Simulizi: Scaila Michael

kuna wakati namuona jamaa Kama bwege ivi wakat mwenyew ata miez miwil aijapita tangu tuachane
80% ya matukio ya stori na yangu yanafanana
 
Jamaa anasikitisha sana...

Ati hataki kumsaliti Scaila, walati demu wake kaenda kufanywa huko na ushahidi anao...


Cc: mahondaw
 
Mwandishi wewe kila mwanamke ni mzuri !!vipi !!?
 
sehemu ya 47

Alihisi kulikuwa na kitu mbali na kuumwa kule nilivyokuwa nimemdanganya, alijaribu kunidadisi lakini alishindwa kupata jibu kabisa, hakujua kuhusu Scaila kwani hata mwanamke huyo alipokuwa nyumbani hapo, nilimuonyesha mapenzi kana kwamba hakukuwa na jambo lolote lililokuwa likiendelea.

Nikaelekea chumbani, nilipokumbuka kuhusu Scaila tu moyo wangu uliniuma sana, yaani nilikuwa na uhakika mwanamke huyo alikuwa katika kitanda cha mtu mwingine akila raha, wakiwa wamefanya mapenzi usiku mzima kitu kilichoniuma kupita kawaida.

Nilipofika chumbani, nikakaa na kuanza kufikiria tena kuhusu Scaila. Naweza kusema hicho ndicho kilikuwa kipindi kigumu kuliko vipindi vyote katika maisha yangu. Huyu mwanamke alinichanganya mno na muda mwingine nilitamani nisiyajue mapenzi kabisa kwani yalikuwa yakiumiza kupita kawaida.

Nilikaa katika hali hiyo kwa dakika kadhaa, nikaamua kuchukua simu kwa lengo la kumpigia Scaila ili niongee naye, simu yake haikuwa ikipatikana kitu kilichoniumiza zaidi.

“Sasa yupo na bwana wake, kwa nini aache simu hewani?” niliisikia sauti ikiniambia moyoni mwangu.

“Ila hawezi kuwa na mwanaume mwingine, mama yake hawezi kuniuza,” hii ilikuwa sauti yangu ya kujifariji kwa kile kilichokuwa kikiendelea.

Sikuwa na hamu ya kwenda katika biashara zangu, nilibaki nyumbani nikiwa nimetulia tu, wakati mwingine nilikuwa nikijiumiza kwa kuangalia mawasiliano yake kwa njia ya WhatsApp aliyokuwa akiyafanya.

Sikuishia hapo tu, kwa kuwa nilikuwa nikihitaji sana ushahidi, nilichokifanya ni kuscreenshot kwenye ile kompyuta na kisha kutuma picha zile katika barua pepe yangu.

Huo ulikuwa kama ushahidi, nilihitaji kuutumia siku ambayo ningeamua kuachana na mwanamke huyo kwani bila kuwa nao, kuna siku angeniambia hakuwahi kuwasiliana na marafiki zake kuhusu klabu, sasa kama sitokuwa na ushahidi basi ingekula kwangu.

Nilikaa mpaka majira ya saa nne asubuhi, nikakumbuka kuhusu taili la gari langu ambalo lilipata pancha, hivyo nikaondoka kwenda gereji kwa kumuita fundi aje nyumbani kwangu na kuziba pancha ile.
 
sehemu ya 48

Hilo halikuwa tatizo, kwa mtu mwenye pesa kama mimi, fundi hakuona ugumu kuja kwani alijua ningemlipa malipo mazuri kabisa, tena kwa sababu ilikuwa ni asubuhi, ingeonekana kuwa bahati sana kwake.

Wakati nikiwa njiani kuelekea kwa mafundi wa gereji ambayo haikuwa mbali na mahali nilipokuwa naishi, nikasikia nikiitwa kwa nyuma, sauti ilikuwa ni ya mwanaume, nikageuka na macho yangu kutua usoni mwa jamaa mmoja.

“Aisee bro mambo vipi!” alinisalimia, lafudhi yake ilikuwa ni ya mtu kutoka Kaskazini.

“Poa tu niaje mwamba!” niliitikia na kumsalimia.
“Ni poa chalii wangu! Ebwana unanikumbuka?” aliniuliza. Akanifanya nimwangalie vizuri.

“Hapana! Nikumbushe!”
“Mimi ndiye chalii wa jana niliyemchukua shemeji kumpeleka kwao,” aliniambia.
Hapo nikamkumbuka, alikuwa yule bodaboda ambaye nilimchukulia usafiri Scaila jana yake kwa lengo la kumpeleka nyumbani kwao Tabata.

“Oh! Nimekukumbuka! Niambie! Shemeji yako alifika salama?” nilimuuliza.
“Daah! Bro kwani pale unataka kuoa?” aliniuliza swali lililonifanya nihisi kitu.
“Ndiyo! Kwani nini?” nilimuuliza, nikawa na hamu ya kutaka kusikia.

“Aisee bro yule demu siyo! Jana uliniambia nimpeleke kwao Tabata lakini aisee njiani si ndiyo akanibadilishia ramani!” aliniambia bodaboda huku akiniangalia kwa macho yaliyojaa huruma nyingi.

“Kivipi tena?” niliuliza.
“Aliniambia nimpeleke Maisha Club! Aisee nilipofika kulikuwa na lijamaa lilikuwa likiwasiliana naye, lilipomuona tu, akateremka na kumfuata. Lile lijamaa lilikuwa na matattoo, likamkumbatia na kuanza kubadilishana mate,” alisema bodaboda yule.

Ni kweli nilikuwa nikijua mambo mengi kuhusu Scaila ila hayo ambayo niliambiwa, yalionekana kama mapya kwani yaliniumiza.

Bodaboda aliendelea kuniambia mengi kuhusu Scaila, alivyopokelewa kwa shangwe na lijamaa hilo lililojichora matattoo na kumlipa kisha kuingia ndani.

Moyo wangu ni kama ulipigwa ganzi, nilihisi akili yangu ikienda sehemu ya mawazo na mawazo yakienda sehemu ya akili. Japokuwa nilijisikia hivyo lakini sikutakiwa kumuonyesha bodaboda maumivu yangu.

“Aisee! Ahsante sana kaka! Ndiyo maana tunaambiwa hawa mademu siyo kabisa,” nilimwambia jamaa yule, nikampa shilingi elfu kumi na kuondoka zangu.
 
Ushahidi mwingine huo
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…