Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,983
- 10,804
- Thread starter
- #61
SEHEMU YA 55 & 56
Patricia aliendelea kubaki hospitalini kwa takribani miezi nane mingine na ndipo hapo akaruhusiwa kutoka hospitalini huku akitakiwa kuwa kwenye uangalizi mkubwa. Kitendo hicho kidogo kilionekana kumpa furaha Martin kwani alikuwa na uhakika wa kumuona Patricia muda wowote ambao angetaka kumuona.
“Kwa kuwa uti wake wa mgongo umevunjika vunjika, kamwe hautoweza kuungika. Ataendelea kuwa katika hali hii mpaka atakapofariki” Dokta aliwaambia.
Kwao iliendelea kuwa taaarifa mbaya kuliko taarifa zot ambazo waliwahi kuzisikia katika maisha yao. Walitamani sana kumuona Patricia akisimama na kuanza kutembea kama siku zile za nyuma alivyokuwa akifanya.
Maisha ya Patricia ya kuwa kitandani yakaanzia katika nyumba ya baba yake, Bwana Thomson. Basi mzee huyo alikuwa akitumia kiasi kikubwa cha fedha kumtibia mtoto wake. Japokuwa Patricia alikuwa kwenye hali mbaya lakini kila siku Bwana Thomson alikuwa akijipa moyo kwamba binti yake huyo angeweza kupona na kuwa mzima kama zamani.
Muda wote Martin alikuwa katika chumba alicholazwa Patricia nyumbani pale. Yeye ndeiye alikuwa akifanya kazi ya kumlisha kwa kutumia mipira ile na hata kukisafisha chombo chake alichokuwa akikitumia kwa ajili ya haja kubwa na ndogo.
Kwa Martin, hakutaka kuupunguza upendo wake, bado alikuwa akiendelea kumpenda Patricia huku akizidi kumpenda kadri siku zilivyozidi kwenda mbele. Patricia kwake alionekana kuwa mwanamke muhimu ambaye wala hakutakiwa kuachwa peke yake kisa alikuwa kwenye hali iliyokuwa na matatizo makubwa.
Hiyo ndio ilikuwa nafasi kubwa kwake ya kumuonyeshea ni kiasi gani alikuwa akimpenda na kumhitaji katika maisha yake. Kila siku alikuwa akilala katika chumba alichokuwa akilala Patricia, hakujali harufu kali ya aja ambayo alikuwa akiipata kila siku chumbani humo, kitu ambacho alikuwa akikijali ni kuwa karibu na Patricia tu.
Miezi ikaendelea kukatika, hatimae Patricia akawa na uwezo wa kuongea vizuri. Kila siku Patricia alionekana kuwa mtu wa kulia tu, moyoni aliumia, alikuwa akijutia uamuzi wake ambao ulimfanya kuhamia nchini Marekani.
Kwake, Martin alionekana kuwa mwanaume pekee ambaye alikuwa na mapenzi ya dhati kwake, upendo mkubwa ambao kila siku Martin alikuwa akimwambia siku za nyuma ulikuwa ukijionyesha katika kipindi hicho cha mateso. Martin hakutaka kuwa na msichana mwingine, msichana ambaye alikuwa akimpenda katika kipindi hicho alikuwa Patricia tu.
“Nakupenda Martin” Patricia alimwambia Martin kwa sauti ya chini.
“Nakupenda pia Patricia. Umekuwa mtu muhimu sana kwangu. Nitaendelea kukupenda katika kipindi chote mpaka pale kifo kitakaponitenganisha nawe” Martin alimwambia Patricia na kisha kumbusu shavuni.
Patricia bado alikuwa akiendelea kuwa katika hali ile ile. Kwa muda wa mwaka wa tatu bado alikuwa kitandani. Martin hakutaka kurudi nchini Tanzania, bado alikuwa akitamani kukaa na Patricia ambaye alikuwa akizidi kumpenda kadri siku zilivyozidi kwenda mbele.
Bwana Thomson alimchukulia Martin kuwa kama mtoto wake wa kumzaa, moyo ambao alikuwa akiuonyesha kwa mtoto wake ulikuwa ukimfariji kupita kiasi. Katika kipindi cha kula chakula, Martin ndiye alikuwa mtu pekee ambaye alikuwa akimlisha chakula Patricia kwa kutumia mipira ambayo ilikuwa imeunganishwa moja kwa moja mpaka tumboni mwake.
Kila siku Martin alikuwa mtu wa furaha. Kwa kipindi kirefu cha nyuma alikuwa akitamani sana kuungana na patricia na hatimae kuishi pamoja, kuwa nae katika kipindi hicho kulionekana kumfariji.
“Hii ni safari yangu ndefu kuelekea kaburini Martin” Patricia alimwambia Martin.
“Hapana. Hapana Patricia. Hautokufa. Hautokufa Patricia’ Martin alimwambia Patricia.
Maneno yale yalionekana kumuumiza Martin, machozi yakaanza kumtoka. Hakupenda kabisa Patricia aongee maneno yale ambayo yalionekana kumuumiza kupita kawaida. Kwake, maneno yale yalionekana kuwa kama msumali wa moto ambao uliingia moja kwa moja moyoni mwake.
Patricia aliendelea kubaki hospitalini kwa takribani miezi nane mingine na ndipo hapo akaruhusiwa kutoka hospitalini huku akitakiwa kuwa kwenye uangalizi mkubwa. Kitendo hicho kidogo kilionekana kumpa furaha Martin kwani alikuwa na uhakika wa kumuona Patricia muda wowote ambao angetaka kumuona.
“Kwa kuwa uti wake wa mgongo umevunjika vunjika, kamwe hautoweza kuungika. Ataendelea kuwa katika hali hii mpaka atakapofariki” Dokta aliwaambia.
Kwao iliendelea kuwa taaarifa mbaya kuliko taarifa zot ambazo waliwahi kuzisikia katika maisha yao. Walitamani sana kumuona Patricia akisimama na kuanza kutembea kama siku zile za nyuma alivyokuwa akifanya.
Maisha ya Patricia ya kuwa kitandani yakaanzia katika nyumba ya baba yake, Bwana Thomson. Basi mzee huyo alikuwa akitumia kiasi kikubwa cha fedha kumtibia mtoto wake. Japokuwa Patricia alikuwa kwenye hali mbaya lakini kila siku Bwana Thomson alikuwa akijipa moyo kwamba binti yake huyo angeweza kupona na kuwa mzima kama zamani.
Muda wote Martin alikuwa katika chumba alicholazwa Patricia nyumbani pale. Yeye ndeiye alikuwa akifanya kazi ya kumlisha kwa kutumia mipira ile na hata kukisafisha chombo chake alichokuwa akikitumia kwa ajili ya haja kubwa na ndogo.
Kwa Martin, hakutaka kuupunguza upendo wake, bado alikuwa akiendelea kumpenda Patricia huku akizidi kumpenda kadri siku zilivyozidi kwenda mbele. Patricia kwake alionekana kuwa mwanamke muhimu ambaye wala hakutakiwa kuachwa peke yake kisa alikuwa kwenye hali iliyokuwa na matatizo makubwa.
Hiyo ndio ilikuwa nafasi kubwa kwake ya kumuonyeshea ni kiasi gani alikuwa akimpenda na kumhitaji katika maisha yake. Kila siku alikuwa akilala katika chumba alichokuwa akilala Patricia, hakujali harufu kali ya aja ambayo alikuwa akiipata kila siku chumbani humo, kitu ambacho alikuwa akikijali ni kuwa karibu na Patricia tu.
Miezi ikaendelea kukatika, hatimae Patricia akawa na uwezo wa kuongea vizuri. Kila siku Patricia alionekana kuwa mtu wa kulia tu, moyoni aliumia, alikuwa akijutia uamuzi wake ambao ulimfanya kuhamia nchini Marekani.
Kwake, Martin alionekana kuwa mwanaume pekee ambaye alikuwa na mapenzi ya dhati kwake, upendo mkubwa ambao kila siku Martin alikuwa akimwambia siku za nyuma ulikuwa ukijionyesha katika kipindi hicho cha mateso. Martin hakutaka kuwa na msichana mwingine, msichana ambaye alikuwa akimpenda katika kipindi hicho alikuwa Patricia tu.
“Nakupenda Martin” Patricia alimwambia Martin kwa sauti ya chini.
“Nakupenda pia Patricia. Umekuwa mtu muhimu sana kwangu. Nitaendelea kukupenda katika kipindi chote mpaka pale kifo kitakaponitenganisha nawe” Martin alimwambia Patricia na kisha kumbusu shavuni.
Patricia bado alikuwa akiendelea kuwa katika hali ile ile. Kwa muda wa mwaka wa tatu bado alikuwa kitandani. Martin hakutaka kurudi nchini Tanzania, bado alikuwa akitamani kukaa na Patricia ambaye alikuwa akizidi kumpenda kadri siku zilivyozidi kwenda mbele.
Bwana Thomson alimchukulia Martin kuwa kama mtoto wake wa kumzaa, moyo ambao alikuwa akiuonyesha kwa mtoto wake ulikuwa ukimfariji kupita kiasi. Katika kipindi cha kula chakula, Martin ndiye alikuwa mtu pekee ambaye alikuwa akimlisha chakula Patricia kwa kutumia mipira ambayo ilikuwa imeunganishwa moja kwa moja mpaka tumboni mwake.
Kila siku Martin alikuwa mtu wa furaha. Kwa kipindi kirefu cha nyuma alikuwa akitamani sana kuungana na patricia na hatimae kuishi pamoja, kuwa nae katika kipindi hicho kulionekana kumfariji.
“Hii ni safari yangu ndefu kuelekea kaburini Martin” Patricia alimwambia Martin.
“Hapana. Hapana Patricia. Hautokufa. Hautokufa Patricia’ Martin alimwambia Patricia.
Maneno yale yalionekana kumuumiza Martin, machozi yakaanza kumtoka. Hakupenda kabisa Patricia aongee maneno yale ambayo yalionekana kumuumiza kupita kawaida. Kwake, maneno yale yalionekana kuwa kama msumali wa moto ambao uliingia moja kwa moja moyoni mwake.