SIMULIZI: Tubu

nasrimgambo

JF-Expert Member
Jan 10, 2017
1,858
2,348
Kijana Rahim anatokea kumpenda binti Sarah katika nyakati za mwisho za uhai wa binti huyo.

Wasichokijua ni kwamba penzi lao limeletwa kwa nguvu ya ajabu ili mtu aliyeharibu maisha ya Sarah atubu na kulipia dhambi yake.


Unaweza pia kuisoma kwenye telegram

 
Mwandishi: Nasri Mgambo
Jina la simulizi: TUBU- DHAMBI HADHARANI

Sehemu: Ya kwanza:Rahim Amuokoa Sarah


Ilikuwa ni usiku wa manane. Kwenye chumba kidogo, chenye godoro tu bila ya
kitanda wala mito na shuka. Sarah alikuwa amelala, huku akiweweseka, maana alikuwa
akiota ndoto mbaya.


Aliota yupo kizimbani, kwenye chumba cha mahakama, akisubiri kusomewa
hukumu. Kila mtu katika chumba cha mahakama alionekana kuwa makini kumsikiliza
hakimu. Sarah nae alikuwa kasimama kizimbani, akitetemeka kwa hofu. Dhahiri Sarah
alionekana kuwa anaogopa hukumu aliyosubiri kupewa. Jasho jembamba lilimchururika
katika uso wake, huku machozi yakimtiririka, na kichwa alikiinamisha.

Hakukuwa na
huruma juu yake.
Mara sauti ya hakimu ikasikika, “kwa mamlaka niliyopewa na jamhuri ya muungano
wa Tanzania, nina kuhukumu adhabu ya kunyongwa mpaka kufa, binti Sarah Frank
Malya, kutokana na mauaji uliyofanya”. Kilio kilimtoka Sarah. Mwisho wake ulikuwa
umefika.


Mara Sarah akakurupuka kwa kilio toka kwenye ndoto hiyo ya kutisha. Ni kweli
jasho jembamba lilimtiririka. Moyoni mwake alikuwa kweli anaogopa alichokuwa
kakiota.


Sarah akainuka toka juu ya godoro alilokuwa amelalia na kisha akapiga magoti
kuomba huku akilia. “Eeh baba uliye mbinguni, mimi mja wako naomba uniepushe na
mabalaa haya ninayopitia, najua nimetenda kosa Mungu wangu, na watu wanataka
nilipie makosa yangu, nami sina pa kukimbilia, nao karibuni huenda watanipata ili
nilipie makosa yangu, ila baba naomba huruma yako. Baba wewe unajua yote niliyopitia
kwenye maisha yangu. Nami najiona sifai, ila wewe ni Mungu wa kutoa misamaha”.


Mara Sarah akanyamaza na kuacha kulia, kisha akaendelea kuomba, “najua mimi ni
mkosaji. Napaswa nitubu dhambi zangu, na kwamba ni kweli imeandikwa kwenye
vitabu kuwa ukweli humweka mtu huru. Ila baba naomba nguvu yako, sina nguvu ya
kukiri nilichokitenda kwa maana siamini kama wana wa adam watakubali kuniweka
huru kwa makosa niliyofanya”


Hicho kilikuwa ni kilio pamoja na maombi ya binti Sarah kwa Mungu wake, ndani ya
chumba kidogo kisicho na kitu cha maana ndani yake, zaidi ya kigodoro chakavu
kilichokosa kitanda. Chumba hicho cha Sarah kilikuwa katika nyumba moja ya kupanga
iliyokuwa katika moja ya vimitaa vingi vya kitongoji cha Mwananyamala katika jiji la Dar
es Salaam.
….……………
 
Kilomita kadhaa kutoka mitaa ya Mwananyamala, kwenye mitaa maarufu ya
Mikocheni, kulikuwa na jumba. Jumba la kifahari, ambalo ndani yake kuliishi familia
yenye uwezo mkubwa.

Humo waliishi Bi. Fahima Abeid pamoja na familia yake ambao
walikuwa ni wanawe wawili wa kiume pamoja na kaka yake, mwanae mkubwa aliitwa
Rahim na mdogo aliitwa Omari, huku mjomba wao yani kaka yake Bi.Fahima alikuwa
akiitwa Mrisho.


Kwa familia ya Bi.Fahima usiku wao ulikuwa ni tulivu, haukuwa wa ndoto za kutisha
na kuweweseka kama ilivyokuwa kwa Sarah wa Mwananyamala, walilala kwa kukoroma
na kama waliota ndoto yoyote, basi huenda waliota ndoto nzurinzuri.

Jua lilipochomoza asubuhi, liliwaamsha ili kuanza siku mpya tena ilikuwa ni siku ya
furaha zaidi kwao, maana ilikuwa ni siku ya kuzaliwa ya Bi. Fahima.
Watoto zake pamoja na mjomba wao walimuandalia keki na kumuimbia nyimbo ya
siku ya kuzaliwa. Akapuliza kuzima mishumaa iliyokuwa kwenye keki, baada ya
kujisemea kimoyomoyo mambo mazurimazuri aliyotamani Mungu ampe kwenye umri
wake mpya. Kisha akakata keki na wakalishana wote kwa furaha.


Majira fulani mchana wa siku hiyo Bi.Fahima alikuwa chumbani kwake pamoja na
housegirl wake. Housegirl wake huyo, alikuwa akiitwa Kirua. Wakati huo Kirua alikuwa
akimsaidia Bi Fahima kupanga nguo zake kwenye sanduku. Juu ya kitanda cha Bi.
Fahima kulikuwa na sanduku pamoja na nguo ambazo Kirua alikuwa akizipanga
kwenye sanduku.


Pembeni kidogo ya sanduku hapo kitandani kulikuwa na nyaraka kadhaa pamoja na
pasipoti ya kusafiria, Bi Fahima alikuwa anaajindaa kwaajili ya safari.


Muda wote huo wakati Kirua anapanga nguo, Bi Fahima alikuwa anaongea na mtu
kwenye simu, alikuwa akisema, “sawa sawa, ndio tunaelekea Singapore mchana wa leo.
Mimi pamoja na mkurugenzi. Kama mlivyoamua kwenye kikao cha bodi, tunaenda
kufanikisha makubaliano baina ya kampuni ya KSUH na kampuni yetu ya DM Trading.
Niwatoe hofu nina imani kubwa na weledi wa bosi pamoja na wa kwangu binafsi,
kwamba tutaweza kuishawishi KSUH kuifanya kampuni yetu ya DM kuwa ndio
msafirishaji wake mkuu wa bidhaa zake zote wanazonunua ama kuuza kutoka kwenye
nchi zote za Afrika mashariki”.


Yani kwa kifupi tuseme maongezi ya Bi Fahima kwenye simu yalikuwa ni maongezi
makubwa makubwa. Yani ni kwamba, Bi Fahima alikuwa akifanya kazi kwenye moja ya
makampuni makubwa ya usafirishaji nchini Tanzania, iliyoitwa Dar es Salaam Maritime
Trading. Kampuni hiyo ilimiliki meli kubwa kubwa na ilijihusisha na usafirishaji wa
mzigo kwenda na kuingia baina ya eneo lote la afrika mashariki na nchi za Asia, Ulaya
na hata marekani. Kampuni hiyo ilikuwa na ofisi zake za makao makuu katika moja ya
majengo marefu huko katikati ya jiji

Na Bi Fahima alikuwa cheo kikubwa kazini na aliaminika sana kwa uhodari wake wa
kufanikisha shughuli za kiofisi.

Kwa kazi yake hiyo, Bi Fahima alikuwa akisafiri mara
kwa mara kwenda ughaibuni, ilikuwa kawaida kwenda nchi kama Uturuki, China,
Singapore hata Canada na Australia kwake kwenda ilikuwa ni jambo tu la kawaida.


Baada ya kumaliza kujiandaa, Bi Fahima aliagana na familia yake, ambao nao
walimtakia safari njema na kumtakia heri ili akafanye kazi iliyompeleka huko Singapore
kwa ufanisi na salama.

Maisha ya familia ya Bi.Fahima yalikuwa na furaha. Hakukuwa na shida wala kasoro
kubwa ya kuwasononesha ama kuwahofisha. Maisha yao yalijawa na furaha na tabasamu
na kumbukumbu nzurinzuri siku zote.
….…………………………..
 
Kijana mkubwa wa familia familia ya Bi.Fahima, yani Rahim, alikuwa ni mtanashati
mwenye umri wa miaka ishirini na tano hivi na mhitimu wa shahada ya kwanza ya
uchumi toka chuo kikuu cha Dar es Salaam.

Alikuwa mcheshi na muongeaji. Na moja
ya hobi zake ilikuwa ni kukimbia na kupunga upepo ama kusoma vitabu kwenye fukwe
zilizokuwa jirani huko mitaa ya kwao ya mikocheni.
Bai, siku moja Rahim alikuwa akifanya mazoezi ufukweni, akikimbia.

Ndipo
akamuona binti wa miaka kama ishirini na tano hivi akiwa anatembea pole pole
akionekana kama kachanganyikiwa na mwenye mawazo mengi.

Binti huyo hakuwa mwengine bali alikuwa ni Sarah, yule binti aliyeishi maeneo ya
Mwananyamala.

Rahim alitamani kufahamu kilichokuwa kinamsibu binti huyo hata kuonekana
mnyonge , mwenye huzuni nyingi na pengine kuchanganyikiwa. Lakini hakuona kama
ilikuwa ni busara kuanza tu kumuongelesha mtu ambae hafahamiani nae na kuanza
kumuuliza maswali ya kibinafsi sana, akaendelea na mazoezi yake pasina
kumuongelesha, lakini pia muda wote aliendelea kumtupia macho.

Sarah siku hiyo alikuwa kavalia gauni la rangi ya kijani, ambalo lenyewe pamoja na
nywele zake ndefu zilikuwa zikipepeswa kwa upepo wa bahari.

Hiyo ilikuwa ni moja ya
siku ngumu sana kwa Sarah. Kichwani alikuwa na wazo moja tu. Nalo lilikuwa ni
kujongea kuelekea uelekeo wa bahari na kujizamisha, ili apoteze maisha. Sarah alikuwa
kapania kujiua siku hiyo.

Taratibu, Sarah alianza kujongea kuelekea kwenye maji toka ufukweni.

Sasa uso
wake uliacha kutiririka machozi. Kitu pekee alichowaza kilikuwa ni kujitosa kwenye
hayo maji, kisha kutapatapa na kufa kabisa, hakutaka kabisa kuoina jioni wala kesho ya
siku hiyo, aliona ni kheri saa hiyo ndio iwe saa ya mwisho ya maisha yake hapa duniani.

Kwa mbali Rahim aliyekuwa akiendelea na mazoezi yake aliweza kumuona Sarah
akielekea majini. Kwa haraka sana akili yake ikamwambia kuwa bitni huyo alidhamiria
kujidhuru.

Akawa anamuona jinsi alivyoendelea kujiingiza katika ya maji, maji yalisha
mvuka Sarah kifua ni mabega ndio yalikuwa yanafuatia. Hatimaye maji yakamfunika
kabisa Sarah
 
Kwa hofu kubwa Rahim akaanza kupiga mayowe na kukimbilia sehemu ile ambayo
Sarah alikuwa amejizamisha.

“Anajiuaaaa, anajiua jamani, anajiua”, watu kadhaa
waliokuwa karibu na eneo hilo waliweza kumuona Rahim akikimbilia eneo hilo na wao
wakaanza kukimbia wakimfuatia.
Rahim akajitupa kwenye maji, akamuona Sarah akiibuka kwenye maji akisukumwa
na mawimbi ya maji huku akitapatapa, macho akiwa ameyatoa, maji yakiingia puani na
midomoni.


Kwa ujasiri Rahim akaogelea hadi akamfikia Sarah na kuanza kumvuta kumrudisha
ufukweni. Sarah, mwenyewe alikuwa yuko hoi.


Kikundi cha watu kilikuwa kimekusanyika kumsaidia Rahim kumuokoa binti huyo
ambaye wao wote hawakuwa wakimjua hata jina.
Baada ya kumfikisha ufukweni, Rahim alimlaza Sarah na kuanza kuminya tumboni,
ili kumtoa maji mengi aliyomeza, huku akiwa na wasiwasi mkubwa.
Sarah alionekana kupoteza fahamu. Rahim akaanza kuhisi kuwa huenda binti huyo
amekufa hivyo akaanza kupaniki, huku akiendelea kumkamua tumbo na kumpulizia
hewa mdomoni.


Mara Sarah akazinduka na kucheua maji mengi, kisha akaanza kukohoa.

Rahim na
kikundi cha watu waliokuweko hapo wakafurahi kuona kuwa binti huyo kazinduka.

Pia walitaka kufahamu huyo binti ni
nani?,anatokea wapi?, na kapatwa na nini hata akataka kujiua.

Hivyo wakabaki hapo pembeni kumsubiri apate nguvu ili wamuhoji.
Baada ya dakika kadhaa kupita Sarah akaanza kuonekana kupata nguvu, taratibu
akaanza kuinuka na kusimama, bila kuzingatia watu waliomzunguka.


“Tulia kwanza, ni vyema uendelee kupumzika, tulia”, aliongea Rahim akimsihi Sarah
atulie. “Achana na mimi, hunijui, sikujui kwanini umeniokoa?”, alijibu Sarah kwa hasira
iliyoambatana na uchovu wa baada ya kumezaa maji mengi na kuzimia, aliwaangalia
Rahim na wezake, huku akianza taratibu kuondoka, aliwaona kuwa ni watu
waliokwamisha mpango wake wa kutaka kujiua.


“Wewe unaitwa nani?, umetokea wapi na kwanini unataka kujtoa uhai wako wa
thamani?” alihoji Rahim kwa shauku na pengine hasira, kichwani mwake hakuweza
kuelewa kabisa iweje binti kama huyo alitaka kujiua.

Pia wale watu wengine
waliokusanyika walikuwa na nyuso zenye maswali kama Rahim, nao walitaka kujuu
kulikoni binti huyo kafikia hatua ya kutaka kujitoa uhai wake.

“Wewe na wenzako, sijawatuma mnisaidie, mniache niondoke”, alijibu Sarah kwa
hasira na kuanza kuondoka eneo hilo akiwaacha Rahim na wale mashuhuda wengine wakibaki
na maswali yao yaliyokosa majibu.
Inaendelea….………………….
 
Kwa hofu kubwa Rahim akaanza kupiga mayowe na kukimbilia sehemu ile ambayo
Sarah alikuwa amejizamisha.

“Anajiuaaaa, anajiua jamani, anajiua”, watu kadhaa
waliokuwa karibu na eneo hilo waliweza kumuona Rahim akikimbilia eneo hilo na wao
wakaanza kukimbia wakimfuatia.
Rahim akajitupa kwenye maji, akamuona Sarah akiibuka kwenye maji akisukumwa
na mawimbi ya maji huku akitapatapa, macho akiwa ameyatoa, maji yakiingia puani na
midomoni.


Kwa ujasiri Rahim akaogelea hadi akamfikia Sarah na kuanza kumvuta kumrudisha
ufukweni. Sarah, mwenyewe alikuwa yuko hoi.


Kikundi cha watu kilikuwa kimekusanyika kumsaidia Rahim kumuokoa binti huyo
ambaye wao wote hawakuwa wakimjua hata jina.
Baada ya kumfikisha ufukweni, Rahim alimlaza Sarah na kuanza kuminya tumboni,
ili kumtoa maji mengi aliyomeza, huku akiwa na wasiwasi mkubwa.
Sarah alionekana kupoteza fahamu. Rahim akaanza kuhisi kuwa huenda binti huyo
amekufa hivyo akaanza kupaniki, huku akiendelea kumkamua tumbo na kumpulizia
hewa mdomoni.


Mara Sarah akazinduka na kucheua maji mengi, kisha akaanza kukohoa.

Rahim na
kikundi cha watu waliokuweko hapo wakafurahi kuona kuwa binti huyo kazinduka.

Pia walitaka kufahamu huyo binti ni
nani?,anatokea wapi?, na kapatwa na nini hata akataka kujiua.

Hivyo wakabaki hapo pembeni kumsubiri apate nguvu ili wamuhoji.
Baada ya dakika kadhaa kupita Sarah akaanza kuonekana kupata nguvu, taratibu
akaanza kuinuka na kusimama, bila kuzingatia watu waliomzunguka.


“Tulia kwanza, ni vyema uendelee kupumzika, tulia”, aliongea Rahim akimsihi Sarah
atulie. “Achana na mimi, hunijui, sikujui kwanini umeniokoa?”, alijibu Sarah kwa hasira
iliyoambatana na uchovu wa baada ya kumezaa maji mengi na kuzimia, aliwaangalia
Rahim na wezake, huku akianza taratibu kuondoka, aliwaona kuwa ni watu
waliokwamisha mpango wake wa kutaka kujiua.


“Wewe unaitwa nani?, umetokea wapi na kwanini unataka kujtoa uhai wako wa
thamani?” alihoji Rahim kwa shauku na pengine hasira, kichwani mwake hakuweza
kuelewa kabisa iweje binti kama huyo alitaka kujiua.

Pia wale watu wengine
waliokusanyika walikuwa na nyuso zenye maswali kama Rahim, nao walitaka kujuu
kulikoni binti huyo kafikia hatua ya kutaka kujitoa uhai wake.

“Wewe na wenzako, sijawatuma mnisaidie, mniache niondoke”, alijibu Sarah kwa
hasira na kuanza kuondoka eneo hilo akiwaacha Rahim na wale mashuhuda wengine wakibaki
na maswali yao yaliyokosa majibu.
Inaendelea….………………….
Tunasubiri muendelezo mkuu,, ukiweka nitag
 
Mwandishi: Nasri Mgambo
Jina la simulizi: TUBU
Sehemu: Ya pili

2. Mwanamke wa Ajabu.

Rahim na wale watu wengine walibaki pale ufukweni wakimtazama jinsi Sarah
alivyowaacha na kuondoka zake.

Hadi wakati huo walikuwa bado hawajajua jina lake.

Walibaki na maswali yao mengi. Yule binti ni nani?, katokea wapi?, kwanini alitaka
kujiua kwa kujizamisha kwenye maji ya bahari?.

Wote hawakuwa na majibu ya maswali
hayo. Ila Rahim alishukuru kuwa walau aliweza kuokoa maisha ya binti huyo. ….………………………..

Jioni ya siku ile Rahim aliitumia kuwasimulia mjomba wake na mdogo wake jinsi
alivyomuokoa binti asiyemfahamu, aliyetaka kujiua kwa kujizamisha majini.

“Inasikitisha sana, inakuwaje hata mtu anafikia hatua ya kutaka kujitoa uhai wake
yeye mwenyewe”, alishangaa Omari, mdogo wake na Rahim.

“Natamani ningekuwepo , mimi nisingeruhusu aondoke mpaka aelezee sababu hasa ya kutaka kujifanyia kitendo
hicho cha kikatili”, aliendelea Omari.

Muda wote mjomba wao alikuwa akiwasikiliza kwa makini. “Maisha yametofautiana
sana, watu hupitia changamoto kwenye maisha na wengine hata hufikia hatua mbaya
zaidi ya kutaka kujitoa uhai wao wenyewe, kama huyo binti. Ndiyo maana siku zote
mimi naamini, tunatakiwa tuishi kwa upendo , kujaliana na kusaidiana”, aliongea
mjomba wao, maneno hayo ya busara, na akaendelea kusifu ushujaa wa Rahim, “umefanya jambo jema sana, kuokoa uhai wa binti huyo, najivunia sana kwa ushujaa
wako na moyo wako mpwa wangu” Rahim na Omari, walikuwa wanaelewana sana na mjomba wao huyo, waliyemuita
‘mjomba Mrisho’.

Alikuwa kama baba kwao. Walimuheshimu sana. Siku zote aliongea
maneno ya busara. Na walipenda sana kusikiliza ushauri wake kwenye masuala yao
waliyopitia kama vijana.

Wao walimuona mjomba wao kama mtu msafi wa roho na tabia, na mwenye busara
nyingi, walijivunia kumuita mjomba. Kila walipopata changamoto yoyote waliyoshindwa
kumuhusisha mama yao kama vijana wa kiume, kimbilio lao lilikuwa kwa mjomba wao, mjomba Mrisho. Mjomba Mrisho alikuwa na miaka hamsini hivi.

Waliishi nae nyumbani kwao
pamoja na mama yao. Japo aliwahi kuwa na mke huko nyuma, mkewe alimuacha na
kuondoka pamoja na watoto.
 
Mrisho hakuwa tajiri kulinganisha na dada yake, Bi Fahima yani mama yao kina
Rahim.

Lakini yeye pia alikuwa akifanya kazi kwenye moja ofisi ndogo za kampuni ya
DM Trading ambayo ndiyo Bi Fahima aliifanyia kazi pia. ….………………………….

Majuma kadhaa yalipita. Rahim aliendelea kuwa na mswali juu ya binti aliyemuokoa. Alitamani amuone tena ili amuulize maswali yake. Kama mazoea yake yalivyokuwa, Rahim aliendelea na desturi yake ya kwenda
kwenye fukwe za karibu na kwao mikocheni, kufanya mazoezi ama kupunga upepo
huku akisoma vitabu alivyopenda. Alifanya hivo huku akiamini kuwa huenda siku moja
atamuona yule binti tena pale ufukweni.

Alianza kujenga tabia ya kuangazaangaza fukwe
yote kila alipofika, akitumaini kuwa huenda atabahatisha kumuona. Haikuwa hivyo, Rahim hakumuona tena yule binti, na kadri siku zilivyokwenda
aliamini kuwa basi hatomuona tena. Hata akaanza kusahau kuangazaangaza ufukwe
kubahatisha kumuona.

Basi siku moja bila kutarajia, Rahim alienda ufukweni kufanya mazoezi. Alikuwa
kavalia mzula (hoody) juu ya nguo zake za mazoezi. Wakati anaendelea na kufanya mazoezi, mara akamuona mtu aliyevalia mzula kama
yeye amekaa peke yake ufukweni.

Alikuwa ni binti. Mwanzoni Rahim hakumzingatia
vizuri huyo binti, aliendelea kufanya mazoezi hadi pale alipomkaribia na kumtupia
macho usoni. Rahim hakuamini macho yake.

Alikuwa ni yule binti ambaye alimuokoa majuma
kadhaa yaliyopita, yani Sarah. Sarah alikuwa amejikalia zake ufukweni amefumba macho kama mtu anayewaza ama
kuombea jambo fulani, alikuwa bado hajamuona Rahim.

Taratibu Rahim akaacha
mazoezi yake na kuanza kujongea hadi alipokaa Sarah. “Samahani”, Rahim alimuongelesha Sarah kumshtua. Taratibu Sarah alifungua
macho yake, na akamuona Rahim amesimama mbele yake.

Mara moja akamkumbuka
kuwa ni yule kijana aliyemuokoa wiki kadhaa zilizopita. “Unanikumbuka?, nilikuokoa. Ulitaka kujizamisha kwenye maji siku ile, nikakuokoa”, aliongea Rahim.

Sarah alibaki anamtazama Rahim bila kumjibu chochote. Rahim akanyoosha mkono
wake wa kulia kumpa salamu Sarah, “Naitwa Rahim, wewe je?”, alijitambulisha Rahim. Sarah hakupokea mkono huo, uso wake ulionesha kubughudhika. “Kwani wewe unataka nni?”, aliongea Sarah, kumuuliza Rahim. “Mimi ninachotaka…..?” aliuliza Rahim huku akiweka tabasamu usoni mwake, kisha
akakaa pembeni ya Sarah, wakawa wako wawili wamekaa hapo ufukweni pamoja.
 
Aliendelea kuongea, “Mimi ninachotaka ni majibu ya maswali yangu”. “Yepi?”, alihoji Sarah. “Wewe ni nani?, unatokea wapi?, kwanini ulitaka kujiua?” Rahim aliyataja maswali
yake, huku sasa uso wake ukibadilika na kuwa siriaz, akimtazama Sarah. Hakukuwa na namna ya Sarah kukwepa kumjibu Rahim maswali yake. Rahim
alionesha hasa kutaka kupata majibu ya maswali hayo.

“Nilitaka kujiua ili kila kitu kinachonikwaza kwenye maisha yangu kiishe, nilifikiri
kuwa labda ningejitoa uhai wangu basi na matatizo yangu yangeisha hapo, haya maisha
kwangu hayana furaha, hukupaswa kuniokoa siku ile, ungeniacha nife”, aliongea Sarah
kwa uchungu huku akijitahidi kutolia. “Unaweza kuniambia jambo hasa linalokufanya ujione unastahili kifo badala ya
kupambania uhai wako?” aliuliza Rahim. “Siwezi kukwambia. Siwezi kumuamini mtu yeyote kumwambia”
“Unamaanisha nini, huwezi kumuamini mtu yeyote kumwambia?”alihoji Rahim. “Wewe jua hivyo siwezi kukwambia, naweza kuharibu zaidi nikikwambia” , alijibu
Sarah


Kauli hiyo ilimpa maswali zaidi Rahim kuliko majibu, “Ni nini hicho?” alihoji. “Nimefanya kosa kubwa, pengine nastahili ninayopitia” alijibu Sarah, kisha
akasimama, Rahim nae akasimama. “Nashukuru kwa ushujaa wako wa kuniokoa, asante sana.

Ila sidhani kama unastahili
kujua zaidi kuhusu mimi ama kunisaidia zaidi ya ulivyofanya”, aliendelea kusema
maneno hayo Sarah, huku akitaka kuanza kuondoka mahala hapo. “Sikia”, alisema Rahim huku akimshika mkono Sarah, “Sikia, mimi sijui umefanya
kosa gani huko kwenye maisha yako. Ninachojua tu ni kwamba, maisha ni zawadi, tena
adimu sana.

Naamini ni haki yetu sote sisi wanadamu kuweza kuwa hai na kupambania
uhai wetu. Sikia, kama unajiona umnyonge sana na dhaifu, unajiona kuwa huwezi
kusimama na kwamba kujitoa uhai ndio suluhu ya maswahibu upitiayo, basi nakuomba
jambo moja tu, jambo moja tu”, aliongea Rahim kwa uchungu mwingi, uso wake
ukionesha hayo maneno yalitoka kwenye uvungu wa moyo wake kabisa na alimaanisha
kila neno. “Jambo gani?”, alihoji Sarah, huku akimuangalia usoni Rahim.

Sarah hakuwahi
kwenye maisha yake kumuona mtu wa kiume akionesha kujali kiasi hicho juu yake. Yeye alijua wanaume wote walikuwa ni watu wagumu wasiojali, hasa aliwaona kuwa ni
wasiomjali yeye. Rahim alionesha usoni mwake jinsi alivyojali hasa juu ya Sarah, japo
 
Japo hawakuwa wakifahamiana, ikumbukwe hadi wakati huo Sarah alikuwa bado hajamtajia
Rahim jina lake.

Huku akiwa bado hajaacha kuushikilia mkono wa Sarah, Rahim aliendelea kuongea, “Ninataka unipe nafasi ya kukuonesha kuwa unastahili kuishi kwa furaha bila
kuhuzunika ama kujiona unastahili kupoteza maisha yako. Naomba nafasi, nikuoneshe
sura nyengine ya maisha tofauti ya hii uliyonayo juu ya maisha yako, hii sura ya majonzi
na kujutia”.

Rahim aliongea maneno hayo toka moyoni mwake hata sasa machozi
yakawa yanamlengalenga machoni mwake. Sarah akabaki anamtazama Rahim machoni. Hakika moyoni mwake alihisi kitu cha
pekee ambacho hakuwahi kukihisi hapo kabla.

Kwake ilikuwa ni mara ya kwanza
kuoneshwa kujaliwa na kuongeleshwa kwa kujaliwa na mtu wa jinsia ya kiume kwa kiasi
hicho ambacho Rahim alionesha kujali na kumuongelesha. Pengine alihisi kuwa
amelala anaota.

“Nataka tuendelee kuwasiliana baada ya leo”. Alisema Rahim, na hatimaye akaachia
mkono wa Sarah. “Kwanza unaitwa nani?” aliuliza Rahim, yani hatimaye alikumbuka
kuwa hadi wakati huo alikuwa bado hata hajui jina la aliyekuwa anazungumza nae. “Naitwa Sarah”, alijibu Sarah.

Naye Rahim akaweka tabasamu usoni na kuweka
mkono wake wa kulia kwenye mfuko wa suruali yake, kisha akatoa kalamu. “Una bahati sana Sarah, huwa sizunguki na peni kipindi nafanya mazoezi ila leo
ninayo”, aliongea Rahim huku akitabasamu, kisha akachukua mkono wa kushoto wa
Sarah na kuunyayua na kuanza kuuandika.

“Hii ni namba yangu, nataka unipigie”, Rahim aliongea huku akionesha kufurahi. “Kwanini unafanya hivi?, kwanza hata haunifahamu.” alihoji Sarah
“Ukinipigia na kuendelea kuwasiliana tutafahamiana, wote wanaojuana kuna kipindi
hawakujuana, ikatokea siku wakafahamiana, hatimaye wakawa wanajuana, basi ndivyo
hivyo hivyo, mimi nawe tutafahamiana”, alisema Rahim na kucheka, nae Sarah
akacheka, kisha akaitazama namba ambayo Rahim aliiandika kwenye kiganja chake cha
mkono, akamtazama, wakatazamana wakitabasamu, kisha Sarah akageuka kuondoka
hapo ufukweni huku akiwa na tabasamu usoni mwake, nyuma Rahim alibaki
akimtazama pia, huku uso wake ukiwa na tabasamu la furaha huku kakenua meno yote.

Wakati hayo yanaendelea hapo ufukweni, bila ya wao Rahim na Sarah kujua, kumbe
kulikuwa na mwanamama kasimama anawatazama.

Alikuwepo anawatazama toka
mwanzo wa maongezi yao na alibaki anawatazama hadi jinsi Sarah alivyokuwa
anaondoka kwa tabasamu hapo ufukweni na kumuacha Rahim akimtazama kwa
kutabasamu pia.
 
Mwanamke huyo alisimama kwenye moja ya minazi iliyokuwapo hapo ufukweni. Alivalia mavazi meupe yaliyong’ara sana.

Hakika hakuonekana kuwa ni binadamu wa
kawaida.

Baada tu ya Sarah kuondoka eneo hilo la ufukweni, mwanamke huyo alibaki
anamtazama Rahim, kisha ghafla akatoweka. Ni wazi hakuwa binadamu wa kawaida. Inaendelea …………………………………….
 
Mwandishi: Nasri Mgambo
Simulizi: TUBU
Sehemu ya Tatu: MZIMU


Zilikuwa ni hisia za ajabu kwa Rahim. Ilikuwa dhahiri kwake kuwa alikuwa
anampenda Sarah. Binti ambaye hakumfahamu vizuri, aliyekutana nae mara mbili tu.


Binti ambaye alikuwa anapitia matatizo kiasi cha kutamani kutaka kujiua.

Kwa akili za kawaida hakuna kijana ambaye angekuwa tayari kujiingiza kwenye
mahusiano na binti ambaye ana matatizo kiasi hicho. Tena asiyetaka kuelezea matatizo
yake kwa madai kuwa hakuna wa kuweza kumsaidia na tena anayekiri kwamba
amefanya kosa kubwa linalomfanya apitie mswahibu yote apitiayo.
Hadi wakati huo bado Rahim alikuwa na maswali. Ni kosa gani kubwa hasa
alilolifanya Sarah?, na je, kutokana na kufanya kosa hilo ni maswahibu gani yalimfika
binti huyo hata aone suluhu pekee ni kutaka kutoa uhai wake?.


Rahim hakupata majibu ya maswali yake hayo. Ila kwake ilikuwa ni dhahiri kuwa
alikuwa ametokea kumpenda Sarah na alitamani apate kumfahamu zaidi.
Na alikuwa ametokea kuwa na hisia nae hasa, kwa maana hata maongezi yake
yaliakisi hilo. Maongezi kati yake na mjomba wake na mdogo wake sasa yalihusisha
kumuongelea Sarah.
“Sikuamini nilipomuona tena ufukweni, maana yalipita majuma kadhaa tangu
nimuokoe alipotaka kujizamisha kwenye maji. Safari hii niliongea na kumuuliza
maswali niliyokuwa nayo kwake, kumbe anaitwa Sarah. Ila bado hataki kuongelea juu
ya matatizo yake yaliyopelekea kutaka kutoa uhai wake”, aliongea Rahim akirudia tena
simulizi yake jinsi alivyokutana na Sarah kwa mara ya pili kule ufukweni.

Hiyo ilikuwa
pengine zaidi ya mara tatu anarudia kusimulia jambo hilohilo kwa mjomba wake na
mdogo wake, nao sasa walianza kuchoka kusikiliza simulizi hiyo kila mara.


“Kaka, hivi si ushatusimulia jinsi ulivyokutana na huyo Sarah?, hivi unajua inachosha
kiasi gani kukusikiliza stori yako hiyohiyo moja?”, aliuliza Omari, akionesha kuboreka
na simulizi ya Rahim jinsi alivyokutana na Sarah.


“Rahim, au umempenda huyo binti?, maana unatuchosha na kusimulia kuhusu yeye
tu, ukienda ukirudi wewe ni kusimulia kuhusu huyo Sarah”, aliuliza bwana Mrisho,


“Unazungumzia nini mjomba?, sio kama unavyofikiria wewe kwamba nimempenda,
mimi namuona tu ni binti anayetilia huruma, na anayeshangaza jinsi alivyokata tamaa,
kwakweli mimi naona anastahili huruma, sio kwamba nampenda” alijitetea Rahim na
kujibaraguza.
….………………………….
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom