SEHEMU YA 26
"huyu mshenzi ananipigia simu wakati yupo na jianaume hapo yaani naumia mimi...naumia jamani nyie niacheni" alizungumza kama anahadithia watu huku akiitizama ile simu.
"hellow mpenzi umelala? Nini mbona simu imeita sana" upande wa pili sauti ya Noela ilimuuliza Timoth.
"hapana nilikuwa naoga,mimi mzima namshukuru Mungu kwa ulinzi wake,nyie huko wazima?"
"sisi wazima sana tu japo Oscar aliugua kidogo mafua"
"ooh! Mpe pole,nitamletea dawa nzuri za kienyeji kutoka Mwanza,bado siku nne nimalize hizo wiki tatu huku"
"karibu sana mume wangu nimekumis sana"
"nimekumis pia mpenzi wangu,usiku mwema mamaa"
"na wewe pia babaa" alimalizia Noela kisha akakata simu.
"mh! Amesema bado siku nne arudi,tumalizie malizie kwa usongo lakini salama " Noela alimwambia Oscar aliyekuwa kifuani pake akimchezea chezea anavyotaka.
"dah! Siku nne chache jamani sasa inabidi dozi iwe alfajiri,asubuhi,mchana,adhuhuri,jioni na usiku eti eeh!" alijibu Oscar kwa kibesi.
***
Kama vile watoto wake wa kuwazaa mama mchungaji alifika na kuwafinyangafinyanga wawili hawa waliokuwa wanapigana
"Mtanieleza leo,mkipenda hapa hapa hadharani na mkiamua mwaweza kufanya hivyo majumbani kwenu" mama mchungaji aliwaambia wawili hao wakati huo mtandio ulikuwa umeanguka tena na kubaki wazi kichwani na usoni.