Simulizi: Roho yake inadai

Simulizi: Roho yake inadai

SteveMollel

JF-Expert Member
Joined
Jul 12, 2015
Posts
8,803
Reaction score
25,442
UTANGULIZI


Kifo kina wivu sana, hutuondolea wale tunaowapenda. Hutuacha na majonzi na kumbukumbu za kuumiza, lakini pia hutubakizia jeraha kubwa ambalo hata likipona basi hutuachia alama ya kovu kwenye paji la uso. Kovu lisilofichika.

Ila ndivyo ilivyo asili, hatuwezi kupambana nayo. Kama tujuavyo, kwakuwa tumeumbwa basi ni lazima kufa. Mikono ya binadamu haina nguvu za kutosha kuzuia kifo labda kukikawiza tu. Na pindi wapendwa wetu wanapotuacha, hata tukiumizwa vipi, twasema ni mapenzi ya Mungu, basi nayo yatimizwe. Amempenda zaidi. Ndio. Sisi tulimpenda lakini Mungu wake aliyemuumba na kumleta miongoni mwetu amempenda zaidi.

Lakini je, ni kweli vifo vyote Mungu amependa? Wapendwa wetu wote waliotutoka, ilikuwa ni amri ya Mungu? Walifikia muda wao wa kuitwa? Na kama HAPANA, basi nao waenda wapi na ingali hawakuitwa?

Basi huko jirani na hata kule kwenye ulimwengu wa mbali tumekuwa tukisikia msemo wa 'DAMU YA MTU HAIENDI BURE' kumaanisha kwamba pale unapoimwaga basi itatafuta thamani yake kwanguvu. Haitakuacha ukaishi salama. Na maisha yako yatakuwa deni kulipia thamani ya damu hiyo ambayo haikuwa na makosa.

Kuna mifano kadhaa ya uhalisia ...

Mnamo mwaka 1999 huko China kwenye jiji la Hongkong, wahusika watatu wa genge la wahuni walimkamata dada mmoja aitwaye Fan Man-yee wakisema kuwa wanamdai dada huyo takribani dola alfu ishirini za kimarekani. Sasa kwakuwa dada Fan Man-yee hakuwa na pesa hiyo anayodaiwa, wakamtesa vibaya kwa mwezi mzima kabla dada huyo hajafa kutokana na majeraha makubwa aliyosababishiwa. Alipokufa, mabwana wale wakakatakata mwili wake, wakachemsha baadhi ya vipande vya mwili wake na kuvitupia vingine kwenye makopo ya taka.

Mmoja wa mabwana hao alikuwa na mpenzi wake wa miaka kumi na mitatu ambaye naye alishiriki kwenye mateso ya marehemu. Mpenzi huyo alikuwa akiitwa Ah Fong. Na iliripotiwa tangu mauaji ya Fan Man-yee yalipotokea, mwanamke huyo, Ah Fong, alidai kuona vitu asivyovifahamu vikimtesa na kumsumbua haswa. Mara kwa mara aliona taswira ya Fan Man-yee ikidai roho yake. Hakuishi amani. Na kwaajili ya kuokoa nafsi yake, akaamua kujisalimisha mwenyewe polisi aliposema yote waliyoyafanya yeye pamoja na genge la mpenzi wake.

Lakini Polisi hawakumwamini Ah Fong. Walipuuzia kwa kudhani ni matatizo tu ya vijana wachipukiao. Ila walipofanyia upelelezi kwenye eneo ambapo Fan Man-yee aliteswa, wakagundua kuna viungo vya binadamu. Lile genge likakamatwa na kesi kupelekwa mahakamani. Ah Fong akatoa ushahidi wote na kupelekea wahusika wa lile genge kuhukumiwa kifungo cha maisha jela.

Mbali na hilo, mnamo mwaka 1987, huko Marekani, bwana mmoja aitwaye Terry Childs alimchoma kisu msichana wa miaka kumi na saba aitwaye Lois Sigala mpaka kifo chake. Teery akashtakiwa na kuhukumiwa miaka 41 jela. wakati akiwa kifungoni, alikiri kufanya mauaji kadhaa. mmoja wa watu aliowaua alikuwa akiitwa Linda Ann Jozovich. Mnamo 1979 alimteka mwanamke huyo akampiga, akamkaba na kumchoma visu mara kadhaa, kisha akaficha mwili wake kwenye milima ya Santa Cruz, California. Ikachukua zaidi ya miaka kumi kugundua mabaki ya mwanamke huyo.


9k=.jpg
9k=.jpg

Terry alisema kuwa ilibidi akiri mauaji aliyoyafanya ili ajiweke huru dhidi ya 'roho' za watu aliowaua. Alisema alikuwa anawaona watu hao kwenye chumba chake cha jela, wakisimama na kumtazama. Akasema pia kuwa Linda Ann amekuwa akimfuata na kumghasi. Lakini alikuja kupotea baada ya yeye kutubu. Na kutubu kwake huko kukapeleka akaongezewa kifungo, cha maisha kabisa, asifae kupewa msamaha wowote ule.


Roho za watu walioonewa, haziendi mpaka zipate haki yake. Zitawanda na kuzurura kutafuta thamani yake iliyonyang'anywa mpaka kutimia kwake kisha ndipo ziende salama kwa amani. Zitagonga mlango ama kufungua dirisha. Zitafuata nyayo na kukutazama nyuma ya miti na mapazia ... mpaka pale zitakapokuwa huru.

