Simulizi: Nini maana ya mapenzi

SEHEMU YA 434

Dora na James walifika nyumbani kwa James usiku ule ila kwa bahati mlinzi wa James alirudi, kumbe alimtimua ila mlinzi alirudi, yani mlinzi alivyomuona James alianza kumuomba msamaha ila James alimshukuru sana mlinzi kwa uwepo wake tena kisha akamsaidia kuharibu kitasa cha mlango na kuingia ndani ambapo ilibidi alale mule na Dora hadi palipokucha ila kiukweli hawakulala kabisa kwani kila mmoja alikuwa na mawazo sana, waliwaza kuhusu simu zao yani simu ndio zilizowatia mawazo zaidi, kiukweli Dora alikuwa amechoka sana na kuamua tu kwenda jikoni kwa James na kupika kisha kuandaa chakula na kuanza kula na James, kwa mara ya kwanza leo James alikula chakula kilichopikwa na Dora, alikula na kumwambia,
“Kheee Dora licha ya kuhangaika hangaika kumbe kupika unajua?”
Dora akacheka na kusema,
“Tena leo nina mawazo yangu ndiomana, ila na wewe James hivi ni wanawake gani wale unakuwa nao? Aina gani ile ya mwanamke ulimuokotea wapi?”
“Hapana unajua Yule mwanamke alikuwa ni mfanyakazi wa humu ndani, na nilianza nae kipindi mke wangu mjamzito maana alikuwa mvivu sana”
“Ndio tabia ya kuhangaika na wasichana wa kazi hiyo, tatizo wanaume huwa hamridhiki hata wake zenu wawafanyie nini ndani, mfano kipindi kile kunibaka, dah huwa sisahau kabisa”
“Aaaah Dora si yashaisha hayo, ila kuna somo tumepata. Unajua kunywa sio vibaya ila kulewa ni vibaya, hebu ona tumekosa hata ufahamu kuwa tunachukuliwa simu. Ngoja tujiandae tu tushughulikie kwanza simu na laini kabla ya yote maana mawasiliano ndio ya muhimu”
“Na gari kasepa nalo, aaah wanawake wengine ni noma”
“Yule muache ila atajutia, vile vitu vinapita tu hakuna kitakachobaki je ataweza kuendelea kulea mtoto mwenyewe!”
“Ila James tutamlaumu tu Yule mwanamke ila ulevi wetu ni mbaya, hebu ona sasa tumelewa na kuanza kutenda matendo ya ajabu kwa Yule mwanamke, tumejitia uchizi kumbe Yule ni chizi zaidi yetu”
Basi walimaliza kula na kujiandaa ambapo Dora alivaa tu nguo baadhi zilizobaki za Bite kwa wakati huo na kutoka na James.

Tony leo alienda kukutana na Tumaini kwenye duka ambalo lilimilikiwa na Erick, ila aliona kama akimwambia Tumaini kuwa mama yake anataka amuone kumfanyie kama usahili, basi Tumaini atakataa kwahiyo aliamua kumwambia kwa njia nyingine,
“Tumaini, mama amekukubali ila anataka uende nyumbani Jumamosi ulale hapo na uondoke Jumapili”
“Hiyo ni ngumu kwangu Tony, siwezi kulala mbali na nyumbani. Baba atasema sana, siwezi labda nije tu kushinda”
“Sawa hakuna shida, basi niahidi kuwa utafanya hivyo na hiyo Jumamosi mimi nitakufata ili twende wote nyumbani”
“Hakuna shida”
Tony hakufikiria kuwa kitu anachotaka mama yake kumpima Tumaini kitakuwa kikubwa, kwani aliamini kila mwanamke lazima awe anajua kupika tena vizuri tu, ingawa hakuwahi kula chakula cha Tumaini ila aliamini kupika anaweza.
Wakati wanaongea ongea, mfanyakazi mmoja wa pale alienda kumuuliza Tumaini,
“Yule mama wa chakula kaja, sijui akuletee nini leo?”
“Ana pilau?”
“Amesema ipo ndio”
Tumaini akamuangalia Tony na kumuuliza,
“Unapendaga pilau?”
“Napenda ndio”
“Pilau ya huyu mama ni nzuri hatari, ngoja niagize tule”
Kisha akamgeukia Yule msichana na kumwambia,
“Mwambie alete pilau sahani mbili, pilau kuku eeeh! Aweke kachumbari ya kutosha na Yule wa juisi mwambie atuletee juisi glasi mbili”
Yule dada akaondoka, ila kwa kitendo kile cha Tumaini kujua hadi vyakula vitamu kilimpa moyo Tony kuwa Tumaini lazima kwenye kupika yupo vizuri, maana hadi anajua chakula kitamu na kibaya.
Baada ya muda chakula kile kililetwa na wakaanza kula, kiukweli kilikuwa kitamu sana hata Tony alikiri kuwa ni kitamu hadi alikipenda,
“Hiki chakula balaa, ni kitamu sijapata kuona. Huyo mama anajua kupika sana, na kuku yake nzuri sana”
“Ni kweli anajua kupika, sasa siku uje ule ndizi utumbo weeee utajikata vidole kwa utamu, anaweka na nazi ni tamu sana”
“Ila pilau kama hii anaipikaje? Mbona wengi wanapika ila sio tamu hivi”
“Mmmmh mwenzangu, kupika kipaji ujue, nahisi huyu mama ni kipaji chake jamani yani anaweza kupika haswaaa”
Akatamani kumuuliza kuwa na yeye anaweza kupika nini cha kusifiwa na watu ila hakutaka kwakweli alihisi pengine anaweza kumuudhi kwahiyo hakumuuliza.
Wakati wanamalizia malizia kula, alifika Erick na kuwakuta wakila, alicheka na kusema,
“Hatimaye dada yangu amepatikana, na wewe umekuwa na mpenzi Tumaini?”
“Toka zako huko”
Erick alicheka tu na kusalimiana na Tony pale huku akimwambia,
“Karibu kwenye ukoo wetu kaka, ila sijui ndio nitakuitaje? Shemeji shemeji, hahahah shemeji mara mbili”
Tony akauliza,
“Kwani vibaya?”
Tumaini akataka kubadilisha mada na kumwambia Erick,
“Erick, nikuagizie chakula, pilau ya huyu mama ni tamu balaa”
Erick akajibu,
“Hapana, yani nimepitia tu hapa mara moja ila sasa hivi naenda kwangu nitakula huko. Chakula cha Erica ni kitamu zaidi, siwezi nikala huku halafu nikashindwa kula chakula cha mke wangu”
Tumaini akauliza,
“Hivi Erica anajua kupika eeeh!”
“Ndio, siku nitawakaribisha kwangu na mke wangu ataandaa chakula mtahisi kimetoka hotelini ila sitaki kumpa mzigo wa kupika maana sasa ni kijacho Yule”
Wakacheka tu, wakaongea ongea pale kisha Erick akawaaga na kuondoka zake kuelekea nyumbani kwake.

Na kweli Erick alipofika tu alimkuta Erica ameshapika tena chakula anachokipenda siku zote, kisha akaandaa na kuanza kula pamoja,
“Erica mke wangu, uwe unapumzika nataka nikuletee msichana wa kazi akusaidie saidie hapa nyumbani”
Erica alifikiria jambo, alifikiria kuhusu msichana wa kazi aliyekuwa nyumbani kwa dada yake kipindi kile na jinsi alivyotembea na shemeji yake, akakataa
“Hapana sitaki msaidizi”
“Kwanini Erica?”
“Sitaki tu”
“Najua unawaza mawazo potofu, mimi nakupenda wewe hata waje wanawake mia moja mbele yangu wakiwa watupu na wewe umevaa ila bado nitakuchagua wewe, Erica amini hilo kuwa nakupenda sana yani hakuna msichana hata mmoja mwenye nafasi kwenye moyo wangu zaidi yako wewe, nakupenda sana malkia wangu”
Erica alifurahi sana kusikia vile ila Erick alimuomba hata kuleta msaidizi ambaye atakuwa anaenda pale nyumbani mchana na kuondoka jioni, mwishowe Erica alikubali kuhusu lile swala alilolisema Erick.
Basi walipomaliza kula simu ya Erick ilianza kuita na alipoiangalia akaona ni namba ya mama yake akapokea,
“Uko wapi saa hizi Erick?”
“Nipo mjini mama”
“Nakuomba ofisini kwangu mara moja kabla sijaondoka”
“Mama, nakuomba nije kesho maana kuna mambo namalizia”
“Mjinga wewe, yani kuniongopea tu. Hutaki kusema ukweli kuwa unaishi na Erica ulidhani sitajua ujinga wako? Na ni biashara gani hiyo ya kuishi na mtoto wa watu bila baraka za wazazi, sasa kesho uje ofisini”
Simu ikakatika, Erica alimtazama Erick na kumuuliza,
“Inamaana mama yako hakujua kama tunaishi wote?”
“Hakujua”
“Hukumwambia? Si ulisema utamwambia kila kitu!”
“Erica mpenzi, siku ile mambo yaliingiliana ndiomana siku ongea nae, ni siku ambayo nilijua kuwa Dora ni muathirika pia nikajua kuwa uliwahi kuwa na mahusiano na George nikapaniki sana”
“Ila Erica mambo mengine bhana, nakumbuka wakati tunaanza mahusiano ulisema tufute yote yaliyopita kwetu, sasa kwa mtindo huu mimi sio nitakufa kwa presha maana sidhani kama kuna rangi umeacha katika kuhangaika na wanawake”
“Mmmh tuache hizo mada Erica”
Yani Erick hakupenda kabisa kuongelea swala la wanawake zake waliopita. Walianza kuongelea tu mustakabali wa nyumba yao unavyoendelea kwa kipindi hiko.
 
SEHEMU YA 436


Erick alifika nyumbani kwake na kukuta lile gari la vifaa lishafika ndio linatua vifaa kwahiyo alisaidiana nao kwanza kisha akaenda ndani, alimkuta Erica na mwanae wamelala muda huo, akamuamsha Erica,
“Kheee utalala nini usiku? Au mambo yale ya kuanza kunishurutisha tukeshe?”
Erica aliinuka pale kitandani huku akitabasamu na kumuuliza Erick kuwa za sehemu aliyotoka na Erick alimpa habari njema ya mama yake kwenda wiki ijayo kwao, kwakweli ile ilikuwa ni habari njema sana kwa Erica kwani alijua kwa vyovyote vile lazima mamake akiongea na mtu mzima mwenzie basi ataelewa,
“Asante sana kwa hilo Erick”
“Usijali Erica ni kazi yangu, ila ngoja nikuulize’
“Niulize”
“Derick ni ndugu yako, ila undugu wako na yeye umekuwaje kuwaje yani?”
“Ni historia ndefu Erick, naomba tuachane na hayo”
“Hapana nieleze Erica”
Erica aliona kumueleza Erick kuhusu mambo ya yeye na Derick ni kujichafulia tu, yani hakutamani kabisa ila kwavile Erick alimsisitiza sana kuwa anahitaji kujua ukweli Erica aliamua kusema ukweli bila kujua kuwa Erick alishakutana na Derick au vipi, Erica alimueleza kila kitu yani kwa mara ya kwanza Erica hakuficha chochote kile kwa Erick, alijitoa muhanga kuwa liwalo na liwe maana mambo mengine aliona kila anavyozidi kuyaficha ndio yanavyozidi kumuumiza.
Ila alishangaa sana kumuona Erick akitabasamu tu kanakwamba ile habari haijagusa moyo wake kabisa, ndio kwanza alimkumbatia Erica na kumwambia,
“Wewe ndio mke wangu, baada ya misukosuko yote sasa umepata pumziko lako la moyo, na mimi baada ya kutangatanga kote sasa nimepata pumziko langu la moyo. Kwasasa najua hakuna habari tena nitakayosikia kuhusu wewe na ikaniumiza wala kwa upande wako hakuna tena habari itakayokuumiza kuhusu mimi”
Erick alionekana kumfurahia tu Erica kisha kuendelea na mambo yao mengine tu na huku wakifurahia swala la wao kuwa pamoja.

Bado Babuu alikuwa na wazo la kumuoa Zainabu, akamuomba siku hiyo apate sehemu ili azungumze nae vizuri maana kila alichoongea bado zainabu alionekana kutokuelewa.
“Hivi kwanini Zainabu hutaki kukubaliana na upendo wangu? Nakupenda kweli, nahitaji uwe mke wangu”
“Babuu, nina miaka thelathini na tatu na wewe una miaka ishirini na tisa huoni tofauti kubwa hapo? Yani kuna tofauti ya miaka minne kweli jamani? Hapana kwakweli”
“Kwani tukioana hiyo miaka inabandikwa kwenye paji za uso, yani mtu akiniona anajua nina miaka mingapi na wewe una miaka mingapi kweli Zainabu? Mimi nakupenda, sidhani kama miaka ni kitu kikubwa katika maisha, unaweza kukutana na mwenye umri mkuwa ila hana akili za malengo na wewe ila mimi nina malengo na wewe Zainabu, ni kweli nakupenda”
“Ila umri tumetofautiana sana Babuu, mimi ni sawa na dada yako tu. Hata watu wakituona watadhani nimekulazimisha kunioa”
“Zainabu, maswala ya kujali maneno ya watu hayafai hata kidogo, ukifikirira ya watu huwezi kusonga mbele, fikiria furaha yako, fikiria maisha yako. Mimi sikuwahi kufikiria kuoa kabisa kwa muda huu ila tangu nimekuona wewe natamani sana kuwa na mke, tafadhali Zainabu nikubalie”
Wakati Babuu anaongea na Zainabu, ile sehemu akakatisha Dora na alivyowaona alisimama, akasogea na kumsalimia Babuu,
“Kheee ndio wewe uliyekuwa unakuja chuo kumlilia lilia Erica! Khee mbona umependeza sana, umekuwa mzuri hadi raha, huyu ndio wifi nini”
Babuu alimuangalia tu Dora maana alionekana kumaliza maneno yote mwenyewe, ila swala la kumuuliza kuwa Yule ndio wifi alimuitikia basi Dora akasema,
“Ila mmependezana sana, Mungu awabariki”
Kisha Dora akaondoka, kwakweli Babuu alishukuru sana maana aliwahi ongea na msichana huyo chuoni kwakina Erica na aliweza kumuona alivyo na mdomo mchafu.
Basi kwakuwa muda nao ulienda sana ikabidi ajitoe kumrudisha Zainabu kwao ila bado alimsisitizia swala la kumpenda ili akikubali basi apelike washenga kwakina Zainabu na amuoe kabisa.

Kesho yake Tony kama alivyokuwa amepanga alienda kumchukua Tumaini ili kumpeleka nyumbani kwao ila hakumwambia ukweli kama mama yake anahitaji kumchunguza kwani alijua lazima Tumaini akatae ukizingatia hapendi kuchunguzwa.
Basi alifika nae kwao na leo mama yake alimkaribisha vizuri sana yani kama sio Yule anayegombanaga nae.
Basi Tumaini alifika pale na kukaa ambapo mama Erica alimtuma Tony sehemu ya mbali kidogo kwani hakutaka aone chochote, Tony akaondoka pale kwao. Mama Erica alitoka na kanga na kumpa Tumaini ajifunge kisha akamwambia,
“Jifunge hii mwanangu tuje kusaidiana kupika kidogo huku jikoni”
Tumaini akaongozana nae hadi jikoni, sababu ilikuwa inakaribia mchana basi mama Erica alibandika sufuria la ugali na kukorogea uji kisha akamwambia Tumaini asonge ule ugali, Tumaini akauliza
“Kwanini nisipike mboga? Mama songa tu ugali mwenyewe”
“Hapana, mboga nitapika. Tusongee tu ugali mwanangu”
Basi Tumaini akaanza kuusonga ule ugali, kwakweli mama Erica alijihisi kucheka jinsi jasho jembamba lilivyokuwa likimtoka Tumaini hadi huyu mama ilibidi atoke jikoni na kumfata Bite,
“Njoo uone kituko cha kaka yako, ugali wa watu wanne tu unamtoa haja, njoo uone”
Bite akaenda kuchungulia jikoni, ni kweli Tumaini alikuwa na hali mbaya sana kwenye kuusonga ule ugali maana alijaza unga halafu ukamshinda kusonga, mama Erica alimfata na kuzima jiko kisha akamuuliza,
“Mbona umejaza unga hivyo?”
“Nilikuwa naweza unga basi ukawa unanirukia kama kuniunguza hivi ndio nikajaza, naomba nisamehe”
“Umewahi kusonga ugali Tumaini?”
Alikaa kimya tu, mama Erica akarudia tena kumuuliza,
“Umewahi kusonga ugali Tumaini?”
“kiukweli sijawahi kusonga ugali”
“Si ungeniambia tu kuwa hujawahi jamani! Haya nitaupika tena, basi maharage yale na nazi nishakuna uyaunge mwanangu sawa au hujui pia?”
“Hapana najua”
Basi mama Erica akaanza kupika tena ugali na Tumaini kuachiwa kuunga maharage ya nazi, alipomaliza alizima jiko na mama Erica alienda kuangalia maharage yaliyoungwa na Tumaini, alimuita Bite, huku Tumaini yuko pale pale,
“Bite mwanangu sijataka kucheka peke yangu, angalia maharage yameungwa nazi haya”
Bite aliangua kicheko kitu kilichomfanya Tumaini ajihisi vibaya sana.

