Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 34,072
- 79,444
- Thread starter
- #21
NITAMLEA
Mtunzi, Robert Heriel
Chungu Cha 09
Usiku uliofuata Johari hakulala. Alikuwa analala huku macho yakiwa wazi, moyo wake ukiwa kama mtu aliyedondoka baharini bila kujua kuogelea. Ndani alimuangalia Neema aliyekuwa amejifunika kwa kitenge kilichokuwa kimetoboka huku akikoroma kwa uchovu wa mtoto mdogo asiye na makosa. Machozi ya Johari yalitiririka kimyakimya. Alihisi dunia imemchoka. Kila njia aliyojaribu haikufika popote. Alijitahidi, alihangaika, aliomba dua, alifanya kazi lakini bado mwisho wa siku anabaki mtu wa kudharauliwa na watu wa mtaani. Mtu wa kukosa hata chakula Cha yeye na bintiye.
Kesho yake hakwenda kuuza uji, hakuwa na mtaji tena. Hakuwa na hata mia moja. Alikaa ndani, akimwangalia Neema akichezea kijiti akisema anapika chakula. Wakati mchana unaingia, mwenye nyumba aligonga mlango kwa nguvu. “Johari, toka kabla sijaita mgambo! Siku zako tatu zimeisha!” alikoroma kama mbwa aliyekosa mfupa.
Johari alifungua mlango polepole, macho yakiwa yamevimba kwa kulia. “Baba mwenye nyumba… nisaidie wiki moja tu, wiki moja nipate pa kuhamia.”
Mwenye nyumba alicheka kwa dharau, “Hayo siyo maisha yangu dada, nachotaka ni kodi yangu! Ukishindwa… toka!”
Johari alifunga mlango huku akitetemeka. Hakuweza kula siku hiyo, wala hakumwandalia Neema kitu cha maana. Alimwekea maji tu na kipande cha maandazi kilichobaki kwenye chakula cha jana.
Wakati wa jioni, akaamua kutembea mtaani angalau apate mawazo ya Nini afanye. Wakati anakatiza mtaa wa pili, akamuona mzee mmoja amekaa chini karibu na duka la dawa, suruali yake ilikuwa imechanika, lakini uso wake ulikuwa na amani ya ajabu. Mzee alimwangalia Johari na akasema kwa sauti ya taratibu lakini yenye uzito: “Binti, hata mtu akizama baharini, ilimradi haujafa bado ana nafasi ya kuona pwani.”
Johari alisimama, akageuka. “Umesema nini mzee?”
Mzee akajibu kwa tabasamu, “Tumaini lipo. Jua linawaka hata kama mawingu yametanda. Ukiona kivuli, jua kuna jua nyuma ya giza.”
Johari hakujua kwa nini machozi yalibubujika. Alijikuta amekaa karibu na huyo mzee na kuanza kusimulia maisha yake yote, kuachwa na baba wa mtoto wake, kufukuzwa kazi, kufilisiwa mirathi, kupoteza kila kitu. Alimsimulia kwa machozi matupu. Baada ya dakika thelathini mzee akanyanyuka, “Binti nakuomba… kama bado unayo miguu ya kutembea na mdomo wa kusema… usikate tamaa. Nenda pale Kariakoo kona ya msikiti wa Manyema, kuna dada mmoja anatafuta mtu wa kufanya kazi ya usafi wa hoteli yake ndogo. Ni kazi ya jioni na asubuhi, unalala ndani na unapata posho ndogo lakini inasaidia.”
Johari hakuamini. “Una uhakika mzee?”
“Si lazima niwe na uhakika,” mzee akajibu kwa busara, “lakini tumaini halina gharama, jaribu.”
Johari alirudi nyumbani na Neema akiwa amebeba matumaini mapya. Hata kama yalikuwa madogo kama punje ya chumvi, moyo wake ulihisi joto jipya.
Alipoamka alfajiri, alienda Kariakoo kama mzee alivyomwelekeza. Alifika kona ya msikiti wa Manyema, akatafuta hoteli ndogo iliyoandikwa “Amani Lodge”. Alipofika, alimkuta mama mmoja mwenye umbo kubwa akiwa anapanga vyombo.
“Asalaam aleykum mama,” Johari alisalimia kwa unyenyekevu.
“Wa aleykum salaam, unahitaji nini?” yule mama akauliza kwa sauti ya amri.
“Nimesikia kuna kazi ya usafi hapa… natafuta kazi,” Johari alijibu kwa unyenyekevu mkubwa.
Mama wa hoteli alimkagua juu mpaka chini. “Una mtoto?” aliuliza.
“Ndiyo, lakini atabaki kwa jirani, sitaleta shida,” Johari alijitetea.
Baada ya ukimya mfupi, mama wa hoteli alitikisa kichwa, “Njoo kesho saa kumi na mbili asubuhi. Utaanza kazi ya kupiga deki na kusafisha vyumba vya wageni. Siyo kazi rahisi, lakini bora kuliko kukaa njaa.”
