Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,983
- 10,804
- Thread starter
- #561
SEHEMU YA 434
Dora na James walifika nyumbani kwa James usiku ule ila kwa bahati mlinzi wa James alirudi, kumbe alimtimua ila mlinzi alirudi, yani mlinzi alivyomuona James alianza kumuomba msamaha ila James alimshukuru sana mlinzi kwa uwepo wake tena kisha akamsaidia kuharibu kitasa cha mlango na kuingia ndani ambapo ilibidi alale mule na Dora hadi palipokucha ila kiukweli hawakulala kabisa kwani kila mmoja alikuwa na mawazo sana, waliwaza kuhusu simu zao yani simu ndio zilizowatia mawazo zaidi, kiukweli Dora alikuwa amechoka sana na kuamua tu kwenda jikoni kwa James na kupika kisha kuandaa chakula na kuanza kula na James, kwa mara ya kwanza leo James alikula chakula kilichopikwa na Dora, alikula na kumwambia,
“Kheee Dora licha ya kuhangaika hangaika kumbe kupika unajua?”
Dora akacheka na kusema,
“Tena leo nina mawazo yangu ndiomana, ila na wewe James hivi ni wanawake gani wale unakuwa nao? Aina gani ile ya mwanamke ulimuokotea wapi?”
“Hapana unajua Yule mwanamke alikuwa ni mfanyakazi wa humu ndani, na nilianza nae kipindi mke wangu mjamzito maana alikuwa mvivu sana”
“Ndio tabia ya kuhangaika na wasichana wa kazi hiyo, tatizo wanaume huwa hamridhiki hata wake zenu wawafanyie nini ndani, mfano kipindi kile kunibaka, dah huwa sisahau kabisa”
“Aaaah Dora si yashaisha hayo, ila kuna somo tumepata. Unajua kunywa sio vibaya ila kulewa ni vibaya, hebu ona tumekosa hata ufahamu kuwa tunachukuliwa simu. Ngoja tujiandae tu tushughulikie kwanza simu na laini kabla ya yote maana mawasiliano ndio ya muhimu”
“Na gari kasepa nalo, aaah wanawake wengine ni noma”
“Yule muache ila atajutia, vile vitu vinapita tu hakuna kitakachobaki je ataweza kuendelea kulea mtoto mwenyewe!”
“Ila James tutamlaumu tu Yule mwanamke ila ulevi wetu ni mbaya, hebu ona sasa tumelewa na kuanza kutenda matendo ya ajabu kwa Yule mwanamke, tumejitia uchizi kumbe Yule ni chizi zaidi yetu”
Basi walimaliza kula na kujiandaa ambapo Dora alivaa tu nguo baadhi zilizobaki za Bite kwa wakati huo na kutoka na James.
Tony leo alienda kukutana na Tumaini kwenye duka ambalo lilimilikiwa na Erick, ila aliona kama akimwambia Tumaini kuwa mama yake anataka amuone kumfanyie kama usahili, basi Tumaini atakataa kwahiyo aliamua kumwambia kwa njia nyingine,
“Tumaini, mama amekukubali ila anataka uende nyumbani Jumamosi ulale hapo na uondoke Jumapili”
“Hiyo ni ngumu kwangu Tony, siwezi kulala mbali na nyumbani. Baba atasema sana, siwezi labda nije tu kushinda”
“Sawa hakuna shida, basi niahidi kuwa utafanya hivyo na hiyo Jumamosi mimi nitakufata ili twende wote nyumbani”
“Hakuna shida”
Tony hakufikiria kuwa kitu anachotaka mama yake kumpima Tumaini kitakuwa kikubwa, kwani aliamini kila mwanamke lazima awe anajua kupika tena vizuri tu, ingawa hakuwahi kula chakula cha Tumaini ila aliamini kupika anaweza.
Wakati wanaongea ongea, mfanyakazi mmoja wa pale alienda kumuuliza Tumaini,
“Yule mama wa chakula kaja, sijui akuletee nini leo?”
“Ana pilau?”
“Amesema ipo ndio”
Tumaini akamuangalia Tony na kumuuliza,
“Unapendaga pilau?”
“Napenda ndio”
“Pilau ya huyu mama ni nzuri hatari, ngoja niagize tule”
Kisha akamgeukia Yule msichana na kumwambia,
“Mwambie alete pilau sahani mbili, pilau kuku eeeh! Aweke kachumbari ya kutosha na Yule wa juisi mwambie atuletee juisi glasi mbili”
Yule dada akaondoka, ila kwa kitendo kile cha Tumaini kujua hadi vyakula vitamu kilimpa moyo Tony kuwa Tumaini lazima kwenye kupika yupo vizuri, maana hadi anajua chakula kitamu na kibaya.
Baada ya muda chakula kile kililetwa na wakaanza kula, kiukweli kilikuwa kitamu sana hata Tony alikiri kuwa ni kitamu hadi alikipenda,
“Hiki chakula balaa, ni kitamu sijapata kuona. Huyo mama anajua kupika sana, na kuku yake nzuri sana”
“Ni kweli anajua kupika, sasa siku uje ule ndizi utumbo weeee utajikata vidole kwa utamu, anaweka na nazi ni tamu sana”
“Ila pilau kama hii anaipikaje? Mbona wengi wanapika ila sio tamu hivi”
“Mmmmh mwenzangu, kupika kipaji ujue, nahisi huyu mama ni kipaji chake jamani yani anaweza kupika haswaaa”
Akatamani kumuuliza kuwa na yeye anaweza kupika nini cha kusifiwa na watu ila hakutaka kwakweli alihisi pengine anaweza kumuudhi kwahiyo hakumuuliza.
Wakati wanamalizia malizia kula, alifika Erick na kuwakuta wakila, alicheka na kusema,
“Hatimaye dada yangu amepatikana, na wewe umekuwa na mpenzi Tumaini?”
“Toka zako huko”
Erick alicheka tu na kusalimiana na Tony pale huku akimwambia,
“Karibu kwenye ukoo wetu kaka, ila sijui ndio nitakuitaje? Shemeji shemeji, hahahah shemeji mara mbili”
Tony akauliza,
“Kwani vibaya?”
Tumaini akataka kubadilisha mada na kumwambia Erick,
“Erick, nikuagizie chakula, pilau ya huyu mama ni tamu balaa”
Erick akajibu,
“Hapana, yani nimepitia tu hapa mara moja ila sasa hivi naenda kwangu nitakula huko. Chakula cha Erica ni kitamu zaidi, siwezi nikala huku halafu nikashindwa kula chakula cha mke wangu”
Tumaini akauliza,
“Hivi Erica anajua kupika eeeh!”
“Ndio, siku nitawakaribisha kwangu na mke wangu ataandaa chakula mtahisi kimetoka hotelini ila sitaki kumpa mzigo wa kupika maana sasa ni kijacho Yule”
Wakacheka tu, wakaongea ongea pale kisha Erick akawaaga na kuondoka zake kuelekea nyumbani kwake.
Na kweli Erick alipofika tu alimkuta Erica ameshapika tena chakula anachokipenda siku zote, kisha akaandaa na kuanza kula pamoja,
“Erica mke wangu, uwe unapumzika nataka nikuletee msichana wa kazi akusaidie saidie hapa nyumbani”
Erica alifikiria jambo, alifikiria kuhusu msichana wa kazi aliyekuwa nyumbani kwa dada yake kipindi kile na jinsi alivyotembea na shemeji yake, akakataa
“Hapana sitaki msaidizi”
“Kwanini Erica?”
“Sitaki tu”
“Najua unawaza mawazo potofu, mimi nakupenda wewe hata waje wanawake mia moja mbele yangu wakiwa watupu na wewe umevaa ila bado nitakuchagua wewe, Erica amini hilo kuwa nakupenda sana yani hakuna msichana hata mmoja mwenye nafasi kwenye moyo wangu zaidi yako wewe, nakupenda sana malkia wangu”
Erica alifurahi sana kusikia vile ila Erick alimuomba hata kuleta msaidizi ambaye atakuwa anaenda pale nyumbani mchana na kuondoka jioni, mwishowe Erica alikubali kuhusu lile swala alilolisema Erick.
Basi walipomaliza kula simu ya Erick ilianza kuita na alipoiangalia akaona ni namba ya mama yake akapokea,
“Uko wapi saa hizi Erick?”
“Nipo mjini mama”
“Nakuomba ofisini kwangu mara moja kabla sijaondoka”
“Mama, nakuomba nije kesho maana kuna mambo namalizia”
“Mjinga wewe, yani kuniongopea tu. Hutaki kusema ukweli kuwa unaishi na Erica ulidhani sitajua ujinga wako? Na ni biashara gani hiyo ya kuishi na mtoto wa watu bila baraka za wazazi, sasa kesho uje ofisini”
Simu ikakatika, Erica alimtazama Erick na kumuuliza,
“Inamaana mama yako hakujua kama tunaishi wote?”
“Hakujua”
“Hukumwambia? Si ulisema utamwambia kila kitu!”
“Erica mpenzi, siku ile mambo yaliingiliana ndiomana siku ongea nae, ni siku ambayo nilijua kuwa Dora ni muathirika pia nikajua kuwa uliwahi kuwa na mahusiano na George nikapaniki sana”
“Ila Erica mambo mengine bhana, nakumbuka wakati tunaanza mahusiano ulisema tufute yote yaliyopita kwetu, sasa kwa mtindo huu mimi sio nitakufa kwa presha maana sidhani kama kuna rangi umeacha katika kuhangaika na wanawake”
“Mmmh tuache hizo mada Erica”
Yani Erick hakupenda kabisa kuongelea swala la wanawake zake waliopita. Walianza kuongelea tu mustakabali wa nyumba yao unavyoendelea kwa kipindi hiko.
Dora na James walifika nyumbani kwa James usiku ule ila kwa bahati mlinzi wa James alirudi, kumbe alimtimua ila mlinzi alirudi, yani mlinzi alivyomuona James alianza kumuomba msamaha ila James alimshukuru sana mlinzi kwa uwepo wake tena kisha akamsaidia kuharibu kitasa cha mlango na kuingia ndani ambapo ilibidi alale mule na Dora hadi palipokucha ila kiukweli hawakulala kabisa kwani kila mmoja alikuwa na mawazo sana, waliwaza kuhusu simu zao yani simu ndio zilizowatia mawazo zaidi, kiukweli Dora alikuwa amechoka sana na kuamua tu kwenda jikoni kwa James na kupika kisha kuandaa chakula na kuanza kula na James, kwa mara ya kwanza leo James alikula chakula kilichopikwa na Dora, alikula na kumwambia,
“Kheee Dora licha ya kuhangaika hangaika kumbe kupika unajua?”
Dora akacheka na kusema,
“Tena leo nina mawazo yangu ndiomana, ila na wewe James hivi ni wanawake gani wale unakuwa nao? Aina gani ile ya mwanamke ulimuokotea wapi?”
“Hapana unajua Yule mwanamke alikuwa ni mfanyakazi wa humu ndani, na nilianza nae kipindi mke wangu mjamzito maana alikuwa mvivu sana”
“Ndio tabia ya kuhangaika na wasichana wa kazi hiyo, tatizo wanaume huwa hamridhiki hata wake zenu wawafanyie nini ndani, mfano kipindi kile kunibaka, dah huwa sisahau kabisa”
“Aaaah Dora si yashaisha hayo, ila kuna somo tumepata. Unajua kunywa sio vibaya ila kulewa ni vibaya, hebu ona tumekosa hata ufahamu kuwa tunachukuliwa simu. Ngoja tujiandae tu tushughulikie kwanza simu na laini kabla ya yote maana mawasiliano ndio ya muhimu”
“Na gari kasepa nalo, aaah wanawake wengine ni noma”
“Yule muache ila atajutia, vile vitu vinapita tu hakuna kitakachobaki je ataweza kuendelea kulea mtoto mwenyewe!”
“Ila James tutamlaumu tu Yule mwanamke ila ulevi wetu ni mbaya, hebu ona sasa tumelewa na kuanza kutenda matendo ya ajabu kwa Yule mwanamke, tumejitia uchizi kumbe Yule ni chizi zaidi yetu”
Basi walimaliza kula na kujiandaa ambapo Dora alivaa tu nguo baadhi zilizobaki za Bite kwa wakati huo na kutoka na James.
Tony leo alienda kukutana na Tumaini kwenye duka ambalo lilimilikiwa na Erick, ila aliona kama akimwambia Tumaini kuwa mama yake anataka amuone kumfanyie kama usahili, basi Tumaini atakataa kwahiyo aliamua kumwambia kwa njia nyingine,
“Tumaini, mama amekukubali ila anataka uende nyumbani Jumamosi ulale hapo na uondoke Jumapili”
“Hiyo ni ngumu kwangu Tony, siwezi kulala mbali na nyumbani. Baba atasema sana, siwezi labda nije tu kushinda”
“Sawa hakuna shida, basi niahidi kuwa utafanya hivyo na hiyo Jumamosi mimi nitakufata ili twende wote nyumbani”
“Hakuna shida”
Tony hakufikiria kuwa kitu anachotaka mama yake kumpima Tumaini kitakuwa kikubwa, kwani aliamini kila mwanamke lazima awe anajua kupika tena vizuri tu, ingawa hakuwahi kula chakula cha Tumaini ila aliamini kupika anaweza.
Wakati wanaongea ongea, mfanyakazi mmoja wa pale alienda kumuuliza Tumaini,
“Yule mama wa chakula kaja, sijui akuletee nini leo?”
“Ana pilau?”
“Amesema ipo ndio”
Tumaini akamuangalia Tony na kumuuliza,
“Unapendaga pilau?”
“Napenda ndio”
“Pilau ya huyu mama ni nzuri hatari, ngoja niagize tule”
Kisha akamgeukia Yule msichana na kumwambia,
“Mwambie alete pilau sahani mbili, pilau kuku eeeh! Aweke kachumbari ya kutosha na Yule wa juisi mwambie atuletee juisi glasi mbili”
Yule dada akaondoka, ila kwa kitendo kile cha Tumaini kujua hadi vyakula vitamu kilimpa moyo Tony kuwa Tumaini lazima kwenye kupika yupo vizuri, maana hadi anajua chakula kitamu na kibaya.
Baada ya muda chakula kile kililetwa na wakaanza kula, kiukweli kilikuwa kitamu sana hata Tony alikiri kuwa ni kitamu hadi alikipenda,
“Hiki chakula balaa, ni kitamu sijapata kuona. Huyo mama anajua kupika sana, na kuku yake nzuri sana”
“Ni kweli anajua kupika, sasa siku uje ule ndizi utumbo weeee utajikata vidole kwa utamu, anaweka na nazi ni tamu sana”
“Ila pilau kama hii anaipikaje? Mbona wengi wanapika ila sio tamu hivi”
“Mmmmh mwenzangu, kupika kipaji ujue, nahisi huyu mama ni kipaji chake jamani yani anaweza kupika haswaaa”
Akatamani kumuuliza kuwa na yeye anaweza kupika nini cha kusifiwa na watu ila hakutaka kwakweli alihisi pengine anaweza kumuudhi kwahiyo hakumuuliza.
Wakati wanamalizia malizia kula, alifika Erick na kuwakuta wakila, alicheka na kusema,
“Hatimaye dada yangu amepatikana, na wewe umekuwa na mpenzi Tumaini?”
“Toka zako huko”
Erick alicheka tu na kusalimiana na Tony pale huku akimwambia,
“Karibu kwenye ukoo wetu kaka, ila sijui ndio nitakuitaje? Shemeji shemeji, hahahah shemeji mara mbili”
Tony akauliza,
“Kwani vibaya?”
Tumaini akataka kubadilisha mada na kumwambia Erick,
“Erick, nikuagizie chakula, pilau ya huyu mama ni tamu balaa”
Erick akajibu,
“Hapana, yani nimepitia tu hapa mara moja ila sasa hivi naenda kwangu nitakula huko. Chakula cha Erica ni kitamu zaidi, siwezi nikala huku halafu nikashindwa kula chakula cha mke wangu”
Tumaini akauliza,
“Hivi Erica anajua kupika eeeh!”
“Ndio, siku nitawakaribisha kwangu na mke wangu ataandaa chakula mtahisi kimetoka hotelini ila sitaki kumpa mzigo wa kupika maana sasa ni kijacho Yule”
Wakacheka tu, wakaongea ongea pale kisha Erick akawaaga na kuondoka zake kuelekea nyumbani kwake.
Na kweli Erick alipofika tu alimkuta Erica ameshapika tena chakula anachokipenda siku zote, kisha akaandaa na kuanza kula pamoja,
“Erica mke wangu, uwe unapumzika nataka nikuletee msichana wa kazi akusaidie saidie hapa nyumbani”
Erica alifikiria jambo, alifikiria kuhusu msichana wa kazi aliyekuwa nyumbani kwa dada yake kipindi kile na jinsi alivyotembea na shemeji yake, akakataa
“Hapana sitaki msaidizi”
“Kwanini Erica?”
“Sitaki tu”
“Najua unawaza mawazo potofu, mimi nakupenda wewe hata waje wanawake mia moja mbele yangu wakiwa watupu na wewe umevaa ila bado nitakuchagua wewe, Erica amini hilo kuwa nakupenda sana yani hakuna msichana hata mmoja mwenye nafasi kwenye moyo wangu zaidi yako wewe, nakupenda sana malkia wangu”
Erica alifurahi sana kusikia vile ila Erick alimuomba hata kuleta msaidizi ambaye atakuwa anaenda pale nyumbani mchana na kuondoka jioni, mwishowe Erica alikubali kuhusu lile swala alilolisema Erick.
Basi walipomaliza kula simu ya Erick ilianza kuita na alipoiangalia akaona ni namba ya mama yake akapokea,
“Uko wapi saa hizi Erick?”
“Nipo mjini mama”
“Nakuomba ofisini kwangu mara moja kabla sijaondoka”
“Mama, nakuomba nije kesho maana kuna mambo namalizia”
“Mjinga wewe, yani kuniongopea tu. Hutaki kusema ukweli kuwa unaishi na Erica ulidhani sitajua ujinga wako? Na ni biashara gani hiyo ya kuishi na mtoto wa watu bila baraka za wazazi, sasa kesho uje ofisini”
Simu ikakatika, Erica alimtazama Erick na kumuuliza,
“Inamaana mama yako hakujua kama tunaishi wote?”
“Hakujua”
“Hukumwambia? Si ulisema utamwambia kila kitu!”
“Erica mpenzi, siku ile mambo yaliingiliana ndiomana siku ongea nae, ni siku ambayo nilijua kuwa Dora ni muathirika pia nikajua kuwa uliwahi kuwa na mahusiano na George nikapaniki sana”
“Ila Erica mambo mengine bhana, nakumbuka wakati tunaanza mahusiano ulisema tufute yote yaliyopita kwetu, sasa kwa mtindo huu mimi sio nitakufa kwa presha maana sidhani kama kuna rangi umeacha katika kuhangaika na wanawake”
“Mmmh tuache hizo mada Erica”
Yani Erick hakupenda kabisa kuongelea swala la wanawake zake waliopita. Walianza kuongelea tu mustakabali wa nyumba yao unavyoendelea kwa kipindi hiko.