Baba Nasma hakutaka kukubali kuwa dawa zake zimedunda kumuita Bahati basi siku hiyo akafunga safari na kwenda kwa mganga mashuhuri, alipofika na kumueleza shida yake Yule mganga alimwambia.
“Mmmh huyu mtu anaonekana mzito sana, tukishindwa unajua dawa itakurudia”
“Hana uzito wowote huyu mtu, najua haiwezi kushindikana nataka tumamalize kabisa maana ananisumbua na dawa zangu”
Basi Yule mganga akaanza kusaidizana nae kufanya zile dawa, ila katika hali ya kushangaza sana baba Nasma alianguka chini na kuwa kimya gafla.


Basi Yule mganga akaanza kusaidizana nae kufanya zile dawa, ila katika hali ya kushangaza sana baba Nasma alianguka chini na kuwa kimya gafla.
Yule mganga alijaribu kumuita lakini Yule mzee hakuitikia kabisa, alimshika shika na kumuona yupo kimya, muda kidogo simu ya Yule baba ikaita, basi Yule mganga akaichukua na kuangalia, akaona jina la mpigaji, ‘Binti yangu Nasma” basi Yule mganga akaipokea na kuanza kuongea, ila kabla hajaongea alimsikia Nasma akisema,
“Baba uko wapi? Usiende tena kwa mganga nimepata suluhisho”
Yule mganga akamjibu Nasma,
“Baba yako yupo huku kwangu, ameanguka na hajitambui kabisa”
Nasma alishtuka sana na kuhitaji kupewa maelekezo ya mahali alipo baba yake. Yule mganga alivyokata simu aliendelea kufanya jitihada za kumuamsha baba Nasma.
Kwa upande wa Nasma alikuwa kwake ila ile habari ilimchanganya vilivyo, aliamua kwenda kwao ili kutaarifu ndugu zake na waende pamoja.
“Mama, nimepata habari baba kaanguka huko kwa mganga”
“Jamani huyu mzee anachotafuta ni nini? Anatafuta kifo huyu, kilichompeleka kwa mganga tena ni nini?”
“Hata mimi nilimkataza wakati ananiambia swala lake la kwenda kwa mganga maana alisema dawa za kumuita Bahati zimegoma”
“Haya ni makubwa sasa kajitafutia, huyo Bahati mshamtesa sana mnafikiri hajabumbuluka tu! Lazima naye ana mganga wake, kapikwa huko kachemshwa huko, unafikiri utamvuta kirahisi tu. Hebu wapigie simu ndugu zako wengine twende tukamuone na tumuwaishe hospitali”
“Mmmh mama uliona wapi uanguke kwa mganga upelekwe hospitali! Ngoja twende huko huko tutapata tu jambo la kufanya.
Basi akaita na ndugu zake wengine na kuanza safari, ni ilikuwa mbali kidogo walipokuwa wakielekea, kwakweli walisikitika sana kwa baba yao kuacha mambo yake na kwenda mbali hivyo kwa mganga.
 
SEHEMU YA 437


Kwa maneno ya pale kwakina Erica yalimfanya Tumaini achukie sana na kutaka kuondoka ila wakati anataka kutoka mlangoni tu akakutana na Tony ambaye alimrudisha ndani kujua nini tatizo, muda huo Tumaini alikuwa amejiinamia chini tu. Tony akamuuliza mama yake,
“Mama, kwani nini tatizo?”
“Nenda jikoni kwanza kajionee kitu cha nazi ndio uje kuuliza nini tatizo, halafu funua kuna sufuria nimefunika pembeni jionee huo ugali wa kula wewe na mkeo”
Tony alienda jikoni kwao, kiukweli alishangaa sana na hakuamini kama Tumaini anaweza kupika vile, akarudi sebleni na kuuliza,
“Nani kapika vile?”
“Unadhani ni nani humu ndani anayeweza kupika mauzauza ya aina ile? Mwanamke uliyemleta hajui kupika yani hajui kabisa kabisa, halafu hataki kusemwa, yeye ni nani katika ulimwengu huu asisemwe? Mtu mzima kama Tumaini ashindwe kusonga ugali wa watu wanne! Ashindwe kuunga maharage ya nazi! Anatupikia mauzauza jamani, yani nazi inasimama dede kweli!”
Tony akajua pale lazima wamemsema sana Tumaini, akajawa na huruma moyoni mwake, akamuangalia mama yake na kumwambia,
“Mama ulinifundisha kazi zote mimi, ulijua ni kazi za kike ila ulinifundisha na nikazijua. Mwanzoni sikujua kwanini umenifundisha ila nikaelewa kuwa niweze kujitegemea pindi ninapoachwa mwenyewe, ila sasa naelewa zaidi kuwa uliona pengine naweza kuoa mwanamke asiyeweza kufanya kazi za kike basi nikamfundisha na tukasaidiana nae. Asante sana mama kwa kunifundisha basi Tumaini atafundishwa na mimi maana huyu ndio mke ambaye kachaguliwa na moyo wangu”
Bite na mama Erica wakatazamana na kusikitika sana, kisha mama yao akasema,
“Unajudanganya Tony, sikukufundisha ili uende kuoa mauzauza kama haya hapana kwakweli”
Bite akaongezea,
“Yani mwanamke ni bonge hata picha za harusi tu hazitapendeza na bado ana kasoro nyingine jamani loh! Unaishije na mwanamke asiyejua kupika! Ataweza kufua kweli huyo, kuosha vyombo, kusafisha ndani au ndio mtajaza wasichana wa kazi kila mahali!”
“Dada, ngoja nikuulize kwahiyo wewe ulivyokuwa unaweka wasichana wa kazi nyumbani kwako ilikuwa kwavile hujui kupika, hujui kuosha vyombo sijui kufua? Hata ujue kupika vipi elewa kuna mkali zaidi yako. Kila siki mama hapa analalamika kuhusu Erica na wakati huo huo anasema hiki chakula angepika Erica kingekuwa kitamu sana, mbona wewe hajawahi kukusifia si inamaana unapika cha kawaida tu, sasa kwanini umshangae Tumaini atajifunza na ataelewa”
“Tony usijifanye unajua sana kulitetea hilo tipwatipwa lako...”
Ile kauli ndio ikamfanya Tumaini ainuke kabisa na kuondoka, Tony aliamua kumfata Tumaini ili aweze kumbembeleza.
Ndani alibaki Bite na mama yao, Bite akasema
“Na aondoke tu, mwanamke kichefichefu, mtoto wa kike hujui kupika jamani ni aibu”
“Ila Bite hapa ni pa kujifunza, unajua huyu Tumaini sio kosa lake ila ni kosa la mama yake yani kapata malezi mabovu huyu, angeweza kupika hata ugali wa mtu mmoja ila anakwambia hajui kabisa ni malezi mabovu kayapata huyu”
“Sasa mama nijifunze nini hapo?”
“Weee nae, unatakiwa kujifunza kulea watoto hakikisha mwanao anaweza kazi zote za nyumbani bila hivyo ataumbuka ukweni kama hivi”
“Hiyo kazi aofanye Erica kwa Angel, mimi mtoto wangu wa kiume huyu sina shaka”
“Bite nawe unaongea kama mgonjwa, utafikiri James alikurushia vidudu sasa vimekimbilia kichwani, aliyekwambia mtoto wa kiume hafundishwi kupika nani? Anatakiwa kujua pia, unafikiri akioa mwanamke kama Tumaini bila kumjua humo ndani si watakula vyakula vibichi hadi wakose choo! Tunatakiwa kufindisha watoto wote kupika, kama mama hakikisha unawajibika vyema kwa mwanao.”
Bite alimuitikia tu ila anamuonaga mama yake kuwa kigeugeu sana maana huwa anabadilika badilika.
 
SEHEMU YA 438

Tony aliondoka na Tumaini kuelekea nae kwao maana Tumaini alionekana kuchukizwa kabisa, alifika nae kwakina Tumaini na kuingia nae ndani bila kujali kuwa pale alitimuliwa, muda kidogo alifika Erick na kuwakuta sebleni ambapo Tony alijaribu kumuelewesha Tumaini maana yeye ni mtu wa kuchukia tu.
Erick aliwasalimia na kusogea karibu yake, alipomuangalia vizuri dadake aligundua kuwa kuna kitu kimemkera, basi alikaa na kumuuliza tony,
“Kwani tatizo nini?”
Ilibidi Tony aeleze kwa ufupi tu kuwa alienda kwao na Tumaini sasa akashindwa kupika na ndugu zake wakamshambulia kwa maneno. Baada ya kuambiwa vile Erick alianza kucheka hadi Tumaini akainuka kumuangalia na Tony ikabidi amuulize,
“Sasa mbona unacheka?”
“Mimi nilijua tu kuna siku itatukia kama hivi Tumaini, nilikuwa nakwambia mara kwa mara hapa kuwa ujifunze kupika sio kusifia tu chakula cha sehemu Fulani kizuri sijui cha sehemu Fulani kizuri maana una mtindo huo sana, jifunze kupika ili watu wasifie mapishi yako wewe. Kufika Chuo sio kujua kila kitu, kuna vitu vingine ni vya kujifunza kimtaani tu”
“Sasa ndio unicheke? Si uniambie kiustaarabu tu, hata hivyo Erica anajua kupika basi awe ananifundisha kupika”
“Hakuna tatizo, Erica anakupenda kwanza atajihisi vibaya kweli kwa hayo yaliyokutokea kwao. Ila pole dada yangu maana Yule mama mmmh! Simpatii picha kapata na cha kuongea si ndio balaa”
Tony akasema kidogo,
“Ila mama ni wa kumzoea tu Yule jamani”
Erick akamwambia Tony,
“Ndio ni wa kumzoea ila kwasasa ni wewe Tony ndio inabidi uwe mstari wa mbele, kuhakikisha dada yangu hadharauliki wala hasemwi vibaya, yani wewe kama mwanaume unatakiwa kuwa mstali wa mbele kufukia kasoro za mwenzi wako, mfano mimi Erica nampenda na kuna ambayo yalipita kwake ila kama mwanaume naamua kusimama upande wake na kumtetea na kuaona kama yale yaliyopita ni changamoto tu. Tumaini haina haja aje kujifunza kupika kwa Erica ila wewe kama mwanaume wake na kupika unajua basi huna budi kumfundisha na panaposhindikana basi unamuuliza Erica. Pole dada yangu”
Tumaini aliitikia tu, kisha Tony akaongezea
“Mimi ningemfundisha tatizo baba yenu hanitaki kabisa hapa, yani akinikuta ni balaa”
“Na huyu mzee nae, hakutaki sababu ipi?”
“Sababu sina gari na nyumba”
“Kwani kila anayeanza maisha ana gari na nyumba? Kila kitu ni mwendo, hakuna anayefika mia bila kuanza na moja. Halafu maisha hayafanani, shemeji yangu usijali nitashughulika swala la dada yangu kujifunza kupika”
Kisha akamwambia kuwa Tumaini asijali kitu maana atakuwa anaenda kumchukua kazini na kumpeleka kwake ili ajifunze funze kupika kwa wifi yake na kisha kurudi nyumbani, alifanya hivyo ili baba yake asiwe ana elewa awe anajua kuwa Tumaini anaendaga kazini na sio kwake.
Kisha wakaongea ongea pale na kumwambia lengo lake,
“Nimekuja kuchukua gari yangu bhana na kukurudishia yako”
“Sawa, ila gari haina mafuta”
“Hamna shida, nitapitia tu kujaza hayo mafuta ila la kwako nilijaza kwahiyo usiwe na wasiwasi”
“Asante”
Kisha Erick akabadilishana funguo pale na dada yake halafu akaondoka maana hakupanga kukaa kwa muda mrefu pale kwao.

Erick alikuwa akirudi nyumbani kwake, ila alipitia kwenye kituo cha mafuta ili kujaza mafuta gari yake kwani dadake alishamwambia kuwa ile gari haikuwa na mafuta ya kutosha, alipokuwa pale kwenye kujaza mafuta, kuna mtu alisogea na kugonga kioo chake, alipomuangalia alimuona kuwa ni Rahim.
Erick alishusha kioo na kusalimiana nae, ambapo Rahim alimwambia Erick kuwa ana mazungumzo nae kidogo, Erick hakuona tatizo kuzungumza na Rahim kwani hakuwa na ugomvi nae. Basi alingoja amalize kujaza mafuta kisha wakaelekea kwenye mgahawa mmoja wapo na Rahim na kukaa kwaajili ya mazungumzo.
“Erick napenda tuongee kuhusu Angel”
“Sawa nakusikiliza”
“Unajua Angel ni damu yangu na nina haki kuwa nae sababu mimi ni baba yake mzazi”
“Sawa Rahim sikatai kuwa wewe ni babake mzazi, ila mimi ni babake mlezi kwahiyo kitu gani ulikuwa unataka? Angel aje ucheze cheze nae au kitu gani unataka?”
“Erick, sijasema tuongee kwa shari ila mimi inaniuma ujue, nina haki kwa Angel halafu anatumia majina yako inakuingia akilini hiyo?”
“Kutumia jina sio tatizo, mimi babangu mzazi anaitwa Jimmy lakini hakuna mahali utakapokuta Erick Jimmy unajua kwanini?”
“Eeeh kwanini?”
“Sababu hakunilea ila kutoitwa jina lake hakujazuia yule mzee kuwa baba yangu mzazi, ni baba yangu mzazi na ninamuheshimu sana. Erica hakukurupuka kumuita Angel Erick, ni sababu wewe hukujali kuhusu mtoto, ulikuwa ukimjibu vibaya na ukimdharau sababu kakuzalia, uliona hatoweza kuishi bila ya wewe na hapohapo hukuthubutu kutoa hela ya matumizi ya mtoto, sio kwamba hukuwa na uwezo! Hapana ila uliamua tu yani ilikuwa ni maamuzi yako kumkomesha Erica ila ulisahau kuwa unamkomesha na mtoto, yule malaika asiyejua chochote na wala hakuhusika kwenye starehe zenu ila ukaamua kumkomesha pia. Angel kutotumia jina lako hakukufanyi wewe kutokuwa baba wa Angel ila unakuwa baba yake kwa misingi ipi? Hujamuoa Erica na unajua ni lazima ataolewa, je akiolewa basi Angel ni jukumu la mume wa Erica na kama ni hivyo basi inamaanisha yule mume ndio baba halali wa Angel. Mzazi mwenzio anapokuwa na mahusiano na mtu mwingine pia sio mwisho wa wewe kuwa baba wa mtoto, unatakiwa kucheza mahali pa kulea mtoto, hivi kwa mfano ungekuwa hata unajitoa nije nishinde shinde na Angel nicheze nae akuzoee hivi angeacha kukupenda? Ungekuwa unamuhudumia mtoto hata kwa kidogo tu usingeonekana wa maana? Ingekuwa hivyo basi Erica asingechukua hatua ya haraka kumbadilisha mtoto jina maana angewaza kuwa unamuhudumiaga”
“Lakini wakati nipo kwenye mahusiano na Erica nilikuwa nampa sana hela”
“Ulikuwa unampa za kumtunza yeye, kwasasa ulitakiwa kuonekana kwa Angel, na kumuhudumia mtu sio mpaka umpe hela, hata ile kujali kwako, kutumia muda wako kwaajili yao kunaonyesha ni jinsi gani unavyojitoa. Ila Rahim hujawahi kufanya hivyo, jirekebishe usishangae watoto wa nje wote wakakukataa pengine hadi na wa ndani nao wakakukataa kama hujui kujirekebisha.”
“Erick unaongea sababu hujui uchungu wa mtoto, hujawa baba wewe”
“Usinichekeshe, kuna baba na baba jina. Wewe kwa Angel ni baba jina, bado hujawa baba kamili kwa Angel, laity ungefanya majukumu yako lazima Angel angekupenda na Erica angekuheshimu hata angeolewa na mwanaume mwingine bado angeweka akilini kuwa Angel ana baba yake anayemjali na kumpenda”
Yale maneno yalimuingia sana Rahim na kujikuta hana kingine cha kuongea na Erick, ikabidi waagane tu.
Erick aliendelea na safari ya kurudi kwake muda huo.
Alimkuta Erica yupo tu akimbembeleza mtoto kulala, ila Angel alipomuona Erick alikimbilia kwa Erick na kulala mikononi mwake.
Baada ya Angel kulala, Erick alikaa na Erica na kuanza kuongea nae habari ambazo zilionekana kumpa rah asana Erica,
“Eeeeh unapenda kuvaa shela la aina gani kwenye harusi yetu?”
“Mmmh lini nitaenda kuchagua shela? Tusichelewe sana Erick kabla tumbo langu halijawa kubwa, nahitaji kusherekea vizuri harusi yetu”
“Tutaenda kuchagua tu shela usijali”
“Halafu nataka kwenye kitchen party yangu nivae nguo kiasilia, nitapendeza eeeh!”
“Ndio utapendeza sana, ila hivi kitchen party ina umuhimu gani?”
“Aaaah ni ile sherehe inahudhuriwa na wanawake tupu halafu wanafundisha namna ya kuishi na mume”
“Namna gani tena Erica, mimi na wewe si tunafundishana humu humu ndani!”
“Erick hujui tu, yani kichen party ni nzuri sana ukiwa mdada, halafu sendoff na mwisho harusi”
“Si utachoka sana mpenzi jamani!”
“Sichoki bhana, hayo ni matukio ya kawaida tu mpenzi”
“Sawa hakuna shida mpenzi wangu”
Erick alimshika Erica kwa upendo sana na kumfanya ajihisi raha mno kuwa karibu na Erick.
Usiku ulipofika waliamua tu kulala ila kila mmoja alifurahia uwepo wa mwenzie.

Asubuhi na mapema, Fetty alienda kwakina Bahati na kumkuta Bahati akisoma Kuran, kwakweli alifurahi sana kwa kuona Bahati amebadilika kiasi kile, basi akamngoja amalize halafu ndio akaanza kuongea nae;
“Basi jana usiku nimeota adui yako amekufa”
“Amekufa?”
“Ndio nimeota amekufa, tena amefia kwa nganga”
“Duh nani huyo?”
“Simjui ila nimeota adui yako amekufa”
Mara kuna simu iliingia kwa Bahati, naye akaipokea, alipata taarifa iliyomshtua kidogo mara dada yake nae akafika pale walipokaa Bahati ba Fetty na kusema,
“Bahati una habari huko! Baba mkwe wako amekufa, tena nasikia kafia kwa mganga”
“Ndio simu hii ndugu wa Nasma kanipigia duh! Alikuwa anaumwa nini?”
“Na wewe huelewi? Si nishakwambia kafia kwa mganga, kuna cha kuumwa tena hapo? Hakuna cha kuumwa labda kamloga mwenye nguvu kumliko, haya twende msibani maana alikufa jana na wanazika leo.”
Ilibidi Bahati ajiandae kwenda msibani, Fetty nae aliamua kwenda ili kujua nini kinaendelea huko msibani.
Walifika msibani na kukuta kuna wengine wanalia haswaa familia yake na wengine walikuwa wakiongea tu, kwa mara ya kwanza Bahati alisikia kwenye msiba ule marehemu akisemwa vibaya, kipindi chote hakumjua vizuri mkwe wake huyo ila siku hiyo alimfahamu kutokana na maneno ya watu wa pale msibani,
“Huyu mzee alikuwa mchawi sana, bora amekufa jamani maana alikuwa akitutesa sana hapa mtaani”
“Mtaa mzima alikuwa akiogopewa balaa sababu ya uchawi wake na akigundua tu kuwa una maendeleo basi utake usitake utamuoa binti yake”
Walikuwa akiongea pale bila kujua kuwa Bahati ni mkwe wa Yule mzee aliyekufa, kisha muda wa kuzika ukafika na wanaume wakaenda makaburini kuzika na wanawake kubaki nyumbani yani Fetty alihakikisha anakaa hadi mwisho wa msiba ili asikilize vizuri na kweli alisikia vizuri sana kilichokuwa kinazungumziwa, aliwasikia wamama wawili wakimzungumzia mzee aliyekufa,
“Jamani mzee alikuwa tishio huyu dah! Bora amekufa tutapumzika jamani”
“Sijui nani kamuweza jamani”
“Nilimuonea huruma Yule kijana Bahati masikini aliuvaa mkenge bila hata kujua, akaja kuoa kwa huyu mzee”
“Lazima alirogwa, huyu mzee unadhani kuna mkwe wake aliyemuacha!”
“Alikuwa ni mjumbe wa siku zote kwahiyo unajikuta unatakiwa tu kuwasiliana nae, huyu mzee ujumbe tu akigombea mwingine anammaliza sijui angekuwa mbunge ingekuwaje jamani, huyu mzee bora Mungu kamchukua tu akapumzike na sisi tupumzike jamani”
Fetty alisikitika sana kwa zile habari za Yule mzee alizozisikia, waliporudi kuzika Fetty alimfata Bahati na kumtaka warudi tu, Bahati hakubisha wala nini maana alijikuta akipenda sana kumsikiliza Fetty kwa kipindi hiko, na walivyofika nyumbani akamuaga na kuondoka zake.
 
SEHEMU YA 439

Dora tangu apate yale majanga hakurudi kwao kabisa yani alikuwa anaenda kwenye mambo yake na kurudi nyumbani kwa James kanakwamba kashaolewa na James vile, na walikuwa wanaishi tu vizuri kama mke na mume na alivaa nguo za Bite ambazo zilibaki kwa mume wake.
Siku hiyo kwa mara ya kwanza alienda Kanisani na James na alivaa nguo ya Bite ambayo Bite alipenda sana kuivaa ilikuwa ni nguo ya kitenge, walipotoka Kanisani walipitia kunywa supu ambapo wakati wa kuondoka Dora alitangulia nje halafu James alienda maliwatoni. Akiwa pale nje alikutana na Tony ambaye alikuwa akikatisha kwenye mgahawa huo, alimshangaa sana Dora kuvaa nguo za dada yake, alizijua sababu dada yake alipenda sana kuvaa nguo hizo, alimuita
“Dora”
Dora aligeuka, na Tony alimsogelea kuongea nae,
“Mbona umevaa nguo za dada Bite?”
“Hata salamu hakuna jamani! Kwani hizi nguo zimeandikwa Bite au?”
“Hapana ila nazitambua hizo nguo sababu alikuwa akizipenda sana”
“Ukiona hivi ujue nimechukua nafasi ya dadako”
“Kwahiyo ndio unaishi na shemeji James!”
“Hayo ni majibu”
“Yani Dora wewe ni msichana wa ajabu sana, ni bora niliachana na wewe maana sio kwa akili mbovu kama hizo za kwako wewe”
“Nina akili mbovu lakini toka dadako aishi na James muulize kama kuna siku amewahi kumshawishi James waende wote Kanisani zaidi yay eye kwenda peke yake! Lakini mimi na akili zangu mbovu nimeweza kumshawishi James na leo tukaenda Kanisani”
“Ama hilo Kanisa liliingiliwa leo, yani mtu kama wewe uwende Kanisani, kweli majanga. Ila bora niliachana na wewe”
“Kwahiyo wewe kuwa na Yule Tumaini ndio unajiona mjanjaaa eeeh! Unakuwa na mwanamke hata mahusiano yake ya nyuma hayaelewi atakuwa anajua kitu huyo!”
Tony akaona kuendelea kuongea na Dora ni kujiaibisha tu, wakati anataka kuondoka akakutana na James akienda alipo Dora, ila Tony hakuongea nae chochote zaidi ya kusikitika tu.
Muda huu aliondoka na kwenda nyumbani kwao na alipomkuta dada yake alimpa taarifa kuwa akachukue nguo zake tu,
“Hivi James anashindwa kumnunulia nguo huyo mwanamke wake hadi avae nguo zangu jamani!”
“kazichukue tu dada”
“Hapana sitazichukua tena ila naona bora nikafungue mwenyewe shtaka la talaka ili James anipe talaka yangu nijue moja.”
Bite alikuwa na hasira sana na Dora maana alihisi kuwa ni mtu mbaya sana kwake.

Leo Babuu alitafuta wazee wa hekima na mshenga kwenda kujitambulisha kwakina Zainabu kwani alikuwa na lengo haswaa la kumuoa, basi walijitambulisha ila Babuu alikuwa na mashaka sana kuwa Zainabu anaweza kukataa ile posa ila Zainabu alikubali na wale kufata taratibu zote za kujitambulisha, wageni walivyoondoka tu pale, leo Mrs.Peter alienda pia nyumbani pale maana hawakuonekana tena tangu wajitambulishe kwahiyo alienda kuomba msamaha,
“Jamani mnisamehe bure hata sijui imekuwaje maana muhusika mwenyewe tukimuuliza hatujibu vizuri kwakweli”
“Hata msijali, wamekuja wengine leo na wamesema wiki ijayo wanakuja kumaliza kila kitu na ndoa kabisa”
Mrs.Peter alishangaa sana ila hakuweza kuongea zaidi na kuagana nao kisha akarudi nyumbani kwake, alimuita mwanae Rahim kumuuliza tena kuwa imekuwaje kuhusu swala la kumuoa Zainabu,
“Eeeh Rahim mwanangu imekuwaje mbona sielewi?”
“Mama, nimeona hakuan maana kuongeza mke wa pili wakati Salma yupo, ananitosha kwakweli”
Yale maneno Salma aliyasikia yani aliona rah asana, aliondoka pale mlangoni alipokuwa akisikiliza na kwenda kumpigia simu Yule mama maana kwake ilikuwa rah asana,
“Niambie mwali wangu, unakero nyingine?”
“Aaaah hapana ila nataka nikupe ushuhuda mwingine, jamani leo nimemsikia mume wangu kwa masikio yangu akimwambia mama yake kuwa hana sababu ya kuoa tena wakati mimi nipo”
“Oooh hiyo ni habari njema binti yangu, sasa siku ukiwa na muda njoo nyumbani kwangu nikufundishe staili ambayo inapendwa sana na wanaume yani mwanaume wako ukimfanyia staili hiyo hata iweje hakuachi abadani”
“Jamani natamani hata nije leo, ila kesho nakuja mama yangu yani naona raha jamani, sijawahi kupendwa kama hivi, huu ndio upendo niliokuwa nauota kila siku maishani”
“Sawa binti yangu yani ukiwa na mimi hakuna mume atakayethubutu kukuacha maana utakachompa kitamfanya akuwaze muda wote na kila muda akuonapo atamani kuwa na wewe karibu kwahiyo usijali”
Salma aliendelea kuongea na Yule mama huku wakipanga mambo mbalimbali na Rahim nae bado aliendelea kuongea na mama yake,
“Sasa nimeenda kule nimekuta kuna watu wametoka pale nasikia wiki ijayo wanaenda kumaliza kila kitu na kumuoa kabisa Zainabu”
Rahim alijihisi vibaya sana, alilaumu sana ukimwi maana ndio umesababisha kumkosa mwanamke mwenye maadili yake kama Zainabu.
Aliongea pale na mama yake ila moyoni mwake alikuwa na mipango mingine kabisa kuwa lazima ajue siku ambayo Zainabu atolewa ili aende kushuhudia na akiweza kupinga ndoa hiyo basi aipinge kwani bado moyo wake alihisi kuwa na hisia na Zainabu.

Jumatatu, mapema kabisa, Bite alijiandaa kwenda mahakamani kwani alitaka kwenda kuandikisha mwenyewe talaka na alitaka kujua taratibu za kuweza kupata talaka yake.
Aliingia kwenye ofisi ila alishtuliwa na mtu mmoja, kumuangalia akamkuta ni kijana ambaye aliwahi kusoma nae, Yule jamaa alimuita,
“Kheee Bite jamani! Upo!”
“Nipo Deo”
Wakakumbatiana kwa furaha na kukumnbushana baadhi ya mambo ya shule,
“Vipi familia, umeolewa nini?”
“Ndio, mbona niliolewa zamani tu”
“Na nyie wanawake mnapenda kuolewa mapema balaa, junaweza kuamini mimi bado sijaoa”
“Kheee na utu uzima huo hujaoa jamani kwanini!”
“Maisha tu, naona wanawake wote waongo jamani, waaminifu mliolewa tayari”
Bite akacheka tu ila alipogundua kuwa Yule anahusika na pale mahakamani aliamua kumueleza kuhusu swala lake, kwakweli Deo alishangaa sana kumuona mtu akiongea kwa furaha kumbe anaugulia moyoni kwa aliyotendewa na mumewe.
“Pole sana, ngoja nikwambie taratibu za talaka”
Basi Deo alimueleza Bite talatib zote za kudai talaka, ambapo iliandaliwa na barua ya kumtaka James afike mahakamani pia, alimrahisishia sababu ni mtu anayemfahamu na wakati wa kuondoka alimsindikiza.
Wakiwa njiani alimuuliza,
“Una watoto wangapi kwasasa Bite?”
“Mmoja tu, na wewe je?”
“Mimi nina wawili ila bado sijaoa”
“Mama yao yuko wapi?”
“Aaah si unajua ujana tena, hao watoto mama zao ni tofauti, ujana maji ya moto wewe acha tu”
Basi waliongea pale na kupeana mawasiliano vizuri na kuagana.
Bite wakati anaondoka akiwa kwenye daladala maana siku hiyo hakutembea na gari yake, aliona mafuta yanamgharimu sana.
Aliwaza vitu mbalimbali ikiwa na kukumbuka kuwa kipindi wanasoma twisheni, Deo aliwahi kumtongoza, akakumbuka jinsi Deo alivyokuwa akimsifia na kumpa ahadi nyingi ila Bite hakuona kama kuna malengo kwenye maisha ya Deon a ndiomana alivyojitokeza James aliona ni vyema kuolewa nae, alivyokumbuka hivyo alicheka mwenyewe na kujiuliza,
“Sijui Deo anakumbuka kuwa aliwahi kunitongoza mmmh!”
Akatabasamu tu na kuelekea nyumbani kwao.

Nyumbani kwakina Bahati walijikuta wakizungumza kuhusu Fetty maana wamemuona mara kadhaa na walijaribu kumuuliza Bahati aliwajibu kuwa hakuna chochote kati yake na Fetty, dada yake mmoja akamwambia,
“Ila Yule mwanamke anaonekana anafaa kuolewa na wewe Bahati, kwanza ana maadili halafu anaongea vizuri. Umemfahamia wapi Yule?”
“Ni rafiki wa Erica Yule”
“Kumbe!”
Wakaangaliana tu ila wakaendelea kusema,
“Ila kiukweli Bahati Yule Nasma hakufai tena, yani hafai kuwa mke wako kabisa”
“Katika akili yangu simuwazi kabisa Nasma, na nimeandaa siku maalumu ambayo nitamtuma mtu ampelekee talaka tatu yani simtaki kabisa”
“Unaandaa siku ya nini kaka, mtume mtu hata leo ampelekee talaka yake”
“Nangoja amalize matanga ya msiba wa baba yake maana ndio ametoka kufiwa Yule kwahiyo atajifanya anachanganya matukio”
“Kwahiyo utamuoa Erica?”
“Siwezi kumpata Erica kwasasa ila ningempata basi ningemuoa nampenda sana ila bado sitaki kuwa mbali na Erica, hivyobasi ninawazo na Yule Fetty kwasasa”
Dada zake walisikika wakipiga kigelegele kwani walitamani sana kaka yao aseme hivyo ingawa hata wao kwa wakati huo walitamani sana kaka yao ampate Erica ila uwepo wa Fetty uliwavutia pia, ila walimuuliza
“Na vipi kuhusu Siwema?”
“Nitamlea tu mimba hadi mtoto akizaliwa nitamlea maana ni damu yangu ila wazo la kumuoa Siwema halipo pia, ile familia hapana kwakweli imenichosha kabisa”
Wakati wanapanga panga, Fetty nae alifika ila alivyotokea tu mbele yao aliwashangaa wakipiga vigelegele, alicheka na kuuliza,
“Kuna nini jamani hapa?”
“Utajua tu wifi”
“Wifi! Kheee kivipi?”
Iibidi Bahati abadili kidogo mada kwani hata kumtongoza Fetty alikuwa bado hajamtongoza.
 
SEHEMU YA 440

Dora aliamua kurudi kwao leo, kwakweli mama yake alimsema sana,
“Huna akili hata kidogo, ni kweli unalalaga nje kwa siku moja na zikizidi sana mbili ila safari hii umezidisha Dora, kwanini hujiheshimu mwanangu? Hivi hutaki leo na kesho kuwa na familia yako!”
Dora alitamani kumwambia mama yake kuwa ameathirika ila alijua ni lazima mama yake atajihisi vibaya sana, na mama yake aliendelea kuongea
“Yani sio wewe sio mdogo wako mnaniumiza kichwa kabisa, mdogo wako nae karudi leo asubuhi hivi mnachofanya ni haki kweli? Kwanini mnanitesa hivi, nione balaa kuzaa watoto kama nyie jamani, ndiomana kuna watu wanasemaga bora angezaa mbuzi anywe supu kuliko binadamu mwenye akili fupi. Dora mwanangu, mamako nimehangaika, nimekusomesha nikiamini leo na kesho utanikomboa kwenye ufukara ila ndio kwanza unasemaga mimi ndio nimekufundisha uwe muhuni sababu sikuwa na hela ya kukupa, kweli Dora! Unasahau malezi yote niliyokupa. Mtoto huna shukrani hata kidogo”
Dora hakumjibu mama yake kwani alijua ni kuzidi kumuongezea hasira tu, basi alimuomba msamaha tu na kwenda chumbani kwake.
Baada ya muda Steve alimuita dada yake na kuongea nae,
“Dada, nilikuomba unitafutie kazi ila hujanitafutia hadi leo unajua kinachoendelea?”
“Nini kinaendelea kwani?”
“Baada ya Sia kukataliwa na familia yote ya Erick, kaamua kutafuta mwanaume mwingine anasema awe anapata pesa ya kutunza ujauzito wake kwahiyo dada kwa Sia kuna mume mwenzangu”
“Wewe nae ulivyomkazania huyo Sia loh! Hatuli hatunywi ni Sia Sia ila uroho wako ndio umekuponza kuwa na mwanamke asiyejielewa kama Sia. Itabidi nifanye kazi ya ziada siku nimpate Yule mwanamaombi nimlete pale kwa Sia ili madawa yaachie ubongo wako huo”
Ila ilikuwa kama anajisumbua tu kwani baada ya muda kidogo Steve aliondoka kwao na kuelekea kwa Sia.
Jioni ya siku hiyo Dora alifikiria sana na kuona ni vyema amueleze mama yake ukweli kuhusu hali yake ya kiafya maana kama kumficha ni atamficha hadi lini, basi alimuita chumbani kwake na kuanza kuongea nae,
“Mama kuna jambo nataka nikwambie”
“Ni jambo gani hilo?”
“Mwanao nilienda hospitali kupima ukimwi…”
Akaona moyo wa mama yake ukienda mbio na huku akiuliza kuwa aambiwe nini kimetokea,
“Huko hospitali wakasemaje Dora, niambie mwanangu, nina watoto wawili tu mimi niambie mwanangu eeeh!”
“Punguza presha basi mama”
“Sawa mwanangu niambie, eeeh hospitali walisemaje mwanangu?”
“Nimeambiwa nimeathirika”
Yule mama kabla Dora hajaendelea kuongea tu alizimia na kumfanya Dora achanganyikiwe huku akifanya utaratibu wa kumpeleka mama yake hospitali.

Dora alitafuta vijana wa kuweza kusaidiana na mama yake na kumpeleka hospitali, walifika nae hospitali na ikaonekana presha ya mama huyo ipo juu sana kwahiyo Dora ilibidi ashughulike pale na mama yake ambaye kwa siku hiyo alilazwa hapo hospitali.
Dora alirudi kwao na kujilaumu sana kumwambia mama yake ukweli kwani katika siku zote huyu mama alionekana kuogopa sana ugonjwa wa ukimwi kuliko kitu chochote kile ndiomana presha ilimpenda sana.
Kiukweli siku hiyo usiku Dora hakulala vizuri na kuwaza tu hali ya mama yake, basi asubuhi na mapema aliamka na kuandaa chakula kwaajili ya mama yake ile asubuhi, akaondoka kwao na kuanza safari ya kwenda hospitali.
Kuna mahali alipita kabla ya kufika hospitali palikuwa na nyumba ya kulala wageni na humo alitoka Sia, alimshangaa sana na kusema
“Sia”
Ila Sia alimnyamazisha na kumuomba asiongee kwa nguvu,
“Dora imenibidi kufanya hivi kwani sina jinsi na hela sina kwahiyo nitaleaje mtoto huyu atakayezaliwa? Kuna mwanaume nimempata nina wiki nae sasa yupo vizuri, ananisaidia kipesa, sasa jana alisema nije kulala nae hapa guest ningekataaje na nina shida na hela?”
“Sia kuna magonjwa wifi yangu eeeh! Mdogo wangu bado mdogo Yule, nilikwambia kila siku uende kwenye maombi mdogo wangu akomboke na midawa ile ila hata hutaki, mdogo wangu angekomboka angeanza kufanya kazi na angekulea wewe na mtoto ila kwasasa anashindwa kwani muda wote anakuwaza wewe, atawezaje kufanya kazi?”
“Nitafanya hivyo ila usiseme kama unanifahamu kuhusu mdogo wako maana Yule mwanaume anatoka sasa hivi kwahiyo nitasema wewe ni rafiki yangu”
Na muda kidogo Yule mwanaume alitoka ndani, basi Sia alitaka kumtambulisha kwa Dora ila kabla ya kumtambulisha Dora alijikuta akijishika kichwa baada ya kumuona Yule mwanaume kwani alikuwa ni George.


Na muda kidogo Yule mwanaume alitoka ndani, basi Sia alitaka kumtambulisha kwa Dora ila kabla ya kumtambulisha Dora alijikuta akijishika kichwa baada ya kumuona Yule mwanaume kwani alikuwa ni George.
Dora alijikuta akisema,
“Mama weeeee!”
Sia alimuangalia kwa mshangao kuwa ni vipi ila kabla hajamuuliza, Dora aliweka mzigo wake chini na kwenda kumkunja George huku akisema,
“Unajijua kabisa ni muathirika lakini unaenda kusambaza ukimwi kwa huyu mwanamke mwenye mimba”
Inaonyesha George hakuelewa vizuri kuwa Sia ana mimba, kwahiyo alionekana kushangaa tu kuwa Sia ana mimba, na kutoa mikono ya Dora iliyomkunja na kumuuliza Sia,
“Nilikuuliza mbona una tumbo kubwa ulisema ni asili ya tumbo lako, kumbe una mimba!”
Dora alisogea katikati yao na kumwambia Sia,
“Huyu mwanaume ana ukimwi, umeua mdogo wangu Sia”
Ile habari ilionekana kumchanganya kabisa Sia kwani alikimbia pale na kumuacha George akiangaliana na Dora, wakati huo Dora alitaka kumvaa mwilini George ili apigane nae sema alipomwangalia vizuri George alimuona kaweka sura ya tofauti na pale akajua kama atamsogelea tena basi atachakazwa, aliinama na kuchukua kifurushi chake ila moyo wake uliuma sana.
Kwa siku ya kwanza Dora alitembea njiani huku machozi yakimuanguka kwani aliwaza kuhusu mama yake kama akijua habari hizo si ndio atakufa kabisa, alipatwa na mawazo sana ila alipokaribia kuingia hospitali alifuta machozi yote na kuingia kumuona mama yake,alishukuru kumuona ameamka na kumpa uji aliobeba ili anywe, mamake alikunywa ule uji ila hakuongea chochote kile yani alionekana akimuangalia tu Dora basi.
Dora hakukaa sana mahali pale kwani alimuaga mama yake na kuondoka kutokana nay ale mawazo aliyokuwa nayo.
Hakuelewa aelekee wapi kwa muda huo ila aliamua kwenda moja kwa moja nyumbani kwao ambapo alijifungia na kulia sana huku akisema,
“Naona kama kila kitu kimenigeukia, nilimpeleka Sia kwa mganga na dawa zikamrudia mdogo wangu, nimesambaza ukimwi na ukimwi umemgukia mdogo wangu. Mungu jamani kwanini lakini, kwanini mimi? Mama yangu atakuwa na hali gani pale akigundua kuwa wanae wote tumeathirika? Mimi kupata ukimwi ni halali yangu ila sio Steve jamani!”
Alijikuta akilia sana ila wazo likamjia kuwa hata akilia hakuna atakachofanya,
“Natakiwa niende kwa Yule mwanamaombi niongee nae maana kulia tu haitasaidia kabisa, nahitaji mdogo wangu awe huru, mdogo wangu asiteseke kwa makosa yangu jamani Dora mimi, nilisema nitamlinda Steve, nini nimefanya sasa jamani? Eeeeh Mungu wangu nihurumie Dora mimi”
Basi akaondoka pale kwao na kuanza kuelekea kwa mwanamaombi.

Kama ambavyo Erick alipanga basi alienda kumchukua dada yake dukani na kwenda nae nyumbani kwake ili akafundishwe kupika na Erica, walifika na kumkuta Erica ametulia tu kisha Erick alimuacha dadako hapo.
Ilikuwa ndio siku ambayo Tumaini alizungumza vizuri na Erica kuliko siku zote, Erica alimuuliza,
“Nianze kukuelekeza kupika nini? Yani chakula gani ambacho hujui kupika”
“Nifundishe kusonga ugali, nielekeza kupika maharage ya nazi halafu nielekeze kupika wali kwenye mkaa”
“Kwani wali unapikaga wapi?”
“Yani mimi mara nyingi napika wali kwenye rice cooker kwahiyo kama siku ile mama yako angesema nipike wali kwenye mkaa ingekuwa shughuli nyingine ila ugali ndio kabisa yani sijawahi kupika”
Basi Erica alianza kuelekezana nae na vingine kupika nae pamoja, walifanya vitu vyote pamoja hata chakula cha siku hiyo walipika pamoja.
Wakiwa wamekaa kupumzika, Tumaini alimshukuru sana Erica na kumwambia,
“Kwakweli Erica wewe ni binti wa ajabu sana yani umesahau kila kitu nilichokuwa nafanya kukupinga jamani ila umenielekeza kwa moyo safi kabisa, asante”
“Usijali wifi yangu”
Tumaini akacheka na kuendelea kuongea,
“Kwakweli uwifi sasa ndio umenoga jamani maana tumekuwa mawifi haswaaa ila kwanini mawifi tunakuwa na hila kiasi kile nilichokuwa nakufanyia wewe jamani! Hata sijui kwanini nilikuwa nakuchukia jamani Erica wakati mwanzoni nilikupenda sana hata nikakwambia uwe mdogo wangu ila kile kitendo cha kutambua ni wifi yangu eti nikakuchukia balaa bila sababu yoyote, sasa ndio yaliyonitokea kwenu duh dadako anaongea jamani hadi nilijihisi vibaya, mara aniseme bonge yani dada yako dah alifanya niumie sana moyoni”
“Mzoeee tu, ila ndio maisha yalivyo”
“Ila dadako Yule hana mawifi kwa mumewe eeeh!”
“Ndio, mumewe hakuwa na madada hata hivyo familia ya mumewe ipo mkoa mwingine yani yeye alipata bahati ila katika maisha kila kitu kina uzuri na ubaya wake hakuna kizuri moja kwa moja na hakuna kibaya moja kwa moja”
Basi walijikuta wakijadili mambo mengi sana ya maisha kwa siku hiyo kwani ilikuwa ni siku nzuri sana kwa upande wao.
Erick alivyorudi alifurahi sana kuona Erica na Tumaini wako pamoja tena vizuri sana na ciku hiyo chakula walikula kwa pamoja huku wakisifia na kukumbushana siku ya kwanza ambayo Tumaini na Erica walipatana na kuwa marafiki, Erick alicheka tu kwani walikuwa wakiongea habari za kuchekeshana na kusahau kabisa kama waliwahi kuwa na tofauti ya aina yoyote ile.

Dora alienda nyumbani kwa yule mwanamaombi kama alivyopanga na alipofika alimkuta ila kabla ya kumueleza chochote alianza kulia kwani hakujiona sawa kabisa, yule mama alitulia ili kumsikiliza Dora alikuwa na tatizo gani, alipotulia sasa ndio alianza kumuuliza ili Dora ajieleze,
"Una tatizo gani?"
"Hata sijui nianzie wapi kukueleza?"
"Wewe nieleze yote yani usifiche kitu, nieleze ili nione nawezaje kukusaidia. Ngoja tuombe kwanza ili Roho mtakatifu atusaidie"
Basi yule mama akaomba kwa muda kidogo halafu alipomaliza ndio Dora alianza kujielezea yale yanayomsibu.
Dora akapumua kidogo, kisha akaanza kumueleza, ingawa yalikuwa ni maelezo marefu ila huyu mama aliyasikiliza kwa makini.
Dora alianza kumuelezea alimdanganya Erica kuwa ana ukimwi ili Erica amuhurumie na kumpatia pesa atakazopewa na mzee Jimmy, kisha akamueleza alivyokwenda kwa mganga kwaajili ya kupata dawa ya mapenzi na shida yake ilikuwa ni kumteka James sababu tu James alimfanyia kitendo kibaya cha kumbaka, kisha akaeleza alivyompeleka Sia kwa mganga kwaajili ya dawa za mapenzi na jinsi mdogo wake alivyokunywa dawa hizo, pia akamueleza jinsi alivyopima na kukutwa na ukimwi na kuamua kuusambaza ugonjwa huo na mwishowe kwa aliyoyagundua siku hiyo.
"Leo nimemkuta meanamke niliyemuambukiza ukimwi akiwa na mwanamke ambaye ndio yule aliyempa madawa mdogo wangu, yani mdogo wangu anaathirika kwasababu yangu, hana hatia Steve ila sababu yangu jamani. Nakumbuka Ericq alinionya ila sikusikia na kujidai kuwa sina mdogo wa kike wa kuweza kutembea na wanaume niliowaambukiza kumbe nampelekea janga mdogo wangu! Na hivi mamangu yupo hospitali maana jana nilivyomueleza kuwa nina ukimwi basi presha ikampanda ndio kalazwa. Yani sielewi hapa, naamini maombi yako ni ya kweli, namuomba Mungu amfungue mdogo wangu, namuomba Mungu mdogo wangu asipatwe na ukimwi nilioueneza. Namuonea huruma mama, katuzaa kwa uchungu na katulea bila msaada wa baba halafu leo hii nimefanya fedheha ya namna hii kweli!! Najijutia mimi Dora"
Dora akawa analia sana, ni wazi mambo ya siku ile yalimuingia akilini maana hakuwa na furaha kabisa, huyu mwanamaombi akaanza kuongea nae sasa,
"Dora, unaamini ya kwamba Mungu anafanya? Mungu anaweza yote?"
"Ndio naamini'
"Basi kabla ya yote yakupasa uokoke, umkabidhi Yesu maisha yako. Je upo tayari nikufanyie sala ya toba?"
Dora aliona ni sawa kuokoka yani kwa muda huo alikuwa tayari kwa chochote kwaajili ya maisha ya mdogo wake na mama yake. Yule mama alimfanyia sala ya toba na baada ya hapo akamueleza,
"Mungu wetu ni Mungu mwenye rehema nyingi, ni Mungu wa hurumq ni Mungu wa Neema. Ukisoma Zaburi 145 mstari wa 8 na 9 unasema “8. BWANA ana fadhili, ni mwingi wa huruma,Si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema,
9. BWANA ni mwema kwa watu wote,Na rehema zake zi juu ya kazi zake zote.” Neno la Mungu li hai na linatufundisha tuwe wakamilifu wakati wote. Umechagua jambo jema kukabidhi maisha yako kwa kristo sasa kitu cha kufanya kwa sasa unakijua?"
"Ndio, natakiwa niombe kwaajili ya mdogo wangu na mama yangu"
"Ni kweli ila unatakiwa uombe kwanza kwaajili yako mwenyewe maana wewe ndio umesababisha yote haya. Unatakiwa uingie kwenye maombi ya toba, yani wewe tubu mbele za Mungu, maombi ya toba yanatuweka karibu na Mungu hakuna aliyesafi mbele za Mungu ila tunajitahidi tu kuenenda katika njia zake, yatupasa kuomba toba. Omba toba kwaajili yako kwa kukesha kwa waganga, omba toba kwaajili ya kusambaza ukimwi. Halafu uwe unaamini kuwa Mungu anakusikia, yani kwasasa uwe katika maombi ya toba. Tutafanya mfungo wa siku tatu yani kuanzia kesho, ni vyema uwe unakuja hapa tunajifunza neno na kuingia kwenye maombi, ili vifungo vyako vifunguliwe ni kuingia kwenye maombi ya toba kwanza na maombi haya yanamuweka Mungu karibu yetu. Omba toba binti yangu yani usichoke wala usijihesabie haki kwa Mungu kwani Mungu atakupa unachostahili. Umenisikia"
"Sawa, sawa"
"Ni kweli kesho utaanza mfungo huo?"
"Ndio nitaanza kufunga"
"Sheria za kufunga unazijua?"
"Hapana sizijui"
"Asubuhi na mapema ingia kwenye maombi ili Mungu akueaidie na huo mfungo, halafu usizini, usiende kudanganya yani katika dhambi zote dhambi ya uongo ina baba yake kabisa ambaye ni shetani, ukiwa muongo ni moja kwa moja unajiunganisha na shetani na kumtoa Mungu katika maisha yako kwahiyo unakuwa umemchagua shetani kuwa baba yako kwamaana hiyo funga yako haitakuwa ya salama. Na yale unayotambua ni dhambi usifanye, unanielewa lakini?"
"Nakuelewa"
"Kesho saa ngapi unakuja?"
"Saa kumi jioni"
"Najua siku ya kwanza ibakuwaga ngumu sana maana utajikuta umetamani chakula, ila kumbuka dhumuni la mfungo wako. Mungu akusaidie binti yangu"
Dora alimshukuru sana yule mama ambapo alifanya maombi na kumruhusu Dora kuondoka muda huo.
 
SEHEMU YA 442

Bahati alionyesha dhamira yake ya ukweli kwa Fetty, hivyo siku hiyo aliandaa talaka na kumpa mtu akampelekee mkewe maana hakuhitaji tena kuishi nae.
Na upande mwingine alitafuta rafiki yake wa karibu kwenda kujitambulisha kwakina Fetty na kufanya harakati za kuoana nae, hakutaka kuchelewa kwani kila alipomfikiria Erica alihisi kugairisha anachotaka kukifanya kwahiyo aliona ni vyema mambo ya kuoana na Fetty yawe ni haraka haraka ili akae na Fetty kwenye nyumba.
Ndugu zake walisaidiana nae kuhusu swala hilo na walisema watahakikisha mambo yatakuwa haraka haraka, dada wa Bahati alienda nyumbani alipokuwa anaishi Bahati na mkewe kwani alitaka Nasma aondoke, alimkuta Nasma katulia kamavile hajapewa talaka,
“Kwahiyo unajisahaulisha Namsa au? Hivi hujui kama umepewa talaka?”
“Kwahiyo kama nimepewa talaka ndio nini?”
“Unatakiwa kuondoka hapa”
“Sikia nikwambie wifi yangu, yani hapa siondoki sijui mtaniondoa na greda au nini ila hapa siondoki kabisa”
“Sasa Bahati anataka kuoa mke mwingine”
“Aoe tu na atanikuta mimi humu humu. Tena ngoja nikwambie wewe nahisi ndio unajisahaulisha, si wewe uliyekuwa ukishadadia mwanzo kuwa kaka yako tumuwekee dawa anioe sio wewe? Si wewe uliyeniambia hadi chakula anachopenda Bahati yani kinachofaa mimi kumuwekea dawa, si wewe? Saizi unataka kujusahaulisha, saizi unajifanya kama hujui. Nimezaa na kaka yenu mnataka niondoke eti kanipa talaka niende wapi sasa? Baba yangu ameshakufa, mnataka mimi niende wapi na mtoto? Yani siondoki tena siondoki kabisa semeni lingine”
“Unajivunia nini wewe?”
“Najivunia ndoa niliyofunga na Bahati, hii talaka siitambui kabisa, talaka ya kutumwa mtu kuniletea? Jamani siondoki, yani hapa labda mniue ila kuondoka siondoki kabisa”
Yule binti aliwakatalia katakata, dada wa Bahati hakutaka kufata sheria maana aliona huyu binti atapata mali ambazo hata hajazitolea jasho ila kwajinsi alivyokuwa anakataa hakuwa na jinsi zaidi ya kurudi kwao na kushauri ndugu zake kuwa wakafate sheria tu maana hakuna namna nyingine.

Mzee Jimmy alienda kwa Ester na kuongea nae, alionekana akijutia mambo yake mengi aliyoyafanya zamani,
“Unajua sikujua kama nimeathirika kumbe nimeathirika zamani tu na nimekuwa nikiambukiza watu ukimwi”
“Kheee hatari Jimmy, ila mimi nina ushauri mmoja tu kwako. Unatakiwa kuokoka”
“Hapana bhana, huo ushauri hapana Ester nitafutie ushauri mwingine, nitaokokaje na wakati sina mke? Nitaokokaje na wakati bado nina kiu na pombe? Nitafutie ushauri mwingine bhana”
“Ushauri wangu kwako ni huo tu Jimmy, unatakiwa kuokoka.”
“Nishauri vingine ila kuokoka hapana jamani”
Basi akamuaga pale ili kuondoka, akashangaa na Dora kufika eneo lile, alimuuliza
“Na wewe umefata nini hapa?”
Ester alimjibu,
“Mwenzio ameokoka”
Mzee Jimmy alicheka sana kisha akamwambia Ester,
“Naona huna kazi za kufanya, hivi hilo swala la kushauri makahaba waokoke nani amekutuma? Yani hadi huyu kahaba unamuita mlokole, wewe mwanamke umechoka kweli”
“Tatizo Jimmy mbishi”
“Sio mbishi, hebu wewe jione ulivyo eti umeokoka na tangu umeokoka umepata faida gani? Toka kipindi kile unatukataa wakina Jimmy kwa madai ya kuokoka, sasa unapata faida gani zaidi ya kujiongezea umasikini. Nitakupeleka siku moja nyumbani kwangu, pamoja na ukimwi wangu huu na ulokole wako huo utanikubali tu najua sababu sijawahi kukufikisha kwangu, endelea tu kudanganywa na huyo kahaba kuwa ameokoka, loh kumbe wanaokoka hadi vichaa! Kwa hilo hunipati, kwaheri”
Mzee Jimmy akaondoka zake, ila huyu mama alimsikitikia sana na kuendelea na mafundisho yake na Dora.

Erick leo jioni alitoka na Erica pamoja na Angel walienda kwenye duka moja la nguo za harusi na kuchagua nguo hapo huku Erick akimwambia Erica,
“Yani kwenu wakikubali tu hata sitaki kuchelewesha mambo, nitakuoa haraka sana. Nahitaji tuishi kama mke na mume, tafadhali nakuomba Erica kwenu wakikubali tu basi tusicheleweshe mambo”
“Erick nilivyo na hamu ya kuolewa na wewe jamani naanzaje kuchelewesha mambo jamani, kwanza mamako anaenda lini kwetu?”
“Alisema Jumamosi yani keshokutwa, kwahiyo mambo yananukia Erica”
“Ila naomba hiyo siku twende pamoja, nimekumbuka sana nyumbani”
“Hakuna tatizo, tutaenda wote tu”
Erica alikuwa akitabasamu tu na kuingoja hiyo siku kwa hamu kwani aliona kama ndio siku ya ndoa yake. Waliendelea kuangalia nguo na kuweka oda kwa nguo walizozipenda, wakati wanatoka pale dukani, wakakutana nje na Derick, ambaye alipomuona Erica alimkimbilia na kumkumbatia ila leo Erica alikuwa kama sio yeye kwani alimsukuma Derick kwa nguvu hadi Derick alianguka chini, kile kitendo kilionekana kumfurahisha sana Erick kwani alicheka mno.
Derick aliinuka kwa hasira kwani aliona kama Erica amemdhalilisha, akataka amsogelee ila Erick alikaa mbele ya Erica kwani Angel alikuwa chini tu amesimama, Erick alimuangalia Derick na kumsikitikia sana kisha akamwambia,
“Shida za maisha yako usitake kumaliza kwa wengine, wanawake wapo wengi sana duniani kwani ni lazima kuwa na dada yako!”
“Sikuwa na nia ya kumfata ili tuwe pamoja, nilitaka kumsalimia ila ona alivyonisukuma jamani kama kichaa”
“Ndio unajiona una akili timamu? Mwenye akili timamu hawezi kufanya kama wewe unavyofanya Derick, unatakiwa kuwa mpole na kutayarisha tu tumbo lako hilo lisilo na shukranu kula msosi kwenye harusi yetu nimesema halina shukrani maana ukila ukimaliza utaenda chooni kujisaidia kwaheri”
Erick alimbeba Angel na kumshika mkono Erica na kuelekea nae kwenye gari yao kisha wakaondoka na kwenda nyumbani.
Mawazo ya Erica yalikuwa ni harusi yake tu kwani alivyofika nyumbani hata akaanza kujaribisha na miondoko atakayotembea siku ya harusi yake,
“Inaonekana umefurahi sana”
“Yani naona raha mno, naona kama ndio leo vile jamani nimemkumbuka mama yangu loh! Jumamosi niende kumuona tu”
Muda ule ule simu ya Erica iliita na Erick alivyoiangalia aliona ni mama yake Erica anapiga kwahiyo akampa apokee ili aongee nae,
“Mwanangu jamani nimekukumbuka! Mimi ni mzazi lazima niongee mwanangu maana mdomo nimeumbiwa ila nimekukumbuka sana mwanangu, nimemkumbuka mjukuu wangu Angel, eeeh Erica unakuja lini nyumbani?”
“Junamosi mama”
“Mwanangu uje kweli, nimekukumbuka sana mwanangu, njoo tuongee. Mjomba wako kaniuliza leo nimekosa hata jibu la kumjibu kuwa tulisomesha mtu au paka, jamani mwanangu nimekukumbuka sana. Mwambie Erick aje afanye taratibu za ndoa yenu, nakukumbuka sana mwanangu”
“Usijali mama, Jumamosi tunakuja na mamake Erick”
“Oooh hiyo ni habari njema sana mwanangu tena njema mno, nafurahi kuisikia habari hiyo karibuni sana”
Erica aliongea ongea pale na mama yake na kukata simu ila alikuwa na furaha kubwa sana kuona hata mama yake amemkumbuka maana hakufikiria kama inaweza kuwa rahisi kiasi hiko.
Basi Angel alipolala Erick alimwambia Erica,
“unajua furaha ya leo haijakamilika”
“kwanini Erick?”
“Tukifanya mambo yetu ndio itakamilika”
Erica alicheka tu ila alijua lengo la Erick kwa muda huo ni kitu gani na kwenda kulala nae tu kwa muda huo.

Asubuhi na mapema Ijumaa, Bite aliamkia kule mahakamani na alipomaliza mambo yake Deo alihitaji kuondoka nae. Waliondoka na kwenda kuzungumza,
“Unajua Bite wewe ni mwanamke mzuri unatakiwa ukae kwenye ndoa na mwanaume aliyetulia na utulie pia, naomba uwe mke wangu. Yani swala la talaka na mumeo likiisha basi uwe mke wangu tafadhali nakuomba Bite”
Kwakweli sababu Bite alikuwa na hasira na mume wake na alitaka kumuonyesha kwamba ingawa tumeachana basi nimepata mwingine mwenye upendo wa dhati, alijikuta akikubali kuwa na Deon a siku hiyo hiyo Deo alimuomba aende nae kwao akamuonyeshe ili Bite aijue familia ya Deo, kwakweli Bite aliona ule ndio upendo wenyewe yani mwanaume asukumwi kuwa nipeleke kwenu ila anaamua mwenyewe kumpeleka mwanamke kwao, basi walipomaliza maongezi pale walianza safari ya kwenda kwakina Deo.
Walifika kwakina Deon a kukaribishwa vizuri sana, kisha Deo alimtambulisha mama yake kuwa Yule ni mwanamke aliyempata na anahitaji kumuoa,
“Karibu mwanangu, ila huyu Deo ana watoto wawili utaweza kuwatunza?”
Deo alimkatisha kidogo mama yake,
“Mama jamani ndio maswali gani hayo?”
“Lazima tuulize mwanangu, kama hukumwambia basi ndio namwambia ajue una watoto wawili je ataweza kuwatunza?”
“Nitaweza mama”
“Haya karibu sana”
Ila Deo hakusema kwao kama Bite anafatilia talaka kwa mume wake, yani hilo swala Deo hakuligusia kabisa, wakati wanamuaga mama yao, akamwambia Deo,
“Dadako anakuja muda sio mrefu, subiri afike nae amfahamu wifi yake”
Na kweli mlango ulifunguliwa na mama yao akasema,
“Ndio huyo, karibu mwanangu”
Bite alishangaa sana kwani wifi yake huyo alikuwa ni Tumaini, alikumbuka jinsi alivyomshushua Tumaini kwao yani alijihisi joto mwili mzima na hakuweza kukaa zaidi na kuamua kuaga tu muda huo huo na kuondoka.

Ile harusi ya Babuu na Zainabu ilifanyika nyumbani kwakina Zainabu siku hii ila Rahim hakujua kinachoendelea kwahiyo alitulia kwake tu, badae akasikia kuwa kuna harusi na Zainabu kaolewa na muda huo anaondoka na mume wake, alijikuta akitoka kwake na kwenda haraka kwa kina Zainabu ila aliwakuta ndio wanaishia, alipouliza vizuri alishangaa kuambiwa kuwa babuu ndiye aliyemuoa Zainabu, kwakweli alimuona Babuu kuwa msaliti mkubwa sana kwake na hafai kabisa, alirudi kwao kwa hasira na kumfata mama yake,
“Kumbe mama Babuu ndio kaenda kumuoa Zainabu?”
“Babuu?”
“Ndio mama, yani Babuu alikuwa akinisindikiza kwa Zainabu kumbe anamtaka yeye!”
“Basi usipaniki mwanangu, Babuu ni ndugu yako huna haja ya kupaniki hivyo”
Akatoka ndani kwao na kwenda baa, akanunua bia za kutosha na kurudi nazo nyumbani kwao kisha akaingia ndani kwake na kuanza kuzinywa, kila leo mrs. Peter alimkatalia mwanae kuwa mlevi ila siku hiyo Salma alienda kumshika mkono na kumpeleka kwenda kumshuhudia mwanae akinywa pombe, aliashtuka sana.
“Kheee Rahim kumbe ni mlevi mwanangu? Yani unakunywa pombe kama maji?”
Rahim hakumjibu mama yake bali aliingia chumbani kwake na kwenda kulala.

Jumamosi ilivyofika mama Erick aliwasiliana na wakina Erick na kukutana nao ili aelekee nao nyumbani kwakina Erica, walikutana njiani wakati Erick, Erica na Angel wakiwa kwenye gari la mbele halafu mama yao akifata nyuma kwenye gari.
Kufika kwakina Erica walisimamisha magari nje kisha wakina Erick wakashuka na mama Erick alishuka, Erica alisogea kumsalimia mama Erick, ila Yule mama alivyomuona mtoto wa Erica alichukia sana na kusema,
“Yani Erick kila atakayemuona huyu mtoto atajua wazi kuwa si damu yako, kwakweli leo nimejionea makubwa, ngoja nikaongee na huyu mamake Erica anitolee haya mauzauza”
Yani mama Erick ndio alitangulia mbele kamavile anaifahamu nyumba ile, alipoingia getini tu mama Erica nae alikuwa ametoka ndani kwake, wakaonana na kukumbukana wakakimbiliana na kukumbatiana. Erick na Erica walishangaa pale getini kuona mama zao wanafahamiana.
 
SEHEMU YA 443

Yani mama Erick ndio alitangulia mbele kamavile anaifahamu nyumba ile, alipoingia getini tu mama Erica nae alikuwa ametoka ndani kwake, wakaonana na kukumbukana wakakimbiliana na kukumbatiana. Erick na Erica walishangaa pale getini kuona mama zao wanafahamiana.
Hawa wamama walionekana kufurahiana sana na kuingia ndani ambapo mama Erica alimkaribisha vizuri sana mama Erick,
“Karibu mdogo wangu Julieth”
“Wow na jina hujanisahau kweli Mungu ni mwema, nimefurahi sana kukuona dada Agness”
Wakaingia ndani ila Erick na Erica hawakuingia kwani walijikuta wamesita kidogo wakijiuliza maswali mawili matatu, Erick alimuuliza Erica,
“Mama yangu na mama yako wamejuana vipi?”
“Hata naelewa basi! Nashangaa tu ila inatisha hii kitu, sitaki kusikia habari kuwa sisi ni ndugu”
“Hakuna kitu kama hiko Erica”
“Mfano tukaambiwa ni ndugu itakuwaje?”
“Erica, kwa jinsi ninavyokupenda hata waseme ndugu yani hata waseme sisi ni mapacha lazima nitakuoa, bora nife kuliko kukukosa. Erica, haiwezekani sisi kuwa ndugu, nina baba yangu una baba yako, nina mama yangu na wewe una mama yako”
“Itakuwa ni vyema kama sisi sio ndugu ila mimi nadhani tusubiri kwanza hapa nje wakituita ndani ndio twende tukaongee nao”
“Hapana Erica, usiwe muoga hivyo twende tu tukaongee nao. Nishakwambia hata tuwe ndugu lazima nikuoe yani swala la mimi kukuoa wewe lipo ndani ya damu na haliwezi kubadilika”
Basi waliinuka na kwenda ndani, waliwakuta mama zao wakiongea kwa furaha sana.
“Jamani milima haikutani ila binadamu hukutana kwahiyo wewe ndio mama yake Erica?”
“Ndio ni mimi, na wewe ndio mama yake Erick?”
“Ndio ni mimi, yani kipindi chote hiki nasema nitakutana wapi na Yule dada kumbe Mungu katumia njia nyingine kabisa. Huyu ndio Yule mtoto wa kipindi kile jamani dah!”
Mama Erick alimuangalia Erica bila kummaliza, kwa mara ya kwanza mama Erick alisimama na kwenda kumkumbatia Erica kwa furaha aliyokuwa nayo kwa wakati huo, Erick ndiye aliyeuliza,
“Jamani mama mmefahamiana vipi hebu tutoeni tongotongo tujue”
Mama Erick alianza kuelezea,
“Najua sijawahi kukupa historia yako najua pia hujui ni kwanini huwa namchukia baba yako, ila siku zote hizi nilitamani sana kukutana na huyu mama basi nimpe shukrani zangu tu”
Erick na Erica walitulia kusikiliza kuwa ilikuwaje, mama Erick aliendelea kuzungumza
“Yani ni hivi hakuna kipindi nilichopata shida kama kipindi cha mimba yako Erick, nilihangaika nayo sana yani sikuwa na msaada wowote ule, siku hiyo nikiwa kwenye pilika pilika zangu uchungu ulinianza ila unajua ikawaje, huyu dada akiwa mjamzito pia ndio alinisaidia, alikuwa yupo njiani na mumewe nadhani walikuwa wanafanya mazoezi basi wakanihurumia na mumewe akakodi gari ambalo nilipanda nao na kuelekea hospitali. Wakati nakimbizwa leba, huku nyuma uchungu nae ukamuanza basi akaletwa kule leba nilipo. Yani nesi aliyetupokea akasema Majmzito kamleta mjamzito mwenzie yani hii ya leo kali, basi nilitangulia mimi kujifungua na baada ya muda nay eye alijifungua Yule nesi alituangalia akasema, “Watoto wenu ni kama mapacha, ningekuwa mimi wa kiume ningemuita Erick na wakike ningemuita Erica” Lile neno liliniingia na kunikaa sana ila sikudhani kuwa dada yangu alisikia pia. Tuliopoenda wodini ndio tulifahamiana vizuri, sikuwa na msaada wowote hivyo basi mume wa dada hapa ndio alikuwa akileta chakula tunakula pamoja yani mimi na dada hapa”
Kisha akapumua kidogo na kumuuliza Mama Erica,
“Dada shemeji nae yuko wapi nimsalimie?”
“Alikufa ndugu yangu”
Mama Erick alionekana kupooza kwa muda kwani inaonyesha hakutegemea kupata habari zile kwa muda ule, kisha akasema
“Masikini jamani kumbe alikufa loh! Kifo hiki, nilikuwa natamani siku moja nionane nae, alinisaidia sana unakumbuka dada alienda hadi kutafuta ndugu zangu na kawaatarifu kuwa nipo hospitali, jamani simsahau Yule mzee”
Mama Erica alionekana kutokutaka kukumbushwa machungu ya mumewe kwahiyo akabadilisha mada na kusema,
“Kumbe wewe Yule mwanao ukamuita Erick, na mimi nikamuita mwanangu Erica. Jamani kumbe Erick huyu ndio mwanao!”
“Ndio dada, Mungu ni mwema sana. Niliwaza nitakulipa nini kwa mambo uliyonifanyia hata kidogo tu nikupe zawadi dada yangu ila sikujua pa kukupata, kwakweli Mungu ni wa ajabu, tulisema watoto wetu watakuwa kama ndugu hawataachana ila tuliovyoondoka pale hospiatali ikawa ni mwisho wa undugu kumbe mungu ana mipango yake ya kuwaweka wote milele”
Wakafurahi na kukumbatiana tena, kiukweli ile kitu ilifanya Erick na Erica wafurahi pia.

Muda huu wakaanza kuzungumzia mahusiano ya watoto wao na wote walionekana kufurahia mahusiano yale yani hata mama yake Erick ambaye alikuwa akikataa kuhusu Erica na mtoto wake alijikuta akifurahia tu, ni pale Erick alipowaambia wazazi wao,
“Jamani wazazi wetu, imekuwa heri sana na tumefurahi jinsi mlivyofurahia ila mimi nina ombi”
Mama yake alimuuliza,
“Ombi gani mwanangu?”
“Naomba, mimi na Erica tuoane mapema iwezekanavyo yani kabla hata ya siku yetu ya kuzaliwa haijafika, nahitaji siku hiyo tuisherekee tukiwa ndani ya ndoa yetu”
Mama Erick na mama Erica waliangaliana na kisha mama Erica aliuliza,
“Itawezekana?”
Mama Erick akajibu,
“Hakuna kinachoshindikana chini ya jua, ila Erick nadhani unajua cha kufanya na unajua ni kitu gani utafanya iwezekane”
“Najua itawezekana, sitaki kukawia, nahitaji kumuoa Erica haraka iwezekanavyo. Naenda kujadiliana na baba najua itawezekana”
“Mmmh Yule baba yako atakubali kweli?”
Atakubali tu mama yani itawezekana tu, najua jinsi gani niongee nae na ninajua atakubali”
“Sawa kama ni hivyo, kwahiyo harusi itakuwa lini?”
“Kesho asubuhi mama nitapiga simu ili kuwapa ratiba kamili ya harusi itakuwa lini yani hakuna tatizo”
Mama Erica alikubaliana na maneno ya Erick ila kwa siku hiyo aliomba Erica asiondoke na abakie hapo nyumbani maana hana tatizo nae tena na hata watakapopanga mipango ya sherehe basi awe pale pale nyumbani.
Basi wakafurahi pale yani mama Erick hakutamani hata kuondoka ila ilibidi tu aondoke akaendelee na shughuli zingine.
Aliondoka pale huku akifurahia njia nzima maana alikuwa akitamani sana kukutana na huyu mama ili ampe hata zawadi kwa jinsi alivyomsaidia katika kujifungua kwake ingawa hakwenda na ndugu hospitali ila wao walikuwa ndio kama ndugu zake.
 
SEHEMU YA 444

Siku ya leo ilikuwa tofauti sana kwa mzee Jimmy kwani aliamka kwake na kujiandaa kisha kwenda kwa Ester, alifika na kumkuta Ester katulia tu akisoma biblia, alikaa na kuzungumza nae,
“Ester, kiukweli huwa najihisi kama sipo sawa vile, nilikupenda wewe ila nilishindwa kufanya ulivyotaka wewe nikaamua kuendelea na maisha mengine sasa nimekuwa mtu mzima nikampenda binti mmoja na kutamani kumuoa kumbe ni mwanamke mwenye mahusiano na mwanangu, nimepata ukimwi bila kujua nimeusambaza kwa watu mbali mbali yani najiona kama sina faida vile, nawaza vitu vingi sana”
“Jimmy faida yako ipo tena kubwa sana, kumbuka wewe ni baba na una watoto ila cha muhimu kufanya ni kuhakikisha watoto wako hawapiti kwenye njia ulizopita wewe”
“Kivipi?”
“Waache watoto wako wafanye vile mioyo yao inavyotaka kufanya, wewe hukuoa ila hainamaana kuwa basi watoto wako wasioe au kuolewa. Unatakiwa uache watoto wako wawe huru kwa wanaowapenda kwasasa, muache Erick amuoe Erica na muache Tumaini aolewe na Tony”
“Kheee unajua hayo maswala!”
“Najua ndio, unawanyima raha watoto wako, usitake makosa yako ya ujanani yatese na watoto wako, unatakiwa kuacha watoto wafurahie maisha. Imeandikwa kwenye Marko 10:7-9 (7.Kwa sababu hiyo mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe;
8. na hao wawili watakuwa mwili mmoja; hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja.
9. Basi alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.) Jimmy huna sababu ya kuzuia watoto waliopendana, waache watoto waoane na waishi kwa furaha tena kama baba unatakiwa kutoa baraka zote kwa watoto wako nao watakukumbuka siku zote za maisha yao na kuheshimu mawazo yako kwao”
Yale maneno yalionekana kumuingia sana Mzee Jimmy na kumuaga pale Ester kwani alionekana anafanya kinyuma kuwakatalia watoto wasioane.

Dora akiwa nyumbani kwao, alienda kujifungia ndani muda huo akiimba na kuanza maombi kwakweli mama yake alishangaa sana kuwa mwanae kawa kitu gani, akamsubiria atoke ili amuulize vizuri.
Muda kidogo alifika Steve na begi lake kwakweli mama yake alifurahi sana kumuona mwanae Steve amerudi, alimfata na kumkumbatia huku akimkaribisha ndani ila Steve alikuwa kamavile bado anajishangaa, alimuangalia mama yake na kumuuliza,
“Mama nimekuwaje mimi kwani?”
“Kwani vipi mwanangu?”
"Hata sijielewi mama, nilikuwa naishi kwa mwanamke mmoja sasa nimeshangaa gafla nimeona hapanifai tena pale nikabeba begi langu na kuondoka"
"Yule mwanamke kakuambiaje?"
"Simuelewi mama maana huwa analia tu"
Muda kidogo Dora alitoka kwenye maombi yake ila alipomuona mdogo wake alifurahi sana na kumkumbatia, na muda ule ule akawaomba waende kwa mwanamaombi, mama yao hakupinga na kujiandaa kisha wakaelekea kwa mwanamaombi.
Walipofika walimkuta Ester akiimba imba na kuwakaribisha vizuri sana,
"Mama, kwakweli nimeona ukuu wa Mungu. Mdogo wangu huyu karudi na mama yangu pia kakubali kuja huku kwenye maombi"
"Hiyo ni habari njema, utukufu ni wa Mungu"
Basi yule mama alianza kufanya maombi pale ila alimuomba jambo moja Dora,
"Kuna jambo halipo sawa hapa, namuhitaji pia mwanamke aliyekuwa akiishi na mdogo wako kwani anatakiwa kufunguliwa pia"
Dora hakubisha na muda huo huo aliondoka na kuelekea anapoishi Sia.
Alifija na kumkuta Sia yupo nje amejiinamia tu, alimshtua na kuanza kuongea nae,
"Sia, tatizo nini?"
Macho ya Sia yalivimba, inaonyesha alilia sana ila alipomuona Dora aliongea nae,
"Dora toka siku niliyogundua kuwa yule George kaathirika sikuwa na raha kabisa, nilirudi hapa nyumbani na kutamani nitembee tu na Steve ili wote tuathirike ila moyo wangu ulikataa hilo, hiyo hali imenitesa sana inafanya nilie kila muda hata hamu ya kula sina, kwenda kupima naogopa, nahofia maisha yangu na maisha ya mwanangu. Sijui hatma yangu jamani"
"Sia usilie kwani kulia sio suluhisho la tatizo lako, nakuomba twende kwenye maombi kwani maombi ndio silaha ya kila kitu"
Sia alikubali bila kinyongo chochote na kuondoka na Dora mahali pale na kuelekea kwa yule mama wa maombi.
Walifika na kumkuta bado akiwafundisha Steve na mama yake ila Sia aliposogea tu kwa huyu mama alianguka chini na kufanya huyu mama kuanza kumuombea, alimuombea kwa muda na kumuacha pale chini, kisha akasaidiana na wakina Dora kumuingiza Sia ndani na kuendelea kuongea nao kwa kuwapa mafundisho ya Mungu.
Jioni alianza tena maombi kwa Sia na alizinduka muda huu, walikaa na kuongea nae, kwakweli Sia alionekana kujutia vitu vingi sana maishani mwake,
"Ni kweli nilitamani sana Erick awe mume wangu, toka siku naanza mahusiano na Erick nilikuwa na ndoto za kuwa mkewe. Ndiomana haikujalisha nilimfumania mara ngapi ila nilimsamehe kwani niliamini ni mume wangu, kipindi hiko sikuangalia mwanaume mwingine kwani mategemeo yangu yalikuwa kwa Erick tu. Kitu kilichofanya mimi nipende sana kuwa na Erick ni pesa alizokuwa nazo na muonekano wake yani kwangu ilikuwa ni fahari sana kusema kuwa nina mahusiano na Erick. Kipindi Erick yupo na Erica bado niliamini kuwa atarudi tu kwangu alivyokawia kurudi ndipo niliamua kwenda kwa mganga ila najutia sana kwani nilitakiwa kuelewa tangia mwanzo kuwa Erick hakuwa na nia ya kunioa ila alinitumia kutimiza haja zake tu"
"Pole binti yangu, usijali kuwa Erick hakupendi sijui nini na nini yani wewe uwe unajua tu jambo moja kuwa Mungu anakupenda sana. Acha kulia sasa, mtazame Yesu msalabani alikufa kwaajili yako"
"Ila nina ukimwi mimi, nini hatma yangu na mwanangu?"
"Sio swala la kuhofia wala kuogopa hilo, wangapi wana ukimwi na bado wanaishi vizuri tu. Maisha ni kumtumainia Mungu, na unaweza shangaa Mungu kakunusuru kutoka huo ugonjwa hata kama ulikutana na mtu mwenye ukimwi, uwezo wa kunusurika upo ni mkubwa tu. Kwanza umeonyesha moyo wa utu kuwa ulipogundua kuwa yule mwanaume kaathirika na ulikuwa nae hukutaka tena kumuambukiza huyu kijana asiye na hatia. Mungu anaweza kukunusuru kwenye hilo janga, muamini Mungu na utashinda. Kwasasa nikushauri tu binti yangu uokoke"
Sia alikubali, mama Dora nae alikubali, Steve pia alikubali basi yule mama aliwafanyia sala ya toba na kuwafundisha maombi kisha kuagana nae, waliahidi kwenda kwenye ibada kesho yake kwani walijihisi kuwa huru kwenye mioyo yao.

Erick alienda kwao moja kwa moja, na muda huo alimkuta baba yake akiongea na Tumaini pamoja na Tony kumbe aliwakuta nyumbani kwake tena, kwahiyo Erick alifika kwenye mazungumzo yao, mzee Jimmy alipomuona Erick alimkaribisha kwenye kile kikao cha dharula,
“Erick karibu, unajua kuna mambo nimefikiria kama baba nimeamua kujirudi maana nadhani nitakachokuwa natenda basi hakina matunda, niliwahi kupenda ila sikuwahi kuoa na utu uzima huu nikatamani kuoa ila mwanamke niliyemtamani kumbe na mwanangu ushapenda, kuna mambo nimeyafikiria sana na nimeona ninavyoenenda basi haitakiwi nienende hivyo. Mwanangu hujaoa ila sitaki uishie kama mimi baba yako maana najua mnajua kama baba yenu nimeathirika, sio siri tena ni kweli mimi sio mzima. Upande mwingine mwanangu Tumaini sitaki uishie kama mimi baba yako au uwe kama mama yako, nimekuuliza hapa mara mbili mbili kuwa huyu mwanaume unampenda?Umenijibu ndio, na iwe kweli sio uolewe halagfu atokee mwingine umkimbie kijana wa watu maana nyie wanawake hamtabiriki ila najua kwako ni tofauti mwanangu maana huyo mwanaume mwingine sijui atakubabaisha na kitu gani tena? Kama pesa kwa baba yako ipo, sijui kama mnanielewa lakini!”
“Tunakuelewa baba”
“Nataka Erick uoe na Tumaini uoelewe. Tony, upo tayari kumuoa binti yangu Tumaini?”
“Ndio nipo tayari”
“Haya nahamia na kwako Erick, linin a wewe utamuoa Erica?”
“Ndio nilikuja kujadiliana na wewe baba kuhusu hilo swala, nahitaji kumuoa Erica ila sihitaji kuchelewa nahitaji kumuoa haraka iwezekanavyo”
“Basi namaliza haya majadiliano, jamani Jumamosi ni harusi Erick utamuoa Erica na wewe Tumaini utaolewa na Tony, msiniulize chochote kile maana kila kitu nitasimamia mwenyewe. Tony umenielewa”
“Nimekuelewa baba”
“Nimemaliza jamani, Erick jiandae Jumatatu tunaenda kujitambulisha kwakina Erica na kumaliza mambo yote siku hiyo kwahiyo waambie wajiandae na Jumamosi ni harusi. Na wewe Tony kafanye utaratibu kwenu Jumanne uje hapa na mshenga na baadhi ya ndugu zako, mama Tumaini nae atakuja tukamilishe mambo halafu Jumamosi sherehe”
“Sasa mzee bado sijajua mahali mtanipangia kiasi gani?”
“Wewe jiandae tu maswala ya mahali tutapanga kiasi gani yasikusumbue kichwa ila jua kwamba Jumamosi sherehe nimemaliza”
Kisha mzee Jimmy akainuka na kwenda chumbani kwake, kwakweli mzee huyu maneno aliyoongea na Ester yalimuingia sana na alijiona kuwa na makosa mno aliyoyafanya enzi za ujana wake hakutaka yajirudie kwa watoto wake.

Leo Erica aliachwa nyumbani kwao pamoja na Angel maana mama yake alishamsamehe kwa yale waliyoongea na kupanga na jinsi alivyomuheshimu yule mama Erick.
"Kesho mwanangu tutafanya kikao cha familia humu ndani maana Erick kasema hataki kukawia kufunga ndoa yenu, anataka birthday yenu ya mwaka huu iwakute ndani ya ndoa kwahiyo kesho tutajadili swala hili. Ila nimefurahi sana leo mwanangu upo nyumbani tena"
Erica alichekelea tu kwani ndoto yake ilikuwa ni kuolewa na kupata baraka zote toka kwa mama yake na ndugu zake.
Usiku wa siku hiyo ulikuwa ni usiku wa furaha sana nyumbani kwakina Erica haswaa kwa Erica yani alilala huku akiwa na tabasamu usoni.
Kulipokucha, mama Erick alimpigia simu Mage na kumpa taarifa vizuri Bite na kumuita Tony ilo wajadili mambo hayo, kisha akaenda kanisani.
Jioni ya siku hiyo ndio walikaa kikao cha familia ili kujadili kuhusu sherehe ya Erick na Erica, muda huo Tony alikuwa bado hajawasili nyumbani ila waliona ni vyema kuanza kuongelea swala hilo,
"Jamani Erick kanipigia simu na kaomba harusi yao iwe Jumamosi ijayo"
"Kheee Jumamosi ijayo, mbona karibu hivyo? Lini tutakusanya michango, lini tutawatangazia watu mbona katushtukiza hivyo!"
"Jamani Erick kasema hataki kuchelewa, anataka harusi ifanyike mapema, kesho anakuja kulipa mahali yani baba zenu wadogo, wajomba zenu nimewapigia simu yani Erick anataka kila kitu cha posa na mahali amalize kesho na Jumamosi harusi"
"Jamani mama, hiyo haiwezekani kwakweli. Tutajipanga muda gani jamani eeeh! Halafu na huko kanisani washatangaza?"
"Mpaka kasema hivyo inamaana tayari, ngoja tumuulize muhusika. Erica hii harusi ya haraka haraka hibi mwanangu mmepanga kweli? Mlifikiria hili na mwenzio?"
"Hapana mama ila naona Erick anataka tuoane upesi"
"Sawa, tukubliane jambo moja hakuna cha kukufanyia Sendoff wala kitchen party sawa!"
Mage akadakia,
"Afanyiwe ya nini mama na wakati alishaishi na mwanaume, halafu alivyopanga nae hivyo hataka alitegemea nini? Yani hapa ni harusi tu ya fasta"
"Ila na wewe Mage usikuze mambo, wewe hata harusi hujafanya halafu mwenzio kutokufanyiwa sendoff tu na kichen party basi ndio unaongea weeee hebu acheni haya mambo yaende kama yalivyopangwa, ukoo wetu wenyewe kigeugeu acha Erick ajiamulie kufanya mapema tu."
Erica aliinuka na kuelekea chumbani kwake na kuacha wakijadili tu.
Muda kidogo Tony alifika na walimueleze waliojadili ila walishangaa pale Tony alipowaambia kuwa nay eye Jumamosi anamuoa Tumaini, Mage alishangaa sana na kuuliza,
“Itawezekanaje?”
“Jamani Yule baba yao kaamua hivyo kasema Erick na Erica wanaoana na mimi na Tumaini tunaoana amesema kila kitu atagharamia yeye”
“Khee makubwa, na hiyo mahali ya kwakina Tumaini utaenda kulipa nini si ndio kujitia aibu?”
“Yule mzee kasema nijiandae tu, basi nitajiandaa kwa uwezo wangu na hiyo Jumanne nitapeleka nilichokuwa nacho maana sihitaji kumkosa Tumaini najua pesa sio tatizo kwa yule mzee na hawezi kunipangia mahali ya kunikomesha kwani nay eye anahitaji nimuoe binti yake yani nitatoa mahali kama desturi tu lakini sio kunikomesha”
“Sawa kama ndio hivyo ila mmmh hizo sherehe sijui jamani”
Wakajadiliana pale kwa muda kidogo kabla ya kupanga mipango ya kesho ila Bite aliwaomba udhuru kuwa kesho anaenda kushughulikia swala lake la talaka, hawakumzuia ila tu walimwambia kama anaweza kuwahi basi awahi kwenye tukio la siku ya kesho.
 
SEHEMU YA 445

Erica akiwa chumbani kwake alipigiwa simu na Erick, akatabasamu na kuipokea,
"Yani Erica nishamiss uwepo wako jamani hadi najihisi vibaya mke wangu, nahitaji harusi yetu iwe haraka tuishi wote"
"Ila Erick, harusi haraka sana hadi nyumbani wamesema hawatanifanyia kitchen party wala sendoff"
"Kwani kitchen party na sendoff vya nini mke wangu jamani! Kikubwa ni mimi na wewe kuoana, nakuomba Erica tusipeleke mbele harusi sababu ya maswala hayo, nahitaji tuoane mapema. Baba yangu kakubali na kasema atasimamia kila kitu, nahitaji tuoane Erica na tuishi wote sidhani kama hayo maswala mengine yana umuhimu wowote kwetu mpenzi"
Kwa maneno ya Erick ilibidi Erica asiwe na pingamizi lingine lolote na kukubali tu jinsi Erick anavyosema kwani kwa upande wake kama kikitokea kitu kingine cha kupinga mapenzi yao kingekuwa mzigo mkubwa sana kwake.
Basi waliagana na kulala huku sura ya Erica ikiwa imejaa tabasamu kubwa.
Kulipokucha aliamka na kumuona mama yake akiandaa mazingira ya kupokea ugeni ambapo hawakukawia kwani kwenye mida ya saa nne ndugu zao waliwasili na mida ya saa tano wakina Erick waliwasili pia, leo ilikuwa ni ajabu sana kwani mzee Jimmy alikuwa mpole kanakwamba hajawahi kusema anataka kumuoa Erica.
Wale ndugu walianza kupanga mambo ya posa na jinsi harusi itakavyokuwa na mzee Jimmy aliwahakikishia kuwa sherehe yote ataigharamikia mwenyewe.

Salma aliamua kwenda hospitali kupima mimba yake na kuanza taratibu za kliniki, alipopimwa aliambiwa kuwa ameathirika alishangaa sana yale majibu maana aliona kama si yeye anayeambiwa habari zile za kuathirika.
Aliondoka pale hospitali na moja kwa moja alienda kuongea na mamake Rahim, muda huo alimkuta Rahim yupo kwa mamake akiongea na simu, aliweka sauti kubwa, ilionyesha alikuwa akiongea na Babuu,
"Yani wewe ndugu yangu umeamua kunisaliti jamani kweli? Yani umeenda kuoa wewe wakati huyo Zainabu nilitaka nimuoe mimi!"
"Sasa kaka lawama za bure hizo, ungemuoaje Zainabu na unajijua wazi umeathirika?"
Rahim alikata ile simu ila yale maongezi yalisikiwa vizuri sana na mama yake, alimuuliza kwa mshangao,
"Rahim kumbe umeathirika!"
Rahim akataka kukataa ila Salma alisogea na kumrushia kile cheti halafu akaanza kusema,
"Kumbe Rahim umeathirika ndiomana ukasema tumuachishe mtoto kunyonya kumbe ukweli unaujua kuwa umeathirika!"
Mamake alichukua kile cheti na kukisoma vizuri kwakweli alisikitika sana, na kumuangalia mara mbili mbili Rahim,
“Kumbe mwanangu kweli ulikuwa muhuni! Nilikuwa nawakatalia wote waliokuwa wanakusema vibaya jamani Rahim, leo umeniabisha na umeenda kumuambukiza Salma asiye na hatia jamani”
Kwa mara ya kwanza leo Rahim alipiga magoti kumuomba msamaha Salma kwa kumuambukiza ukimwi ila lile lilikuwa pigo kubwa sana kwa Salma kwani hakutegemea jinsi alivyokuwa akijibidiisha kwenye kumpa mume wake mapenzi kumbe alikuwa anauzoa na ukimwi.

Bite alienda mahakamani na James alienda na kusaini talaka yao ila James alionekana kutokufurahia kabisa swala la wao kuachana.
James alipotoka hapo alienda nyumbani kwakina Dora Alifika na kumkuta Dora anasoma biblia, alimshangaa sana na kumuuliza,
"Dora na biblia wapi na wapi jamani!"
"Kila kitu kinawezekana chini ya jua, tunatakiwa tumtegemee Mungu"
"Kheee makubwa haya, basi tuachane na hayo. Dora nina mawazo hatari, mke wangu kaniacha, yani leo rasmi tumeenda kusaini talaka sababu tu ya kuathirika"
"Ila si mlikula kiapo kuwa hakuna cha kuwatenganisha zaidi ya kifo?"
"Ni kweli ila ukimwi umenitenganisha na mke wangu, Dora ni wapi nitaenda kumaliza haja zangu mimi? Naomba ukaishi nami nyumbani kwangu"
"James, Dora wa sasa sio Dora yule wa mwanzo. Kitakachonitoa nyumbani na kwenda kuishi na mwanaume ni ndoa na si vinginevyo"
"Kwahiyo Dora unataka nikuoe?"
"Nioe ndio, yani ndoa pekee ndio itaweza kufanya niishi na wewe"
"Sawa hakuna shida, mke wangu nimeachana nae mahakamani, naomba nikaoane na wewe huko huko mahakamani"
"Sawa ila fata taribu zote kama kuja kwetu utambulike halafu tutaenda kuoana ila pia tunaweza kufungia kanisani"
"Aaah kanisani mpaka sherehe Dora gharama zingine hizo"
"Unajua sherehe ni mipango ya watu tu ila kuoana bila sherehe inawezekana, twende tuoane na kuishi kwani ni lazima sherehe? Sio ya muhimu tunaweza kuoana na kuishi vizuri tu bila sherehe"
James akaona kama ni hivyo basi ni rahisi kwake akamuahidi kwenda na mshenga nyumbani kwao siku ya kesho ili kujaribu kufata zile sheria zinazotakiwa maana kwa wakati huo James hakuona mwanamke mwingine wa kumwambia habari zake za shida ya kimwili zaidi ya Dora.

Bahati akaona isiwe shida, aliamua kuuza shamba lake moja na kuongezea hela na kununua nyumba ili akiamua kuishi na Fetty basi aishi nae kwenye nyumba nyingine, ila kuna shamba ambalo Bahati hakuligusia hata kuhusu kuliuza hata dada zake walimshangaa ila hawakutaka kumdadisi sana.
Bahati alikuwa na wazo la kumuoa Fetty ila kuna jambo ambalo lilikuwa likisumbua sana moyo wake na jambo hilo ni kuhusu Erica yani Bahati alihisi hakuna mwanamke atakayeweza kumpenda kama Erica, basi alipokamilisha mambo yake ya kununua nyumba nyingine siku hiyo jioni aliondoka kwao na kuelekea kwakina Erica.
Alimkuta mamake Erica ndio anasafisha safisha maana wageni walishaondoka kwa muda huo, mama Erica nae alimshangaa kumuona na kumuuliza
"Wewe kiumbe kumbe upo?"
"Nipo mama na upendo wangu kwa Erica upo pale pale"
"Pole sana, yani hapa walikiwepo wageni kwaajili ya sherehe ya Erica. Jumamosi hii Erica na Erick wanaoana"
"Kheee mama, Erica anaolewa?"
"Inamaana hujanisikia au kitu gani? Erica anaolewa ndio, yani wewe tafuta ustaarabu mwingine tu"
"Ila mama nampenda sana Erica"
Mama Erica alianza kumuonea huruma Bahati na kuongea nae kwa upole,
"Sikiliza mwanangu, si unampenda sana Erica eeeh!! Sasa mimi nakushauri mwanangu, kama wampenda hivyo Erica basi muache abakie na furaha yake, furaha ya Erica ni pamoja na wewe ukifurahi, Erica akikuona umeoa atafurahi zaidi. Jumamosi ni harusi ya Erica ila onyesha upendo wa kweli kwa Erica kwa kumpongeza, sikia Bahati hutakiwi kuwa na chuki kwa mume wa Erica ila unatakiwa kumfanya ampende zaidi Erica"
"Ila mama nitawezaje kumpenda msichana mwingine?"
"Kwani kikubwa ulichokipenda kwa Erica ni kitu gani?"
"Erica ni msichana mpole, halafu ni muelewa na ana upendo sana yani hata kama hakupendi ila kuna vitu atakufanyia uwezo kuuhisi upendo wake"
"Basi hata utakayempata utaweza kumtengeneza awe kama Erica, usimfiche kitu mwenzi wako, mwambie unachopenda na usichopenda na hiyo itakusaidia sana katika kusonga mbele"
Bahati alijaribu kumuelewa mama Erica na hakika alimuelewa kwani alipanga akiondoka hapo basi kesho yake akafanye harakati ili ndoa yake na Fetty iweze kutimia kisha Jumamosi aweze kuhudhuria harusi ya Erica.
Basi alimshukuru mama Erica na kuondoka zake kurudi kwake kwa muda huo.

Kesho yake Bahati aliongea na Fetty na kujipanga kwenda kwao ili akafanikishe swala la kuweza kumuoa, maana maneno ya mama Erica yalikuwa yakimuingia akilini mwake kuwa endapo ataoa basi itakuwa ni furaha kubwa sana kwa Erica, kwakweli alipomueleza tena Fetty kuhusu swala la kutaka kumuoa Fetty hakupinga kabisa swala hilo kwani alikubali na siku hiyo hiyo Bahati alienda kujitambulisha nyumbani kwakina Fetty.
Wakati huo Tony nae alikuwa nyumbani kwa mzee Jimmy kujitambulisha na kufanya taratibu za sherehe ya Jumamosi, muda huo hata kaka yake Tumaini nae alikuwepo kwenye hilo tukio na walivyomaliza kaka wa Tumaini alimtafuta Bite ili wajadiliane nae kuhusu hilo swala,
“Kuna jambo hapa, kumbe Yule mdogo wangu Tumaini anaolewa na mdogo wako?”
“Ndio, siku ile nilishtuka kumuona kwenu sababu namfahamu Tumaini yani sijui inakuwaje, mimi na wewe tutaendeleaje sasa?”
“Kwani kuna tatizo basi! Sidhani kama kuna tatizo mimi na wewe sio ndugu na wale wamependana ndiomana wameoana na sisi na yetu tutafanya sababu tumependana, kuangalia ya watu kutafanya nikae bila kuoa maisha yote”
“Sawa nimekuelewa, na wewe kwetu utakuja lini Deo?”
“Aaaah nitakuja tu”
“Ila subiri kwanza, subiri upepo utulie, nimeachana na mume wangu hivi karibuni tu halafu nionekane napeleka mwanaume mwingine nyumbani itakuwa nimeanza na wewe siku nyingi, subiri upepo utulie na tutaoana”
Deo alikubaliana na Bite kuhusu hilo kwani aliona ni la maana itaonekana Bite alipanga kuachana na mumewe ili aolewe nay eye kwahiyo hakuona kama ni swala zuri kwakweli, aliona ni vyema kusubiri kama wanavyoshauriwa.
 
SEHEMU YA 446

Siku hiyo Sia alienda kwanza kwa Yule mwanamaombi kuomba nae, na kumwambia kuwa anahitaji kwenda hospitali kuanza kliniki na kupima ukimwi,
“Sia hebu kuwa na imani kuwa Mungu anaweza, kwanini unaogopa hivyo? Kuwa na imani mwanangu, hujapima una wasiwasi wa bure, mimi naona kuwa Mungu kakuepusha kwenye janga hilo mwanangu, kuwa na amani”
“Sawa, nashukuru kwa kunitia nguvu”
Sia alimpigia simu Steve na akaongozana nae kwenda hospitali ambapo walipewa ushauri kwa pamoja na kupima, majibu yakaletwa kuwa hawajaathirika kwakweli ilikuwa ni ajabu sana kwa Sia, yani hakuamini kabisa kuwa amepona toka mikononi mwa George, alijisemea mwenyewe,
“Kuanzia leo mimi Sia sitafanya tena uzinzi, nimekoma. Bora nife masikini lakini kutumia mwili wangu kwaajili ya kupata kipato hapana kwakweli, siwezi fanya hivyo tena”
Walivyotoka hapo, walienda moja kwa moja kwa Yule mwanamaombi ili kuongea nae tena.
Yule mama aliwauliza tu maswali machache,
“Je mnaweza kuishi pamoja”
“Ndio”
“Basi muoane tu ni vizuri zaidi”
“Ila sina kazi sijui nitawahudumiaje?”
“Maisha ni kuamua yani usifikirie huwezi, kila kitu kinawezekana, mwanzoni hukuweza sababu akili yako ilichanganywa na madawa ila kwasasa utaweza kujishughulisha na wewe Sia utaweza kujishughulisha pia na mtaendeleza familia yenu”
Wakakubaliana na huyu mama, ingawa Steve alitambua kuwa Sia alimuwekea madawa ila aliamua kuishi nae moja kwa moja tu na kulea pamoja mtoto wao atakaye zaliwa.
Basi wakaondoka hapo na kuelekea kwakina Dora ili kuwapa taarifa, walikuta kuna ugeni yani James alikuwa ameenda kuongea na familia ile kuhusu swala lake la kutaka kuoana na Dora, kwakweli Steve alifurahi kusikia hivyo pia na wakawapa habari njema ya majibu kutoka hospitali.
 
SEHEMU YA 447

Kesho yake ilikuwa ni ndoa ya James na Dora mahakamani, walijiandaa vizuri kabisa na kwenda kuongea na mwanasheria wao kuwafungisha ile ndoa.
Bite alikuwepo mitaa hiyo ya mahakama maana alienda kuonana na Deo, ila alishangaa sana kuona James na Dora wakifunga ndoa, alimuuliza Deo
“Kwani sheria hapa mahakamani zinasemaje? Hii ndoa mbona haraka hivi, imetangazwa kweli?”
Deo alimshangaa Bite kuwa anawasiwasi gani kwa James kuoa wakati yeye ndiye aliyeenda mahakamani kudai talaka yake?
Deo alimshangaa Bite kuwa anawasiwasi gani kwa James kuoa wakati yeye ndiye aliyeenda mahakamani kudai talaka yake?
Akamuangalia mara mbili mbili na kumuuliza,
“Hivi si ni wewe uliyekuja kuketa ombi la talaka hapa mahakamani! Si ni wewe uliyesema tumshurutishe mumeo ili asikatae kuja kusaini talaka! Leo vipi tena una mashaka na kuoa kwake?”
“Hapana ila….!”
“Ila nini sasa Bite? Ulimpenda mumeo ila mbona ulikuja kudai talaka?”
“Ameathirika”
“Sio tatizo, kuna wanaoishi na watu walioathirika, swala la wewe kuja kudai talaka sio kwasababu ameathirika tu ila kuna mambo mengine ambayo huyataki kwa mume wako ndio yamekufanya udai talaka”
“Ila nimeshangaa yani kuachana tu majuzi halafu leo anaoa kweli?”
“Ukiona hivyo ujue huyo mwanamke alikuwepo na kumuacha mume wako hakujamkomesha wala nini zaidi kumempa nafasi tu ya kuweza kuishi na Yule amtakaye”
Bite alikuwa kimya tu kwani alichoambiwa kilikuwa na ukweli mtupu ila hakuweza kukaa hapo kushihudia ndoa ya James na Dora bali aliondoka na kurudi kwao.
Alienda kwao na kumkuta mama yake ambaye alimueleza kuhusu James kuoa, mama yake alimuuliza,
“Sasa wewe una wasiwasi gani mwanangu? Kama James anaoa mwache aoe na wewe utapata mume utaolewa si ushaachana na James”
“Ila mama ni mapema mno, inaonyesha yule Dora alishapanga na James kuoana”
“Kumbe mwanamke mwenyewe ni Dora! Umesahau mwanangu, si tulimpa wenyewe ushauri hapa James kuwa akamuoe Dora! Basi kafata ushauri wetu”
“Kwahiyo mama na mimi naweza kuolewa?”
“Ndio inawezekana, ushaachana na mumeo kwahiyo nafasi ya kuolewa wewe ni kubwa sana. Ukipata mwenzi wako usisit kumleta”
Bite alifikiria kidogo na akaona ni vyema afanye hivyo kuwa ampeleke Deo nyumbani kwao maana alijikuta kashapata wivu kutokana na harusi ya James na Dora.
 
SEHEMU YA 448


Dora na James walipomaliza waliunana na familia zao ambapo mama Dora aliandaa chakula kidogo cha kula pamoja kama familia kwahiyo walijumuika pamoja na kula chakula kile halafu Dora na James wakaenda nyumbani kwa James sasa, walivyofika mlinzi alimwambia James,
“Yule mwanamke wako alikuja?”
“Mwanamke wangu? Kivipi?”
“Si Yule mama James?”
“Aaaah alifuata nini sasa jamani, si aliondoka kwa kunitesa sana Yule, si aliondoka bila kuwaza ya mbele, sasa anataka nini tena? Sikia nikwambie, saivi atakayekuja hapa ukiwa unanipa taarifa sema Fulani amekuja maana hakuna mwanamke wangu mwingine zaidi ya huyu niliyetoka kumuoa”
Mlinzi aliitikia kisha Dora na James wakaingia ndani, na kuanza kupanga yatakayokuwepo, James ndio alianza kuongea,
“Dora, najua ushahangaika sana, ushatembea na wanaume wengi sana na hadi kuyazoa ya kuyazoa ila bado ukaamua kutulia sasa na kumgeukia Mungu, kwa upande wangu pia nishahangaika sana na sasa naahidi kutulia. Dora, nakuomba mke wangu tutulie ili tuweze kuishi maisha marefu, kwani hata madaktari wanashauri hivi, ukiwa na ukimwi na ili uishi maisha marefu inakupasa utulie, naomba tutulie Dora na letu liwe moja”
“Sina mpango tena wa kuhangaika, nilikuwa na akili mbovu sana. Sikuhangaika sababu natafuta penzi la kweli hapana yani kuhangaika ilikuwa ni hulka yangu na nilivyojigundua nina ukimwi ndio nikawa moto wa kuotea mbali, nilijua ukipata ukimwi unatakiwa kuusambaza kumbe sivyo, swala la kusambaza ukimwi tunawatesa hata wasiostahili kuteseka, tunawaumiza hata wasiostahili kuumia. Mfano Sia, aliamua kuhangaika ilia pate pesa ya kumlisha yeye na kiumbe na sio kwamba aliamua kuhangaika na wanaume mbalimbali ila alitafuta mmoja wa kumsaidia kulea kumbe Yule mmoja tayari nilishamuambukiza ugonjwa, kwahiyo ningemteketeza Sian a mtoto wake na tena ningemteketeza na mdogo wangu”
“Na wameponaje wale?”
 
SEHEMU YA 449

“Unajua ukimtegemea Mungu ni vizuri sana, Mungu ndiye hukumu wa haki na si mwanadamu. Mtu yeyote anaposikia Fulani ana ukimwi huwa anakuwa na wazo kuwa mtu huyo ni malaya wakati kuna wengine wanapata ugonjwa bila hata ya kuwa malaya, alikuwa na wa kwake mmoja huyo wa kwake ndio kaenda kuuzoa huko na shida zake. Ila nilichogundua ni kimoja, katika swala lolote badala ya kukaa na kumlilia mwanadamu maana kuna mambo mengi mwanadamu hawezi kukusaidia, mwingine atakuonea huruma, na mwingine atakucheka na mwingine atakusanifu, hayo machozi ni haki kwenda kulia mbele za Mungu maana Mungu ni mwingi wa rehema, amejaa huruma yani Mungu atatuhurumia. Yule mama wa maombi kanifundisha vitu vingi sana, kaniambia hakuna mtenda mema katika dunia ila tumezidiana katika kutenda dhambi, nab ado hupaswi kujiona ni bora kushinda mwenzio mbela za Mungu, kikubwa ni kujishusha alivyonifundisha namna ya kuomba toba kwa Mungu nilikuwa naingia kwenye maombi nikiomba toba na kulia kwa yale niliyoyatenda ila Mungu kamnusuru Sia, Steve na mtoto wao. Nimeunga hoja ya kwamba waishi pamoja, ingawa na madawa sijui nini ila yameisha nab ado Steve amesema ataendelea kuishi na Sia, mwanzoni nilikuwa nalalamika sana ila sikujua kusudi la Mungu, Steve alikuwa hawezi kutongoza, Steve hakuwa na mwanamke kabisa hata mama aliwaza kuwa hajui kama mbele ya safari Steve ataoa ila kamfata mwanamke Yule na mimba kampatia inaonyesha mdogo wangu amekuwa kidume”
Hapo James akacheka, kuna ujumbe uliingia kwenye simu ya Dora na simu ya James, walianza kusoma na kushangaa kwa pamoja,
“Kheee Jumamosi ni hasuri ya Erica na Erick?”
“Ndio nashangaa, halafu Jumamosi si keshokutwa?”
“Ndio na tumealikwa”
“Twende James, twende yukashuhudie unajua wale wamepitia misukusuko sana na hata sikufikiria kama wataoana, twende tu hiyo Jumamosi”
James na Dora walikubaliana kuhudhuria harusi ya Erica na Erick.
 
SEHEMU YA 450

Sian a Steve walivyotoka kwenye harusi ya Dora na James waliamua kwenda kwa mwanamaombi kuongea nae, walimkuta na kuanza kuongea nae ambapo walimwambia lengo lao la kutaka kuoana,
“Tunahitaji kufunga ndoa mama, hivi itawezekana?”
“Ndio inawezekana maana kila kitu ni maamuzi tu hata msiwe na mashaka ya aina yoyote, mnataka kuoana lini?”
“Muda wowote ila hatuna pesa za kufanya sherehe”
“Kufunga ndoa sio lazima mfanye sherehe, nyie ni kuwa na maamuzi na nia moja tu. Kwenye Biblia mnaweza kuona jinsi gani ndoa ilivyo kitu cha muhimu sana. Kwahiyo mmeamua jamnbo jema”
Walishukuru sana, kuna ujumbe uliingia kwenye simu zao kuwa Jumamosi ni harusi ya Erick na Erica, kwakweli Sia alimuangalia Yule mwanamaombi na kumwambia,
“Inawezekana kesho mimi na Steve tukaoana?”
“Inawezekana ndio, njooni tu mapema niwapeleke kwa mchungaji awafundishe kuhusu ndoa na ndio awafungishe ndoa ila mje na ndugu zenu ambao watakuwa ni mashahidi wa ndoa hiyo”
“Sawa, hakuna tatizo”
Wakakubaliana nae kuwa kesho yake wataenda na ndugu zao kwaajili ya kufunga ndoa, na pia Sia alimshirikisha Yule mwanamaombi kuhusu harusi ya Erick na Erica na wote walisema kuwa watahudhuria.

Salma alikuwa na mawazo sana, na kikubwa alikuwa akimfikiria mwanae tumboni kwani alijua ndio mwisho wa maisha yake, yani alihisi kupata ukimwi basi ndio ameshakufa tayari, Mrs.Peter akaona isiwe shida na kwenda kumtafuta mshauri ambaye pia ni mama aliyeathirika na kuishi na virusi vya ukimwi.
Basi alifika nae kwake na kumuita Salma akae na huyo mama waweze kuzungumza nae, Salma alienda na Mrs.Peter alimtambulisha Salma kwa Yule mama,
“Salma, huyu anaitwa Bi.Aisha nimemleta hapa aweze kukushauri jinsi ya kuishi na hiyo hali wala usifikirie kuwa ni mwisho wa maisha, karibu”
Basi bi.Aisha alianza kuongea na Salma kwa kumsalimia kwanza na kuanza kumuelezea,
“Salma, unaniona mimi? Hivi ni rahisi kuamini nikikwambia mimi nimeathirika?”
“Hapana”
“Sasa mimi nimeathirika nina zaidi ya miaka kumi na sita sasa maana nilijigundua nina ukimwi wakati mtoto wangu ana mwaka mmoja ambaye pia ameathirika na sasa ana miaka kumi na sita kwahiyo mimi ndani ya huu ugonjwa nina zaidi ya miaka kumi na sita, unajua ni kitu gani kinachotufanya tuendelee kuishi kwa muda mrefu na bila kusumbuliwa na magonjwa? Kwanza kabisa ni kumtegemea Mungu, pia kulala vizuri, kupata muda wa kutosha kulala, kuzingatia ushauri wa wataalamu wa afya. Kupata ukimwi sio mwisho wa maisha, ukipata ukimwi usifikirie ndio kifo chako, hapana, yani sio mwisho wa mwaisha mwanangu. Tunaishi nao, tunazunguka nao na tunafanya majukumu yetu kwahiyo usiwe na shaka”
Yule mama akaanza kumueleza namna anavyoweza kuishi na virusi vya ukimwi,
“Mwanangu atapona kweli? Nina mashaka kuwa ataupata pia?”
“Mwanao atapona tu vizuri, cha muhimu wahi kliniki, fata ushauri unaopewa na wanao atapona kabisa”
“Na kuhusu kunyonya je? Au ndio nimuachishe nikimzaa tu!”
 
SEHEMU YA 451

“Hapana, mtoto unamnyonyesha kama kawaida, ambacho huwa kinasumbua ni pale mtoto akiota meno na kukung’ata wakati ananyonya halafu mdomoni awe na vidonda inakuwa rahisi kupata ugonjwa, ila ipo njia rahisi tu ya kuendelea kumnyonyesha mwanao ingawa una ukimwi na ingawa ameota meno maana maziwa ya mama ni muhimu sana kwa afya ya mtoto”
“Njia gani hiyo”
“Unakamua maziwa na mtoto anaendelea kunywa maziwa yako huku huna mashaka ya kumuambukiza na wewe unakula vizuri na kupata muda mzuri wa kupumzika na kumtegemea Mungu tu katika maisha utaona mwanako atakavyokuwa na afya nzuri”
Huyu mama alimshauri vizuri sana hadi Mrs.Peter alifurahia ushauri wake na kuita watoto wake wengine wapate ushauri pia na wajue jinsi ya kuishi na wale walioathirika kwenye himaya yao, Rahim aliitwa, John na mkewe Neema nao waliitwa kwahiyo walifika na kwenda kumsikiliza bi.Aisha, ambaye aliwaelekeza namna ya kuishi na muathirika,
“Jamani Ukimwi sio mwisho wa maisha, kupata ukimwi sio mwisho wa ndoto zako, kama ni mama utaendelea kuwa mama na kama ni baba basi utaendelea kuwa baba. Mume wangu alikufa sababu ya kutengwa na jamii na jambo lile lilikaa moyoni mwake, hakuna kitu kinaumiza kwa muathirika kama jamii kukutenga, jamani msitutenge maana na sisi tunaweza kufanya majukumu mnayoyafanya ila tu mtusaidie, mafano umesikia kuna matunda Fulani labda ukila yanaongeza kinga ya mwili ndio vitu vya kuja kutushauri ila sio kumtenga mwathirika, naye ni mwanajamii kama nyie”
Aliwaelekeza pale na walionekana kuelewa, kuna ujumbe ukaingia kwenye simu ya John, Mrs.Peter na Rahim, walisoma kwa pamoja na kujikuta wakiambiana,
“Eti Jumamosi ni harusi ya Erick na Erica, tunaambiwa tusikose yani tumealikwa tu”
Rahim alitabasamu ilibidi wote wamuulize, aliwaambia
“Wale ni wapendanao, yani wimbo wa Erica ni kumpenda Erick, waache waoane na mimi nitakwenda”
Wote wakakubaliana kwenda hadi Yule bi.Aisha mtoa ushauri nae alisema kuwa ataenda kwenye harusi hiyo, waliendelea kuongea na kucheka huku wakifurahi.
 
SEHEMU YA 452

Bahati alikuwa kwao na ndugu zake pamoja na Fetty alikuwepo yani kulikuwa kama na kikao kwani hadi Nasma na mdogo wake na mama yao alikuwepo, wakati wanajadiliana pale kuna ujumbe uliingia kwenye simu ya Bahati na Fetty, ila Bahati ndio aliusoma mwanzoni ila ujumbe ule ulionekana kama kubadilisha fikra za Bahati kwani baada ya kuusoma tu, alisema pale kwenye kikao,
“Jamani kesho naenda kumuoa huyu Fetty, sitahitaji tena ushauri na Jumamosi nitaenda nae kushuhudia harusi ya Erica na Erick”
Nasma pia alijikuta akitamani kushuhudia harusi hiyo, mwanamke aliyemchukia wala haolewi na Bahati bali anaenda kuolewa na mtu mwingine kabisa, ndugu wa Bahati nao walisema kuwa wataenda, kwahiyo kile kikao wakajikuta wakianza kuzungumzia kuhusu harusi ya Erick na Erica na kusahau hata dhumuni la mikao chao.
Ikabidi mama Nasma amalizie tu kile kikao,
“Nasma, hunabudi kukubali kuwa Bahati amuoe Fetty maana hawezi tena kuishi na wewe, Mungu atakujaalia mwanangu na utampata mwanaume mwingine”
Nasma alikubali ila kishingo upande kwani alikuwa akimfikiria mwanae na maisha atakayoishi baada ya hapo bila mume ila hakuwa na namna zaidi ya kukubali tu.
Walimaliza kikao na kuanza kutayarisha maandalizi ya kesho maana Bahati alisema kuwa kesho yake lazima amuoe Fetty.
Na kweli ilipofika Ijumaa kama ambavyo walipanga basi ilifanyika harusi ya Bahati na Fetty na walifurahi tu pamoja na hakuna aliyekuwa na kinyongo kwa wakati huo.
Baada ya harusi, Bahati na Fetty walielekea kwenye nyumba yao mpya, ila kitu ambacho kilimshangaza Fetty ni siku hiyo usiku kumuoa Bahati amekaa tu akifikiria mambo huku akiandika, hakuelewa anaandika nini na hakutaka kumsumbua pia kwani alijua kwamba kama kuna umuhimu way eye kutambua hilo basi ataambiwa na kama hakuna umuhimu basi hatoambiwa.
 
SEHEMU YA 453

Ilifika Jumamosi, siku ambayo Erica na Erick walikuwa wanafunga ndoa na Tumaini na Tony walikuwa wanafunga ndoa pia kama ambavyo baba yao mzee Jimmy alitaka, maana alihitaji harusi za watroto wake azifanye kwa siku moja na waalike wote wanaowahitaji, mzee huyu hakutaka mchango wa mtu yeyote Yule ila aliamua mwenyewe kufanya harusi za wanae alisema kama mtu hela ya mchango ni bora akawatunze maharusi au anunue zawadi kwaajili ya maharusi ila yeye aliamua kuifanya shughuli mwenyewe.
Walienda saluni kurembwa, ilikuwa kama Erica ni msimamizi wa Tumaini na Tumaini ni msimamizi wa Erica maana hakutafutwa msimamizi mwingine na kwa upande wa Erick na Tony ilikuwa vile vile,
Wakiwa saluni, Tumaini alimwambia Erica,
“Unajua ni maajabu haya yani sikutegemea kama mimi na wewe tutaolewa siku moja na tutakuwa zaidi y ndugu maana wote tumebadilishana, wewe umeolewa na kaka yangu na mimi naolewa na kaka yako”
Erica alitabasamu tu kwani furaha aliyomuwa nayo moyoni ilikuwa ni kubwa sana, kwakweli walipambwa na wakapambika.
Baada ya hapo ilikuwa ni safari ya kanisani ambapo Angel na Junior nao walipambwa vizuri na walisimamia vizuri harusi ya watu wale ambapo Mage alikuwa ndio mshika watoto.
Walienda kanisani na vigelele vilitawala kila kona, na baada ya kanisani sasa, jioni yake walienda ukumbini huko ndio ilikuwa furaha kila kona na watu walikuwa wengi sana.
Ilikuwa ni kusherekea mwanzo mwisho ila katika tukio ambalo hawakulidhania ni tukio waliloambiwa kuna mtu anataka kusoma ujumbe kwa maharusi wa siku hiyo, Yule mtu alikaribishwa na Mc, wale maharusi walimshangaa sana kwani mtu huyo alikuwa ni Bahati, alifika mbele na kusalimia watu kisha alianza kutoa ujumbe wake,
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom