Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,339
- 51,884
SIKU YANGU YA KUFA ILIPITA.
Na, Robert Heriel
Siku ile SIRIEL ndiye Huyo mficha Siri za mungu alinijia nyakati za usiku nikiwa nimelala, alikuja kama ndoto usingizini, nami sikujua yakuwa nilikuwa naota au nilikuwa katika matendo halisi. Lakini nilimuona kwa macho yangu, na hata hivi leo ninamkumbuka.
Alikuwa na umbo la kibinadamu lenye pembe tatu, kila pembe kulikuwa na bawa moja, hivyo alikuwa na mabawa matatu. Uso wake ulikuwa wa siri sana. Ulikuwa uso wenye fumbo ambao ulibeba macho mawili, pua na mdomo. Alikuwa na umbo kubwa lenye urefu wa futi kumi na nne kwenda juu na upana wa futi tatu na nusu. Rangi yake ilikuwa ya kijivu. Kichwani alikuwa na Upaa wenye nywele chache za rangi ya huzurungi.
Basi akaitoa mikono yake mitatu iliyokuwa ndani ya mabawa; kwani kila bawa lilikuwa na mkono. Akaninyoshea mkono wake akinikazia macho yake makubwa yenye rangi ya damu na mboni nyeusi. Moyo wangu ukazimia kwa hofu, nikaogopa kwani nilijua ule ndio mwisho wangu, na yule niliyemuona ndiye mtoa roho.
Lakini ajabu ni kuwa Siriel alinyanyua mdomo wake akasema;
"Nimekuja kwa amani Taikon, usiwe na hofu kwa maana nimekuja kukukimbiza na kifo. Nawe utaitwa Aliyekimbia kifo. Jina langu ni Siriel, Mficha Siri za mungu. Amka Tuondoke" Sauti yake ilikuwa kama fumbo lisiloelezeka, maneno yake yalikuwa ya siri, ajabu alinifanya nielewe.
Nikampa mkono wangu wa kuume, naye akanipokea na kunivuta kwa nguvu kutoka kitandani. Kisha nikarushwa kama upepo lakini kumbe bawa lake tayari lilikuwa limenidaka na mkono wake ukanikamata kwa nguvu nyingi. Hapo moyo wangu haukuwa na nguvu tena ya kudunda, wala macho yangu hayakuweza kuona tena, hatimaye nilipoteza akili yangu kwenye giza totoro, hapo nikazirai.
Kitambo kidogo nisichoweza kukumbuka kilikuwa muda gani nikazinduka. Hapo nilijikuta nipo kwenye nchi tambarare yenye ardhi yenye nyufa nyufa: ardhi yenye rangi kama chokaa iliyofifia, mbele yangu kama maili ishirini naliuona mlima mdogo wenye urefu kwenda juu sawa na mita elfu mbili hivi. Hapakuwa na giza wala halikuwepo jua; Nikashindwa kuelewa ile ilikuwa ni alfajiri au ilikuwa ni jioni.
Hapakuwa na upepo, na juu yalikuwepo mawingu yaliyojitenga tenga na kuachia anga la samawati kuonekana.
Nikageuka kushoto na kulia wala hapakuwa na mtu, wala yule Siriel sikumuona. Tena nchi ile ilifanana na nchi ya wafu, nilihisi huenda haya ni makazi mapya ya wafu ambapo mimi ndio nitakuwa mfu wa kwanza kupelekwa mahali pale. Jambo lililonifanya nigundue kuwa nchi ile ilikuwa ni nchi ya wafu ni mazingira yake jinsi yalivyokuwa. Hapakuwa na mti wowote wa kijani isipokuwa visiki vya miti vya zamani vilivyokauka ambavyo vilikuwa vimeachana kwa umbali. Nyasi zilikuwa zimekauka siku nyingi mno.
Nikatembea ningali nikitazama huku na huku nione kama ningemuona mtu yeyote Lakini sikumuona mtu wala sikuona kiumbe yeyote mahali pale. Moyoni mwangu nikajisemea; Nipo nchi ya wafu, sasa wafu wengine watakuwa wapo wapi.
Basi nikatembea nikiufuata ule mlima kwa zaidi ya maili tano mpaka nilipochoka. Nikahisi Mkojo umenibana, nikachojoa nguo kisha nikakojoa. Looh! Nilipokojoa ghafla tetemeko kubwa likapiga. Nyufa za ile ardhi zikaongezeka. Natazama nikaona pale nilipokojolea pakipasuka pasuka na kwa hamaki na tisho Kiganja chenye vidole vilivyogawanyika kikatokea. Hapo wasiwasi ukanivaa kwa nguvu. Nikarudi nyuma nyuma huku nikitazama jambo hilo la kutisha.
Punde ardhi ilipasuka na Siriel alitokea. Alikuwa amejaa matope; Nilifikiri matope yale huenda yamesababishwa na Mkojo wangu. Niliogopa mno, kitendo cha kumkololea Siriel nilikiona kama kosa baya lisiloweza kusameheka.
Nilishangaa kumuona Siriel akicheka kwa nguvu hali iliyosababisha mawingu ya angani kugongana na radi kutokeo. Hii iliniambia jambo moja kuwa Siriel alikuwa na nguvu na uwezo mkubwa sana. Basi akaniambia nimfuate, nami nikamfuata.
Tulitembea kuufuata ule mlima. Wote tulikuwa kimya yeye akiwa mbele mimi nikiwa nyuma yake. Siriel hakuwa na mavazi, Mbawa yake ndio yalikuwa kama nguo kwake. Miguu yake ilikuwa ya pembe tatu, huku akiwa na kidole kimoja kilichokuwa kwenye pembe ya mbele ya nyayo zake. Nilishangaa sana, nilimuona kama kiumbe cha ajabu.
Nikatamani nimuulize kule tunapoelekea ni wapi, lakini akili yangu ikanionya. Ilinibidi nimfuate kama bendera ifuatavyo upepo.
Tulifika. Kisha akasema;
" Nimekukimbiza huku nyuma ya jua, kusiko na giza wala mwanga. Huku nimekuleta ili umkimbie Zeruel ambaye ametumwa kuchukua roho yako"
Hapo nikashtuka kusikia maneno hayo, yalikuwa maneno yaliyoifanya akili yangu ichanganyikiwe.
Kisha akachora pale chini umbo la mstatili lenye urefu wa nchi 50 na upanda wa nchi 30. Kisha akatembea mate lile umbo. Ghafla nikaona picha ya video pale chini kwenye lile umbo la mstatili.
Ilikuwa video iliyowaonyesha viumbe mfano wa malaika wenye mbawa. Viumbe wale walikuwa wamegawanyika, wapo walioluwa na mbawa mbili, wapo waliokuwa na mbawa nne, wapo waliokuwa na mbawa sita. Aliyekuwa na mbawa tatu alikuwa ni mmoja. Huyo nikataka kujua anaitwa nani kwa maana alikuwa akifanana na Siriel kwa maumbile.
" Huyo mwenye mbawa tatu ni nani?" Nilimuuliza " Huyo anaitwa KaaSiriel, ni pacha wangu. Hao wenye mbawa mbili wanaitwa Dharawidi, hawa wenye mbawa nne wanaitwa Fazawidi, wenye mbawa sita huitwa Tauwidi. Sisi wenye Mbawa Tatu tunaitwa Siriuwidi"
Siriel aliongea akitazama ile video pale chini ya ardhi. Maelezo hayo yalinivutia sana, nilitamani kujua habari za viumbe hao.Kisha Siriel akaniambia;
"Huyu ndiye Zeruel, huyu ni mtoa roho"
Hapo nilimtazama huyo Zeruel pale kwenye video. Alikuwa ni jamii ya Tauwidi yaani wenye mbawa sita na mikono miwili. Alikuwa kabiba karatasi iliyokunywa kama bomba.
"Hicho alichobeba Zeruel kinaitwa 'Lauta Bagama' ambayo inamajina ya siku hiyo ya watu atakaowachukua roho zao"
Siriel aliongea akimtazama Zeruel. Hapo nikamuona Zeruel kupitia video akiondoka kwa namna ya ajabu na mbawa zake. Mwendo wake ulikuwa wa ajabu mno, aliruka juu na kuzunguka na kufanya mbawa zake kuwa kama waridi. Kisha akasimama tena, akaondoka akaingia kwenye chumba akiwaacha wale wengine kwenye ukumbi.
" Hicho chumba kinaitwa Otoma, ni chumba cha kuwekea kumbukumbu ya viumbe waliotolewa roho na Zeruel. Chumba hiko anaingia Zeruel na mungu tuu. Umeona jina lako?" Siriel alisema.
Nilishtuka sana baada ya kuona jina langu kwenye ile karatasi baada ya Zeruel kufungua ile Lausta Bagama. Niliona tarehe, siku, mwaka, muda, mazingira ya kifo changu kupitia ile Lausta Bagama.
" Inamaana natakiwa kesho nife?"
Niliuliza huku nikitazama ile video kwa wasiwasi
" Kifo cha mtu hupangwa na mungu, lakini namna atakavyokufa hupangwa na Janalaidana, huyu ndio hupanga namna tukio zima la kifo chako litakavyokuwa. Sisi hupenda kumuita Laidana yaani Mwenye sanaa ya kifo"
Siriel alisema huku uso wake ukikunjuka kwa tabasamu.
Hapo nikamuona Zuriel yaani mtoa roho za watu akitoka na kutembea kwa kasi kuelekea upande wenye giza.
"Anaenda wapi sasa?" Niliuliza kwa hofu nikidhani huenda muda wa Zuriel kuja kunitoa roho umefika.
" Anaenda kwenye chumba kiitwacho X2, ambapo hapo ndio hufanyia shughuli zake. X2 ni chumba ambacho roho zote zilizopo duniani huonekana kupitia mtambo uitwao Dahel. Kila roho iliyopo duniani hupewa code yake, hivyo popote mtu alipo lazima Zuriel amuone kwa mtambo huo"
"Si ninyi mnasema kuwa huwezi kikimbia kifo?"
Siriel aliuliza.
"Ndio, kifo hakikimbiwi" Nikajibu.
" Kifo kinakimbiwa, na kimekimbiwa mara kadhaa. Ili ukimbie kifo lazima uingie chumba hicho yaani X2. Ukifika humo unatakiwa ujue code ya mtu unayetaka asife yaani akikimbie kifo. Ukishajua Code yake basi, umemaliza kila kitu"
" Code ya roho ya mtu ipo kwenye ile Lausta Bagama ambapo kuna jina lake, siku atakapokufa, muda, mwezi mwaka, na namna atakavyokufa, kwa mbele kuna code yenye tarakimu thelasini na sita, hizo ndio code" Siriel alisema.
Hapo nikamuona Zuriel akibonyeza Dahel punde ukafunguka, na hapo akaingiza zile code zilizomo kwenye Lausta bagama, alichukua dakika ishirini.Punde nikaona watu kwenye ule mtambo ndio hiyo Dahel.
" Watu wote unaowaona kwenye huo mtambo watakufa kesho, nawe ukiwemo" Siriel alisema.
Moyo ukapiga paah baada ya kujiona kwenye ule mtambo nikiwa nimelala kitandani.
"Yamebaki masaa kumi na sita roho yako itoke. Nimekuja huku kukusaidia. Sitaki ufe, nina sababu ya kufanya hivi"
Siriel aliongea maneno hayo huku akinitazama na macho yake mekundu yenye mboni nyeusi.
Kisha akasogelea kisiki chenye matawi yaliyokauka na kukata jiti kubwa. Alafua akanambia nilale chini. Nami nikalala. Kisha akachora kupitia pembeni yangu kwa kufuata umbo langu. Alianzia kichwani mpaka kwenye unyao wangu. Kisha akaniambia niamke. Nikaamka, akamalizia kuchora macho, pua na mdomo. Kisha akaniambia niukojolee ule mchoro mdomoni.
Nilisikia aibu kukojoa mbele yake lakini sikuwa na jinsi nilichojoa nikakojoa kwa kujilazimisha lazima kwani sikuwa namkojo muda ule.
Nilipokojoa tuu ghafla ule mchoro ulibadilika ukawa dongo lililosimama bila ya nguo. Lile dongo lilisimama mbele yetu pasipo kusema kitu. Siriel akalimwagia kitu kama maji likabadilika likawa na ngozi kama yangu. Kisha nikaambiwa nilikumbatie. Kwa hofu nikalifuata moyo ukipiga kite. Nikalikumbatia nikiwa nimefumba macho. Nilipofumbua nilishtuka kuona lile dongo limebadilika na kuwa na sura yangu kabisa. lilikuwa limefanana na mimi kama mapacha waliofanana.
Hapo Siriel akachukua damu ya lile dongo ambalo muda huo limekuwa binadamu aliyefanana na mimi. Alipomaliza akasema: " Sasa subiri niondoke niende Tibeli, nikapeleke hii damu kisha nitarudi. Sitakawahi baada ya masaa matano nitakuwa nimewasili"
Siriel aliongea na kisha akaondoka akiniacha mimi na yule dongo ambaye muda huo alikuwa akinitazama bila ya kusema chochote.
Kitambo kidogo kilipita bila ya mimi na yule pacha wangu kuzungumza. Nikaona nimuulize;
"Unajua chochote?"
"Hapa ni wapi? Nawe ni nani unayefanana na mimi?"
Yule Mtu aliongea sauti inayofanana na mimi kabisa.
" Upo nyuma ya Jua, Nami ninaitwa Taikon,"
Nilimjibu.
" Taikon ni mimi, nambie wewe unaitwa nani? Na yule Siriel kaenda wapi?" Yule dongo aliongea kwa sauti ya juu akinifokea.
Niliogopa mno. Pia nikajiuliza alimjuaje Siriel wakati ametengenezwa pale pale nikiwepo.
" Mimi ndiye Taikon, Siriel kaenda Tibeli. Nambie unaitwa nani?" Nilijikaza nikamuuliza tena.
Hapo akanifuata na kunikaba kooni, muda huo alikuwa uchi wa mnyama. Mikono yake ilikuwa ya baridi kama maiti, macho yake bado yalikuwa na mchanga yalinitazama kwa ukali. Alizidisha kunikaba kwa nguvu mpaka nikahisi siwezi tena kupumua.
Kwa upesi nikampiga teke la kwenye kende akaniachia na kuanza kugugumia kwa maumivu lilikuwa pigo baya sana kwake.
Muda hup video ilikuwa ikiendelea pale chini, punde nilimuona Siriel akiingia kwenye ule ukumbi waliokuwamo wale viumbe wenye mbawa mbili,tatu.nne na mbawa sita. Alikaguliwa na moja ya walinzi walindao lango kuu la Tibeli. Niliomba kimoyo moyo asijekutwa na kile kichupa cha damu ya dongo. Bahati ilikuwa yake, kichupa hakikuonekana.
Nilimuona Siriel akimfuata pacha wake Kaasiriel wakakumbatiana kwa upendo, nikajikuta natabasamu. Nilipenda jinsi walivyokuwa wanapendana. Baadaye niliwaona wakizungumza jambo kwa kitambo kisha Kaasiriel akamuacha Siriel pale ukumbini akaenda moja kwa moja kwenye kile chumba cha Otama. Akabisha hodi lakini hakujibiwa. Akajua chumba kile hakina Mtu. Akaondoka akaenda moja kwa moja kwenye chumba kiitwacho X2 ambacho kinamifumo ya roho zote. Hapo akabisha mara moja mlango ukafunguliwa na Zuriel.
Wakaongea kidogo kisha wakatoka wote kuelekea ukumbini, kumbe Siriel alikuwa kajificha kwenye kona, walipopita tuu akaenda na kuingia kwenye kile chumba X2, nikamuona Siriel akabadilisha Code zangu na kuingiza Code za dongo. Kwa haraka sana alipobadilisha, chumba kizima kikatoa alamu ya hatari jambo ambalo lilimfanya Zuriel ajue kuna mtu kaingia kwenye chumba cha X2 na kushika ule mtambo uitwao Dahel.
Siriel alijigeuza ukuta na kubadili Code za ukuta kusudi asionekane. Zuriel alipoingia hakukuta mtu. Akashangaa ni kwa nini alamu ilie. Hapo akawa na mashaka huenda kuna kitu kinaendelea. Akakumbuka ujio wa Kaasiriel alivyokuja na kumchukua akaenda naye ukumbini na hakuwa na jambo la maana. Siriel akatoka pale ukutani akaenda kwa Kaasiriel akamuaga na kuondoka. Yalikuwa yameshaisha masaa manne.
Baada ya lisaa limoja Siriel alirudi na kunikuta pale aliponiacha na dongo wangu. " Kila kitu kimeenda sawa. Sasa Nitaondoka hapa na Huyu alafu baadaye nitarudi kukuchukua" Siriel aliongea kama mtu aliyebakiwa na muda mchache. Ni kweli yalikuwa yamebaki masaa mawili tuu ili roho yangu ichukuliwe na Zuriel.
Aliondoka na moja kwa moja alifika Duniani. Hapo niliwaona kupitia Video iliyokuwepo pale chini.
Nilishangaa kujiona nikiwa duniani nikiendelea na shughuli zangu. Nikajisemea huenda kile ni kivuli changu. Siriel akiwa na Dongo niliwaona wakiwa wamesimama mbele ya kivuli changu kilichopo duniani, Siriel akashika kile kivuli changu ambacho muda huo kilikuwa kinatembea na rafiki zangu ambao muda huo walijua ni mimi kumbe ni kivuli changu.
Alivyokishika kivuli changu kikajikwaa na kupepesuka kama mtu anayetaka kuanguka. Hapo hapo Siriel akamuunganisha Dongo na kivuli changu. Rafiki zangu walinizoza na kuniambia nitembee kwa umakini, wasijue yule hakuwa mimi bali ni kivuli changu.
Zilikuwa zimesalia Dakika kumi Roho yangu ichukuliwe. Siriel alirudi kwa kasi mpaka nyuma ya Jua. Akanikuta nikitazama video. "Kazi imekwisha, subiri tumsubiri Zuriel nafikiri dakika tano zijazo atakuwa eneo la tukio" Siriel alisema. Punde video ilimuonyesha Zuriel akiwa maeneo ya duniani akivizia ule mchanganyiko wa kivuli changu na dongo. Akaitoa roho ya dongo akidhani ni Roho yangu. Basi akamaliza kazi. Nikadondoka, Dongo akafa wakati mimi kivuli changu kikiendelea kuishi.
Baadaye Zuriel akaondoka moja kwa moja mpaka chumba cha Otama ambacho ni maalumu kwa kuhifadhia roho na kumbukumbu za watu waliokwisha kufa.
Siriel akanambia tusubiri siku tatu, kisha zilipoisha siku tatu akanichukua na kunirudisha duniani kwenye kile kivuli changu.
Je, nini kitaendelea? Je, Taikon hatakufa kisa siku yake ya kufa imeshapita?
Usikose mkasa huu wa kusisimua wenye visa matata.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Na, Robert Heriel
Siku ile SIRIEL ndiye Huyo mficha Siri za mungu alinijia nyakati za usiku nikiwa nimelala, alikuja kama ndoto usingizini, nami sikujua yakuwa nilikuwa naota au nilikuwa katika matendo halisi. Lakini nilimuona kwa macho yangu, na hata hivi leo ninamkumbuka.
Alikuwa na umbo la kibinadamu lenye pembe tatu, kila pembe kulikuwa na bawa moja, hivyo alikuwa na mabawa matatu. Uso wake ulikuwa wa siri sana. Ulikuwa uso wenye fumbo ambao ulibeba macho mawili, pua na mdomo. Alikuwa na umbo kubwa lenye urefu wa futi kumi na nne kwenda juu na upana wa futi tatu na nusu. Rangi yake ilikuwa ya kijivu. Kichwani alikuwa na Upaa wenye nywele chache za rangi ya huzurungi.
Basi akaitoa mikono yake mitatu iliyokuwa ndani ya mabawa; kwani kila bawa lilikuwa na mkono. Akaninyoshea mkono wake akinikazia macho yake makubwa yenye rangi ya damu na mboni nyeusi. Moyo wangu ukazimia kwa hofu, nikaogopa kwani nilijua ule ndio mwisho wangu, na yule niliyemuona ndiye mtoa roho.
Lakini ajabu ni kuwa Siriel alinyanyua mdomo wake akasema;
"Nimekuja kwa amani Taikon, usiwe na hofu kwa maana nimekuja kukukimbiza na kifo. Nawe utaitwa Aliyekimbia kifo. Jina langu ni Siriel, Mficha Siri za mungu. Amka Tuondoke" Sauti yake ilikuwa kama fumbo lisiloelezeka, maneno yake yalikuwa ya siri, ajabu alinifanya nielewe.
Nikampa mkono wangu wa kuume, naye akanipokea na kunivuta kwa nguvu kutoka kitandani. Kisha nikarushwa kama upepo lakini kumbe bawa lake tayari lilikuwa limenidaka na mkono wake ukanikamata kwa nguvu nyingi. Hapo moyo wangu haukuwa na nguvu tena ya kudunda, wala macho yangu hayakuweza kuona tena, hatimaye nilipoteza akili yangu kwenye giza totoro, hapo nikazirai.
Kitambo kidogo nisichoweza kukumbuka kilikuwa muda gani nikazinduka. Hapo nilijikuta nipo kwenye nchi tambarare yenye ardhi yenye nyufa nyufa: ardhi yenye rangi kama chokaa iliyofifia, mbele yangu kama maili ishirini naliuona mlima mdogo wenye urefu kwenda juu sawa na mita elfu mbili hivi. Hapakuwa na giza wala halikuwepo jua; Nikashindwa kuelewa ile ilikuwa ni alfajiri au ilikuwa ni jioni.
Hapakuwa na upepo, na juu yalikuwepo mawingu yaliyojitenga tenga na kuachia anga la samawati kuonekana.
Nikageuka kushoto na kulia wala hapakuwa na mtu, wala yule Siriel sikumuona. Tena nchi ile ilifanana na nchi ya wafu, nilihisi huenda haya ni makazi mapya ya wafu ambapo mimi ndio nitakuwa mfu wa kwanza kupelekwa mahali pale. Jambo lililonifanya nigundue kuwa nchi ile ilikuwa ni nchi ya wafu ni mazingira yake jinsi yalivyokuwa. Hapakuwa na mti wowote wa kijani isipokuwa visiki vya miti vya zamani vilivyokauka ambavyo vilikuwa vimeachana kwa umbali. Nyasi zilikuwa zimekauka siku nyingi mno.
Nikatembea ningali nikitazama huku na huku nione kama ningemuona mtu yeyote Lakini sikumuona mtu wala sikuona kiumbe yeyote mahali pale. Moyoni mwangu nikajisemea; Nipo nchi ya wafu, sasa wafu wengine watakuwa wapo wapi.
Basi nikatembea nikiufuata ule mlima kwa zaidi ya maili tano mpaka nilipochoka. Nikahisi Mkojo umenibana, nikachojoa nguo kisha nikakojoa. Looh! Nilipokojoa ghafla tetemeko kubwa likapiga. Nyufa za ile ardhi zikaongezeka. Natazama nikaona pale nilipokojolea pakipasuka pasuka na kwa hamaki na tisho Kiganja chenye vidole vilivyogawanyika kikatokea. Hapo wasiwasi ukanivaa kwa nguvu. Nikarudi nyuma nyuma huku nikitazama jambo hilo la kutisha.
Punde ardhi ilipasuka na Siriel alitokea. Alikuwa amejaa matope; Nilifikiri matope yale huenda yamesababishwa na Mkojo wangu. Niliogopa mno, kitendo cha kumkololea Siriel nilikiona kama kosa baya lisiloweza kusameheka.
Nilishangaa kumuona Siriel akicheka kwa nguvu hali iliyosababisha mawingu ya angani kugongana na radi kutokeo. Hii iliniambia jambo moja kuwa Siriel alikuwa na nguvu na uwezo mkubwa sana. Basi akaniambia nimfuate, nami nikamfuata.
Tulitembea kuufuata ule mlima. Wote tulikuwa kimya yeye akiwa mbele mimi nikiwa nyuma yake. Siriel hakuwa na mavazi, Mbawa yake ndio yalikuwa kama nguo kwake. Miguu yake ilikuwa ya pembe tatu, huku akiwa na kidole kimoja kilichokuwa kwenye pembe ya mbele ya nyayo zake. Nilishangaa sana, nilimuona kama kiumbe cha ajabu.
Nikatamani nimuulize kule tunapoelekea ni wapi, lakini akili yangu ikanionya. Ilinibidi nimfuate kama bendera ifuatavyo upepo.
Tulifika. Kisha akasema;
" Nimekukimbiza huku nyuma ya jua, kusiko na giza wala mwanga. Huku nimekuleta ili umkimbie Zeruel ambaye ametumwa kuchukua roho yako"
Hapo nikashtuka kusikia maneno hayo, yalikuwa maneno yaliyoifanya akili yangu ichanganyikiwe.
Kisha akachora pale chini umbo la mstatili lenye urefu wa nchi 50 na upanda wa nchi 30. Kisha akatembea mate lile umbo. Ghafla nikaona picha ya video pale chini kwenye lile umbo la mstatili.
Ilikuwa video iliyowaonyesha viumbe mfano wa malaika wenye mbawa. Viumbe wale walikuwa wamegawanyika, wapo walioluwa na mbawa mbili, wapo waliokuwa na mbawa nne, wapo waliokuwa na mbawa sita. Aliyekuwa na mbawa tatu alikuwa ni mmoja. Huyo nikataka kujua anaitwa nani kwa maana alikuwa akifanana na Siriel kwa maumbile.
" Huyo mwenye mbawa tatu ni nani?" Nilimuuliza " Huyo anaitwa KaaSiriel, ni pacha wangu. Hao wenye mbawa mbili wanaitwa Dharawidi, hawa wenye mbawa nne wanaitwa Fazawidi, wenye mbawa sita huitwa Tauwidi. Sisi wenye Mbawa Tatu tunaitwa Siriuwidi"
Siriel aliongea akitazama ile video pale chini ya ardhi. Maelezo hayo yalinivutia sana, nilitamani kujua habari za viumbe hao.Kisha Siriel akaniambia;
"Huyu ndiye Zeruel, huyu ni mtoa roho"
Hapo nilimtazama huyo Zeruel pale kwenye video. Alikuwa ni jamii ya Tauwidi yaani wenye mbawa sita na mikono miwili. Alikuwa kabiba karatasi iliyokunywa kama bomba.
"Hicho alichobeba Zeruel kinaitwa 'Lauta Bagama' ambayo inamajina ya siku hiyo ya watu atakaowachukua roho zao"
Siriel aliongea akimtazama Zeruel. Hapo nikamuona Zeruel kupitia video akiondoka kwa namna ya ajabu na mbawa zake. Mwendo wake ulikuwa wa ajabu mno, aliruka juu na kuzunguka na kufanya mbawa zake kuwa kama waridi. Kisha akasimama tena, akaondoka akaingia kwenye chumba akiwaacha wale wengine kwenye ukumbi.
" Hicho chumba kinaitwa Otoma, ni chumba cha kuwekea kumbukumbu ya viumbe waliotolewa roho na Zeruel. Chumba hiko anaingia Zeruel na mungu tuu. Umeona jina lako?" Siriel alisema.
Nilishtuka sana baada ya kuona jina langu kwenye ile karatasi baada ya Zeruel kufungua ile Lausta Bagama. Niliona tarehe, siku, mwaka, muda, mazingira ya kifo changu kupitia ile Lausta Bagama.
" Inamaana natakiwa kesho nife?"
Niliuliza huku nikitazama ile video kwa wasiwasi
" Kifo cha mtu hupangwa na mungu, lakini namna atakavyokufa hupangwa na Janalaidana, huyu ndio hupanga namna tukio zima la kifo chako litakavyokuwa. Sisi hupenda kumuita Laidana yaani Mwenye sanaa ya kifo"
Siriel alisema huku uso wake ukikunjuka kwa tabasamu.
Hapo nikamuona Zuriel yaani mtoa roho za watu akitoka na kutembea kwa kasi kuelekea upande wenye giza.
"Anaenda wapi sasa?" Niliuliza kwa hofu nikidhani huenda muda wa Zuriel kuja kunitoa roho umefika.
" Anaenda kwenye chumba kiitwacho X2, ambapo hapo ndio hufanyia shughuli zake. X2 ni chumba ambacho roho zote zilizopo duniani huonekana kupitia mtambo uitwao Dahel. Kila roho iliyopo duniani hupewa code yake, hivyo popote mtu alipo lazima Zuriel amuone kwa mtambo huo"
"Si ninyi mnasema kuwa huwezi kikimbia kifo?"
Siriel aliuliza.
"Ndio, kifo hakikimbiwi" Nikajibu.
" Kifo kinakimbiwa, na kimekimbiwa mara kadhaa. Ili ukimbie kifo lazima uingie chumba hicho yaani X2. Ukifika humo unatakiwa ujue code ya mtu unayetaka asife yaani akikimbie kifo. Ukishajua Code yake basi, umemaliza kila kitu"
" Code ya roho ya mtu ipo kwenye ile Lausta Bagama ambapo kuna jina lake, siku atakapokufa, muda, mwezi mwaka, na namna atakavyokufa, kwa mbele kuna code yenye tarakimu thelasini na sita, hizo ndio code" Siriel alisema.
Hapo nikamuona Zuriel akibonyeza Dahel punde ukafunguka, na hapo akaingiza zile code zilizomo kwenye Lausta bagama, alichukua dakika ishirini.Punde nikaona watu kwenye ule mtambo ndio hiyo Dahel.
" Watu wote unaowaona kwenye huo mtambo watakufa kesho, nawe ukiwemo" Siriel alisema.
Moyo ukapiga paah baada ya kujiona kwenye ule mtambo nikiwa nimelala kitandani.
"Yamebaki masaa kumi na sita roho yako itoke. Nimekuja huku kukusaidia. Sitaki ufe, nina sababu ya kufanya hivi"
Siriel aliongea maneno hayo huku akinitazama na macho yake mekundu yenye mboni nyeusi.
Kisha akasogelea kisiki chenye matawi yaliyokauka na kukata jiti kubwa. Alafua akanambia nilale chini. Nami nikalala. Kisha akachora kupitia pembeni yangu kwa kufuata umbo langu. Alianzia kichwani mpaka kwenye unyao wangu. Kisha akaniambia niamke. Nikaamka, akamalizia kuchora macho, pua na mdomo. Kisha akaniambia niukojolee ule mchoro mdomoni.
Nilisikia aibu kukojoa mbele yake lakini sikuwa na jinsi nilichojoa nikakojoa kwa kujilazimisha lazima kwani sikuwa namkojo muda ule.
Nilipokojoa tuu ghafla ule mchoro ulibadilika ukawa dongo lililosimama bila ya nguo. Lile dongo lilisimama mbele yetu pasipo kusema kitu. Siriel akalimwagia kitu kama maji likabadilika likawa na ngozi kama yangu. Kisha nikaambiwa nilikumbatie. Kwa hofu nikalifuata moyo ukipiga kite. Nikalikumbatia nikiwa nimefumba macho. Nilipofumbua nilishtuka kuona lile dongo limebadilika na kuwa na sura yangu kabisa. lilikuwa limefanana na mimi kama mapacha waliofanana.
Hapo Siriel akachukua damu ya lile dongo ambalo muda huo limekuwa binadamu aliyefanana na mimi. Alipomaliza akasema: " Sasa subiri niondoke niende Tibeli, nikapeleke hii damu kisha nitarudi. Sitakawahi baada ya masaa matano nitakuwa nimewasili"
Siriel aliongea na kisha akaondoka akiniacha mimi na yule dongo ambaye muda huo alikuwa akinitazama bila ya kusema chochote.
Kitambo kidogo kilipita bila ya mimi na yule pacha wangu kuzungumza. Nikaona nimuulize;
"Unajua chochote?"
"Hapa ni wapi? Nawe ni nani unayefanana na mimi?"
Yule Mtu aliongea sauti inayofanana na mimi kabisa.
" Upo nyuma ya Jua, Nami ninaitwa Taikon,"
Nilimjibu.
" Taikon ni mimi, nambie wewe unaitwa nani? Na yule Siriel kaenda wapi?" Yule dongo aliongea kwa sauti ya juu akinifokea.
Niliogopa mno. Pia nikajiuliza alimjuaje Siriel wakati ametengenezwa pale pale nikiwepo.
" Mimi ndiye Taikon, Siriel kaenda Tibeli. Nambie unaitwa nani?" Nilijikaza nikamuuliza tena.
Hapo akanifuata na kunikaba kooni, muda huo alikuwa uchi wa mnyama. Mikono yake ilikuwa ya baridi kama maiti, macho yake bado yalikuwa na mchanga yalinitazama kwa ukali. Alizidisha kunikaba kwa nguvu mpaka nikahisi siwezi tena kupumua.
Kwa upesi nikampiga teke la kwenye kende akaniachia na kuanza kugugumia kwa maumivu lilikuwa pigo baya sana kwake.
Muda hup video ilikuwa ikiendelea pale chini, punde nilimuona Siriel akiingia kwenye ule ukumbi waliokuwamo wale viumbe wenye mbawa mbili,tatu.nne na mbawa sita. Alikaguliwa na moja ya walinzi walindao lango kuu la Tibeli. Niliomba kimoyo moyo asijekutwa na kile kichupa cha damu ya dongo. Bahati ilikuwa yake, kichupa hakikuonekana.
Nilimuona Siriel akimfuata pacha wake Kaasiriel wakakumbatiana kwa upendo, nikajikuta natabasamu. Nilipenda jinsi walivyokuwa wanapendana. Baadaye niliwaona wakizungumza jambo kwa kitambo kisha Kaasiriel akamuacha Siriel pale ukumbini akaenda moja kwa moja kwenye kile chumba cha Otama. Akabisha hodi lakini hakujibiwa. Akajua chumba kile hakina Mtu. Akaondoka akaenda moja kwa moja kwenye chumba kiitwacho X2 ambacho kinamifumo ya roho zote. Hapo akabisha mara moja mlango ukafunguliwa na Zuriel.
Wakaongea kidogo kisha wakatoka wote kuelekea ukumbini, kumbe Siriel alikuwa kajificha kwenye kona, walipopita tuu akaenda na kuingia kwenye kile chumba X2, nikamuona Siriel akabadilisha Code zangu na kuingiza Code za dongo. Kwa haraka sana alipobadilisha, chumba kizima kikatoa alamu ya hatari jambo ambalo lilimfanya Zuriel ajue kuna mtu kaingia kwenye chumba cha X2 na kushika ule mtambo uitwao Dahel.
Siriel alijigeuza ukuta na kubadili Code za ukuta kusudi asionekane. Zuriel alipoingia hakukuta mtu. Akashangaa ni kwa nini alamu ilie. Hapo akawa na mashaka huenda kuna kitu kinaendelea. Akakumbuka ujio wa Kaasiriel alivyokuja na kumchukua akaenda naye ukumbini na hakuwa na jambo la maana. Siriel akatoka pale ukutani akaenda kwa Kaasiriel akamuaga na kuondoka. Yalikuwa yameshaisha masaa manne.
Baada ya lisaa limoja Siriel alirudi na kunikuta pale aliponiacha na dongo wangu. " Kila kitu kimeenda sawa. Sasa Nitaondoka hapa na Huyu alafu baadaye nitarudi kukuchukua" Siriel aliongea kama mtu aliyebakiwa na muda mchache. Ni kweli yalikuwa yamebaki masaa mawili tuu ili roho yangu ichukuliwe na Zuriel.
Aliondoka na moja kwa moja alifika Duniani. Hapo niliwaona kupitia Video iliyokuwepo pale chini.
Nilishangaa kujiona nikiwa duniani nikiendelea na shughuli zangu. Nikajisemea huenda kile ni kivuli changu. Siriel akiwa na Dongo niliwaona wakiwa wamesimama mbele ya kivuli changu kilichopo duniani, Siriel akashika kile kivuli changu ambacho muda huo kilikuwa kinatembea na rafiki zangu ambao muda huo walijua ni mimi kumbe ni kivuli changu.
Alivyokishika kivuli changu kikajikwaa na kupepesuka kama mtu anayetaka kuanguka. Hapo hapo Siriel akamuunganisha Dongo na kivuli changu. Rafiki zangu walinizoza na kuniambia nitembee kwa umakini, wasijue yule hakuwa mimi bali ni kivuli changu.
Zilikuwa zimesalia Dakika kumi Roho yangu ichukuliwe. Siriel alirudi kwa kasi mpaka nyuma ya Jua. Akanikuta nikitazama video. "Kazi imekwisha, subiri tumsubiri Zuriel nafikiri dakika tano zijazo atakuwa eneo la tukio" Siriel alisema. Punde video ilimuonyesha Zuriel akiwa maeneo ya duniani akivizia ule mchanganyiko wa kivuli changu na dongo. Akaitoa roho ya dongo akidhani ni Roho yangu. Basi akamaliza kazi. Nikadondoka, Dongo akafa wakati mimi kivuli changu kikiendelea kuishi.
Baadaye Zuriel akaondoka moja kwa moja mpaka chumba cha Otama ambacho ni maalumu kwa kuhifadhia roho na kumbukumbu za watu waliokwisha kufa.
Siriel akanambia tusubiri siku tatu, kisha zilipoisha siku tatu akanichukua na kunirudisha duniani kwenye kile kivuli changu.
Je, nini kitaendelea? Je, Taikon hatakufa kisa siku yake ya kufa imeshapita?
Usikose mkasa huu wa kusisimua wenye visa matata.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300