SIMULIZI: Sababu ni Kifo chako baba (Season one)

Man Middo tz

Senior Member
Sep 9, 2020
154
230
SIMULIZI: SABABU NI KIFO CHAKO BABA! (Kisa cha kweli cha kusisimua)
SEHEMU YA KWANZA (01)
MTUNZI: Man Middo Tz +255 655 969 973

Hakika kila kukicha shukrani kwa Muumba kwa kukufikisha siku nyingine ingawa huwezi kujua siku hiyo itakua ya furaha au huzuni. Basi nakumbuka ilikua siku ya tarehe 23 mwezi wa 3 mwaka wa 2009. Katika siku hii ninayoikumbuka katika maisha yangu yote, ilianza vizuri tu kama siku nyingine.

Masaa yalivyozidi kwenda moyo wangu ulikua ukinienda mbio sana. Sikujua kwanini lakini furaha ilianza kupotea kadri masaa yalivyozidi kwenda. Kila nilipomtazama baba, nuru usoni mwake ilipotea kabisa!! Nakumbuka siku hii tulikua likizo ndogo ya wiki hivyo watoto wote tulikua nyumbani, basi siku hii alikua akitutizama sana wanae.

Sikutishwa na kututazama sana kwasababu baba yangu mzee Nelson Magoma alikua akitupenda sana wanae. Lakini kilichonitisha ni pale nilipomuona baba yangu akitokwa na machozi wakati akitukazia jicho wanae. Pia akaanza kutoa nasaha

“Wanangu nawapenda sana, someni sana, someni kwa bidii mje kumsaidia mama yenu kwasababu huko mbeleni maisha yenu yatakua magumu”

Baba ananigeuzia jicho huku akionekana kujawa na uchungu dhidi yangu, moyo wangu ulizidi kunienda mbio ingawa niliamini baba yangu kwakua ni mtu wa imani. Pia ni mwalimu huenda nasaha zile anatoa kwa dhati ili wanae tujue ni kipi anakimaanisha. Jicho la baba kwangu sio tu kuwa lilikua la upendo wa dhat lakini pia lilionyesha uchungu ndani yake, akaniambia

“Nyamlya Soma sana mwanangu, unakili sana na una kila kitu kwasasa”

Sikujua anamaanisha nini lakini mimi nikamuitikia kwa kutikisa kichwa tu. Kitu kingine ni pale aliponiita jina la ukoo baadala ya jina langu la Anna Nelson Magoma au Hesha jina langu la utani.

Baba yangu alikua akinipenda sana. Alikua akionyesha mapenzi makubwa kwangu sio kwamba hakuwapenda wengine lakini kuna kitu kilimfanya baba anikubali sana nitakisema mbeleni.

Uuuh! Siku hiyo usiku baada ya chakula baba akatuita wanae wote tukakusanyika, wakati huo nikashukuru Mungu siku kama imepita salama kwakua yale matukio yaliyojaa uchungu yamepita. Basi baba baada ya kutuita akasema.

“Nimewaita hapa nataka leo tufanye maombi ya kifamilia, Anna naomba uongoze maombi sawa”

“Sawa baba” nikatikia.

Kusema ukweli pamoja na umri wangu wa miaka 11 Wakati huo lakini nilikua naweza kufanya maombi sana kuwazidi ndugu zangu wengine wakubwa. Basi nikaongoza maombi nikamaliza, baada ya kumaliza baba akasema

“Haya maombi ya leo ni muhimu sana naomba hata nikiwa sipo muwe mnaomba hivi, muwe mnakusanyika hivi kama familia, nawapenda sana wangu”

Nasaha ile ikanifanya nijawe na huzuni na moyo wangu uniende mbio, lakini pia hata nilipomtazama mama alionekana mwenye kutafakari yale maneno aliyotamka baba. Sikujali sana kwasababu usiku umefika tukaagana kisha nikaingia chumbani kwangu, dada zangu wakenda zao, hao walikua wakilala kwa bibi yangu na wazazi wakaingia chumbani kwao kulala wakiwa na mdogo wangu wa mwisho mwenye umri wa miaka mitano.
***

Daah! Nikikumbuka machozi yanitoka! Basi nilivyofika kitandani nikajilaza, muda huo wa saa nne usingizi haukukawia nikalala. Ilivyofikausiku nadhan ilikua kama saa 6:30 hivi nikiwa usingizini nilistuka nikasikia kishindo kwa mbali sana huko nje! Lakini maajabu usingizi ukanipitia tena. Kwa mazingira ya kijijin ni kawaida muda kama huo kuwa kwenye usingizi mzito. Lakini baada ya kama dakika 10 purukushani zikanishtua usingizini. Nilivyoamka nikwa bado na usingizi singizi nikasikia sauti za wanaume wakisema

“Mama toa hela…” Mwingine akasikika akisema

“Wee mwanamke tunataka hela tuondoke….au tuwaue watoto wote” Mara ikasikika nyingine kutoka nje ikisema

“Mpigeni kwanza ndio atatoa hela”

Muda huo nilikua nimekaa kitandani sielewi nini kinaendelea zaidi ya zile sauti, Mungu wangu!! Ghafla nikaskia panga kama sita au saba mfululizo kana kwamba mtu anakata miti vile Daah! Damu zikanienda mbio mwili ukatetemeka. Mama nae akaanza kulia kwa kupiga ukunga.

“OOOOH mama nakufaaa... Mama eeh!!”

“Ukiendelea kupiga kelele atafia hapa hapa na wanao wote, bora uwe kimya”

Kweli mama akatii, Sasa kile kitendo cha kumsikia mama analalamika kikanijaza uchungu na kuniuma mnoo, nikatoka kuelekea seblen.

Mawazo yangu niliamini baba ndio anampiga mama, sasa nilipofika sebleni nikakuta wanaume nazani wanafika 5 au 6 kila mmoja kafunga tochi kwenye paji la uso.

Sikuwatambua pia kutokana na kile kilio sikufuatilia ni akina nani. Sasa nilivyosimama mbele ya mmoja wao hakuniona alikua bize anapanga vitu vya baba kuweka kwenye briefcase kubwa ya baba! Alikua akiweka nguo za baba, saa ya ukutani, saa za mkononi, kioo na vingine vidogo dogo. Basi nilipovitambua vile vitu nikamuliza

“Kaka mbona mnapanga vitu harafu Mama anapigwa na baba kwani wamegombana nini? Na nyie mmetokea wapi”

Alivyosikia hivyo ndio akagundua kuwa nipo pale, mmoja akanifuata akanipiga na panga kwa bapa kama ananichapa, harafu akaniongoza hadi chumbani huku naugulia maumivu. Pamoja na maumivu lakini nilikua namuliza maswali ila hajibu, nikafika kitandani akasema

“Lala hapo harafu nikuone unatoka uone”

Nikatii akanifunika shuka akatoka, sasa hapo akili ndio ikarudi na kutambua kuwa hapa kuna hatari kubwa. Yale matukio yote ya mchana kutwa yakanza kujirudia, akili yangu ikanituma na kujua baba yupo kwenye hatari.

Kwa jinsi baba alivyokua ananipenda hata awe na hasira kiasi gani nikimsemesha tu lazima aniambie, mimi nilikua mdogo sana lakini nilikua kama mshauri wa familia. Sasa akili ikanituma nimfuate baba ila hofu nimeambiwa hakuna kutoka. Ghafla nikasikia kishindo kikali sana kama kuna mzigo unanguka kutokea chumbani kwa baba na mama.

Kitendo kile kikanikurupusha nikavaa ujasiri nikatoka, nia yangu nikamuone baba lakini ile kutoka tu nilikutana na kipigo kikali mno. Bonge la bao na mateke huku wakisema

“Wewe si umeambiwa ulale husikii, Toka apaa..!!”

Sasa aliponipiga kofi la uso likanipeperusha nikajikuta nakutana na utelezi nikakunguka, hapo chini nikagundua kilichoniangusha ni damu tena nzito ikitokea chumbani ambako baba yupo. Ile damu illikua imetapakaa hadi sebleni damu nyingi mnoo uuuh! Hapo nguvu zikaniishia nikamsikia mama akisema

“Anna mwanangu rudi chumbani ulale ili ubaki msaada kwa ndugu zako”

Sauti ile ikaninyong’onyesha sana, kupitia kauli hiyo ya mama nikagundua mmoja kati ya baba au mama atakufa! Kumbe wakati huo baba yupo kwenye hali mbaya sana…………ITAENDELEA.

JE UNAJUA KIPI KILIFUATIA? JE KWANINI MZEE NELSON ANAULIWA KIKATILI HIVYO? ANNA ATAVUMILIA?

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA ILI KUJUA KWANINI ANNA ANASEMA “SABABU NI KIFO CHAKO BABA” HATUJUI KIPI KIMETOKEA KWENYE MAISHA YAKE HADI IKAWA SABABU NI KIFO CHA BABA YAKE.NUKUU “Katika maisha wanasema HAKUNA KITAKACHO DUMU MILELE HIVYOHUTAKIWI KUJIPA MAWAZO MENGI KWASABABU HAIJALISHI UNA HALI MBAYA KIASI GANI IPO SIKU ITABADILIKA TU” Ni kweli hiyo kauli, lakini kwa baadhi ya watu ni tofauti kabisa kuna watu toka wanze kupatwa na matatizo katika maisha yao imekuamwendelezo tu tena muda mwingine yakawa yanazidi baadala ya kupungua. Tazama Anna anasema “Sababu ni kifo chako baba” akimaanisha sababu ni kifo cha baba yake ndio maana anakumbwa na matatizo makubwa.Kikubwa kama umzima wa afya mshukuru Mungu sana kwa kila jambo kuna watu wanatamani waishi maisha kama yako lakini haiwezekani.
 
Hongera mkuu kwa kuandika story ndefu ila jiandae kisaiklojia .

kuna wajuaji humu jf

kuna watoa lawama kwanini unapost story nusu nusu.

Sasa jiandae kwa lolote mapema.
 
Hongera mkuu kwa kuandika story ndefu ila jiandae kisaiklojia .

kuna wajuaji humu jf

kuna watoa lawama kwanini unapost story nusu nusu.

Sasa jiandae kwa lolote mapema.
Shukran mkuu! Hiyo season one Ina episodes 70 ndefu km hivyo km ni kuimaliza maana yake nipost kwa siku 70 mfululizo
 
SIMULIZI: SABABU NI KIFO CHAKO BABA! (Kisa cha kweli cha kusisimua)
SEHEMU YA PILI (02)
MTUNZI: Man Middo Tz +255 655 969 973

ILIPOISHIA……….Ile damu illikua imetapakaa hadi sebleni damu nyingi mnoo uuuh! Hapo nguvu zikaniishia nikamsikia mama akisema“Anna mwanangu rudi chumbani ulale ili ubaki msaada kwa ndugu zako” Sauti ile ikaninyong’onyesha sana, kupitia kauli hiyo ya mama nikagundua mmoja kati ya baba na mama atakufa! Kumbe wakati huo baba yupo kwenye hali mbaya sana……........SONGANAYO

Sasa nikiwa pale chini naendelea kuugulia maumivu nikawatambua watu watatu, sasa kitendo cha kuwatambua wale watu kikanifanya nianze kumuita mama

“Mama, Mama mbona wamekuja kuwapiga au wanamdai baba?”