Johari hakuamini. Hakukumbuka mara ya mwisho aliambiwa ‘karibu’ kwenye kazi. Alimshukuru mama wa hoteli, akaondoka akiwa na mwanga mdogo wa matumaini.
Lakini aliporudi nyumbani, alikuta mwenye nyumba akiwa na watu wawili, mgambo. “Nimechoka na huyu mwanamke, leo anatoka kwa lazima!” Johari alilia, akaomba lakini hakuwa na msaada. Akapewa dakika ishirini kuchukua virago vyake. Alimfunga Neema mgongoni na kubeba godoro lake chakavu.
Wakiwa hawana pa kwenda, walilala kwenye kituo cha daladala ya Kinyerezi, kwenye benchi la mbao. Usiku ulikuwa na baridi, mbu walikuwa kama wanamla moyo wake. Lakini angalau alikuwa na matumaini kuwa kesho ana kazi.
Johari akajifunika na kitenge alichokuwa nacho, akamkumbatia Neema kwa nguvu huku machozi yakitiririka kimyakimya usiku kucha.
Asubuhi alijikaza, akasali kimyakimya, kisha akaelekea kwenye kazi mpya Amani Lodge akiwa na matumaini mepesi kama jani linalopeperushwa na upepo, lakini moyo wake ukiwa mgumu kama jiwe la kusaga.
*****
Siku ya kwanza ya kazi ilimkuta Johari na Neema wakiwa wamebanana kwenye viti vya lodge, wamekaa kama wageni wanaosubiri huduma. Johari alikosa pa kumwacha Neema. Alihangaika kutafuta jirani wa kumwachia lakini hakuna mtu aliyetaka kujitwisha mzigo wa mtoto wa mtu. Alijua kabisa kazi ya hoteli siyo mchezo, lakini hakuwa na namna. Kuliko kumwacha Neema apotelee mitaani, bora amchukue kazini.
Dakika chache baadaye mama mwenye lodge, Mama Halima, alitokea akiwa amevalia dera la rangi ya kijani kibichi, kitambaa kichwani na buti ndefu miguuni. Alimkazia Johari macho, macho ya mtu mwenye miaka mingi kwenye mtaa, anayejua kuchuja watu kwa sekunde tano tu.
"Johari! Ulisikia nilichokuambia jana eeh? Kazi ya lodge siyo sehemu ya kuleta watoto! Hapa watu wanashinda wakiwa na stress, wengine wakiwa na wanawake wa mtaani… Unaleta mtoto hapa atasikia maneno mabaya. Sitaki stress za watoto hapa," alifoka kwa sauti ya kutisha.
Johari alitetemeka, mikono ikatetema vibaya. Alimshikilia Neema kwa nguvu, machozi yakianza kutiririka. “Mama Halima… tafadhali… sina pa kumwacha mwanangu. Nimehangaika… hakuna wa kumchukua. Nitafanya kazi vizuri, hata kama ni kuosha vyoo nitafanya. Huyu ni damu yangu… sitaki kuachana naye. Tafadhali… tafadhali sana.”
Mama Halima alinyamaza. Akamwangalia Neema ambaye alikuwa kakaa kimya, macho yakiwa yametulia. Mtoto huyo hakulia, hakuwa na vurugu, alikuwa mpole. Hali hiyo ilimgusa mama Halima kwa namna ambayo hata yeye hakuelewa. Akakunja sura, akahema kwa nguvu.
“Usinililie hapa! Mimi sipendi drama za wanawake. Leo kazi ni ya majaribio. Ukifanya kazi vizuri bila malalamiko ya wateja, utanisihi mwenyewe nikuache umlete huyu mtoto. Lakini nikisikia shida… nakutoa hapa papohapo.”
Johari alijikuta akipiga magoti kwa shukrani, akambusu mkono mama Halima. “Asante mama, Mungu akuzidishie riziki,” alisema kwa sauti ya unyonge.
Siku ya kazi ilianza. Johari alipiga deki hadi sakafu ikang’aa kama kioo. Alisafisha vyoo mpaka hata mende walishangaa. Wateja waliridhika. Mama Halima alikuwa anapita mara kwa mara kuangalia, lakini hakusikia lawama yoyote. Neema alikuwa akikaa pembeni kwenye kona ya mapokezi, mara nyingine akisaidia kufuta meza kwa kitambaa kidogo.
Mwisho wa siku, Mama Halima alimuita Johari na kumpa noti kumi za elfu kumi, akasema, “Hiyo ni advance ya mshahara wako wa mwezi… ninaona unajitahidi. Ukiendelea hivi utakuwa mtu wangu wa nguvu”
Johari alishindwa kujizuia, alilia kama mtoto mdogo. Alimwambia Neema, “Unaona mwanangu… mwanga umeanza kutokea.”
Baada ya kazi ya siku tatu mfululizo, Johari aliamua kutumia sehemu ya hela ile kupanga chumba cha kawaida kule Manzese. Alienda akakodi chumba kidogo cha giza kisicho na umeme. Chumba kilikuwa kimepinda ukuta, hakikuwa na umeme lakini kilikuwa salama. Walikula mihogo ya kukaanga wakashukuru Mungu kwa hatua ya kwanza.
Wiki mbili zikasogea, Johari alianza kuona maisha yanabadilika. Akawa anaweza kununua unga wa sembe, maharage, hata sabuni ya kufulia. Alikuwa anatoka kazini na kurudi akiwa na tabasamu dogo usoni. Alianza kufahamiana na wafanyakazi wenzake akawa mtu wa kupendwa lodge nzima.
Siku moja wakati wa kazi ya usiku, alikuja mteja mmoja kwenye lodge, kijana mwembamba, wa miaka ya kati, mwenye suti safi na perfume ya kuvutia. Aliomba chumba, akapewa namba 9, akakaa siku mbili mfululizo. Johari alikuwa ndiye wa kufua nguo zake, kusafisha chumba chake na kumletea kahawa ya asubuhi. .Kijana huyo alikuwa anaitwa Lucas Lakini sio mwashambwa. Alikuwa ni fundi wa magari, mwenye gereji kubwa pale Buguruni. Lakini alikuwa pia mtu mwenye roho nzuri. Siku ya tatu alimwambia Johari, “Mrembo, sijawahi kuona dada anayefanya kazi kwa roho ya dhati kama wewe. Kila nikikuangalia unaweka moyo wako kwenye kazi.”Johari alishusha macho, kwa sababu hakuwa na mazoea ya maneno ya wanaume. Aliamua kuwa mkweli. “Nina binti, ndio kila kitu kwangu. Sifanyi kazi kwa kujipendezesha, nafanya kwa kutafuta chakula cha mwanangu.”
Lucas alishangaa. “Una mtoto?”
“Ndiyo, Neema. Ana miaka miwili na miezi saba,” Johari alijibu kwa unyenyekevu.
Lucas alimtazama Johari kwa macho yenye huruma. Akasema, “Nitakuwa nakuja hapa mara kwa mara. Najua mateso ya maisha yanavyotafuna watu wa aina Yako, single mother. Nikija sitaki upige deki kwenye chumba changu, utakuja kukaa tupige stori.”
Johari alicheka, akasema, “Sawa bosi. Tuko pamoja.”
Lucas alianza kuja mara kwa mara. Kila akija alikuwa na zawadi ndogo kwa Neema, aidha pipi, aidha uji mzuri wa watoto au mchele kidogo kwa ajili ya nyumbani. Polepole moyo wa Johari ukaanza kubadilika. Aliyewahi kusema hatapenda tena, akaanza kuona kuna watu bado wana moyo wa ubinadamu.
Mwezi mmoja na nusu ulipofika, Lucas aliamua kusema kilichokuwa moyoni mwake. Siku hiyo alikuwa amekuja lodge akiwa na zawadi ya gauni jipya la mtoto na kilo mbili za mchele.
“Johari, sina maneno mengi. Najua maisha yamekupiga sana. Sijakuona kwenye mavazi ya fahari lakini nimeona tabia yako. Sikujali kwa sura yako, nimependa moyo wako. Kama uko tayari, nataka nikuoe.”
Johari alitetemeka. Alishindwa kujizuia. Aliangalia maisha yake jinsi yalivyomfinya, jinsi alivyoishi kwenye mto wa machozi bila msaada. Huyu kijana mzuri alikuwa anaona thamani kwenye moyo wake, sio mwili wake. Ilikuwa ndoto iliyokuwa haipo kichwani mwake.
Lakini alikaa kimya. Alijua ni mapema. Alijua bado kuna mengi ya kujua kuhusu Lucas. Lakini kwa mara ya kwanza baada ya muda mrefu… moyo wake uliona mwanga. Neema alimkumbatia mamake, akasema kwa maneno yasiyoeleweka vizuri, “Mama atacheka sasa?”
Johari alicheka, macho yakiwa na machozi.
Ndani ya chumba chake cha giza Manzese, kwenye godoro lililochoka, Johari alijua safari mpya inaanza. Safari ya matumaini, safari ya upendo, safari ya maisha mapya.
**********
Siku zilianza kusonga, hazikuwa zimeganda kama awali, maisha ya Johari na Neema yakaanza kuwa na ladha mpya. Ingawa chumba cha Manzese kilikuwa cha giza, kilianza kupata mwanga wa matumaini. Johari alikuwa akiamka kila asubuhi na kwenda kazini akiwa na tabasamu, siyo kama mwanzo alipokuwa anakwenda kwa kulia na kuomboleza moyoni. Neema naye alizoea maisha mapya, alijua mama anarudi mchana na jioni akiwa na kitu angalau, hata kama ni mandazi au kipande cha sabuni, alikuwa na hakika kuna kitu kutoka kwa mama.
Lucas naye hakuacha kuonekana. Kwa wiki mbili mfululizo, alikuja lodge mara tatu, akizungumza na Johari kama rafiki, akimsikiliza, akimwelewa. Hakutaka kulazimisha penzi wala kumpa presha Johari. Aliamua kuwa mwanamume wa tofauti.
Siku moja Johari aliporudi kazini mchana wa Jumapili, Lucas alikuwa pale mapokezi, tayari ameketi akisubiri. Alimwambia Johari, “Leo huna haja ya kupiga deki wala kufagia. Leo ni siku yako ya mapumziko. Nimeshaongea na mama Halima. Kuna sehemu nataka twende.”
Johari alijaribu kupinga kwa heshima lakini Lucas alimsihi. Mama Halima naye alitabasamu na kusema, “Leo nenda kapate hewa, si kila siku kupiga deki hadi mikono igeuke.”
Johari alichukua khanga yake ya zamani, akamchukua Neema, wakaelekea Kariakoo walipokutana na Lucas kwenye gari lake dogo aina ya Passo. Johari hakuamini macho yake, ilikuwa mara ya kwanza kupanda gari binafsi baada ya muda mrefu. Lucas aliwapeleka kwenye mgahawa mdogo lakini safi, walikula wali na kuku, Neema akapata juice na keki. Walikaa hadi jioni wakizungumza mambo ya maisha. Kwa mara ya kwanza baada ya muda mrefu, Johari alicheka kutoka ndani ya moyo. Alihisi kama mwanamke, si mtumwa wa maisha.
Lakini baada ya siku kadhaa kurudi kazini, maisha yakamgonga tena kwa namna nyingine. Aliitwa na mama Halima na kuambiwa kuna mabadiliko kwenye lodge, baadhi ya wafanyakazi wapya wameshaajiriwa. Johari atahitaji kupunguza siku zake za kazi, atafanya shift moja tu kwa wiki tatu. Hii ilimaanisha mshahara wake mdogo utapungua zaidi.
Johari hakutaka kumuambia Lucas mara moja. Alijua asingeweza kuendelea kulipia chumba chake Manzese kwa kipato kidogo alichobakiwa nacho. Aliumia moyo wake ukavunjika tena, lakini hakutaka kurudi nyuma. Aliamua kurudi kwenye biashara yake ya uji kwa upande mmoja na kufanya kazi ya lodge upande mwingine.
Kwa msaada wa Lucas aliyemkopesha elfu themanini, Johari alinunua chupa za chai tano, ndoo moja, na sukari ya kuanzia biashara ndogo ya uji. Alianza kupika alfajiri kabisa na kwenda kuuza uji maeneo ya Magomeni kabla ya kwenda kazini jioni. Muda mwingi alikuwa amechoka sana lakini moyo wake haukukubali kukata tamaa.
Neema alizidi kukua, sasa alikuwa anaelewa dunia ilivyokuwa na magumu. Alimuangalia mama yake anavyohangaika kila siku, akisema, “Mama naweza kusaidia kusambaza uji?”
Johari alimkumbatia bintiye na machozi yakimtoka. “Mwanangu, sitaki maisha haya yakukondoe moyo. Sitaki maisha haya yakufundishe kukata tamaa. Utasoma, utakuwa mtu mkubwa, mama atapambana hadi tone la mwisho la damu.”
Lucas aliendelea kuwa karibu, alikuja mara kwa mara kusaidia hata biashara ya uji, alikuwa anampelekea Johari mchele au sabuni bila ya kujisifu. Alikuwa mtu wa vitendo, siyo maneno matupu. Johari aliona mabadiliko makubwa. Alijifunza kuwa upendo siyo maneno matamu bali ni vitendo vya msaada wa kweli.
Baada ya miezi miwili, Lucas alimwambia, “Johari, nimeanza mipango ya kuanzisha gereji yangu nyingine pale Gongo la Mboto, nataka unisaidie kuwa msimamizi wa ofisi. Wewe ni mtu mchapakazi, siogopi kukupa nafasi hii. Na pia… nataka tujenge maisha pamoja kama familia, si kwa huruma, bali kwa heshima.”
Johari alilia. Aliyapitia mengi, aliumizwa, alichekwa, alisahaulika, lakini hatimaye akaona kuna mtu aliye tayari kumpa nafasi mpya si kwa kumhurumia bali kwa kutambua thamani yake. Alimwangalia Neema na kumuambia, “Tumaini ni kweli halifi, hata maisha yakupige vipigo kiasi gani… mwisho wa siku kuna mtu atakutambua kwa thamani yako ya kweli.”
Johari akajua… safari ilikuwa bado ndefu, lakini hakukuwa na sababu ya
kuogopa tena.
ITAENDELEA…
Tunaingia Chungu Cha 10.
Twende tusiende,
Twedreee
Chuma kinakuja,..
Mtanisamehe Kwa arosto
Mtunzi, Robert Heriel
Chungu Cha 09
Usiku uliofuata Johari hakulala. Alikuwa analala huku macho yakiwa wazi, moyo wake ukiwa kama mtu aliyedondoka baharini bila kujua kuogelea. Ndani alimuangalia Neema aliyekuwa amejifunika kwa kitenge kilichokuwa kimetoboka huku akikoroma kwa uchovu wa mtoto mdogo asiye na makosa. Machozi ya Johari yalitiririka kimyakimya. Alihisi dunia imemchoka. Kila njia aliyojaribu haikufika popote. Alijitahidi, alihangaika, aliomba dua, alifanya kazi lakini bado mwisho wa siku anabaki mtu wa kudharauliwa na watu wa mtaani. Mtu wa kukosa hata chakula Cha yeye na bintiye.
Kesho yake hakwenda kuuza uji, hakuwa na mtaji tena. Hakuwa na hata mia moja. Alikaa ndani, akimwangalia Neema akichezea kijiti akisema anapika chakula. Wakati mchana unaingia, mwenye nyumba aligonga mlango kwa nguvu. “Johari, toka kabla sijaita mgambo! Siku zako tatu zimeisha!” alikoroma kama mbwa aliyekosa mfupa.
Johari alifungua mlango polepole, macho yakiwa yamevimba kwa kulia. “Baba mwenye nyumba… nisaidie wiki moja tu, wiki moja nipate pa kuhamia.”
Mwenye nyumba alicheka kwa dharau, “Hayo siyo maisha yangu dada, nachotaka ni kodi yangu! Ukishindwa… toka!”
Johari alifunga mlango huku akitetemeka. Hakuweza kula siku hiyo, wala hakumwandalia Neema kitu cha maana. Alimwekea maji tu na kipande cha maandazi kilichobaki kwenye chakula cha jana.
Wakati wa jioni, akaamua kutembea mtaani angalau apate mawazo ya Nini afanye. Wakati anakatiza mtaa wa pili, akamuona mzee mmoja amekaa chini karibu na duka la dawa, suruali yake ilikuwa imechanika, lakini uso wake ulikuwa na amani ya ajabu. Mzee alimwangalia Johari na akasema kwa sauti ya taratibu lakini yenye uzito: “Binti, hata mtu akizama baharini, ilimradi haujafa bado ana nafasi ya kuona pwani.”
Johari alisimama, akageuka. “Umesema nini mzee?”
Mzee akajibu kwa tabasamu, “Tumaini lipo. Jua linawaka hata kama mawingu yametanda. Ukiona kivuli, jua kuna jua nyuma ya giza.”
Johari hakujua kwa nini machozi yalibubujika. Alijikuta amekaa karibu na huyo mzee na kuanza kusimulia maisha yake yote, kuachwa na baba wa mtoto wake, kufukuzwa kazi, kufilisiwa mirathi, kupoteza kila kitu. Alimsimulia kwa machozi matupu. Baada ya dakika thelathini mzee akanyanyuka, “Binti nakuomba… kama bado unayo miguu ya kutembea na mdomo wa kusema… usikate tamaa. Nenda pale Kariakoo kona ya msikiti wa Manyema, kuna dada mmoja anatafuta mtu wa kufanya kazi ya usafi wa hoteli yake ndogo. Ni kazi ya jioni na asubuhi, unalala ndani na unapata posho ndogo lakini inasaidia.”
Johari hakuamini. “Una uhakika mzee?”
“Si lazima niwe na uhakika,” mzee akajibu kwa busara, “lakini tumaini halina gharama, jaribu.”
Johari alirudi nyumbani na Neema akiwa amebeba matumaini mapya. Hata kama yalikuwa madogo kama punje ya chumvi, moyo wake ulihisi joto jipya.
Alipoamka alfajiri, alienda Kariakoo kama mzee alivyomwelekeza. Alifika kona ya msikiti wa Manyema, akatafuta hoteli ndogo iliyoandikwa “Amani Lodge”. Alipofika, alimkuta mama mmoja mwenye umbo kubwa akiwa anapanga vyombo.
“Asalaam aleykum mama,” Johari alisalimia kwa unyenyekevu.
“Wa aleykum salaam, unahitaji nini?” yule mama akauliza kwa sauti ya amri.
“Nimesikia kuna kazi ya usafi hapa… natafuta kazi,” Johari alijibu kwa unyenyekevu mkubwa.
Mama wa hoteli alimkagua juu mpaka chini. “Una mtoto?” aliuliza.
“Ndiyo, lakini atabaki kwa jirani, sitaleta shida,” Johari alijitetea.
Baada ya ukimya mfupi, mama wa hoteli alitikisa kichwa, “Njoo kesho saa kumi na mbili asubuhi. Utaanza kazi ya kupiga deki na kusafisha vyumba vya wageni. Siyo kazi rahisi, lakini bora kuliko kukaa njaa.”
Johari hakuamini. Hakukumbuka mara ya mwisho aliambiwa ‘karibu’ kwenye kazi. Alimshukuru mama wa hoteli, akaondoka akiwa na mwanga mdogo wa matumaini.
Lakini aliporudi nyumbani, alikuta mwenye nyumba akiwa na watu wawili, mgambo. “Nimechoka na huyu mwanamke, leo anatoka kwa lazima!” Johari alilia, akaomba lakini hakuwa na msaada. Akapewa dakika ishirini kuchukua virago vyake. Alimfunga Neema mgongoni na kubeba godoro lake chakavu.
Wakiwa hawana pa kwenda, walilala kwenye kituo cha daladala ya Kinyerezi, kwenye benchi la mbao. Usiku ulikuwa na baridi, mbu walikuwa kama wanamla moyo wake. Lakini angalau alikuwa na matumaini kuwa kesho ana kazi.
Johari akajifunika na kitenge alichokuwa nacho, akamkumbatia Neema kwa nguvu huku machozi yakitiririka kimyakimya usiku kucha.
Asubuhi alijikaza, akasali kimyakimya, kisha akaelekea kwenye kazi mpya Amani Lodge akiwa na matumaini mepesi kama jani linalopeperushwa na upepo, lakini moyo wake ukiwa mgumu kama jiwe la kusaga.
*****
Siku ya kwanza ya kazi ilimkuta Johari na Neema wakiwa wamebanana kwenye viti vya lodge, wamekaa kama wageni wanaosubiri huduma. Johari alikosa pa kumwacha Neema. Alihangaika kutafuta jirani wa kumwachia lakini hakuna mtu aliyetaka kujitwisha mzigo wa mtoto wa mtu. Alijua kabisa kazi ya hoteli siyo mchezo, lakini hakuwa na namna. Kuliko kumwacha Neema apotelee mitaani, bora amchukue kazini.
Dakika chache baadaye mama mwenye lodge, Mama Halima, alitokea akiwa amevalia dera la rangi ya kijani kibichi, kitambaa kichwani na buti ndefu miguuni. Alimkazia Johari macho, macho ya mtu mwenye miaka mingi kwenye mtaa, anayejua kuchuja watu kwa sekunde tano tu.
"Johari! Ulisikia nilichokuambia jana eeh? Kazi ya lodge siyo sehemu ya kuleta watoto! Hapa watu wanashinda wakiwa na stress, wengine wakiwa na wanawake wa mtaani… Unaleta mtoto hapa atasikia maneno mabaya. Sitaki stress za watoto hapa," alifoka kwa sauti ya kutisha.
Johari alitetemeka, mikono ikatetema vibaya. Alimshikilia Neema kwa nguvu, machozi yakianza kutiririka. “Mama Halima… tafadhali… sina pa kumwacha mwanangu. Nimehangaika… hakuna wa kumchukua. Nitafanya kazi vizuri, hata kama ni kuosha vyoo nitafanya. Huyu ni damu yangu… sitaki kuachana naye. Tafadhali… tafadhali sana.”
Mama Halima alinyamaza. Akamwangalia Neema ambaye alikuwa kakaa kimya, macho yakiwa yametulia. Mtoto huyo hakulia, hakuwa na vurugu, alikuwa mpole. Hali hiyo ilimgusa mama Halima kwa namna ambayo hata yeye hakuelewa. Akakunja sura, akahema kwa nguvu.
“Usinililie hapa! Mimi sipendi drama za wanawake. Leo kazi ni ya majaribio. Ukifanya kazi vizuri bila malalamiko ya wateja, utanisihi mwenyewe nikuache umlete huyu mtoto. Lakini nikisikia shida… nakutoa hapa papohapo.”
Johari alijikuta akipiga magoti kwa shukrani, akambusu mkono mama Halima. “Asante mama, Mungu akuzidishie riziki,” alisema kwa sauti ya unyonge.
Siku ya kazi ilianza. Johari alipiga deki hadi sakafu ikang’aa kama kioo. Alisafisha vyoo mpaka hata mende walishangaa. Wateja waliridhika. Mama Halima alikuwa anapita mara kwa mara kuangalia, lakini hakusikia lawama yoyote. Neema alikuwa akikaa pembeni kwenye kona ya mapokezi, mara nyingine akisaidia kufuta meza kwa kitambaa kidogo.
Mwisho wa siku, Mama Halima alimuita Johari na kumpa noti kumi za elfu kumi, akasema, “Hiyo ni advance ya mshahara wako wa mwezi… ninaona unajitahidi. Ukiendelea hivi utakuwa mtu wangu wa nguvu”
Johari alishindwa kujizuia, alilia kama mtoto mdogo. Alimwambia Neema, “Unaona mwanangu… mwanga umeanza kutokea.”
Baada ya kazi ya siku tatu mfululizo, Johari aliamua kutumia sehemu ya hela ile kupanga chumba cha kawaida kule Manzese. Alienda akakodi chumba kidogo cha giza kisicho na umeme. Chumba kilikuwa kimepinda ukuta, hakikuwa na umeme lakini kilikuwa salama. Walikula mihogo ya kukaanga wakashukuru Mungu kwa hatua ya kwanza.
Wiki mbili zikasogea, Johari alianza kuona maisha yanabadilika. Akawa anaweza kununua unga wa sembe, maharage, hata sabuni ya kufulia. Alikuwa anatoka kazini na kurudi akiwa na tabasamu dogo usoni. Alianza kufahamiana na wafanyakazi wenzake akawa mtu wa kupendwa lodge nzima.
Siku moja wakati wa kazi ya usiku, alikuja mteja mmoja kwenye lodge, kijana mwembamba, wa miaka ya kati, mwenye suti safi na perfume ya kuvutia. Aliomba chumba, akapewa namba 9, akakaa siku mbili mfululizo. Johari alikuwa ndiye wa kufua nguo zake, kusafisha chumba chake na kumletea kahawa ya asubuhi. .Kijana huyo alikuwa anaitwa Lucas Lakini sio mwashambwa. Alikuwa ni fundi wa magari, mwenye gereji kubwa pale Buguruni. Lakini alikuwa pia mtu mwenye roho nzuri. Siku ya tatu alimwambia Johari, “Mrembo, sijawahi kuona dada anayefanya kazi kwa roho ya dhati kama wewe. Kila nikikuangalia unaweka moyo wako kwenye kazi.”Johari alishusha macho, kwa sababu hakuwa na mazoea ya maneno ya wanaume. Aliamua kuwa mkweli. “Nina binti, ndio kila kitu kwangu. Sifanyi kazi kwa kujipendezesha, nafanya kwa kutafuta chakula cha mwanangu.”
Lucas alishangaa. “Una mtoto?”
“Ndiyo, Neema. Ana miaka miwili na miezi saba,” Johari alijibu kwa unyenyekevu.
Lucas alimtazama Johari kwa macho yenye huruma. Akasema, “Nitakuwa nakuja hapa mara kwa mara. Najua mateso ya maisha yanavyotafuna watu wa aina Yako, single mother. Nikija sitaki upige deki kwenye chumba changu, utakuja kukaa tupige stori.”
Johari alicheka, akasema, “Sawa bosi. Tuko pamoja.”
Lucas alianza kuja mara kwa mara. Kila akija alikuwa na zawadi ndogo kwa Neema, aidha pipi, aidha uji mzuri wa watoto au mchele kidogo kwa ajili ya nyumbani. Polepole moyo wa Johari ukaanza kubadilika. Aliyewahi kusema hatapenda tena, akaanza kuona kuna watu bado wana moyo wa ubinadamu.
Mwezi mmoja na nusu ulipofika, Lucas aliamua kusema kilichokuwa moyoni mwake. Siku hiyo alikuwa amekuja lodge akiwa na zawadi ya gauni jipya la mtoto na kilo mbili za mchele.
“Johari, sina maneno mengi. Najua maisha yamekupiga sana. Sijakuona kwenye mavazi ya fahari lakini nimeona tabia yako. Sikujali kwa sura yako, nimependa moyo wako. Kama uko tayari, nataka nikuoe.”
Johari alitetemeka. Alishindwa kujizuia. Aliangalia maisha yake jinsi yalivyomfinya, jinsi alivyoishi kwenye mto wa machozi bila msaada. Huyu kijana mzuri alikuwa anaona thamani kwenye moyo wake, sio mwili wake. Ilikuwa ndoto iliyokuwa haipo kichwani mwake.
Lakini alikaa kimya. Alijua ni mapema. Alijua bado kuna mengi ya kujua kuhusu Lucas. Lakini kwa mara ya kwanza baada ya muda mrefu… moyo wake uliona mwanga. Neema alimkumbatia mamake, akasema kwa maneno yasiyoeleweka vizuri, “Mama atacheka sasa?”
Johari alicheka, macho yakiwa na machozi.
Ndani ya chumba chake cha giza Manzese, kwenye godoro lililochoka, Johari alijua safari mpya inaanza. Safari ya matumaini, safari ya upendo, safari ya maisha mapya.
**********
Siku zilianza kusonga, hazikuwa zimeganda kama awali, maisha ya Johari na Neema yakaanza kuwa na ladha mpya. Ingawa chumba cha Manzese kilikuwa cha giza, kilianza kupata mwanga wa matumaini. Johari alikuwa akiamka kila asubuhi na kwenda kazini akiwa na tabasamu, siyo kama mwanzo alipokuwa anakwenda kwa kulia na kuomboleza moyoni. Neema naye alizoea maisha mapya, alijua mama anarudi mchana na jioni akiwa na kitu angalau, hata kama ni mandazi au kipande cha sabuni, alikuwa na hakika kuna kitu kutoka kwa mama.
Lucas naye hakuacha kuonekana. Kwa wiki mbili mfululizo, alikuja lodge mara tatu, akizungumza na Johari kama rafiki, akimsikiliza, akimwelewa. Hakutaka kulazimisha penzi wala kumpa presha Johari. Aliamua kuwa mwanamume wa tofauti.
Siku moja Johari aliporudi kazini mchana wa Jumapili, Lucas alikuwa pale mapokezi, tayari ameketi akisubiri. Alimwambia Johari, “Leo huna haja ya kupiga deki wala kufagia. Leo ni siku yako ya mapumziko. Nimeshaongea na mama Halima. Kuna sehemu nataka twende.”
Johari alijaribu kupinga kwa heshima lakini Lucas alimsihi. Mama Halima naye alitabasamu na kusema, “Leo nenda kapate hewa, si kila siku kupiga deki hadi mikono igeuke.”
Johari alichukua khanga yake ya zamani, akamchukua Neema, wakaelekea Kariakoo walipokutana na Lucas kwenye gari lake dogo aina ya Passo. Johari hakuamini macho yake, ilikuwa mara ya kwanza kupanda gari binafsi baada ya muda mrefu. Lucas aliwapeleka kwenye mgahawa mdogo lakini safi, walikula wali na kuku, Neema akapata juice na keki. Walikaa hadi jioni wakizungumza mambo ya maisha. Kwa mara ya kwanza baada ya muda mrefu, Johari alicheka kutoka ndani ya moyo. Alihisi kama mwanamke, si mtumwa wa maisha.
Lakini baada ya siku kadhaa kurudi kazini, maisha yakamgonga tena kwa namna nyingine. Aliitwa na mama Halima na kuambiwa kuna mabadiliko kwenye lodge, baadhi ya wafanyakazi wapya wameshaajiriwa. Johari atahitaji kupunguza siku zake za kazi, atafanya shift moja tu kwa wiki tatu. Hii ilimaanisha mshahara wake mdogo utapungua zaidi.
Johari hakutaka kumuambia Lucas mara moja. Alijua asingeweza kuendelea kulipia chumba chake Manzese kwa kipato kidogo alichobakiwa nacho. Aliumia moyo wake ukavunjika tena, lakini hakutaka kurudi nyuma. Aliamua kurudi kwenye biashara yake ya uji kwa upande mmoja na kufanya kazi ya lodge upande mwingine.
Kwa msaada wa Lucas aliyemkopesha elfu themanini, Johari alinunua chupa za chai tano, ndoo moja, na sukari ya kuanzia biashara ndogo ya uji. Alianza kupika alfajiri kabisa na kwenda kuuza uji maeneo ya Magomeni kabla ya kwenda kazini jioni. Muda mwingi alikuwa amechoka sana lakini moyo wake haukukubali kukata tamaa.
Neema alizidi kukua, sasa alikuwa anaelewa dunia ilivyokuwa na magumu. Alimuangalia mama yake anavyohangaika kila siku, akisema, “Mama naweza kusaidia kusambaza uji?”
Johari alimkumbatia bintiye na machozi yakimtoka. “Mwanangu, sitaki maisha haya yakukondoe moyo. Sitaki maisha haya yakufundishe kukata tamaa. Utasoma, utakuwa mtu mkubwa, mama atapambana hadi tone la mwisho la damu.”
Lucas aliendelea kuwa karibu, alikuja mara kwa mara kusaidia hata biashara ya uji, alikuwa anampelekea Johari mchele au sabuni bila ya kujisifu. Alikuwa mtu wa vitendo, siyo maneno matupu. Johari aliona mabadiliko makubwa. Alijifunza kuwa upendo siyo maneno matamu bali ni vitendo vya msaada wa kweli.
Baada ya miezi miwili, Lucas alimwambia, “Johari, nimeanza mipango ya kuanzisha gereji yangu nyingine pale Gongo la Mboto, nataka unisaidie kuwa msimamizi wa ofisi. Wewe ni mtu mchapakazi, siogopi kukupa nafasi hii. Na pia… nataka tujenge maisha pamoja kama familia, si kwa huruma, bali kwa heshima.”
Johari alilia. Aliyapitia mengi, aliumizwa, alichekwa, alisahaulika, lakini hatimaye akaona kuna mtu aliye tayari kumpa nafasi mpya si kwa kumhurumia bali kwa kutambua thamani yake. Alimwangalia Neema na kumuambia, “Tumaini ni kweli halifi, hata maisha yakupige vipigo kiasi gani… mwisho wa siku kuna mtu atakutambua kwa thamani yako ya kweli.”
Johari akajua… safari ilikuwa bado ndefu, lakini hakukuwa na sababu ya
kuogopa tena.
ITAENDELEA…
Tunaingia Chungu Cha 10.
Twende tusiende,
Twedreee
Chuma kinakuja,..
Mtanisamehe Kwa arosto