Simulizi: Pendo Huru

Simulizi: Pendo Huru

Xav Emmanuel

JF-Expert Member
Joined
Jul 12, 2018
Posts
215
Reaction score
316
Karibu katika Simulizi Mwanzo - Mwisho ya PENDO HURU.
Nafasi ya Mapenzi ya kweli katika jamii,
Nafasi ya wazazi katika mapenzi ya watoto.
Mioyo migumu iliyobeba siri zinazo angamiza nchi... Utamaduni na Mila katika nchi ya Malindi.

Karibuni sana.



MTUNZI: XAVERY EMMANUEL LUOGA
SIMULIZI: “PENDO HURU’
NAMBA: 0672493994

EPISODE 01
SEHEMU YA KWANZA

Kilikuwa ni kijiji cha malindi katika nchi ya Tegemeo. Ilikuwa ni asubuhi ambayo shughuli mbalimbali za maendeleo ziliendelea, kila mja hakuacha kujishughulisha katika jambo ambalo linapaswa kufanywa kwa wakati huo, ndege, wanyama na binadamu wengine hawakuacha kupiga kelele za asubuhi kuashilia kuwa kumekucha, si kuku tu aliyesikia akiunguruma kijijini hapo hata mbuzi nao walitoka katika mabanda yao. Kijiji kiliamka vizuri siku hiyo.

“La mgambo… la mgambo… La Mgambo” tufe lilisikaka kila kona ya kijiji, hakuna aliyefanya kazi. Kila mmoja akaacha akifanyacho kujua ni nini hasa wito wa tangazo hilo. Vichwa vya watu viligongana kwa kujibizana kuwa, ulikuwa ni wito wa mfalme, lakini hakuna ambaye alijua nini sababu ya wito huo.

“La Mgambo likisikika ujuwe kuna jambo.. tunahitajika wakazi wote wa kijiji wa malindi katika uwanja wa Mbio Ndefu karibu na lango la Mfalme. Kuna wito kadhaa….” Mtoa tangazo aliendelea kuungurumisha sauti yake katika kipaza kile cha pembe la ng’ombe. Hakuna aliyetoa sababu ya kutosikia wito huo kwa sababu, heshima ya mfalme ilikuwa ni kubwa sana kiasi kwamba kukahidi agizo lilikuwa ni tatizo ambalo litapelekea tatizo lingine.

Umati wa watu ulikusanyika kwa wingi katika uwanja huo wa Mbio Ndefu kwa kusikiliza wito, kila kona kelele zilikuwa ni nyingi kwani katika sehemu hiyo watu wanakuwa ni wengi, na wengi wao ndio kwa mara ya kwanza wanakutana, wengine wanamuda mrefu toka waachane kwahiyo walitumia fursa hiyo adimu ya wito wa mfalme.

Kimya kilitanda ghafla mara baada ya mfalme kupandishwa katika jukwaa la juu lililotengenezwa kwa miti migumu, mfalme alionekena kuchoka sana kwa kushindwa hata kuonyesha nguvu ya ukakamavu mashavuni kwake, alibota sana.

Licha ya kuvaa nguo kubwa kumrudisha katika hadhi yake ya utawala kipindi cha ujana, lakini lengo la miaka kwenda mbele haikuchoka, miaka ikaendelea kumuumbua mfalme na kuthibitisha kuwa mfalme amechoka sasa.

Pembeni kidogo kulikuwa na binti mrembo ambaye kwa asilimia zote alifanana kabisa na na mwanamke mwingine aliyekuwepo upande wake wa kulia, aliyesimama upande wa kulia alikuwa ni Mama yake. Mke mkubwa wa mtukufu mfalme Bana, walifanana kuanzia sura hadi rangi na vimo vyao, kila kitu kililandana.

Nyuma ya mfalme kulikuwa na idadi kubwa ya walinzi ambao waliongozwa na kijana shupavu amabye hakuna asiyemfahamu kijijini hapo. Alikuwa mtu wa miraba minne. Mweusi kupita neno Nyeusi. Kama macho yako yatakuwa ya kulegalega unaeweza kumpita kwa kumfananisha na mkaa. Alipopanda mfalme wote wakawa kimya na kumpisha mfalme aongee.

“Wananchi, nipo hapa kutoa ufafanuzi wa kufunguliwa ghurudumu ya michezo ya kimalindi ya utamaduni katika uwanja huu wa Mbio Ndefu. Mashindano hayo yataanza kipindi kijacho cha wiki mbili baadae, wito wangu ni kuwa kila mshiriki ajiandae vyema katika kinyanganyilo cha zawadi nono ambacho kila mtu anakijua. Pia washindi wote kwa upande wa kiume na wa kike watajishindia taji na nafasi ya cheo kikubwa katika utawala wangu. Kohno!” mfalme akakohoa kidogo kisha kuendelea.

“Kila mshiliki atajiandikisha kama ulivyo utaratibu wa miaka yote na ni lazima kushiliki kama unakipaji. Siku ya hitimisho la mashindano hayo nitatangaza..” Mtukufu mfalme alibwabwaja maneno ya vishindo vya kila aina. Alikuwa serious sana na maisha. Hakuna nyau aliye mtisha katika utawala wake. Alikuwa Mungu wa Malindi lakini kibaya kuliko vyote bado hakupata mrithi. Hadi kuzeeka kwake hakuwai kupata mtoto wa kiume. Kila mbegu aliyopanda kwake ilikuwa ni mbichi, ikawa nyepesi kuharibika. Ikafia mbali. Na hakuna kidume kamwe!.

**********
“Bwanah! Sadiki eh!, lo!, mimi sina neno kabisa juu ya mtoto wa Mfalme!, sina nguvu kabisa Kaka!. Siku ukisikia nimekufa basi ni sababu ya presha ya kumkosa Binti Zawadi katika moyo wangu. Nampenda..” zilikuwa ni tambo za Saleh kwa rafiki yake Sadiki. Wote walishikana mabega na wakiongozana kurudi makwao.

“Kakaa!, Kaka!, unamjua Abunuasi wewe?. Hahahahaha!, huwa napenda sana ndoto zako za mchana mchana. Toka kuzaliwa kwangu Malindi, katu sijawai kuona Ufalme unarishishwa kwa mtoto wa fukara na asiye na hata chembe ya umaharufu… ilaa!, Jasiri hakati tamaa na mimi sio mmoja wapo watao uangaike!. Rafiki yangu!!! Kumpata Zawadi…, lazima kupigana Kufa na Kupona. Yule sio Zawadi tena. Kama baba ndio vilee umri umemtupa mkono. Nadhani madaraka yote yapo chini yake..” Sadiki naye hakuacha kumkumbata rafiki yake kwa kumpa uhalisia wa maisha. Mdogomdogo safari ikashika kasi, kila moja akitoa na kuweka mada yake kuhusu mapenzi na maisha yao. Hadi kufika kwao njia panda ya kuachana kila mmoja alikwenda kweke.

***************
Saleh na Sadiki ni marafiki wa kutupwa, usiombe ukutane na Saleh, basi umekutana na Sadiki. Alikadhalika kwa Sadiki. Wawili hao walishibana haswa katika maisha. Ufukara kwao haukuwa kikwazo kabisa katika kuendelea sebene la maisha. Walilidhika na shughuli ndogondogo za kijijini huku, Saleh akiwa moja ya wafuataji wakubwa wa ndogo ya Baba yake. Baba yake alikuwa muwindaji na mtoto hakuwa na budi kuifuata ndoto ya baba.

Sadiki yeye alikuwa bingwa katika michezo ya sarakasi, kupiga na kucheza ngoma. Sadiki alikuwa bize kuongelewa Malindi nzima katika suala la usakataji na utambaji ngoma za asili. Usiombe aanze, katu kumaliza kwake kutakukera. Utatamani sana ulale na yeye akikuburudisha kwa fanaka yake ya aina yake.

Saleh na Sadiki Waliishi katika maisha ya kufarijiana na kusaidiana katika kila hatua. Hakuna jambo la kutenganisha ndoa hii. Imefungwa kwa kufuri la roho.! Sadiki na Saleh walishibana. Hakuna aliyekula robo tatu, wote walipatiana nusu nusu angali familia zao hazikuishi karibu sana. Zilikuwa na umbali kiasi, lakini kwao wakaitumia kama fursa na sio changamoto.

**********
Pembezoni kidogo mwa kijijini cha Malindi alikuwako nyumba chakavu waliyoishi moja ya familia inayojishughulisha na shughuli ya kilimo na uwindaji. Ilitosha kabisa kuitwa familia kwa kuwa hakuna kilichokosekana.

Ilikuwa ni nyumba ya kina Saleh, pilikapilika za hapa na pale zilikuwa ziliendelea. Kwa hamu kubwa Mama Saleh alikuwa akimsubiri kijana wake kumuagiza baadhi ya vitu. Mama naye umri ulianza kumpotea. Alishindwa kabisa kuhesabu siku zake zinazoendelea.

“Ulipita hadi kwa Mzee Chomeo?..” Lilikuwa ni swali kutoka kwa Mama Saleh ambalo lilimkuta Saleh akiwa bado hatua chache kumkaribia.

“Shkamo Mama.. Baba Salamu…!, Hapana Mama, Sadiki naye maneno mengi, wala hatujafika kwao. Maneno yametuchelewesha.” Saleh hakuwa mchoyo wa salamu, akazigawa kwa idadi ya wakubwa wake. Jibu lake lilimpeleka hadi ndani na masikio yake kuruhusu sauti ya mama yake iitike katika ngoma za masikio yake.

“Marhaba Baba…! Penyapo nilikuwa nakusubiri unisaidie kupeleka hivi vitu kwa Mama Zena!” Mama akatoa dukuduku lake la kumsubili mwanaye kwa kitambo.

“Baba kwani, hamjafika kwenye mkutano?” Saleh akamchokonoa baba yake aliyoko bize kuchonga zana zake za uwindaji.

“Tusiende alafu?. Hatuna jeuri hiyo. Tuliongozana sote, tukawai kurudi.” Akajibu kwa ustadi bila kupepesa macho.

Tayari Saleh iliingia ndani na kutoka nje. Mikono yake ikawa kiunoni na macho kuangalia jua, ilionesha kuna kitu aliendea kuchukua ndani na kulikosa.

“Sasa mwanangu, kipindi hiki yakupasa kuwai nyumabani, siku hizi si za kucheza cheza kabisa. Kazi ni nyingi!” Mama alitoa maneno ya kuashilia kitu, lakini Saleh alikuwa bado mbali kuwaza. Akazitoa pumzi kwa urefu zaidi na kusindikizwa na kajeri kutoka kwa baba yake ambaye aliiona hali ya saleh toka atoke ndani.

“Dogo, kama maji yamezidi unga fuata tu ombi la mama yako. Oa!” kauli hiyo ya Baba Seleh ilifanya Mama Saleh atanue mbavu zake kwa cheko la uzee. Wazazi wote hao wawili walitamani sana kuona kijana wao anashughulikia mapema suala la kuoa. Wakawa wanampiga vijembe tu.

“Mwanangu mimi nitakufa na sijaonja hata radha ya kuitwa Bibi!, huoni Haya?, mwenzako Sadiki ndio huyoooo hatua moja kama sio mbili zimebaki. Hadi posa tayari!. Wabaki wewe tu kijijini hapa. Mimi baba Saleh unajua hadi kuna muda nawaza kuwa wanawake wote wameshaisha hapa kijijini..!, waliobaki sina imani nao. Sasa mwanangu sijui ni padire?” Mama Seleh akatia kijembe kwa kumuunganisha na Mume wake.

Saleh hakujibu neno zaidi ya kutabasamu tu. Alijua fika kuwa wazazi wake wapo katika hatua kubwa mno ya kutaka kushudia ndoa na mtoto kutoka kwake. Lakini bado hawajui kwamba nafsi ya saleh imeegema kwa Binti wa mfalme na si mwingine. Ikabaki kuwa siri yake tu moyoni. Alificha nyasi karibu na moto.

“Wangejua!!!” Saleh alimungunya maneno rohoni na kukusanya vyombo kutoka kwa mama yake ambavyo Vilikuwa vinaelekea kwa mama Zena.

“Mwanangu!!! hata Zena huyohuyo mbona mzuri tu!, hurudi nae basi!!.. hahaha!” ilikuwa ni furaha na kijembe kingine kutoka kwa Mama. Kijembe kilichomsindikiza Saleh kwa juhudi kubwa kwani katu katakata kulisikia hata hilo jina la Zena ambalo Mama yake amelitaja. Alilimezea tu mate na kuendelea na safari.

***********************
“Mama vitu hivi apa nimeagizwa, mi hata sikia nipo na kazi nawahi!” Haraka ya Saleh ilikuwa ipo kasi mno. Alimkabidhi Mama Zena vyombo, na kuomba kuondoka. Hakutaka maongezi zaidi na Mama Zena kwani alijia pilikapilika za Mama huyo, anamaneno kama chiriku.

“Saleh!!” ilikuwa ni sauti ya upole kutoka kwa Mama Zena. Hakusubiri sauti hiyo ipotee bure Mama Zena, tayari alimsogelea Saleh ambaye mapema alianza kutoa mguu wake kuondoka.

“Ivi Saleh, mwanangu mimi Zena anakasoro gani?” alihoji Mama Zena na kufanya Saleh kuwa kimya uso ukimshuka.

“Huna la kunidanganya!, nafahamu kila kitu. Hana kasoro mwanangu!, kwa nini unamuumiza sasa?, yani hadi mwanamke anakupenda nusu kufa lakini hutaki?!. Mzazi gani anapenda kuona mtoto wake anaumia?!” ilikuwa ni risala fupi kutoka kwa Mama Zena kwenda kwa Seleh.

“Lakini Mama tulishayamaliza hayo na Binti yako!..”. alijitetea Saleh.

“Loh! Mwa’mwa’mwa’mwa!, Kuyamaliza? Kivipi!!. Hujui kama mwanangu anaumia? Halali, hali. Nyumba haina amani!. Mimi najua ulimtaka radhi mwanangu kwa kuwa humpendi, na na na… haupo tayari kuwa naye. Lakini mimi kama Mama. Ninalisimamia suara hii. Nitatufuta hata mganga wa nje ya kijiji. Mwanangu lazima aolewe na wewe... Babae ilo penda!, usipende!, nenda nalo. Huwezi cheza na Akili zangu hata siku moja. Khaa!” Mama Zena sasa alipandisha lile zimwi lake la wakati yupo kijana. Alipigania nafsi ya Binti yake ambaye alishaweka bayana kufa kwa ajili ya Saleh. Kila gharama itatumika lazima mbwa apate chakula.

Saleh akaondoka kwa Mama Zena. Akaondoka na furushi la maneno ya lazima ambalo alishinikizwa alibebe na Mama Zena. Kichwa chake hakina hesabu nyingine zaidi ya Binti wa Mfalme tu Zawadi. Saleh alikuwa kwingine kama Zena alivyokufa kwake.. aliondoka kwa Mama Zena bila hata kuangaria nyuma. Alikaza miguu kama askari anaye asiyelipwa mshahara wake kwa miezi. Akatoweka Saleh

ITAENDELEA…

#LIKE, #COMMENT & #SHARE..
PH%20Cover.jpeg


Starxav
 
MTUNZI: XAVERY EMMANUEL LUOGA
SIMULIZI: “PENDO HURU’
NAMBA: 0672493994

EPISODE 02
SEHEMU YA PILI.

Taa ziliendeleza kung’aza kasri ya Mfalme, eneo kubwa Lilikuwa na walinzi wengi walio imara kutoruhusu hata upepo mbaya kupata. Askari walikuwa imara mno katika lindo.

Mlangoni mwa nyumba kubwa alisimama mlinzi wa mwisho. Mlinzi mbabe kuliko wote. Mlinzi mwenye kila aina ya taji alilijishindia katika mashindano mbalimbali ndani ya kijiji cha Malindi. Alikuwa maarufu sana kwa ulinzi wa mfalme toka ujana wake.
Ukizungumzia umbo lake la mraba, halitoshi kabisa kubeba dhana ya kumlinda mtu mzito kama Mfalme Bana. Ongeza na rangi yake nyeusi ya kuvutia. Ilivutia kwa sababu kwa kijiji hicho ikihesabu rangi nyeusi kama aliyokuwa nayo Ibo unaweza usifike hata tatu. Kila ukihesabu utakomea kwa huyohuyo Ibo. Alikuwa mweusi kwelikweli.

Ibo alikuwa na sifa kubwa ya kuhakikisha kasri, mfalme na kijiji kizima kinakuwa na usalama. Usipomjua huyu mtu basi unarusiwa kukatwa kichwa kwa ushamba. Yote tisa Ibo alikuwa na mwili wa kuvutia kila aina ya wadada. Alikuwa na kuanzia six hadi twelve parks. Alichongeka kwa mazoezi ya kumlinda Mfalme hadi mwisho wa maisha yake. Ibo ni shupavu…

Ndani ya nyumba kubwa kulikuwa na mjadala uliendelea kuyoyoma kutafuta masaa ya kulala. Ilikuwa ni muda wa Zawadi kudondosha chozi mara baada ya kukerwa na lazimishwa ya baba yake kuolewa na Ibo. Baba alimchagua Ibo kuwa mrithi wa himaya yake ikiwa sababu kubwa ni ushupavu na uelewa wake kuhusu utawala. Ikumbukwe mfalme hakufanikiwa kupata Mtoto wa kiume. Bali binti Zawadi ndiye alikuwa mtoto mkubwa wa Mfalme.

“Zawadi Mama!, Huyo ndiye mtu Sahihi na bora kwa wakati huu. Umri wangu upo hatihani sasa. Lazima nipate mrithi mapema sana kabla sijapotea. Siwezi pigana na hii hali. Ibo!, Ibo!, Ibo tu ndiye pekee ambaye lazima akuoe. Mwanangu. ‘Ndio ya mfalme ni ndiyo ya watu wote’. Hakuna la kupinga. Utake usitake. Hakuna sababu ya kukataa kutoolewa na Ibo.” Baba alikuwa katili sana katika kufanya maamuzi yake. Tayari roho na moyo wake aliukabidhi kwa kijana wake Ibo. Ambaye ndiye hadi sasa amefikisha vigezo vya kumuoa Binti yake. Alichotaka Mfalme ni kupata mrithi Sahihi ya Malindi.

Kulikuwa na ulazima wa kulazimisha ndoa sababu kubwa ni kurithisha miliki ya Malindi kwa mtawala mpya. Miaka ya Mtukufu Mfalme Bana ilishafika hatiyani. Jahazi Lilikuwa huru kuzama.

Hadi Mfalme anaenda kupumzika, bado Zawadi hakuweka bayana sababu za kukataa kuelewa na Ibo. Aliendelea kuteseka na hisia zake bila kumshilikisha mtu yeyote. Mama Zawadi hakuwa na la zaidi, alimshawishi tu Binti yake aolewe kwa sharti la Baba yake. Mwanamke hakuwa na neno Malindi. Alifuata neno la mwanaume.

Ushawishi wa kiza ukawafanya kusahau kabisa mwanga, wingu la usingizi likatanda katika mboni zao. Likasafisha machozi ya Zawadi na kumlaza kabisa. Zawadi alilala kwa kubembelezwa na kiza cha usiku. Nyota zilishuhudia tu. Muda huo bado zilikuwa hazijalala.

**********
Ahsubuhi na Mapema, Saleh na ndugu yake wa kutupwa Sadiki walikuwa katika kuandaa bustani zao. Kila mmoja alishachafuka mno kwa jasho na tope la asubuhi hiyo. Jembe la Saleh Lilikuwa zito mno kutokana na kuwa na mawazo mengi kichwani. Mawazo yake yalimfanya kusahau kama yupo kazini na akashindwa kabisa kutoa ushilikiano kwa Sadiki ambaye alikuwa anachezea jembe kama hana akili nzuri. Anakwatua tu.

“Sadiki kaka!, ebu nipe kwanza mchongo!. Nampataje Zawadi!!. Nampenda!” Saleh aliweka jembe chini kwa mawazo na kutafuta kivuli cha kupoza wazo lake. Alikata majani kadhaa katika mti wa karibu na kuyahifadhi chini kama kitako. Akakaa kusubili wazo la mwenzie.

“Saleh!, mbona nimepata khabari kuhusu Zena!, Msahau Zawadi Tafadhali.. yule kwa levo yako HAWEZEK… Mhhh!! labda..” Sadiki hakumaliza maneno yake, akafumba mdomo. Macho yake hakuyatoa katu alipotazama. Alionana na kitu cha kushangaza. Ndio cha kushangaza kwani ni adimu sana asubuhi kama hiyo kukutana uso na Binti wa mfalme. Tena mtu ambaye jina lake ametoka kutajwa sio mda mrefu.

“Za.. za.. Zawadi?!!” Sadiki aliuliza baada ya macho yake kuhakikisha kweli aliyopo mbele yake ni Zawadi. Maneno yake yalimuinua Saleh kitakoni na kusimamia kuangaza japo kuona mng’ao wa pekee wa Binti wa mfalme, mtu ambaye yupo moyoni.

Ni kweli alikuwa Zawadi Binti ya Mfalme Bana. Alikuwa hatua chache sana toka walipo marafiki hao wawili. Kunyanyuka kwa Saleh kulifanya Zawadi kupunga mkono kwa nguvu sana. Na kwa ishara Saleh akaitwa.

Akaitwa Saleh, hakuwa na la kufanya zaidi ya kuitika wito wake wa kwanza kwa Binti ya Mfalme. Angali Saleh alikuwa akitetemeka lakini la Asha alipata pumzi ya uanaume. Akasogea palipo Malkia huyo.

“Saleh, wanitenga mwezio, hata huonekani!” Zawadi akajitolea uvivu kwa kijiviringisha mzima mzima kwa Saleh. Wapambe waliomsindikiza Zawadi walikuwa mbali na tukio. Aliwaacha hatua chache kuficha siri ya moyo wake. Zawadi pia alimpenda sana Saleh. Lakini katu hakuwahi kusema.

“Ha.. hamna Binti wa Mtukufu mfalme!, heshima kwako!” Saleh akainamisha kichwa chake chini kupisha salamu ifike kwa mtoto wa Mfalme.

“Bhaanaa!, niite jina langu Saleh!.” Zawadi hakutaka kabisa heshima ambazo Saleh anazionesha waziwazi. Alijiona hana kitu kwa Saleh. Hawezi sema hazima yake kwa wanaume kwani tamaduni ya Malindi haipaswi kwa mtoto wa kike kumdhihaki mwanaume kwa kumtamkia kuwa anampenda. Bali haki ni kusubiri tu kuambiwa kuwa anapendwa.

Zawadi alijinyonga nyonga sana, hakuna alichoongea na kueleweka, kila neno alikuwa anakosea na kuomba kurudia tena. Saleh yeye alishindwa kueleza hisia zake kutokana na hadhi yake kwa Binti wa Mfalme.

Zawadi yeye tamaduni zilimbana. Zikamshika kisawasawa. Akashindwa sema kabisa. Akamaliza kucha zote kwa kuzikata na kulamba akiwa anatafuta maneno ya kuongea. Alimpenda sana Saleh ambaye toka utoto wao walikuwa wanafahamiana tu. Hakuna la zaidi. Waliishi na hisia zao mwilini na kubaki kuwatesa kama nyuki wamtesavyo mhusika aliyevamia mzinga wao. Hakuna walichoongea, mwisho wakaagana na kila mmoja kurudi katika hamsini zake.

“Naona mtoto anang’ata kucha,. nini!, ushamaliza eh?”, Sadiki alikuwa tayari kashatoboa mdomo wake na kuruhusu mahojiano ya Saleh ambaye ndio kwanza alikuwa anacheka na kurudi sehemu alikaa mwanzo.

“Mzee hakuna chochote kile. Bado kamba ngumu. Na sidhani kama nitampata Zawadi, daah!, we kaka acha tu.. naumia!” Saleh aliongea huku akigongagonga jembe lake kutoa tope.

“Sasa mbona alikuita kwa wito wa mikwara hivi?, Mhhh mimi nadhani kuna kitu moyoni mwa Zawadi. Inabidi usilegeze kamba. Kaza Kaka!. Zawadi anakupenda sana, lakini ukionesha uoga basi mtende huo utaanguka nyumba nyingine. Tumia fursa, mwambie ukweli kaka!” Sadiki hakuacha neno. Tayari aliyajaza masikio ya Saleh wazo jipya na leye mantiki sana.

Saleh alikuwa hana kabisa uzoefu na mapenzi, bado utoto ulimsumbua sana. Haikujua jinsi ya kumwingia mwanamke na kumweleza ya moyoni. Alijua kuwa mapenzi ni chai, yanamiminwa tu popote pale. Alishindwa kabisa hata kutumia mipira iliyokufa kumshambulia mpinzani. Yote alipiga nje. Wataalamu wa mambo ya mahaba wanasema kuwa Saleh alikuwa Domo Zege. Alikuwa na mdomo mzito Saleh.

“Dah! Kaka kwani ukimpenda mtu ndio unakuwa katika hali kama hii. Yaani leo kuitwa tu na yeye! Tayari moyo wangu umeitika ndiondio! kama zote!, leo nitalala nikikesha macho, nitafanya sherehe ndotoni kama Mwenyezi Mungu ataniruhusu kulala leo. Hahahahahaha” Saleh alimaliza na kicheko kikubwa sana. Waliongea sana na kujengana kiakiri. Sadiki alishapevuka kuhusu mapenzi. Hakuna wa kumdanganya kijijini Malindi. Alijua wapi yanaanza na wapi yanaishia mapenzi. Kiufupi Sadiki alikuwa Mwalimu.

****************
ITAENDELEA KESHO…

#LIKE, #COMMENT & #SHARE.....!

Starxav
 
MTUNZI: XAVERY LUOGA
SIMULIZI: “PENDO HURU"
Namba: 0672493994
@Star_xav

EPISODE 03
****************
“Zena Binti yangu!, Umeshindwa tumia mbinu za zaidi kupata unachokitaka?, vipi ushajaribu kumfuata kwao?, ushajaribu kumchinjia Kuku?, vipi kuhusu mauno yako!, hana habari nayo. Mwanangu hata mwili bhana. Nataka kupata unachokitaka. Hakuna mwanaume mjanja kwa mwanamke mpevu. Ungo wako umevunjia wapi wewe? Au uliutoboa na kutupa?” Lilikuwa ni fundo la mwisho mwisho la Mama Zena kwa mwanaye Zena ambaye alichoshwa kabisa na habari za bintiye kulalama kila siku kwa kukosa mtu anayempenda.

Maneno ya mama yake yalikuwa kama maji tu mtoni, hakujua chanzo chake wala kikomo chake, zaidi maneno ya mama yake aliyafanya kama dalaja la kumpeleka mbali kimawazo. Aliwaza tayari ameshaolewa na Saleh.

Alimpotezea Mama yake ambaye alikuwa anabwabwaja tu kwa kumfunda Zena. Mama Zena alishamkamilisha Binti yake katika kila idara, alishindwa kuelewa kwa nini Zena anashindwa na kijana kama Saleh wakati kijiji kizima kishamtongoza!. Alichoka Mama Zena.

Zena ni Binti pekee wa Mama Zena ambaye alizaliwa na kulelewa pasi na baba. Zena katu hakuwai kuonja raha ya penzi kutoka kwa baba yake. Zena alikuwa maarufu kijiji kizima kwa uhodari wake wa kukunja na kukunjua nyonga. Alijua kutikisa kila kiungo cha mwili. Katika kila shindano la uchezaji toka kushiliki kwake yeye Malindi, ndiye alikuwa kinara. Alishapewa taji la kike mara kadhaa kwa kuwa mshindi. Hakuwa na mpinzani katika kucheza kwa upande wa wanawake.

Ukiongelea uzuri wa Zena ongelea tu maumbile yake yanavyoshawishi kuinua maungo ya yote ya mwanaume. Zena ni moja ya wanawake wachache ambao wanapatikana kijiji kizima. Ambao Mungu aliwapa Zawadi ya umbo zuri na makalio ya kutosha. Zena sio mrefu kiivyo, hapana!, ni mfupi kiasi kuweza kuhimili hipsi yake iliyotanuka isiweze kudondoka. Zena alikuwa mweupe wa asili, alikuwa na macho ya goroli na kope za kuchanua. Hakika Malindi walipata mwanamke. Mwananme mwenye uzuri wa umbo tu, tabia zinafanana na Mama yake.

“Mwanaguu!!, mimi pia nitafanya kila niwezalo, sitaki ufanye nyumba yangu ni sehemu ya kilio. Nakupenda mwanangu. Saleh ni wako. Huna mpinzani!.” Mama Zena alikazia bila kujali Binti yake anamsikiliza au la!. Alichojali yeye ametoa lile kongo la dukuduku moyoni. Hakika hakuna mama hampaye chakula cha moto mtoto wake.

********
Upande wa Mama na Baba Seleh bado hawakuacha kuongelea suala la kijana wao kuwa kimya kuhusu kuoa. Waliamua kulivalia njuga kwa kuangalia ni mwanamke yupi kijijini hapo anafaa kabisa kuwa na kijana wao. Kila wakipiga mahesabu ya kutoa na kuzidisha wanapata jibu Zena. Kila wakijumlisha na kugawanya, jibu linabaki kuwa Zena. Hadi hapo hawakuwa na budi katika kumhamasisha kijana wao avute jiko kabla Zena kuolewa na mwanamme mwingine.

“Baba nanii… Saleh!, Kijana atatuumiza kichwa huyu. Anatutia nuksi ujue. Hapa akigoma kuleta mwanamke basi mimi mama nipo tayari kumvika radhi!” Mama alionyesha yupo katika hatua za mwisho za kumshawishi kijana wake.

Kwa sehemu kama Malindi, umri wa Saleh ulitosha kabisa kuvuta jiko. Tena zaidi ya mmoja. Sasa ni jambo la kushangaza kwa kijana kama Saleh kuwa kimya nyakati zote hizo hadi mvi kutaka kumuota.

“Mke wangu!, kwani kusema Zena tabia zake hazirekebishiki? Au hazivumiliki?.” Swali la Baba Seleh lililenga kupata majibu kutoka kwa mke wake.

“Ah tabia gani Ba Saleh.. kukatika Mauno? Sasa hicho si kipaji jamani. Umesahau mume wangu jamani enzi zangu?!” Mama Saleh akajitapa kwa kumpeleka zama za ujana wao Baba Saleh. Wote wakabaki kusahau kuusu Zena na kuanza kurudishana enzi hizo. Enzi ambazo ziliwakuta wao wapo wabichi kabisa.

SEHEMU YA TATU

Naam majira ya jioni toka kuonana na Seleh, Zawadi alikuwa akiwaza juu ya njama za kumpata mwanaume huyo. Zawadi aliona kila dalili ya Saleh kuwa naye kimapenzi lakini kikwazo bado kilikuwa kwa upande wa Saleh. Zawadi alipenda sana Saleh aweke bayana nia yake. Licha ya baba yake kumshinikiza mara kadhaa kuelewa na mtu Ibo lakini moyo wa Zawadi haukuwa upande wa baba yake hata kidogo. Alisadiki katika kuhakikisha anaolewa na Saleh. Liwalo na lile.

Mapenzi bhana!, kuna muda yanachekesha sana. Unaweza kumpenda mtu aliye na wewe kwa kuhisi tu na yeye anakupenda. Vilevile unaweza kumjali mtu kama unampenda kwa kijitoa kila kitu wakati mtu huyo hana hata mpango na wewe, si hivyo tu vilevile wote mnaweza kupendana kutoka moyoni kabisa lakini kukawa na vikwazo zinavyosababisha msikutane au msiambiane ukweli. Mnabaki kuumia tu moyoni. Hichi ndicho kilimfakamia Zawadi, aliumia peke yake peke yake na Saleh aliumia peke yake peke yake. Wote walijijazia sababu ya vipingamizi vya kuto kuambiana ukweli.

Jioni ya siku hii haikuisha kama zinavyoishaga jioni nyingine. Zawadi aliwaza kumkera baba yake mtukufu mfalme. Aliona bora aweke bayana kuwa hampendi na hayupo tayari kuelewa na mtu ambaye Baba yake amemuwekea. Ukazuka mtafaruku na mpasuko wa familia. Kasri ya Mfalme ikatoboka. Walilia wengi.

“Saleh!!” Mfalme alipatwa na mshangao mara baada ya mtoto wake kumtakia bayana kuwa anampenda sana Saleh na yupo tayari kufanya lolote awe naye lakini si kuolewa na kijana ambaye hampendi.

“Ebu.. Ebu rudia.., rudia tena!!” Mfalme alipagawa kiasi cha kujiona kuwa hajasikia vizuri. Kwa sasa alisogeza sikio lake la kushoto mdomoni kwa Binti yake huku akiruhusu tena kufumba macho kwa kusubiri hilo jina la kijana mgeni masikioni mwake.

“Baba nampenda Saleh!” bila hiyana Zawadi alisadiki kabisa kurudia kila alichokisema mwanzo, hakupepesa macho hata kidogo. Akamtukana baba yake huyo ambaye kwa miaka takribani ishirini na ushee alimuheshimu kama Binti wa heshima mno. Leo Zawadi alimtukana kwa dhati kabisa baba yake.

Kama ilivyo kwa fahari mmoja anapokutanishwa na mwenzake, katu hawawezi kukaa katika zizi moja. Lazima wagombane, sasa Kiburi cha Zawadi kilikumbana na hasira za Mfalme. Hakuchukua raundi Zawadi tayari alivimba uso mzima. Alipokea kibao kitakatifu toka katika kiganja cha baba yake. Radha ya kibao hiki ilimkuta Zawadi akiwa tayari chini amezimia, radha yake aliisikilizia hukohuko usingizini. Mtukufu Mfalme Bana hana maksihara kabisa. Saleh! Khaa ndo kidudu gani!.

“Ba Zawadi jamani jamani jamani jamani, utaua!!, jamani Ba Zawadi utaniiiulia mtoto uwiii”. Mama Zawadi hakuwa mbali na eneo la tukio. Tayari alikuwa karibu kumpepea Binti yake aliyezimisha na kofi la uzee na baba yake.

“Huyo Saleh ndio nani?” Bana hakuwa na mchezo kabisa kabisa, hakujali hali ya mtoto wake aliyemzimisha pale chini, alikuwa naroho ya kumfahamu huyo kijana mgeni aliengia chumbani kwa Baba na Mama yake bila kipisha hodi.

“Ba Zawadi nini hiki!!, umemuumiza mwanangu!” Swali la Mfalme halikupata jibu. Mke wake aliendelea tu kutoa manung’uniko yake juu ya kitendo alichofanya mume wake.

“Yaani Zawadi toka apate hii barehe ya miaka ishirini amekuwa kichaa kama Mama yake!, Mnafundishana upuuuuzi upuuzi!, haya nani huyo Saleh?.” Swali lilelile lisilojibiwa mwanzo likaulizwa tena. Napo pia likakosa jibu.

“Mama Zawadi, si naongea na wewe lakini?, husikii yani. Eh!, husikii sauti yangu?” Mfalme Bana hakuwa na la kushuka, tayari mzuka wa hasira ulimpanda. Aliona nyumba nzima imeweuka kwa kufundishana mambo ambayo yapo kinyume na mipaka yake. Alianza kuzitikisa nywele za Mama Zawadi.

“ni mototo!!!, jamani ni Mtoto wa Mzee Selemani, upande ulee karibu na bonde!” Mama Zawadi aliona isiwe shali, akajibu kwa mkato na kuendelea kumpulizia upepo bintie kumpa unafuu... Naaam akafanikiwa. Akaamka Zawadi, Kesi ikawa kesi tena. jumba likamuangukia Zawadi. akajuta kuamka.....

ITAENDELEA KESHO.....

#LIKE, #COMMENT & #SHARE..

Starxav
 
MTUNZI: XAVERY LUOGA
SIMULIZI: “PENDO HURU’
NAMBA: 0672493994 (WhatsApp)
@Star_xav

EPISODE 04
“Mtoto wa Mzee Selemani, upande ulee karibu na bonde!” Mama Zawadi aliona isiwe shali, akajibu kwa mkato na kuendelea kumpulizia upepo bintie ili aamke. Akaamka Zawadi, ikawa kesi tena.

“Ehnee nieleze vizuri!, Saleh ni nani?? na mlikutana wapi?” Lilikuwa swali ambalo pia halikuwa na majibu. Lilimdondosha tu chozi Zawadi. Safari hii hakulia pekeyake. Aliungana na mama yake mzazi.

Wakalia kwa ushilikiano, lakini haikuwa mwisho wa kuandamwa na Mfalme, alitaka maelezo makini ya kumfanya ajuwe je Zawadi alitoka vipi katika kasri, na nani alimpa ruhusa, na huyo Saleh sijui walionana vipi hadi kupendana. Kwa kweli yalikuwa ni mambo ya kusogezeana tu mipira. Hakuna majibu sahihi kutoka pande zote mbili. Mama Zawadi anajua mengi sana kuhusu historia ya Mume wake, huwa akitaka kufanya ubaya basi hana chaguo lazima atekeleze. Sasa walificha kusema kuhusu Saleh maana walijua kinachofuata.

“Zawadi!, mimi Baba yako Mtukufu Mfalme. Nimetoa tamko sio maoni ni lazima. Utaolewa na Ibo. Sahau kukusu huyo kijana. Ukiendelea kutia mvuto jina lake masikioni mwanagu hutamuona tena. Kama unampenda mwache aishi.” Mfalme aliongea huku akitetemeka kuficha hasira zake. Baada ya kuona anakosa ushilikiano wa maelezo Mfalme akawapisha Mama Zawadi na bintiye wayajenge na yeye akaenda kupumzika. Akaenda kulala Mtukufu mfalme baada ya jambajamba hile.

“Zawadi!!” kwa sauti ya chini mama Zawadi akamwita mtoto wake. Hakuitika, ila alimtazama tu Mama yake usoni.

“Tutakufa mwanangu!, Mfuate tu baba yako!” Lilikuwa wazo ambalo halikukubaliwa kichwani mwa Zawadi. Alibaki kulia tu bila kutoa neno.

“Kwani huyo Saleh anajua kama unampenda? Na je unajuaje kama hana mtu?” Maswali yale yalimfanya Zawadi kukata chozi ghafla. Akakaa sawa na kujibu moja moja japo kwa tabu.

“Ma!.. Mama, Saleh nampenda, haijalishi anajua au la. Hakika sitaona raha katika hii dunia iwapo Saleh akinitoka mikononi mwangu. Nampenda sana Saleh Mama!.” Zawadi alijimwaga kwa sauti ya chini.

“Mwanangu hachana na Saleh. Kuna vitu bado huvijui japo umri wako upo tayari kuvifahamu vitu hivyo. Mwanangu achana na Saleh, Mbona Ibo naye ni kijana mzuri tu! Pia anasifa kubwa sana hapa kijijini japo….. hmmmm!” alisita Mama Zawadi.

“Mamaa!, Mamaa!, Mapenzi yenu ya zamani sana, hayafanani kabisa na karne hii. Mama nadhani hukumpenda wewe Baba, ila tu ulikuwa naye sababu ya cheo chake. Nalijua hilo Mama!” Zawadi akafunguka.

“Mwanangu, nakuambia hivyo kwa sababu…, sasa subiri tu nikupe siri!, nimekuambia nikupe nini?” aliuliza Mama Zawadi akimwangalia kwa makini Binti yake.

“Siri!” Zawadi akaitika na kukaa sawa.

“Mwanangu, Baba yako akijua kuwa Saleh ni mtoto wa Hadija! Tumekwisha. Koo yao na koo yetu haifungamani. Kuna ugomvi mkubwa sana koo hizi. Kuna vitu vipo nyuma ya panzia mwanangu. Tutakufa wote humu ndani, baba yako si unamjua lakini?”. Mama Zawadi alijaribu kutia Ndimu kidogo japo kumpoza kwa siri ya uongo.

“Hmmm!! Mama unanitisha, mimi Ibo hapana Mama. Mapenzi ni uhuru. Nipeni nafasi Mama!”.

“Zawadi na wewe king’ang’anizi mmmmh! Aya!” Mama Zawadi hakutaka kumpa ubuyu mwingi mtoto wake. Alimuonjesha kidogo tu basi, aliogopa atapata kansa kwa kumlisha ubuyu wenye kemikali. Waliagana kila mmoja kwenda kulala. Nyumba ilikuwa kimya sana siku hiyo. Doa lilishaingia kwa Mfalme. Nani atarithi Miliki hii ya Malindi?. swali likabaki hewani, likapishana na mbingu, nyota na vimondo, mwishowe likatua tena chini Malindï. bado swali halikupata jibu.

*************
Upande wa Saleh nako alikuwako katika mtafaruku, usiku uleule Saleh alimchukiza Baba yake kwa kuto mshilikisha katika masuala yake ya ndoa. Baba akadhibiti hasira yake na kwenda kulala. Saleh akabaki na Mama ambaye alikuwa na jambo la kuongea na mtoto wake.

“Saleh!, We Saleh!!, Najua Baba Yako Hajui, Lakini Mimi Najua Kila Kitu.!”
“Kuhusu Nini Mama?”
“Kuhusu Nini?, Kwanza Shusha Ilo Domo Lako!, Ongea Polepole Uko Khaa!”
“Enhe Nini Wajua?”
“Zawadi”
“Kafanyaje?”
“Khaa! Taila wewe!. Humjuhi Zawadi wewe?”
“Ndio namjua si Binti ya mfalme?”
“Nani asijue hilo, afu nimekuambia shusha ilo domo wewe!!!”
“Zawadi kafikaje hapa Mama?”.

“We jifanye tu mwendawazimu. Unajua anakotokea Zawadi?, unajua Zawadi ni nani kwetu?, unamjua Baba yake vizuri wewe? Unajua historia ya Malindi?” Mama Saleh aliorodhesha maswali kedekede. Yote hayakumuhusu Saleh ila yalimuhusu yeye mwenyewe kuyatolea maelezo ya kina.

“Mama unaongelea nini?”. bado Saleh hakumwelewa Mama yake.

“Naongelea mdomo!!... khaa!, Zawadi sio aina yako!, utakufa mwanangu. Na punde tu anaolewa na Ibo huna taarifa?”

“Ibboo!!” Saleh sasa akakunja ndita. aliguswa na taarifa iliyomchanganya ubongo.

“Kelele we mtoto!!” Mama Zawadi alionesha kukerwa mno na kitendo cha Saleh kuongea kwa nguvu. Saleh hakuweza kabisa kupunguza sauti. alilipepesa domo kwa sauti ya Mushki. Mama yake alikuwa anamchanganya.

“Mwanangu!, hujui mengi katika hiki kijiji, ngoja nikujuze leo. Alafu wewe ndio utachague usuke au unyoe.” Alimweka sawa mtoto wake na kisha kuendelea.

“Si unajua kuwa huyu wa Sasa sio Baba yako mzazi!!?” Mama Saleh alishaanza kazi. Alianza kumpa muweweseko mwepesi kurahisisha Saleh kuelewa somo.

“Ndiyo uliniambia”
"Na je unajua wewe sio mtoto wangu wa kwanza una kaka yako marehemu?”
“Ndio pia najua!”.

“..Sasa mwanangu, ipo hivi, kwanza nikuombe, vumilia wewe kama manaume kwa yote nitakayo kuambia leo, vumilia, vumilia sawa baba!” Mama Saleh akamshika bega mtoto wake na kuendelea. alianza kumwaga mchele sasa.

“Saleh wewe na kaka yako mmeshea wazazi kwa maana Mama mmoja na Baba kutoka uzao mmoja. Kipindi hicho kabisa cha mwanzo kipindi mimi bado mbichi kabisa, msichana mdogo sana nilikuwa Nakaa nyumba moja hivi karibu na kasri ya Mtukufu Mfalme wa kwanza ambaye ni Baba wa Mflame huyu. Mfalme huyo alikuwa anatambulika sana kwa jina la Bana. Sio Bana huyu mzembe, alikuwa Bana mwenyewe. shupavu, jasiri na mpenda haki. binadamu mapungufu lazima....

Basi mwanangu, kuna siku nilipata mwaliko wa kuwa kati ya wasichana ambao natakiwa kuelekea chumbani kwa mfalme kupamba na kufanya usafi. Nilifanikiwa kuingia salama kabisa, tena kwa kujitapa kuingia katika chumba cha mfalme. Lakini sikutoka mwenyewe mwanangu, niliinga mwenyewe na kutoka na kaka yako.

Hakuna anayepinga kuwa Mama yako nilikuwa mzuri. Nilikuwa mzuri zaidi ya Zena. Mimi nilikuwa mzuri kwa ndani na nje pia. Uzuri wangu ukawa kivutio kwa mfalme. Akatumia fursa hiyo kunitamani. Sikuwa na nguvu ya kukataa penzi la mfalme. Japo ndio ilikuwa mara ya kwanza kufanya mapenzi, lakini nilivumilia mwanangu. Mfalme akaharibu usichana wangu siku hiyo. Kwa kuwa ndio kwanza nilianza kushuhudia radha za mapenzi na utamu wake, nikanogewa hata kurudi tena siku aliyoniitaji. Alinihaidi kunipa vingi sana mwanangu. Mama yako nikawa tajiri wa mawazo, maskini wa kujiongeza.

Kama zilivyo mbio za sakafuni!, hatimaye nikafika katika kitovu cha ukingo. Mama yako nikashika mimba. Ikawa siri kati yangu na mfalme, kwa kuwa mfalme pia alikuwa na mke mwingine ambaye tayari alishamzalia mtoto wa kiume ambaye ndiye Ndiye Bana huyu wa Sasa. Na kutokana na taratibu za kifalme kuwa Mfalme atakiwa kuwa na wanawake zaidi za watatu ikawa tataizo kwangu. kwani tayari alishatimiza idadi hiyo mapema sana. Akanitorosha na kunipeleka mbali sana na kunishauri niitoe mimba hiyo. Nikamuaidi kufanya hivyo. Tukahama na Mama yangu mzazi na kuishia mbali. Tuliishi karibu na msitu wa Malindi. Sikufanikiwa kutoa mimba ya kaka yako. Nilizaa. Baada ya kuzalishwa na Mama yangu nilimpoteza, yeye alifariki huko. Mama alifariki na kuniacha na Kaka yako. nilijifungua nikiwa bado mdogo sana.

Basi nikalea mwanangu weee!, hadi akawa mtu na miaka kadhaa. Mwanangu alikuwa mzuri sana katika uwindaji. Alikuwa mzuri katika kufanya mawindo ya kila mnyama. Kwa tamaa za kuiona Malindi, tukahama mimi na mwanangu na kuja katika kijiji hiki nilicho kimbia mwanzo. lakini hatukusogea karibu na kijiji. tulikuwa mbali kidogo.

Mwanangu, shughuli za hapa na pale zikaendelea. Mama yako bado nilikuwa mzuri, bado nilikuwa naita, bado nilikuwa nakipaji mwanangu. Mwanangu. Mimi nilikuwa mwimbaji na Mchezaji mzuri sana hapa kijijini. Nashukuru kipindi hicho nahamia hapa. Tayari Mzee Bana alishafariki ambaye ndiyo baba wa kaka yako. Alifariki bila kumwona mwanaye. Kufa kwake kukawa nafuu kwetu kwa kuishi kwa amani hapa Malindi. Tayari utawala alishaushika huyu Mtoto wa Mfalme Bana. Huyu alikuwa kinyume cha baba yake. Ni muuaji, katili na mnyanyasaji sana.

Naam yakaanza kutokea mashindano kadhaa ya uchezaji na Uimbaji Malindi. Nikaibuka mshindi, yakatokea tena mengne nikaibuka mshindi. Nikawa mshindi wa jumla wa zama zile. Nilikuwa moto mwanangu kushinda huyu Zena. Hakuna aliyetia guu kwangu, niliwamwaga kama kenge wa maji machafu. nani asinipende Malindi na mtoto bado nilikua naita?,....!

ITAENDELEA Episode 5..…

Starxav
 
Mtunzi: XAVERY LUOGA
Simulizi:“PENDO HURU’
Namba; 0672493994
@Star_xav

EPISODE 05
Naam mwanangu, yakaanza kutokea mashindano kadhaa ya uchezaji na Uimbaji Malindi. Nikaibuka mshindi, yakatokea tena mengine nikaibuka mshindi. Nikawa mshindi wa jumla wa zama zile. Nilikuwa moto mwanangu kushinda huyu Zena....

Kama kawaida ya maskini kuwa ananyang’anywa kila kidogo alichokuwa nacho. Kushinda kwangu kukawa mvuto kwa mtukufu Mfalme ambaye kwa muda huo kama ningebahatika kubaki katika kasri kipindi cha baba yake basi angeniita Mama. kwa kuwa nilisha zaa na Baba yake.

Basi pale, akanialika nikaburudishe katika tamasha lao la utamaduni. Ilikuwa usiku mwanangu. Nikashindwa kutoka mwenyewe kwa sababu ya giza. Nikalala na mfalme. Mwanangu mapenzi ni uchizi sana, nilijisahau mimi mwanangu. Tukalala wote usiku mzima. Siwezi kumzushia kuwa alinilazimisha hapana, kwani ndio ya Mfalme ni ndio ya watu wote. Tukalala wawili na Mungu akatuongezea mtu mwingine. Kwa maana tuliamka watatu siku hile. Hiyo ndio siku ambayo ulipatikana wewe Saleh. Saleh wewe ni mtoto wa kwanza wa Mfalme Bana, na ni mtoto wa kwanza na wa mwisho wa kiume kuwai kupatikana katika uzao wake. Lakini hakujui baba yako. Mfalme hakujui kabisa yani... hajui. ngoja tu niseme sa nitafanyaje ?.

Saleh naomba nisamehe sana kwa kutokuambia ukweli kuhusu baba yako toka mwanzo. Mda wa kumjua Baba yako ulikuwa bado haujatimia. Lakini sasa nipo kwako kuomba samahani!, mwananu wewe ni mtoto wa mfalme.” Mama Saleh alikohoa kidogo kwa aibu na kumwangalia mtoto wake ambaye alikuwa amejawa na hofo ya mawazo tu. Alikuwa ameduwaa mno kwa simulizi hiyo kutoka kwa Mama yake. Saleh hakuonesha sura ya uaminifu hata kidogo.

“Chanzo cha wewe kutokuwa karibu na baba yako ni kuwa, Baba yako kwa wakati huo alifungiwa kuwa na mtoto wa aina yoyote, Malindi inasheria zake kali sana. zimewekwa kama laana. ole wako uvunje. mfalme alishavunja kwa kulala na kijakazi mimi. nilimpunguzia heshima ya kuendelea kulinda siri, hivyo bila kujua ni aina gani mtoto niliyenaye tumboni mwangu alinitafuta kunitokomeza. eh ! lazima nitokomee nani wa kufa kati ya mimi na mfalme??. Hivyo nikakimbia nawe mbali. tena mbali zaidi ya mwanzo nikisongana na ujauzito wangu.

Kwanza kabla hapo Saleh!, wakati bado sijaanza hata kugundua kama nina ujauzito. Kulitokea tatizo katika msitu huu wa Malindi kulisemekana eti kuna mnyama wa ajabu ametokea na kuwatafuna wanakijiji. Akatafutwa mtu ambaye anaweza kupambana na mnyama huyo. Wakaitwa wawindaji wote Malindi, na mwanangu ambaye ni kaka yako hakukosa. Alikuwa mmoja wao. Basi wakatumwa kupambana na mnyama huyo. Mwananguu!, hiyo pia ikawa siku yangu ya mwisho kuonana na kaka yako. Zilikuja tu taalifa kuwa mashujaa wote walioenda kupambana na mnyama huyo walikufa. Walikufa wote yani. Lakini walikufa likiwa tatizo limetatuliwa. Mnyama huyo wa ajabu walisema tu naye amekutwa amekufa kando ya mashujaa hao. Nikamsahau mwanangu. Ndipo hapo nilipokuja kugundua kuwa nina mimba yako mwanangu. kaka yako nilimpoteza angali yu mdogo bado. sijui nani alimuingiza katika mchezo mchafu mwanangu.

Nimekulea kwa siri sana mwanangu. Hadi unakuwa mkubwa hivi. Mfalme ameshanisahau, ni kipindi kirefu sana toka tutengane. Hana kumbukumbu kuhusu mimi kabisa, zilishapotea. Kwa tamaa zake za wanawake wengine, kila aliyemzalisha alimuua kabla ya kujifungua.

Sasa mwanangu nilikuwa sipendi nikuambia yote haya kwa kuwa kwa sasa naona ukaribu wako na Binti wa mfalme utasababisha mengi sana. Sasa ni juu yako unyoe au usuke.” Mama Saleh aliishia hapo. aibu aliyo nayo ilianza kupotea taratibu... ama kweli mama ni mama, akitenda kosa, hakosi kujisafisha.

“Kwahiyo Mama! Mimi na Zawadi ni ndugu?” Saleh akanyong’onyea kwa historia hiyo. Aliambiwa mazito mno. Ukubwa wake ukamfanya avumilie. Hakutaka hivyo vyeo vya Baba yake. Alilia tu penzi lake basi. bado aliuliza kuhusu Zawadi.

“Hapana mwanangu!, Zawadi si Mtoto halisi wa Mtukufu Mfalme!. Mke mkubwa wa Mfalme ambaye ni Mama Zawadi, alizaa nje ya Mfalme. Alizaa na mlinzi wa mfalme. Ila ameiba tu uzao huo ili asiachike. Hili jambo tunajua wachache sana, watu wa kufuatilia mambo. Na hata ukisema sasa hakuna atakaye kuelewa kwa sababu ushahidi wote umeshatengenezwa kwa kuamisha uma kuwa mtoto Zawadi ni wa kwanza kwa mfalme.

Kwa upande wa mfalme anawatoto wanne hadi sasa wote wa kike. Na anawatoto wawili nje ya kasri ambao alizaa na mimi. Toka awakane watoto wangu, bado analaana ya kutozaa mtoto wa kiume, na kwa umri wake hadi sasa ndio hawezi kuzalisha tena.

Hupo huru kumpenda Zawadi lakini siri hii weka moyoni. Wewe ndio uchagua mbichi na mbivu.” Mama Saleh alimaliza kwa kuinuka na kumwacha kijana wake katika fikra nzito. Alikuwa na lundo la maswali la namna ya kufanya. Mama alimwaga tope la utelezi, akamwacha kijana wake ajifunze kubalansi miguu yake tope lisimwangushe...

“Mzee Bana ni baba yangu?” Saleh alirudia rudia tu maneno hayo. Alirudia hadi akiwa usingizini. Ndoto zote za siku hiyo zilikua za kweli. hakulala Saleh.

******
Kwa kweli Malindi inahistoria nzito sana. Ni siri nyingi mno zimejificha kando ya utawala huu. Wanaojua ni wachache na ndio hao wamekaa kimya. Wamekaa kimya kwelikweli. Kimya kabisa hawataki kufichua uozo. Hata mambo yanayoendelea katika Msitu wa Malindi. Ni mauaji ya watu wanaojalibu kupinga sera na sheria au kumpinga mfalme moja kwa moja. Watu waliteketea kwa siri sana.

SEHEMU YA NNE

Malindi ilikuwa kimya kidogo kutafakari hali ya mji, wakazi wake hususani vijana walikuwa bize kujichua haswa lengo ni kuhakikisha wanaibuka kidedea katika mashindano ya utamaduni ambayo siku zake zilikuwa usoni. Zilishakatika siku. Hazikuwa na wakumsubiri. Mbio kukimbia mbele zikasonga.

“Atepetepetepee tetete te, atepetepetepee pepepe,” Ilikuwa ni ngoma ambayo ilimpeleka Zena kila pande ya dunia. Aliviringa vizuri kiuno chake bila haya mbele ya rafiki zake, wote walikuwa hawana akili mbele ya ngoma. Walichojua ni kufuata ala na kutikisa kila kinachotikisika. Walikuwa wehu wa mdundo.

Zena alikuwa kiongozi kwa kupiga makofi huku nyonga yake ikifuata mawimbi ya sauti. Walikuwa watatu tu lakini walitosha kabisa katika kusherehesha furaha yao. Mmoja alikuwa mpigaji ngoma kwa ustadi bila kujali mpasuko wa sauti kuelekea mbali, wa pili alikuwa mwoga wa kuonesha kipaji chake hadharani mbele ya rafiki zake wawili. Wa tatu alikuwa funga kazi. Alikuwa chizi Zena.

Yeye alitamani kuimba Malindi yote isikie, alitamani acheze hadi bahari zote zikunyanyike kumtazama. Hakujali umbali na kikomo cha sauti yake. Aliimba kwa sauti kushindana na sauti ya ngoma. Achana na aina ya mauno ambayo Mama Zena alitumia dekania nzima ya maisha yake kumfunza. Hayakuwa mazoezi tena. Yalikuwa ni maandalizi ya vita vya Malindi. Ama Zena ni mshindi bila kushindana..

“Zenaa... Zena Dada!, Sikia nikuambie!” Yule mwingine aliyecheza naye alimtaka Zena kutulia, lakini jitihada zake hazikuzaa matunda. Akatoa mguu wake hadi kwa mpigaji ngoma. Akamsimamisha!.

“Da Zenaa!, Mda umeenda.!” Alilopoka na kusubiri shali ya Zena.

“Looh! Chevuu! Nawe piga ngoma bhana!” Amri ikatolewa. Hakuna wa kumpinga zena, mpigaji alianza tena kuungurumisha.

Aliyesitisha kuendelea na ngoma akanyonga midomo yake kwa kuchukizwa na maamuzi ya rafiki yeke huyo. Akajimwaga chini ‘puuh!’ akatulia.

“Lakini acha Tui, acha tuwai.. nimekumbuka kitu”. Zena akatoa tena amri ya kushitisha kwa ngoma hiyo. Tayari hamu ya kucheza ilishamtoka. Akawa mpole ghafla.

“Na hapo huna mume. Ukiwa naye si utatuchicha sote hapa Malindi!” Aliyekaa akatoa dongo kwa Zena. Akalipotezea jicho la Zena lililo kali kama pilipili. hakuna na utani Zena kwa muda huo.

Zena alimkata jicho rafiki yake kwa kuongea jambo ambalo hata yeye alikuwa analifikia mda huo. Saleh alimuingia kichwani Zena. Alitaka kumuwai sehemu ambayo Saleh anakuwepo kwa mda huo. Haraka wakabeba ngona kuelekea kusini. Tui na mwenzake walikuwa wakifuata oda tu. Hawakuwa na cha maana kwa mwamba huyo.

********
Safari yao ya pamoja ilikwama njiani punde tu walipofika eneo la tukio.

“Nyie nendeni”. Zena alitoa amri pasi kutaka maswali kutoka kwa wenzie. Macho yake yalikuwa hayajatulia kumtafuta mpendwa wake Saleh. Alijua wazi kuwa yupo kukabiliana naye. Hakupoteza mda. Akawatoa wenge wenzake kwa kuwakimbiza makwao. Naye akachochora upande wake.

“Saleh!” Sauti ya kubashiri ilitoka kwa Zena kumwendea kijana aliye na jaba la mawazo pembezoni mwa jiwe. Hakukosea Zena alikuwa ni Saleh.

“Zena!” Saleh akaitika wito ule kutoka kwa Zena. Wote wakatazamana. Ikawa fursa kwa Zena kujitokeza kimahaba kwa Saleh. Akasogea Zena.

“Saleh!” akaita tena. Alishakuwa karibu ya Saleh tayari. Akaanza kujinyonga nyonga Zana. Alitamani kitu kutoka kwa Saleh. lakini aibu ilimshika. haikutaka kumwacha.

“Ndio Zena niambie!”
“Unajua nini Saleh?” Zena hakuwa na neno la zaidi. Alijikwatua tu hadi kumfikia Saleh karibu na mdomo.

Midomo wa Saleh na Zena ikawa karibu Zaidi. Harufu ya kubarehe ikatalii katika macho ya Saleh. Bila hiyana barehe hiyo ikaacha mabaka ya muhemuko wa hisia. Macho ya Saleh yakajifunga tu yenyewe. macho ya Saleh yalikuwa kama boneti bovu la gari aina ya Toyota, likabamiza nyuzi za chini ya jicho. likafumba kabisa.

Zena sasa akaanza kutumia fursa ambayo Mungu Baba wa Mbinguni amemtunuku. Alitaka kumaliza kila kitu siku hiyo. Alitaka kumuonesha sababu ya kuolewa naye kwa asilimia mia moja, hii ni mbinu ya kivita, hakuchomoka Saleh, akabaki kuganda kwa Zena.

Zena akaanza fujo za kupapasa ulimi wake kando ya lipsi za Saleh. Alifanya hivyo polepole huku akiruhusu sekunde nyingi kupotea. Hakuchelewa Zena. Tayari mdomo ulishajaa maji. Maji ya uhai. Maji ya Ushindi. Mdomo ulikuwa unatafuta sehemu ya kuyamwaga maji hayo. Na sehemu sahihi ikapatikana. Saleh alikuwa kama mwenda wazimu. Aliruhusu hisia kumtawala mwili mzima. Alikuwa bwege kwa mda. Anawezaje kuchomoka kwa Malkia wa mapenzi kama Zena?. Hakuna na Sababu ya kukataa, alishashika pabaya Saleh. Alikua anatetemeka tu.

ITAENDELEA Episode ya 6…
USISAHAU KUACHA LIKE NA KOMENT ILI TWENDE SAWA...
Xavery Luoga.

Starxav
 
Mtunzi: XAVERY LUOGA
Simulizi: “PENDO HURU’
Namba: 0672493994 (Sap)
@Star_xav

EPISODE 06
Zena akaanza fujo za kupapasa ulimi wake kando ya lipsi za Saleh. Alifanya hivyo polepole huku akiruhusu sekunde nyingi kupotea. Hakuchuchelewa Zena. Tayari mdomo ulishajaa maji. Maji ya uhai. Maji ya Ushindi. Mdomo ulikuwa unatafuta sehemu ya kuyamwaga maji hayo. Na sehemu sahihi ikapatikana. Saleh alikuwa kama mwenda wazimu. Aliruhusu hisia kumtawala mwili mzima. Alikuwa bwege kwa mda. Anawezaje kuchomoka kwa Malkia wa mapenzi kama Zena?. Hakuna Sababu ya kukataa, alishashikwa pabaya Saleh. Alikua anatetemeka tu.
Zena hakuishia hapo, akaanza kutalii ulimi wake ndani ya mdomo wa Saleh. Kazi na dawa. Zena hakuacha kunogesha na miguno ambayo alifundishwa tayari na Mama yake mzazi. Alikua anatoa sauti za mahaba Zena.
Bado hakuchoka Zena tayari mkono wake wa kushoto ukashika vizuri shingo ya Saleh. Wa kulia nao haukubaki nyuma, ukaanza kushuka taratibu kuanzia kifuani mwa mwamba huyu aliyekamatika, ukashuka kiunoni mwa jemedari dhaifu. Hatimaye ukaishia katika sehemu nyeti za Saleh.

Nani hapendi raha!. Hakuna. Tayari Saleh alishaama dunia. Kila kitu mwilini mwake kilipata joto. Mishipa ikamsimama kama Treni la vyuma libebalo mizigo. Alikufa oza Saleh. Akajikuta na yeye anatoa ushirikiano usio wa lazima. Mikono yake ikaanza papasa taratibu sehemu za mwili wa Zena ambao ulikua hauna stracture inayotakiwa kwa wakati huo.

Kiuno cha Zena kilijawa na mji mzima wa mwanza. Tayari daladala ilishafika nyegezi. Dereva alibisha honi tu habiria washuke. Japo walichelewa lakini walifika salama. Saleh alikamata vyema kiuno cha Zena. Akajisahau kwa kuzikamata tu shanga za Zena. Zena akabinuka kidogo kumbana zaidi Saleh. Inaonekana wote walikuwa wanaumri mmoja. Walifanana vimo. Kiuno cha Zena kikawa sawasawa kabisa na kiuno cha Saleh. Zena akijiongeza kwa mubadilisha miguu, aliinua wa kushoto kwa sekunde moja akahisi umechoka, akabadili wa kulia. yote kumtega kijana wa watu mgeni kwenye mji huo. Mchezo ukaendelea hadi kipindi cha pili.

Naaam! Nani awezaye kuua Nyoka kwa fimbo ya mbali!!!... Hakunaaa!. Zena alikuwa mjanja sana katika mambo hayo. Alimnyanyua Saleh hadi kufika katika jiwe lililopo karibu yao. Akajiegesha juu ya mwili sa Saleh, yeye akiwa juu, mpumbavu mwenzake akiwa chini. Wote wakiwa wapo mbali mno. Walitembea pamoja siku hiyo. Hatua kwa hatua kumaliza nyanda za juu kusini.

Sikupata kuyasikia vizuri mapigo ya moyo wa Zena, mapigo yake ya moyo yalizibwa na mihemo aliyokuwa anatoa kwa ustadi, alikuwa anapokezana ala za sauti tu, toni ya juu ikipana basi ya chini inapokea. Nakumbuka zena alikuwa bingwa wa kuhesabu. Shule ya Malindi ilimsomesha vizuri. Alianza na A akaja E, I ikafuata. O ikawa kitivo cha kupanua mapaja wake. Alipofika U, akarudisha irabu hizo mwanzo hadi kufika tena A. Zena alikuwa analia.

Nisiwe mwongo, mapigo ya moyo ya Saleh ndiyo yalikuwa yanasikika Malindi nzima. Moyo ulijawa na sherehe ya kufurahia miundo mbinu ya Zena. Hali ya kuwa mwili wa Zena haukuvikwa nguo sehemu zote, ukafanya joto lake limchome Saleh. Akaungua. Akawa hatihani kupoteza uhai. Alikuwa na ugonjwa wa moyo Saleh. Saleh ninaye mjua mm tayari amekufa katika vita vya mapenzi ya kale.

Basi zoezi likawa mbali sana. Saleh alisi ameshajitolea haja ndogo tayari. Kwa maana angaika angaika ya Zena kwenye ikuru yake ilizidi mipaka. Aliapata muwasho wa mahaba. Alikuwa anataka kitu Saleh. Kitu ambacho hakuwai kupata katika maisha yake zaidi ya kusimuliwa tu na Sadiki.

Hapa na hapa hapa na pale, ukatokea mshituko!, kuna mtu alishuhudia mtanange huu. Tena bora hata angekuwa Mama na Saleh! Ah! Wapi?, anapata wapi nguvu za kutembea mbali kote huku?. Sio yeye.!. Alikuwa mtu haswa. Mutu wa mutu wake.

“Saleh!!!!!” akaita kwa mshtuko. Ilikuwa Sauti ya Mtoto wa Mfalme, si mwingine bali ni Zawadi. Alipenyeza katika maeneo hayo kwa lengo la kumuona mwandani wake ambaye siku hiyo kuna ujumbe alimbebea.

Zawadi alikuja kumwaga ukweli wa pendo lake la dhati kwa Saleh. leo aliamua kufunga kazi kuja kuvunja miiko ya Malindi. alikuja kumwambia ukweli Saleh ni jinsi gani anateseka juu yake. Alikuwa na nia ya kuonana na salehe siku hii. Na kweli alimuona. Alimuona akimsaliti mbele ya macho yake mawili. Zawadi hakuna na la msalia mtume. Hakutia neno pale. Mbio zikamkimbiza kuelekea kwao. Akawaacha na butwaa lao la kustukiwa. Aibu ikamjaa Saleh. Alikosea. Tena Alikosea mno, fungu la kumi la kutoa kanisani, alinunulia mchanga wa kutengenezea sanamu. la nini sasa ?!.

“Bebii!” Zena hakuonesha kujali hali hiyo, hali ambayo ilikatishwa na binti wa mfalme. alitaka amalizie hamu zake zote alizokuja nazo siku hiyo. Lakini alikosa ushilikiano kutoka kwa Saleh. Alishabadilika Saleh.

“Saleh mbona hivyo!” ilikuwa ni sauti ya mahaba mazito kutoka kwa Zena. Hakuambulia chochote kile kutoka kwa Saleh. Saleh aling’ang’ana kuchomoka mahali pale.

“Zawadii!” akaita Saleh!, lakini wapi, alishapotea Zawadi. Zimwi la mapenzi likamtoka Saleh akaweka sawa ikuru yake isidondoshe chozi lingine.

“Buanaa!!” Zena hakutaka kabisa kusikua la mkuu, akashinikiza kumzuia Saleh. Saleh ambaye hakuwa tena mahali pale. Alishahama kitambo tu.

“Niache Zena!, Nini hiki?” Saleh alihoji kana kwamba alikuwa mgeni maeneo yale. Alikuwa kama mtu aliyezinduka toka usingizini. Lakini kama ilivyo kwa mtaka cha uvunguni. Zena akazogeza tena domo lake kinywani mwa Saleh. Mungu akamwonesha upepo wa kufumba macho akafumba macho Zena. Alijua bado Saleh yupo mikoni mwake. Hapana!, hapana, Saleh hakuwa kwake tena. Alishateleza.

“Paah!” kilikuwa ni kibao ambacho kilikusanya Nyota zote za Malindi na kuzipeleka akilini mwa Zena. Zena hakuona mbele kwa sekunde kazaa. Akajichomoa mikononi mwa Saleh kwa kujiweka imara asidondoke. Baada ya sekunde akakaa sawa. alisubiri kwanza harufu za kofi hilo zimwingie vizuri ndipo aanguke na kilio.

Akagundua alipigwa kibao na sio ngumi. Kilio kikachukua nafasi. Alilia Zena kwa maumivu mazito yaliyomkuta. Just imagine inapigwa kofi na mkulima mabaye kwake yeye jembe ndio kitega uchumi chake! Utatoka salama kweli?. lazime hkimbilie hospitali ya mkoa tena ukiwa na bima ya miaka mi tano ya matibabu.

Baada ya wenge la Zena, Saleh alikimbia kule alikoelekea Zawadi. Alimuwahi kumweleza ukweli na si kile alichojionea. Lakini hakukuta mtu Saleh. Tayari Zawadi alishafika alipoeenda. Hakuna na chaguo lingine Zawadi. Alishaweka tiki kuwa Saleh sio wake tena.

Saleh akamkosa Zawadi na kurudi nyumbani, alimwacha zawadi augue na donda la maumivu. Alichanganya mambo siku hiyo. Alikutwa katika mda mbaya sana.

Japo alimuwaza sana Zawadi lakini Zena naye akachukua nafasi. Aliwaza vitendo vile vigeni machoni pake kutoka kwa Zena. Saleh akalivulia kofia penzi la mwanzo la Zena. Lilimkalibisha ujanani akiwa na akili timamu..

“Saleh nini baba!” Mama yake akamshitua, akamtoa kabisa mawazoni.

“Hamna mama. Najiskia hovyo!”

“Ah!, pole baba eh!, kapumzike mwanangu. Usiwaze sana niliyokuambia mwanangu. Chukulia kawaida sawa!. Pole sana Saleh!. Aya nenda baba.”

Mama Saleh alijua Saleh yupo katika wakati wa kuwaza yale aliyomwambia. Alijua fika yatamuumiza kichwa lakini Saleh yeye alikuwa na yake. alimshika Zawadi mkono wa kulia na zena wa kushoto.

Mama akamchukua mtoto wake toka nje alikokuwa nawaza na kumsindikiza hadi ndani. Alipoingia tu ndani Salehe, na Sadiki naye akatia timu. Alifika kumwona rafiki yake kipenzi. Moja kwa moja akapitiliza hadi ndani baada ya salamu jambo jipya likatokea….

*********
ITAENDELEA Episode ya 7
KOMENT YAKO MUHIMU...

Starxav
 
Mtunzi: XAVERY LUOGA
Simulizi: “PENDO HURU’
Namba: 0672493994. (WhatsApp)
@Star_xav
EPISODE 07
Akamchukua mtoto wake toka nje alikokuwa nawaza na kumsindikiza hadi ndani. Alipoingia tu ndani Salehe na na Sadiki naye akatia timu. Alifika kumwona rafiki yake kipenzi. Moja kwa moja akapitiliza hadi ndani baada ya salamu… jambo jipya likajitokeza...

***********
Mbio za Zawadi zilimfikisha hadi mikononi mwa mama yake. Alishindwa hata asimulie nini kwa kile ambacho alikiona. Machozi na sauti ya kilio vilimwogopesha Mama yake. Akataka kujua kulikoni!.

“Kulikoni mama?” akauliza.

“Ma… maa maamaa! Mama mi ni… me… ku… bali…, nimekubali kuolewa na Ibo mama!.” Jambo jipya likabeba nafsi ya Mama Zawadi. eti mwanae amekubali kuolewa na mtu asiyempenda.

“Na kwanini unalia?”. Swali likaja mbele ya Zawadi. Akashindwa kujieleza. Akamung’unya tu maneno.

“Mama… Saleh!.. yoyoyooo jamani!!!!” Alilia Zawadi. Tena alilia kilio cha mbwa. Aliumia sana kwa kitendo alichokutana nacho. Tamaa ya mapenzi na Saleh itatoweka ghafla.

“kafanyaje??, Wewe!!” Mama Zawadi alimtikisa bintiye bila kujali kilio chake. Alitaka sababu ya kupelekea kumliza namna hile.

“Mama Saleh ana mwa-namke!. Kumbe anampenzi mda mrefu tu na hata!, hata mama hakuwai kuniambia! Huwiiiii!” alilia Zawadi.

“Mwanamke?, yamekukutaje haya yote hadi ujue hilo?, umesimuliwa??” alihoji mama.

“Mhhhhhh Ma.. kusimuliwa!” Zawadi aliruka juu kupinga kauli ya mama yake. Wenge la mapenzi bado Lilikuwa linamuandama. Akaendelea kutamba.

“Nisimuliwe na nani Mama!” akapunguza sauti Zawadi. Akaacha kulia ghafla. Akatamka jina la adui yake.
“Mama kwa macho mawili. Saleh huyu hapa, Zena huyu hapa. Wanafanya mapenzi!” aliwehuka Zawadi.

“Ati nini???”
“Eh!”
“Zena huyu mwanachakalamu???”
“Kwani kuna Zena wangapi hapa Malindi?”
“Ndi'o wanafanya mapenzi?”

“Unamuuliza nani sasa??” Zawadi na Mama yake waligawana uchizi, wote walijikuta wanachoshwa na suala kama hilo. Hawakutarajia kabisa kama jambo kama hilo linaweza kutokea.

“Sasa!”
“Sasa nini Mama!!!!, mimi sitaki uwiii, sitaki mimi tena. Simtaki Saleh. Nenda haraka mwambie Baba nimekubali.. nenda Mama!”

“Zawadi unahakika au ndio hasira!”

“Khaa!, hunielewi mama?” Zawadi alikuwa kweli anamaanisha. Hakutaka kuwasumbua wapenzi hao wapya. Akawaacha waburudike na mapenzi yao hadharani. Akatafuta uelekeo wake. Akasahahu kuwa Pendo la huru linasubiriwa na uvumilivu. Halifi pendo la kweli.

Ni kweli kabisa Zawadi hakuwai kuwa na mahusiano ya kimapenzi na Saleh lakini moyoni mwake alishaamini kuwa Saleh ni mtu pekee na muhimu sana kwake. Alikadhalika kwa Saleh naye vivyo hivyo. Waliishi kupendana moyoni tu, huku kila mmoja akiumia kivyake bila kuambiana ukweli. Zawadi akakata tama na kufanya maamuzi ya hasira ya kutamka kuwa yupo tayari kuelewa na mtu ambaye amepangiwa naye. Yalikuwa ni maamuzi ya hasira kutoka kwa Zawadi. Hakuangalia moyo tena. Moyo ulimsaliti. Akautupa kando.

*******
Ndani ya chumba cha Saleh ikaota soga. Hii ni mara baada ya Sadiki kuwasili. Wote wawili walijiunga katika dimbwi la maongozi hawakufichana vitu wawili hao.

“Kaka! Hmmm leo mimi sina maana kabisa!” Saleh alianzisha mazungumzo ambayo yalimkuta bado Sadiki amesimama kando ya kitanda cha kamba cha Saleh.

“Kwanini wasema hivyo kijana!” Sadiki akaitika wito huku akijivuta kando ya kitanda hicho na kuweka makalio yake.

“Kaka nimekosa tumaini langu la kila siku. Leo mimi Saleh nimeonja uchungu wa mapenzi. Najuta!” aliongea tena fumbo lililomfumba Sadiki. Akabaki kuduwaa tu sadiki.

“Kaka leo Zena katokea wapi. Alinikuta kwenye lile jiwe kando na bustani. Sijui hata alinipa nini kaka!. Nililegea huwezi amani. Amenichezea sana Zena leo!” aliweka wazi sasa.

“Oooh! Hahaha wacha we!” akanogesha Sadiki.

“Kaka! Nilikuwa sio mimi. Na tena hata bora ingekuwa siri,. Kaka nimekutwa na Zawadi nikifanya huo ufuska!.”

“Zawadi tena?”
“Ndio!, alipita maeneo yale alinikuta tumekumbatiana kabisa na Zena na tunafanya yetu!. Haikuwa dhamira yangu kaka. Nimeshampoteza”

“Daaah!, Zawadi huyuhuyu Shemela?” aliuliza kwa utani Sadiki lakini hakuonesha kama ni hali ya utani.

“Zawadi Binti Mfalme!!, kwani wapo wangapi?”.
“Sasa ikawaje?”
“aliondoka tu kwa hasira. Nilimuita sana, hakugeuka hata”
“Alikuwa peke yake?”
“Ndio!”
“Na huyo zena ikawaje”
“Hata linaelewa, aliendelea kunishinikiza tujamiiane pale hadharani, nikaona anazingua, nikamtia kofi” Saleh alinyanyuka kitandani na kuonesha ishara ya kupiga hewani. Sadiki alishituka.

“ulimpiga!!”
“Ndio!, anazingua bhana. Sijui aliniwekea vinini jamani. Yule mwanamke mchawi!”

“Sasa si umekosa vyote kaka!”
“Vyote? Nini na nini?”
“Hukupasa kumpiga yule mwanamke. Huzijui hisia Saleh. Zena pia anakupenda sana”

“Sadiki, nakuita kwa jina lako kaka. Hata Zawadi ananipenda na aliumia sana juu ya kitendo kile. Kama angekuwa hanipendi katu asingeumia na kuondoka vile. Angevumilia.”

“Dogo sikia. Hapa ukishangaa utakosa vyote. Niambie moja, nani unampenda tufanye mpango?”

“Zawadi!”
“Kama ni Zawadi basi mtafute, ongea naye. Mpange hata vya uongo. Ila sikushauri katika hilo. Maana inaweza kuwa tatizo kwako. Nasikia juu juu tu kuwa Zawadi alishakabiziwa kwa Ibo. Lakini kama upo tayari kufa juu yake sawa. Mtafute.”

“Daah! Kaka. Sina hisia juu ya Zena. Ilitokea tu bahati mbaya leo alinikuta nipo na mawazo. Nampenda Zawadi”

“Sawa fanya mtafute mapema kwa maana atakuwa karibu kukuchukia kwa kitendo hicho. Usipomtafuta mapema utatengeneza chuki juu yako na usimpate tena katika maisha yako.”

“Sawa kaka nimekuelewa!”

“Ko ndo leo umeonja vya mtoto mzuri Zena!.”

“Yaani kaka, nilijikuta nashika zile nyamanyama za kiunoni. Mtoto anagumia hadi dhambi. Sijui alikuwa anafanya kusudi. Hapa ninawsiwasi sijui kama nina mate kweli maana nilimimina yote kinywani mwa Zena” Saleh aliongea kwa vitendo. Alijaribu kutema chini kuona kama yapo kweli au la. Kitendo ambacho kilileta kelele chumba kizima. Walicheka na kutaniana sana. Sadiki alicheka ushamba wa Saleh katika mapenzi. Alijua kabisa rafiki yake huyo hajawai kugusa mwanamke katika barehe yake. Alikuwa bikra wa kiume Saleh!.

Mawazo hayakuwaisha. Waliendelea kujumuisha suala la mashindano ambalo liliamkia siku yake ya pili. Sadiki kama mmoja wa washiliki alikuwa anachukua Baraka za mwisho mwisho kutoka kwa rafiki yake huyo ambaye miaka yote amekuwa mstari wa mbele katika kufanikisha azma ya yeye kunyakua taji la kwanza.
Mazungumzo yalikuwa marefu mno yasiyo na mipaka…

..........

Naaaam, Zawadi rasmi kajikabidhisha kwa Ibo. Saleh matatani kusosa wote. Sadiki anakindumbwe ndumbwe cha kuwania taji la Utamaduni Malindi, Zena Mauno naye ni Mshiriki kwa upande wa wanawake... hii yote ni Episode ya 8.

ITAENDELEA…

Follow Me; Instagram, twitter, Facebook @Star_xav

Starxav
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom