Simulizi : Safari Ndefu Kuelekea Kaburini

SEHEMU YA 55 & 56


Patricia aliendelea kubaki hospitalini kwa takribani miezi nane mingine na ndipo hapo akaruhusiwa kutoka hospitalini huku akitakiwa kuwa kwenye uangalizi mkubwa. Kitendo hicho kidogo kilionekana kumpa furaha Martin kwani alikuwa na uhakika wa kumuona Patricia muda wowote ambao angetaka kumuona.
“Kwa kuwa uti wake wa mgongo umevunjika vunjika, kamwe hautoweza kuungika. Ataendelea kuwa katika hali hii mpaka atakapofariki” Dokta aliwaambia.
Kwao iliendelea kuwa taaarifa mbaya kuliko taarifa zot ambazo waliwahi kuzisikia katika maisha yao. Walitamani sana kumuona Patricia akisimama na kuanza kutembea kama siku zile za nyuma alivyokuwa akifanya.
Maisha ya Patricia ya kuwa kitandani yakaanzia katika nyumba ya baba yake, Bwana Thomson. Basi mzee huyo alikuwa akitumia kiasi kikubwa cha fedha kumtibia mtoto wake. Japokuwa Patricia alikuwa kwenye hali mbaya lakini kila siku Bwana Thomson alikuwa akijipa moyo kwamba binti yake huyo angeweza kupona na kuwa mzima kama zamani.
Muda wote Martin alikuwa katika chumba alicholazwa Patricia nyumbani pale. Yeye ndeiye alikuwa akifanya kazi ya kumlisha kwa kutumia mipira ile na hata kukisafisha chombo chake alichokuwa akikitumia kwa ajili ya haja kubwa na ndogo.
Kwa Martin, hakutaka kuupunguza upendo wake, bado alikuwa akiendelea kumpenda Patricia huku akizidi kumpenda kadri siku zilivyozidi kwenda mbele. Patricia kwake alionekana kuwa mwanamke muhimu ambaye wala hakutakiwa kuachwa peke yake kisa alikuwa kwenye hali iliyokuwa na matatizo makubwa.
Hiyo ndio ilikuwa nafasi kubwa kwake ya kumuonyeshea ni kiasi gani alikuwa akimpenda na kumhitaji katika maisha yake. Kila siku alikuwa akilala katika chumba alichokuwa akilala Patricia, hakujali harufu kali ya aja ambayo alikuwa akiipata kila siku chumbani humo, kitu ambacho alikuwa akikijali ni kuwa karibu na Patricia tu.
Miezi ikaendelea kukatika, hatimae Patricia akawa na uwezo wa kuongea vizuri. Kila siku Patricia alionekana kuwa mtu wa kulia tu, moyoni aliumia, alikuwa akijutia uamuzi wake ambao ulimfanya kuhamia nchini Marekani.
Kwake, Martin alionekana kuwa mwanaume pekee ambaye alikuwa na mapenzi ya dhati kwake, upendo mkubwa ambao kila siku Martin alikuwa akimwambia siku za nyuma ulikuwa ukijionyesha katika kipindi hicho cha mateso. Martin hakutaka kuwa na msichana mwingine, msichana ambaye alikuwa akimpenda katika kipindi hicho alikuwa Patricia tu.
“Nakupenda Martin” Patricia alimwambia Martin kwa sauti ya chini.
“Nakupenda pia Patricia. Umekuwa mtu muhimu sana kwangu. Nitaendelea kukupenda katika kipindi chote mpaka pale kifo kitakaponitenganisha nawe” Martin alimwambia Patricia na kisha kumbusu shavuni.
Patricia bado alikuwa akiendelea kuwa katika hali ile ile. Kwa muda wa mwaka wa tatu bado alikuwa kitandani. Martin hakutaka kurudi nchini Tanzania, bado alikuwa akitamani kukaa na Patricia ambaye alikuwa akizidi kumpenda kadri siku zilivyozidi kwenda mbele.
Bwana Thomson alimchukulia Martin kuwa kama mtoto wake wa kumzaa, moyo ambao alikuwa akiuonyesha kwa mtoto wake ulikuwa ukimfariji kupita kiasi. Katika kipindi cha kula chakula, Martin ndiye alikuwa mtu pekee ambaye alikuwa akimlisha chakula Patricia kwa kutumia mipira ambayo ilikuwa imeunganishwa moja kwa moja mpaka tumboni mwake.
Kila siku Martin alikuwa mtu wa furaha. Kwa kipindi kirefu cha nyuma alikuwa akitamani sana kuungana na patricia na hatimae kuishi pamoja, kuwa nae katika kipindi hicho kulionekana kumfariji.
“Hii ni safari yangu ndefu kuelekea kaburini Martin” Patricia alimwambia Martin.
“Hapana. Hapana Patricia. Hautokufa. Hautokufa Patricia’ Martin alimwambia Patricia.
Maneno yale yalionekana kumuumiza Martin, machozi yakaanza kumtoka. Hakupenda kabisa Patricia aongee maneno yale ambayo yalionekana kumuumiza kupita kawaida. Kwake, maneno yale yalionekana kuwa kama msumali wa moto ambao uliingia moja kwa moja moyoni mwake.
 
SEHEMU YA 57

Akapiga magoti chini na kisha uso wake kuusogeza karibu na uso wa Patricia na kisha kumbusu. Kila wakati alikuwa akitamani kumbusu Patricia, japokuwa msichana huyo alikuwa amekonda kupita kiasi lakini bado alikuwa akimpenda. Hakukuwa na msichana yeyote katika ulimwengu huu ambaye alikuwa akimpenda kama jinsi ambavyo alikuwa akimpenda Patricia.
“Hali ya hewa inaonekana kumsumbua mgonjwa. Itatupasa kusafiri kurudi nchini Tanzania pamoja nae” Bi Beatrice alimwambia Martin.



“Mbona ni uamuzi wa haraka hivyo mama?” Martin aliuliza huku akionekana kushtuka.
“Ndivyo tulivyoamua pamoja na baba yake. Itatupasa kurudi nchini Tanzania kwani mgonjwa wetu amefikia ukingoni kupata nafuu. Hatoweza kupata nafuu zaidi ya hapo” Bi Beatrice alimwambia Martin.
Hakukuwa na kitu kilichoendelea zaidi ya harakati za kurudi nchini tanzania kuanza. Martin hakutaka kumficha Patricia, alichokifanya ni kumwambia juu ya kie kitu ambacho kilikuwa kimepangwa na kukubalika na kila mtu.
“Tunarudi Tanzania. Najua kwamba haukuwa na ndoto ya kurudi Tanzania, haina budi kwa sasa Patricia” Martin alimwambia Patricia.
“Niko tayari kurudi. Niko tayari kwa kitu chochote kutokea maishani mwangu ila si kukupoteza wewe. Umekuwa mfariji wangu mkubwa Martin” Patricia alimwambia Martin.
Mipango ya safari ikawa imekamilika, ndege ambayo ilikuwa ikimilikiwa na Bwana thomson ikaandaliwa na kisha safari kuanza huku ndani ya ndege kukiwa na watu wasiozidi saba. Bwana Thomson alikuwa mmoja wapo, hakutaka kubaki Marekani, alitaka kuwasindikiza ili akutane na daktari ambaye angekuwa anafika nyumbani kila siku kwa ajili ya kumuona Patricia.

Je nini kitaendelea?
Je Huo ndio utakuwa mwisho wa Patricia hasa baada ya kurudi nchini Tanzania?
 
SEHEMU YA 77

bado alikuwa akitamani kukaa na Patricia ambaye alikuwa akizidi kumpenda kadri siku zilivyozidi kwenda mbele.
Bwana Thomson alimchukulia Martin kuwa kama mtoto wake wa kumzaa, moyo ambao alikuwa akiuonyesha kwa mtoto wake ulikuwa ukimfariji kupita kiasi. Katika kipindi cha kula chakula, Martin ndiye alikuwa mtu pekee ambaye alikuwa akimlisha chakula Patricia kwa kutumia mipira ambayo ilikuwa imeunganishwa moja kwa moja mpaka tumboni mwake.
Kila siku Martin alikuwa mtu wa furaha. Kwa kipindi kirefu cha nyuma alikuwa akitamani sana kuungana na patricia na hatimae kuishi pamoja, kuwa nae katika kipindi hicho kulionekana kumfariji.
“Hii ni safari yangu ndefu kuelekea kaburini Martin” Patricia alimwambia Martin.
“Hapana. Hapana Patricia. Hautokufa. Hautokufa Patricia’ Martin alimwambia Patricia.
Maneno yale yalionekana kumuumiza Martin, machozi yakaanza kumtoka. Hakupenda kabisa Patricia aongee maneno yale ambayo yalionekana kumuumiza kupita kawaida. Kwake, maneno yale yalionekana kuwa kama msumali wa moto ambao uliingia moja kwa moja moyoni mwake.
Akapiga magoti chini na kisha uso wake kuusogeza karibu na uso wa Patricia na kisha kumbusu. Kila wakati alikuwa akitamani kumbusu Patricia, japokuwa msichana huyo alikuwa amekonda kupita kiasi lakini bado alikuwa akimpenda. Hakukuwa na msichana yeyote katika ulimwengu huu ambaye alikuwa akimpenda kama jinsi ambavyo alikuwa akimpenda Patricia.
“Hali ya hewa inaonekana kumsumbua mgonjwa. Itatupasa kusafiri kurudi nchini Tanzania pamoja nae” Bi Beatrice alimwambia Martin.
“Mbona ni uamuzi wa haraka hivyo mama?” Martin aliuliza huku akionekana kushtuka.
“Ndivyo tulivyoamua pamoja na baba yake. Itatupasa kurudi nchini Tanzania kwani mgonjwa wetu amefikia ukingoni kupata nafuu. Hatoweza kupata nafuu zaidi ya hapo” Bi Beatrice alimwambia Martin.
Hakukuwa na kitu kilichoendelea zaidi ya harakati za kurudi nchini tanzania kuanza. Martin hakutaka kumficha Patricia, alichokifanya ni kumwambia juu ya kie kitu ambacho kilikuwa kimepangwa na kukubalika na kila mtu.
“Tunarudi Tanzania. Najua kwamba haukuwa na ndoto ya kurudi Tanzania, haina budi kwa sasa Patricia” Martin alimwambia Patricia.
“Niko tayari kurudi. Niko tayari kwa kitu chochote kutokea maishani mwangu ila si kukupoteza wewe. Umekuwa mfariji wangu mkubwa Martin” Patricia alimwambia Martin.
Mipango ya safari ikawa imekamilika, ndege ambayo ilikuwa ikimilikiwa na Bwana thomson ikaandaliwa na kisha safari kuanza huku ndani ya ndege kukiwa na watu wasiozidi saba. Bwana Thomson alikuwa mmoja wapo, hakutaka kubaki Marekani, alitaka kuwasindikiza ili akutane na daktari ambaye angekuwa anafika nyumbani kila siku kwa ajili ya kumuona Patricia.

Je nini kitaendelea?
Je Huo ndio utakuwa mwisho wa Patricia hasa baada ya kurudi nchini Tanzania?

ITAENDELEA
Mkuu mbona unarudia rudia episode za jana au mimi ndio sielewi
 
SEHEMU YA 58



Taarifa zilikuwa zimekwishatolewa kwamba Martin alikuwa akirudi nchini Tanzania baada ya kukaa nchini Marekani kwa muda wa mwaka mmoja na nusu. Katika kipindi hiki hakuwa akirudi peke yake kama kipindi kingine, kwa sasa alikuwa akirudi na msichana ambaye alikuwa akimpenda, msichana ambaye alikuwa ameyabadilisha maisha yake, Patricia.
Watu wakakusanyika katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere kwa ajili ya kuwapokea watu hao. Mabango mbalimbali ambayo yalikuwa yakimtakia Patricia afya njema yalikuwa yakionekana kushikwa na watu wengi ambao walikuwa wamekusanyika uwanjani hapo.
Saa saba na robo mchana ndege ikaanza kuingia uwanjani hapo. Watu wakaanza kujisogeza huku waandishi wa habari wakizishika kamera zao vizuri. Ndege iliposimama, Bwana Thomson pamoja na mpenzi wake, Bi Beatrice wakaanza kuteremka. Baadae, kitanda kilichombeba Patricia kikaanza kuteremshwa huku Martin akiwa pembeni. Watu wakashindwa kujizuia, machozi yalikuwa yakiwatoka huku vilio vikianza kusikika uwanjani hapo
Hali aliyokuwa nayo Patricia ilionekana kumgusa kila mtu, watu walionekana kuumizwa kupita kawaida. Martin alikuwa pembeni, alionekana kuwa mnyonge na hata lile tabasamu ambalo alikuwa akilitoa halikuwa lile tabasamu ambalo lilizoeleka kuonekana usoni mwake.
Moja kwa moja waandishi wa habari wakaanza kumsogelea na kuanza kumuhoji baadhi ya maswali. Kila kitu ambacho alikuwa akikiongea mahali hapo bado alikuwa akisisitiza upendo wake mkubwa ambao alikuwa nao juu ya Patricia.
“Ninampenda. Ninamuhitaji sana” Martin aliwaambia.
Kitu alichokifanya Bi Beatrice ni kuwashukuru watu wote elfu mbili ambao walikuwa wamejitolea muda wao kufika uwanjani pale kwa ajili ya kuwapokea na kisha safari ya kuelekea nyumbani kuanza.
Muda wote Martin alikuwa pembeni ya Patricia, hakutaka kukaa mbali nae hata mara moja. Kwake, bado Patricia alionekana kuwa msichana ambaye alihitaji uangalifu mkubwa kutoka kwake.
“Najua nitakufa Martin” Patricia alimwambia Martin huku akionekana kukata tamaa.
“Haiwezekani. Hautokufa”
“Unanifariji tu Martin. Nitakufa tu. Yaani ni afadhali nife Martin kuliko kuendelea kuteseka kitandani namna hii” Patricia aimwambia Martin ambaye alibaki kimya.
 
SEHEMU YA 59

Tayari machozi yakaanza kumtoka Martin. Kukata tamaa kwa Patricia kulionekana kumuumiza kupita kawaida. Alijua kwamba Patricia alikuwa katika hali mbaya lakini bado hakutaka kumpoteza.
*********
Tajiri mkubwa, Bwana Jonathan alionekana kuridhika na ile ajali ambayo ilikuwa imetokea, mipango yake ambayo alikuwa ameipanga akaiona ikiwa imekwenda kama vile alivyopanga kabla. Moyo wake ukawa unasherehekea, kitendo cha Patricia na Banana kulazwa hospitalini kilionekana kumfurahisha.
Moyo wake ulikuwa ukimpenda na kumtaka sana Patricia, kitendo cha kumkatalia mara kwa mara ndicho kilimfanya kuamua kuipanga ajali ile mbaya. Kila alipokuwa akiona Patricia na Banana wapo hospitalini alikuwa akijisikia faraja kupita kiasi moyoni mwake.
Siku ziliendelea kukatika huku nae akijifanya kufika hospitalini pale kwa ajili ya kuwaangaia wagonjwa wake. Kila alipokuwa akifika hospitalini hapo alikuwa akifurahia kupita kawaida, tayari aliona kwamba alikuwa amewaweza kwa kipindi hicho.
Kadri siku zilivyozidi kwenda mbele na ndivyo hali za wagonjwa wale zilivyozidi kuwa mbaya kiasi ambacho moyo wake ukaanza kuingiwa na wasiwasi zaidi. Ni kweli alitaka wawili wawe wapatwe na ajali ile ambayo alikuwa ameipanga lakini moyo wake haukutaka watu wale wakae hospitalini kwa kipindi kirefu.
Kadri hali ilivyozidi kwenda mbele na ndivyo ambavyo hali ya Patricia na Banana zilivyozidi kuwa mbaya. Bwana Jonathan akaanza kujutia kile ambacho alikuwa amekifanya, mara kwa mara alipokuwa akilala alikuwa akipata ndoto na mawazo ya ajabu ajabu.
Moyo wake ukaanza kujawa na majuto. Kila siku alikuwa akijikalia kitandani mwake akilia. Kadri picha ya Patricia na Banana zilivyokuwa zikimjia kichwani kwa jinsi walivyokuwa kule hospitalini alikuwa akiumia zaidi. Usiku hakulala vizuri, utajiri mkubwa ambao alikuwa nao ukaonekana kutokuwa na furaha kabisa.
Hali ilizidi kuwa mbaya kwake hasa pale ambapo Banana alipofariki. Akaanza kuihisi damu ya Banana ikimlilia kila usiku alipokuwa akilala. Ndoto mbaya za kutisha na kusisimua zilikuwa zikimuandama kila siku. Amani akakosa moyoni mwake, akawa mtu wa mawazo kupita kawaida.
 
SEHEMU YA 60

Alitamani kutubu juu ya kile kitu ambacho alikuwa amekifanya, hakujua dunia ingemchukulia vipi na watu wangemuonaje. Kutubu ndicho kitu ambacho alikuwa akitaka kukifanya kwa kuamini kwamba angeweza kuwa na amani moyoni mwake kama ilivyokuwa zamani.
Kila siku alikuwa akipiga magoti na kutubu mbele ya Mungu wake lakini hali ile haikuweza kumtoka, damu ya Banana ilikuwa ikimlilia kila siku. Mipango yake mingi ya biashara ikaonekana kuanza kwenda hovyo, muda mwingine Bwana Jonathan alionekana kuwa kama mtu ambaye alichanganyikiwa.
Kila siku alikuwa akiongea peke yake, akili yake ikaonekana kuanza kuharibika kutokana na mawazo mabaya pamoja na mambo ya ajabu ajabu ambayo yalikuwa yakimjia kichwani mwake. Walinzi wake walionekana kumshangaa sana, hali ambayo alikuwa nayo katika kipindi hicho ilionekana kuwa tofauti kabisa na zamani.
Tayari mkewe, Bi Leticia alikuwa amekwishaanza kuyaona mabadiliko ya mume wake jambo ambalo likapelekea kuanza kufanya mawasiliano na watu wa Saikolojia na kumpeleka mumewe katika ofisi za watu hao. Huko ndipo ambapo akili ya Bwana Jonathan ikaanza kushughulikiwa kwa kuambiwa mambo mengi kama kuifanya akili hiyo irudi kama zamani.
Kila siku Bwana Jonathan alikuwa akipelekwa kwa watu hao lakini bado hali haikuweza kubadilika kabisa. Kila siku alikuwa akiona mauza uza hasa nyakati za kulala, sauti za ajabu ajabu zilikuwa zikisikika masikioni mwake huku wakati mwingine picha ya Patricia akiwa kitandani ikimjia pamoja na kuona jeneza lililoandikwa jina la Banana pembezoni mwa chumba chake.
Kazi zote ambazo alikuwa akizifanya akamuachia mtoto wake, Robert. Kadri muda ulivyozidi kwenda mbele na ndivyo ambavyo Bwana Jinathan alivyozidi kuchanganyikiwa mpaka kufikia hatua kubwa zaidi ya kuanza kutupa vitu huku na kule.
Kila mtu ambaye alikuwa akisikia juu ya hali aliyokuwa nayo Bwana Jonathan alikuwa akishangaa, hakukuwa na mtu ambaye aliamini kama tajiri yule alikuwa amechanganyikiwa kiasi cha kupelekwa katika hospitali ya vichaa iliyokuwa hapo jijini New York.
 
SEHEMU YA 61

Hakukuwa na mtu ambaye aliujua ukweli zaidi yake yeye pamoja na wale watu ambao alikuwa ameshirikiana nao. Bwana Jonathan akawa amechanganyikiwa kwa asilimia mia moja. Mauza uza ambayo yalikuwa yakionekana kwake hayakuwa yakipungua, mara kwa mara alikuwa akipiga kelele huku akiliita jina la Banana kitu ambacho kilionekana kuwashangaza manesi na madaktari.
Kila siku mkewe, Bi Leticia alikuwa akimtembelea katika hospitali ile. Kwa wakati huo na ile hali ambayo alikuwa nayo, Bwana Jonathan hakuwa akimtambua mtu yeyote yule. Kila alipokuwa akimuona mke wake na mtoto wake, aliwaona watu wageni ambao walikuwa wamekuja kumtembelea.
Mara kwa mara alikuwa akilitaja jina la Patricia na Banana, hakukuwa na mtu aliyeelewa sababu ambayo ilimpelekea Bwana Jonathan kuyatamka majina hayo ya watu ambao walikuwa wamepata ajali kipindi cha miezi sita iliyopita.
Mwaka wa kwanza ukapita, wa pili ukapita na wa tatu kuingia. Bwana Jonathan alikuwa katika hali ile ile ambayo ilikuwa ikiwashangaza watu wote. Wapo ambao waliamini kwamba mzee huyo alikuwa amerogwa na watu ambao hawakupenda kumuona akiendelea kuvuna kiasi kikubwa cha fedha.
Mara kwa mara waandishi wa habari walikuwa wakielekea kwa mganga Mutinho ambaye alikuwa na asili ya Brazil aliyekuwa akiishi pale nchini Marekani na kuanza kumuuliza chanzo cha ugonjwa wa Bwana Jonathan.
Mganga Mutinho ndiye alikuwa mganga mashuhuri nchini Marekani ambaye alikuwa akitumia uchawi wa nyumbani kwao Brazil na kuwaponya watu, kuwapa watu utajiri, mafanikio na hata umaarufu mkubwa duniani. Watu wengi ambao walikuwa wakihitaji kufanikiwa katika maisha yao walikuwa wakimfuata Mutihno ambaye alikuwa akiwapa dawa na baada ya siku saba kupata kile ambacho walikuwa wakikihitaji.
Mgana Mutihno alikuwa na jina kubwa nchini Marekani, umaarufu wake ndio uliwafanya Wabrazil wengi kuanza kuruhusiwa nchini Marekani kwa kuonekana kwamba wangeweza kuwa kama Mutinho ambaye alionekana kuwa msaada mkubwa kwa watu ambao walikuwa wakitafuta mafanikio na umaarufu nchini Marekani
Kila alipokuwa akiulizwa na waandishi wa habari juu ya hali ya Bwana Jonathan, Mutinho hakutoa jibu lolote zaidi ya kutaka mtu huyo kupelekwa kanisani na kufanyiwa maombezi.
 
SEHEMU YA 62

Jibu lile likaonekana kumshangaza kila mtu. Mganga yule ambaye kila siku alikuwa akiupinga Ukristo kwa nguvu zote leo ndio alikuwa akitaka mtu huyo apelekwe kanisani kufanyiwa maombezi. Kila mtu alionekana kushtushwa na ushauri ule wa mganga Mutinho.
Mganga Mutinho hakuishia hapo, akaanza kuwaambia waandishi mambo mengi ambayo yangemfanya yeye kushindwa kabisa kumtibia Bwana Jonathan kwa kuwaambia kwamba ugonjwa ule haukuwa na wakurogwa au mchezo mchafu ambao matajiri hasa wa Marekani walikuwa wakipenda kutumia bali ulikuwa ni ugonjwa ambao wala haukutakiwa kutolewa na nguvu za majini kwa sababu yasingeweza kabisa.
Bi Leticia alipoambiwa kuhusu kumpeleka mumewe kwenye kanisa lolote nchini Marekani, akaonekana kupinga. Katika maisha yake alikuwa kama mumewe, alikuwa akiuchukia Ukristo kupita kawaida. Hakuupenda Ukristo, kila siku katika maisha yake alitamani dini hiyo ipotee kabisa na dunia nzima kuwa wapagani kama jinsi alivyokuwa yeye na familia yake.
Toka siku ambayo Bi Leticia alipopewa ushauri kuhusu kumpeleka mumewe kufanyiwa maombezi na ndio siku ambayo ugonjwa ule wa mumewe ukazidi kuongezeka na kuwa mbaya zaidi. Kila mtu ambaye alikuwa akipita mbele yake, Bwana Jonathan alikuwa akichukua viti, chupa na vitu vingine na kuanza kumrushia.
Madaktari wakaona hali kuwa mbaya zaidi, walichoamua kukifanya kwa wakati huo ni kumfunga minyororo Bwana Jonathan huku tiba ambayo wala haikuonekana kuwa na mafanikio ikiendelea kutolewa mwilini mwake.
“Impossible (Haiwezekani)” Bi Leticia aliwaambia waandishi wa habari ambao walimpelekea ushauri wa mganga Mutinho.
Huo ndio msimamo ambao alikuwa ameuweka katika maisha yake. Aliapa kutokuingia kanisani kabisa, kutokana na kuuchukia Ukristo basi hata kanisa alilichukia kabisa. Kila siku alipokuwa akiambiwa kuhusiana na ushauri ule wa kumpeleka mumewe kufanyiwa maombezi kanisani bado aliendelea kupinga.
Ilikuwa ni afadhali umchome hata kisu lakini si kumwambia kuingia kanisa. Kila mtu alionekana kumshangaa Bi Leticia. Kama mwanamke huyo alimuamini sana mganga Mutinho kama Wamarekani wengi walivyomuamini, sasa kwa nini hakuwa akiamini kama ushauri wake ule ungeweza kufaa?
 
SEHEMU YA 63

Kadri alivyozidi kukataa na ndivyo hali ya mumewe ilivyozidi kuwa mbaya zaidi na zaidi. Katika kipindi hiki Bwana Jonathan akaanza kujidhuru yeye mwenyewe. Akaanza kujipiga piga huku akijing’ata ng’ata kila wakati hali ambayo ilimfanya muda wote kutokwa damu.
Hali ile ilitisha, kila siku ilikuwa ikimliza Bi Leticia lakini kamwe hakutaka kuufuata ushauri wa kukubali kumpeleka mumewe kanisani kufanyiwa maombezi, bado aliendelea kukataa.

Maisha yakaanza nchini Tanzania, bado Patricia alikuwa mtu wa kulala kitandani huku mipira ya chakula ikiwa imepitishwa kama kawaida yake. Hali yake bado ilikuwa ikionekana mbaya pale kitandani. Wazazi wake walikuwa ni watu wa kuhuzunika kila wakati, mioyo yao ilikuwa ikimshukuru Martin ambaye kamwe hakutaka kutoka nje ya nyumba ile, kila siku alikuwa ndani akikaa pamoja na Patricia huku akimhudumia kwa kila kitu.
Watanzania wengi wakaonekana kuguswa na hali ambayo alikuwa nayo Patricia jambo ambalo likawafanya kumiminika ndani ya nyumba ile kwa lengo la kumuona msichana huyo ambaye alikuwa katika matatizo makubwa. Kila mtu ambaye alikuwa akimwangalia Patricia alikuwa akilia, hakukuwa na mtu ambaye aliamini kwamba duniani kulikuwa na mtu ambaye alikuwa na matatzo makubwa kama aliyokuwa nayo Patricia.
Wachungaji mbalimbali walikuwa wakienda kumwangalia Patricia na kumfanyia maombi huku nao hata mashehe kutoka sehemu mbalimbali wakimiminika nyumbani pale na kumuombea dua. Kila mmoja alikuwa akiamini kitu kimoja kwamba kungetokea siku ambayo Mungu angefanya miujiza na hatiamae Patricia kupona na kuwa mzima kabisa.
Martin alikuwa akionekana kuwa na huzuni muda wote, maisha yake yalikuwa yamebadilika kwa asilimia mia moja. Furaha haikupatikana tena moyoni mwake, alikuwa mtu wa majonzi kila siku. Mtu ambaye kila siku alikuwa akitamani kumuona tena alikuwa amekwishamuona ila tatizo lilikuwa ni hali ambayo alikuwa amemkuta nayo.
Bwana Thomson alikaa kwa muda wa mwezi mmoja huku akiwa amekwishamuandaa daktari ambaye kila siku alikuwa akitakiwa kufika mahali hapo kwa ajili ya kumhudumia Patricia huku akiwa amekwishalipia gharama za mwaka mzima. Ingawa daktari alikuwa akimhudumia Patricia lakini kamwe Martin hakutaka kuondoka chumbani humo, bado alikuwa akitamani kuwa na Patricia katika kipindi chote.
 
SEHEMU YA 64

Watu ambao walikuwa wamesoma nao katika kipindi cha nyuma katika shule ya Sekondari ya Salma Kikwete wakaanza kufika nyumbani hapo. Hali ambayo walimkuta nayo Patricia, wasichana wakashindwa kujizuia, walikuwa wakilia kama watu waliofiwa.
“Patricia. Unanikumbuka?” Msichana mmoja alimuuliza Patricia.
“Nakukumbuka. Rosemary” Patricia alijibu huku kwa mbali akiachia tabasamu.
“Pole sana Patricia. Sikutarajia kukuona ukiwa katika hali hii. Hali yako imenigusa sana” Rosemary alimwambia Patricia.
“Usijali Rosemary. Naendelea vizuri. Kila kitu ni mipango ya Mungu” Patricia alimwambia Rosemary.
Martin alikuwa amesimama pembeni ya Patricia, muda wote mkono wake ulikuwa umekishika kiganja cha Patricia, hakutaka kumuachia, aliona kama Patricia angeondoka endapo tu asingekuwa amemshika.
Muziki ambao alikuwa akiufanya, hakuufanya tena japokuwa jina lake bado lilikuwa kubwa huku watu wengi wakitamani kumuona tena akiingia studio na kurekodi wimbo wowote na hata kupanda jukwaani kwa mara nyingine baada ya miaka miwili kupita bila kufanya hayo.
Ingawa muziki ulikuwa ni kipaji chake ambacho alikuwa amezaliwa nacho lakini kwa wakati huo hakutaka kabisa kujiingiza katika muziki. Kwanza alikuwa akitaka kupata muda zaidi wa kukaa na Patricia, msichana ambaye alikuwa akimpenda sana kwa kipind hicho.
“Lakini haya matatizo hadi lini? Binti yangu atapata nafuu lini?” Bi Beatrice alimuuliza Martin.
“Madaktari walisema kwamba huu ndio mwisho wa maendeleo yake. Inaniuma sana mama, inaniuma sana kumuona Patricia akiwa katika hali hii” Martin alimwambia Bi Beatrice.
Kila siku walikuwa ni watu wa kutiana moyo kutokana na hali ile ambayo alikuwa nayo Patricia. Miezi sita ikakatika lakini bado Patricia alikuwa katika hali ile ile kama alivyokuwa zamani. Martin aliumia kupita kawaida
“Kuna kitu nataka kukwambia Patricia. Ila naomba ukubaliane nami ili nifurahi” Marin alimwambia Patricia
“Kitu gani?”
“Ninakupenda sana”
“Hilo nafahamu. Hicho ndio kitu chenyewe ulichotaka kuniambia?” Patricia alimuuliza.
“Hapana. Kuna kitu kimoja cha muhimu sana” Martin alimwambia Patricia.
“Niambie Martin”
 
SEHEMU YA 65

Martin akabaki kimya kwa muda, akaanza kumwangalia Patricia, machozi yakaanza kumtoka. Kulia ndio ilikuwa ni sehemu ya maisha yake katika kipindi hicho cha shida, mara kwa mara alikuwa akilia hasa katika kipindi ambacho alikuwa akimwangalia Patricia.
“Nataka........” Martin alisema na kukaa kimya.
“Unataka nini?” Patricia aliuliza.
“Nataka kukuoa. Nataka uwe mke wangu wa ndoa” Martin alimwambia Patricia huku akimshika mkono japokuwa alijua fika kwamba Patricia hakuhisi chochote kama alishikwa mkono kutokana na kupooza.
“Kunioa?” Patricia aliuliza kwa mshtuko.
“Ndio”
“Hapana Martin. Hapana Martin” Patricia alisema huku nae akianza kutokwa na machozi.
“Kwa nini?”
“Sijiwezi kitandani Martin. Siko kama siku ya kwanza tulipofanya mapenzi hotelini. Nipo hapa kama gogo tu. Itakuwaje unioe? Sitoweza hata kukuzalia watoto, na hata kama tukifanya mapenzi, sitohisi chochote Martin. Nimekuwa gogo katika jamii ya watu, sistahili kuolewa wala kuwa na mpenzi Martin” Patricia alimwambia Martin.
“Hata kama Patricia. Ninahitaji kukuoa. Ninahitaji kufanya kile kitu ambacho nilikuahidi kama tu ungekuwa mpenzi wangu” Martin alimwambia Patricia.
“Hapana Martin”
“Kwa nini Patricia? Nataka kukuoa tu, sitohitaji kufanya mapenzi na wewe na wala sitohitaji mtoto kwako. Ninachokihitaji ni kukuoa tu” Martin alimwambia Patricia.
“Mart....”
“Usinikatalie Patricia. Nimefanya mambo mengi kwako. Wewe ndiye ambaye umenifundisha kupenda katika maisha yangu. Ninakupenda Patricia, ninahitaji kuwa nawe, ninahitaji kukuoa na uwe mke wangu wa ndoa” Martin alisema huku machozi yakianza kumtoka.
Patricia hakuongea kitu chocchote kile, alibaki kimya huku akimwangalia Martin. Kwa jinsi Martin alivyokuwa akionekana, alionekana kuwa na uhitaji wa kuwa na Patricia. Hakutaka kusikia kitu chochote kile, kitu ambacho alikuwa akikitaka ni kuwa na Patricia tu.
“Nimekubali” Patricia alimwambia Martin ambaye alitamani kuruka ruka kwa furaha.
*******
Hali ya Bwana Jonathan haikuwa na unafuu hata kidogo, kila siku alikuwa akiendelea kuwa vile vile. Minyororo ilikuwa imeifunga mikono yake na miguu yake huku katika kipindi hiki hata mdomo wake ukiwa umewekewa gundi ya karatasi kwa ajili ya kumzuia kutokujing’ata.
 
SEHEMU YA 66

Taarifa kwamba Bwana Jonathan alikuwa kichaa zilikuwa zikiendelea kuwashtka watu mbalimbali duniani, hawakujua ni kitu gani kilikuwa kimetokea mpaka kuwa katika hali hiyo, hawakujua kama mawazo ndio yalikuwa chanzo au kulikuwa na kitu kingine.
Viongozi mbalimbali wa nchi walikuwa wakikusanyika katika hospitali hiyo kwa ajili ya kumuona. Hawakuruhusiwa kuingia mpaka kule alipokuwa kwani kama wangefika huko basi ni lazima wangezua tatizo jingine zaidi.
Siku ziliendelea kukatika, Bi Leticia hakukubali kabisa mume wake apelekwe kanisani kufanyiwa maombezi. Kadri siku zilivyozidi kwenda mbele na ndivyo ambavyo hali yake ilivyozoso kuwa mbaya zaidi. Mwisho wa siku, Bi Leticia akakubali japo kishingo upande.
Siku ya Jumapili ikawadia, Bi Leticia pamoja na wafanyaazi wake wakaanza kuelekea katika hospitali hiyo ambako wakambeba Bwana Jonathan na kuanza kuondoka nae mahali hapo. Njiani ilikuwa ni matatizo, Bwana Jonathana alikuwa akipiga kelele huku wakati mwingine akivipiga vioo vya gari.
Wanaume watatu ambao walikuwa na nguvu za kutosha walikuwa wamemshika vilivyo Bwana Jonathan kama kumzuia asiweze kuleta madhara yoyote ndani ya gari lile.Safari nzima Bi Leticia alikuwa amekasirika, ndita zilikuwa zimekujamana usoni mwake, kitendo cha kusaliti amari na kukubali kumpeleka mume wake kwenda kanisani kilionekana kumuumiza na kujiona kama kuusaliti uamuzi wake ambao alijiwekea wa kutokukanyaga kanisani.
Kanisa la Pentekoste ambalo lilikuwa likiongozwa na mchungaji Henry White ndilo kanisa ambalo Bwana Jonathan alikuwa njiani akipelekwa. Kanisa hilo ndio lilikuwa kanisa kubwa jijini New York, watu wengi walikuwa wakipenda kwenda katika kanisani lile kwa kuwa miujiza mbalimbali ilikuwa ikifanyika kila Jumapili.
Viziwi walikuwa wakifanyiwa maombezi, wakaanza kusikia, bubu walikuwa wakifanyiwa maombezi na kuanza kuongea tena huku viwete nao wakifanyiwa na maombezi na kutembea tena. Idadi ya washirika elfu ishirini ambao walikuwa wakipatikana kanisani humo walionekana kuongezeka kadri siku zilivyozidi kwenda mbele.
Mchungaji White, kazi yake kubwa kanisani ilikuwa ni kuwafanyia watu maombezi, alimuamini Mungu wake ambaye alikuwa akimwamini katika maisha yake yote, alijua fika kwamba Mungu wake hakushindwa na kitu
 
SEHEMU YA 67

chochote kile.
Kufanya miujiza ndio ilikuwa sehemu ya maisha yake. Mungu alikuwa akimtumia kuponya watu wengi waliokuwa na matatizo mbalimbali na kuwafungua watu ambao walikuwa wamefungwa katika vifungo vya giza vilivyojaa mateso makali
Wachawi walikuwa wakitupa vitu vyao na kuokoka, watu ambao walikuwa wakishuhudia miujiza mbalimbali walikuwa wakiyakabidhi maisha yao kwa Yesu jambo ambalo liliwafanya watu wengi waliokuwa wakichukia Ukristo kufanya kila mipango kutoka kulichoma kanisa lile moto kama makanisa ya Nigeria lakini ulinzi mkubwa ulionekana kuimarishwa katika kanisa hilo.
Saa 3.30 asubuhi, gari aina ya McLloyd 23 lilikuwa likipaki katika eneo la kanisa hilo. Ibada bado ilikuwa ikiendelea kama kawaida kanisani hapo. Kitendo cha kuingia ndani ya eneo la kanisa lile, Bwana Jonathan alikuwa akianza kupiga kelele, hali ya ukichaa ambayo alikuwa nayo ikaonekana kuzidi kuongezeka zaidi na zaidi.
“Let me out of here (Niacheni niondoke mahali hapa)” Mdomo wa Jonathan ulisema.
Watu ambao walikua nje ya kanisa lie wakaanza kulisogelea gari lile ambapo mlango ukafunguliwa na Bwana Jonathan kutolewa. Akashikwa pande zote na kuanza kuingizwa ndani ya kanisa lile.
Sauti ya Bwana Jonathan bado ilikuwa ikisikika, katika kipindi kile, si yeye ambaye alikuwa akipiga kelele bali zile roho ambazo zilikuwa ndani yake ndizo ambazo zilikuwa zikipiga kelele. Mchungaji White alipomuona, akaachia tabasamu pana huku akinywa maji yaliyokuwa pale madhabahuni.
“God told me about this man (Mungu aliniambia kuhusu mtu huyu)” Mchungaji White alisema huku akiachia tabasamu pana jingine.
Bwana Jonathan bado alikuwa akileta vurumai katika mikono ya watu ambao walikuwa wamemshika, alionekana kama kutaka kukimbia mahali hapo na kutoka nje. Ingawa Bi Leticia alikuwa hatamani kuingia kanisani lakini muda ule akaanza kujihisi mtu wa tofauti moyoni mwake.
Akaanza kuhisi hali ya amani moyoni mwake, hali ambayo hakuwahi kuipata kabla ya hapo. Moyo wake ukaonekana kujawa na furaha japokuwa hakujua furaha ile ilikuwa imetokea sehemu gani. Kipindi cha nyuma alijiona kuwa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom