mireille
JF-Expert Member
- Mar 4, 2020
- 606
- 665
Sura ya: 1
Alissa Maziku alitazama kwenye kioo na kufuatilia midomo yake laini na iliyojaa kwa lipstick. Mrembo, mrembo sana.
Ngozi yake maji ya chungwa ilionekana nyororo na maridadi chini ya mwanga unaong'aa na macho yake safi yalikuwa ya kupendeza sana ambayo yaliwavuta watu ndani kwa mtazamo wa kwanza. Pamoja na midomo yake maridadi, Alissa aliwafanya watu watake kumbusu. Alijitazama utu wake kamili kwenye kioo, na akatabasamu kwa kuridhika.
Akiminya ufunguo wa chumba mkononi mwake, huku akikandamiza mapambano yake ya ndani ya moyo, hatua kwa hatua, alitembea hadi kwenye chumba cha hoteli cha nyota tano mwishoni mwa korido la ukumbi.
Kila alipopiga hatua, alisikia sauti za wasiwasi kutoka kwa kila mtu karibu naye.
"Alissa, daktari alisema kwamba Seidrick alikuwa karibu kufa. Ukizingatia kwamba aliwahi kuokoa maisha yako, nyie mlikua pamoja, na ni mchumba wako, unaweza kufikiria njia, Alissa? Wewe ndiye pekee unayeweza kumwokoa sasa……” Mama yake Seidrick Masolwa aliomba kwa bidii, macho yake yakiwa yamevimba kutokana na kulia.
"Dada, ikiwa kuna mtoto ambaye damu yake inaendana na kaka Seidrick, damu yake ya kitovu inaweza kumokoa Seidrick. Huu unaweza kuonekana ujinga zaidi lakini ndo njia pekee. Lakini hakuna mtu aliye na damu sawa na Sedrick, anawezaje kuwa na mtoto?" Mellisa Maziku, mdogo wake Alissa alikuwa na wasiwasi. “Ikiwa kaka Seidrick angeweza kukudunga mimba, hiyo ingekuwa bahati kwetu, lakini sasa yu dhaifu na hawezi hata…… Dada, utafanya nini?”
Ni kweli, daktari alisema Seidrick hakuwa na afya ya kumpa mwanamke mimba. Licha ya kwamba hakuwa na afya ya kushiriki tendo la ndoa, lakini pia uzalishaji wake wa mbegu za kiume ulikuwa dhaifu kutokana na kuishiwa damu mwili. Inasemekana kuwa huchukua karibu matone 40 ya damu kutengeneza tone moja tu la mbegu za kiume. Isingewezekana kwa Seidrick kutungisha mimba kwa njia za kupandikiza.
Ikiwa kitu kingempata Seidrick, Alissa angepaswa kufanya nini? Nani angemletea furaha? Kwa kuongezea, aliwahi kuokoa maisha yake. Sasa kwa kuwa maisha yake yalikuwa hatarini, angewezaje kukaa mbali? alihitaji kurudisha fadhila.
Seidrick, mchumba wa Allisa, alizaliwa na ugonjwa wa aleji ya damu, au mzio wa damu. Ni aina ya hitilafu ambayo husababisha damu kuchafuka mara kwa mara. Sasa kwa kuwa Seidrick alipata ajali na alitakiwa kuongezewa damu, hakuna damu yoyote iliyomkubali, hata ile iliyokuwa ni kundi moja la damu pamoja na yake. Mzio wake wa damu ulikataa damu zote.
Daktari alishauri kuwa alitakiwa mtu ambaye ana damu inayofanana na Seidrick kwa kila kitu, ikiwa ni pamoja na mzio wa damu, ndiye angeeweza kumwongezea damu Seidrick. Haikuwa rahisi kumpata mtu wa namna hiyo.
Mwishowe, kwa kuwahurumia sana, daktari akaamua kufichua rekodi za mgonjwa aliyewahi kugundulika na ugonjwa huo. Damu ya mtu huyo ingeweza kumponya Seidrick, kwa maana ilifanana kwa kila kitu. Mtu huyo naye alikuwa na ugonjwa wa mzio wa damu. Watu wa namna hii hawataikiwa kuona damu. Wakiona hata tone tu la damu basi damu yote mwilini mwao inachafuka!
Lakini, mtu huyo ambaye angeweza kumwongezea damu Seidrick na kuweza kumponya hakuwa mtu wa kawaida. Alikuwa ni tajiri, kiburi na mwenye majivuno ambaye kwa mtazamo wa kwanza asingeweza hata kuzungumza nao. Nani alikuwa na ujasiri hata wa kumsogelea?
Kwa kuwa Allisa alikuwa na deni la maisha kwa Seidrick, na vilevile alikuwa ni mchumba wake, alijitolea kumsaidia kwa njia isiyo ya kawaida. Aliamua kuutoa ubikra wake na mapenzi yake ya kwanza kwa mtu huyo, aze naye na kupata mtoto mwenye damu adimu kama hiyo ili aweze kumponya huyo mchumba wake. Ndiyo, alifanya mafekeche ili aweze kupata mtoto kwa damu ya Kenrick! Daktari alisema hata kitovu tu cha mtoto atakayezaliwa na baba mwenye damu ya namna hiyo, angeweza kumponya Seidrick.
Alissa alisimama mbele ya chumba hicho cha hoteli ya nyota tano na kushusha pumzi ndefu kwa mara ya tatu. Mtu aliyekuwa ndani ya chumba hicho alikuwa ni Kendrick Mayala, mtu aliyekuwa na damu adimu sawa na Seidrick Masolwa.
Alissa Maziku alitazama kwenye kioo na kufuatilia midomo yake laini na iliyojaa kwa lipstick. Mrembo, mrembo sana.
Ngozi yake maji ya chungwa ilionekana nyororo na maridadi chini ya mwanga unaong'aa na macho yake safi yalikuwa ya kupendeza sana ambayo yaliwavuta watu ndani kwa mtazamo wa kwanza. Pamoja na midomo yake maridadi, Alissa aliwafanya watu watake kumbusu. Alijitazama utu wake kamili kwenye kioo, na akatabasamu kwa kuridhika.
Akiminya ufunguo wa chumba mkononi mwake, huku akikandamiza mapambano yake ya ndani ya moyo, hatua kwa hatua, alitembea hadi kwenye chumba cha hoteli cha nyota tano mwishoni mwa korido la ukumbi.
Kila alipopiga hatua, alisikia sauti za wasiwasi kutoka kwa kila mtu karibu naye.
"Alissa, daktari alisema kwamba Seidrick alikuwa karibu kufa. Ukizingatia kwamba aliwahi kuokoa maisha yako, nyie mlikua pamoja, na ni mchumba wako, unaweza kufikiria njia, Alissa? Wewe ndiye pekee unayeweza kumwokoa sasa……” Mama yake Seidrick Masolwa aliomba kwa bidii, macho yake yakiwa yamevimba kutokana na kulia.
"Dada, ikiwa kuna mtoto ambaye damu yake inaendana na kaka Seidrick, damu yake ya kitovu inaweza kumokoa Seidrick. Huu unaweza kuonekana ujinga zaidi lakini ndo njia pekee. Lakini hakuna mtu aliye na damu sawa na Sedrick, anawezaje kuwa na mtoto?" Mellisa Maziku, mdogo wake Alissa alikuwa na wasiwasi. “Ikiwa kaka Seidrick angeweza kukudunga mimba, hiyo ingekuwa bahati kwetu, lakini sasa yu dhaifu na hawezi hata…… Dada, utafanya nini?”
Ni kweli, daktari alisema Seidrick hakuwa na afya ya kumpa mwanamke mimba. Licha ya kwamba hakuwa na afya ya kushiriki tendo la ndoa, lakini pia uzalishaji wake wa mbegu za kiume ulikuwa dhaifu kutokana na kuishiwa damu mwili. Inasemekana kuwa huchukua karibu matone 40 ya damu kutengeneza tone moja tu la mbegu za kiume. Isingewezekana kwa Seidrick kutungisha mimba kwa njia za kupandikiza.
Ikiwa kitu kingempata Seidrick, Alissa angepaswa kufanya nini? Nani angemletea furaha? Kwa kuongezea, aliwahi kuokoa maisha yake. Sasa kwa kuwa maisha yake yalikuwa hatarini, angewezaje kukaa mbali? alihitaji kurudisha fadhila.
Seidrick, mchumba wa Allisa, alizaliwa na ugonjwa wa aleji ya damu, au mzio wa damu. Ni aina ya hitilafu ambayo husababisha damu kuchafuka mara kwa mara. Sasa kwa kuwa Seidrick alipata ajali na alitakiwa kuongezewa damu, hakuna damu yoyote iliyomkubali, hata ile iliyokuwa ni kundi moja la damu pamoja na yake. Mzio wake wa damu ulikataa damu zote.
Daktari alishauri kuwa alitakiwa mtu ambaye ana damu inayofanana na Seidrick kwa kila kitu, ikiwa ni pamoja na mzio wa damu, ndiye angeeweza kumwongezea damu Seidrick. Haikuwa rahisi kumpata mtu wa namna hiyo.
Mwishowe, kwa kuwahurumia sana, daktari akaamua kufichua rekodi za mgonjwa aliyewahi kugundulika na ugonjwa huo. Damu ya mtu huyo ingeweza kumponya Seidrick, kwa maana ilifanana kwa kila kitu. Mtu huyo naye alikuwa na ugonjwa wa mzio wa damu. Watu wa namna hii hawataikiwa kuona damu. Wakiona hata tone tu la damu basi damu yote mwilini mwao inachafuka!
Lakini, mtu huyo ambaye angeweza kumwongezea damu Seidrick na kuweza kumponya hakuwa mtu wa kawaida. Alikuwa ni tajiri, kiburi na mwenye majivuno ambaye kwa mtazamo wa kwanza asingeweza hata kuzungumza nao. Nani alikuwa na ujasiri hata wa kumsogelea?
Kwa kuwa Allisa alikuwa na deni la maisha kwa Seidrick, na vilevile alikuwa ni mchumba wake, alijitolea kumsaidia kwa njia isiyo ya kawaida. Aliamua kuutoa ubikra wake na mapenzi yake ya kwanza kwa mtu huyo, aze naye na kupata mtoto mwenye damu adimu kama hiyo ili aweze kumponya huyo mchumba wake. Ndiyo, alifanya mafekeche ili aweze kupata mtoto kwa damu ya Kenrick! Daktari alisema hata kitovu tu cha mtoto atakayezaliwa na baba mwenye damu ya namna hiyo, angeweza kumponya Seidrick.
Alissa alisimama mbele ya chumba hicho cha hoteli ya nyota tano na kushusha pumzi ndefu kwa mara ya tatu. Mtu aliyekuwa ndani ya chumba hicho alikuwa ni Kendrick Mayala, mtu aliyekuwa na damu adimu sawa na Seidrick Masolwa.