Lakini je, vipi pale roho hiyo itakapoanza kulipiza kisasi kwa mji mzima kama kisasi kizazi kwa kizazi? Vipi pale roho hiyo inapodai thamani kubwa ambayo ni ngumu kuilipa?



***



Nitatuma simulizi hii hapa kutokana na ratiba yangu. Kwa wale watakaoihitaji, basi wanifuate whatsapp 0685 758 123 kwa ada ya shilingi alfu tatu tu.



Karibuni ...



ONYO: USISOME UKIWA UNATEMBEA BARABARANI.
 
*ROHO YAKE INADAI*


*Simulizi za series za Steve*



Massachusetts, Boston, 1975.


Mwanaume mmoja mrefu aliyevalia suti na koti refu jeusi alisogelea mstimu wa umeme na kusimama hapo. Mwanaume huyo alikuwa ni mzee wa makamo ya hamsini na, na mkononi mwake alikuwa amebebelea makaratasi kadhaa rangi nyeupe ielekeayo kuwa kahawia.


Alikuwa ameupinda mdomo, na macho yake yalionyesha kuchoka. Hata mwendo wake uliunga mkono hilo. Alichomoa karatasi mojawapo kati ya zile alizozibeba, akaibandika hapo mstimuni na kabla hajatazama kama karatasi hiyo imekaa vema, akaendelea na safari yake.


Bila shaka alikuwa na kazi kubwa mbele yake. Kazi ya kumaliza yale makaratasi aliyobebelea mkononi kwa kuyabandika kila mahali paonekanapo.


Mzee huyu aitwa Brewster. Mji wote huu wa Boston wamtambua kama mfanyakazi wa daraja la chini kwenye ofisi ya serikali ya mtaa. Wakimtambua kama mmojawapo wa wakongwe kwenye kazi hiyo, haswa ya ubandikaji wa makaratasi na usambazaji mwingine wa taarifa.


Sasa mzee huyu aelekea kuchoka, lakini bado haikuonekana ni nani anaweza kufanya kazi kama yeye. Kazi ambayo imejawa na kujitolea zaidi kuliko kipato.


Basi karatasi ile aliyoibandika ikiwa haijakaa vema, na pengine gundi ikiwa haijakolea, ikabanduka toka mstimuni na kudondoka chini. Upepo ukaipuliza na karatasi hiyo ikapepea na kupepea mpaka kwenye eneo la nyumba fulani ndogo iliyosanifiwa vema na mbao. Hapo mtoto mmoja akaiokota na kuitazama. Mtoto wa kiume mwenye makadirio ya miaka ya kumi na miwili ama mitatu.


ATAFUTWA! Kichwa cha habari kilisomwa vivyo. NI MIEZI MIWILI SASA TANGU ASIONEKANE NYUMBANI KWAO. TOA TAARIFA OFISI YA SERIKALI YA MTAA PUNDE UTAKAPOKUWA NAYO.


Tangazo hilo lilikuwa limeambatana na picha isiyo na rangi ya binti mdogo mwenye makadirio ya miaka kumi. Kwenye picha hiyo binti huyo alikuwa amebanwa nywele zake mafundo mawili na meno yake makubwa ya mbele hayakuwa yanaonekana akiwa ametabasamu. Alikuwa ana mapengo ila akionekana mwenye furaha.


Binti huyo alikuwa anaitwa Kacie.


“Brian!” sauti ya kike iliita. Basi mtoto yule aliyekuwa ameshikilia lile karatasi litangazalo kupotelewa kwa mtoto, akageuka kutazama mlangoni. Huko akamwona mamaye. Mwanamke mwembamba mwenye nywele nyeusi ti. Alikuwa amevalia gauni joshi la maua limfikialo magotini. Alikuwa amewekea mikono yake kiunoni.


“Kwanini husikii, Brian?” mama akauliza.


Brian akatazama tena lile karatasi alilolishikilia mkononi, kisha akakimbia kumfuata mamaye.


“Mpaka sasa hivi hujala, unazurura tu. Sipendi hiyo tabia, Brian!” mama alifoka lakini Brian hakuonekana kujali sana. Aliendea sehemu ya kula akaketi, na punde mama yake aliyepitia jikoni akaja akiwa amebebelea chakula sahanini. Akamwamuru Brian afungue kinywa.


“Chakula kiishe, Brian. Sawa?” mama akasema akitoa macho kutishia. Aliposema hayo akataka kwenda, ila akasita. Akatazama vema karatasi iliyokuwepo mezani, ile ambayo Brian alikuwa ameiokota huko nje. Hapo akaona picha na maelezo.


Akainyakua na kuyasoma vema. Punde akasema, “Kacie.” kwa sauti ya chini na macho yake yakiwa yamebebelea fikira.


“Nimemkumbuka sana,” akadakia Brian akitazama sahani yake ya chakula. Uso wake alikuwa ameufuma kwa huzuni.


“Najua umemkumbuka sana, Brian,” mama akasema akifanya namna ya kuketi kando na Brian. “Usijali atapatikana. Sawa?”


“Lini?” Brian akamuuliza mama yake. Bado alikuwa anatazama chakula chake.


“Sijui lini, Brian, ila atapatikana tu,” mama akaeleza akimpatipati Brian begani.


