SIMULIZI: MY LIFE MY HISTORY.

SIMULIZI: MY LIFE MY HISTORY.

incredible terminator

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2016
Posts
2,533
Reaction score
4,286
My LIFE MY HISTORY SHORT FILM STORY.

1. 1992-1995 Kwa kipindi hiki nilipendwa sana na Mzazi wangu kila nilipokuwa nikilia alinibembeleza na kuninyamazisha na kunipa vitu vizurii na vya kuvutia ili tu vinipatie faraja na kunifulahisha Mama alinipa maua, pamoja na Majani mazuri ya kuvutia labda alinipa vyote hivi kwasababu hakuwa na uwezo wa kuninunulia Vimagari vya watoto pamoja na Vindege vya kuchezea, hakika kwa kipindi hiki sikuwa najua lolote kuhusiana na maisha wala ndoto za baadae..!

2. 1996-2000, Kwa kipindi hiki nilikuwa mbali na Mikono ya Mama, hapa mama aliniacha nikacheze na watoto wenzangu, na kwa kipindi hiki nilipata malezi ya kaka zangu ambao ndio walionekana kuwa karibu sana na mimi waliniadhibu nikikosea na kuniogesha, nahata siku zingine pia walinisemea kwa Mama pale nilipokuwa nimefanya makosa ya uvujanji wa sheria za kimalezi, Kwa kipindi hiki nilikula peke yangu bila kulishwa na mtu na pia kuna baadhi ya siku zingine kaka waliniogesha na pia kuna baadhi ya siku walinitaka nioge peke yangu, hapo ndio ilikuwa fulaha yangu maana nilikuwa nikiambiwa nioge peke yangu hapo siku hiyo nitajipaka maji nitalala bila kujisugua na kujitonesha makovu ya vidonda nilivyokuwa napata kutokana na michezo ya kitoto ambayo nilikuwa nikiumia kila siku,

Kwa kipindi hiki nilichukia sana kuoga na hapa ndipo akili yangu ilianza kupata ndoto, Ndoto zenye asili ya kitoto, ndoto zenye makusudio ya kitoto,

Kwa hapa nilianza kupata ndoto ya Nikija kuwa mkubwa sitakuja kulazimishwa kuoga tena, wala sitakuja kuwa natoneshwa vidonda vyangu katika mda kuogeshwa nitaishi kivyangu na sitaumizwa tena na kaka waliokuwa wakiniogesha,
Huo ndio uliokuwa mwanzo wa kuanza kupata ndoto, kwani kwa kipindi hicho adui yangu mkubwa alikuwa maji ya baridi sabuni na dodoki.

3. 2001-2006 Kwa kipindi hichi nilikuwa sipo tena mikononi mwa uangalizi wa kaka na Mama yangu tena, bali nilikuwa chini ya uangalizi wa Walimu wangu ambao walikuwa wakiniimbisha A E I O U
ITAENDELEA......
 
Ilipoishia....A E I O U ...INAENDELEA.....

Kuanzia saa moja hadi saa sita Hakika kwa kipindi hiki niliyachukia sana maisha hayo kwani ni maisha ambayo yalininyima uhuru wa kucheza na wenzangu, kwani awali nilizoea sana kwenda na wenzangu maporini kuchunga mbuzi, na kwa kutokana na ukorofi wangu niliokuwa nao na maisha ya kukulia uswahilini nilikuwa nachapwa sana na Mwalimu wangu kwa lengo la kuniweka katika mstari ulionyooka

Na hapa sasa ndipo nilipoanza kupata tena Ndoto nyingine kuwa nikikuwa mkubwa nitalipiza kisasi kwa watesi wangu wote nikianza na mwalimu na hata kaka ambao walikuwa wakinilazimisha kudamka asubuhi na kuwahi shuleni kuhesabu namba, hakika nilitaman sana nami siku moja nikuwe kijana mkubwa ili nikapambane nao na hata ikibidi niwape kipondo kama kile walichokuwa wakinipatia na hata ikibidi niwaondoe kabisa ndani ya uso wa Duna hii,

Hapo pia ni miongoni mwa ndoto nilizokuwa na nazo enzi hizo katika maisha yangu, kutokana na akili yangu ya kitoto niliamini kabisa adui yangu mkubwa ni shule pamoja na Mwalimu wangu alienifundisha kuhesabu namba sikuwahi kutambua kama yupo adui yangu zaidi ya huyo ambae kwangu alionekana kero kubwa sana.

4. 2007-2012, Katika kipindi hiki nilikuwa na uwezo wa kujielewa japo si kwa sana niliwaona marafiki zangu walioacha shule na kujiingiza katika maisha mitaani, niliwatamani sana kwa uhuru waliokuwa nao kwani wao mda wote walionekana wenye fulaha na wenye uhuru wa kufanya kila walitakalo walicheza mpira na hata kusindikizana majumbani kwao usiku na mchana, nakumbuka niliwahi kumtamani sana Suzani mtoto wa Mzee Hamidu lakini nilipojaribu kumwelezea ya moyoni alinicheka sana na kuniambia mimi bado ningali mdogo sana, bado ningali soma sina uwezo wa kumtimizia mahitaji yake,......
ITAENDELEA....
 
ILIPOISHIA... alinicheka sana na kuniambia mimi bado ningali mdogo sana, bado ningali soma sina uwezo wa kumtimizia mahitaji yake,....."INAENDELEA

...hakika usemi huu uliziibua hisia nzito zenye simanzi na majonzi akilini mwangu, nilihisi kama kuna moto umewashwa mwilini mwangu alinipandishia hasira zilizonijaa kichwani, katika hasira zangu zote nilizielekeza katika Familia yangu pamoja na umri wangu, hapa nilijiuliza kwanini mama alinipeleka shuleni?

pia kwanini ananiambia kuwa maisha yangu yanategemea elimu?

Na je mbona marafiki zangu wangali wanaishi kwa amani na upendo na familia zao ile hali hawasomi? Maswali yangu yote yalikosa majibu, kwani kwa ukali aliokuwa nao mama yangu mzazi nilijua fika kuwa asinge azimia wala kukubaliana na kunijibu maswali yangu,

Na hapa nilijikuta nafungua ukrasa mpya wa kuwa na ndoto ambayo niliipa uzito na kuamini ipo siku itatimia na si nyingine bali niliamini ipo siku nitahitimu Elimu yangu ya Kidato cha Nne na nitakuwa huru,

Pia nilijipa matumaini kuwa pamoja na kumkosa Suzani ambae tayari alionekana kunidharau kutokana na hali yangu ya uanafunzi na kigezo kuwa sikuwa na uwezo wa kumhudumia, Pia nilijipa moyo kuwa nikimaliza shule nitafanya biashara nitapata kipato kikubwa na nitawapata wasichana warembo na wazuri zaidi yake, Hakika kwa kipindi hiki niliamini kuwa maisha ni mepesi sana pasina shule, Pia niliamini kuwa kipimo cha mafanikio katika maisha ni kuwa na biashara yako na kumumiliki mrembo mzuri, niliamini sana katika maisha ya starehe nadhani hii labda ilitokana na umri niliokuwa nao kwa kipindi kile!

Sikuweza kujua kama kuna maisha zaidi nje ya kuwa na Msichana mrembo na kubadilisha viwanja, pia sikuamini katika vikwazo vyovyote kimaisha bali niliamini kuwa maisha ni mepesi sana pale nitakapokuwa nje ya shule!

5. 2013-2016, Katika kipindi hiki nimshukuru mungu kidogo japo sio kwa sana nilikuwa nimefanikisha kufikia umri ambao silazimishwi kufanya maamuzi, ITAENDELEA....
 
ILIPOISHIA... nilikuwa nimefanikisha kufikia umri ambao silazimishwi kufanya maamuzi....., INAENDELEA...

pia nilikuwa nimepata nafasi japo kwa uchache ya kukaa nje ya shule ambayo niliamini ndio adui mkubwa kwangu na ndicho kikwazo kwa maendeleo yangu japo nilivyojaribu mambo yalienda ndivyo sivyo hapa nilianza kukumbuka usemi wa mama yangu mzazi wa "Mwanangu kuwa uyaone"

Hakika akili ya utoto ilinidanganya na hisia za ujana zikanichanganya bila kujua kiama cha uzee kitafikia,

Nilipomaliza Elimu ya upili (secondary) niliamini sasa nimekaribia ndoto zangu za kuwa mfanyabiashara mkubwa nimiliki magari na Mabinti wazuri, Nizunguke kila pande ya Tanzania nizimalize starehe zote zilizopo huku ulimwenguni! Lakini mambo hayakuwa kama nilivyokusudia kila nililolipanga liliyeyushwa kama urimbo juani na kila nilichokijaribu kilimiminika kama maji kwenye ndoo yenye tobo, hakika mambo hayakuwa kama nilivyo yapangilia.......!

Kikubwa nataka leo Tupate Funzo kuwa Malego na ndoto hubadilika kadri majukumu na siku zinavyozidi kwenda

Written Youngtozy1992
[HASHTAG]#HISTORY[/HASHTAG] OF MYLIFE

Short film coming soon[emoji814]
 
ILIPOISHIA... nilikuwa nimefanikisha kufikia umri ambao silazimishwi kufanya maamuzi....., INAENDELEA...

pia nilikuwa nimepata nafasi japo kwa uchache ya kukaa nje ya shule ambayo niliamini ndio adui mkubwa kwangu na ndicho kikwazo kwa maendeleo yangu japo nilivyojaribu mambo yalienda ndivyo sivyo hapa nilianza kukumbuka usemi wa mama yangu mzazi wa "Mwanangu kuwa uyaone"

Hakika akili ya utoto ilinidanganya na hisia za ujana zikanichanganya bila kujua kiama cha uzee kitafikia,

Nilipomaliza Elimu ya upili (secondary) niliamini sasa nimekaribia ndoto zangu za kuwa mfanyabiashara mkubwa nimiliki magari na Mabinti wazuri, Nizunguke kila pande ya Tanzania nizimalize starehe zote zilizopo huku ulimwenguni! Lakini mambo hayakuwa kama nilivyokusudia kila nililolipanga liliyeyushwa kama urimbo juani na kila nilichokijaribu kilimiminika kama maji kwenye ndoo yenye tobo, hakika mambo hayakuwa kama nilivyo yapangilia.......!

Kikubwa nataka leo Tupate Funzo kuwa Malego na ndoto hubadilika kadri majukumu na siku zinavyozidi kwenda

Written Youngtozy1992
[HASHTAG]#HISTORY[/HASHTAG] OF MYLIFE

Short film coming soon[emoji814]
[emoji116] [emoji3] [emoji11] [emoji3] [emoji3] [emoji3]
 
My LIFE MY HISTORY SHORT FILM STORY.

1. 1992-1995 Kwa kipindi hiki nilipendwa sana na Mzazi wangu kila nilipokuwa nikilia alinibembeleza na kuninyamazisha na kunipa vitu vizurii na vya kuvutia ili tu vinipatie faraja na kunifulahisha Mama alinipa maua, pamoja na Majani mazuri ya kuvutia labda alinipa vyote hivi kwasababu hakuwa na uwezo wa kuninunulia Vimagari vya watoto pamoja na Vindege vya kuchezea, hakika kwa kipindi hiki sikuwa najua lolote kuhusiana na maisha wala ndoto za baadae..!

2. 1996-2000, Kwa kipindi hiki nilikuwa mbali na Mikono ya Mama, hapa mama aliniacha nikacheze na watoto wenzangu, na kwa kipindi hiki nilipata malezi ya kaka zangu ambao ndio walionekana kuwa karibu sana na mimi waliniadhibu nikikosea na kuniogesha, nahata siku zingine pia walinisemea kwa Mama pale nilipokuwa nimefanya makosa ya uvujanji wa sheria za kimalezi, Kwa kipindi hiki nilikula peke yangu bila kulishwa na mtu na pia kuna baadhi ya siku zingine kaka waliniogesha na pia kuna baadhi ya siku walinitaka nioge peke yangu, hapo ndio ilikuwa fulaha yangu maana nilikuwa nikiambiwa nioge peke yangu hapo siku hiyo nitajipaka maji nitalala bila kujisugua na kujitonesha makovu ya vidonda nilivyokuwa napata kutokana na michezo ya kitoto ambayo nilikuwa nikiumia kila siku,

Kwa kipindi hiki nilichukia sana kuoga na hapa ndipo akili yangu ilianza kupata ndoto, Ndoto zenye asili ya kitoto, ndoto zenye makusudio ya kitoto,

Kwa hapa nilianza kupata ndoto ya Nikija kuwa mkubwa sitakuja kulazimishwa kuoga tena, wala sitakuja kuwa natoneshwa vidonda vyangu katika mda kuogeshwa nitaishi kivyangu na sitaumizwa tena na kaka waliokuwa wakiniogesha,
Huo ndio uliokuwa mwanzo wa kuanza kupata ndoto, kwani kwa kipindi hicho adui yangu mkubwa alikuwa maji ya baridi sabuni na dodoki.

3. 2001-2006 Kwa kipindi hichi nilikuwa sipo tena mikononi mwa uangalizi wa kaka na Mama yangu tena, bali nilikuwa chini ya uangalizi wa Walimu wangu ambao walikuwa wakiniimbisha A E I O U
ITAENDELEA......
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom