nasrimgambo
JF-Expert Member
- Jan 10, 2017
- 1,920
- 2,529
- Thread starter
- #41
Wakati Mrisho akilia hapo dining room , alichokuwa hajui ni kwamba kulikuwa na
mtu aliyemsikia jinsi alivyokuwa ameamka na kutoka hadi hapo dining room usiku
huo na kuanza kulia na kuongea peke yake.
Huyo mtu alikuwa ni dada yake, yani Bi
Khadija. Khadija alikuwa macho usiku huo, na alikuwa katoka kwenda kunywa maji, na ndio
akamkuta kaka yake akiwa hapo dining room , akiongea peke yake.
Hakutaka kumshtua, alitaka kwanza aelewe kaka yake alikuwa anaongea nini peke
yake usiku huo, alisimama nyuma akimtazama jinsi kaka yake alivyolia kama mtu
aliyechanganyikiwa, ambaye mikono yake alikuwa kaiweka usoni huku akiendelea
kuongea mwenyewe peke yake, “Unanitafutia nini wewe Rebecca, umefariki miaka
mingi sana?”, alilia Mrisho huku Khadija akisikiliza huku akijawa na maswali, huyo
Rebecca alikuwa nani?, na anamtafutia nini kaka yake hadi analia hivyo peke yake usiku, na hasa alijiuliza huyo Rebecca kafa miaka mingi, alikuwa ni nani hasa.
Uso wa Khadija ulikuwa na maswali, moyo wake ulikuwa na maswali kichwa chake
pia kilikuwa na maswali, hadi akashindwa kujizuia ikabidi amuulize kaka yake.
“Kaka kulikoni?, mbona unazungumza peke yako usiku wote huu?”, aliuliza Khadija
kwa Mrisho, ambaye alishtuka na kugeuka haraka, hakutarajia kuwa kuna mtu yuko
macho usiku huo mahala hapo.
Uso wa Mrisho ulikuwa umejawa na machozi kwa kulia, huku akiwa na mshtuko wa
uwepo wa dada yake mahala hapo. Uso wa Khadija ulikuwa ni uso wenye maswali
mazito.
Kimya kikatawala kati yao. “Unafanya nini hapa usiku huu, huu si muda wa kulala”, aliongea Mrisho kwa dada
yake, akiondoa kimya kilichojitokeza. “Nimeamka kuja kunywa maji, nimekukuta unalia na kuongea peke yako mahala
hapa”, alijibu BiKhadija,
“Kwanini unalia hapa?, usiku huu, kwanini unaongea peke
yako?”, aliendelea kuuliza
Mrisho alikosa majibu ya kujibu, akaona njia pekee ya kutoka hapo ni kujitia kisirani
kisicho na sababu,
“Achana na mimi, naenda kulala, achana na mimi” aliongea Mrisho
kwa hasira na kuanza kusonga ili atoke hapo dining room, ila kabla hajampita dada
yake, Khadija kwa kutumia mkono wake wa kushoto alidaka mkono wa kulia wa
Mrisho na kuzuia asiondoke,
“Mrisho, acha kutaka kukwepa maswali yangu. Nimekukuta unalia hapa usiku huu, huku ukiongea peke yako, juu ya mwanamke anaitwa Rebecca na nimekusikia kwa
masikio yangu vizuri kabisa, ukilia ukisema, unanitafutia nini, unanitafutia nini wewe
umefariki miaka mingi iliyopita”,
aliongea Bi Khadikja huku uso kakaza akitaka hasa
kujua yaliyokuwa yanamsibu kaka yake.
Mrisho akawa kabaki kasimama hana majibu zaidi ya kueleza.
“Au umeanza
kuchanganyikiwa, maana hata Rahim na Omari wameniambia kipindi nimesafiri uliwahi
kuamka usiku hadi nje kwenye ule mti mkubwa na kuitilia mwanamke kwa jina la
Rebecca usiku wa manane ukidai kuwa ulimuona huyo mwanamke, ilhali hakukuwa na mwanmke yeyote usiku huo” aliongea Bi Khadija,
alikuwa kashasimuliwa na watoto
wake jinsi mjomba wao alitoka usiku hadi nje mbele ya nyumba kwenye mti mkubwa
akidai kusikia sauti ya kulio ya mwanamke aliyeitwa Rebecca
mtu aliyemsikia jinsi alivyokuwa ameamka na kutoka hadi hapo dining room usiku
huo na kuanza kulia na kuongea peke yake.
Huyo mtu alikuwa ni dada yake, yani Bi
Khadija. Khadija alikuwa macho usiku huo, na alikuwa katoka kwenda kunywa maji, na ndio
akamkuta kaka yake akiwa hapo dining room , akiongea peke yake.
Hakutaka kumshtua, alitaka kwanza aelewe kaka yake alikuwa anaongea nini peke
yake usiku huo, alisimama nyuma akimtazama jinsi kaka yake alivyolia kama mtu
aliyechanganyikiwa, ambaye mikono yake alikuwa kaiweka usoni huku akiendelea
kuongea mwenyewe peke yake, “Unanitafutia nini wewe Rebecca, umefariki miaka
mingi sana?”, alilia Mrisho huku Khadija akisikiliza huku akijawa na maswali, huyo
Rebecca alikuwa nani?, na anamtafutia nini kaka yake hadi analia hivyo peke yake usiku, na hasa alijiuliza huyo Rebecca kafa miaka mingi, alikuwa ni nani hasa.
Uso wa Khadija ulikuwa na maswali, moyo wake ulikuwa na maswali kichwa chake
pia kilikuwa na maswali, hadi akashindwa kujizuia ikabidi amuulize kaka yake.
“Kaka kulikoni?, mbona unazungumza peke yako usiku wote huu?”, aliuliza Khadija
kwa Mrisho, ambaye alishtuka na kugeuka haraka, hakutarajia kuwa kuna mtu yuko
macho usiku huo mahala hapo.
Uso wa Mrisho ulikuwa umejawa na machozi kwa kulia, huku akiwa na mshtuko wa
uwepo wa dada yake mahala hapo. Uso wa Khadija ulikuwa ni uso wenye maswali
mazito.
Kimya kikatawala kati yao. “Unafanya nini hapa usiku huu, huu si muda wa kulala”, aliongea Mrisho kwa dada
yake, akiondoa kimya kilichojitokeza. “Nimeamka kuja kunywa maji, nimekukuta unalia na kuongea peke yako mahala
hapa”, alijibu BiKhadija,
“Kwanini unalia hapa?, usiku huu, kwanini unaongea peke
yako?”, aliendelea kuuliza
Mrisho alikosa majibu ya kujibu, akaona njia pekee ya kutoka hapo ni kujitia kisirani
kisicho na sababu,
“Achana na mimi, naenda kulala, achana na mimi” aliongea Mrisho
kwa hasira na kuanza kusonga ili atoke hapo dining room, ila kabla hajampita dada
yake, Khadija kwa kutumia mkono wake wa kushoto alidaka mkono wa kulia wa
Mrisho na kuzuia asiondoke,
“Mrisho, acha kutaka kukwepa maswali yangu. Nimekukuta unalia hapa usiku huu, huku ukiongea peke yako, juu ya mwanamke anaitwa Rebecca na nimekusikia kwa
masikio yangu vizuri kabisa, ukilia ukisema, unanitafutia nini, unanitafutia nini wewe
umefariki miaka mingi iliyopita”,
aliongea Bi Khadikja huku uso kakaza akitaka hasa
kujua yaliyokuwa yanamsibu kaka yake.
Mrisho akawa kabaki kasimama hana majibu zaidi ya kueleza.
“Au umeanza
kuchanganyikiwa, maana hata Rahim na Omari wameniambia kipindi nimesafiri uliwahi
kuamka usiku hadi nje kwenye ule mti mkubwa na kuitilia mwanamke kwa jina la
Rebecca usiku wa manane ukidai kuwa ulimuona huyo mwanamke, ilhali hakukuwa na mwanmke yeyote usiku huo” aliongea Bi Khadija,
alikuwa kashasimuliwa na watoto
wake jinsi mjomba wao alitoka usiku hadi nje mbele ya nyumba kwenye mti mkubwa
akidai kusikia sauti ya kulio ya mwanamke aliyeitwa Rebecca