Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 34,061
- 79,423
Simulizi; NITAMLEA
Mtunzi; Robert Heriel
+225693322300
Taikon Publisher Presents
Chungu 01.
“Kosa lake nini mpaka nimuue mtoto huyu asiye na hatia? Sitaki kuingia kwenye majuto ya kukitoa kiumbe hiki. Nitakubali majina yote ya dhihaka na kejeli. Lakini nitakulinda mwanangu. Mimi ni Mama, mlinzi wa daima.”
Maneno haya yaliandamana na machozi mazito yaliyomiminika usoni pa Johari, msichana mwenye umri wa miaka ishirini na moja. Alikuwa amesimama mbele ya kioo, ndani ya chumba kidogo alichopanga karibu na Chuo cha Uhasibu Dar es Salaam. Mikono yake miwili ilishika tumbo lake kwa upole na hofu, kana kwamba akiomba msamaha kwa mtoto aliye ndani yake.
Mimba ilikuwa ya miezi mitano. Alianza kuiona sura yake ikibadilika,
Sura ya binti mrembo aliyekuwa kivutio chuoni, sasa ilipotea taratibu. Alikua mnyonge, mwenye macho yaliyojaa usingizi wa mawazo, na tabasamu ambalo lilizikwa na siri nzito ya maisha.
Johari alikuwa msichana wa ndoto kubwa. Tangu akiwa shule ya sekondari alijulikana kwa bidii yake. Alikuwa na matumaini ya kumaliza chuo, kupata kazi nzuri, na kumnunulia mama yake nyumba ndogo kijijini Kisarawe. Lakini sasa… ndoto hizo zilikuwa kivuli cha jana.
Kilichomsumbua zaidi siyo mimba, bali ni woga wa baba yake—Mzee Hemed—mwanajeshi mstaafu mwenye misimamo mikali. Alimlea kwa mkono wa chuma, akisahau kuwa Johari si mwanajeshi bali ni msichana wa kawaida anayehitaji kueleweka. Johari alikua akiishi kwa uoga wa kupoteza heshima kwa familia, lakini zaidi, kuumiza moyo wa mama yake ambaye kila siku alimtumia ujumbe wa maombi na maneno ya matumaini.
Simu yake ililia. Alikuwa ni Salma, rafiki yake wa karibu chuoni. Johari hakuwa na nguvu ya kupokea. Alitaka kulala, lakini usingizi ulimkwepa kama majibu ya maswali aliyokuwa nayo moyoni.
“Baba ataniua… mama atalia… watu watanicheka… lakini mtoto wangu hana hatia. Ananipigapiga ndani kwa matumaini. Mimi ni Mama, lazima nimlinde.”
Alikaa kitandani, akaandika ujumbe kwenye daftari lake la siri:
“Najua kuna adhabu kubwa ya kuvunja heshima ya familia, lakini ninahisi pia kuna adhabu kubwa ya kumwua asiye na hatia. Iwapo nitafukuzwa, iwapo nitabaki pekee, nitakubali… lakini moyo wangu hautakubali kumuua mwanangu.”
********
Usiku ulipita kwa taabu. Johari hakulala. Aliutazama mfanano wake kwenye dari ya chumba chake, akihisi ukimya ukimzidi. Saa kumi alfajiri, aliinuka taratibu, akaswali na kuliweka daftari lake la siri chini ya mto.
Simu ililia tena. Salma.
Aliipokea kwa mara ya kwanza baada ya siku mbili.
“Hallo… Salma?” Sauti yake ilikuwa dhaifu.
“Eeh bwana wee! Umepotea! Kila mtu chuoni anakutafuta. Uko wapi? Hata kwa presentation hatukukuona jana!” Salma aliongea kwa kasi ile ile ya kawaida.
Johari alikaa kimya sekunde kadhaa.
“Salma…” aliita kwa sauti ya chini.
“Naam?”
“Nataka nikuambie siri moja. Lakini usijisikie vibaya. Usinihukumu.”
Salma alinyamaza. Kisha akauliza kwa sauti ya utulivu:
“Upo salama?”
Johari alitulia, akavuta pumzi ndefu.
“Mimi ni mjamzito.”
Kimya. Ni kama dunia iliganda.
Salma hakusema kitu kwa sekunde kadhaa.
“Mungu wangu…” alihemea.
“Mi… mimba ni ya nani Johari?”
Johari alikosa jibu. Machozi yalimtiririka kimya kimya.
“Ningependa nijue, lakini hata mimi sijui tena kama bado yuko upande wangu au alikimbia.”
Salma alinyamaza tena.
“Unamaanisha amekukimbia?”
“Siku ile nilimwambia, alinyamaza. Hakusema kitu. Aliondoka usiku uleule. Na tangu siku hiyo, simu haipatikani. Sijui hata kama yupo Tanzania tena.”
Salma alihisi moyo wake ukivunjika kwa niaba ya rafiki yake.
“Mungu wangu Johari… hivi umebeba mimba ya mwanaume aliyekuacha?”
“Ndiyo. Na bado nina masomo. Na bado sina kazi. Na bado baba yangu hajui. Salma, nina hofu, nina huzuni, lakini pia nina mapenzi makubwa kwa huyu mtoto aliyetumboni”
Salma alikata simu kwa muda mfupi. Dakika tano baadaye, alishika mlango wa chumba cha Johari.
“Fungua. Tuko pamoja.”
Johari alifungua mlango. Marafiki wawili walikumbatiana kimya, kwa muda mrefu. Kisha Salma akasema kwa sauti ya upole:
“Tutatafuta suluhisho. Lakini ahadi yangu ni moja—hutapitia haya yote peke yako.”
Lakini siku tatu baadaye, Johari alipata barua kutoka chuoni…
Barua ya kuitwa kwenye kikao cha nidhamu.
Kosa: Kutohudhuria masomo, na uvumi wa kuwa mjamzito.
Na huku akiwa hajamweleza Baba yake bado, Johari alikuwa anakabiliwa na vita kubwa zaidi…
*****"""""******
Siku ya kikao ilifika. Johari alitembea kwa miguu hadi chuoni. Hakuwa na nauli, na hata kama angekuwa nayo, moyo wake haukuwa tayari kwa starehe ya usafiri. Kila hatua aliyoipiga, alihisi kama anajipeleka mwenyewe kwenye hukumu isiyoepukika.
Alivaa gauni refu la rangi ya buluu iliyofifia, aliyolivaa mara ya mwisho kwenye maombi ya familia kijijini. Hapo chuoni, macho yote yalikuwa kwake. Vichwa vikageuka kumtazama kwa shauku, mengine kwa kejeli. Vicheko vya chinichini, na maneno makali.
Kwenye mlango wa ofisi ya nidhamu, alisimama kwa sekunde kadhaa kabla ya kugonga.
“Ingia,” sauti nzito ya mwanaume ilisikika.
Ndani ya ofisi walikuwamo watu wanne: Mshauri wa wanafunzi, Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Wanafunzi, Mwanasaikolojia wa chuo, na Katibu wa kikao. Hawakumtazama kama mwanafunzi. Walimtazama kama tatizo.
“Bi Johari Saidi. Kwa mujibu wa kifungu cha 4.2.1 cha kanuni za nidhamu, umeitwa kujieleza kwa kutohudhuria masomo bila taarifa, na kusababisha vurugu kwa uvumi wa kuwa na mimba ambayo haijathibitishwa rasmi.”
Johari alinyamaza. Alijua hiyo ilikuwa tu lugha ya heshima. Hukumu tayari ilikuwa moyoni mwao.
“Una la kujieleza?” aliulizwa.
Alisimama. Akasema kwa sauti iliyojaa hisia:
“Ndiyo. Nina mimba. Miezi mitano. Sijakataa. Sijatoroka. Nimejificha kwa sababu ya hofu, siyo kiburi. Nilipitia hali ya mshtuko, usaliti, na hofu ya kufukuzwa hata kabla ya kujieleza. Lakini hata kama nikifukuzwa chuo, siwezi kumuua mwanangu ili niendelee na masomo. Siwezi. Nimechagua kuwa mama. Mtu wa kwanza atakayempenda huyu mtoto, hata kama dunia haitampenda.”
Ukimya uliingia. Mwanasaikolojia alimtazama Johari kwa macho yaliyojaa huruma. Lakini macho ya Mkuu wa Idara yalibaki makali.
“Kwa kanuni za chuo, mimba bila ndoa ni ukiukwaji wa maadili,” alisisitiza.
“Na?” Johari aliuliza kwa ujasiri wa ghafla. “Na maisha ya huyu mtoto ni kosa langu? Maadili ya nani? Maadili hayaanzi na tumbo. Yanaanzia kwenye utu.”
Mshauri wa Wanafunzi alinyamaza kwa muda. Kisha akasema:
“Tutakupa jibu wiki ijayo. Ondoka.”
Johari alitoka kwa miguu ile ile, lakini moyo wake ulikuwa na majeraha zaidi. Watu wengine walimwona akipita, lakini hakuna aliyejua kwamba alikuwa anakwenda kuaga chuo chake kimya kimya.
Usiku huo, akiwa amejifungia chumbani, simu yake ililia. Ilikuwa ni baba yake, Mzee Hemed.
Moyo ulimganda. Alishika simu kwa mkono wa baridi.
Aliikata.
Kisha akalia. Sana.
Baada ya kukata simu ya baba yake, Johari alikaa kimya kwa zaidi ya dakika ishirini. Simu ililia tena. Tena. Tena. Aliweka ‘silent’. Hakutaka kusikia chochote. Hakuwa tayari. Hakuwa na maneno ya kutosha kueleza kile anachopitia.
Lakini saa tatu usiku, ujumbe mfupi uliingia:
“Nataka nikuone kesho saa moja asubuhi. Usikose.”
—Mzee Hemed.
Moyo wa Johari ulianza kupiga haraka kama ngoma ya harusi ya huzuni. Hakuwa amewahi kumkataa baba yake. Lakini sasa, alikuwa na sababu ya kumuogopa zaidi ya kawaida. Alikumbuka maneno ya baba yake mwaka jana:
“Mwanangu, dunia hii ya leo si ya wanyonge. Ukikosea njia, usiniangalie. Nimekulea kwa nidhamu, sitaki aibu.”
Johari alijua hiyo “aibu” ndiyo ilikuwa ndani ya tumbo lake sasa. Mzigo wa maamuzi aliyoyafanya. Na sasa alipaswa kumkabili baba yake — mwanamume aliyeamini ukamilifu wa familia kuliko upendo wa kweli.
Asubuhi, Johari alivaa baibui kubwa la buluu iliyokolea. Alifunga kilemba, akaficha sura yake. Alipanda daladala hadi Tabata, alipokuwa baba yake akiishi kwenye nyumba ya jeshi. Mtaa ulikuwa kimya. Alipofika mbele ya mlango, alihema kwa sekunde kadhaa.
Kabla hajagonga, mlango ulifunguliwa. Mzee Hemed alikuwa amesimama mlangoni tayari. Sura yake ilikuwa ngumu. Macho yake yalikuwa kama shoka la hukumu.
“Ingiza miguu ndani,” alisema kwa sauti ya kawaida lakini ya baridi.
Johari aliingia kimya kimya. Alikaa kwenye sofa aliyokulia tangu akiwa mtoto. Kumbukumbu zilimvamia. Picha za utoto, harufu ya sabuni ya baba, sauti ya redio ya TBC usiku… lakini yote hayo yalichafuliwa na kitu kimoja: siri aliyobeba.
Mzee Hemed alikaa kiti cha mbele yake, akamwangalia.
“Nimekuwa nikisikia uvumi. Na sasa nimeona kwa macho yangu. Ni kweli?”
Johari alinyanyua uso wake. Kwa mara ya kwanza, macho yao yaligongana.
“Ni kweli baba. Nina mimba.”
Mzee Hemed alifunga macho yake kwa sekunde. Akavuta pumzi ndefu. Kisha akasimama.
“Hivi… ndivyo ulivyoamua kurudisha mkono wa kulelewa? Kwa aibu?”
Johari alijaribu kujieleza. “Baba, sikukusudia. Ilinitokea. Sikujua namna ya kukueleza…”
“Wewe unadhani kulea mtoto ni mchezo? Au unajua gharama za kuishi dunia hii? Unaelewa maana ya kubeba jina la familia?” Mzee Hemed alizidi kupandisha sauti.
Lakini kisha… kimya kilifuata. Johari alilia. Bila sauti. Bila maneno.
Mzee Hemed alimuangalia binti yake. Akaona binti mdogo aliyelelewa kwa mikono yake mwenyewe. Aliona uso wa mke wake aliyefariki miaka miwili iliyopita. Aliona uoga, maumivu na majuto — lakini pia aliona kitu kingine: msimamo.
Mzee Hemed alipunguza sauti. Kwa mara ya kwanza, sauti yake ilionekana dhaifu.
“Baba wa mtoto yuko wapi?”
“Aliniacha, baba. Sijui aliko.”
Mzee Hemed alikaa tena. Alishusha pumzi.
“Basi, wewe na mtoto huyo… mko mikononi mwangu. Sitakubali damu yangu itemwe njiani. Lakini pia sitakuficha: safari itakuwa ngumu.”
Johari alinyamaza. Kisha akasema:
“Baba, sitaki pesa. Sitaki huruma. Nataka nafasi ya kusimama tena. Kwa ajili yangu. Kwa ajili ya mwanangu.”
Mzee Hemed alinyosha mkono wake. Kwa mara ya kwanza tangu utotoni, alimshika Johari mkono na kusema:
“Tutaanza na kuandika barua ya rufaa chuoni. Hii familia haitajificha.”
*******
Siku mbili baada ya kukutana na baba yake, Johari alirudi chuoni kwa ajili ya kusikiliza uamuzi wa kikao cha nidhamu. Alikuwa amevaa sare ya chuo, japo ilibana kidogo tumboni. Uso wake ulikuwa wa utulivu usio wa kawaida, utulivu unaozaliwa si kwa sababu ya matumaini bali kwa sababu ya kukubali hatima.
Moyo wake haukuwa mwepesi. Lakini sasa alikuwa na mtu wa kumsindikiza babaake, -Mzee Hemed. Mwanajeshi mstaafu, ambaye aliingia kwenye ofisi ya Mkuu wa chuo kwa mguu mzito lakini uso wenye msimamo.
Walipoketi kwenye kiti cha wageni nje ya ofisi, wanafunzi walipita kwa macho ya kushangaa. Wengine walinong’onezana, wengine walijipitisha kusalimia hivyohivyo basi ilimradi. Lakini hakuna aliyejua kuwa siku hiyo Johari alikuwa anapigania haki ya kuishi kama mama, mwanafunzi, na mwanadamu.
Dakika kumi baadaye, mlango ulifunguliwa.
“Bi Johari, tafadhali ingia.”
Akaingia na baba yake nyuma yake. Waliketi. Kamati ile ile ilikuwa mezani.
Lakini kabla hawajaanza kuzungumza, Mzee Hemed alinyanyuka. Alisogea mbele, akawatazama mmoja mmoja.
“Naomba niseme kabla ya binti yangu. Nimeitikia kuwa naye hapa kama mzazi. Najua heshima ya taasisi hii. Lakini naomba muelewe kwamba Johari hakuvunja sheria ya chuo kwa kukusudia, bali alianguka kama binadamu yeyote anavyoweza kuanguka. Na sasa, kama mwanajeshi aliyepigana vita vya kweli, siwezi kuona mwanangu akipotezwa kwa kosa moja. Anahitaji nafasi ya pili. Kama mzazi, siwajibiki tu kumhukumu, bali kumpa sababu ya kusimama tena.”
Ukumbi ulitulia. Hakuna aliyesema neno kwa dakika moja.
Mkuu wa Taaluma alichukua faili, akasoma barua yao ya rufaa.
Kisha akasema:
“Kwa kuzingatia hali ya kipekee, na ushauri wa mwanasaikolojia wa chuo, tumekubaliana: Johari atapewa likizo ya masomo ya miezi sita. Atarudi baada ya kujifungua, kwa masharti ya kuhudhuria vipindi vya ushauri na msaada wa kijamii.”
Johari alishusha pumzi nzito. Machozi yalimtoka. Lakini kwa mara ya kwanza, yalikuwa ya faraja.
Baba yake alimshika bega. Hakuongea, lakini ulimwengu wote wa Johari ulijua — kwa kimya kile tu — kwamba hatakuwa peke yake tena.
Siku hiyo usiku, Johari aliliandika tena daftari lake la siri:
"Leo nimerudi kutoka kwenye kaburi la kukata tamaa. Niliamini hakuna anayeweza kunielewa. Sasa najua, hata mtu mkali anaweza kuwa kinga yako. Baba amenirudia. Dunia haijabadilika, bado kuna lawama, kejeli na macho ya mashaka. Lakini nimejifunza… si lazima dunia inipokee. Lakini mwanangu ananihitaji. Na hiyo tu, inanitosha.”
Mwezi mmoja baadaye, simu yake iliita.
Jina lisilosahaulika lilionekana kwenye skrini: “Dennis.”
Mwanaume aliyempa ujauzito. Aliyemtoroka.
Na kilichoandikwa kwenye ujumbe wake…
“Tuna haja ya kuzungumza. Kitu muhimu sana.”
Je, Dennis amerejea kwa sababu ya mtoto? Ana siri gani? Je, Johari ana sababu ya kumsikiliza tena, au ni mwanzo wa jeraha jipya?
Itaendelea!
Nitamlea Ndio habari ya Mjini.
Kaa humuhumu!
Robert Heriel
Taikon Master kwa Sasa Dar es salaam
Mtunzi; Robert Heriel
+225693322300
Taikon Publisher Presents
Chungu 01.
“Kosa lake nini mpaka nimuue mtoto huyu asiye na hatia? Sitaki kuingia kwenye majuto ya kukitoa kiumbe hiki. Nitakubali majina yote ya dhihaka na kejeli. Lakini nitakulinda mwanangu. Mimi ni Mama, mlinzi wa daima.”
Maneno haya yaliandamana na machozi mazito yaliyomiminika usoni pa Johari, msichana mwenye umri wa miaka ishirini na moja. Alikuwa amesimama mbele ya kioo, ndani ya chumba kidogo alichopanga karibu na Chuo cha Uhasibu Dar es Salaam. Mikono yake miwili ilishika tumbo lake kwa upole na hofu, kana kwamba akiomba msamaha kwa mtoto aliye ndani yake.
Mimba ilikuwa ya miezi mitano. Alianza kuiona sura yake ikibadilika,
Sura ya binti mrembo aliyekuwa kivutio chuoni, sasa ilipotea taratibu. Alikua mnyonge, mwenye macho yaliyojaa usingizi wa mawazo, na tabasamu ambalo lilizikwa na siri nzito ya maisha.
Johari alikuwa msichana wa ndoto kubwa. Tangu akiwa shule ya sekondari alijulikana kwa bidii yake. Alikuwa na matumaini ya kumaliza chuo, kupata kazi nzuri, na kumnunulia mama yake nyumba ndogo kijijini Kisarawe. Lakini sasa… ndoto hizo zilikuwa kivuli cha jana.
Kilichomsumbua zaidi siyo mimba, bali ni woga wa baba yake—Mzee Hemed—mwanajeshi mstaafu mwenye misimamo mikali. Alimlea kwa mkono wa chuma, akisahau kuwa Johari si mwanajeshi bali ni msichana wa kawaida anayehitaji kueleweka. Johari alikua akiishi kwa uoga wa kupoteza heshima kwa familia, lakini zaidi, kuumiza moyo wa mama yake ambaye kila siku alimtumia ujumbe wa maombi na maneno ya matumaini.
Simu yake ililia. Alikuwa ni Salma, rafiki yake wa karibu chuoni. Johari hakuwa na nguvu ya kupokea. Alitaka kulala, lakini usingizi ulimkwepa kama majibu ya maswali aliyokuwa nayo moyoni.
“Baba ataniua… mama atalia… watu watanicheka… lakini mtoto wangu hana hatia. Ananipigapiga ndani kwa matumaini. Mimi ni Mama, lazima nimlinde.”
Alikaa kitandani, akaandika ujumbe kwenye daftari lake la siri:
“Najua kuna adhabu kubwa ya kuvunja heshima ya familia, lakini ninahisi pia kuna adhabu kubwa ya kumwua asiye na hatia. Iwapo nitafukuzwa, iwapo nitabaki pekee, nitakubali… lakini moyo wangu hautakubali kumuua mwanangu.”
********
Usiku ulipita kwa taabu. Johari hakulala. Aliutazama mfanano wake kwenye dari ya chumba chake, akihisi ukimya ukimzidi. Saa kumi alfajiri, aliinuka taratibu, akaswali na kuliweka daftari lake la siri chini ya mto.
Simu ililia tena. Salma.
Aliipokea kwa mara ya kwanza baada ya siku mbili.
“Hallo… Salma?” Sauti yake ilikuwa dhaifu.
“Eeh bwana wee! Umepotea! Kila mtu chuoni anakutafuta. Uko wapi? Hata kwa presentation hatukukuona jana!” Salma aliongea kwa kasi ile ile ya kawaida.
Johari alikaa kimya sekunde kadhaa.
“Salma…” aliita kwa sauti ya chini.
“Naam?”
“Nataka nikuambie siri moja. Lakini usijisikie vibaya. Usinihukumu.”
Salma alinyamaza. Kisha akauliza kwa sauti ya utulivu:
“Upo salama?”
Johari alitulia, akavuta pumzi ndefu.
“Mimi ni mjamzito.”
Kimya. Ni kama dunia iliganda.
Salma hakusema kitu kwa sekunde kadhaa.
“Mungu wangu…” alihemea.
“Mi… mimba ni ya nani Johari?”
Johari alikosa jibu. Machozi yalimtiririka kimya kimya.
“Ningependa nijue, lakini hata mimi sijui tena kama bado yuko upande wangu au alikimbia.”
Salma alinyamaza tena.
“Unamaanisha amekukimbia?”
“Siku ile nilimwambia, alinyamaza. Hakusema kitu. Aliondoka usiku uleule. Na tangu siku hiyo, simu haipatikani. Sijui hata kama yupo Tanzania tena.”
Salma alihisi moyo wake ukivunjika kwa niaba ya rafiki yake.
“Mungu wangu Johari… hivi umebeba mimba ya mwanaume aliyekuacha?”
“Ndiyo. Na bado nina masomo. Na bado sina kazi. Na bado baba yangu hajui. Salma, nina hofu, nina huzuni, lakini pia nina mapenzi makubwa kwa huyu mtoto aliyetumboni”
Salma alikata simu kwa muda mfupi. Dakika tano baadaye, alishika mlango wa chumba cha Johari.
“Fungua. Tuko pamoja.”
Johari alifungua mlango. Marafiki wawili walikumbatiana kimya, kwa muda mrefu. Kisha Salma akasema kwa sauti ya upole:
“Tutatafuta suluhisho. Lakini ahadi yangu ni moja—hutapitia haya yote peke yako.”
Lakini siku tatu baadaye, Johari alipata barua kutoka chuoni…
Barua ya kuitwa kwenye kikao cha nidhamu.
Kosa: Kutohudhuria masomo, na uvumi wa kuwa mjamzito.
Na huku akiwa hajamweleza Baba yake bado, Johari alikuwa anakabiliwa na vita kubwa zaidi…
*****"""""******
Siku ya kikao ilifika. Johari alitembea kwa miguu hadi chuoni. Hakuwa na nauli, na hata kama angekuwa nayo, moyo wake haukuwa tayari kwa starehe ya usafiri. Kila hatua aliyoipiga, alihisi kama anajipeleka mwenyewe kwenye hukumu isiyoepukika.
Alivaa gauni refu la rangi ya buluu iliyofifia, aliyolivaa mara ya mwisho kwenye maombi ya familia kijijini. Hapo chuoni, macho yote yalikuwa kwake. Vichwa vikageuka kumtazama kwa shauku, mengine kwa kejeli. Vicheko vya chinichini, na maneno makali.
Kwenye mlango wa ofisi ya nidhamu, alisimama kwa sekunde kadhaa kabla ya kugonga.
“Ingia,” sauti nzito ya mwanaume ilisikika.
Ndani ya ofisi walikuwamo watu wanne: Mshauri wa wanafunzi, Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Wanafunzi, Mwanasaikolojia wa chuo, na Katibu wa kikao. Hawakumtazama kama mwanafunzi. Walimtazama kama tatizo.
“Bi Johari Saidi. Kwa mujibu wa kifungu cha 4.2.1 cha kanuni za nidhamu, umeitwa kujieleza kwa kutohudhuria masomo bila taarifa, na kusababisha vurugu kwa uvumi wa kuwa na mimba ambayo haijathibitishwa rasmi.”
Johari alinyamaza. Alijua hiyo ilikuwa tu lugha ya heshima. Hukumu tayari ilikuwa moyoni mwao.
“Una la kujieleza?” aliulizwa.
Alisimama. Akasema kwa sauti iliyojaa hisia:
“Ndiyo. Nina mimba. Miezi mitano. Sijakataa. Sijatoroka. Nimejificha kwa sababu ya hofu, siyo kiburi. Nilipitia hali ya mshtuko, usaliti, na hofu ya kufukuzwa hata kabla ya kujieleza. Lakini hata kama nikifukuzwa chuo, siwezi kumuua mwanangu ili niendelee na masomo. Siwezi. Nimechagua kuwa mama. Mtu wa kwanza atakayempenda huyu mtoto, hata kama dunia haitampenda.”
Ukimya uliingia. Mwanasaikolojia alimtazama Johari kwa macho yaliyojaa huruma. Lakini macho ya Mkuu wa Idara yalibaki makali.
“Kwa kanuni za chuo, mimba bila ndoa ni ukiukwaji wa maadili,” alisisitiza.
“Na?” Johari aliuliza kwa ujasiri wa ghafla. “Na maisha ya huyu mtoto ni kosa langu? Maadili ya nani? Maadili hayaanzi na tumbo. Yanaanzia kwenye utu.”
Mshauri wa Wanafunzi alinyamaza kwa muda. Kisha akasema:
“Tutakupa jibu wiki ijayo. Ondoka.”
Johari alitoka kwa miguu ile ile, lakini moyo wake ulikuwa na majeraha zaidi. Watu wengine walimwona akipita, lakini hakuna aliyejua kwamba alikuwa anakwenda kuaga chuo chake kimya kimya.
Usiku huo, akiwa amejifungia chumbani, simu yake ililia. Ilikuwa ni baba yake, Mzee Hemed.
Moyo ulimganda. Alishika simu kwa mkono wa baridi.
Aliikata.
Kisha akalia. Sana.
Baada ya kukata simu ya baba yake, Johari alikaa kimya kwa zaidi ya dakika ishirini. Simu ililia tena. Tena. Tena. Aliweka ‘silent’. Hakutaka kusikia chochote. Hakuwa tayari. Hakuwa na maneno ya kutosha kueleza kile anachopitia.
Lakini saa tatu usiku, ujumbe mfupi uliingia:
“Nataka nikuone kesho saa moja asubuhi. Usikose.”
—Mzee Hemed.
Moyo wa Johari ulianza kupiga haraka kama ngoma ya harusi ya huzuni. Hakuwa amewahi kumkataa baba yake. Lakini sasa, alikuwa na sababu ya kumuogopa zaidi ya kawaida. Alikumbuka maneno ya baba yake mwaka jana:
“Mwanangu, dunia hii ya leo si ya wanyonge. Ukikosea njia, usiniangalie. Nimekulea kwa nidhamu, sitaki aibu.”
Johari alijua hiyo “aibu” ndiyo ilikuwa ndani ya tumbo lake sasa. Mzigo wa maamuzi aliyoyafanya. Na sasa alipaswa kumkabili baba yake — mwanamume aliyeamini ukamilifu wa familia kuliko upendo wa kweli.
Asubuhi, Johari alivaa baibui kubwa la buluu iliyokolea. Alifunga kilemba, akaficha sura yake. Alipanda daladala hadi Tabata, alipokuwa baba yake akiishi kwenye nyumba ya jeshi. Mtaa ulikuwa kimya. Alipofika mbele ya mlango, alihema kwa sekunde kadhaa.
Kabla hajagonga, mlango ulifunguliwa. Mzee Hemed alikuwa amesimama mlangoni tayari. Sura yake ilikuwa ngumu. Macho yake yalikuwa kama shoka la hukumu.
“Ingiza miguu ndani,” alisema kwa sauti ya kawaida lakini ya baridi.
Johari aliingia kimya kimya. Alikaa kwenye sofa aliyokulia tangu akiwa mtoto. Kumbukumbu zilimvamia. Picha za utoto, harufu ya sabuni ya baba, sauti ya redio ya TBC usiku… lakini yote hayo yalichafuliwa na kitu kimoja: siri aliyobeba.
Mzee Hemed alikaa kiti cha mbele yake, akamwangalia.
“Nimekuwa nikisikia uvumi. Na sasa nimeona kwa macho yangu. Ni kweli?”
Johari alinyanyua uso wake. Kwa mara ya kwanza, macho yao yaligongana.
“Ni kweli baba. Nina mimba.”
Mzee Hemed alifunga macho yake kwa sekunde. Akavuta pumzi ndefu. Kisha akasimama.
“Hivi… ndivyo ulivyoamua kurudisha mkono wa kulelewa? Kwa aibu?”
Johari alijaribu kujieleza. “Baba, sikukusudia. Ilinitokea. Sikujua namna ya kukueleza…”
“Wewe unadhani kulea mtoto ni mchezo? Au unajua gharama za kuishi dunia hii? Unaelewa maana ya kubeba jina la familia?” Mzee Hemed alizidi kupandisha sauti.
Lakini kisha… kimya kilifuata. Johari alilia. Bila sauti. Bila maneno.
Mzee Hemed alimuangalia binti yake. Akaona binti mdogo aliyelelewa kwa mikono yake mwenyewe. Aliona uso wa mke wake aliyefariki miaka miwili iliyopita. Aliona uoga, maumivu na majuto — lakini pia aliona kitu kingine: msimamo.
Mzee Hemed alipunguza sauti. Kwa mara ya kwanza, sauti yake ilionekana dhaifu.
“Baba wa mtoto yuko wapi?”
“Aliniacha, baba. Sijui aliko.”
Mzee Hemed alikaa tena. Alishusha pumzi.
“Basi, wewe na mtoto huyo… mko mikononi mwangu. Sitakubali damu yangu itemwe njiani. Lakini pia sitakuficha: safari itakuwa ngumu.”
Johari alinyamaza. Kisha akasema:
“Baba, sitaki pesa. Sitaki huruma. Nataka nafasi ya kusimama tena. Kwa ajili yangu. Kwa ajili ya mwanangu.”
Mzee Hemed alinyosha mkono wake. Kwa mara ya kwanza tangu utotoni, alimshika Johari mkono na kusema:
“Tutaanza na kuandika barua ya rufaa chuoni. Hii familia haitajificha.”
*******
Siku mbili baada ya kukutana na baba yake, Johari alirudi chuoni kwa ajili ya kusikiliza uamuzi wa kikao cha nidhamu. Alikuwa amevaa sare ya chuo, japo ilibana kidogo tumboni. Uso wake ulikuwa wa utulivu usio wa kawaida, utulivu unaozaliwa si kwa sababu ya matumaini bali kwa sababu ya kukubali hatima.
Moyo wake haukuwa mwepesi. Lakini sasa alikuwa na mtu wa kumsindikiza babaake, -Mzee Hemed. Mwanajeshi mstaafu, ambaye aliingia kwenye ofisi ya Mkuu wa chuo kwa mguu mzito lakini uso wenye msimamo.
Walipoketi kwenye kiti cha wageni nje ya ofisi, wanafunzi walipita kwa macho ya kushangaa. Wengine walinong’onezana, wengine walijipitisha kusalimia hivyohivyo basi ilimradi. Lakini hakuna aliyejua kuwa siku hiyo Johari alikuwa anapigania haki ya kuishi kama mama, mwanafunzi, na mwanadamu.
Dakika kumi baadaye, mlango ulifunguliwa.
“Bi Johari, tafadhali ingia.”
Akaingia na baba yake nyuma yake. Waliketi. Kamati ile ile ilikuwa mezani.
Lakini kabla hawajaanza kuzungumza, Mzee Hemed alinyanyuka. Alisogea mbele, akawatazama mmoja mmoja.
“Naomba niseme kabla ya binti yangu. Nimeitikia kuwa naye hapa kama mzazi. Najua heshima ya taasisi hii. Lakini naomba muelewe kwamba Johari hakuvunja sheria ya chuo kwa kukusudia, bali alianguka kama binadamu yeyote anavyoweza kuanguka. Na sasa, kama mwanajeshi aliyepigana vita vya kweli, siwezi kuona mwanangu akipotezwa kwa kosa moja. Anahitaji nafasi ya pili. Kama mzazi, siwajibiki tu kumhukumu, bali kumpa sababu ya kusimama tena.”
Ukumbi ulitulia. Hakuna aliyesema neno kwa dakika moja.
Mkuu wa Taaluma alichukua faili, akasoma barua yao ya rufaa.
Kisha akasema:
“Kwa kuzingatia hali ya kipekee, na ushauri wa mwanasaikolojia wa chuo, tumekubaliana: Johari atapewa likizo ya masomo ya miezi sita. Atarudi baada ya kujifungua, kwa masharti ya kuhudhuria vipindi vya ushauri na msaada wa kijamii.”
Johari alishusha pumzi nzito. Machozi yalimtoka. Lakini kwa mara ya kwanza, yalikuwa ya faraja.
Baba yake alimshika bega. Hakuongea, lakini ulimwengu wote wa Johari ulijua — kwa kimya kile tu — kwamba hatakuwa peke yake tena.
Siku hiyo usiku, Johari aliliandika tena daftari lake la siri:
"Leo nimerudi kutoka kwenye kaburi la kukata tamaa. Niliamini hakuna anayeweza kunielewa. Sasa najua, hata mtu mkali anaweza kuwa kinga yako. Baba amenirudia. Dunia haijabadilika, bado kuna lawama, kejeli na macho ya mashaka. Lakini nimejifunza… si lazima dunia inipokee. Lakini mwanangu ananihitaji. Na hiyo tu, inanitosha.”
Mwezi mmoja baadaye, simu yake iliita.
Jina lisilosahaulika lilionekana kwenye skrini: “Dennis.”
Mwanaume aliyempa ujauzito. Aliyemtoroka.
Na kilichoandikwa kwenye ujumbe wake…
“Tuna haja ya kuzungumza. Kitu muhimu sana.”
Je, Dennis amerejea kwa sababu ya mtoto? Ana siri gani? Je, Johari ana sababu ya kumsikiliza tena, au ni mwanzo wa jeraha jipya?
Itaendelea!
Nitamlea Ndio habari ya Mjini.
Kaa humuhumu!
Robert Heriel
Taikon Master kwa Sasa Dar es salaam