea kwa utulivu wa ajabu.



Mmoja wao akasema kwa kejeli bwana mdogo kama hutotupatia tunacho hitaji usifikilie kama utatoka salama hapa



“Tutakichukua kwa lazima



“Ooh Basi sikilizeni ikiwa mnaamini kua mimi ndie ninahiyo Luminark basi msifikilie kua kuwa nitawakabidhi kilahisi. Ni lazima mniue kwanza ndio mchukue. Alisema liam



Bwana mdogo kwakua unajifanya mjeuli basi tutakuonyesha. Alisema mmoja wa wale watu



“Basi karibu... mjaribu bahati,” alijibu Liam uku akiwa na tabasamu.



Walijirusha kwa kasi ya ajabu. Mmoja akaenda juu, mwingine chini, wawili wakizunguka pande zake. Mikono yao ilianza kutoa nuru za ajabu, mithili ya nishati ya giza iliyochanganywa na moshi wa kung’aa.



Liam hakusogea hata kidogo lakini Alifunga macho sekunde moja, kisha akafungua tena — macho yake yakawaka kwa mwanga wa hudhurungi yalio kua yakin'gaa kwenye giza.



Alipoona wa kwanza akimfikia, aligeuka kwa kasi isiyo ya kawaida, akampiga ngumi iliyozalisha miale ya rangi nyekundu. Yule mtu akarushwa mita kadhaa na kuanguka kama gunia na papo hapo mwili wake ukaanza kuganda... Sekunde tatu baadaye, alibadilika kuwa jiwe jeupe linalong’aa kama almasi na kupasuka vipande viwili.



Mwingine akaruka kutoka juu, akizalisha miale ya moto uku mkononi akiwa na upanga mweusi ulio kua unatoa mwanga mweupe uliochanganyika na miale ile ya moto na kuufanya kua wenye kuvutia. Liam alikwepa na kuushika ule upanga mikononi mwake, kisha akauvunja vipande viwili kana kwamba ulikuwa ni fimbo na pale pale alikishika kile kipande chaupanga na kumchoma yule mtu kwenye shingo kisha akamsindikiza na teke lililo mmlusha mita kadhaa. Akaanguka chini kwa kishindo... na sekunde mbili baadaye — naye pia akabadilika kuwa jiwe la kung’aa.



Watu wale walipigwa na butwaa kwa mtu uyo kuwaua kwa shambulizi mojamoja na kingine kuvunjwa kwa upanga kwani upanga uo si kwamba ni wa kawaida bali ni mgumu sana na ngingumu kuvunjika ukichangana na nguvi ya ajabu ulio kua nayo walishangaa kwa liam kuweza kuuvuja na pale pale waliona mtu walie mfata si lahisi kama walivyo zani



“watu dhaifu kama nyinyi mnathubutu kujitokeza mbele yangu na kutaka Luminark. haha hakika mnaflaisha sana. Alisema liam kwa tabasamu



Waliobaki wawili wakaanza kushirikiana—walianza kuongea lugha isio eleweka, walikua wanamzunguka liam kwa kasi, na kufanya duara la moshi uliochanganyikana na miale inayo ng'aa wenye nguvu kumzunguka pia. Liam hakutaka kusubili wamalize kile wanacho kifanya hivyo pale pale, alinyanyua mkono wake wa kulia juu, na mkono wake ukang'aa — na kwa ghafla mwanga mkali ukapasuka kutoka mwilini mwake, ukafagia hewani, ukiyakata mawimbi ya giza kama upanga.



Ardhi ikapasuka kwa mlipuko wa mwanga huo na watu wale walikunbwa na wimbi la nguvu isiyo ya kawaida na kuwafanya kulushwa mita kadhaa



Wote wakaanguka chini, wakitetemeka. Liam akawaangalia akiwa amesimama juu ya kifusi cha vumbi lililotanda.



Hatimae pakawa Kimya Giza lilitulia tuli



Liam aliangalia kwa sekunde chache miili ya watu wale iliokua imegeuka mawe yanayong'aa mithili ya armas. akavuta pumzi ndefu. Na pale pale kwa sauti ya chini, alianza kunong’ona maneno yasio eleweka kugha yake.



Palepale miili ile ilio kua imegeuka mawe pamoja na Vipande vyote vilivyo zagaa vilianza kuyayuka kisha taratibu vikaondoka hewani — vikayeyuka kama moshi wa nuru, vikatoweka bila hata chembe ya ushahidi.


Kisha liam aliyafumba macho yake yalio kua bado yanatoa mng'ao na baada ya kuyafumbua yalikua yameludi katika hali ya kawaida


ITAENDELEA

Ukiitaji kuendelea bila kusubili hapa bonanza link hii utaipata kwa halaka - SEHEMU YA 3: Makazi ya Kivuli
 
SEHEMU YA: 3

Nguvu walizokuwa nazo wale watu waliomvamia Liam zilitokana na kiapo cha kale cha giza kilichoitwa “The Veil of Umbros” — agano la kale la wachache waliotamani nguvu za haraka kwa gharama ya nafsi zao.


The Evil Umbros ilikuwa ni mkataba wa kipepo uliosainiwa na roho zao mbele ya mwanazuoni wa giza aitwaye Kael’Thun, zaidi ya miaka 300 iliyopita. Agano hilo lilitoa nguvu zisizo za kibinadamu — nguvu za kasi, uzito wa miguu mithili ya chuma, na uwezo wa kushambulia kwa moshi wa giza,, moja kati ya kanuni za nguvu zao


"Wakishindwa kupambana au kujeruhiwa vibaya, mwili wao huzuiwa kurudi kuwa wa kawaida.


Pia Wakifa, mwili wao unageuka kuwa jiwe la kipekee — liitwalo “Garnyx Stone” — ambalo linahifadhi sehemu ya nguvu za agano hilo.


Kwa hiyo, wale watu waliomvamia Liam walikuwa ni watu kutoka kundi linalo tokea Korea liitwalo “The Covenant of Nyx,” kundi la giza lililoingia agano la The Veil of Umbros, wakitumika kama watendaji wa kazi chafu za kutafuta vitu vya kale— ili wapeleke kwa mabwana wao.


Sababu ya wao kugeuka mawe: Agano hilo liliwalinda dhidi ya kifo cha kawaida, lakini pia liliwatia laana ya milele: wakifa, roho zao hushikwa ndani ya mwili uliogeuka kuwa jiwe, ili wasiweze hata kuingia kuzimu au kuishi tena.


Na kwa vile miili hiyo ya mawe huhifadhi chembechembe za nguvu, makundi ya giza hujaribu kuyachukua tena na kuyatengeneza upya kwa uchawi wa kale.


Liam alikua na uzoefu na watu wa aina hiyo kwani sio mara yake ya kwanza kukutana na watu wa aina hiyo hivyo alijua namna ya kudili nao kilahisi ndio maana hawakumpa.shida pia alijua njia ya kuharibu kabisa Garnyx Stone — kwa kutumia maneno ya kale ya Nadharia ya Mwisho (Final Doctrine), ambayo huharibu chembechembe zote za uchawi zilizobebwa na miili ile baada ya kugeuka mawe


Ila watu kama hao pindi wanapo kutana na watu wa kawaika ata kama wanamafunzo ya kimapigano kiasi gan ningumu sana kuwashinda


Usiku huo Liam aliludi Hotel akiwa ametulia kimya. Walinzi wa lango walimfungulia bila kuuliza chochote. Mvua ndogo ilikuwa imenyunyiza barabara za Masaki, ikiacha sakafu ya vioo kwenye maegesho ya magari.


Alipofika ukumbini, akajielekeza moja kwa moja kwenye mgahawa wa hoteli. Alikaa kwenye kona ya ndani, karibu na dirisha lililotoa mwanga mwepesi wa taa za barabarani. Alijitakia sahani ya wali wa nazi na samaki


Wakati akila, hakuwa na wasiwasi tena. Moyo wake ulionekana kuwa katika hali ya utulivu wa ajabu, licha ya yote yaliyotokea masaa machache kabla.


Alipomaliza kula, akapanda juu chumbani kwake. Akajimwagia maji ya moto bafuni, kisha akavaa tracksuit na kujilaza kitandani. Mwili wake ulikuwa umechoka, lakini akili yake ilikuwa bado inachakata. Licha ya kelele za maisha za Dar es Salaam nje ya dirisha lake, yeye aliishi ndani ya kimya chake.


“Dar es Salaam… ni jiji linalocheka, lakini lina mengi linayoficha,” alijinong’oneza kabla ya macho kufunga.


----------


Siku iliyofuata, jua lilipoanza kupenya kwenye mapazia ya chumba chake, Liam aliamka mapema. Alioga, akavaa fulana nyeupe safi, suruali ya kitambaa laini, na viatu vyepesi vya ngozi.


Alishuka chini kwa kifungua kinywa,alikutana na Edina — msichana wa mapokezi — alimsalimia kwa tabasamu pana.


“Habari za asubuhi, Liam,” alisema Edina kwa sauti yenye uzuri wa kawaida.


“Habari nzuri Edina. Sijui kama ni wewe au kahawa zenu, lakini kila nikikuona nahisi siku yangu inaanza vizuri,” alisema Liam kwa utani.


Edina alicheka, akatikisa kichwa.


“Utaanza kunibebesha majivuno sasa.”


“Majivuno yanastahili mrembo kama wewe mwenye tabasamu la dhati,” alisema Liam huku akimkazia macho, lakini kwa namna ya utulivu.


Baada ya kifungua kinywa, Liam aliamua kutoka nje, kutembea kidogo katikati ya Masaki. Aliingia kwenye maduka kadhaa, akanunua miwani ya jua, fulana mbili, na kikombe cha kahawa katika duka moja dogo la pembeni ya barabara.


Alitembea hadi Coco Beach, akakaa kwenye mnazi, akatazama bahari. Alizungumza na vijana wawili waliokuwa wanauza mishikaki.


Liam alikua kashaanza kulizoea jiji — si kwa macho ya mgeni tena, bali kwa moyo wa mtu anavyojitafuta. Siku nzima aliimalizia akiwa Beach


Jiji lilimzoesha, lakini hakuweza kuzoea kukaa bila kufanya jambo lolote. Licha ya ukweli kwamba alikuwa na pesa ya kutosha kuendelea kuishi maisha ya kifahari katika Lush Bay Hotel ya Masaki, moyoni alihisi shimo tupu — kama roho yake ilikua inahitaji kitu zaidi ya starehe: kitu cha kufanya. Kitu kitakachomfanya ahisi tena.


Aliporudi hotelini usiku mmoja baada ya kutoka matembezini, aliingia moja kwa moja chumbani, akafungua laptop yake kuangalia habari za hapa na pale. Wakati huo, hakutafuta chochote maalum. Lakini kama kawaida ya ulimwengu wa leo — kila mtu hufuatiliwa — tangazo moja lilijitokeza upande wa kulia wa skrini yake, kwa sauti isiyoandikwa bali inayoonekana kusema: “Looking for something real?”


Tangazo hilo lilionyesha picha ya walinzi waliovaa sare nadhifu, wakiwa na nembo iliyoandikwa “ Royal Shield Security” — kampuni ya ulinzi binafsi. Chini yake, maandishi yalisomeka:

“Do you have what it takes to stand between danger and safety? Join Royal Shield Security.. We’re not just guards, we’re guardians.”

Liam alicheka kimya kimya.


"Guardians? Mko mbali sana na ninacholinda mimi." Alisema Liam kwa kejeli ya taratibu, lakini alihisi mvuto wa ajabu kuelekea tangazo hilo.


Aliibonyeza link. Tovuti ilifunguka. Kulikuwa na fomu rahisi ya maombi ya kazi, maelezo mafupi kuhusu kampuni, na kigezo cha kuwa “mwenye uwezo wa kipekee wa kutambua hatari na kushughulika nayo kwa weledi na usiri.”


Alikaa kimya kwa sekunde kadhaa, macho yake yakisoma mistari ile bila kuyumbisha.


"Inaonekana dunia hii haiko tofauti sana na ile niliyozoea... watu bado wanahitaji kulindwa." Alisema kwa sauti ya kutafakari.


Hata hivyo, hakuwa tayari kujiingiza haraka. Kama kawaida yake, Liam hakufanya maamuzi ya papara.


Aliifunga laptop na kulala kifudifudi kitandani, macho yakitazama dari huku masikio yake yakisikiliza sauti ya kiyoyozi na kelele za mbali za magari ya barabarani.


Ilikua ni Asabuh, jua la Dar es Salaam lilichomoza taratibu likiangaza kuta nyeupe za Lush Bay Hotel. Kwenye ghorofa ya tano, Liam Carter alikuwa tayari ameshaamka. Akiwa amevaa t-shirt nyeupe na suruali fupi ya kijani kibichi, alikaa kwenye meza ya kona ya chumba chake, kikombe cha kahawa mkononi na laptop mbele yake.


Aliikumbuka tovuti aliyoiangalia usiku uliopita — Royal Shield Security. Bila kusita tena, aliiwasha laptop na kufungua ukurasa ule ule. Safari hii hakusita. Akaingia moja kwa moja kwenye fomu ya maombi.


Aliandika jina lake:


Liam Carter.


Tarehe ya kuzaliwa?


Akaleta tarehe ya kubuni — iliyomfanya aonekane kama kijana aliyekomaa lakini bado mwenye nguvu.


Uraia?


Tanzania


Uzoefu?


Hapo ndipo alipotulia kidogo, macho yake yakikodolea sehemu ya "Experience in Security or Military Background."


"Kwa kuwa huu ni mchezo wa kivuli, ni lazima nivae kivuli hicho sawasawa." Alisema Liam kwa sauti ya kujinong’oneza.


Liam kutokana na kuanmtaalam aliamua kufoji vitu vingi kupitia koneshen zake aliweza kufoji kua aliwahi kua mwanajeshi wa nchi ya malekani


Aliendelea kuandika kwa ufasaha kana kwamba alikuwa ameishi hayo maisha. Kwa namna alivyoandika, hata mtu mwenye akili ya kuchambua wasifu angeamini. Alimalizia fomu kwa kuambatanisha picha ya pasipoti (ambayo pia ilikua ya bandia lakini yenye uhalisia wa hali ya juu), kisha akabonyeza SUBMIT.


Kompyuta ilitoa mlio wa “Ping!” na ukurasa mpya ukajitokeza:
Liam alicheka kidogo.

Thanks for application Mr Carter Our recruitment team will review your submission and contact you shortly

"Wakijua ukweli, watanitaka zaidi — si kunikataa." Alisema Liam huku akiinyanyua kahawa yake na kunywa kwa utulivu.


Aliinuka, akafungua pazia na kuangalia bahari kwa mbali, macho yake yakimetameta kwa utulivu wa mtu asiyeeleweka kiurahisi. Hakuwa amejaza fomu ya kazi kwa sababu ya pesa. Alikuwa anatafuta kivuli kipya cha kuishi ndani yake — na kwa sasa, kazi ya mlinzi ilimfaa kwa kuendelea kuzugia na angalau itamfanya kua bize


Baada ya kutuma maombi ya kazi ya ulinzi, Liam Carter alijiegemeza kwenye kiti chake akitazama skrini ya laptop kwa muda. Akavuta pumzi ndefu, kisha akakunja vidole vya mikono yake kama mtu anayefikiria jambo zito.


"Kama nataka kuishi maisha ya kawaida... siwezi kuendelea kuishi hotelini milele Alinong’ona


Alichukua simu yake na akaingia mtandao pedwa wa Instagram nakuamua kutafuta dalali wa nyumba lakinai aliwezq kukutana na kampuni inayo jihusisha na uuzaji wa nyumba hivyo Alifungua programu ya WhatsApp Business ya kampuni ile, akaandika ujumbe moja kwa moja kwa wakala:

Hello I'm looking for a luxurious house to purchase in Dar es Salaam. Preferably private, spacious, and secure. Budget is flexible. Contact me as soon as possible.

Dakika tatu baadaye, akajibiwa:

Karibu sana Haraka Realty. Tunaweza kukusaidia bila tatizo. Tutahitaji baadhi ya taarifa zako na pia kukutumia chaguo chache za nyumba kulingana na vigezo vyako. Tuanze na location gani unapendelea?

Liam akaandika:

Somewhere serene but close enough to the city. Masaki, Oysterbay, or even Bahari Beach if the property is right.

Simu yake ikatoa mlio wa video na picha — nyumba tatu za kifahari zenye uzio wa kisasa, mabwawa ya kuogelea, maegesho ya magari manne, na bustani za kijani kibichi. Moja yao ilikuwa ya kuvutia hasa. Ghorofa mbili, mlango wa mbele wa glasi nzito, na veranda iliyoangalia bahari.


Aliitazama kwa makini.


“Hii inaweza kuwa ngome yangu kwa muda.” Alisema kwa sauti ya chini.


Kisha akaandika:

That third one. I want to view it in person. Can we schedule it for tomorrow morning?

Absolutely. We’ll send one of our agents to pick you up from your location. Just share the details.

Liam alitabasamu. Hatua kwa hatua, alianza kujenga kivuli kipya cha maisha. Sehemu ya kuishi. Kazi (angalau kwa jina). Na taratibu, mizizi ya historia mpya ilianza kuchomeka katika ardhi ya joto ya Dar es Salaam.


**********************


Kesho yake, Liam aliamka mapema kabla hata ya jua kuchomoza vizuri. Alivaa shati nyeupe safi na suruali ya khaki, akavaa miwani yake meusi na viatu vya ngozi vilivyoonekana kama vile havijawahi kukanyaga vumbi. Saa moja kamili, ujumbe uliingia kwenye simu yake kutoka kwa wakala wa Haraka Realty:

Good morning Mr. Carter. Our agent is on the way to pick you up. ETA: 10 minutes.

Liam aliteremka chini ya Lush Bay Hotel akiwa mtulivu. Edina alikuwa zamu ya mapokezi, akamtazama kwa macho ya udadisi.


“Una safari ya mapema leo?” Aliuliza kwa tabasamu.


“Kidogo tu. Nataka kuona kama Dar inaweza kuwa nyumbani,” alisema Liam kwa sauti ya utulivu, kisha akaondoka bila kuongeza neno.


Gari jeusi aina ya Toyota Land Cruiser V8 lilimsubiri nje. Mtu mmoja wa kiume, mwenye suti nyeusi, akashuka na kumfungulia mlango.


“Mr. Liam? I’m Raymond from Haraka Realty. Karibu.” Alisema kwa sauti ya kutolidhidhwa na liam


Safari haikuchukua muda mrefu. Kwa maana seemu ambayo nyumba hiyo ilikuepe ni masaki hapo hapo. Mwisho walifika kwenye geti kubwa la kijani, lililokuwa na alama ya metali: “Villa Nyota.”


Geti lilipofunguliwa kwa rimoti, gari likaingia taratibu ndani.


Nyumba aliyokuta... haikuwa ya kawaida.


Ilikuwa ni gorofa la ghorofa mbili lililosimama kwenye ekari moja ya ardhi. Juu ya paa lake palikuwa na balcony pana inayoangalia bahari. Mlango wa mbele ulikuwa wa mbao nzito ya mninga, ukifunguka kwa mzunguko mlegevu wa kisasa. Sakafu ya ndani ilikuwa ya marumaru meupe yaliyong’ara, ukuta ukiwa na uchoraji wa sanaa ya Kiafrika na viti vya kifahari vya ngozi.


Kulikuwa na vyumba vitano vikubwa, kila kimoja kikiwa na bafu lake binafsi. Kulikuwa pia na studio ndogo ya ndani, ofisi, chumba cha mazoezi, na basement ndogo ya starehe.


"Nimewahi kulala hotelini, lakini hapa... hapa panapumua." Alisema Liam kwa utulivu, macho yake yakizunguka chumba kikuu cha wageni.


Raymond akacheka. "Ni mojawapo ya nyumba bora tulizonazo. Imejengwa kwa mteja aliyeghairi kununua dakika ya mwisho. Unaweza kuichukua kwa urahisi."


"Sijawahi kupenda nyumba ya mtu mwingine hivi." Alisema Liam. "Nipe siku mbili. Nikimaliza mambo yangu mengine, nitatoa jibu."


Raymond akatikisa kichwa kwa heshima"Tunaweka pending kwa ajili yako mr liam"


*******


Siku mbili baada ya kutembelea nyumba hiyo ya kifahari katika eneo la masaki, Liam Carter aliamua kuichukua. Alikutana na Raymond, wakala wa Haraka Realty, katika ofisi yao iliyopo Ostabei. Baada ya kusaini makubaliano na lasmi liam kua ndio mmiliki wa jumba hilo liam alitumia takriban dola laki 5 kununua nyumba hiyo


Liam, akiwa na utulivu wake wa kawaida, wakati wa kukamilisha makubaliano ya nyumba. Alijua kuwa ili kuendelea na maisha yake mapya, alihitaji kuwa makini na kila hatua anayochukua, kuhakikisha kuwa anadhibiti taarifa zinazomhusu na kudumisha taswira ya mtu wa kawaida


ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 4
Ilikua ni siku ya jumamosi jion Jua lilikuwa limeanza kupinduka wakati Liam Carter alisimama mbele ya mlango mkuu wa nyumba yake mpya iliyoko Masaki. Hii ilikuwa ni siku ya kihistoria kwake—siku ya kuhamia rasmi kwenye makazi aliyoyanunua siku chache zilizopita.


Nyumba hiyo ilikua na kila kitu na baadhi ya sehemu ambazo liam hakuvutiwa nazo aliwaambia wamlekebishie sikuile wanafanya makubaliano ya kuinunua


Hakuwa na msafara, wala hakukuwa na kelele za wajakazi au magari ya mizigo. Alikuwa yeye peke yake, na begi moja tu la mgongoni. Kwa mtu mwingine, hili lingeonekana kama maigizo au ufukara wa ghafla. Lakini kwa Liam, kila kitu kilikuwa kimetulia kwenye mpango alioujua yeye mwenyewe.


Mlinzi aliyekuwa langoni alimsalimia kwa heshima kubwa.


“Karibu tena bwana mkubwa. Tumekamilisha kila kitu kama ulivyoagiza.” Alisema mlinzi huyo, akifungua geti la kisasa lililokuwa limepambwa kwa alama ya kifahari ya L.


“Vizuri. Na zile kasoro nilizotaja?” Alisema Liam kwa sauti ya utulivu.


“Kila kitu kimewekwa kama ulivyo hitaji vitu vyote sasa viko sawa.” Alijibu mlinzi huyo.


Liam aliingia ndani akipitia njia ya mawe iliyoelekea kwenye mlango wa mbele. Nyumba hiyo ya ghorofa moja ilikuwa ya kuvutia – vyumba vitano vya kulala, sebule kubwa yenye dari la vioo, jiko la kisasa, ofisi ya ndani, bustani ya mbele na bwawa la kuogelea nyuma. Samani zote ziliwekwa tayari na zilionekana kutokea duka la kifahari.


Alipofungua mlango na kuingia ndani, akavuta pumzi ndefu ya hewa ya baridi ya kiyoyozi, halafu akalisogeza begi lake hadi kona ya sebule na kulitua. Akazunguka taratibu ndani ya nyumba, akitembea kwa utulivu kana kwamba alikuwa akisoma historia iliyojificha kwenye kuta.


Baada ya muda mfupi, alikwenda jikoni, akafungua jokofu, na kuchukua juisi baridi ya tikiti maji. Alikunywa glasi moja taratibu huku macho yake yakiwa yameelekezwa dirishani, akiangalia bustani iliyopambwa kwa taa ndogo ndogo za usiku.


“Hatimaye,” alisema Liam kwa sauti ya chini, “Sasa nimepata sehemu ninayoweza kuita nyumbani.”


Jioni hiyo, Liam akiwa kwenye nyumba yake mpya, alijilaza kwenye kochi kubwa la sebuleni, huku televisheni ikiwa imefunguliwa lakini macho na akili yake vikiwa mbali kabisa. Hakujua kama alikuwa anafikiria kuhusu kazi, maisha, au zile siri nzito alizozibeba moyoni. Lakini kabla hata hajazama vizuri kwenye mawazo yake, simu yake iliita.


Aliinua taratibu, akaangalia namba isiyojulikana, halafu akapokea.


"Hallo?" Alisema kwa sauti ya kawaida.


"Habari za jioni. Bwana liam napiga simu hii kutoka ofisi za Royal Shield Security


Tunapenda kukuarifu kuwa maombi yako ya kazi yamepitishwa kwa hatua ya awali. Tafadhali fika kesho saa mbili asubuhi kwa ajili ya usaili." Alisema sauti ya kike kwa sauti ya kirafiki lakini ya kiofisi.


Sawa, nashukuru kwa taarifa." Alijibu Liam kwa utulivu.


"Karibu sana. Ofisi zetu zipo maeneo ya Mikocheni, nyuma ya hospitali ya TMJ. Tafadhali hakikisha umevaa rasmi." Aliongeza sauti hiyo kabla ya kukata simu.


Liam alitabasamu kidogo. "Mwanzo mzuri." Alijinong'oneza


Alipomaliza, alipanda ghorofani kwenye chumba chake kikuu, akajilaza juu ya kitanda kikubwa chenye mashuka meupe ya pamba laini. Usingizi ulimchukua bila kupambana.


*****


Asubuhi ya jua tulivu iliangaza kwa upole kupitia madirisha ya gorofa aliyohamia Liam. Alikuwa ameamka mapema, kama kawaida yake. Alikua amevalia suti ya bluu, alisimama mbele ya kioo na kujitazama suti ile ilimpendeza sana mtu yoyote a gemuona na kusikia alikua akienda kwenye interview tena kazi ya ulizi asinge amini kabisa kwani Liam alionekana kama mwanamitindo ukizingatia na sura nzuri alio kua nayo hakuendana kabisa na kazi ya urinzi, kwa dakika kadhaa. Alijitazamu na kujikubali Uso wake ulikuwa mtulivu,


Alijichukulia pochi, simu, na bahasha ndogo iliyokuwa na nakala ya fomu ya kazi aliyotuma mtandaoni – ile aliyodanganya kuwa aliwahi kuwa mwanajeshi. Alitoka nje na kupanda taksi aliyoiita kupitia programu ya simu.


Njia yote ya kuelekea kwenye kampuni ya ulinzi, hakusema chochote. Macho yake yalitazama madirisha ya jiji kwa mbali, lakini akili yake ilikuwa mbali zaidi. Alikuwa anajiandaa kwa siku muhimu – siku ya interview yake ya kwanza nchini tangu kurejea Tanzania. Ata yeye alijishangaa imekuaje ameamua kutafuta kazi tena ya urinzi


Baada ya dakika 25, taksi ilifika mbele ya jengo la kisasa lenye maandishi makubwa: Royal Shield Security


Ni kampuni maarufu ya ulinzi binafsi jijini Dar es Salaam kampun hiyo ilijipatia umalifu kutokana na kusifika kua na walizi wenye mafunzo ya hali ya juu hivyo kupelekea watu mashuhuli, wafanya biashara wakubw, pamoja na baadi ya vigogo kuchukua walinzi kutoka katika kampuni hiyo, ukiachana na hivyo kampuni hiyo ilichukua watu wenye sifa maalum hivyo ili wakuajili ni lazima uwe na ujuzi wa mapigano ndio sifa ya kwanza walio zingatia. Liam baada ya kushuka kwenye taksi alikwenda adi getini na kugonga, Baada ya mlinzi wa lango kufungua alimkagua kwa macho makali na kumuuliza:


"Nikusaidie nini


"Niko apa kwa ajili ya interview?”alijibu Liam kwa sauti ya utulivu. “Naitwa Liam


Mlinzi yule alimluusu kuingia na Alipelekwa hadi kwenye sehemu ya mapokezi. Msichana wa mapokezi, aliyevalia sare za kampuni, alimkaribisha kwa tabasamu dogo na kumpatia kitambulisho cha muda. Kisha alimuonyesha sehemu ya kusubiri.


Liam alikaa kwenye sofa la rangi ya samawati lililowekwa pembeni mwa chumba, akisubiri. Muda mfupi baadaye, alisikia jina lake likiitwa:


“Liam Carter, tafadhali fuata mimi,” alisema kijana mmoja mwenye mwonekano mkali.


Akaongozwa hadi kwenye chumba cha mahojiano kilichopambwa na picha za mafanikio ya kampuni hiyo – picha za walinzi wao wakiwa kwenye kazi pamoja na viongozi wakubwa wa serikali na wageni mashuhuri.


Mezani waliketi watu wawili – mwanaume wa makamo aliyevaa suti ya kijivu, na mwanamke kijana aliyeonekana kuwa afisa wa rasilimali watu.


Watu hao baada ya kumuona liam waliingiwa na dharau na kua katika nyuso za kukatishwa tama


Kwani Liam hakua vile wao walivyo talajia. Ukweli ni kwamba takribani wiki mbili nyuma kampani hiyo iliweza kupokea tenda au odaa kutoka katika familia yenye nguvu na ushawishi mkubwa sana nchini familia hiyo ilihitaji bodyguard na vigezo ilivyo taka iliitaji bodyguard mwenye uwezo mkubwa wa dalaja la juu na aliitajika kwa ajili ya kumlinda memba mmoja wa wamilia hiyo sasa kwa kipindi hichi kampini hiyo haikua na bodyguard mwenye sifa ambazo familia hiyo iliitaji walio kuepo walikua ni wa kawaida sasa kampuni hiyo hawakutaka kuipoteza tenda kama hiyo ambayo ingewapa pesa nyingi na kuifanya kampuni yao kuzidi kupata jina kwani kufanya kazi na familia hiyo ilikua ni baati moja kubwa sana kwao hivyo hawakutaka kuiachia na kuona ikiangukia kwenye kampuni nyingine sas takribani wiki mbili walikua wakiangaika kutafuta mtu ambae atakae endana na sifa hizo wangeweza hata kutafuta mtu kutoka nje ya nchi lakini walipewa angalizo mtu anaeitajika awe mtanzania halisi muda walio pewa ulikua ni mchache sana sasa baada ya kupokea maombi na kuona sifa ambazo liam aliziweka matumaini yao yote waliyaelekeza kwa liam sas kitendo cha kumuona na muonekano wake waliingiwa na nyuso za kukata tamaa


Licha ya hayo yote waliamua tu kumkalibisha hivyo hivyo Liam Karibu sana, Mr Liam,” alisema mwanaume huyo kwa sauti ya mamlaka . “Tueleze kwa kifupi uzoefu wako katika masuala ya ulinzi au kazi za kijeshi.”


Liam alijibu kwa kujiamini. Alizungumza kwa utulivu mkubwa, akielezea jinsi alivyojihusisha na kazi za usalama kwa miaka kadhaa, akionyesha kana kwamba ni mtaalamu wa mapigano na silaha. Aliwasilisha kila kitu kwa ustadi, bila kuruhusu hata chembe ya shaka kuonekana.


Kwa jinsi alivyokua akiwajibu iliwafanya kuingiwa na imani nae ila hawakuamini moja kwa moja hivyo waliitaji kujilizisha kwa vitendo zaidi hivyo walimtaka kuona uwezo wake wa mapigano Liam hakua na shida hiyo walielekea katika chumba maalumu kwa ajili ya majalibia na uko Liam aliweza kuonyesha uwezo wa hali ya juu wa mapigano na kuweza kumlinda mtu qkiwa katika hatali yalikua ni mapigano ya kawaida tu. Waliweza kumfulahia sana Liam na kumkubali kutokanq na uwezo alio uonyesha


Masaa 4 mbele ndio Muda ambao intreview iliisha kwa heshima kubwa kabisa


“Tutawasiliana nawe ndani ya siku mbili,” alisema yule afisa wa HR kwa sauti ya uchangamfu na furaha kubwa sana


Liam alitoka nje ya jengo hilo akiwa mtulivu. Macho yake yalikuwa yamelegea kidogo, lakini ndani yake alijua alikuwa amecheza karata kwa usahihi. Alijua pia kazi hiyo ingeweza kumweka karibu na watu wa aina tofauti


Baada ya kutoka kwenye interview katika kampuni ya Royal Shield Security, Liam alirudi nyumbani kwake kule Masaki. Hali ya hewa ilikuwa ya utulivu, upepo mdogo ukivuma kwa upole kutoka baharini. Alifungua mlango wa sebuleni, akapita hadi jikoni kunywa maji baridi kabla ya kujilaza kwenye sofa. Alionekana kuchoka lakini bado mwenye akili iliyobeba tafakari nyingi.


Simu yake iliita. Alipotazama, aliona jina la Edina. Alishangaa kidogo, lakini akapokea kwa sauti ya utulivu.


“Haloo,” Alisema Liam.


“Liam, unamaanisha kabisa uliamua kuondoka bila hata kuniaga sasa kuna haja gani ya kua marafiki?” Alisema Edina kwa sauti yenye hisia zilizochanganyika na maumivu.


“Liamu kusikia lawama hizo alishidwa


Acheke ama alie. Nisamehe… sikupanga iwe hivyo.” Alijibu Liam kwa sauti ya pole.


“Kila siku ulikuwa ukishuka pale mapokezi, hata kama ulikuwa mtu wa kimya, nilikuzoea. Halafu ukaondoka tu ghafla kama mtu anayekimbia kitu.” Alisema Edina kwa sauti ya chini lakini yenye uzito.


Liam alikaa kimya kwa sekunde chache kabla hajajibu. “Nimekuwa nikijaribu kutuliza maisha yangu, Edina. Kulikuwa na mambo ambayo nilihitaji kuyakamilisha. Sikukusudia kukuacha bila taarifa.”


“Ulikuwa mtu wa tofauti, Liam. Ulikuwa mtu wa heshima, si wa kubadili mawazo ghafla… nilitegemea angalau ungeniambia.” Aliongeza Edina kwa sauti ya kukata tamaa.


“Nimekosea, na nakubali. Sikupaswa kuondoka hivyo.” Alisema Liam kwa ukweli.


Edina alikaa kimya kwa sekunde chache, halafu akasema kwa upole: “Sawa. Nimekuelewa. Lakini usirudie tena. Si watu wote wanaweza kustahimili ukimya wako.”


“Nitalikumbuka hilo,” Alisema Liam.


Simu ikakatwa kwa utulivu, lakini kimya kilichofuata kilibeba hisia nzito kwa pande zote mbili. Liam alibaki akitazama dari kwa mawazo mengi kichwani—akijua fika kuwa kila uhusiano anaojenga sasa, una msingi wa uongo aliolazimika kuishi nao.


*****


Upande mwingine jengo refu lenye vioo vinavyomeremeta lilisimama kwa fahari katikati ya eneo la kifahari la jiji, likionekana kutawala mandhari kwa sura yake ya kisasa na nembo iliyokuwa imechorwa kwa herufi za dhahabu: VELORA COMPANY . Ndani ya jengo hilo, froo ya 18, kulikuwa na ofisi ya kifahari iliyopambwa kwa mapambo ya bei ghali, maua safi yaliyowekwa kwenye vase ya kioo, na harufu ya marashi ya kifaransa iliyotamalaki angani.


Katika ofisi hiyo, kulikuwepo na msichana mwenye mvuto wa kipekee, umbo la kuvutia, ngozi laini yenye rangi ya kahawia iliyonyooka kama ya malkia wa kale. Alikuwa na macho ya kutazama kwa ukali lakini yakibeba busara ya ndani, mdomo uliochorwa kwa uangalifu na rangi ya waridi iliyowekwa kwa ustadi. Nywele zake ndefu zilikuwa zimefungwa kwa ustadi nyuma ya kichwa, na alivalia suti ya kifahari ya rangi ya navy blue iliyomkaa kama iliyoshonwa kwa ajili yake tu.


Ingawa umri wake haukuwa mkubwa—miaka isiyozidi 25—sauti yake ya kutembea, namna alivyotazama watu, na jinsi alivyotoa maagizo, vyote vilidhihirisha mamlaka, msimamo na nguvu alizokuwa nazo. Alikuwa ni Mkurugenzi Mkuu wa VELORA, kampuni kubwa ya biashara za kimataifa, teknolojia na mali zisizohamishika.


Msaidizi wake binafsi, mwanamke mwenye miwani na mkononi alishikilia baadhi ya mafaili, aliingia taratibu akigonga mlango kwa heshima.


“Samahani mkulugenzi ninajambo la kuwakilisha,” Alisema msaidizi huyo kwa sauti ya upole. “Kampuni ya ulinzi Royal Shield Security imetuma ujumbe asubuhi ya leo. Wanasema mlinzi binafsi anayekidhi mahitaji yako amepatikana, na wako tayari kupanga muda wa kukabidhiana kwa makubaliano ya awali.”


Msichana huyo mrembo alinyanyua kichwa chake taratibu, akimtazama msaidizi wake kwa macho makali lakini ya kutulia. “Kwa hiyo hatimaye wamepata mtu?” Alisema kwa sauti yenye mamlaka, bila kuinua sauti. “Nataka majina, rekodi zake, na siku ya kumpokea. Sitaki kupoteza muda wangu na mtu wa kawaida.”


“Ndiyo mkulugenzi. Nimeagiza faili lake lifikishwe mapema leo kutoka kwao.” Alijibu msaidizi wake kwa heshima.

“Vizuri. Nipe kila taarifa punde ifikapo mezani kwangu. Na usimwambie mtu yeyote kuhusu hili mpaka niamue mwenyewe.” Alisema huku akiangalia nje ya dirisha, ambapo jiji lilikuwa likisonga kwa mwendo wa kasi. Macho yake yakionekana kutazama mbali zaidi ya vioo vya jumba hilo—kana kwamba yalikuwa yakitafuta kitu ambacho bado hakijafika.


ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 5
Jengo refu la Velora Company lilisimama mithili ya mnara wa mamlaka katikati ya jiji. Sakafu ya mwisho, iliyozungukwa na kuta za kioo kilichochongwa kwa ustadi, ilihifadhi utulivu uliokuwa wa kipekee. Hapo ndipo alipokuwapo. Mwanamke ambaye hakuhitaji sauti ya juu kuamrisha, wala sura kali kuogopwa—macho yake yalitosha


Wengi walimtazama kama binti wa kizazi kipya—lakini ofisini, hakuna aliyeweza kumsogelea bila heshima ya hali ya juu. Alizoea kufanya maamuzi mazito akiwa ameketi mkao wa kawaida kabisa, kama mtu aliyekulia kwenye meza za wakuu wa dunia.


Wengine waliwahi kusema, “Mwanamke huyo si tajiri tu, labda ni kiumbe kutoka sayal nyingine.”


Wengine walimuita kivuli cha familia ya kifalme ya biashara.


Lakini kwa watu waliomjua kwa jina, waliita kwa sauti ya mchanganyiko wa hofu na heshima:


Diana.


Mlango wa ofisi yake ulifunguliwa kwa heshima. Msaidizi wake wa karibu, msichana mwenye umbo dogo na uso uliojaa nidhamu—Naila—aliingia kwa mala nyingine taratibu. Mikononi mwake alishikilia faili la samawati.


“Mkulugenzi,” alisema kwa sauti tulivu lakini thabiti, “hili ni faili kutoka kwa Royal Shield Security. lina taarifa zote.”


Diana aliinua macho kwa taratibu. Akamwangalia Naila bila tabasamu, lakini macho yale yalikuwa na maana elfu moja. Bila kusema neno, alinyosha mkono wake, na kulipokea faili kwa umakini.


“Walileta saa ngapi?” aliuliza, sauti yake ikiwa kama mvua ya usiku—tulivu lakini yenye uzito.


“.Ni Dakika chache tu zilizo pita. Wamesema kila kitu kiko ndani. Uhakiki, wasifu, rekodi na picha. Kama ukikubaliana, wanaweza kupanga utambulisho rasmi,” Naila alijibu kwa staha.


Diana alinyamaza. Alishika faili hilo kwa mikono miwili, akalisogeza mezani, lakini hakulifungua. Badala yake, aliangalia juu kidogo kama aliyekuwa akisoma maandiko yasiyoonekana kwenye dari la kioo.


“Naila,” alitamka kwa sauti ya chini lakini yenye mamlaka, “niachie hili hapa. Nitalipitia baadaye.”


“Una uhakika Mkulugenzi? Maofisa wa kampuni walionekana—”


“Nimekwambia nitalipitia baadaye,” alirudia kwa utulivu wa mtu mwenye utaratibu usiopingika.


Nila akainama kidogo, akatoka, akifunga mlango kwa uangalifu.


Diana alibaki peke yake. Ukimya ulitanda kana kwamba chumba kizima kilikuwa kikisubiri yeye afungue faili hilo. Lakini hakulifungua. Alilikazia macho tu, kana kwamba alikuwa akisubiri faili hilo lijifungue lenyewe.


Kwa sababu moyoni mwake… kulikuwa na hisia kuwa ndani ya faili hilo, hakukuwa na mtu tu—kulikuwa na tukio, sura, au kivuli ambacho kingebadilisha kila kitu.


Na kwa mara ya kwanza, jina lisilosikika likaanza kuchora mstari wa hatima kati ya nguvu, siri, na moyo wake wenye barafu.


*****


Siku hiyo liam mala baada ya kutoka kwenye ile interview alikua yuko tu nyumbani kutokana na kua mgeni hakua na malafiki wala mtu yoyote anae mfahamu zaidi ya Edina.Kwa siku nyingi sasa tangu arejee nchini, maisha ya Liam yamekuwa ya kimya. Alikuwa kama kivuli kinachopita mitaani bila kugusa ardhi. Aliishi kama mtu wa kawaida, kwa bidii akiepuka kujadili maisha yake ya zamani, hata na watu wachache waliomfahamu juu juu.


Lakini jioni hiyo, kuna kitu kilimsukuma. Labda ilikuwa hewa ya joto-joto yenye unyevunyevu, au ile kelele ya mbali kutoka kwenye bar ya jirani, au labda ni mwangwi wa ndani uliomwambia:


Akasimama taratibu, akakunjua mikono kama mtu aliyekuwa amepotea katika usingizi mrefu. Akaelekea bafuni, akaoga kwa maji ya uvuguvugu, akavaa suruali ya jeans nyeusi na fulana ya buluu yenye maandishi madogo ya kifaransa. Kiatu cha kisasa cha Nike alichokivaa kilikamilisha muonekano wake wa mtu ambaye hakuwa na haraka na dunia.


Alifungua simu yake, akaingia kwenye Bolt, na kuweka oda:


Wakati akisubiri, alisimama kwenye varanda yake ndogo, akinywa maji ya chupa, macho yake yakitazama magari yakipita taratibu barabarani.


Baada ya dakika saba, gari lilifika. Toyota Axio nyeusi iliyo safi. Dereva alimpigia honi fupi.


Liam taratibu, akafunga mlango wa nyumba yake, akapanda kwenye gari bila kusema mengi.


“Karibu boss,” dereva alimsalimu kwa heshima.


“Asante kaka nipeleke club yoyote ilio changamka ,” Liam alijibu kwa sauti ya kawaida.


Sawa hakuan shida boss," alijibu deleva huyo hakuonekana kua na maneno mengi kama ilivyo kwa madereva wengine


Njia nzima liam, alikaa kimya, macho yake yakizunguka kutazama jiji lilivyo. Aliona vijana waliovaa vizuri wakitoka maeneo ya Mikocheni, wanaume waliokaa pembeni mwa bar wakijadili siasa, akina dada waliokuwa kwenye bodaboda wakicheka kwa sauti kubwa, na taa za jiji zikiwa zinachomoza kwa rangi zenye ahadi ya usiku mrefu.


Alipofika, taa za club ziliangaza kwa rangi ya zambarau na samawati clubhiyo iliitwa Mzuka Empire. Muziki wa Afrobeat ulikuwa unavuma kwa nguvu ndani ya kuta. Watu walikuwa wanapiga picha nje, wengine wakifuta jasho kabla ya kuingia tena kucheza.


Mala baada ya kumalizana na taks au bolt,Uber Mlinzi alimwangalia kwa makini. Liam hakuwa mtu wa kupita bila kutazamwa mara mbili. Ukarimu wake wa kimya na sura iliyokuwa na mchanganyiko wa huzuni na mvuto, vilimfanya aonekane tofauti.


“Karibu ndani ndugu yangu,” mlinzi alisema kwa heshima.


Liam alitabasamu kidogo na kuingia.


Ndani, club ilikuwa hai kama moto. Taa zilizocheza sakafuni, muziki uliotia moyo, na harufu ya pombe mchanganyiko na marashi ya bei ghali vilimkaribisha kama mkono wa dunia ukimwambia: “Karibu tena.”


Alichukua kiti pembeni ya meza ya kona, karibu na dancefloor lakini si katikati. Alimwamuru mhudumu:


“Niwekee whisky kavu. Bila barafu. Shot mbili tu mwanzo.”


“Unaonja au unaanza?” mhudumu alitania kwa kicheko.


Liam akasema bila kutabasamu, “Naweka utulivu kwenye damu.”


Mhudumu alicheka.”


Alipotazama wachezaji wa dancefloor, watu waliocheka, waliokumbatiana, waliopoteza muda katika raha, Liam alijihisi mtu wa dunia kwa mara ya kwanza. Alijihisi tangu alipo ingia Tanzania ni kama maisha yake yamebadilika. Hakuhisi kuwa tofauti.


Kwa siku hiyo Liam alikuwa tu kijana wa kawaida, aliyeamua kunywa usiku mmoja, katika mji ambao bado unajaribu kumkumbatia.


Usiku uliendelea kupamba moto ndani ya Aurum Lounge. Muziki ulishika kasi, taa ziliendelea kucheza na kuangaza kwa rangi zilizokata giza, na sauti za vicheko, vilio vya furaha na kelele za music kuchezwa mezani vilichanganyika


Liam alikuwa ameegemea nyuma kwenye kiti chake, kinywaji mkononi, macho yakiwa yanacheza juu ya sakafu ya club lakini akili yake ikiwa kimya kabisa. Alikuwa na utulivu wa mtu asiye na haraka, mtu ambaye dunia haimpigi kelele. Lakini ndani ya macho yake kulikuwa na mwangaza wa mtu ambaye hawezi kupuuzwa.


Katika kona moja ya club, kwenye meza iliyojitenga na msongamano, mwanaume mmoja mrefu, aliyevalia suti nyeusi ya kuvutia na shati jeupe lililotulia kifuani, alikuwa akimwangalia Liam. Tangu Liam alipoketi, mwanaume huyo hakuacha kumfuatilia kwa macho. Ilikuwa si macho ya uhasama, bali ya kuchunguza, kuchambua—kama mtu anayemwangalia mgeni aliyeingia kwenye himaya yake.


Liam alihisi. Hakuwa mtu wa kawaida; hisia zake zilikuwa makini. Aligeuza shingo kidogo, akapeleka macho kwa haraka kwenye kona ile. Walipokutana macho na yule mwanaume, mwanaume huyo alicheka kidogo tu na kunywa kinywaji chake kana kwamba hakukuwa na chochote cha ajabu. Liam alimpuuza. Akaendelea na kinywaji chake.


Dakika chache baadaye, kama upepo wa manukato mazito ya Chanel, mwanamke mmoja mrembo sana alijitokeza karibu na meza ya Liam. Alikuwa mrefu kiasi, amevaa nguo ya kijivu iliyomkaa mwilini kama ngozi ya pili, na viatu virefu vilivyofanya miguu yake ionekane kama ya malkia. Alikuwa amekunja nywele kwa ustadi wa kisasa, na midomo yake mekundu ilisonga kwa tabasamu la kujiamini.


"Hi... Samahani, naweza kukaa hapa?" aliuliza bila hofu wala aibu, huku akiweka mkono wake mmoja mezani kama mtu aliyeshafika.


Liam alimtazama kwa sekunde chache, kisha akasema kwa sauti ya utulivu, "Ni meza ya wazi. Karibu."


Akatabasamu kwa upana, akaketi.


"Naitwa Sasha," alisema moja kwa moja, akimpelekea Liam mkono wa salamu. "Wewe ni nani? Au nikuite Mr. Hendsom?"


Liam alicheka kidogo kwa puani, akachukua mkono wake na kusema, "Liam."


"Liam," alirudia kwa sauti tamu kama melody. "Jina lako linaendana na sura yako. Mtu asiye na kelele, lakini hatakiwi kupuuzwa."


Aliongea naye kwa muda, akicheka, akimuuliza maswali, akimsifia fulana yake, macho yake, hata jinsi alivyoegemea kwenye kiti. Liam alijibu kwa staha, lakini bila kumpa nafasi ya kuingia ndani zaidi. Alijua aina hiyo ya wanawake—wanaokuja kama moto wa karatasi, unaowaka haraka lakini haudumu.


Lakini kadri walivyoendelea kuzungumza, Liam alihisi macho mengine yakiwa juu yao. Kisha kelele ya kistaarabu ya club ikakatizwa ghafla na sauti ya mwanaume iliyopasua utulivu wake:


"Sasha!"


Sauti hiyo ilijaa mshangao, hasira na uchungu. Watu waliogeuka, baadhi wakikodolea macho. Sasha alishika kichwa, kana kwamba alisahau kitu muhimu sana. Liam aligeuza uso wake, akamwona mwanaume mmoja aliyekuwa na mwili wa mazoezi, macho mekundu kwa hasira, akiwa amesimama mbele ya meza yao.


"We unafanya nini hapa? Huyu ni nani sasa?" mwanaume alifoka.


Sasha alijaribu kuongea, "Baby siyo kama unavyofikiria—"


"Usiniite baby hapa mbele ya mtu mwingine! Umenifanya mjinga sasa, eeh?"


Aligeuka kwa hasira kumkazia Liam macho.


"Wewe ni nani? Mwanaume wa watu unaingilia mahusiano ya watu wengine?"


Liam aliinua mikono, akasema kwa sauti ya kawaida kabisa, "Sikufanya chochote. Alikuja mwenyewe na akaketi."


"Usinijibu! We si mwanaume? Unamkubali mwanamke wa mtu? Au unajifanya huelewi?"


Bila onyo, mwanaume huyo alirusha ngumi ya kwanza. Haraka. Ghafla. Lakini Liam alijisogeza upande wa kushoto kwa ustadi wa ajabu—ngumi ikapita hewani. Kabla hajapumua, ngumi ya pili ikafuata kwa hasira zaidi—lakini Liam aliinama na kuepuka tena, bila hata kuonekana kuwa na hofu.


Watu waliokuwa karibu wakashtuka. Sasha akapiga kelele, "Stop it, Jamal! Unafanya nini?"


Liam akasema kwa sauti ya kutulia, "Sijasema tusi. Sijarudisha shambulizi. Nimekueleza ukweli. Shobo ni za mwanamke wako."


Maneno hayo yaliongeza hasira kwa Jamal. Akavuta pumzi kwa nguvu, akajiandaa kurusha ngumi ya tatu—


Lakini kabla hajakamilisha hatua hiyo, mkono mmoja mzito ulianza kushikilia bega lake kwa nguvu. Jamal aligeuka—na uso wake ukakutana na uso wa mwanaume alikua ni yule mwanaumealie kua akimuangalia sana liam.


"Acha. Hii si seemu ya kuanzisha vulugu. Wala si uwanja sahihi," mwanaume huyo alisema kwa sauti ya kuamuru, isiyohitaji kupigiwa kura.


Jamal alitaka kujibu, lakini alipoangalia macho ya mwanaume huyo, akaona jambo aliloshindwa kulitafsiri. Labda ni onyo. Labda ni mamlaka. Labda ni kitu kingine kisichoelezeka.


Akasukuma mkono wake, akageuka kwa hasira na kuondoka huku akitukana kwa chini.


Sasha alifuatilia nyuma yake akipiga kelele, "Baby! Subiri tafadhali! Si kama unavyofikiria!"


Club ikarudia hali ya kawaida taratibu.


Liam aligeuka kumtazama mwanaume aliyemwokoa. Waliangaliana kimya kwa muda mfupi. Halafu, mwanaume huyo akamwambia:


"Sikujua kama ni leo nitakuona uso kwa uso, Liam. Karibu tena nyumbani."


Halafu, bila kusema neno zaidi, aliondoka kuelekea upande mwingine wa club, akapotea kwenye mwanga wa taa za samawati.


Liam alibaki pale mezani, akikodolea macho seemu ambaye mwanaume huyo alisimama kabla ya kuondoka Akili yake ilikuwa bado haijakaa sawa tangu tukio ndani ya club lilipotokea. Mwanamke aliyemshobokea ghafla, mpenzi wake aliyewaka hasira kama moto wa petroli, na yule mwanaume wa ajabu aliyemwokoa. Kila kitu kilihisi kama tukio lililopangwa, lakini hakukuwa na ushahidi


"Liam alikua akiwaza Yule jamaa... alimaanisha nini kusema 'karibu tena nyumbani'?" Ananijua? Aliwai kuonana nae wapi? Au ni bahati mbaya?" Liam alijiwazia


Lakini majibu hayakupatikana. Akili yake haikutoa sauti. Na wakati mwingine, kimya kina maana zaidi ya maneno.


Alihisi kama maneno yale yalibeba kumbukumbu aliyosahau, au njia ya kuelekea kwenye ukweli alioutafuta kwa muda mrefu. Lakini kama kawaida yake, Liam alijua namna ya kuyasukuma mbali maswali ya aina hiyo.


"Acha muda uongee," alijisemea kimoyomoyo.


Kutokana na jambo lililo tokea Liam hakuitaji kuendelea kubaki teka kwenye club hiyo hivyo alichukua maamuzi ya kuondoka


Baada ya kutoka nje ya club Alichukua simu yake ili aliquest Bolt, lakini kabla hajakamilisha, hatua tatu mbele yake alizuiliwa njia. mbele walisimama watu watatu. Mmoja alikuani yule Jamaa aliyemshambulia club aliekua akiitwa jamal na wanaume wengine wawili kuusu yule mwanamke sasha yeye hakuwepo—Jamal—mwenye mwili wa misuli na sura ya dharau. Kulia na kushoto kwake walikuwa vijana wawili waliovaa mashati meusi na suruali za jeans zilizokunjwa


Jamal alitabasamu kwa dharau.


"Ndani ya clubu ulikuwa na bahati, umepata mtetezi. Hebu sasa tuone hapa nje ni nani atakaye kusaidia..."


Liam kusikia hivyo alipigwa na butwaa kwani alizmdhani mambo yote yalikua yamekwisha sasa nan angejua mbumbe ndia kwanza shuhuli imeanza


Jamal aliwaamuru vijana wake kwa ishara ya kichwa. Wakamkaribia Liam kwa kasi, macho yao yakiwa na uchu wa kumshugulikia vyema liam. Mmoja alirusha ngumi ya kulia—Liam aligeuka kwa ustadi, akaisogeza bega kwa kasi, na mkono ule ukapita. Mwingine alijaribu kumpiga teke—Liam alikanyaga mbele ghafla na teke likamkosa mwelekeo.


Kwajinsi walivyo kua wakishambulia ilionekana dhaili hawakua na mafunzo yoyote kwani walishambulia bila mpangilio lakini kadri walivyo jalibu kumshambulia Liam yeye aliwakwepa tu bila kuludisha shambulizi


Kilichowashangaza si kwamba Liam aliwakwepa, bali namna alivyokwepa bila juhudi yoyote. Kama anacheza mchezo anaoujua kwa mazoea


Jamal alisononeka kuona wenzake wakishindwa. Kwa hasira, aliamua kuingia yeye mwenyewe. Lakini licha yavyo haikusaidia chochote kwani kila walipo jalibu ilikua ni kama mtoto anaejalibu kupigana na baba yake


"Bado tu mnataka kuendelea licha ya kunishambulia na mmeshindwa kunigusa hata mara moja?" Liam aliuliza kwa sauti ya kutulia, lakini iliyojaa onyo.


Lakini Jamal hakuacha. Alirusha ngumi ya haraka upande wa kushoto wa uso wa Liam. Liam aliinama kidogo, akaikwepa, na kabla hajainuka vizuri, ngumi ya pili ikaja upande wa kulia. Hata hiyo aliikwepa, akirudi nyuma kwa ustadi wa ajabu.


"Hamwelewi, siyo? Bado tu basi ngoja niwape kile mnacho staili?" aliongeza Liam kwa sauti ya chini ilio jaaa msisitizo.


ITAENDELEA
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom