Maji Chai
JF-Expert Member
- Dec 8, 2018
- 266
- 367
sehemu ya 01
Sikumbuki nillifikaje nyumbani, ila nakumbuka mara ya mwisho nilikuwa safarini kwa ajili ya likizo ndefu ya mwezi wa kumi na mbili. Ila si tu kufika nyumbani, nilifikaje nyuma ya mlango? Wakati yote hayo nilisikia vilio nje, sikutaka kupitwa na vilio hivyo kwani hata shuleni nilitambulika kama 'Baba sipitwi'.
Niliusukuma mlango ule wa mbao uliokuwa umechoka na ghafla kukaribishwa nje na wingu kubwa la watu waliokuwa wakiangua vilio. Ikafatwa na sauti ambayo haikuwa ngeni maskioni mwangu, ilikuwa sauti ya mtu ambaye nilikuwa kondoo wake naye alikuwa mchungaji wangu Haris. "Mavumbini tumetoka, na mavumbini tutarudi".
Maneno yake yakanitia woga, yakanikumbusha hali niliyokuwa nimemwacha nayo mama aliyekuwa si wa maji wa chai. Machozi yakaanza kunitirika huku nikielekea kwa Haris aliyekuwa kasimama mbele ya jeneza. Muda wote huu nilikuwa nikimlaani vikali aliyekuwa kaniweka nyuma ya mlango kwani nilijua fika alikuwa akitaka nisiuone mwili wa mamangu kipenzi Bi.Zakish.
Nilikaribia kwenye jeneza tayari kumtizama mamangu kwa mara ya mwisho, alikuwa ni mwanamke mwenye uzuri wa aina yake. Nywele ndefu kama singa ya farasi, ngozi nyororo yenye rangi ya mtume na midomo ambayo haikuwahi kaukiwa mate uliojawa meno yaliyokuwa yamemkaa bambam mdomoni.
Ila yote hayo tulikuwa tumeyafukia kwenye kaburi la sahau, kwani kipindi naenda shule ngozi yake ilikuwa imeanza kuparara na kuwa na mabakamabaka sikwambii ya chui, huku mabega yakimwagika yakimwacha kikongwe.
Nillivuta pumzi ndefu tayari kukabiliana na lolote nitakalo liona ndani ya lile jeneza. Nilijua fika nilikuwa nakutana na fuvu la mama peke yake. Ila amini usiamini..................
Itaendelea
Sent from my SM-J500F using JamiiForums mobile app
Sikumbuki nillifikaje nyumbani, ila nakumbuka mara ya mwisho nilikuwa safarini kwa ajili ya likizo ndefu ya mwezi wa kumi na mbili. Ila si tu kufika nyumbani, nilifikaje nyuma ya mlango? Wakati yote hayo nilisikia vilio nje, sikutaka kupitwa na vilio hivyo kwani hata shuleni nilitambulika kama 'Baba sipitwi'.
Niliusukuma mlango ule wa mbao uliokuwa umechoka na ghafla kukaribishwa nje na wingu kubwa la watu waliokuwa wakiangua vilio. Ikafatwa na sauti ambayo haikuwa ngeni maskioni mwangu, ilikuwa sauti ya mtu ambaye nilikuwa kondoo wake naye alikuwa mchungaji wangu Haris. "Mavumbini tumetoka, na mavumbini tutarudi".
Maneno yake yakanitia woga, yakanikumbusha hali niliyokuwa nimemwacha nayo mama aliyekuwa si wa maji wa chai. Machozi yakaanza kunitirika huku nikielekea kwa Haris aliyekuwa kasimama mbele ya jeneza. Muda wote huu nilikuwa nikimlaani vikali aliyekuwa kaniweka nyuma ya mlango kwani nilijua fika alikuwa akitaka nisiuone mwili wa mamangu kipenzi Bi.Zakish.
Nilikaribia kwenye jeneza tayari kumtizama mamangu kwa mara ya mwisho, alikuwa ni mwanamke mwenye uzuri wa aina yake. Nywele ndefu kama singa ya farasi, ngozi nyororo yenye rangi ya mtume na midomo ambayo haikuwahi kaukiwa mate uliojawa meno yaliyokuwa yamemkaa bambam mdomoni.
Ila yote hayo tulikuwa tumeyafukia kwenye kaburi la sahau, kwani kipindi naenda shule ngozi yake ilikuwa imeanza kuparara na kuwa na mabakamabaka sikwambii ya chui, huku mabega yakimwagika yakimwacha kikongwe.
Nillivuta pumzi ndefu tayari kukabiliana na lolote nitakalo liona ndani ya lile jeneza. Nilijua fika nilikuwa nakutana na fuvu la mama peke yake. Ila amini usiamini..................
Itaendelea
Sent from my SM-J500F using JamiiForums mobile app