Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,054
- 463,971
- Thread starter
- #81
SEHEMU YA 15
Nilishtuka sana, nilijiona kama mtu ambaye alikuwa kwenye mlango wa kuelekea kwenye mafanikio makubwa. Ile ilikuwa ni almasi, kipande kikubwa kabisa ambacho kama ningekiuza basi ningepata pesa nyingi mno na kuwa tajiri mkubwa.
Hii ilimaanisha kwamba ningechukua msichana yeyote ninayemtaka na kulala naye, ningenunua simu kubwa zaidi, kujenga nyumba ya kifahari na kukunua gari moja matata kabisa.
Nilifurahi lakini sikutakiwa kuwa na pupa, kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kutaka kumfahamu zaidi yule mzee, nilimfanyia utu, hii haikumaanisha kwamba nilitakiwa niachache naye kisa tu nimepata almasi.
Siku hiyo mchana nikaondoka na kuelekea hospitalini kumuona mzee huyo. Nilipofika hapo, nikakutana na manesi ambao walinipeleka mpaka kwenye chumba alichokuwa ambapo huko nikakutana na familia yake iliyokuwa na majonzi mno.
Kulikuwa na mwanamke mmoja mtu mzima ambaye nahisi ndiye alikuwa mke wake, mabinti wawili wazuri wa umri wangu lakini pia kulikuwa na kijana mwingine.
Nesi akanitambulisha kwao kwamba mimi ndiye niliyemuokoa kutoka kwa wauaji na kumchukua kumpeleka hospitalini hapo. Walifurahi na kunishukuru kwani mimi ndiye niliokoa maisha yake.
Niliwahadithia kilichokuwa kimetokea, walinisikiliza na kunishangaa, haikuwa rahisi kwa binadamu wa kawaida kwenda kumuokoa mtu kwa watu waliokuwa na bastola na wakati hakukuwa na kitu mkononi.
Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa urafiki wangu na familia hii, tuliendelea kuwa karibu na kukutana hospitalini hapo kuzungumza huku upande mwingine wa moyo wangu nikiwa na hamu ya kufahamu kuhusu yule mzee.
“Mimi naitwa Nurat,” aliniambia msichana mmoja miongoni mwa wale watoto wa mzee yule.
“Ulijitambulisha mule ndani!” nilimwambia huku nikicheka.
“Najua! Ila ninahitaji kukufahamu zaidi!”
“Naitwa Edward Francis! Nipo singo, sijaoa, sina demu, mpenzi wala mke,” nilimwambia huku nikitabasamu, akaanza kucheka.
Nilishtuka sana, nilijiona kama mtu ambaye alikuwa kwenye mlango wa kuelekea kwenye mafanikio makubwa. Ile ilikuwa ni almasi, kipande kikubwa kabisa ambacho kama ningekiuza basi ningepata pesa nyingi mno na kuwa tajiri mkubwa.
Hii ilimaanisha kwamba ningechukua msichana yeyote ninayemtaka na kulala naye, ningenunua simu kubwa zaidi, kujenga nyumba ya kifahari na kukunua gari moja matata kabisa.
Nilifurahi lakini sikutakiwa kuwa na pupa, kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kutaka kumfahamu zaidi yule mzee, nilimfanyia utu, hii haikumaanisha kwamba nilitakiwa niachache naye kisa tu nimepata almasi.
Siku hiyo mchana nikaondoka na kuelekea hospitalini kumuona mzee huyo. Nilipofika hapo, nikakutana na manesi ambao walinipeleka mpaka kwenye chumba alichokuwa ambapo huko nikakutana na familia yake iliyokuwa na majonzi mno.
Kulikuwa na mwanamke mmoja mtu mzima ambaye nahisi ndiye alikuwa mke wake, mabinti wawili wazuri wa umri wangu lakini pia kulikuwa na kijana mwingine.
Nesi akanitambulisha kwao kwamba mimi ndiye niliyemuokoa kutoka kwa wauaji na kumchukua kumpeleka hospitalini hapo. Walifurahi na kunishukuru kwani mimi ndiye niliokoa maisha yake.
Niliwahadithia kilichokuwa kimetokea, walinisikiliza na kunishangaa, haikuwa rahisi kwa binadamu wa kawaida kwenda kumuokoa mtu kwa watu waliokuwa na bastola na wakati hakukuwa na kitu mkononi.
Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa urafiki wangu na familia hii, tuliendelea kuwa karibu na kukutana hospitalini hapo kuzungumza huku upande mwingine wa moyo wangu nikiwa na hamu ya kufahamu kuhusu yule mzee.
“Mimi naitwa Nurat,” aliniambia msichana mmoja miongoni mwa wale watoto wa mzee yule.
“Ulijitambulisha mule ndani!” nilimwambia huku nikicheka.
“Najua! Ila ninahitaji kukufahamu zaidi!”
“Naitwa Edward Francis! Nipo singo, sijaoa, sina demu, mpenzi wala mke,” nilimwambia huku nikitabasamu, akaanza kucheka.