Mama hakunijibu lakini kusikia hivyo alitaka aje kunizuia nisiendelee kutamka maneno yale kwani ningewataja ningekufa pale pale. Mama akazuiwa kutoka huko chumbani alipo akasema

“Anna mwanangu ukiongea chochote utakufa nenda chumbani”

Wale wanaume wakaja wawili kunibeba hadi chumbani wakanilaza kitandani tena, Mwilini nilikua na maumivu makubwa mnoo. Nikawa nasikiliza kwa umakini mkubwa huku sina nguvu hata ya kujigeuza kwasababu maumivu ya kupigwa yalikua makali mnoo.

Waliponipiga hawakuangalia wapige wapi walipiga popote tu. Basi nikatulia kwani wakati huo nishatambua hatari iliyopo, ingawa maajabu toka purukushani zote hizo zianze sijamsikia baba akiongea chochote. Hapo nilijawa na wasiwasi mkubwa mnoo.
Sasa wakati natafakari kuhusu baba mara nikasikia sauti

“Kama mmemaliza jipangeni tuondoke”

Mara nikasikia watu wanaruka juu ya meza, vishindo vikasikika nyuma ya nyumba, hapo kwetu hapakua na geti lakini palikua na mlango wa nyuma ambao ndio walibomoa wakapitia hapo.

Ukimya ulitawala kama dakika 5 bila kusikia sauti ya mama, sasa hapo nikajawa na hofu nikizani wameondoka na baba na mama.

Wakati huo hapo ndani kukawa giza la ajabu maana mwanzo zile tochi zao palikuwa ni zaidi ya umeme. Mara ghafla kuna mtu akaja chumbani akanitikisa nikageuka nikagundua ni mama, nikamkumbtia kwa nguvu lakini cha ajabu alikuwa uchi na kaloa damu mwili mzima. Swali langu la kwanza kwake lilikuwa

“Hizi damu ni za nani” Mama hakunijibu, nikampa shuka ajistiri mama hakulipokea…nikamuuliza

“Baba yuko wap namtaka baba”

Hakunijibu ila akaniinua akimaanisha nimfuate, kweli nikamfuata tukaelekea chumbani lakini bado giza lilikuwepo kwasabu kama ujuavyo kijijini vibatari ndio vinatumika hatukua na umeme.

Basi akatafuta kiberiti humo chumbani alipokiona akakiwasha akammulika baba pale alipolala kwa ile njiti ya kiberiti akanambia

“Pita hapa baba yako huyu hapa”

MUNGU WANGU! Sikuamini nilichokiona omba tu usimuliwe kama hivi! kwanza nguvu zikaisha mara mbili yake. Baba alikua amekatwa katwa kila sehemu ya mwilli yani mwili wake waliugeuza kama bucha, mwili wote ulikua umetapakaa damu hata macho sikuyaona.

Kwa mapenzi niliyokua nayo kwa baba nikataka hata kumshika tu nione kama bado ni mzima, Nikaenda kumuangukia baba lakini mama akanidaka akasema

“Kuwa jasiri” akanivuta nje akanambia “Njoo” tukafungua mlango tukaelekea nje kwenye nyumba ya bibi mzaa baba, alikuwa akilala na dada zangu na mdogo wangu anaenifuata.

Kwa mazingira ya kijijini paliachana ingawa sio sana. Tulivyofika tukaanza kuwaamsha hawaamki hadi tukapiga yowe ndo watu wa kijijini wakaja kwa wingi hasa wanaume....Wanaume Wakamtoa baba nje alikua bado anapumua kidogo ingawa kila akitoa pumzi damu nyingi zinatoka nje kama lita 5 hivi.

Sasa wakamlaza mlangoni wakati huo wamepiga simu polisi wanasubiri gari la polisi lifike, ndugu zangu wote walianza kutokwa na machozi, kila mtu aliyefika pale uso wake ulibadilika, halikua tukio la kawaida ingawa matukio kama hayo kwa mkoa wa Mara hutokea mara nyingi.

Baba akiwa kalala pale alijivuta akionekana kuwa na maumivu makali sana, akavuta mkoba wangu wa madaftari ya shule ndo akauegemea lakini hakuwa na uwezo hata wa kufumbua macho.

Kwa kweli ukimtazama unaweza usile nyama tena kwasababu jicho la kushoto halikuwepo, kichwa walikipasua hakikuwa kinaonekan wala kueleweka, Mkono wa kushoto ulikuwa umekatwakatwa kama nyama (oooh! Baba yangu uko wapi, nimemiss tabamu lako, utu wako wema wako na upendo wako kwangu baba ...R.I.P daddy)

Baadae baba akamuita mama, alipofika hakuweza kuongea maana hata maneno yake ilikua shida kujua anatamka nini, mara ghafla akaniita watu wakanisogeza kwasababu sikua na nguvu tena. Kufika kuongea hakuweza alichokifanya baba akanipungia mkono tu nikashindwa kujizuia nilia kwa sauti lakini watu wakanizuia wakiniambia

“TULIA ANNA BABA YAKO HAJAFA”

Baadae akamuita mama tena lakini hakuweza kuongea tena, sasa wakati narudi kumuona baba nimeboreka hatari, bibi akanishika bega huku akilia akaniambia

“Leo baba yenu wamemuua mtajuta sana wajukuu zangu… mwanangu amekufa mtahangaika sana”

Bibi ingawa ni mtu mzima lakini alishindwa kujizuia, kwa upande wangu mimi niliona kama baba kaniacha mimi tu. Kutokana na utoto sikutafakari bibi kamaanisha nini, nikamktoa mkono wake kwa nguvu huku nikimwambia

“Hata wewe utajuta sio sisi tu” (OOH my grandmom Nisamehe ulikua utoto, uko wapi bibi yangu)

Hatimae polisi wakafika pale, wakafanya utaratibu wao wakamchukua baba, mama na watu baadhi wakaelekea mjini hospitali ya mkoa ambapo ni kama saa zima na dakika kadhaa kutoka nyumbani, lakini walipofika nusu safari sehemu moja panaitwa Nyabange, baba yangu kipenzi alijigeuza kwa nguvu zote akasema

“Mama Akwilini nilindie wanangu wasome”

Huo ndo ukawa mwisho wa uwepo wa baba kwenye uso wa hii dunia chungu, R.I.P BABA. Tuliupumzisha mwili wake kwenye makaburi ya familia!

Maisha mapya yakaanza, Kwanza ilikua ngumu sana kuishi maisha yale bila uwepo wa baba haswa kwangu. Mapenzi ya baba kwangu yalikua makubwa mnoo kuzidi hata ya mama naongea hivi kwa jinsi nilivyokua naishi na wazazi wangu.

Katika kipindi hicho kwanza tulikuwa Kama hatujielewi hasa mama, bibi na mimi, hatukua sawa kiakili kutokana na tukio lile la kinyama. Kilikuwa kipindi kigumu mno kwa mama kuondokewa na mumewe kipenzi tena kwa tukio la kigaidi akishuhudia kuanzia dakika ya kwanza hadi mwisho.

Bibi na uzee wake alikua kama anaelekea kuchanganyikiwa! Hapo ndio niliona namna bibi alivyokua akimpenda mwanae. Kwa upande wangu sikueleweka kabisa, hapo nyumbani hatukua sawa yani hata tukisikia mngurumo wa pikpiki barabarani tunahisi wamerudi kutuua (Watu wasiojulikana)

Kesi ikafunguliwa baadhi ya wahusika wakashikwa, mama alichuliwa na jeshi la polisi mara kwa mara kwajili ya upelelezi. Kwa upande mwingine wanakijiji waliguswa sana na tukio lile, sasa wakajipanga kuteketeza wahusika wote wa ujambazi hapo kijijini.

Baadhi ya wahusika walikamatwa hivyo walikua wakifika mahakamani wanatajana, sasa wanakijiji wakisikia tu wanatoka kwenda kwake kuteketeza mali zake au kumtafuta mhusika. Katika matukio yote hayo ilitulazimu kuungana nao hata ikipigwa mbiu usiku wa manani.

Sasa toka hapo ndio mateso, tabu na vipindi vichache vya furaha katika dunia hii vikaanza ndio maana nasema “SABABU NI KIFO CHAKO BABA”…….ITAENDELEA.

JE KWANINI WAMEMUUA MZEE MAGOMA KINYAMA HIVYO SABABU NI NINI?

JE NI MATESO GANI YALIANZA BAADA YA HAPO? JE HAO WASIOJULIKANA HAWAKURUDI TENA?

MAJIBU YOTE YAPO EPISODE YA 3 USIKOSE.

NUKUU “Magumu katika maisha yako hayaji kukuondoa, ila yanakuja kukusaidia kutambua uwezo na nguvu yako iliyojificha. Kwa kipindi kigumu walichonacho familia hii inahitaji uwezo wa Mungu pekee kuweza kusimama imara. Tujifunze kuishi kwa kumtegemea Mungu na tuombe sana kama uko na familia yako nzima omba kila siku yasiwakute masaibu kama haya. Katika maisha thamini sana LEO kwakua JANA imepita na KESHO huijui. Kila ukiamka mshukuru Mungu na uombe uwe salama hujui dakika mbili mbeleni kutatokea nini”

By @middotz_ on Twitter and Instagram
 
SIMULIZI: SABABU NI KIFO CHAKO BABA! (Kisa cha kweli cha kusisimua)
SEHEMU YA PILI (02)
MTUNZI: Man Middo Tz +255 655 969 973

ILIPOISHIA……….Ile damu illikua imetapakaa hadi sebleni damu nyingi mnoo uuuh! Hapo nguvu zikaniishia nikamsikia mama akisema“Anna mwanangu rudi chumbani ulale ili ubaki msaada kwa ndugu zako” Sauti ile ikaninyong’onyesha sana, kupitia kauli hiyo ya mama nikagundua mmoja kati ya baba na mama atakufa! Kumbe wakati huo baba yupo kwenye hali mbaya sana……........SONGANAYO

Sasa nikiwa pale chini naendelea kuugulia maumivu nikawatambua watu watatu, sasa kitendo cha kuwatambua wale watu kikanifanya nianze kumuita mama

“Mama, Mama mbona wamekuja kuwapiga au wanamdai baba?”

Mama hakunijibu lakini kusikia hivyo alitaka aje kunizuia nisiendelee kutamka maneno yale kwani ningewataja ningekufa pale pale. Mama akazuiwa kutoka huko chumbani alipo akasema

“Anna mwanangu ukiongea chochote utakufa nenda chumbani”

Wale wanaume wakaja wawili kunibeba hadi chumbani wakanilaza kitandani tena, Mwilini nilikua na maumivu makubwa mnoo. Nikawa nasikiliza kwa umakini mkubwa huku sina nguvu hata ya kujigeuza kwasababu maumivu ya kupigwa yalikua makali mnoo.

Waliponipiga hawakuangalia wapige wapi walipiga popote tu. Basi nikatulia kwani wakati huo nishatambua hatari iliyopo, ingawa maajabu toka purukushani zote hizo zianze sijamsikia baba akiongea chochote. Hapo nilijawa na wasiwasi mkubwa mnoo.
Sasa wakati natafakari kuhusu baba mara nikasikia sauti

“Kama mmemaliza jipangeni tuondoke”

Mara nikasikia watu wanaruka juu ya meza, vishindo vikasikika nyuma ya nyumba, hapo kwetu hapakua na geti lakini palikua na mlango wa nyuma ambao ndio walibomoa wakapitia hapo.

Ukimya ulitawala kama dakika 5 bila kusikia sauti ya mama, sasa hapo nikajawa na hofu nikizani wameondoka na baba na mama.

Wakati huo hapo ndani kukawa giza la ajabu maana mwanzo zile tochi zao palikuwa ni zaidi ya umeme. Mara ghafla kuna mtu akaja chumbani akanitikisa nikageuka nikagundua ni mama, nikamkumbtia kwa nguvu lakini cha ajabu alikuwa uchi na kaloa damu mwili mzima. Swali langu la kwanza kwake lilikuwa

“Hizi damu ni za nani” Mama hakunijibu, nikampa shuka ajistiri mama hakulipokea…nikamuuliza

“Baba yuko wap namtaka baba”

Hakunijibu ila akaniinua akimaanisha nimfuate, kweli nikamfuata tukaelekea chumbani lakini bado giza lilikuwepo kwasabu kama ujuavyo kijijini vibatari ndio vinatumika hatukua na umeme.

Basi akatafuta kiberiti humo chumbani alipokiona akakiwasha akammulika baba pale alipolala kwa ile njiti ya kiberiti akanambia

“Pita hapa baba yako huyu hapa”

MUNGU WANGU! Sikuamini nilichokiona omba tu usimuliwe kama hivi! kwanza nguvu zikaisha mara mbili yake. Baba alikua amekatwa katwa kila sehemu ya mwilli yani mwili wake waliugeuza kama bucha, mwili wote ulikua umetapakaa damu hata macho sikuyaona.

Kwa mapenzi niliyokua nayo kwa baba nikataka hata kumshika tu nione kama bado ni mzima, Nikaenda kumuangukia baba lakini mama akanidaka akasema

“Kuwa jasiri” akanivuta nje akanambia “Njoo” tukafungua mlango tukaelekea nje kwenye nyumba ya bibi mzaa baba, alikuwa akilala na dada zangu na mdogo wangu anaenifuata.

Kwa mazingira ya kijijini paliachana ingawa sio sana. Tulivyofika tukaanza kuwaamsha hawaamki hadi tukapiga yowe ndo watu wa kijijini wakaja kwa wingi hasa wanaume....Wanaume Wakamtoa baba nje alikua bado anapumua kidogo ingawa kila akitoa pumzi damu nyingi zinatoka nje kama lita 5 hivi.

Sasa wakamlaza mlangoni wakati huo wamepiga simu polisi wanasubiri gari la polisi lifike, ndugu zangu wote walianza kutokwa na machozi, kila mtu aliyefika pale uso wake ulibadilika, halikua tukio la kawaida ingawa matukio kama hayo kwa mkoa wa Mara hutokea mara nyingi.

Baba akiwa kalala pale alijivuta akionekana kuwa na maumivu makali sana, akavuta mkoba wangu wa madaftari ya shule ndo akauegemea lakini hakuwa na uwezo hata wa kufumbua macho.

Kwa kweli ukimtazama unaweza usile nyama tena kwasababu jicho la kushoto halikuwepo, kichwa walikipasua hakikuwa kinaonekan wala kueleweka, Mkono wa kushoto ulikuwa umekatwakatwa kama nyama (oooh! Baba yangu uko wapi, nimemiss tabamu lako, utu wako wema wako na upendo wako kwangu baba ...R.I.P daddy)

Baadae baba akamuita mama, alipofika hakuweza kuongea maana hata maneno yake ilikua shida kujua anatamka nini, mara ghafla akaniita watu wakanisogeza kwasababu sikua na nguvu tena. Kufika kuongea hakuweza alichokifanya baba akanipungia mkono tu nikashindwa kujizuia nilia kwa sauti lakini watu wakanizuia wakiniambia

“TULIA ANNA BABA YAKO HAJAFA”

Baadae akamuita mama tena lakini hakuweza kuongea tena, sasa wakati narudi kumuona baba nimeboreka hatari, bibi akanishika bega huku akilia akaniambia

“Leo baba yenu wamemuua mtajuta sana wajukuu zangu… mwanangu amekufa mtahangaika sana”

Bibi ingawa ni mtu mzima lakini alishindwa kujizuia, kwa upande wangu mimi niliona kama baba kaniacha mimi tu. Kutokana na utoto sikutafakari bibi kamaanisha nini, nikamktoa mkono wake kwa nguvu huku nikimwambia

“Hata wewe utajuta sio sisi tu” (OOH my grandmom Nisamehe ulikua utoto, uko wapi bibi yangu)

Hatimae polisi wakafika pale, wakafanya utaratibu wao wakamchukua baba, mama na watu baadhi wakaelekea mjini hospitali ya mkoa ambapo ni kama saa zima na dakika kadhaa kutoka nyumbani, lakini walipofika nusu safari sehemu moja panaitwa Nyabange, baba yangu kipenzi alijigeuza kwa nguvu zote akasema

“Mama Akwilini nilindie wanangu wasome”

Huo ndo ukawa mwisho wa uwepo wa baba kwenye uso wa hii dunia chungu, R.I.P BABA. Tuliupumzisha mwili wake kwenye makaburi ya familia!

Maisha mapya yakaanza, Kwanza ilikua ngumu sana kuishi maisha yale bila uwepo wa baba haswa kwangu. Mapenzi ya baba kwangu yalikua makubwa mnoo kuzidi hata ya mama naongea hivi kwa jinsi nilivyokua naishi na wazazi wangu.

Katika kipindi hicho kwanza tulikuwa Kama hatujielewi hasa mama, bibi na mimi, hatukua sawa kiakili kutokana na tukio lile la kinyama. Kilikuwa kipindi kigumu mno kwa mama kuondokewa na mumewe kipenzi tena kwa tukio la kigaidi akishuhudia kuanzia dakika ya kwanza hadi mwisho.

Bibi na uzee wake alikua kama anaelekea kuchanganyikiwa! Hapo ndio niliona namna bibi alivyokua akimpenda mwanae. Kwa upande wangu sikueleweka kabisa, hapo nyumbani hatukua sawa yani hata tukisikia mngurumo wa pikpiki barabarani tunahisi wamerudi kutuua (Watu wasiojulikana)

Kesi ikafunguliwa baadhi ya wahusika wakashikwa, mama alichuliwa na jeshi la polisi mara kwa mara kwajili ya upelelezi. Kwa upande mwingine wanakijiji waliguswa sana na tukio lile, sasa wakajipanga kuteketeza wahusika wote wa ujambazi hapo kijijini.

Baadhi ya wahusika walikamatwa hivyo walikua wakifika mahakamani wanatajana, sasa wanakijiji wakisikia tu wanatoka kwenda kwake kuteketeza mali zake au kumtafuta mhusika. Katika matukio yote hayo ilitulazimu kuungana nao hata ikipigwa mbiu usiku wa manani.

Sasa toka hapo ndio mateso, tabu na vipindi vichache vya furaha katika dunia hii vikaanza ndio maana nasema “SABABU NI KIFO CHAKO BABA”…….ITAENDELEA.

JE KWANINI WAMEMUUA MZEE MAGOMA KINYAMA HIVYO SABABU NI NINI?

JE NI MATESO GANI YALIANZA BAADA YA HAPO? JE HAO WASIOJULIKANA HAWAKURUDI TENA?

MAJIBU YOTE YAPO EPISODE YA 3 USIKOSE.

NUKUU “Magumu katika maisha yako hayaji kukuondoa, ila yanakuja kukusaidia kutambua uwezo na nguvu yako iliyojificha. Kwa kipindi kigumu walichonacho familia hii inahitaji uwezo wa Mungu pekee kuweza kusimama imara. Tujifunze kuishi kwa kumtegemea Mungu na tuombe sana kama uko na familia yako nzima omba kila siku yasiwakute masaibu kama haya. Katika maisha thamini sana LEO kwakua JANA imepita na KESHO huijui. Kila ukiamka mshukuru Mungu na uombe uwe salama hujui dakika mbili mbeleni kutatokea nini”

By @middotz_ on Twitter and Instagram
Karibu tusome pamoja SIMULIZI za mahusiano na domestic violence

 
IMGJ_9771.jpg
 
SIMULIZI: SABABU NI KIFO CHAKO BABA!
(Kisa cha kweli cha kusisimua)
SEHEMU YA TATU (03)
MTUNZI: Man Middo Tz
WHATSAPP: +255 655 969 973

ILIPOISHIA.......... sasa wanakijiji wakisikia tu wanatoka kwenda kwake kuteketeza mali zake au kumtafuta mhusika. Katika matukio yote hayo ilitulazimu kuungana nao hata ikipigwa mbiu usiku wa manani. Sasa toka hapo ndio mateso, tabu na vipindi vichache vya furaha katika dunia hii vikaanza ndio maana nasema “SABABU NI KIFO CHAKO BABA……………..

(Leo tuanzie hapa katika kujua maisha yake halisi toka yupo tumboni kwa mama yake hadi kufikia kifo cha baba yake ili tuelewe na kufahamu anna au hesha ni binti wa aina gani)

SONGA NAYO…………………..Nirudi nyuma kidogo juu ya maisha yangu na mpaka kufikia kifo cha baba yangu, Mwaka 1998 mwezi wa 3 ndio nikazaliwa. Kwa mujibu wa baba na mama yangu, kipindi cha ujauzito wangu kulikua na matatizo tofauti tofauti. Kwanza kwa kawaida mimba ni miezi 9 lakini ujauzito wangu ulifika miezi 11 kasoro mwezi mmoja tu kufika mwaka. Mama yangu alikua amechoka sana katika kipindi hicho cha ujauzito wangu maana anasema tumbo lilikua kubwa sana, ila hospitali wakasema asubiri tu mtoto yupo salama atajifungua.

Mama amesema kipindi hicho cha ujauzito wangu alikuwa hatoki nje, mara nyingi alikua akijfungia tu ndani kwasababu mtoto (mimi) alikua akimsikia akiunguruma na kuguna tena kwa sauti.

Watu walikua wakisikia hiyo sauti hivyo akaamua asitoke nje ili habari zile zisienee kwasababu watu walianza kupita pale nyumbani kushuhudia na kusikia. Mimba ilivyofika miezi 11, siku moja alipita mzee mmoja mpita njia akaingia ndani kuomba maji akapewa maji lakini ghafla mzee akaacha maji huku akimtazama mama, inasemekana mzee huyo alionekana kuwa mwenye kushangazwa sana na ujauzito ule wa mama, akamwambia mama

“Wewe mama utakufa na hiyo mimba, hivi hujiulizi hiyo ni mimba gani hamuendi hata kuuliza kwa wataalamu”

Muda wote mama alikua amenyamaza, yule baba akagiza kiwembe akaletewa akamchanja chale mama yangu tumboni na mgongoni huku akimtamkia maneno ya kimila kama waganga wa kienyeji wanavyofanya. Yule babu akamwambia mama kuwa

“Utamzaa mtoto wa kike mnene sana ataitwa jina nyamlya”

Hili ni jina la kiukoo nilipewa kipindi nipo tumboni. Yule babu alivyomaliza akasema

“Naomba akaitwe mume wako”

Baba akaenda kuitwa kutoka shuleni kwasababu baba alikua ni mwalimu, alivyofika akamwambia

“Ndugu yangu muda wote umeshindwa kuliza kwa wataalamu, Ila kuna bibi yako humu tumboni analalamika (ile mingurumo) hamumuiti jina ndio maana amakuja kwako”

Wanasema baba alibaki kushangaa tu asijue kipi amwambie yule babu, kwa mujibu wa maelezo yao kipindi hicho wazazi wangu walishachoka hivyo yoyote atakaejitokeza baba na mama walimpokea.

Hivyo baba hakua na lakusema zaidi ya kumshukuru yule babu. Sasa baada ya yule babu kuondoka usiku huo huo mama akapata uchungu nikazaliwa na wazazi wangu wakanipa jina hilo hilo.

Nimezaliwa nikiwa mnene kama alivyosema yule babu, na mpaka leo kiasili ubonge haushi hata nipitie shida zai aina gani.**Nilipofikisha miezi minne nikaanza kuugua mwili mzima, niliugua mpaka nywele zikawa ninanyonyoka hadi zikaisha kichwani, nilibaki na madonda kichwani hakuna nywele hata moja.
Sasa ikawa kazi kwa wazazi kunitiibia, nikapelekwa hospitali lakini sikupona.

Haikuishia hapo wakanipeleka kwa mganga wa kienyeji lakini hali ndio kwanza inazidi kuwa mbaya. Wanasema ilifikia kipindi wakakata tamaa kabisa na kuzoea ile hali kuwa siponi, lakini siku moja kwenye gari wakakutana na mzee mmoja. Huyo mzee alikua anaona kila kitu kinachoendelea sijui nielezeje lakini ramli sio ramli, basi yule mzee kasema

“Jina mlilomuita linataka vitu vyake”
sijui ni vitu gani mpaka leo sivijui

“Lakini huyu bado ni mchanga itawezekanaje?” baba alimuliza yule mzee. “Itabidi akafanyiwe tambiko"

Kweli nikaenda kufanya tambiko kwajili yangu nikapewa maziwa na asali nikapona.

Baada ya kupona maisha yakaenda vizuri bila shida, Sasa maajabu ya Mungu huwezi kuamini hata kidogo, nilipofika darasa la 3 hadi la 4, nikaanza kuwa na nguvu za ajabu. Nikaweza kuona hata wachawi, wakati wengine hawamuoni mimi nilikua na uwezo wa kumuona.

Pia nikawa naota ndoto za maono na kuona vitu lakini katika hali moja ya kutisha sana. Katika hali hiyo unaweza ukashangaa lakini mfano nilikua naweza hata kusema mwalimu fulani atakufa au huu mtihani sitoufanya na kweli lazima inatokea hivyo.

Sasa katika hali hiyo wazazi na ndugu zangu wote wakanza kuniogopa, kila mtu akawa ananikwepa. Maajabu baadala yapungue ndio kwanza kama kuna moto umechochewa, sasa siku moja nikaamka asubuhi nimechanjwa na nimenyolewa nywele.

Aisee usiombe haya yakutokee, kuanzia siku hiyo matatizo yakaongezeka, sasa nikawa naota kila siku nipo kwenye mti nimefungwa kamba nabembea harafu chini kuna mashimo mawili makubwa sana. Sasa ndani ya mashimo hayo kulikua na moto mkali mnoo, sasa nikiwa juu ya ile kamba naanza kuzunguka kwa kasi sana kama kama tairi fulani, hiyo inafanyika ili kujua nitadondokea wapi kati ya yale mashimo.

Sasa usiku nikawa nateseka sana hadi napiga yowe mama wananisikia, au niote natembea juu ya mlima mrefu sana harafu kanjia kembamba sana.

***

Nilipofika darasa la 5 hii sasa ikazidisha roho ya uoga kwa watu dhidi yangu, nikaanza kupotea yani mfano tunakula au tumelala baadae wanafamilia watashtukia sipo maeneo yale hakuna atakae jua.

Katika hali hiyo naweza nisionekane hata siku nzima ingawa baadae nitarudishwa kimaajabu, sasa ikawa wamenzoea hivyo japo Baba ndio alijenga sana ukaribu na mimi kuwazidi ndugu wote.

Matatizo hayakuishia hapo, Sasa nikiwa hapo hapo darasa la tano nikaumwa majipu ambayo yakazagaa mwili mzima ikawa ni kulala tu wakawa wakinidunga sindano yanatoka shimo kubwa. Shimo hilo ilikua kidondo ambacho kinachimba kwa ndani unaweza usiamini lakini mpaka leo matako yangu ukiyaona utaelewa mwili ulijichimba hadi wakaacha kunitibu, ingawa Mungu akajaalia hatimae nikapona.

Katika kipindi chote hicho sikukata tama kwasababu kwanza nilikua mtoto, na hata nilipojiona watofauti na wenzangu baba yangu alinionyesha upendo hadi kujona nipo sawa tu na wezangu ndio maana hadi leo yanayonitokea kwasababu baba hayupo.

Mwaka wa 2009 nikiwa nimetoka katika mapito makubwa kutoka ujauzito wangu, kutoka upele mwili mzima hadi kunyonyoka nywele, kuota ndoto za ajabu kwenye mashimo ya moto, kupotea kimaajabu na kurudi pamoja na kutokwa na majibu hadi kutengeneza mashimo.

Hatimae yule mfariji wangu mkubwa, yule aliyekua na mapenzi ya dhati kwangu, yule aliye kuwa beneti na mimi zaidi ya wote katika matatizo yangu anauliwa kikatili.

Hapo nipo darasa la 6 nyumbani, siku ambayo nimeilezea episode mbili zilizopita ambapo baba yangu alichinjwa kinyama na majambazi, wakampiga sana mama na mimi pia.

Msiba huu ulibadilisha maisha yangu karibia yote, kwasababu kutokana na matatizo yaliyokua yametokea kwangu kama kuumwa baadhi ya ndugu na watu walionizunguka walinitenga lakini baba alikua analala na mimi ili tu nisijione watofauti.

Hiyo ni kwasababu mama yangu hakuwa bize kabisa na mimi kama ilivyokua kwa watoto wake wengine, sijui lakini nadhani aliona huenda mimi ni kama mkosi kwao. Toka kifo cha baba ikawa sababu ya haya yote yaliyonitokea, mpaka leo……………………….ITAENDELEA.

USIKOSE KUJUA KIPI KILIMTOKEA ANNA BAADA YA KIFO CHA BABA YAKE?

Simulizi hii ina mafunzo mengi sana, huko mbele kuna vipindi vya furaha na burudani. Usikose kujua kipindi chake cha mahusiano yalivyonoga.

Usipange kukosa episodes zijazo follow page zangu fb na Instagram.

USIKOSE EPISODE INAYOFUATA.

NUKUU “Wanasemaga maisha ni zawadi, Na mimi nasema kuamka kila siku ni fursa ya kuishi. Hivyo kama unamka ukiwa mzima, unaenda kulala bila tatizo lolote mshukuru Mungu kwani huko ndio kubarikiwa kwenyewe. Muombe MUNGU msamaha zaidi ya muombavyo akujalie kazi au kupata kitu fulani kwasababu tunakosea kwa kujua au kwa kutokujua. Jifunze kuishi bila kumbagua mwingine haijalishi anaonekanaje, haijalishi anapitia hali gani kwasabu hiyo yote ni mipango ya Mungu”
 
SIMULIZI: SABABU NI KIFO CHAKO BABA! (Kisa cha kweli cha kusisimua)
SEHEMU YA NNE (04)
MTUNZI: Man Middo Tz
WHATSAPP +255 655 969 973

Baada ya kuona maisha ya toka nazaliwa hadi kifo cha baba leo tunaendelea maisha ya baada ya kifo cha baba kama jina la stori linavyojieleza. Sasa baada ya kifo na maziko ya baba ambacho kilitokea katika kipindi cha likizo ndogo ya wiki.

Hatimae tukafungua shule, ilitulazimu turudi shule ingawa bado tunaugulia machungu moyoni. Walimu walionyesha mapenzi makubwa sana kwetu, hii ni kwasababu baba yangu mzee Nelson Magoma alikua ni mwalimu.

Na sababu kubwa ya kifo chake ni kuwa Baba alikchukua mkopo kwajili ya ujenzi sikujua ni shilingi ngap kwa wakati huo lakini kwa hela ya kujengea itakua kubwa kidogo. Pia Baba alikua mhasibu kanisani (Muweka hazina), mhasibu wa ukoo (Muweka hazina wa ukoo) na pia mhasibu wa kikundi cha walimu shuleni hivyo kwa wakati huo alikua na makusanyo ya pesa zote na wale majambazi walizichukua zote pamoja na kuutoa uhai wake (R.I.P BABA)

Mama yangu lile tukio lilimuathiri kidogo hivyo hakua ametulia, karibia familia nzima tuliogopa kuona hata gari. Mama akawa kama sio yeye lakini baadae akatulia, sasa baada ya kutulia akapewa utaratibu wa kufuatilia mirathi.

Ukoo wakafanya kikao na kumteua baba mkubwa kuwa msimamizi wa mirathi, huyu baba mkubwa kwa kipindi hicho alikua ni daktari kabla hajastaafu.Katika watu walioteseka sana kutokana na kifo cha baba ni mimi Anna Nelson Magoma (au Hesha kwa jina lingine), kwani sikuweza hata kuzoea ile hali ya kutokumuona baba. Kwa kweli nilitia huruma, machozi hayakukauka mashavuni mwangu, Tukio lile likawa kama movie kichwani mwangu.

Ukatili ule ukawa haupotei kichwani mwangu hata usiku usingizi ulikua wa tabu. Maisha hayo yakanitesa mnoo, hata shule sikuona umuhumu wake na hii ni kwasababu yule aliyekua ananiambia

“una IQ kubwa sana mwanangu utakuja kuwa mchungaji mkubwa baadae” hayupo tena.

Ndugu zangu wengine walianza kuzoea hali ya kuishi bila baba, mimi nilijitenga mara nyingi nilikua nakaa peka yangu. Kutokana na hali hiyo nikaja kuchukuliwa na mwalimu mmoja anaitwa Madam Tedy hapo ni darasa la 6 hadi la 7.

Sasa hapo ndio nikaanza kusoma ingawa mimi sikuona kama naelewa chochote pamoja na kwamba marehemu baba na baadhi ya walimu walikua wakiniambia nina uwezo mkubwa kiakili.

***

Maisha ya familia yangu kiujumla: Tumezaliwa 9 wakike 6 na wakiume 3, lakini katika hao 9 watatu wametangulia mbele za haki wakiwa ni wanaume wawili na mwanamke mmoja.

Hivyo tumebaki 6, wakike wa tano na wakiume mmoja ambae ndio wa mwisho. Katika kuzaliwa mimi ni wa 5 lakini pia hata wazazi wangu wote kila mmoja ni wa 5 kuzaliwa katika familia zao.

Dada yangu wa kwanza Aneth alijiunga kidato cha kwanza mwaka 2004 wakati huo mimi nipo darasa la kwanza, lakini alisoma miezi mitatu tu baada kurudishwa nyumbani alivyogundulika kuwa ni mjamzito.

Aliyempa ujauzito alikua ni mwanafunzi pia hivyo akaomba aendelee na masomo ili akimaliza amuoe dada, Alikubaliwa wakati huo dada yupo nyumbani.

Mahusiano baina ya familia yetu na ya kwao yalikua ni makubwa sana, dada yangu akaja kujifungua maisha ya kulea yakaendelea lakini maajabu akiwa katika harakati za kumsubiri mwenzake ahitimu, dada akaanzisha mahusino na kijana mwingine pale kijijini ambae alikua ni mwanafunzi pia.

Upendo wote wa yule kijana wa kwanza ambae ndio mzazi mwenzake ukayeyuka, baadae wazazi wakagundua. Dada akapingwa vikali na wazazi wangu kutokana na tabia ile ya kudhalilisha.

“Hivi Aneth si unamchumba wako wewe na tulikubaliana akihitimu akuoe huyu mwingine wa nini na kwanini unaonyesha tabia mbaya tena ya kudhalilisha?”

Dada hakua mtu wa kujibu chochote aliahidi tu kuacha lakini hakucha, basi baadae dada alivyoona anagasiwa akamua kutoroshwa na huyo mpenzi wake. Huyo kijana alikua amebakiza wiki mbili tu kabla ya mtihani wa mwisho, hivyo elimu yake ikaishia hapo.

Dada na huyo kijana wakaenda kuanzisha maisha mengine huko bila sisi kujua huku akiacha kile kichanga nyumbani. Mpaka leo wanaishi kama mke na mume lakini misukosuko ya kimaisha na hali duni katika familia yupo tu kama mama wa familia hana shughuli yoyote.

Dada yangu wa pili anaitwa Julieth, huyu nae akiwa darasa la saba tu akapata ujauzito, akasimamishwa masomo kutokana na tatizo hilo. Dada Juli sio tu aliwaumiza wazazi lakini pia ilikua ni pigo kwao kwasababu Baba yangu aliamini urithi mzuri ni kutupatia Elimu, pia ukizingatia baba alikua ni mwalimu.

Hivyo baba ilimuumiza sana kuona binti yake wa pili anashika ujauzito tena akiwa darasa la saba.Dada Juli baadae alikuja kupata mchumba mwingine akamuoa hadi leo wanaishi wote, kwani mtoto wake wa kwanza haikujulikana mpaka leo kuwa alizaa na nani. Kwahiyo wakati kifo cha baba kinatokea, tulikua tumebaki hapo nyumbani wabinti wa tatu na kijana mmoja ambae hata shule ilikua bado hajaanza.

Hivyo ule uchungu wa baba siku ile mchana ambayo usiku atakufa akitusia tusome sana, ni uchungu ulionogeshwa na zile mimba za dada zangu wawili wa kwanza.

***

Sasa tuendelee maisha baada ya kifo cha baba, basi baadae nilisoma darasa la saba huku nikiona utofauti mkubwa sana wa maisha bila uwepo wa baba. Hiyo ni kwasababu kila nikiamka na kirudi nyumbani nikisalimia hakuna aliyekua akinichangamkia tena zaidi ya bibi yangu.

Ndugu zangu wote akiwemo mama hawakua bize na mimi, ni kama vile sikuepo tu nyumbani au kama vile nilikua mtoto wa kufikia sijui mpaka leo sababu ni nini.Bibi yangu ambae ndio akawa mfariji wangu, muda mwingi alikua akinitazama sana kama mtu anaekuonea huruma. Bibi aliathiriwa mno na msongo wa mawazo, hali ambayo ilimletea presha na kudhofisha afya yake.

Afya kudhoofu ilichangiwa sana na bibi kukataa kula chochote akidai haoni thamani ya maisha bila uwepo wa mwanae (baba) Sasa kutokana na kuumwa umwa kila mara mwaka na hali ya kutokula baada ya mwaka mmoja wa kifo cha baba nikampoteza nae bibi yangu kipenzi………….ITAENDELEA.

USIKOSE HUKO MBELE INANOGA ZAIDI.

NUKUU “Wanasema Mungu anampa mja wake matatizo anayoweza kuyatatua lakini ni wazi kuna muda ukiyatazama matatizo yako, ukitazama mitihani yako unahisi kabisa kama haustahili na hauoni njia ya kuyatatua.

Mtazame Anna amekumbwa na mitihani toka yupo tumboni kwa mama, anazaliwa toka kichanga anakua kimitihani, watu wanamtenga wakiwemo wa karibu yake.

Mungu anaona haustahili kutengwa Baba yake anakua karibu yake lakini anaondoka kinyama katika uso wa dunia. Mungu anambakishia bibi masikini Bibi nae anafariki tena akiwa binti mdogo tu.

NOTE: Kama unakaa na familia yako zaidi ya dakika 30 mnaongea mnacheka basi mshukuru Mungu sana kwasababu tayari wewe ni tajiri, kuna mwenzako anatafuta dakika mbili tu akae watete jambo na familia lakini haiwezekani tena”

Nifollow Twitter @manmiddo
Instagram @middotz_
 
SIMULIZI: SABABU NI KIFO CHAKO BABA! (Kisa cha kweli cha kusisimua)
SEHEMU YA TANO (05)
MTUNZI: Man Middo Tz
WHATSAPP +255 655 969 973

ILIPOISHIA……………....Bibi yangu ambae ndio akawa mfariji wangu, muda mwingi alikua akinitazama sana kama mtu anaekuonea huruma. Bibi aliathiriwa mno na msongo wa mawazo, hali ambayo ilimletea presha na kudhofisha afya yake.

Afya kudhoofu ilichangiwa sana na bibi kukataa kula chochote akidai haoni thamani ya maisha bila uwepo wa mwanae (baba) Sasa kutokana na kuumwa umwa kila mara mwaka na hali ya kutokula baada ya mwaka mmoja wa kifo cha baba nikampoteza nae bibi yangu kipenzi…………SONGANAYO

Kumpoteza bibi sio tu ilikua pigo kwangu, ila zaidi ya hapo nilijiona sina thamani kabisa katika dunia, kibaya zaidi bibi amekufa nikiwa namtazama kwa macho yangu. Kifo chake hakikufanana na cha baba lakini nikakifananisha kwani wote nimewashuhudia wakikata roho.

Baada ya kumpumzisha bibi sasa nikaanza ukurasa mpya wa kuishi bila baba wala bibi, niliwaza sana nitaishi maisha ya aina gani kwa wakati huo sikupata jibu sahihi. Katika kipindi chote hicho nilikua nikiishi kule kwa madam Tedy.

**
Dada yangu ninaemfuata alijaaliwa uzuri wa kipekee, alikua mwenye mvuto sana. Anaitwa Sankah, Wakati huo yeye alikua kidato cha kwanza, Mimi nimemaliza la saba nasubiria matotokeo.

Sasa katika hali ile ya uzuri si jambo la kushangaa kwa yeye kutongozwa na wanaume wengi na kweli ikawa hivyo, na hatimae dada Sankah akazama katika penzi zito na kijana ambae nilikua nasoma nae primary.

Nilichukizwa sana na kile kitendo, Hata mama yangu hakupendezwa na hicho kitendo ikabidi akanywe aachane na huyo kijana.

“Mama mimi sitaki kuendelea kusoma naomba tu uniruhusu niolewe” Dada akimpa taarifa hiyo mama.

“Unasemaje wewe mpumbavu, Hivi nyie watoto mmerogwa na nani! Yani wote hamtaki shule mnawaza ndoa tu! Dada zako hivyo na wewe hivyo hivyo, aisee hapana ni lazima usome kwanza wewe umechukua jina la bibi yangu, bibi yangu hakua hivyo. Kwahiyo naomba utambue kwasasa hakuna nafasi ya kuolewa ila ya kusoma tu, sawa!”

“Lakini mimi mama sitaki shule mnanilazimisha”

“Eeeh! Sitaki kusikia tena na ole wako nisikie huendi au hujaenda shule uone”

Dada alichukia sana mama kumwambia aende shule, kwa mawazo yake aliona analazimishwa na kwamba shule hakuna faida yoyote.

Sasa maajabu dada baaada ya kuona mama ameweka msimamo akaamua kubeba ujauzito kabisa! Mungu wangu! Aisee mama alionekana kama amechanganyikiwa.

Mama hakupendezwa na kile kitendo kwasababu ilikua ni binti yake wa tatu anabeba mimba tena akiwa shule, chozi la mama lilidondoka kwa uchungu huku akimwambia dada kuwa

“Sankah unataka maisha gani mwanangu, kwanini umeshindwa kujifunza kwa dada zako unaamua kufuata walichokifanya. Mwanangu umesahau hata usia wa baba yako unaamua kubeba mimba ili tu uolewe! Hivi mnaona ndoa ni mchezo tu eeh! Haya amueni mnavyoamua”

Dada yangu akawa ameacha shule kwa njia kama hiyo, katika kipindi hicho kesi ya baba bado ilikua inaendelea mahakamani, pia masuala ya kufuatilia mirathi yaliendelea na mama ndio alikua anafuatilia kila kitu.

***
Katika hali isiyokua ya kawaida, hali iliyoniumiza na kunitoa chozi hadi kumkumbuka baba yangu zaidi ya mara 20 ni pale mama alipoanzisha mahusiano na mwanaume mwingine na kumuweka hadharani.

Hapo nilitoneswa kidonda kilichokua kinaelekea kupona, kilichokua kinaniumiza ni kuwa kesi ya baba bado ilikua haijaisha pia bado hata mirathi haijapatikana.

Pia niliamini kwa mwaka mmoja tu haukutosha kwa mama kuwa na mwanaume mwingine tena ukizingatia mume wake aliuawa kikatili mbele ya macho yake.

Nilijua anatafuta faraja, lakini sikuamini kabisa kama ile itakua faraja kwake kutokana na kifo cha baba.

Lakini pia, niliona watoto 9 walitosha kabisa kwa mama kutambua kuwa yeye ni mtu mzima hastahili tena kuishi na mwanaume ndani ya nyumba ya mume wake aliyekufa kikatili.

Sasa akawa namleta hata mchana, yule mbaba akawa analeta hadi baadhi ya mahitaji, sasa hapo ikanibidi nianze kuiba picha za baba zote na kuzihamishia kwenye albam moja lengo niwe na namtazama baba lakini pia sikutaka yule mwanaume azione hata kidogo.

Sasa mimi na dada tukaanza kupinga ujio wa yule mwanaume ili asije pale.

“Hivi Hesha (Ana) huyu mwanaume anakuja kufanyaje hapa, si wakutaniane tu huko sisi hatuhitaji tena mlezi hapa baba alikua anatosha ashaondoka mbele ya haki basi tutaishi hivyo hivyo”

“Hata mimi sioni hata robo ya faida ya yeye kuja hapa zaidi ya kutukumbusha tu machungu ya baba yangu”

Sasa chakushangaza mimi na dada wote hatukumpenda huyo mwanaume lakini mama akanichukia mimi wazi wazi.

Tena kipindi hicho kulifanyika sherehe za darasa la saba, mimi sikufanyiwa kutokana na mama alionyesha chuki dhidi yangu.

Hata wakati natoka kule kwa madam nilipokua naishi, kufika nyumbani niliwakuta watu wote wanaishi kwa furaha isipokua mimi ambae sikua na hata wa kumuuliza swali.

Sijui kwanini karibu ndugu zangu wote walinichukia, yani hakuna hata aliyenipenda dada zangu, wadogo wangu na baba wadogo wakafikia hatu ya kusema

“Yani wewe mtoto siku ukikua utakuja kuleta shida”

Maneno yao ya kashfa sikujali kwasababu nilishakubali misukosuko ni sehemu ya maisha yangu, hivyo sikujibizana wala kuhoji, kimya ndio ikawa jibu langu.

Sasa maisha baada ya kumaliza shule na maisha ya kuishi pale nyumbani yalikua ni magumu mno kwasababu tangu baba afariki ikawa hakuna nguo mpya, hakuna kiatu, hakuna atakaenitoa kwenda mjini lakini wenzangu wanaenda.

Kiufupi nilikua mpweke sana dada yangu alikua anaukaribu na mdodgo wangu, yani walikua wanashea kitu chochote kuulizana au kusaidiana kitu.

Chuki dhidi yangu sasa familia nzima ikawa waziwazi kwangu, hadi kwenye chakula nikawa nanyimwa shart wao wale kwanza ndio mimi nile.

Yani mfano wao wakiwa hawapo siruhusiwi kula mpaka warudi, nikiwajibu chochote tu ilikua ni kupokea kipigo.

Kiufupi sikua na utofauti na mtoto yatima, nyumbani nikapaona pachungu sana.

Machozi yanatoka mpaka yanakauka najiuliza nimemkosea nini Mungu sipati jibu, sasa dada zangu wakawa na tabia mbaya za kuingiza wanaume ndani kabisa, yani nikiwa ndani wananifukuza ili waingize mabwana zao.

Kitendo hicho kiliniumiza sana kwasababu Mama nae ana mume mwingine na ndugu zangu nao wanaingiza mabwana ndani hakika nikamkumbuka baba sana.

Siku zikasogea nakumbuka ilipofika sikukuu ya chrismass mwaka 2010, hii siku ni miongoni mwa siku ambazo sizisahau, kwani nilishangaa ndugu zangu wote wana nguo mpya , wakapewa na hela za soda mimi peke yangu sina hata kitu.

Kwa umri wangu huo wa miaka 13 vitu kama nguo siku za sikukuu ni muhimu na lazima upende, sasa hebu fikiria kwa umri huo unaishi na mama yako mzazi harafu unaona ndugu zako wote wana nguo mpya wewe unamanguo tena mengine yamechanika.

Siku hiyo ya sikuu nilijuta sana, ndugu msomaji hebu fikiria kwa msichana ambae unaanza kupevuka harafu hata nguo za ndani huna hebu fikiria ni aina gani ya maisha nilikua nayaishi!!!.

Basi siku hiyo nilibaki tu nyumbani na kuimba kwaya huku wenzangu wakienda kutembea.

Siku mbili baada ya sikukuu ya chrismass matokeo ya darasa la saba yakatoka, nikawa nimefaulu lakini maajabu ikawa sioni dalili zozote za kuandaliwa vifaa.

Basi siku moja akaja mama mmoja hivi alikua ni mratibu Elimu, huyu mratibu alikuaga rafiki yake na baba enzi za uhai wake.

Kitendo cha kumuona tu nikakumbuka mbali sana, ni kama nilitonesa kidonda kwani nikakumbuka jinsi tulivyokua tunaenda benki yeye na baba, nikakumbuka akiwa na baba lazima apitie dukani kunichagulia nguo.

Siku moja waliwahi kubishana na baba akidai kuwa mimi ni genius na kiongozi mkubwa hapo baadae na baba akabisha akimwambia mwanangu ni nabii na mtumishi wa Mungu hapo baadae.

Sasa chozi likanza kudondoka akanibeba akaniuliza (Huyu mama natamani hata asingekuja siku ile)

“Mama mchungaji unashida gani mbona umepauka hivi?” nikaanza kumuelezea haswa juu ya shuele akasema

“Ngoja nitamshawishi mama yako twende wote kwangu ukasomee huko” (Ningejua nisingekubali kwenda kwake)…………....ITAENDELEA.

Kwanini Anasema Angejua Asingeenda Kwake? Usikose Kifuatacho Utaona Kile Ambacho Unasikia Tu.

NUKUU “Kwa bahati mbaya hakuna anayeona MACHOZI yako, HUZUNI yako, MAUMIVU yako lakini kila mtu katika familia anajua wewe ni mkosefu haustahili amani, haustahili kuvaa, hautahili kula vizuri.

Haya ndio maisha ya Hesha (ANNA) anaishi maisha kama vile yupo jela, hebu tazama umri alionao na matatizo anayopata. Kila hatua apigayo ni matatizo tu.

Tunatakiwa kumshukuru Mungu pale unapoishi kwa amani, unacheka bila shida yoyote, Jifunze kumshukuru Mungu kwa kila neema aliyokupatia”

Man Middo tz
On Twitter @manmiddo
 
SIMULIZI: SABABU NI KIFO CHAKO BABA! (Kisa cha kweli cha kusisimua)
SEHEMU YA SITA (06)
MTUNZI: Man Middo Tz
WHATSAPP: +255 655 969 973

TULIPOISHIA…………. Siku moja waliwahi kubishana na baba akidai kuwa mimi ni genius na kiongozi mkubwa hapo baadae na baba akabisha akimwambia mwanangu ni nabii na mtumishi wa Mungu hapo baadae.

Sasa chozi likanza kudondoka akanibeba akaniuliza (Huyu mama natamani hata asingekuja siku ile)

“Mama mchungaji unashida gani mbona umepauka hivi?” nikaanza kumuelezea haswa juu ya shuele akasema

“Ngoja nitamshawishi mama yako twende wote kwangu ukasomee huko” (Ningejua nisingekubali kwenda kwake)…………....SONGANAYO.

“Mama Aneth pole kwanza na matatizo maana toka msiba hatujaonana tena, mimi leo nimekuja tu kuwasalimia vipi wanao wote wanaendeleaje?”

“Wanaendelea vizuri Mungu anasaidia kama unavyowaona”

“Ni kweli, Anna amefaulu sasa nilikua na ombi kutokana na majukumu yako hapa naomba nikaishi nae kuna shule kule ya karibu nitamtafutia”

“Uuuh! Kwa kweli utakua umesaidia sana kwenda nae”

Mama Hakuonyesha hata dalili ya kumia, machoni mwake alionyesha kufurahi kwasababu ni kama anapokelewa mzigo mzito kwake.

Basi nikaenda kuishi kwa mratibu, alikua anaishi mjini. Nilipofika nikakuta familia kubwa tu, nikaanza kuzoea mazingira ya pale, kulikua na chumba cha wasichana na ambako mwanzo ndio nilikua nalala uko.

Nikajitahidi kuyazoea mazingira yale lakini ikashindikana wao walikua wakiongea Kihaya tu muda wote. Mwenyeji wangu alikua ni mratibu ambae asubuhi alikua anaenda kazini hivyo nikawa nashinda ndani tu.

Jinsi mwenyewe nilivyokua hata nguo nzuri ya kubadilisha sikua nayo, hapo nikahisi hata wale ndugu zake kuongea kihaya huenda wananisema vibaya.Nilikaa kama siku nne na upweke tu ilivyofika siku ya tano Mratibu akaniletea nguo mbili mpya sketi na tisheti moja. Mmh sasa ilivyofika usiku akaniita akaniambia

“Hesha kuanzia leo utakua unalala na mimi chumbani kwangu”

Huyu mratibu hakua na mume, basi akaleta juice tukanywa nikafurahi sana kwa nafasi aliyonipa kwasababu nilikua tu mpweke muda mwingi. Basi baada ya hapo tukaenda chumbani tukajiandaa nikapanda kitandani na yeye akapanda kitandani, kawaida yangu nilishajizoesha lazima nisali kila ninapopanda kitandani.

Sasa nilipomaliza kusali nikamkuta yule mama kakaa tu kitandani akanimbia

“Naomba unikune mwili mzima nawashwa ila usije ukamwambia mtu yoyote”

Mmh! Sikushangaa kumkuna ila kule kusema nisimwambie mtu yoyote nikajikuta nimezubaa, na wakati huo muda wakulala hivyo hakua na nguo alikua uchi.

Basi akalala kifudifudi akawa ananielekeza nimkune wapi mgongoni mara kwenye mbavu yani sehemu tofauti za mwili wake, Kwa kweli nafanya hivyo kwa woga ila nikafanya hivyo hivyo.

Sasa baadae akajigeuza akalala chali kisha akaniambia

“Funga mlango halafu uzime na hiyo taa”

Kweli nikaenda kufanya hivyo, sasa nilivyorudi kitandani nikaendelea kumkuna hivyo hivyo ingawa sikuona kama anawashwa, halafu jinsi ninavyomkuna ni kama mtu anafurahia hivi sijui nielezeeje ila alikua anapandwa na msisimko fulani hivi. Mmh! Sasa baadae mwenzangu alizidi kunishangaza alivyoniambia kuwa

“Nivue chupi”

Uuwiii! Hapo nilihisi shoti mwilini kwanza anaongea kwa sauti ya kimahaba hivi, aisee hapo nikakataa nikamwambia hapana akasema kuwa

“Kama unakataa kesho asubuhi naenda kukuripoti kwenu kuwa umeniibia pesa”

Daah! Hapo nikatafakari nyumbani hela ikipotea nachapwa hata kama nikiwa sipo nambiwa mimi kuwa ndio nimeiba sembuse leo akienda kusema. Pia walikua wanamuamini sana na ukizingatia nilikua sijamaliza hata wiki pale.

Sasa ikabidi nikubali mziki nikaanza kumvua chupi kisha nikaanza kumkuna taratibu mpaka sehemu za siri mmh! Wewe mama huko uliko Mungu anakuona! Basi baadae akaniambia

“Ninyonye maziwa”

Hapo nilitishika sana lakini nadhani hata akili ilikua bado changa nilikua nafikiria kugoma lakini nikawaza akienda kunisingizia nyumbani kwamba nimeiba sitakua salama halafu mimi wasingeniamini nikisema kuwa ameniambia nimfanye vile.

Kama ujuavyo kiongozi kama yule tena msomi ilikua ngumu kwa mimi kusema na watu wakaniamini. Sasa nikaendelea na kazi yangu nikamnyonya maziwa yake huku akiniambia niendelee kumkuna tuseme kumtomasa maana ndio ilikua ni nia yake.

Tukalala ila usingizi ulichelewa kuja kwa siku ile, ilipofika asubuhi akaniamsha tena akaniamuru nifanye kama usiku lakini safari hii akaniambia kuwa

“Niweke vidole ukeni”

Aliongea huku anagugumia sijui ilikua ni raha au ni nini! Siamini kama nilifanya vile yani nadhani sikua mimi kabisa.

Sasa alipoona ameridhika akajiandaa akaenda kazini, aliporudi tukilala usiku kazi ikawa hiyo hiyo kila siku, maisha sasa yakawa ya aina hiyo mwezi ukakatika nikiwa pale kwa mratibu.

Sasa ndugu zake wote hakuna aliyekua anajua kuwa mimi usiku namfanyia vile (namsaga) yule mama, Sasa siku hiyo akanimabia “Ninyonye ukeni”……………..ITAENDELEA.

JE UNAFIKIRI HESHA (Anna) ATAFANYA HIVYO TENA?

AU SAFARI HII ATAGOMA! JE ATAENDA SHULE AU ATAENDELEA KUTUMIKA VILE?

UNAFIKIRI NDUGU WA YULE MRATIBU WAKIJUA ITAKUAJE? USIKOSE KUJUA YOTE HAYO.

NUKUU “Kama wewe ni mzazi basi hutakiwi kumuamini mtu yoyote hata kama anacheo gani, yeyote anaesema nataka kuishi na mwanao hutakiwi kumpa 100% kuwa ni mwema kwako.

Haya kama uonavyo katika episode hii mratibu Elimu anamfanyisha binti wa watu uchafu wa namna hiyo je wale wengine ambao hawajasoma.

Usimwamini mtu ambaye bado ni kijana na bado hana mke au mume najua unasema ndugu zako hawapo hivyo au wewe haupo hivyo ila wanasema kinga ni bora kuliko tiba hivyo chukua tahadhari”

TUENDAKO NDIO HATARI ZAIDI HII NI MOJA YA SIMULIZI BORA ITAKAYOKUFUNZA MENGI USIYOYAJUA AU UNAYOSIKIA TU.

Nifollow Twitter @middotz_
 
SIMULIZI: SABABU NI KIFO CHAKO BABA! (Kisa cha kweli cha kusisimua)
SEHEMU YA SABA (07)
MTUNZI: Man Middo tz
WHATSAPP +255 655 969 973



Mmh! Mungu wangu weeh! Ule uchafu sitokuja niusahau kabisa najiuliza kwanini yule mama alishindwa kutafuta bwana wakafanya watakavyo kuliko kule kusagana!?

Sasa ikafikia hatua akanivalisha hadi dildo nimfanye! Mungu wangu kama unasoma hapa usije ukajaribu haya, maana siamini hadi leo kama nina huruma mimi.

****
Sasa muda huo wenzangu kidato cha kwanza washanza shule kama mwezi na nusu mimi sijui hata nitaendaje nipo tu pale nafanyishwa kazi za kingono.

Kila nilipomkumbusha kuhusu shule yule mama alisingizia tu kuwa ngoja ajipange, nikawa nawaza nakuzidi kumgeukia mama kumtupia lawama kuwa huenda walipanga nije mjini ili nisisome na huyu huenda alivyoambiwa hivyo alikubali kwasababu ya hii kazi yake.

Siku hiyo mratibu hayupo pale nyumbani nikaomba simu ili nimsalimie mama nikapewa alivyopokea nikamwambia

“Shikamoo mama”

“Marahaba unaendeleaje na shule, na masomo unaelewa” hapo nikashangaa sana nikamwambia

“Yani mama umenileta mjini ili tu nisisome, kwanini mama angu unanifanyia hivi toka nije huku sijui kama kuna shule au laa” mama akashangaa sana kaniambia kuwa

“Khee! Inamanaa huendi shule! Mimi mratibu ameniambia unaenda shule tangu shule zifunguliwe hebu ngoja kwanza nimpigie”

Nikamuacha ampigie kwanza nilichoka na yale maisha ya kutumikishwa kingono, ila sikumwambia mama kama ananifanyia hivyo yule mama.

Baadae mama kampigia yule mratibu wakagombezana huko lakini baadae wakaelewana mratibu akamwambia mama kuwa

“Nitatafuta shule lakini tulipie ada pamoja” mama akamwambia kuwa

“Siku zote unanidanganya kuwa mtoto anasoma kwahiyo kama haumpeleki mrudishe ili nijue hela yote natoa mimi”

Sasa ikawa ni wakati mgumu sana kwa mratibu, kunikosa hataki na kunisomesha anaona mtihani kwasababu pia ingemlazimu nikakae shule.

Hivyo hakutaka kwasababu tayari nilishakua fundi wake kitandani, kumbuka yote hayo nilikua na miaka 13 tu.

Sasa siku moja nikakumbuka kuwa wakati baba yupo hai kuna pesa aliwahi kumkopesha mratibu nikamwambia kuwa

“Naomba ile pesa anayokudai baba nipe niende shule”

Kipindi hicho nilikua nimeanza kubadilika kwanza nilimuona tu kama demu wangu, hivyo sikua namuogopa sana.

Basi alivyoona sipo sirias na mama amechachamaa ananitaka, nikashangaa siku hiyo usiku akanihamisha pale kwake kisiri siri hata ndugu zake hawajui akanipeleka sehemu nyingine sipajui.

Aisee kufika ilikua bonge la nyumba tena yenye uzio na kila kitu ndani, sasa hapo akawa anakuja pale mara kwa mara nimfanyie huduma yake.

Kwa kweli sikua na jinsi nilifanya nikimtimizia anaondoka, lakini nilianza kuingiwa na hisia na kile kitendo.

Sasa kumbe mama kamwambia kuwa nimetoroka pale kwake kwasababu eti sitaki kusoma.

Siku moja alivyokuja akaniachia sh 22,000 kaniambia kuwa

“Kuna mtu ataleta mkaa hapa, akija mpe hii hela kisha umwambie auingize ndani”

“Sawa” nikaitikia.

Kweli muda wa saa 3 asubuhi kuna kijana akaja na baiskeli akiwa na mkaa, sasa kufika nikawa namfahamu ni kijana wa kijijini kwetu. Akanishangaa sana akaniambia

“Wewe upo hapa halafu nyumbani nimeambiwa unatafutwa umetoroka kwasababu eti hutaki kusoma”

“Kwanza usipige simu popote kama umeniona”

Niliona akipiga simu italeta shida kubwa kwa mratibu, nae hakua na simu nikashukuru Mungu.

Kwa kweli kuja kwa yule kijana ikawa kama neema kwangu kwasababu moyoni niljisemea

“Hata iweje leo huyu naondoka nae”

Sasa nikamwambia kuwa

“Ni kweli nyumbani natafutwa, ila naomba kwanza ukubali kunipeleka nyumbani ila chonde chonde usimwambie mratibu kuwa wewe ndio umenitoa pale. Akikuliza wewe sema tu ulileta mkaa kisha ukaondoka”

Akakubali nikashukuru Mungu sana, basi nikaingia ndani kujiandaa kufika nikakuta kuna kimkoba cha mratibu nikakichukua kukikagua ndani kuna nini, aisee kuangalia nakutana na hela nyingi elfu kumi kumi sikuhesabu nikachukua zote nguo zangu nikaweka kwenye kibegi changu cha Bob marley

(Enzi hizo heshima kubwa kuwa kibegi kama hicho)

Tukatoka pale akanipandisha kwenye ile baikeli, palikua ni mbali hadi kufika Musoma mjini takribani kilemeta 5 au zaidi.

Sasa kufika mjini yule kijana kaniambia

“Sasa hapa itabidi nikupandishe gari maana tukienda wote hivi watu wataona na watasema mimi ndio nimekuleta”

“Dah! Umeongea jambo la maana sana, Asanteh msaada huo”

Akanipandisha gari akanilipia nauli nikaondoka hadi nyumbani, nilipofika walishangaa sana kila mmoja akuliza nilikua wapi.

Safari hii kila mmoja alinichangamkia kidogo nadhani ni kwasababu ya ile dhana kuwa damu ni nzito kuliko maji.

Basi Baadae nikamhadithia mama kila kitu ila mambo ya kusagana sikumwambia kwasababu ningemwambia mama asingenichulia kawaida, na hata mahitaji asingenipa kama ipasavyo.

Lakini pia kwakua najua mama ni mtu wa kubadilika sikumuonyesha zile pesa nilizotoka nazo kule kwa mratibu nikazificha mwenyewe.

Maisha mapya yakaendelea nikamkumbusha mama kuhusu shule, akaenda kuniombea shule ya kata ambayo nilichaguliwa, Muda huo ni mwezi wa tatu toka shule zifunguliwe.

Shule ilikua mbali, ni kijiji cha pili kutoka kijijini kwetu, nikashukuru Mungu afadhali naweza kutimiza ndoto zangu.

Sasa siku ya kwenda kununua mahitaji ya shule mama akampa yule mume wake aisee sikua na amani kabisa. Yani siku hiyo nilimuwaza baba mnoo, yule mwanaume hakuweza kutimiza hata robo yale aliyokua akinifanyia baba.

Kifua changu kilikua kizito kwa kumchukia hata yeye hakuonyesha upendo alinionyesha wazi anachukia na anafanya vile kwa mapenzi yake tu kwa mama basi.

Sasa tulipofika mjini nashangaa ananinunulia vitu ambavyo kama napewa msaada, ninavyotaka hataki, sikua hata na nguo za ndani namuomba eti anakataa.

Sketi ya shule akaninulia ndefu mpaka naikanyaga na hivyo nilikua kibonge nilionekana kituko balaa.

Madaftari akanunua atakayo yeye, baadae nikamuomba aninunulie begi la nguo nashangaa ananisonya huku ananisema sema vibaya, halafu pesa sio yake pesa ni ya baba yangu mzazi maana kipindi hicho mama ashanza kupokea mirathi hivyo pesa alitoa kwenye akaunti.

Basi tukawa hatusemeshani hadi tunarudi nyumbani, kwanza sikumheshimu kama baba yangu, sasa siku ya kwenda shule akapewa yeye anipeleke aisee nikaumia mnoo………….ITAENDELEA.

JE UNAJUA KITAKCHOMTOKEA HUKO SHULE?

JE UNAJUA ATAENDA KUKAA BWENI AU ATAPANGISHA CHUMBA?

JE ATAISHI KWA AMANI, JE YULE MRATIBU HATAMFUATILIA TENA?

USIKOSE KUJUANI KIPI KILIMTOKEA.

NUKUU “Katika maisha mtegemee MUNGU kwa kila jambo na ukifanya hivyo utaona miujiza yake, usichoke ukakufuru Mungu kwasababu ya matatizo yanayokuandama amini kuwa ipo siku yatakwisha na utakua huru.

Kama unasoma hapa na maisha yako yanafanana na ya Anna basi amini ipo siku yatakwisha kama unamtegemea Mungu pekee”

Usingoje hadi nipost jipatie mwendelezo muda wowote ni sh 200 tu kwa episode.

LIKE NA COMMENT ZENU ZINAONGEZA HAMASA YA KUPOST KILA SIKU. SHUSHA LIKE NA COMMENT YAKO
 
SIMULIZI: SABABU NI KIFO CHAKO BABA! (Kisa cha kweli cha kusisimua)
SEHEMU YA NANE (08)
MTUNZI: Man Middo Tz
WHATSAPP: +255 655 969 973

ILIPOISHIA…………… Sketi ya shule akaninulia ndefu mpaka naikanyaga na hivyo nilikuakibonge nilionekana kituko balaa. Madaftari akanunua atakayo yeye, baadae nikamuomba aninunulie begi la nguo nashangaa ananisonya huku ananisema sema vibaya, harafu pesa sio yake pesa ni ya baba yangu mzazi maana kipindi hicho mama ashanza kupokea mirathi hivyo pesa alitoa kwenye akaunti.

Basi tukawa hatusemeshani hadi tunarudi nyumbani, kwanza sikumheshimu kama baba yangu, sasa siku ya kwenda shule akapewa yeye anipeleke aisee nikaumia mnoo………….SONGANAYO.

Basi yule mzee akanipeleka ila kwa kweli sikua huru mbele yake kama ilivyokua kwa baba, nilikua namuonea aibu harafu simpendi, kubwa zaidi alikua ananikumbusha machungu.

Tukafika shule nikasajiliwa vizuri, sasa pakukaa kumbe walishapanga na mama ni wapi nikakae.

Akanichukua akanipeleka hapo nitakapokua naishi palikua ni jirani na shule. Yule mzee ndio alionekana kumshawishi mama kunileta pale kwasababu kulikua na mtoto wake anasoma alikua kidato cha nne pamoja na rafiki yake mmoja.

Sikujua wanamahusiano gani na yule mama pale, huyo mama mwenye nyumba alikua na watoto wanne, binti yake wa kwanza alikua kafeli darasa la saba akawaamerudia la 6.

Hivyo kwa ujumla tukawa familia ya watu nane. Sasa tukaanza maisha mapya pale yule mama akanipa maelekezo kuwa

“Karibu hapa ndio utaishi ila lazima tusaidiane kazi, kuanzia leo utasaidiana kazi na mwenzako (binti yake) kazi zenyewe kwenda kuokota kuni porini, kupika, kufagia, kufunga mbuzi, kuchota maji, kufua na zingine zitakazojitokeza”

Sikua na namna nikaitikia ingawa huo mlolongo wa hizo kazi ulinitisha kwa kiasi fulani, basi maisha ya kaanza hivyo mwanzoni tukawa watu wenye furaha sana tunashirikiana kwenye hizo kazi na mwanae.

Sasa walikua wakulima wa mpunga na mahindi harafu shamba lilikua mbali tunatembea masaa mawili hadi kufika shambani.

Sasa kuanzia hapo ndio nikanza kuyaona maisha kuwa magumu, kazi zikawa nyingi hata muda wa kupumzika huoni.

Fikiria tunasoma lakini ule muda wa kusoma ukifika unajikuta unashikwa na usingizi hadi huwezi tena kujisomea.

Yule mama alikua anapika pombe ya gongo aisee hapo ndio ndio niliona kweli matatizo nimeumbiwa mimi, kwasababu asubuhi ukiamka ni shule ukirudi shule unabadilisha nguo hata muda wa kula hakuna unachukua chakula unakula huku unatembea hadi porini kukata kuni mbichi za kupikia gongo na kavu za chakula.

Tukirudi nyumbani tumechoka tupo hoi muda huo usiku ushaingia, hakuna kupumzika tunaenda kutafuta maji usiku huo huo tunapika, asubuhi alfajil saa 10 tunasoma pombe kupeleka wanakopikia shule kwenda ni saa mbili hata sura zikawa zimebadilika kama sio msichana muda wote siriasi hakuna hata kucheka.

Hata shule kwenyewe nilikua mchafu sana, kwanza nilikua muoga kuomba mahitaji nyumbani au pale ninapoishi.

Lakini pia kwa upande mwingine mama nilimlaumu sana kwasababu ni kama alinsahau hukusu mahitaji kama msichana. Hebu fikiria msichana wa kidato cha kwanza nina chupi moja tu, siketi moja na shati moja tena bila hata vest.

Aisee nilikua naonekana kama kituko shuleni, nikapewa kila jina kutokana na muonekano wangu pamoja kutokujijali.

Sasa kutokana na usiriasi wangu hakuna mtu aliyetamani kuniomba urafiki, sikua karibu na mtu yoyote kwa jinsi nilivyokua hata mimi mwenyewe sikutaka ukaribu kwasababu sikua na hadhi ya kuwa na rafiki.

Hata notes sikua nazo kama wanafunzi wengine, vipindi vya ziada sikua naenda wala michezo sikua naenda kwa kuona aibu na sikua na nguo nzuri hata moja....... ITAENDELEA.

Haya ni madogo yenye nafuu katika makubwa na mazito yaliyomo ndani ya story hii.

Usikose......
 
SIMULIZI: SABABU NI KIFO CHAKO BABA! (Kisa cha kweli cha kusisimua)
SEHEMU YA NANE (08)
MTUNZI: Man Middo Tz
WHATSAPP: +255 655 969 973

Siku moja hii sitoisahau, nilitoka shuleni mapema saa 4 nilikua naumwa sana, basi nikafika nyumbani sina nguvu nikawa nimelala.

Siku hiyo yule mama mlezi alirudi muda kama wa saa 8 akaanza kupika mimi nipo ndani hajui sasa baadae akasikia kikohozi asee moto uliwaka

“Yani wewe Hesha umerudi unashindwa kupika mpaka saizi saa 8 hii, tabia gani mbaya hii”

“Mama nimerudi najisikia vibaya naumwa”

Kweli alivyokuja kunishika akagundua kweli naumwa harafu machozi yanitoka tu, basi akanipa panado lakini sikunywa nahisi kutapika tu. Ilipofika saa 9 akaaga akasema

“Mimi natoka lakini hakikisheni ikifika jioni mpeleke kuni bustanini (huko ndio wanapika pombe)”

“Sawa mama”Nikaitikia,

Binti yake anaitwa Frida, aliporudi akakuta naumwa nikampa maagizo niliyoachiwa hakunijibu, akabeba kuni zake akapeleka.

Sasa ilipofika saa 1 jioni yule mama akarudi akakuta bado nimelala nahisi baridi moja hatari kichwa kinauma harafu njaa inauma, aisee yule mama hakunielewa

“Wewe kwanini mpaka saizi umelala, kwanza kuni zangu umepeleka?”

Akauliza kwa jaziba, Nikamjibu huku natetemeka

“Mama najisikia vibaya sana, kichwa nahisi pia baridi kale hata nguvu sina”

“Sasa unategemea mimi naelewaje, yani kumwa kichwa tu usifanye kazi yoyote”

Akatoka akafunga zile kuni kisha akasema

“Yani ili tuelewane hizi kuni zifike bustanini”

Kwa jinsi alivyokua mkali na mtu wa amri na ndio mume ndio mke maana alimshika mpaka mume wake, nikainuka nikajikongoja hadi nje kujitwisha tu ikawa kazi nikajitahidi ukafika kichwani ila hapo hapo kizunguzungu kikanishika.

Nikaanza kujikongoja kuzipeleka lakini sikuweza kufika hata nusu safari Mungu Wangu usiombe yakukute! Nikadondoka na zile kuni na ubichi wake zikaja kunilalia juu hapo hapo nikaanza kuvuja damu puani…………..ITAENDELEAJE

HESHA ALIPATA MSAADA?

JE MZIGO ULE HAUKUMUUMIZA?

JE YULE MAMA ATAMPELEKA HOSPITALI? USIKOSE KIFUATACHO.

NUKUU “Katika maisha usiende msibani kwa mtu kuonyesha ni jinsi gani unamjali, hebu onyesha ni kiasi gani unamjali wakati huu akiwa anapumua”

Wamama kama hawa wapo wengi sana katika jamii zetu anakutesa awezavyo lakini siku ukifa ndio hao hulia kwa uchungu akijifanya anakupena sana, tena utasikia nimeishi nae vizuri huyu amenisaidasana kumbe ulikua humpendi. Tujifunze kuishi kwa wema na kuwajaliwengine kumbukeni utu ni bora kuliko kitu.

On Twitter and Instagram @middotz_
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom