Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,081
- 464,063
SEHEMU YA 01-Nyemo Chilongani
“Unahitaji kuwa nani baadaye?” lilikuwa swali la kwanza mzee Jackson Gwamaka alimuuliza binti yake aliyeitwa Nandy aliyekuwa akisoma darasa la sita katika Shule ya Msingi Kurasini, jijini Dar es Salaam.
“Nitataka kuwa muimbaji wa nyimbo za Injili, nitataka nimuimbie Mungu mpaka viwete watembee, vipofu waone na wenye matatizo mbalimbali waponywe,” alijibu binti huyo mrembo huku akimwangalia baba yake kwa sura iliyojaa tabasamu pana.
“Unahisi utaweza kumuimbia Mungu maisha yako yote?”
“Ndiyo! Nitamuimbia mpaka naingia kaburini. Nitataka nimtumikie yeye tu katika maisha yangu,” alijibu msichana huyo.
Mzee Gwamaka akamwangalia binti yake kwa mara nyingine, tabasamu pana likatawala usoni mwake. Alimpenda Nandy, alikuwa mtoto wake pekee katika maisha yake.
Moyo wake ulikuwa na faraja kubwa, alipenda kumuona Nandy akizungumzia kuhusu ukuu wa Mungu. Kila siku alimlea binti yake katika mazingira ya kidini huku akimwambia kuhusu ubaya wa wanaume.
Hakutaka kumuona binti yake akipotea, katika maisha yake alitamani kumuona akiendelea kumsifu Mungu mpaka pale atakapoingia kaburini. Mke wake, alifariki dunia siku alipokwenda kujifungua hospitalini. Moyo wake ulimuuma, alilia sana na ndiyo maana kwa Nandy alikuwa roho yake, faraja yake na hakutaka kumuona binti yake huyo akipotea.
Kila siku alimfundisha Nandy Neno la Mungu, alimwambia mambo mengi makuu ambayo Mungu alikuwa akiyatenda tangu kipindi cha Isaka,Yakobo na vizazi vingine vilivyofuata vikiwemo vya Mfalme Daudi na Suleimani.
Mbali na kutamani kumtumikia kumtumikia Mungu, Nandy alikuwa miongoni mwa mabinti waliokuwa na sura nzuri kupita kawaida japokuwa alikuwa akiishi kwenye umasikini mkubwa.
Mtaani hapo Kurasini alipokuwa akikaa, gumzo lilikuwa yeye tu. Alikuwa na umri mdogo lakini kila mtu aliyekuwa akimwangalia aliamini kwamba msichana huyo angekuja kutingisha sana siku za usoni.
Barabarani, wanaume walimtolea macho, kila aliyemwangalia hakuacha kumwangalia mara moja, alimwangalia mara mbili-mbili huku wengine wakidiriki kusimama na kumwangalia mpaka alipopotea katika macho yao.
“Unahitaji kuwa nani baadaye?” lilikuwa swali la kwanza mzee Jackson Gwamaka alimuuliza binti yake aliyeitwa Nandy aliyekuwa akisoma darasa la sita katika Shule ya Msingi Kurasini, jijini Dar es Salaam.
“Nitataka kuwa muimbaji wa nyimbo za Injili, nitataka nimuimbie Mungu mpaka viwete watembee, vipofu waone na wenye matatizo mbalimbali waponywe,” alijibu binti huyo mrembo huku akimwangalia baba yake kwa sura iliyojaa tabasamu pana.
“Unahisi utaweza kumuimbia Mungu maisha yako yote?”
“Ndiyo! Nitamuimbia mpaka naingia kaburini. Nitataka nimtumikie yeye tu katika maisha yangu,” alijibu msichana huyo.
Mzee Gwamaka akamwangalia binti yake kwa mara nyingine, tabasamu pana likatawala usoni mwake. Alimpenda Nandy, alikuwa mtoto wake pekee katika maisha yake.
Moyo wake ulikuwa na faraja kubwa, alipenda kumuona Nandy akizungumzia kuhusu ukuu wa Mungu. Kila siku alimlea binti yake katika mazingira ya kidini huku akimwambia kuhusu ubaya wa wanaume.
Hakutaka kumuona binti yake akipotea, katika maisha yake alitamani kumuona akiendelea kumsifu Mungu mpaka pale atakapoingia kaburini. Mke wake, alifariki dunia siku alipokwenda kujifungua hospitalini. Moyo wake ulimuuma, alilia sana na ndiyo maana kwa Nandy alikuwa roho yake, faraja yake na hakutaka kumuona binti yake huyo akipotea.
Kila siku alimfundisha Nandy Neno la Mungu, alimwambia mambo mengi makuu ambayo Mungu alikuwa akiyatenda tangu kipindi cha Isaka,Yakobo na vizazi vingine vilivyofuata vikiwemo vya Mfalme Daudi na Suleimani.
Mbali na kutamani kumtumikia kumtumikia Mungu, Nandy alikuwa miongoni mwa mabinti waliokuwa na sura nzuri kupita kawaida japokuwa alikuwa akiishi kwenye umasikini mkubwa.
Mtaani hapo Kurasini alipokuwa akikaa, gumzo lilikuwa yeye tu. Alikuwa na umri mdogo lakini kila mtu aliyekuwa akimwangalia aliamini kwamba msichana huyo angekuja kutingisha sana siku za usoni.
Barabarani, wanaume walimtolea macho, kila aliyemwangalia hakuacha kumwangalia mara moja, alimwangalia mara mbili-mbili huku wengine wakidiriki kusimama na kumwangalia mpaka alipopotea katika macho yao.