bioto
JF-Expert Member
- Oct 1, 2017
- 1,261
- 2,095
- Thread starter
- #21
MTOTO WA MAAJABU: 14
Kwenye mida ya saa tano usiku, Juma alienda na ile dawa hadi mlangoni, kisha akanuiza maneno yake na kutaka kuinyunyizia ila alishangaa kushikwa mguuni, alishtuka sana na kuangalia ni nani kamshika! Alishangaa kuona ni mtoto wao ndio kamshika.
Kwakweli Juma alijikuta akiogopa sana hata akajikuta anashindwa cha kuongea chochote kile na kuita,
“Anna, Anna”
Anna akatoka nje na kwenda hadi pale ambapo Juma akamwambia Anna,
“Mbona umemuachia mtoto atembee usiku huu?”
“Hata sikujua shemeji, halafu kumbe sikufunga mlango wa chumbani kwetu. Samahani shemeji”
Anna akainama na kumbeba mtoto yule halafu kwenda nae chumbani, kwakweli Juma alishindwa kuendelea na chochote pale kwa wakati ule zaidi ya kurudi chumbani ambapo alimkuta mkewe amekaa halafu kachukia sana na kuanza kumfokea Juma,
“Ulienda kufanya nini muda huu huko nje wakati tumelala?”
“Sikuwa nje mke wangu, nilienda jikoni kunywa maji”
“Muongo wewe, toka lini ukanywa maji usiku? Hata hiyo si ulinunua maji wewe na kuweka humu chumbani, umeshindwa nini kuchukua hayo na kuyanywa?”
Hapo Juma alikaa kimya na kumfanya Mariam aendelee kuongea,
“Hebu sema ukweli kama una mwanamke huko au ni itu gani maana haiwezekani kabisa kwa kitu unachokisema”
Juma huwa hapendi marumbano na mkewe wake, hivyobasi akamuomba kwa muda huo waweze kulala tu,
“Naomba tulale Mariam, hata hivyo nimechoka sana”
Mariam akamuangalia mumewe na muda huu hakusema neno zaidi zaidi na yeye kujilaza tu pale kitandani.
Leo kulipokucha tu, Juma alijiandaa na kuondoka zake yani leo hata chai hakunywa sababu akili yake ilikuwa ikiwaza mambo mengi sana kwa wakati mmoja haswa swala la mke wake na Anna, ni mambo ambayo yalimtatiza sana.
Mariam alipoamka leo alienda kama kawaida sebleni kunywa chai huku akilalamika kuchoka sana, basi Anna alimwambia waongee kidogo akimaliza kunywa chai na kweli alipomaliza waliweza kuongea sasa,
“Dada, si unalalamika kila siku kuchoka?”
“Ndio nachoka sana, hata sijui nifanyeje kwakweli”
“Dada, unaonaje tukiwa tunasaidiana na mimi kazi”
“Sasa ndio sitochoka?”
“Ndio dada maana utakuwa unaushughulisha mwili wako”
“Hapana hapo nitachoka zaidi, jamani mimi kufanya kazi za ndani siwezi, huwa naona uvivu sana Anna. Wewe endelea tu kwakweli maana mimi siwezi kabisa kufanya hiyo kazi”
Anna alishindwa jinsi ya kuendelea kumshawishi kwahiyo alimuacha vile vile aendelee kulala na kuchoka.
Juma leo hakukaa sana kwenye shughuli zake kwani moja kwa moja alienda kwao kuzungumza na mama yake maana yale mambo yalimtatiza sana.
Alimkuta mama yake pale na kumsalimia kisha kuzungumza nae,
“Mama sikiliza, hali ya mke wangu kuamka na kusema kuwa kachoka sana kwakweli mimi binafsi hainiridhishi kabisa, ni wazi yule binti anamtesa mke wangu sana ndiomana mke wangu anachoka sana”
Mama yake alimuangalia na kumwambia,
“Pole, sasa nikusaidiaje?”
“Sasa mama nimetumia kila njia ili kumkamata yule binti lakini imeshindikana”
“Mfano njia gani uliyotumia?”
Juma alimueleza mama yake jinsi alivyoenda kwa mganga na jinsi mganga alivyompa dawa na vile ilivyokuwa usiku, mama yake alishangaa sana na kuuliza,
“Kwani mwanao anatembea?”
“Ndio anatembea mama”
“Kheeee makubwa hayo, yule mtoto anatembea jamani? Katambaa lini sasa?”
“Hata mimi sijawahi kumuona akitambaa ila tu nilimuona akitembea, inasemekana ni chakula anachokula”
“Mnampa chakula gani siku hizi zaidi ya yale maziwa mliyokuwa mkiyatengeneza kiajabu?”
“Siku hizi anakula chakula tunachokula sisi, amekua yule mtoto inasemekana alikua toka tumboni”
“Mmmmh siwezi kubisha sana, ingawa mimi ni mtu mzima ila sijawahi kushuhudia mtoto wa hivi, huenda kuna ukweli. Ila hapo usiku ndio sijaelewa, alikuwa anafanya nini sasa hadi kakushika mguu?”
“Hata sielewi, Anna alisema kuwa alisahau kufunga mlango ndio mtoto katoka chumbani kwake”
Kidogo huyu mama akashangaa na kuuliza,
“Inamaana siku hizi mtoto analala na Anna?”
“Ndio mama, analala na Anna”
Huyu mama akapumua kidogo na kusema,
“Kheeee ila Juma kweli mke wako ni mvivu, hadi kulala na mwanae anaona uvivu loh!! Haya tuachane na hayo, ila mimi kuna hisia mbaya napata kwa mtoto wenu”
“Hisia gani mama?”
“Nahisi mtoto wenu ni mchawi pia”
Hapa Juma alipinga vikali na hakutaka kumuelewa kabisa mama yake, yani kuita mtoto wao ni mchawi? Kwakweli alichukia Juma na muda ule ule akaamua kumuaga mama yake ila mama yake akamwambia,
“Usichukie Juma mwanangu, sikuwa na nia mbaya kukwambia hivyo. Ila kwa ushauri wangu, nenda kaongee na mke wako ili mumfukuze huyo Anna anayewasumbua kwenye nyumba yenu”
Juma alimuitikia tu na kuondoka zake maana alishachukia kabisa.
Wakati Anna amekaa mchana huu akila na Mariam, alianza kuongea nae kuhusu mumewe Juma,
“Dada, hujawahi kupata matatizo yoyote ya shemeji kuwataka wadada wa kazi!”
Mariam akashtuka sana na kusema,
“Hapana, namuamini sana mume wangu”
“Ni vizuri kumuamini ila wadada wengine wa kazi sio waaminifu kabisa, unaweza shangaa kumbe anatoka na mume wako”
“Nashukuru Mungu sijapata wadada wa hivyo kabisa, sema hata hivyo huwa sidumu na msichana wa kazi, wewe Anna umekuwa wa pekee sana kwangu kwakweli hadi nahitaji kuishi nawe hapa kwa maisha yote”
“Asante dada, unajua kwanini nimekuuliza hivyo?”
“Eeeeh kwanini?”
“Kuna nyumba moja hivi kulikuwa na mdada wa kazi, basi baba mwenye nyumba kila siku akawa anasema huyu mdada anaondoke, simtaki kumbe yule baba kamtaka yule mdada ila mdada kamkataa sababu ana msimamo, basi wenye nyumba wakahisi mdada wa kazi ni mbaya wakaamua kumfukuza. Kisha yule baba akamleta hawara yake kama mdada wa kazi”
“Khaaa jamani, ila wanaume wana mambo ya ajabu”
“Tena sana dada yangu”
“Ila Anna nina usingizi hapa balaa, nasubiri kidogo tu chakula kishuke shuke nikalale”
“Sawa dada”
na kweli alikaa baada ya muda mfupi tu alilala.
Usiku wa leo, Juma alikuwa na mawazo yake ambayo kayapanga toka mchana alipotoka nyumbani kwao kwahiyo walipoenda kulala na Mariam aliamua kuongea nae kwanza,
“Mke wangu Mariam, kuna jambo nahitaji tufanye kwenye nyumba yetu”
“Jambo gani hilo?”
“Nahitaji tumfukuze Anna humu ndani, kusiwe na mfanyakazi kama yeye, kama msaidizi tutatafuta mwingine”
“Kwanini umeamua hivyo?”
“Mke wangu huyu Anna simuelewi”
“Humuelewi kivipi?”
“Yupo kama mchawi jamani!”
“Khaaaa mchawi mwenyewe na huo umalaya wako ulioanza kuufikiria, unafikiri hayo mawazo yako sijayapata? Yani unachopanga wewe ujue kwangu kimeshafikiriwa muda sana, kwahiyo wewe unataka kumfukuza Anna hapa ili ulete hawara yako aje kunisaidia kazi! Hapana hilo halikubaliki”
“Kheee Mariam umekuwaje? Kumbuka ni wewe ndiye uliyekuwa unasema kuwa siwezi kukusaliti”
“Nilisema ndio ila wanaume hamuaminiki kabisa”
“Imekuwaje nisiaminike tena? Ni kipi kimebadilika kwangu Mariam? Mimi ni Juma yule yule wa siku zote, nimebadilika nini sasa?”
Mariam hakumjibu mumewe bali alijigeuza na kulala huku akilalamika kuwa amechoka kama kawaida yake.
Kulipokucha tu Juma alijiandaa vizuri kabisa na hata kunywa chai hakunywa wala nini kwani moja kwa moja alienda tena kwa yule mganga wake kwani alihisi kuwa huenda safari hii akamsaidia.
Basi alivyofika na kuingia, yule mgaga akacheka na kumwambia Juma,
“Nilijua tu itashindikana maana pale kwako pamekuwa pazito sana”
“Sasa nifanyeje babu?”
“Weka kwanza salamu ya wazee”
Basi Juma aliweka pesa na kuendelea kumsikiliza yule babu tu.
Basi babu alitoa dawa ambayo ilikuwa kama maji halafu akamwambia Juma,
“Hii dawa, nenda kaweke kwenye jagi la maji ya kunywa, weka yote halafu acha mkeo na huyo mdada wa kazi wanywe, halafu utapata jibu ya hiko unachotaka kufahamu. Najua hii utafanikiwa”
“Nitafanikiw ababu, naona kabisa nitafanukiwa, asante sana babu”
Juma alimshukuru sana na kuondoka zake, yani hakutaka hata kwenda tena kwenye shughuli zake kwani kwa muda huo moja kwa moja alirudi nyumbani kwake kwani yeye alikuwa na hamu sana ya mkewe kugundua kuwa Anna ni mchawi, alitamani sana mkewe ajue kuwa anachoka kwaajili ya Anna.
Juma alifika kwake na kukuta ndio Anna anaandaa chakula mzani, wakati huo Mariam amekaa kwenye kochi tu yani Juma aliona ndio wakati sahihi kabisa ule.
Basi alienda jikoni na kuchukua jagi la maji na kujaza, kisha akaweka ile dawa yote na kupeleka mezani huku akisema,
“Anna umeandaa chakula bila hata kuweka maji!”
“Ningeweka shemeji, ila nilienda kwanza kuchukua maji ya kunawa, ila umenisaidia shemeji asante”
Juma alitabasamu tu, basi Anna alimfata Mariam na kumwambia,
“Dada jamani yani umekaa tu wakati mumeo ndio yupo kuandaa maji ya kunywa, hukumuona dada?”
“Aaaah Anna, haya maisha ya mimi na mume wangu yaache tu kama yalivyo, kwani hajui kama mimi nachoka sana? Anajua vizuri, asikuumize kichwa”
Basi sasa Mariam alisogea mezani na kumsalimia mumewe ambapo Juma alimwambia Mariam,
“Mke wangu si unywe maji kwanza halafu ndio ule!!”
“Weeee mambo ya wapi hayo? Ninywe maji kwanza halafu nishibe maji tu niache kula chakula! Mimi nakula kwanza halafu maji badae”
Juma akamuangalia Anna na kumwambia pia,
“Na wewe Anna si unywe maji kwanza ndio ule chakula!”
“Na mimi kama dada, hata sijazoea kunywa maji kabla ya chakula shemeji”
Basi wote wakapakua kile chakula na kuanza kula, yani Juma alikuwa anatamani sana wanywe maji maana pale wakinywa maji tu ndio kila kitu kitagundulika.
Wakiwa wanaendelea kula, mara waliona tu lile jagi likisukumwa na kuangushwa chini ambapo lilimwaga maji yote, hapo Mariam alishangaa,
“Khaaaa jamani, wewe mtoto kuanza kutembea ndio unapanda hadi mezani, sasa kutupa jagi ndio nini?”
Juma aliangalia na kusikitika sana, hadi alijikuta akikosa hamu ya kula kabisa kwani hakuongea kitu zaidi ya kuacha kula na kuondoka zake.
Anna alimuangalia na kumuuliza Mariam,
“Dada, mbona shemeji ameacha chakula?”
“Sijui, labda ameshiba”
“kamuulize dada?”
“Huwa sina muda huo, mtu mzima halazimishwi kula. Akiwa na njaa atakuja mwenyewe kula, yani mimi niache kushiba nianze kuulizana na watu kwanini umeacha chakula, kama amekula huko alipokuwa nitajuaje?”
“Labda kachukia mtoto kuangusha jagi dada?”
“Yani kuangusha jagi tu ndio achukie, lingekuwa limevunjika je si angejinyonga kabisa? Aniondolee balaa mie”
Kisha Anna alienda kuleta maji mengine ambapo walikula na kumaliza pale na walikuwa wameshiba kabisa.
Juma hakutoka tena chumbani, alijikuta akitafakari sana bila ya jibu lolote yani alikuwa kama haamini chochote kile ambacho kinatokea katika ile familia yao.
Muda huu Mariam alienda chumbani na kumkuta mumewe kajiinamia tu na mawazo akamuuliza,
“Wewe vipi una matatizo gani?”
“Kwakweli Mariam, naomba tumfukuze Anna, mimi siwezi kuishi na Anna humu ndani”
“Sababu kubwa ya kumfukuza Anna ni nini?”
“Anna ni mchawi mke wangu, yule binti ni mchawi kabisa nakwambia”
“Hivi Juma uchawi unaujua wewe? Ukiambiwa toa ushahidi kwa hoja yako kuwa Anna ni mchawi utatoa ushahidi gani?”
“Sina haja ya ushahidi ila Anna ni mchawi, tena ni mchawi sana, nataka aondoke kwenye nyumba yangu”
“Sikia nikwambie Juma, siku ya kuondoka Anna hapa ujue ni siku hiyo hiyo na mimi nitaondoka, siwezi kuangalia ukitaka kumnyanyasa mtu asiyekuwa na hatia sababu tu ya mawazo na hisia zako, muache Anna Kama alivyo”
Kwakweli Juma alichukia sana hata hakujua imekuwaje hadi akili za mke wake kutekwa kiasi kile na Anna.
Siku ya leo ndio Juma alienda tena kwenye shughuli zake ila alikuwa na hasira sana kiasi kwamba alikuwa akitembea huku akiongea peke yake maana alikuwa amejaza hasira kubwa sana kwenye moyo wake.
Basi Juma alifanya shughuli zake huku akiwa na mawazo sana kwa siku ya leo, alipomaliza akaondoka ila njiani alikutana na yule binti ambaye huwa wanakutana mara kwa mara,
“Niambie baba Mishi”
“Hivi mara ngapi nikukatalie kumuita mwanangu jina hilo?”
“Haya yameisha, vipi ulifanikiwa?”
“Nifanikiwe wapi? Sikuweza kumbamba wala nini”
“Ila ngoja nikuulize!”
“Niulize tu”
“Hivi wewe hufurahii kula chakula anachopika mke wako? Hufurahii kuona kazi za nyumbani kwenu zikifanywa na mkeo?”
“Na wewe acha kunichanganya, sasa ningekuwa nafurahia ni kwanini tulitafuta msaidizi? Sipendi mke wangu achoke, ona hata unyumba sipati maana kila siku amechoka”
“Ngoja nikuulize tena, toka mkeo ajifungue umeshawahi kupata unyumba?”
“Sijwahi sababu ya mtoto”
“Kwahiyo saivi ni mdada wa kazi amekuwa kikwazo, ngoja nitakusaidia ila kwanini hakunitafuta nikusaidie?”
“Ningekutafutaje? Sijui unapopatikana”
“Ngoja tukikutana safari ijayo nitakwambia jinsi ya kunipata mimi”
Kisha yule mtu alisogea na kuchuma majani Fulani kisha akamwambia Juma,
“Haya majani, ukifika kwako yatwange halafu ukimaliza kuyatwanga jipake wewe na mkeo nataka muone kila kitu ambacho Anna huwa anafanya kwenye nyumba yenu ila mkiona msimfanye chochote kibaya Anna, kama kumfukuza basi mumfukuze kwa utaratibu tu hata msimfanye chochote kibaya”
“Sawa nashukuru sana nimekuelewa, kwahiyo haya majani ni uhakika nitambamba yule mchawi?”
“Ndio, haya majani ni uhakika, yanakufanya uone kila kitu ambapo yeye hatojua kama mnaona kila kitu”
“Asante sana”
Yani Juma alimshukuru sana huyu mdada na kumuaga kwa muda huu ambapo yeye moja kwa moja alirudi nyumbani kwake.
Juma alipofika kwake, alienda kuwasalimia tu ndani kisha akweka vizuri mzigo aliofika nao pale, na baada ya hapo sasa akatoka nje.
Alichukua kinu kidogo na kuanza kuyaponda yale majani, ila muda kidogo mtoto wake alifika pale alipokuwa anaponda halafu akamuuliza Juma,
“Baba, kwanini unapenda uvivu wa mama?”
Itaendelea….!!!
Kwa mawasiliano 0629980412 likes zikifika 300 na share 100 naweka kingine chap chap
Kwenye mida ya saa tano usiku, Juma alienda na ile dawa hadi mlangoni, kisha akanuiza maneno yake na kutaka kuinyunyizia ila alishangaa kushikwa mguuni, alishtuka sana na kuangalia ni nani kamshika! Alishangaa kuona ni mtoto wao ndio kamshika.
Kwakweli Juma alijikuta akiogopa sana hata akajikuta anashindwa cha kuongea chochote kile na kuita,
“Anna, Anna”
Anna akatoka nje na kwenda hadi pale ambapo Juma akamwambia Anna,
“Mbona umemuachia mtoto atembee usiku huu?”
“Hata sikujua shemeji, halafu kumbe sikufunga mlango wa chumbani kwetu. Samahani shemeji”
Anna akainama na kumbeba mtoto yule halafu kwenda nae chumbani, kwakweli Juma alishindwa kuendelea na chochote pale kwa wakati ule zaidi ya kurudi chumbani ambapo alimkuta mkewe amekaa halafu kachukia sana na kuanza kumfokea Juma,
“Ulienda kufanya nini muda huu huko nje wakati tumelala?”
“Sikuwa nje mke wangu, nilienda jikoni kunywa maji”
“Muongo wewe, toka lini ukanywa maji usiku? Hata hiyo si ulinunua maji wewe na kuweka humu chumbani, umeshindwa nini kuchukua hayo na kuyanywa?”
Hapo Juma alikaa kimya na kumfanya Mariam aendelee kuongea,
“Hebu sema ukweli kama una mwanamke huko au ni itu gani maana haiwezekani kabisa kwa kitu unachokisema”
Juma huwa hapendi marumbano na mkewe wake, hivyobasi akamuomba kwa muda huo waweze kulala tu,
“Naomba tulale Mariam, hata hivyo nimechoka sana”
Mariam akamuangalia mumewe na muda huu hakusema neno zaidi zaidi na yeye kujilaza tu pale kitandani.
Leo kulipokucha tu, Juma alijiandaa na kuondoka zake yani leo hata chai hakunywa sababu akili yake ilikuwa ikiwaza mambo mengi sana kwa wakati mmoja haswa swala la mke wake na Anna, ni mambo ambayo yalimtatiza sana.
Mariam alipoamka leo alienda kama kawaida sebleni kunywa chai huku akilalamika kuchoka sana, basi Anna alimwambia waongee kidogo akimaliza kunywa chai na kweli alipomaliza waliweza kuongea sasa,
“Dada, si unalalamika kila siku kuchoka?”
“Ndio nachoka sana, hata sijui nifanyeje kwakweli”
“Dada, unaonaje tukiwa tunasaidiana na mimi kazi”
“Sasa ndio sitochoka?”
“Ndio dada maana utakuwa unaushughulisha mwili wako”
“Hapana hapo nitachoka zaidi, jamani mimi kufanya kazi za ndani siwezi, huwa naona uvivu sana Anna. Wewe endelea tu kwakweli maana mimi siwezi kabisa kufanya hiyo kazi”
Anna alishindwa jinsi ya kuendelea kumshawishi kwahiyo alimuacha vile vile aendelee kulala na kuchoka.
Juma leo hakukaa sana kwenye shughuli zake kwani moja kwa moja alienda kwao kuzungumza na mama yake maana yale mambo yalimtatiza sana.
Alimkuta mama yake pale na kumsalimia kisha kuzungumza nae,
“Mama sikiliza, hali ya mke wangu kuamka na kusema kuwa kachoka sana kwakweli mimi binafsi hainiridhishi kabisa, ni wazi yule binti anamtesa mke wangu sana ndiomana mke wangu anachoka sana”
Mama yake alimuangalia na kumwambia,
“Pole, sasa nikusaidiaje?”
“Sasa mama nimetumia kila njia ili kumkamata yule binti lakini imeshindikana”
“Mfano njia gani uliyotumia?”
Juma alimueleza mama yake jinsi alivyoenda kwa mganga na jinsi mganga alivyompa dawa na vile ilivyokuwa usiku, mama yake alishangaa sana na kuuliza,
“Kwani mwanao anatembea?”
“Ndio anatembea mama”
“Kheeee makubwa hayo, yule mtoto anatembea jamani? Katambaa lini sasa?”
“Hata mimi sijawahi kumuona akitambaa ila tu nilimuona akitembea, inasemekana ni chakula anachokula”
“Mnampa chakula gani siku hizi zaidi ya yale maziwa mliyokuwa mkiyatengeneza kiajabu?”
“Siku hizi anakula chakula tunachokula sisi, amekua yule mtoto inasemekana alikua toka tumboni”
“Mmmmh siwezi kubisha sana, ingawa mimi ni mtu mzima ila sijawahi kushuhudia mtoto wa hivi, huenda kuna ukweli. Ila hapo usiku ndio sijaelewa, alikuwa anafanya nini sasa hadi kakushika mguu?”
“Hata sielewi, Anna alisema kuwa alisahau kufunga mlango ndio mtoto katoka chumbani kwake”
Kidogo huyu mama akashangaa na kuuliza,
“Inamaana siku hizi mtoto analala na Anna?”
“Ndio mama, analala na Anna”
Huyu mama akapumua kidogo na kusema,
“Kheeee ila Juma kweli mke wako ni mvivu, hadi kulala na mwanae anaona uvivu loh!! Haya tuachane na hayo, ila mimi kuna hisia mbaya napata kwa mtoto wenu”
“Hisia gani mama?”
“Nahisi mtoto wenu ni mchawi pia”
Hapa Juma alipinga vikali na hakutaka kumuelewa kabisa mama yake, yani kuita mtoto wao ni mchawi? Kwakweli alichukia Juma na muda ule ule akaamua kumuaga mama yake ila mama yake akamwambia,
“Usichukie Juma mwanangu, sikuwa na nia mbaya kukwambia hivyo. Ila kwa ushauri wangu, nenda kaongee na mke wako ili mumfukuze huyo Anna anayewasumbua kwenye nyumba yenu”
Juma alimuitikia tu na kuondoka zake maana alishachukia kabisa.
Wakati Anna amekaa mchana huu akila na Mariam, alianza kuongea nae kuhusu mumewe Juma,
“Dada, hujawahi kupata matatizo yoyote ya shemeji kuwataka wadada wa kazi!”
Mariam akashtuka sana na kusema,
“Hapana, namuamini sana mume wangu”
“Ni vizuri kumuamini ila wadada wengine wa kazi sio waaminifu kabisa, unaweza shangaa kumbe anatoka na mume wako”
“Nashukuru Mungu sijapata wadada wa hivyo kabisa, sema hata hivyo huwa sidumu na msichana wa kazi, wewe Anna umekuwa wa pekee sana kwangu kwakweli hadi nahitaji kuishi nawe hapa kwa maisha yote”
“Asante dada, unajua kwanini nimekuuliza hivyo?”
“Eeeeh kwanini?”
“Kuna nyumba moja hivi kulikuwa na mdada wa kazi, basi baba mwenye nyumba kila siku akawa anasema huyu mdada anaondoke, simtaki kumbe yule baba kamtaka yule mdada ila mdada kamkataa sababu ana msimamo, basi wenye nyumba wakahisi mdada wa kazi ni mbaya wakaamua kumfukuza. Kisha yule baba akamleta hawara yake kama mdada wa kazi”
“Khaaa jamani, ila wanaume wana mambo ya ajabu”
“Tena sana dada yangu”
“Ila Anna nina usingizi hapa balaa, nasubiri kidogo tu chakula kishuke shuke nikalale”
“Sawa dada”
na kweli alikaa baada ya muda mfupi tu alilala.
Usiku wa leo, Juma alikuwa na mawazo yake ambayo kayapanga toka mchana alipotoka nyumbani kwao kwahiyo walipoenda kulala na Mariam aliamua kuongea nae kwanza,
“Mke wangu Mariam, kuna jambo nahitaji tufanye kwenye nyumba yetu”
“Jambo gani hilo?”
“Nahitaji tumfukuze Anna humu ndani, kusiwe na mfanyakazi kama yeye, kama msaidizi tutatafuta mwingine”
“Kwanini umeamua hivyo?”
“Mke wangu huyu Anna simuelewi”
“Humuelewi kivipi?”
“Yupo kama mchawi jamani!”
“Khaaaa mchawi mwenyewe na huo umalaya wako ulioanza kuufikiria, unafikiri hayo mawazo yako sijayapata? Yani unachopanga wewe ujue kwangu kimeshafikiriwa muda sana, kwahiyo wewe unataka kumfukuza Anna hapa ili ulete hawara yako aje kunisaidia kazi! Hapana hilo halikubaliki”
“Kheee Mariam umekuwaje? Kumbuka ni wewe ndiye uliyekuwa unasema kuwa siwezi kukusaliti”
“Nilisema ndio ila wanaume hamuaminiki kabisa”
“Imekuwaje nisiaminike tena? Ni kipi kimebadilika kwangu Mariam? Mimi ni Juma yule yule wa siku zote, nimebadilika nini sasa?”
Mariam hakumjibu mumewe bali alijigeuza na kulala huku akilalamika kuwa amechoka kama kawaida yake.
Kulipokucha tu Juma alijiandaa vizuri kabisa na hata kunywa chai hakunywa wala nini kwani moja kwa moja alienda tena kwa yule mganga wake kwani alihisi kuwa huenda safari hii akamsaidia.
Basi alivyofika na kuingia, yule mgaga akacheka na kumwambia Juma,
“Nilijua tu itashindikana maana pale kwako pamekuwa pazito sana”
“Sasa nifanyeje babu?”
“Weka kwanza salamu ya wazee”
Basi Juma aliweka pesa na kuendelea kumsikiliza yule babu tu.
Basi babu alitoa dawa ambayo ilikuwa kama maji halafu akamwambia Juma,
“Hii dawa, nenda kaweke kwenye jagi la maji ya kunywa, weka yote halafu acha mkeo na huyo mdada wa kazi wanywe, halafu utapata jibu ya hiko unachotaka kufahamu. Najua hii utafanikiwa”
“Nitafanikiw ababu, naona kabisa nitafanukiwa, asante sana babu”
Juma alimshukuru sana na kuondoka zake, yani hakutaka hata kwenda tena kwenye shughuli zake kwani kwa muda huo moja kwa moja alirudi nyumbani kwake kwani yeye alikuwa na hamu sana ya mkewe kugundua kuwa Anna ni mchawi, alitamani sana mkewe ajue kuwa anachoka kwaajili ya Anna.
Juma alifika kwake na kukuta ndio Anna anaandaa chakula mzani, wakati huo Mariam amekaa kwenye kochi tu yani Juma aliona ndio wakati sahihi kabisa ule.
Basi alienda jikoni na kuchukua jagi la maji na kujaza, kisha akaweka ile dawa yote na kupeleka mezani huku akisema,
“Anna umeandaa chakula bila hata kuweka maji!”
“Ningeweka shemeji, ila nilienda kwanza kuchukua maji ya kunawa, ila umenisaidia shemeji asante”
Juma alitabasamu tu, basi Anna alimfata Mariam na kumwambia,
“Dada jamani yani umekaa tu wakati mumeo ndio yupo kuandaa maji ya kunywa, hukumuona dada?”
“Aaaah Anna, haya maisha ya mimi na mume wangu yaache tu kama yalivyo, kwani hajui kama mimi nachoka sana? Anajua vizuri, asikuumize kichwa”
Basi sasa Mariam alisogea mezani na kumsalimia mumewe ambapo Juma alimwambia Mariam,
“Mke wangu si unywe maji kwanza halafu ndio ule!!”
“Weeee mambo ya wapi hayo? Ninywe maji kwanza halafu nishibe maji tu niache kula chakula! Mimi nakula kwanza halafu maji badae”
Juma akamuangalia Anna na kumwambia pia,
“Na wewe Anna si unywe maji kwanza ndio ule chakula!”
“Na mimi kama dada, hata sijazoea kunywa maji kabla ya chakula shemeji”
Basi wote wakapakua kile chakula na kuanza kula, yani Juma alikuwa anatamani sana wanywe maji maana pale wakinywa maji tu ndio kila kitu kitagundulika.
Wakiwa wanaendelea kula, mara waliona tu lile jagi likisukumwa na kuangushwa chini ambapo lilimwaga maji yote, hapo Mariam alishangaa,
“Khaaaa jamani, wewe mtoto kuanza kutembea ndio unapanda hadi mezani, sasa kutupa jagi ndio nini?”
Juma aliangalia na kusikitika sana, hadi alijikuta akikosa hamu ya kula kabisa kwani hakuongea kitu zaidi ya kuacha kula na kuondoka zake.
Anna alimuangalia na kumuuliza Mariam,
“Dada, mbona shemeji ameacha chakula?”
“Sijui, labda ameshiba”
“kamuulize dada?”
“Huwa sina muda huo, mtu mzima halazimishwi kula. Akiwa na njaa atakuja mwenyewe kula, yani mimi niache kushiba nianze kuulizana na watu kwanini umeacha chakula, kama amekula huko alipokuwa nitajuaje?”
“Labda kachukia mtoto kuangusha jagi dada?”
“Yani kuangusha jagi tu ndio achukie, lingekuwa limevunjika je si angejinyonga kabisa? Aniondolee balaa mie”
Kisha Anna alienda kuleta maji mengine ambapo walikula na kumaliza pale na walikuwa wameshiba kabisa.
Juma hakutoka tena chumbani, alijikuta akitafakari sana bila ya jibu lolote yani alikuwa kama haamini chochote kile ambacho kinatokea katika ile familia yao.
Muda huu Mariam alienda chumbani na kumkuta mumewe kajiinamia tu na mawazo akamuuliza,
“Wewe vipi una matatizo gani?”
“Kwakweli Mariam, naomba tumfukuze Anna, mimi siwezi kuishi na Anna humu ndani”
“Sababu kubwa ya kumfukuza Anna ni nini?”
“Anna ni mchawi mke wangu, yule binti ni mchawi kabisa nakwambia”
“Hivi Juma uchawi unaujua wewe? Ukiambiwa toa ushahidi kwa hoja yako kuwa Anna ni mchawi utatoa ushahidi gani?”
“Sina haja ya ushahidi ila Anna ni mchawi, tena ni mchawi sana, nataka aondoke kwenye nyumba yangu”
“Sikia nikwambie Juma, siku ya kuondoka Anna hapa ujue ni siku hiyo hiyo na mimi nitaondoka, siwezi kuangalia ukitaka kumnyanyasa mtu asiyekuwa na hatia sababu tu ya mawazo na hisia zako, muache Anna Kama alivyo”
Kwakweli Juma alichukia sana hata hakujua imekuwaje hadi akili za mke wake kutekwa kiasi kile na Anna.
Siku ya leo ndio Juma alienda tena kwenye shughuli zake ila alikuwa na hasira sana kiasi kwamba alikuwa akitembea huku akiongea peke yake maana alikuwa amejaza hasira kubwa sana kwenye moyo wake.
Basi Juma alifanya shughuli zake huku akiwa na mawazo sana kwa siku ya leo, alipomaliza akaondoka ila njiani alikutana na yule binti ambaye huwa wanakutana mara kwa mara,
“Niambie baba Mishi”
“Hivi mara ngapi nikukatalie kumuita mwanangu jina hilo?”
“Haya yameisha, vipi ulifanikiwa?”
“Nifanikiwe wapi? Sikuweza kumbamba wala nini”
“Ila ngoja nikuulize!”
“Niulize tu”
“Hivi wewe hufurahii kula chakula anachopika mke wako? Hufurahii kuona kazi za nyumbani kwenu zikifanywa na mkeo?”
“Na wewe acha kunichanganya, sasa ningekuwa nafurahia ni kwanini tulitafuta msaidizi? Sipendi mke wangu achoke, ona hata unyumba sipati maana kila siku amechoka”
“Ngoja nikuulize tena, toka mkeo ajifungue umeshawahi kupata unyumba?”
“Sijwahi sababu ya mtoto”
“Kwahiyo saivi ni mdada wa kazi amekuwa kikwazo, ngoja nitakusaidia ila kwanini hakunitafuta nikusaidie?”
“Ningekutafutaje? Sijui unapopatikana”
“Ngoja tukikutana safari ijayo nitakwambia jinsi ya kunipata mimi”
Kisha yule mtu alisogea na kuchuma majani Fulani kisha akamwambia Juma,
“Haya majani, ukifika kwako yatwange halafu ukimaliza kuyatwanga jipake wewe na mkeo nataka muone kila kitu ambacho Anna huwa anafanya kwenye nyumba yenu ila mkiona msimfanye chochote kibaya Anna, kama kumfukuza basi mumfukuze kwa utaratibu tu hata msimfanye chochote kibaya”
“Sawa nashukuru sana nimekuelewa, kwahiyo haya majani ni uhakika nitambamba yule mchawi?”
“Ndio, haya majani ni uhakika, yanakufanya uone kila kitu ambapo yeye hatojua kama mnaona kila kitu”
“Asante sana”
Yani Juma alimshukuru sana huyu mdada na kumuaga kwa muda huu ambapo yeye moja kwa moja alirudi nyumbani kwake.
Juma alipofika kwake, alienda kuwasalimia tu ndani kisha akweka vizuri mzigo aliofika nao pale, na baada ya hapo sasa akatoka nje.
Alichukua kinu kidogo na kuanza kuyaponda yale majani, ila muda kidogo mtoto wake alifika pale alipokuwa anaponda halafu akamuuliza Juma,
“Baba, kwanini unapenda uvivu wa mama?”
Itaendelea….!!!
Kwa mawasiliano 0629980412 likes zikifika 300 na share 100 naweka kingine chap chap