nasrimgambo
JF-Expert Member
- Jan 10, 2017
- 1,920
- 2,529
- Thread starter
- #21
Juma moja lengine likapita bila ya Rahim kupokea simu ama ujumbe toka kwa
Sarah. Alitegemea binti huyo kuwa atampigia simu ama japo atamtumia ujumbe.
Taratibu akaanza kuhisi kuwa pengine Sarah hatomtafuta. Hisia hiyo ilianza
kumkwaza, kwa maana sasa ilikuwa dhahiri kwake kuwa alikuwa anampenda.
Naalitamani waonane tena kwa mara nyengine, pengine hata amuambie lililo moyoni
mwake. Lakini siku zilikuwa zimepita na Sarah hakumtafuta kabisa Rahim.
Ila pasina kutarajia siku moja, Rahim akiwa bize na mambo yake simu iliita. Ilikuwa
ni namba ngeni. Kupokea hakuamini masikio yake , alisikia sauti ya Sarah, hatimaye
Sarah aliamua kumpigia.
“Habari, nimekukumbuka, za toka siku ile?”, alisalimia Sarah. Sauti yake ambayo
pengine ni ya kawaida sana safari hii haikuwa ya kawaida masikioni mwa Rahim.
Alionakuwa sauti hiyo ilikuwa laini na tamu, hata akakosa maneno ya kujibu salamu ya Sarah,
akawa kama amepigwa na bumbuwazi, alihisi hisia za ajabu, hatimaye alikuwa kapokea
simu aliyokuwa akiisubiri kwa hamu toka kwa binti huyo.
“Natamani tuonane, hata mimi nilikuwa nimekumiss, natamani nikuone”, aliongea
Rahim, kwenye simu. “Sawa tunaweza kuonana”, lilikuwa ndilo jibu la Sarah.
Kama ilivyokuwa kwa Rahim kuwa alikuwa ameelemewa na hisia nzito za kumpenda
Srah basi pia ilikuwa hivyohivyo kwa Sarah.
Sarah alimuona Rahim kama mtu wa ajabu. “Sijawahi kukutana na mtu wa aina hii
kwenye maisha yangu”, Sarah alijiambia , “ulikuwa wapi siku zote?, ungekuja mapema
kwenye maisha yangu”, aliendelea kujiuliza Sarah moyoni mwake.
….…………………………………………..
Maisha yake yote Sarah alikutana na watu wa hovyo, kuanzia kwenye familia ya kwao
na ndugu na marafiki, pia hadi wakati huo na umri wake wa miaka ishirini na mitano
alikuwa hajawahi kupendana na mtu na hakuwai kufikiria hapo kabla, kwamba hilo
litatokea, maana watu kadhaa aliowahi kuhisi ni wema kwake wote waligeuka kuwa
wapuzi.
Yaliyomtokea Sarah kwenye maisha yake kuanzia kwenye familia yake na ndugu na
marafiki na mahusiano, yalikuwa ni simulizi ambazo yeye binafsi hakupenda
kuzisimulia kabisa, kwake zilikuwa ni simulizi za kuhuzunisha zilizomtwika donda
ambalo aliona kuwa halina siku ya kupona.
Maswahibu hayo pengine yalielezea kwanini Sarah aliishi maisha aliyoishi. Sarah
aliishi maisha ya peke yake, kwenye chumba chake kimoja alichopanga maeneo ya
Mwananyamala. Hakuwa na familia wala ndugu aliokuwa na ukaribu nao wa
kuwambilia.
Sarah. Alitegemea binti huyo kuwa atampigia simu ama japo atamtumia ujumbe.
Taratibu akaanza kuhisi kuwa pengine Sarah hatomtafuta. Hisia hiyo ilianza
kumkwaza, kwa maana sasa ilikuwa dhahiri kwake kuwa alikuwa anampenda.
Naalitamani waonane tena kwa mara nyengine, pengine hata amuambie lililo moyoni
mwake. Lakini siku zilikuwa zimepita na Sarah hakumtafuta kabisa Rahim.
Ila pasina kutarajia siku moja, Rahim akiwa bize na mambo yake simu iliita. Ilikuwa
ni namba ngeni. Kupokea hakuamini masikio yake , alisikia sauti ya Sarah, hatimaye
Sarah aliamua kumpigia.
“Habari, nimekukumbuka, za toka siku ile?”, alisalimia Sarah. Sauti yake ambayo
pengine ni ya kawaida sana safari hii haikuwa ya kawaida masikioni mwa Rahim.
Alionakuwa sauti hiyo ilikuwa laini na tamu, hata akakosa maneno ya kujibu salamu ya Sarah,
akawa kama amepigwa na bumbuwazi, alihisi hisia za ajabu, hatimaye alikuwa kapokea
simu aliyokuwa akiisubiri kwa hamu toka kwa binti huyo.
“Natamani tuonane, hata mimi nilikuwa nimekumiss, natamani nikuone”, aliongea
Rahim, kwenye simu. “Sawa tunaweza kuonana”, lilikuwa ndilo jibu la Sarah.
Kama ilivyokuwa kwa Rahim kuwa alikuwa ameelemewa na hisia nzito za kumpenda
Srah basi pia ilikuwa hivyohivyo kwa Sarah.
Sarah alimuona Rahim kama mtu wa ajabu. “Sijawahi kukutana na mtu wa aina hii
kwenye maisha yangu”, Sarah alijiambia , “ulikuwa wapi siku zote?, ungekuja mapema
kwenye maisha yangu”, aliendelea kujiuliza Sarah moyoni mwake.
….…………………………………………..
Maisha yake yote Sarah alikutana na watu wa hovyo, kuanzia kwenye familia ya kwao
na ndugu na marafiki, pia hadi wakati huo na umri wake wa miaka ishirini na mitano
alikuwa hajawahi kupendana na mtu na hakuwai kufikiria hapo kabla, kwamba hilo
litatokea, maana watu kadhaa aliowahi kuhisi ni wema kwake wote waligeuka kuwa
wapuzi.
Yaliyomtokea Sarah kwenye maisha yake kuanzia kwenye familia yake na ndugu na
marafiki na mahusiano, yalikuwa ni simulizi ambazo yeye binafsi hakupenda
kuzisimulia kabisa, kwake zilikuwa ni simulizi za kuhuzunisha zilizomtwika donda
ambalo aliona kuwa halina siku ya kupona.
Maswahibu hayo pengine yalielezea kwanini Sarah aliishi maisha aliyoishi. Sarah
aliishi maisha ya peke yake, kwenye chumba chake kimoja alichopanga maeneo ya
Mwananyamala. Hakuwa na familia wala ndugu aliokuwa na ukaribu nao wa
kuwambilia.