FEBIANI BABUYA
JF-Expert Member
- Mar 5, 2022
- 2,232
- 4,388
- Thread starter
- #41
HADITHI: THE ODYSSEY OF GAVIN LUCA (LIONELA)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+
********************
UKURASA WA KUMI NA SITA
SONGA NAYO................
“Kuna kipindi niliwahi kuwaza kwamba kwanini kuna watu wanakufa mapema! Jambo lile liliwahi kuniumiza kichwa kwa muda mrefu ila baadae nilipata jibu moja rahisi la jumla. Watu wanakufa mapema kwa sababu wengi wanastahili kufa, kuna watu wanatakiwa kutokuwepo duniani ili dunia iwe sawa na mambo yaweze kwenda kama ambavyo watu wamejipangia ila baadhi ya watu hao wakiendelea kuwa hai unaweza kuwa mwanzo mbaya wa baadae ya taifa hili” hayo ni maneno ambayo yalitoka kwenye kinywa cha jaji na ndiyo ambayo yalimfanya mwanaume huyo kusita kutoka na kugeuka ili ayasikilize kwa umakini zaidi.
“Hiki ambacho kimetokea hapa ni kazi mheshimiwa, sio mambo personal kama ambavyo unahisi wewe. Mimi nalipwa ili kufanya hii kazi na ndiyo inanitambulisha popote pale hivyo kama unaona nimevuka mipaka kwenye hili naomba unisamehe sana”
“Shilingi imetengenezwa kwa kutofautishwa na pande mbili, upande mmoja unafahamika kama kichwa na upande mwingine unafahamika kama mkia. Ambao waliitengeneza hawakuwa wajinga wala wapuuzi kuzitofautisha hizo pande mbili, zilitofautishwa kwa sababu kuna maana kubwa kuweza kufanya hivyo ila sio watu wote ambao huwa wanalizingatia sana jambo hili, wengi huwa wanahisi kwamba aliye kuja na hilo wazo alipoteza muda tu.
Lakini sio kweli mtu huyu aliwaza mbali sana na siku ambayo wewe utakuja kuelewa utofauti wa hizo pande mbili, ndiyo siku ambayo utakuja kunielewa yale ambayo nimeyazungumza hapa siku ya leo ila huenda muda hautakuwa rafiki kwako zaidi ya kutamani ungeelewa mapema. Nakutakiwa siku njema afisa, unaweza kwenda kwa sababu nahitaji muda wa kupumzika”
Aliambiwa maneno mazito ambayo hayakuwa na maana nzuri kwenye tafsiri, alijua kabisa mheshimiwa alikuwa anamaanisha nini kusema vile ila asingeweza kushindana naye kwa sababu alikuwa ni kigogo na kumgusa hovyo ilikuwa ni hatari kwake yeye na kwa kazi yake kwa ujumla. Alitoka ndani ya hilo eneo akiwa ameimaliza kazi ambayo aliona kabisa hata taarifa ambayo aliipata kwa mtu yule ilikuwa ya uongo ila sio kila mtu angelitambua hilo, wananchi walikuwa wanaenda kuiamini ila sio yeye, alijua kabisa kiongozi huyo alikuwa na mengi nyuma ya pazia ambayo hakuyasema juu ya tukio lile ambalo lilikuwa limetokea. Kwa bahati mbaya hakuwa na huo uwezo wa kumlazimisha.
LUGALO MILITARY BASE.
Moja kati ya maeneo ambayo yanaogopeka na kuheshimika sana ndani ya mipaka ya Tanzania, ni eneo ambalo linamilikiwa na jeshi na ndipo yalipo makao makuu ya jeshi la ulinzi la wananchi ya Tanzania JWTZ. Linapo ishia eneo la jeshi hilo barabara itokayo mwenge kwenda Tegeta kuna daraja kubwa ambalo watu huwa wanalitumia kuvukia kutoka upande mmoja kwenda upande mwingine. Pembezoni mwa daraja hilo ndipo kuna hifadhi ambayo inamilikiwa na jeshi na ukiingia kwenye hifadhi hiyo unakuwa umeingia eneo husika moja kwa moja. Eneo hilo huwa lipo kama hakuna watu mpaka pale ambapo utatia maguu yako ndani ya eneo hilo ndipo unakuja kuelewa sababu ya kwanini watu wengi huwa wanapaogopa sana.
Usiku wa saa saba na dakika zake hamsini na tisa, pembezoni mwa mti mmoja ambao upo karibu na barabara karibia kabisa na ulipo ukuta mfupi wa chuma ambao umeandikwa kwa rangi ya damu ya mzee kwa maandishi makubwa LUGALO MILITARY BASE, kuna mwanaume alikuwa amekaa kwa kuegamia mti huo pembeni yake akiwa na upanga mmoja mkali ambao ulikuwa unaonekana kwa mbali kutokana na jinsi ulivyokuwa mkali.
Bwana huyo alikuwa ameweka bastola moja juu ya paja lake huku nyingine ikiwa kiunoni, kwenye mwili wake alikuwa amevaa nguo zote nyeusi za jeans na buti ambalo lilikuwa linafanana na nguo zake. kwenye uso wake kulikuwa na kofia nyeusi aina ya pama ambayo ilimziba kumfanya asionekane kwa mtu ambaye angekuwa mbali. Hapo alipokuwa ameketi alifanya mwanga kumulika kwa mbali kiasi kwamba mtu angehisi ni wale wadudu watoao mwanga nyakati za usiku wanapokuwa wanaruka ruka hewani lakini kwake ilikuwa ni tofauti na jambo hilo.
Kwenye mkono wake wa kulia alikuwa anaivuta sigara na ndiyo ambayo ilikuwa inatoa mwanga ambao ulikuwa unaonekana, sigara hiyo alikuwa anaivuta kwa msisimko mkubwa kana kwamba kuna jambo la mhimu alikuwa analisubiri eneo hilo kwa nyakati hizo. Hakuwa na wasiwasi kabisa juu ya ujio wake hilo eneo, alionekana kuwa kwenye mahesabu yake na alijua jambo ambalo alikuwa analifanya kwa nyakati zile ndiyo sababu kubwa ambayo ilimpa imani ya mahesabu yake.
Akiwa lile eneo alisikia hatua kwa mbali na mazungumzo ambayo yalitoka kwa watu ambao walioekana kujuana kiundani na vizuri zaidi. Watu hao walionekana kuwa ni zaidi ya watu wawili lakini sauti zile zilipungua zikawa za chini zaidi na ndiyo sehemu ambayo alikuwa anaisubiria kwa hamu zaidi. Utulivu ule ulimpa jibu kwamba wale watu walikuwa wameugundua uwepo wake ndani ya lile eneo hivyo ulikuwa ni muda mwafaka wa kufanikisha jambo ambalo lilimpeleka pale nyakati zile za usiku.
Ni kweli ule mwanga wa sigara yake ndio ambao ulitoa taarifa juu ya uwepo wa mtu eneo lile, ule mshtuko uliwafikia wanajeshi ambao walikuwa zamu kuhakikisha usalama wa eneo hilo. Walikuwa wanaamini hakuna mtu mwingine ambaye alitakiwa kuwepo eneo hilo zaidi yao kitu ambacho walikuwa sahihi kabisa lakini hali ya pale ilionekana kuwa tofauti kidogo hivyo wakahisi huenda alikuwa ni mvuta bangi wa mtaani ambaye walitakiwa kukesha naye na kumnyoosha.
Sababu hiyo ikawafanya wanajeshi wawili tu kujongea kuelekea eneo la tukio, bwana yule alikuwa nyuma ya mti hivyo kwenye tochi ya mwanajeshi mmoja ambayo alikuwa ameimulika, bwana huyo alikuwa anaonekana kwenye mabega yake tu. Licha ya kusikia zile hatua za watu zikielekea ule upande bado hakuwa na shaka wala hofu, aliendelea kuivuta sigara yake kwa utulivu akiwa anauachia moshi hewani kwa mbwembwe nyingi.
Wanajeshi walikuwa wawili, mmoja alipita upande mmoja na mwingine alipita upande mwingine hivyo wakatokezea kwa mbele yake, hakuwa na eneo la kukimbilia ila huenda hawakuwa na uelewa kwamba mtu huyo hakwenda pale kwa bahati mbaya wala hakwenda pale ili kuweza kuwakimbia watu hao ila wasingeweza kulijua hilo kwa haraka namna ile, walihitaji muda jambo ambalo halikuwa rafiki kwao.
“Unajua upo wapi hapa?” aliuliza mwanajeshi mmoja akiwa anammlika na tochi usoni ambayo ilionekana kumkera kwa sababu alifumba macho akizikunja ndita zake.
“Lugalo”
“Unaelewa sheria za hili eneo?”
“Ndiyo, hakuna raia anaruhusiwa kuingia hili eneo vinginevyo atakumbana na adhabu kali”
“Kwahiyo wewe ni kidume mpaka ukata kuja kutuvimbia kwenye eneo letu siyo?”
“Mpo wangapi hili eneo?” alijibu mwanaume huyo kwa sauti nzito zaidi akiwa hana hata wasiwasi lakini swali lake lilionekana kuwa kichekesho. Yule mwanajeshi ambaye alikuwa amemlika ile tochi yake alihisi kama kuna kitu amekiona pembeni ya eneo lile hivyo akalazimika kuweza kuhamisha mwanga ndipo alishangaa kuona upanga ambao ulikuwa unang’aa sana huku kwenye paja la mwanaume yule pakiwa na bastola. Alishtuka na kugundua kwamba bwana huyo hakuwa kibaka wala mvuta bangi bali alikuwa ni muuaji, jambo lile ndilo ambalo lilimfanya atake kupiga kelele kuwashtua wenzao ila muda wa kufanya maamuzi haukuwa rafiki kwake.
Ni wakati ambao alipokea buti zito la goti akakosa balansi na kutaka kuangukia mbele kwani hakutarajia huku akiachia tusi zito kulaani shambulio lile lakini wakati anainama, ule upanga ulishikwa na kuzungushwa ambapo ulipita kwenye shingo yake. Mwenzake alipuliza filimbi aliwa anarusha buti lake ambalo lilidakwa na kwa mbele ule upanga ukasokomezwa kwenye sehemu zake za siri bwana yule akasimama ambapo alirusha ngumi yake ikatua kwenye taya na kuzivunja. Mwanajeshi yule alitamani kuweza kujinasua ndipo ile bastola ilipo tumika, alipigwa risasi mbili kichwani kutoka kwenye bastola ambayo haikufungwa kiwambo cha kuzuia sauti kiasi kwamba ule mlio wa risasi ulisikika mbali na pale na hayo yote mhusika alionekana kuyafanya makusudi kabisa kwa hesabu zake.
Hakujulikana alikuwa ni nani na kulikuwa na sababu zipi mpaka yeye kuvamia ndani ya kambi ya jeshi na kuanza kufanya mauaji ya namna hiyo. Ile filimbi na mlio wa risasi uliwafanya wanajeshi ambao hawakuwa mbali na lile eneo kusogea wakiwa na silaha zao tayari kupambana na hatari yoyote ambayo ingekuwepo ndani ya eneo lile. Walifika pale pakiwa kimya, ni miili ya wenzao tu ambao ilikuwa imetapakaa pale mhusika akiwa hayupo.
Ukurasa wa kumi na sita unafika mwisho.
FEBIANI BABUYA.
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+
********************
UKURASA WA KUMI NA SITA
SONGA NAYO................
“Kuna kipindi niliwahi kuwaza kwamba kwanini kuna watu wanakufa mapema! Jambo lile liliwahi kuniumiza kichwa kwa muda mrefu ila baadae nilipata jibu moja rahisi la jumla. Watu wanakufa mapema kwa sababu wengi wanastahili kufa, kuna watu wanatakiwa kutokuwepo duniani ili dunia iwe sawa na mambo yaweze kwenda kama ambavyo watu wamejipangia ila baadhi ya watu hao wakiendelea kuwa hai unaweza kuwa mwanzo mbaya wa baadae ya taifa hili” hayo ni maneno ambayo yalitoka kwenye kinywa cha jaji na ndiyo ambayo yalimfanya mwanaume huyo kusita kutoka na kugeuka ili ayasikilize kwa umakini zaidi.
“Hiki ambacho kimetokea hapa ni kazi mheshimiwa, sio mambo personal kama ambavyo unahisi wewe. Mimi nalipwa ili kufanya hii kazi na ndiyo inanitambulisha popote pale hivyo kama unaona nimevuka mipaka kwenye hili naomba unisamehe sana”
“Shilingi imetengenezwa kwa kutofautishwa na pande mbili, upande mmoja unafahamika kama kichwa na upande mwingine unafahamika kama mkia. Ambao waliitengeneza hawakuwa wajinga wala wapuuzi kuzitofautisha hizo pande mbili, zilitofautishwa kwa sababu kuna maana kubwa kuweza kufanya hivyo ila sio watu wote ambao huwa wanalizingatia sana jambo hili, wengi huwa wanahisi kwamba aliye kuja na hilo wazo alipoteza muda tu.
Lakini sio kweli mtu huyu aliwaza mbali sana na siku ambayo wewe utakuja kuelewa utofauti wa hizo pande mbili, ndiyo siku ambayo utakuja kunielewa yale ambayo nimeyazungumza hapa siku ya leo ila huenda muda hautakuwa rafiki kwako zaidi ya kutamani ungeelewa mapema. Nakutakiwa siku njema afisa, unaweza kwenda kwa sababu nahitaji muda wa kupumzika”
Aliambiwa maneno mazito ambayo hayakuwa na maana nzuri kwenye tafsiri, alijua kabisa mheshimiwa alikuwa anamaanisha nini kusema vile ila asingeweza kushindana naye kwa sababu alikuwa ni kigogo na kumgusa hovyo ilikuwa ni hatari kwake yeye na kwa kazi yake kwa ujumla. Alitoka ndani ya hilo eneo akiwa ameimaliza kazi ambayo aliona kabisa hata taarifa ambayo aliipata kwa mtu yule ilikuwa ya uongo ila sio kila mtu angelitambua hilo, wananchi walikuwa wanaenda kuiamini ila sio yeye, alijua kabisa kiongozi huyo alikuwa na mengi nyuma ya pazia ambayo hakuyasema juu ya tukio lile ambalo lilikuwa limetokea. Kwa bahati mbaya hakuwa na huo uwezo wa kumlazimisha.
LUGALO MILITARY BASE.
Moja kati ya maeneo ambayo yanaogopeka na kuheshimika sana ndani ya mipaka ya Tanzania, ni eneo ambalo linamilikiwa na jeshi na ndipo yalipo makao makuu ya jeshi la ulinzi la wananchi ya Tanzania JWTZ. Linapo ishia eneo la jeshi hilo barabara itokayo mwenge kwenda Tegeta kuna daraja kubwa ambalo watu huwa wanalitumia kuvukia kutoka upande mmoja kwenda upande mwingine. Pembezoni mwa daraja hilo ndipo kuna hifadhi ambayo inamilikiwa na jeshi na ukiingia kwenye hifadhi hiyo unakuwa umeingia eneo husika moja kwa moja. Eneo hilo huwa lipo kama hakuna watu mpaka pale ambapo utatia maguu yako ndani ya eneo hilo ndipo unakuja kuelewa sababu ya kwanini watu wengi huwa wanapaogopa sana.
Usiku wa saa saba na dakika zake hamsini na tisa, pembezoni mwa mti mmoja ambao upo karibu na barabara karibia kabisa na ulipo ukuta mfupi wa chuma ambao umeandikwa kwa rangi ya damu ya mzee kwa maandishi makubwa LUGALO MILITARY BASE, kuna mwanaume alikuwa amekaa kwa kuegamia mti huo pembeni yake akiwa na upanga mmoja mkali ambao ulikuwa unaonekana kwa mbali kutokana na jinsi ulivyokuwa mkali.
Bwana huyo alikuwa ameweka bastola moja juu ya paja lake huku nyingine ikiwa kiunoni, kwenye mwili wake alikuwa amevaa nguo zote nyeusi za jeans na buti ambalo lilikuwa linafanana na nguo zake. kwenye uso wake kulikuwa na kofia nyeusi aina ya pama ambayo ilimziba kumfanya asionekane kwa mtu ambaye angekuwa mbali. Hapo alipokuwa ameketi alifanya mwanga kumulika kwa mbali kiasi kwamba mtu angehisi ni wale wadudu watoao mwanga nyakati za usiku wanapokuwa wanaruka ruka hewani lakini kwake ilikuwa ni tofauti na jambo hilo.
Kwenye mkono wake wa kulia alikuwa anaivuta sigara na ndiyo ambayo ilikuwa inatoa mwanga ambao ulikuwa unaonekana, sigara hiyo alikuwa anaivuta kwa msisimko mkubwa kana kwamba kuna jambo la mhimu alikuwa analisubiri eneo hilo kwa nyakati hizo. Hakuwa na wasiwasi kabisa juu ya ujio wake hilo eneo, alionekana kuwa kwenye mahesabu yake na alijua jambo ambalo alikuwa analifanya kwa nyakati zile ndiyo sababu kubwa ambayo ilimpa imani ya mahesabu yake.
Akiwa lile eneo alisikia hatua kwa mbali na mazungumzo ambayo yalitoka kwa watu ambao walioekana kujuana kiundani na vizuri zaidi. Watu hao walionekana kuwa ni zaidi ya watu wawili lakini sauti zile zilipungua zikawa za chini zaidi na ndiyo sehemu ambayo alikuwa anaisubiria kwa hamu zaidi. Utulivu ule ulimpa jibu kwamba wale watu walikuwa wameugundua uwepo wake ndani ya lile eneo hivyo ulikuwa ni muda mwafaka wa kufanikisha jambo ambalo lilimpeleka pale nyakati zile za usiku.
Ni kweli ule mwanga wa sigara yake ndio ambao ulitoa taarifa juu ya uwepo wa mtu eneo lile, ule mshtuko uliwafikia wanajeshi ambao walikuwa zamu kuhakikisha usalama wa eneo hilo. Walikuwa wanaamini hakuna mtu mwingine ambaye alitakiwa kuwepo eneo hilo zaidi yao kitu ambacho walikuwa sahihi kabisa lakini hali ya pale ilionekana kuwa tofauti kidogo hivyo wakahisi huenda alikuwa ni mvuta bangi wa mtaani ambaye walitakiwa kukesha naye na kumnyoosha.
Sababu hiyo ikawafanya wanajeshi wawili tu kujongea kuelekea eneo la tukio, bwana yule alikuwa nyuma ya mti hivyo kwenye tochi ya mwanajeshi mmoja ambayo alikuwa ameimulika, bwana huyo alikuwa anaonekana kwenye mabega yake tu. Licha ya kusikia zile hatua za watu zikielekea ule upande bado hakuwa na shaka wala hofu, aliendelea kuivuta sigara yake kwa utulivu akiwa anauachia moshi hewani kwa mbwembwe nyingi.
Wanajeshi walikuwa wawili, mmoja alipita upande mmoja na mwingine alipita upande mwingine hivyo wakatokezea kwa mbele yake, hakuwa na eneo la kukimbilia ila huenda hawakuwa na uelewa kwamba mtu huyo hakwenda pale kwa bahati mbaya wala hakwenda pale ili kuweza kuwakimbia watu hao ila wasingeweza kulijua hilo kwa haraka namna ile, walihitaji muda jambo ambalo halikuwa rafiki kwao.
“Unajua upo wapi hapa?” aliuliza mwanajeshi mmoja akiwa anammlika na tochi usoni ambayo ilionekana kumkera kwa sababu alifumba macho akizikunja ndita zake.
“Lugalo”
“Unaelewa sheria za hili eneo?”
“Ndiyo, hakuna raia anaruhusiwa kuingia hili eneo vinginevyo atakumbana na adhabu kali”
“Kwahiyo wewe ni kidume mpaka ukata kuja kutuvimbia kwenye eneo letu siyo?”
“Mpo wangapi hili eneo?” alijibu mwanaume huyo kwa sauti nzito zaidi akiwa hana hata wasiwasi lakini swali lake lilionekana kuwa kichekesho. Yule mwanajeshi ambaye alikuwa amemlika ile tochi yake alihisi kama kuna kitu amekiona pembeni ya eneo lile hivyo akalazimika kuweza kuhamisha mwanga ndipo alishangaa kuona upanga ambao ulikuwa unang’aa sana huku kwenye paja la mwanaume yule pakiwa na bastola. Alishtuka na kugundua kwamba bwana huyo hakuwa kibaka wala mvuta bangi bali alikuwa ni muuaji, jambo lile ndilo ambalo lilimfanya atake kupiga kelele kuwashtua wenzao ila muda wa kufanya maamuzi haukuwa rafiki kwake.
Ni wakati ambao alipokea buti zito la goti akakosa balansi na kutaka kuangukia mbele kwani hakutarajia huku akiachia tusi zito kulaani shambulio lile lakini wakati anainama, ule upanga ulishikwa na kuzungushwa ambapo ulipita kwenye shingo yake. Mwenzake alipuliza filimbi aliwa anarusha buti lake ambalo lilidakwa na kwa mbele ule upanga ukasokomezwa kwenye sehemu zake za siri bwana yule akasimama ambapo alirusha ngumi yake ikatua kwenye taya na kuzivunja. Mwanajeshi yule alitamani kuweza kujinasua ndipo ile bastola ilipo tumika, alipigwa risasi mbili kichwani kutoka kwenye bastola ambayo haikufungwa kiwambo cha kuzuia sauti kiasi kwamba ule mlio wa risasi ulisikika mbali na pale na hayo yote mhusika alionekana kuyafanya makusudi kabisa kwa hesabu zake.
Hakujulikana alikuwa ni nani na kulikuwa na sababu zipi mpaka yeye kuvamia ndani ya kambi ya jeshi na kuanza kufanya mauaji ya namna hiyo. Ile filimbi na mlio wa risasi uliwafanya wanajeshi ambao hawakuwa mbali na lile eneo kusogea wakiwa na silaha zao tayari kupambana na hatari yoyote ambayo ingekuwepo ndani ya eneo lile. Walifika pale pakiwa kimya, ni miili ya wenzao tu ambao ilikuwa imetapakaa pale mhusika akiwa hayupo.
Ukurasa wa kumi na sita unafika mwisho.
FEBIANI BABUYA.