“Atakuwa ameenda wapi?” Brian akauliza. “Mbona hakuniaga? Nilimfanya chochote kibaya?”


Mama akashusha pumzi. “Brian, hukumfanya chochote kibaya. Kacie atakuwa ametekwa na watu wabaya. Watu wadhalimu. Ndiyo maana huwa sipendi uwe unazurura zurura huko nje. Sio salama.”


Brian akanyamaza kidogo. Bado alikuwa anatazama chakula chake lakini macho yake yakionyesha yu mbali kimawazo. Alipigapiga kijiko kwenye sahani, akiwa ametulia kabisa, akasema kwa sauti ya chini, “Labda Faris anajua Kacie alipo.”


“Kwanini unasema hivyo?” mama akadadisi. Hapa alionekana kuwa makini sana. Alimtazama mwanaye kwa macho yaliyogubikwa na ndita.


“Alikuwa wa mwisho kucheza na Kacie kule karibu na msituni,” akasema Brian kwa sautii yake ya chini kisha akamtazama mamaye. Mama akatikisa kichwa.


“Brian, kula. Sawa?” Kisha akanyanyuka na kwenda zake.


Kila mtu ndani ya mji anajua habari hizi za Faris kuwa mtoto wa mwisho kumwona Kacie kabla hajapotea lakini haikusaidia kitu kwenye upatikanaji wake. Tangu Faris amwone Kacie kwa mara ya mwisho amekuwa bubu. Amekuwa mlemavu wa akili. Amekuwa mtoto anayeongea maneno yasiyoeleweka.


Amekuwa wa kufungiwa ndani. Hakuna anayeelewa anachoongea. Hakuna anayetaka kuwa naye karibu.


Pengine Faris angeweza kutoa taarifa muhimu sana juu ya Kecie. Ila hilo halikuwezekana. Na basi kwa namna hiyo, taarifa hafifu za Kecie zilipatikana toka kwa polisi ambao waliona nyayo za Kecie zikizamia msituni.


Na zaidi mdoli wake alioudondoshea chini kabla nyayo zake hazijapotea kabisa kwenye udongo. Mdoli huo tangu ulipopatikana, wazazi wake wameuhifadhi kama kumbukumbu ya mtoto wao huyo wa pekee.


Umekuwa wakati mgumu sana kwao kuishi pasipo mtoto wao. Wamekuwa wapweke. Nyumba imepoa. Na hata juhudi zao za kupata mtoto mwingine ziligonga mwamba.



***


Baada ya miaka kumi …



Mambo kadhaa yalikuwa yamebadilika ndani ya mji wa Boston. Maendeleo huja pamoja na muda. Nyumba kadhaa zilikuwa zimejengwa, hata pia watu kadhaa wapya walikuwa wameongezeka ndani ya mji wa Boston. Idadi iliongezeka.


Lakini mbali na mabadiliko hayo, bado Kecie hakuwa amepatikana. Hakuna mtu aliyekuwa anajua wapi Kecie alipo. Na kwasababu hii ya muda, kuna baadhi ya watu hata wameshamsahau Kecie isipokuwa wale watu wake wa karibu kama vile wazazi wake na wale marafiki.


Ngo! Ngo! Ngo!


Mwanaume mmoja mrefu mwenye nywele nyeusi alibisha hodi na kungojea majibu. Punde mlango ukafunguliwa na mwanamke mtu mzima, makadirio ya miaka kasoro na hamsini. Mwanamke huyo akatabasamu na kusema, “Brian … karibu!”


Kijana yule akazama ndani. Na kumbe alikuwa ni Brian. Alikuwa amekua haswa, ila uso wake ule wa kitoto haukuwa umepotea. Brian ni mkimya. Macho yake ya pole na lipsi zake nyembamba.


Alikaa kitini kama mtu anayehisi baridi, akatazama huku na kule.


“Unaendeleaje Brian?” akauliza mwenyeji.


“Naendelea vizuri, sijui wewe Mrs Garett.”


“Sijambo. Mama yako aendeleaje?”


“Hajambo. Amenituma nikufikiishie salamu zake.”


“Ahsante sana, amekuwa mkarimu sana kwangu. Nawe pia … umepita muda mrefu lakini huachi kuja kun’tembelea.”


“Usijali Mrs Garett. Kecie alikuwa ni rafiki yangu, na itabakia kuwa hivyo siku zote. Haijalishi nimebanwa kiasi gani, siku hii ni maalum sana. Kila inapowasili naienzi maana ndiyo siku ambayo nilimpoteza rafiki yangu Kecie.”


Mrs Garett akanyamaza kidogo. Macho yake yalikuwa yanaelekea kuwa mekundu. Alisimama akamwambia Brian, “Ningoje, nakuja. Acha nikuandalie chakula.”


Akaenda zake na Brian akawepo pale sebuleni peke yake. Akatazama huku na huko ndani ya sebule. Ni muda hakuwa amekuja hapa. Baada ya kama dakika moja, akasikia mlango unafunguliwa, kutazama akamwona binti mdogo makadirio ya miaka nane, tisa ama kumi. Binti huyo alikuwa amevalia gauni limfikalo juu kidogo ya magoti.


Nywele zake zilikuwa nyeusi ndefu, ameziachia huru. Macho yake madogo yalikuwa na kiini cheusi. Mdomo wake ulikuwa mdogo kama ka-tone. Mashavu yake yalikuwa mapana na masikio yake mazuri yalikuwa yamesimama kuchomoza toka kwenye nywele zake.


“Hey!” Brian akamsalimu lakini binti huyu hakujibu. Alimtazama Brian na kisha akaketi kitini pasipo kuongea jambo.


“Hey, mimi ni Brian, wewe ni nani binti mzuri?” Brian alisema kwa tabasamu. Binti yule hakujibu, akaendelea kumtazama. Brian akanyamaza na muda si mrefu Mrs Garett akaja sebuleni.


“Olivia, unafanya nini hapa?” kumbe yule binti aitwa Olivia. Alisimama upesi baada ya kuambiwa hivyo, na akashika njia kwenda zake. Akaelekea chumbani na kuufunga mlango.


Mrs Garett akatabasamu akimtazama Brian, “Anaitwa Olivia. Nilimtoa kituo cha kulelea yatima aniondoe na upweke wa hapa nyumbani.”


Kisha akaketi.


“Unajua tangu nimpoteze Kecie nilikuwa mpweke sana, niliona kuna haja ya …”


“Naelewa, Mrs Garett,” Brian akamkatisha mwanamke huyo. “Anaonekana ni mkimya sana.”


Mrs Garett akatabasamu. “Ni mwenye aibu sana. Si mtu wa kuchangamana na wenzake. Nadhani kuna kitu kishawahi kumdhuru huko nyuma.” Mrs Garett akapandisha mabega juu. “Pengine atakuwa sawa akikaa hapa.”


Wakateta kiasi, na baada ya kama robo saa, Mrs Garett akaleta chakula. Wakala ukimya ukiwa umetawala kwa kiasi kikubwa.


“Vipi kuhusu Olivia?” Brian akauvunja ukimya. Aliuliza akiwa anatazama chakula.


Mrs Garett akaguna. Akatafuna na kusema, “Atakuja kula ukiondoka. Nadhani nimekuambia ni mwenye aibu sana.”


Brian hakuongea tena mpaka anamaliza chakula chake. Akamuaga Mrs Garett na kumwambia atakuwa anakuja hapo kadiri atakavyokuwa anaupata muda. Wakakumbatiana na Mrs Garett akamsindikiza Brian mpaka mlangoni.


Brian akashika barabara kwenda zake. Alipotembea kwa hatua kumi, hakujua nini kilimshtua, akageuka na kutazama nyumba ya Mrs Garett. Kwenye mojawapo ya chumba, dirishani, akamwona yule binti Olivia akiwa anamtazama. Mkononi mwake alikuwa amebebelea mdoli.


Mdoli wa Kecie.



***
 
*ROHO YAKE INADAI --- 02*


*Simulizi za series za Steve*



ILIPOISHIA


Brian akashika barabara kwenda zake. Alipotembea kwa hatua kumi, hakujua nini kilimshtua, akageuka na kutazama nyumba ya Mrs Garett. Kwenye mojawapo ya chumba, dirishani, akamwona yule binti Olivia akiwa anamtazama. Mkononi mwake alikuwa amebebelea mdoli.


Mdoli wa Kecie.


ENDELEA


Brian akasimama na kutazama vema. Pengine alidhan hakuona vema, ila kweli alikuwa sahihi. Mdoli ule ulikuwa ni Kecie. Lakini Brian hakuwa anajiuliza sana kuhusu mdoli ule, bali Olivia. Alihisi pengine mtoto huyo hayuko sawa.


Olivia baada ya kuona Brian anamtazama sana, akapotea pale dirishani. Alishusha pazia Brian akaenda zake.


“Hey Brian!” gari ilisimama kandokando mwa Brian baada ya kijana huyo kutembea hatua kadhaa. Lilikuwa ni gari lisilo na paa, na ndani yake walikuwapo wasichana wawili. Mmoja alikuwa na nywele nyeusi na mwingine akiwa na nywele rangi nyeupe.


Wasichana hawa walikuwa wamevalia matabasamu kwenye nyusoni. Macho yao yalionyesha uchangamfu lakini pia ujana wao.


Tukirudi kwenye gari walilokuwa wanalitumia, ilikuwa wazi lilikuwa ni gari ghali sana. Ukitazama miaka hiyo na gari hilo waweza kuona ni mambo ambayo yanakinzana kwa namna fulani. Hili lilionyesha wasichana hawa ni watu wa aina gani.


“Twaweza kukusogeza, Brian?” aliuliza msichana mwenye nywele nyeusi ambaye ndiye alikuwa dereva. Jina lake ni Wayde. Ni mtoto wa kwanza na wa pekee wa seneta wa Massachusetts, bwana Stuart McKenzie.


Mwenzake aliyekuwa naye beneti aitwa Silvia. Ni rafiki mkubwa wa Wayde. Naye pia ni mzaliwa wa familia ya watu wenye hadhi, baba yake akiwa mfanyabiashara mkubwa wa silaha.


Watatu hawa, Brian na Wayde na Silvia, husoma shule moja ya upili.


Baada ya Wayde kumuuliza Brian, alimtazama Silvia na kucheka kisichana kisha wakarudisha tena nyuso zao kumtazama Brian ambaye alikuwa anaigiza kutabasamu.


“Usijali, nitatembea tu. Si mbali ninapoelekea,” Brian akajibu akipandisha mabega yake.


“Unaenda nyumbani kwenu?” Wayde akauliza.


“Ndio, naenda nyumbani,” Brian akajibu. “Nimetoka kutembelea familia ya Garett na sina cha kufanya kwa sasa. Nadhani mama yanhu atahitaji kuniona.”


“Mama yako atahitaji kuwa na mumewe kwa sasa!” Silvia akatania kisha wakacheka pamoja na Wayde. “Inabidi uwape nafasi na wao waonyesane mahaba. Vipi tukienda mahali kustarehesha akili? Najua utakuwa unamfikiria rafiki yako Kecie!” akasema Wayde akimtazama Brian kwa macho ya ushawishi. Brian hakuwa mtu wa kustarehe, bali wa kujifungia ndani kusoma ama kutazama mambo kadhaa.


Hakuona kama ile ‘ofa’ ingempendeza, basi kwakuwa wasichana wale wasingemwaca kwa amani akaona awakubalie lakini kwa masharti.


“Twende kwanza maktaba kuu, kuna vitu nataka kuvipitia huko.”


“Umeanza sasa, Brian!” akalalama Wayde. “Huchoki kutazamana na vitabu wewe?”


“Nimesikia kile kitabu cha Dokta Hamill kimekamilika,” akasema Brian. “Ningependa kukitazama, pengine naweza ku…”


“Twende!” Wayde akamkatisha. Brian akazama ndani ya gari na kutimka mpaka maktaba kuu ya Massachusetts. Hakuwa na vigezo vya kuingia humo ndani, hakutembea na kitambulisho, ila kwakuwa alikuwa na Wayde alifahamu msimamizi hatompa pingamizi.


Na kweli.


“Unaweza kuingia ndani!” msimamizi akasema akimtazama kijana huyo kana kwamba mzazi anavyomtazama mwana mkaidi. Basi Brian akazama ndani na kunyookea moja kwa moja kwenye shelfu aijuayo, akapembua na kupembua, akatoa kitabu kimoja kilichosomeka, ‘NYUMA YA MITI - simulizi ya Massachusetts.’ kilichoandikwa na Dkt. Hamill Smith.


Kilikuwa ni kitabu kipya kabisa, na bwana huyo aliyekiandika akiwa ni Mkuu wa shule wasomayo Brian na wenzake wale wawili, Wayde na Silvia.


**


“Muda wote huo?” akalalama Silvia akikunja sura. Walikuwa wamekaa kwenye gari kwa kama lisaa sasa wakimngojea Brian atoke maktaba. Hata makalio yalikuwa yanawauma sasa.


Wayde akapiga honi mara nne akitazama mlangoni mwa maktaba. Sura yake ilikuwa imefura. Asingoje muda, Brian akatoka maktaba akiwa anakimbia. Akatumbukia ndani ya gari na wakaenda zao.


“Huwezi amini nilichokiona, Wayde,” Brian akavunja ukimya. “Kile kitabu ni muhimu sana na kimenifanya nijue kuwa Dkt Hamill anajua mambo mengi sana kuhusu huu mji. Natazamia kuonana naye.”


Hakuna aliyezungumza naye. Wote walikuwa wamekunja nyuso zao wasionekane hata kama wana dalili ya kuteta.


“Samahani,” akasema Brian. “Nimewakwaza, ila sikudhamiria kuwa hivyo.”


“Nimekusamehe, Brian,” akasema Wayde. “Ila siku nyingine sitakupitisha tena hapo. Ona hata tumeshachelewa!”


Walikuwa wanaelekea kwenye tafrija ya mwenzao aliyekuwa anasheherekea kumbukumbu ya siku yake ya kuzaliwa. Watu walikuwa wamefurika kwenye hiyo tafrija haswa vijana wa makamo ya miaka ishirini na. Walikuwa wanakunywa, na kucheza muziki uliokuwa unapigwa kwanguvu haswa.


Brian hakuweza kustahimili mambo haya. Baada ya kuwapumbaza wakina Wayde, alitoka kwenda nje na kuketi huko. Alidhamiria kukaa huko mpaka tafrija hiyo itakapokwisha au yatakapopita masaa kadhaa ili akiomba ruhusa ya kuondoka isiwe tabu.


Basi akiwa amekaa huko nje peke yake, na kwa mbali muziki ukiwa unaendelea kuchezwa, akili yake ikamezwa na mawazo. Na mawazo haya ni kuhusu kitabu kile cha Dkt Hamill. Alifikiria sana juu ya maudhui yake, na kwa namna kubwa akahisi kitabu kile kina kitu cha kumweleza juu ya kupotea kwa Kecie.


Aliamini hivyo kabisa. Na akiwa mawazoni humo akapata haja ya kumwona Faris. Hapa akapata wazo. Kwakuwa wakina Wayde bado yupo ndani kwenye tafrija basi anaweza kutumia gari lake kwenda kumwona Faris mara moja nje kidogo ya mji wa Boston, huko walipohamia na familia yake.


Hakungoja, akazama ndani kwenda kumwona Wayde na kumweleza haja yake. Kwakuwa Wayde hakuwa na ratiba ya kuondoka karibuni na pia vilevile alitaka kumfurahisha Brian, basi akampatia funguo kijana huyo aende huko atakapo.


“Kuwa salama, Brian,” alimuaga hivyo na kumpatia busu shavuni. Basi Brian akashika barabara na kuendesha kwa mwendo wa wastani. Yalikuwa ni majira ya saa mbili usiku sasa.


Baada ya kama dakika arobaini na tano akawa amefika mbele ya nyumba ya wakina Faris. Nyumba ilikuwa pweke iliyozingirwa na miti mingi. Kulikuwa ni giza japo taa zinawaka kutokana na mrundiko wa miti hii. Na zaidi kulikuwa kimya.


Punde Brian alipozima gari, mlango wa nyumba hiyo ukafunguliwa akatoka mzee aliyevalia overoli na kofia. Mkononi alikuwa amebebelea bunduki ndefu ya kuwindia. Akaangaza kumwona mgeni.


“Ni mimi Brian!” Brian akapaza sauti akinyoosha mikono yake juu.



***



“Faris, una mgeni,” mama mmoja mzee mwenye uso wa kichovu alisema baada ya kuufungua mlango wa chumba, Brian akaingia ndani.


“Usikae naye karibu sa …” mama alitahadhari, Brian akamkatisha.


“Najua, usijali.”


Mama akaenda zake.


Chumba hiki kilikuwa hovyo sana. Nguo zilikuwa shaghalabaghala, huku na kule. Sakafuni kulikuwa na maji yaliyofanya matope.


Kwenye kona ya kitanda alikuwa amekaa kijana wa kiume aliyekuwa ametulia sana. Amevalia shati lililochoka, na suruali iliyochanika mapajani. Nywele zake ni nyingi, macho yake ni mekundu. Mdomo wake mkavu na uso wake umepauka.


Mikono yake yote miwili ilikuwa imefungiwa kwenye kingo ya kitanda kwa kamba nzito ya manila. Kamba hiyo ilifanya mikono yake kuwa mekundu na hata kutengeneza majeraha kadhaa.


“Faris,” Brian akaita. “Ni mimi Brian, rafiki yako. Nimekuja kukuona.”


Faris hakusema kitu. Alikuwa anatazama sakafu kwa macho poozi.


“Faris!” Brian akamsogelea. “Ni mimi … ni mimi Brian, nitazame!”


Faris hakujali. Ni kama vile hakuwa anasikia jambo lolote. Alikuwa kama alivyokuwa tokea mwanzoni.


“Pole sana, Faris. Natamani sana kukusaidia urudi kwenye hali yako lakini siwezi kwa sasa. Nimekuwa mtumwa sana. Akili yangu haikomi kuwaza yale tuliyokuwa twafanya utotoni. Utoto wetu ulikuwa mzuri sana. Nashindwa kuacha Kecie na wewe mtokomee kabisa.”


“Kecie!” Faris akafungua mdomo kwa mara ya kwanza. “Kecie … Kecie … Kecie!” alipaza sauti kana kwamba mtu aliyekumbuka kitu cha kuogofya.


Akamtazama Brian. Akaendelea kurudia jina la Kecie akipaza sauti. Brian akajitahidi kumtuliza.


“Nini wataka kusema, Faris? Sema nakusikia!”


Faris alibwabwaja maneno mengi yasiyoeleweka. Alitota jasho jingi. Macho yalimtoka na mdomo wake akauchanua kadiri alivyoweza. Alijitahidi sana kuongea lakini hakuwa anaeleweka hata kidogo!


Brian akiwa anajiuliza ni namna gani afanye, akaona kitu fulani kwenye kingo za kitanda cha Faris. Kulikuwa kuna mikwaruzo kadhaa, mikwaruzo ambayo alipoitazama kwa makini aligundua ni michoro.


Michoro ya vitu vya ajabu.




***
 
Dah story nzuri sana but chakushangaza siku ya pili inaingia hauna hata pages 2 ila kuna ambao wakipost vitu kama hivi humu ndani ya 12hrs unakuwa na page 4 so on.

Shukrani sana mkuu kwa kutuchangamsha akili.
 
We chalii una kipaji aicee

Kazi safi hii.
 
Baada ya kufukuza mwizi kimya kimya kwa muda mrefu, hatimae nimeamua kuvunja ukimya. UPO VIZURI STEVE
 
*ROHO YAKE INADAI --- 03*


*Simulizi za series za Steve*



ILIPOISHIA


Brian akiwa anajiuliza ni namna gani afanye, akaona kitu fulani kwenye kingo za kitanda cha Faris. Kulikuwa kuna mikwaruzo kadhaa, mikwaruzo ambayo alipoitazama kwa makini aligundua ni michoro.


Michoro ya vitu vya ajabu.


ENDELEA


“Faris,” Brian akaita. “Ni nini hii?” akauliza akiwa anatazama michoro ile iliyochorwa na Faris kwenye kingo za kitanda. Tena kwa kukutumia kucha.


Hakujua vitu avionavyo ni nini, michoro ilikuwa hafifu na isiyo ya wazi, ila kwa mbali alihisi kupata angalau wazo. Aliona kama vile kuna binti njiti, kuna mwanaume njiti mrefu na kuna mtu mwingine njiti kwa kando. Mkononi mwa binti yule njiti aliyekuwa amechorwa, alikuwa ameshikilia kitu.


Juu kidogo ya mchoro huo, kulikuwa hakuonekani vema kwani damu zilizogandia zilikuwa zimetapakaatapakaa papo. Basi kwakuwa Brian alikuwa anataka kujua zaidi. Akakwangua damu hizo kwa kucha zake apate kuona kama kuna lolote.


Akaona maandishi kadhaa hapo. Yalikuwa ni ya lugha ngeni ambayo hakuwa anajua ina maanisha nini. Ila akayanakili maneno yale na kuyahifadhi kichwani. Akaendelea kutazama na kutazama. Vingine hakuwa anavielewa kabisa, na ubaya hakuweza kumuuliza Faris amwelezee chochote kile.


Kitu pekee ambacho Faris anajua kukitamka na kueleweka ni jina la Kecie tu. Na hajalishi imepita miaka mingapi, bado akisikia jina la Kecie hushtuka, hugomba, huogopa.


“Faris,” Brian akaita. “Naenda rafiki yangu. Nitakuja kukutazama tena siku nyingine. Sawa?”


Brian akasimama akimtazama Faris. Alikuwa ametulia tuli kama alivyomkuta mwanzoni. Na alipomtazama vema vidoleni mwake akaona ni namna gani Faris alikuwa amejiumiza na hata kujing’oa kucha kwenye vidole viwili vya kati. Yote kwasababu ya kuchuna kingo za kitanda kwa kuchora na kuandika.


Akamwonea huruma sana. Akampa mgongo na kwenda zake kuwakuta wazazi wa Faris sebuleni.


“Nashukuru, nataka kwenda sasa,” akasema akitabasamu kwa mbali. Baba Faris, bunduki yake ikiwa mapajani, akamtazama Brian kwa macho yake ya kizee kisha akamuuliza,


“Kuna lolote umepata?”


Sauti yake ilikuwa kavu kama ya mvuta sigara ama mnywa pombe kali.


Brian akatikisa kichwa. “Hapana,” akajibu. “Ila nimefurahi kumwona.”


Baba yake Faris akashusha pumzi ndefu puani. Akahamishia macho yake chini akibinua mdomo wake legevu. “Kuna muda natamani kummaliza apumzike … naona anateseka sana.”


Akapinda tena mdomo wake na kunyanyua nyusi zake juu kadiri awezavyo.


“Naumia sana kumwona katika hali ile. Japo sina kitu cha yeye kurithi, nilitamani sana awe na furaha kama watoto wengine.”


“Pole sana, Mr York,” Brian akampooza. “Ila bado ana umri mdogo, na hatuwezi jua ya mbeleni. Ni mapema sana kukata tamaa.”


“Mapema?” akauliza baba Faris. Macho yake yalionyesha udhaifu. Akatikisa kichwa chake kilichofunikwa na kofia. “Si mapema. Ona ninavyokongoroka, uzee unanitafuna. Mpaka arejee kwenye hiyo hali unayosema, bado nitakuwa hai?”


Brian hakusema kitu, alitazama chini. Mkono wa baridi wa mama yake Faris aliyekuwa ameketi kwenye kiti cha karibu naye ukamgusa.


“Nenda sasa. Muda wazidi kwenda na si vema kutembea nyakati za usiku ukiwa peke yako,” mama akamshauri akimtazama kwa macho ya msisitizo.


“Nashukuru, niwatakie wakati mwema.” Brian akaaga akaendaze.


Akatia chombo moto na kuanza safari yake ya kurudi kule kwenye tafrija kumkuta Wayde pamoja na Silvia. Alikuwa ndani ya muda. Hakutaka kuchelewa ili kuepusha kuwakwaza tena wale mabinti kwa kungoja muda mrefu, hata pia mama yake nyumbani.


Akatembea kwa mwendo wa robo saa akivuka miti. Safari yake ikiwa imetawaliwa na ukimya wa hali ya juu. Na mbali na taa zimulikazo barabara kukiwa kiza totoro. Miti imefungamana chini na hata juu kusiwe na dalili ya kiumbe chochote.


Nyuma kulikuwa giza na mbele kulikuwa giza. Upepo ukipuliza, miti ilikuwa inaruruma na kutengeneza sauti kana kwamba wanakwaya waimba. Upepo ukiwa umetulia, basi hakuna kinachosikika isipokuwa injini ya gari.


Brian alikuwa anatazama aelekeapo kwa macho yaliyotuama. Alikuwa ana mawazo kichwani mwake, ungelitambua hilo kwa kuutazama tu usowe. Alikuwa amekunja ndita na kinywa amekiacha wazi. Kuna mambo yalikuwa yanamtatiza. Kuna mambo yalikuwa yanamnyima raha.


Taswira ya Faris ilikuwa inamjia kichwani. Maneno yake yalikuwa yanajirudia masikioni mwake japo hayaelewi. Laiti angelikuwa anatembea eneo lenye watu, ni wazi angesababisha ajali. Mazingatio yake yalikuwa duni sana.


Ila akiwa fikirani humo, akahisi kuona kitu. Kitu kilichomshtua. Ni kama vile alimwona binti mdogo aliyevalia gauni jeupe kandokando ya barabara akampita kwa kasi.


Akageuza shingo yake kutazama nyuma kama atamwona binti huyo, hakumwona! Akawaza ni nini hicho? Ni kweli amemwona mtu ama ni mawazo yake. Na kama kweli kamwona mtu, ni nani na anafanya nini usiku msituni?


Moyo wake ulipiga mafunda. Na kwa namna moja ama nyingine akaongeza mazingatio barabarani tofauti na hapo awali. Akaongeza pia na mwendokasi.



***



“Nilidhani utatukalisha tena!” alisema Silvia akitabasamu. Alikuwa pamoja na Wayde wakiwa wamesimama na wasichana watatu pembezoni mwao, wote wakiwa wametoka kwenye tafrija iliyotoka kukoma muda si mrefu.


Wakajipakia kwenye gari na kumtaka Brian awapeleke majumbani maana walikuwa wamelewa, wasingeweza kuendesha. Kweli walikuwa wananuka pombe na hata kuongea kwao na kujichekesha hovyo kulionyesha namna gani kilevi kilivyowakolea.


Brian akawapeleka, na kama dereva wa taksi, akamshusha mmoja baada ya mwingine mpaka pale alipombakiza Wayde peke yake garini. Kwakuwa Wayde alikuwa anaishi karibu na Brian, haikuwa shida kwake kujisukuma kufika nyumbani hata katika hali yake ile ya ulevi.



***



Saa nane na nusu mchana …



Kengele ya mwisho wa vipindi iligonga, wanafunzi wakasimama na kila mmoja kuanza kufanya jitihada za kutoka ndani ya darasa isipokuwa kwa Brian pekee. Alikuwa ametulia kwenye kiti kama mtu ambaye hakusikia kengele. Watu wote walipotoka darasani ndipo akanyanyuka na kuweka begi lake mgongoni. Akiwa anatazama chini, akawa anatembea kwa mwendo wa taratibu kufuata geti lilipo.


Alipochomoza tu nje, akapiga hatua tatu, mara akasikia sauti inamwita. Kutazama akamwona mwanaume fulani aliyevalia nadhifu. Alikuwa ameegemea gari jeusi la thamani.


“Haraka, mvulana!” mwanaume huyo akamwamrisha. Brian alipofikia gari hilo, akaamriwa aingie ndani. Humo akakutana na Wayde akiwa pamoja na baba yake. Akapata hofu. Hata kusalimia alishindwa.


“Kijana,” akaita baba yake Wayde. Mzee mnene mwenye mustachi mweupe kwa mvi. Macho yake yamezama ndani. Sauti yake nzito ya kukoroma.


“Sitaki kukuona na binti yangu. Sawa?” akasema akimtazama Brian. Brian akatikisa kichwa. Na mzee yule asiseme kitu kingine tena, akampatia Brian ishara ya kichwa. Brian akatoka kwenye gari, gari likaondoka akibakia kulitazama likiyoyoma.


Kwa hofu aliyokuwa nayo, akaona ni kheri arudi shule na akae huko mpaka atakapoona ametuliza nafsi. Alihofia pengine vijana wa seneta wangeweza kumfanya jambo endapo wangemwona mahali ambapo hamna watu.


Akarejea na kukaa darasani peke yake, akawaza anawaza kumhusu Wayde. Ni nini jana kimetokea. Baba yake amejuaje kuhusu yeye.


Akiwa kwenye lindi hilo la mawazo, akashtuliwa na sauti ya viatu. Alipotazama ni nani akamwona Dkt Hamill, mkuu wa shule, mwanaume mrefu mwenye makadirio ya miaka sitini na, yu mbele ya darasa. Akashangazwa. Haraka akamsalimu.


“Mbona upo mwenyewe darasani? Kuna shida?” Dkt Hamill akauliza.


“Hapana,” Brian akajibu. “Hamna shida.”


“Kabisa?”


“Ndio, hamna shida. Hamna shida kabisa.”


“Sawa. Uwe na wakati mwema.”


Lakini Brian kichwani mwake akaona hii ilikuwa ni fursa adhimu kwake. Dkt Hamill ni mtunzi wa kile kitabu kinachoelezea misitu ya Massachusetts. Kitabu anachokipenda na kumsisimua kwa habari zake. Kwanini asimuulize maswali kadhaa kukihusu? Habari za kinywa zaweza kuwa sisimuzi kuliko za maandishi!


Basi akiwa anamtazama Dkt Hamill aenda zake kuufuata mlango, akapaza sauti, “Kitabu chako ni kizuri sana. Nakipenda haswa.”


Dkt akasimama na kumtazama kwa tabasamu la mbali. Japo mwanaume huyu alikuwa ni mzee, alikuwa mkakamavu sana.


“Kweli?” akauliza.


“Ndio, kweli,” Brian akajibu. “Natumai nitakimaliza ndani ya juma hili nitakapopata muda … lakini,” akasita kidogo. “Lakini ni ya kweli yale yote uliyoyaandika mule?”


“Ni kweli,” Dkt akamjibu. “Ni kweli kwa kila tone. Ila sitajibu swali lako lolote lile maana majibu yote yapo mulemule.”


Dkt aliposema hayo akapiga hatua kuuendea mlango atoke. Brian akapaza tena sauti, “Nina swali moja tu. Na wala si toka kwenye kile kitabu. Tafadhali unaweza nisaidia?”


“Lipi hilo?” Dkt akauliza. Brian akamtajia yale maneno aliyoyasoma toka kwenye kingo ya kitanda cha Faris. Dkt akamuuliza akimkazia macho, “Umeyaona wapi hayo maneno?”




***
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom