Simulizi: Harakati za Jason Sizya

fungate.jpeg

136

Kisha kikapita kitambo kifupi cha ukimya mle ndani huku kila mmoja akionekana kuzama kwenye tafakuri yake. Macho ya Olivia yalikuwa yananitazama kiwiziwizi na mdomo wake ulikuwa unanisubiri huku akili yake ikiwa mbali, mkono wake mmoja ulikuwa shingoni. Sikujua tafsiri halisi ya hali hiyo na hivyo kujikuta nikiwa njia panda.

“Samahani Jason, sikuwa nimekujulisha mapema kuhusu hiki kilichonifanya nije nyumbani kwako saa hizi, lakini naamini utanisamehe na kukubali ombi langu,” hatimaye Olivia alivunja ukimya, kisha akaongeza, “Naomba kama una nafasi unisindikize sehemu. Sikuwa nimepanga kwenda na wewe lakini nimegundua kuwa wewe kwa sasa umekuwa mtu muhimu sana kwangu.”

“Unataka nikusindikize wapi?” nilimuuliza Olivia huku moyoni mwangu nikihisi kuwa na furaha ya aina yake.

“Kuna sehemu nataka twende… nina kikao cha kibiashara na wawakilishi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) leo saa 8:00 mchana, kwa ajili ya ile project yangu. Nakwenda kufanya presentation,” Olivia alisema huku akitabasamu.

“Dah, sasa mbona umenishtukiza? Ungeniambia mapema ili nijiandae,” nilisema huku nikishusha pumzi.

“Mapema ipi na wakati tumekutana jana tu na kikao hiki kilishapangwa wiki mbili zilizopita? Wazo la kukushirkisha nimelipata usiku nikiwa kitandani, nisamehe kwa hilo,” Olivia alisema huku akionekana kukata tamaa.

“Kwa hiyo unataka nijiandae sasa hivi twende?” nilimuuliza kwa shauku huku nikiinua mkono wangu wa kushoto kutazama saa yangu.

“Ndiyo, kama hautojali,” Olivia alisema huku akiendelea kutabasamu.

“Usihofu, nina nafasi ya kutosha, nipe dakika chache tu nijimwagie maji chapchap,” nilimwambia huku nikiinuka na kuelekea chumbani.

Ilinichukua dakika kumi na tano tu kujiandaa na kuvaa suti niliyoamini ingeendana kwa kiasi kikubwa na suti ya Olivia. Ilikuwa suti nzuri ya rangi ya samawati brandi ya Dunhill, shati zuri la rangi ya maruni la kitambaa brandi ya Barba, tai shingoni ya rangi ya bluu na viatu ghali vya ngozi halisi kutoka nchini Switzerland vya rangi ya maruni. Kisha nikajipulizia manukato ya gharama kubwa aina ya Clive na kukamilisha utanashati wangu ulionipa mwonekano wa kijanja.

Nilirudi pale sebuleni nikitembea kwa madaha, nikamkuta Olivia akiwa amesimama akiitazama kwa umakini picha kubwa ya Rehema. Alipogundua kuwa nimerudi aligeuza shingo yake kuniangalia kisha akaachia mshangao. Ukweli nilikuwa nimependeza sana, maana ukiambatana na mrembo kama huyo kwenda sehemu inakubidi uwe umetoka ‘chicha’ ili mwendane.

Wow! You look so handsome,” Olivia aliniambia huku akiachia tabasamu kisha akageuza shingo yake kuitazama ile picha ya Rehema pale ukutani.

“Huyu ukutani ndiye Rehema?” Olivia aliniuliza huku akielekeza kidole chake cha shahada kwenye picha ya Rehema. Niliitazama ile picha kana kwamba nilikuwa naiona kwa mara ya kwanza kisha nikabetua kichwa changu kukubali.

“Wala hukusema uongo, ni kweli tunafanana sana!” Olivia alisema huku akianza kupiga hatua taratibu akianza kutoka nje.

Niliweka vizuri vitu vyangu pale sebuleni kisha nikamfuata Olivia kule nje na kumkuta akiwa tayari amepanda ndani ya gari lake na kuliwasha kisha akakanyaga pedeli ya mafuta na kuusikilizia mvumo wa taratibu wa gari. Nilipanda ndani ya gari na kufunga mkanda.

Baada ya gari kuunguruma kwa dakika chache Olivia akatumbukiza gia ya kurudi nyuma na kukanyaga pedeli ya mafuta huku akinyonga usukani, na hapo gari likaanza kurudi kinyumenyume likipita katikati ya ile barabara nzuri iliyotengenezwa kwa vitofali vidogo vilivyovutia kisha akaligeuza.

Gari lilipokaa sawa nami nikabonyeza kitufe cha OPEN kwenye remote ya kufungulia geti na hapo geti likaanza kufunguka taratibu, gari likasogea hadi kwenye geti na tulipotoka lile geti likajifunga lenyewe taratibu.

Olivia aliliondoa gari na kuingia barabarani kisha alikata kushoto na kuingia katika barabara nyingine na hapo akaongeza mwendo hadi tulipofika katika eneo la Nyihogo akakata na kuingia upande wa kushoto akiifuata barabara kuu ya lami inayoelekea katika nchi za Rwanda, Uganda na Burundi.

Kwa muda huo barabara hiyo ilikuwa na magari mengi hasa malori ya mizigo yaliyoelekea nchi jirani na hivyo Olivia alilazimika kuikwepa foleni ile ndefu ya magari katika barabara ile na kuingia barabara iliyoelekea Uhindini.

Hapo aliongeza mwendo japo barabara ile ilikuwa inapitwa na magari mengi lakini hayakusababisha msongamano, na baada ya kitambo fulani cha safari tulijikuta tumefika kwenye makutano ya barabara nyingine za mtaani na Olivia alikata tena na kuingia upande wa kushoto kama aliyekuwa akiifuata barabara ya kuelekea Zongomera kisha tukaingia tena upande wa kulia kuifuata barabara iliyokwenda kutokea katika stendi ya mabasi ya Kahama.

Baada ya mwendo fulani tulianza kupita katika eneo la stendi ya mabasi ya Kahama upande wetu wa kulia, na upande wa kushoto tuliyapita majengo ya benki ya NMB, jengo la Kampuni ya Simu na benki ya CRDB na hapo tukaingia kushoto kuifuata barabara iliyoelekea ofisi za Halmashauri ya Manispaa ya Kahama. Baada ya mwendo mfupi tukaanza kuyapita majengo ya Hospitali ya Wilaya, kisha Parish ya Kanisa Katoliki, na baadaye Ofisi za Manispaa na hatimaye tuliyafikia majengo ya Chuo cha Maendeleo ya Wananchi cha Mwanva na kisha tukaenda kuungana na barabara kuu ya kuelekea nchi za Rwanda, Uganda na Burundi.

Muda wote nilikuwa nimetulia kimya nikimtazama Olivia kwa chati huku nikiwa sijui tunaelekea wapi. Mwanzoni nilidhani kuwa huenda tulikuwa tunaenda Hotel Latitude lakini sasa nilitambua kuwa si huko. Niliona kabisa Olivia akiendesha kuelekea sehemu nyingine kabisa. Nje ya mji wa Kahama, nikashangaa!

Aliendelea kuendesha na kuingia upande wa kulia sehemu ambayo hakukuwa na makazi mengi ya watu, kulikuwa na nyumba chache zikiwa mbalimbali sana, na baada ya dakika chache tukawa tumefika kwenye jengo moja jipya la ghorofa tano. Hadi hapo tulikuwa tumetumia takriban dakika 35 kutoka nyumbani kwangu eneo la Mwime.

Nje ya lile jengo kulikuwa na milingoti kadhaa yenye bendera za nchi mbalimbali kama Tanzania, Kenya, Uingereza, India, Afrika Kusini na China zilizokuwa zinapepea taratibu.

* * *

Endelea...
 
fungate.jpeg

137

Hofu


Saa 7:45 mchana…

OLIVIA aliliegesha gari lake katika viunga vya maegesho ya magari vya lile jengo jipya ambalo nilipolitazama vizuri niligundua kuwa ni jengo la Krystal Park Hotel lililojengwa kwa ufanisi wa hali ya juu. Eneo la mbele la maegesho ya magari ya lile jengo kulipandwa miti mirefu ya kivuli aina ya Quercus virginiana katikati ya bustani nzuri ya maua baina ya sehemu moja ya maegesho ya magari na sehemu nyingine.

Nyakati za usiku taa hafifu za ardhini zilikuwa zinawaka na kumulika eneo lile na hivyo kulifanya eneo lote lipendeze. Katika maegesho yale kulikuwa na magari kadhaa ya kifahari na basi dogo la hoteli kwa ajili ya kubeba wafanyakazi.

Olivia alishusha pumzi na kuchukua simu yake ya mkononi toka kwenye pochi yake ndogo, akatafuta namba na kuipiga kisha akaiweka sikioni kusikiliza wakati ikiita, haikuchukua muda ikapokewa.

“Tumeshafika hapa Krystal Park, uko upande gani?” aliongea kwa sauti tulivu kisha akasikiliza kidogo na kubetua kichwa chake. “Okay, tunaingia sasa hivi.”

Aliposema hivyo akakata simu yake na kuirudisha kwenye pochi kisha akageuza shingo yake kunitazama na kuachia tabasamu pana huku akifungua mlango wa gari na kushuka.

“Tumefika,” aliniambia baada ya kuniona nikiwa bado nimeketi kwa utulivu nikiwa sijui nifanye nini.

Nilishuka na kumfuata, tukaanza kukatisha kwenye viunga vile vya maegesho ya magari taratibu na kuelekea mbele ya lile jengo kulipokuwa na mlango mkubwa wa kioo na varanda pana yenye ngazi iliyofunikwa kwa kofia nzuri ya zege. Katika eneo lile la chini ya lile jengo kulikuwa na supermarket moja kubwa na duka moja la kubadilishia fedha za kigeni.

Tulikaribishwa na vijana wawili wahudumu wa ile hoteli waliokuwa wamesimama kando ya ule mlango wa kuingilia kwa ndani. Vijana wale walikuwa wamevaa sare za kazi, suruali za rangi nyeusi, mashati meupe yenye kola za rangi ya bluu bahari na makoti ya suti ya rangi ya bluu.

“Habari za kazi?” Olivia aliwasalimia wale vijana huku akiwatazama kwa tabasamu.

“Salama dada, karibuni Krystal Park,” wale vijana walimjibu Olivia kwa bashasha zote za kirafiki huku wakiendelea kutabasamu. Muda huo ule mlango mkubwa wa kioo ulikuwa unajifungua wenyewe taratibu mara tu tulipoukaribia, tukaingia ndani na kulakiwa kwa bashasha zote na wahudumu wa ile hoteli ambao pia walivaa suruali nyeusi, mashati meupe yenye kola za rangi ya bluu bahari na makoti ya suti ya rangi ya bluu, sura zao zilikuwa zimepambwa na tabasamu la kirafiki muda wote.

Tuliwasalimia kisha tukapita moja kwa moja tukiuvuka ule ukumbi wa mapokezi na kuelekea upande wa kushoto na kufika kwenye ukumbi wa mgahawa wa Utulivu Grill ambao ulikuwa kwa ajili ya chakula cha Kitanzania na cha kimataifa. Eneo lote lilikuwa na hewa safi iliyosambazwa taratibu na viyoyozi na sakafu ilikuwa na tarazo maridadi zilizokuwa na nakshi za kupendeza.

Tuliuvuka ule mgahawa uliokuwa na meza nyingi za kulia chakula zenye umbo mstatili zilizozungukwa kwa viti nadhifu vyenye foronya laini.

Meza zile zilikuwa zikimefunikwa kwa vitambaa visafi vya rangi nyeupe na juu yake kuliwekwa kadi ngumu za kupendeza zenye orodha ya vyakula na vinywaji vinavyopatika katika hoteli ile. Pia kulikuwa na karatasi laini nyeupe za tishu za kufutia mikono na vifaa vyote muhimu vya kujipatia maakuli kama uma, visu na vijiko, na bila kusahau vikasha vya chumvi ya mezani na vimbaka vya kuchokolea meno.

Pembeni ya meza zile kulikuwa na makochi mazuri ya sofa yaliyopangwa kuzizunguka meza fupi za vioo katika mpangilio mmoja uliovutia na mwisho wa ukumbi ule kulikuwa na kaunta kubwa ya vinywaji.

Madirisha makubwa ya vioo ya ukumbi ule yalikuwa yamefunikwa kwa mapazia marefu na ukutani kulikuwa na runinga bapa zilizokuwa zinarusha vipindi mbalimbali vya burudani.

Ndani ya ule ukumbi kulikuwa na watu wachache walioketi wakijipatia mlo na vinywaji huku wakiendelea na maongezi yao. Watu hao walitukodolea macho wakati tukipita, kwa namna tulivyokuwa tumependeza. Yeyote aliyetuona angeweza kufikiri kwamba tulikuwa wapenzi, tena tuliopendana mno. Kwa mara ya kwanza tangu ule mkasa wa Rehema nilijikuta nafarijika mno, nilijiona kuwa mwanamume ambaye thamani yangu ilikuwa imerudi.

Ukumbi ule haukuwa mkubwa na ulikuwa umetenganishwa na ile sehemu ya mapokezi kwa ukuta mdogo uliokuwa unamruhusu mtu yeyote kuweza kuona mle ndani bila usumbufu wowote.

Tulipovuka eneo lile tukatokea katika ukumbi mwingine wa burudani uliokuwa unatazama eneo kubwa lenye bustani nzuri yenye miti mbalimbali na bwawa la kuogelea na hivyo kutengeneza mgawanyo mzuri wa starehe tofauti zenye utulivu zinazoweza kufanyika kwa wakati mmoja. Katika eneo lile kulikuwa na watu wachache hasa Wazungu waliokuwa wanaendelea na maongezi yao ya kibiashara katika viti vizuri na meza fupi za mbao huku wakijipatia vinywaji.

Tulisimama kidogo eneo lile huku Olivia akionekana kutafuta kitu mara nikamwona mwanamume mmoja mrefu mwenye mwili wa kimazoezi na rangi ya ngozi yake ilikuwa ni maji ya kunde akiwa ameketi kwenye kiti kimoja pembeni kabisa akiwa na tarakilishi mpakato. Sura yake ilikuwa ya tabasamu na macho yake yalikuwa makali kama ya kachero mbobezi.

Yule mwanamume alimuona Olivia na kupunga mkono, tukamfuata na kusalimiana naye, kisha Olivia akanitambulisha kuwa yule mwanamume alikuwa anaitwa Fadhil Mbezi, mwanasheria wa kampuni yake. Baada ya hapo akamwambia Fadhil kuwa mimi ndiye yule mwanamume ambaye walikuwa wameongea na nilitakiwa kuungana nao kwenye kikao hicho muhimu. Fadhili alinitupia jicho na kubetua kichwa chake huku akiachia tabasamu. Nilibaki njia panda kwa sababu sikujua Olivia alikuwa amemwambia nini Fadhil kuhusu mimi.

Muda huo huo nikamwona mhudumu mmoja wa kike akitufuata pale tulipokuwa na kutusalimia kwa adabu kubwa na kwa bashasha zote. Kisha akaongea jambo na Olivia kwa sauti ya chini huku akiachia tabasamu. Kwa mtazamo wa haraka haraka ilionekana kuwa wawili hao walikuwa wanafahamiana.

Kisha yule mhudumu alituashiria tumfuate huku yeye akitangulia mbele, tukaelekea sehemu kulipokuwa na vyumba vya lifti za lile jengo la hoteli za kuelekea juu. Tulipofika kwenye zile lifti yule dada mhudumu alibonyeza kitufe fulani ukutani na mlango wa ile lifti ukafunguka kisha tukaingia ndani ya lifti, na akabonyeza kitufe cha namba akiiamuru lifti itufikishe kwenye ghorofa ya tano ya lile jengo.

Mlango ulipojifunga ile lifti ilianza kupanda juu hadi ilipofika katika ghorofa ya tano ya lile jengo, ikagota na mlango wa kile chumba cha lifti ukafunguka kuturuhusu tutoke. Tulitokea kwenye ukumbi mpana uliomezwa na utulivu wa aina yake ukipakana na milango mitatu, mmoja ukiwa upande wa kushoto na miwili upande wa kulia.

Katikati ya ule ukumbi kulikuwa na kitufe kikubwa chekundu cha kengele ya hatari kikiwa pembeni ya mtungi mkubwa wa gesi ya kuzimia moto wa dharura. Juu ya dari ya ukumbi ule kulikuwa na taa ndefu za mtindo wa kupendeza zilizoangaza mwanga wa wastani na hivyo kuyafanya mandhari ya ule ukumbi yawe tulivu na ya kupendeza.

Tuliufuata mlango mmoja uliokuwa na maandishi ya “Conference Room”, mlango huo ulikuwa umejitenga na ile mingine. Yule mhudumu aliusukuma taratibu ule mlango na kuturuhusu kuingia, tukajikuta tukitokea ndani ya ukumbi mdogo wa kisasa wa mikutano wenye uwezo wa kuchukua watu ishirini.

Ulikuwa ni ukumbi wenye kila aina ya kionjo cha daraja la kimataifa ukiwa na viyoyozi na madirisha makubwa ya vioo yaliyofunikwa na mapazia safi marefu yaliyosogezwa kando kidogo kuruhusu mwanga wa jua kupenya kwa urahisi kutoka nje na kuangaza mle ndani.

Ulikuwa na meza ndefu ya mbao za mti wa mninga iliyozungukwa na viti kumi na sita vyenye foronya laini vilivyopangwa katika mpangilio uliovutia. Meza hiyo ilitengenezwa kwa namna ya kipekee na ilikuwa na kioo katika eneo la katikati na pembeni kukiwa na spika maalumu za kuongelea. Ukutani kulikuwa na runinga bapa.

Ndani ya ukumbi ule tuliwakuta watu watatu waliokuwa nadhifu sana, wanaume wawili waliokuwa wamevalia suti nzuri na mwanamke mmoja aliyekuwa amevaa gauni zuri la kitenge walikuwa wameketi kwa utulivu kwenye viti vyao huku wakionekana kusubiri kwa hamu, na nilitambua kuwa ni sisi ndio tuliokuwa tukisubiriwa kwani baada ya kuingia tu wote walisimama na kutulaki kwa bashasha.

Nilijikuta nikishikwa na hofu ya ghafla na miguu yangu ilikuwa inagongana wakati tukiwasogelea, sikuelewa hofu ile ilikuwa imetoka wapi! Olivia aligundua jambo hilo na kunisogelea kisha akaninong’oneza sikioni, “Don’t be nervous…”

Nilitabasamu huku nikisalimiana na wale watu tuliowakuta ndani ya ule ukumbi ambao baadaye niliwatambua kuwa ndio wawakilishi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika alionieleza Olivia kabla, na baada ya salamu wote tuliketi kwenye viti. Mimi, Olivia na Fadhili tukiketi upande mmoja na wale watu tuliowakuta waliketi upande mwingine wa ile meza, kisha utambulisho ukaanza.

Nilishtuka sana na hofu kunitambaa mwilini huku mapigo ya moyo wangu yakibadili mwendo na kwenda kasi baada ya Olivia kunitambulisha kama mshirika wake wa kibiashara. Nilihisi kijasho chepesi kikinitoka mwilini licha ya kwamba mle ukumbini kulikuwa na kiyoyozi kikubwa kilichokuwa kinasambaza hewa safi yenye ubaridi mkali.

Baada ya utambulisho wa pande zote mbili kikao cha kibiashara kati yetu na wale wawakilishi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika kikachukua nafasi. Kilikuwa kikao kizito…

* * *

Endelea...
 
fungate.jpeg

138

Una furaha?


Saa 8:35 mchana.

SIKUWA nimetegemea kitu kama kile kutokea katika kipindi hicho. Tangu nikuitane na Olivia mambo makubwa yalikuwa yanatokea kwa haraka sana kwenye maisha yangu. Niliona ni kama ndoto. Kikao kile kilikuwa kimenijengea heshima kubwa mno kwa wale wawakilishi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika, heshima ambayo sikuwa nimetarajia kuipata. Kwa kweli Olivia alikuwa ameniheshimisha mno mbele ya wale watu.

You did great… sikutegemea kabisa kama ungeweza kuwa msaada mkubwa kwenye kikao cha leo. Jason you are amazing!” Olivia alininong’oneza sikioni wakati tukiinuka toka kwenye viti vyetu baada ya kikao cha kibiashara kati yetu na wawakilishi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika kumalizika.

Sikujibu kitu bali niliachia tabasamu tu, kisha nilitoa kitambaa na kujifuta jasho jepesi lililokuwa likinitoka usoni licha ya hewa safi yenye ubaridi mkali iliyosambazwa mle ukumbini na kiyoyozi kikubwa. Mambo yaliyokuwa yametokea mle ukumbini yalikuwa kama ndoto kwangu. Sikuwa nimetarajia kabisa kuwa mambo yangekwenda kama vile.

Nisingeweza hata kuelezea ni jinsi gani nilivyokuwa nimefurahi moyoni kukutana na wawakilishi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika jambo lililokuwa limeniongezea mtandao wa marafiki.

Wale wawakilishi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika walinifuata na kunipa mkono wa pongezi kwa jinsi nilivyoonekana kujua mambo mengi kwa kuwa nilikuwa na taarifa nyingi kutokana na utaalamu wangu adimu wa kukaa nyuma ya tarakilishi na kubofya kicharazio ili kuifanya dunia kuwa sawa na kijiji. Huo ulikuwa mchana wa kipekee sana kwangu. Nilifurahia sana kwa namna ambayo Olivia alivyonifanya niyasahau masaibu yote yaliyokuwa yamenikumba. Kila nilipomtazama Olivia usoni nilishindwa kuamini kama ni yeye kweli ndiye aliyeweza kunifanya nikawa na furaha kubwa namna ile!

“Nina furaha ya ajabu sana leo Jason. Umenifanya nione kuwa sikuwa nimekosea kukuamini na kukushirikisha kwenye mipango yangu kwa jinsi ulivyoonesha kuwa una akili nyingi na uwezo mkubwa wa kupambanua mambo magumu,” Olivia alinong’ona tena huku akishindwa kuificha furaha yake.

Kisha Olivia aliwaalika wale wawakilishi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika ukumbi wa chakula kwa ajili ya chakula cha mchana huku alinishika mkono, tukaanza kutoka nje ya ule ukumbi na kuelekea kwenye vyumba vya lifti za kushuka chini.

“Hata hivyo, naomba nichukue nafasi hii kukuomba sana samahani kwa kukushtukiza kuhusu jambo hili,” Olivia alisema huku akinitazama usoni.

“Usijali, Olivia… cha msingi ni kwamba kila kitu kimekwenda sawa,” nilisema katika namna ya kumtoa shaka. Wakati huo tulikuwa tumefika kwenye lifti na Olivia alibonyeza kitufe cha kuita lifti ili itupeleke chini, na mara mlango wa chumba cha lifti ukafungua na kuturuhusu kujitoma ndani.

“Najua utasema nisijali lakini nilikushirikisha kwenye mazungumzo ya kibiashara pasipo kwanza kukueleza kinagaubaga kuhusu mchakato wenyewe ulivyo. Haukuwa umejiandaa…”

“Nimekwambia usijali kwa yote,” nilimkatisha Olivia kabla hajamaliza sentensi yake. “Uliponiomba niambatane nawe kwenye kikao kati yako na wawakilishi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika nilikwisha jiandaa kisaikolojia. Na kuhusu kunishtukiza, yeah… I was a bit nervous lakini kuwa karibu nawe ilinipa ujasiri mkubwa hata nikaweza kutoa mchango wangu kwa kadiri nilivyoweza,” nilisema kwa msisitizo na kumfanya Olivia atabasamu.

Olivia alinitazama usoni kwa sekunde kadhaa kisha akasema, “Jason, you are amazing. Nilifanya makusudi kukuomba uje kushiriki kikao hiki lengo langu lilikuwa kuona kama nimepata rafiki mwerevu na mwenye kufahamu mambo mengi. Though you were nervous but what you did was wonderful…” Olivia alisema huku akinishika mkono, tukatoka nje ya kile chumba cha lifti baada ya kufika chini.

Kisha tuliongozana kuelekea kwenye ukumbi wa mgahawa wa Utulivu Grill ambao ulikuwa kwa ajili ya chakula cha Kitanzania na cha kimataifa. Niligundua kuwa ulikuwa mgahawa mzuri wa kisasa wenye huduma zote muhimu kama aina ya vyakula mbalimbali vya watu wa mataifa tofauti na utulivu wa kutosha.

Hatimaye tukatafuta meza moja iliyojitenga kwenye kona moja ya mgahawa ule na kuketi huku tukijitenga na watu wengine. Sehemu ile tuliyoketi ilituwezesha kuongea mengi ya kibinafsi yaliyotuhusu pasipo wasiwasi wowote. Mhudumu mmoja wa mgahawa ule alifika haraka kutusikiliza nikamwagiza wali kuku, maharage na saladi nyingi ya mboga za majani. Olivia yeye aliagiza biriani ya kuku na saladi ya mboga za majani.

Vyakula vile vilipoletwa na mhudumu tukaanza kuvishambulia huku kila mmoja akionekana kuwa na njaa, na wakati tukielekea kumaliza chakula Olivia alianzisha tena maongezi huku akishindwa kuificha furaha yake.

“Nimefurahi sana Jason kwa sababu hukuweza kuniangusha. Umeweza kuziteka akili za watu wa ADB. Sijawahi kuwa na furaha kama siku ya leo. Na furaha yote hii imechangiwa na wewe. You really made my day.” Olivia alisema huku akiinua bilauri ya maji na kuyanywa maji yote yote.

Kwa sifa alizokuwa akinipa Olivia nilihisi kama vile dunia yote ilikuwa kwenye himaya yangu, kitu kimoja tu sikuwa na uwezo nacho, uwezo wa kusimamisha muda uliokuwa ukienda kwa kasi ya ajabu. Nilitaka niendelee kuwa na mrembo yule asiyechosha kuwa naye. Nilihisi kuipata furaha ya ajabu ambayo sikuwa nimeipata kwa kitambo tangu ule mkasa ulionifanya kufarakana na Rehema.

“Jason mbona uko kimya sana? Unawaza nini?” Olivia aliniuliza baada ya kuniona nikiwa kimya nikimtazama.

“Nilikuwa nafikiria…” nilisema na kusita kidogo huku nikishusha pumzi za ndani kwa ndani. “Ningependa sasa kusikia the story about your affairs with your handsome ex-boyfriend,” niliongeza na kumfanya Olivia agune mara tu nilipomaliza sentensi yangu.

Ex-boyfriend!” Olivia aliniuliza kisha akaachia kicheko.

Yap! someone you loved, someone whom your heart belonged to him. Na kama uko tayari kumsamehe ili muwe kama zamani!” nilisema huku nikimtazama Olivia kwa tuo.

“Eti kumsamehe!” Olivia alisema na kucheka tena. Sikushangaa kwa sababu toka nilipomfahamu Olivia niligundua kwamba alikuwa anapenda mno kucheka.

“Usinifurahishe Jason, after what I got from him, I don’t think I will ever love again. Kwa sasa ninaishi maisha yangu ya furaha and I have lots of friends and lots to do… so what do I need a man for?” Olivia alisema huku akitingisha kichwa chake taratibu.

Endelea...
 
fungate.jpeg

139

Maneno ya Olivia yalionesha wazi kwamba mwanadada huyo alitendwa kisawasawa kiasi cha kumfanya asitamani tena uhusiano na mwanamume. Ni kweli alikuwa na maisha yake mazuri yaliyojaa furaha na amani hivyo alionesha hakutaka kupata tena matatizo. Kwa upande fulani nilijikuta nikikubaliana na maneno yake japo sikujua ni nini kilichokuwa kimemtokea.

Ukiachana na habari za uhusiano wake wa nyuma, bado sikuelewa huyu Olivia alikuwa na kitu gani hasa, kwani kwa muda mfupi niliokutana naye aliweza kuufuta unyonge wote kichwani kwangu na kunijengea mtazamo mpya.

“Unaweza kuwa na kila kitu, Olivia… unaweza kuwa na fedha, marafiki, kazi na kila kitu… lakini je, una furaha?” nilimuuliza Olivia.

Olivia alijimiminia maji kwenye bilauri yake kisha akayanywa yote na kuiweka chini ile bilauri, alibaki kimya kwa sekunde kadhaa huku akinitumbulia macho.

“Mbona hunijibu?” nilimuuliza Olivia huku nikiwa nimemkazia macho.

“Furaha ipi unayoizungumzia?” Olivia aliniuliza huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani.

“Furaha ya moyo. Najua una vitu vyote unavyovihitaji maishani lakini moyo wako una furaha?” nilimuuliza tena huku nikiwa nimeyatuliza macho yangu kwenye uso wake.

“Ndiyo, nina furaha… simply because kila kitu ninachokitaka nakipata. Kikubwa ni kwamba nipo huru, moyo wangu una amani na nina uhuru wa kufanya chochote nikitakacho. Unadhani kuna furaha zaidi ya hiyo?” Olivia aliniuliza huku akiwa amenikazia macho.

“Nafahamu hilo, lakini hapa nazungumzia ndani ya moyo wako… je, una furaha?” nilimuuliza tena kwa msisitizo.

“Ndiyo, nina furaha moyoni mwangu,” Olivia alijibu huku akiyakwepa macho yangu na kutazama kando. “Please, Jason, can we change the subject.”

Kabla sijasema neno lolote wale wawakilishi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika wakafika pale kwenye meza yetu na kutushukuru kwa chakula kisha wakaomba namba yangu ya simu kwa sababu hawakujua ni wapi wangeweza kuniona tena baada ya kikao hicho.

Nasi hatukukaa sana, tuliinuka tayari kwa kuondoka. Hata hivyo Olivia alipokea ujumbe kuwa Mkurugenzi wa Krystal Park Hotel alitaka kuongea naye, yalikuwa mazungumzo ya kibiashara. Kikao chao kilichukua muda mrefu kisha viongozi fulani wa Manispaa ya Kahama nao waliofika hapo hotelini kuonana naye baada ya kuwasiliana nao kwa simu.

Wakati tukiondoka eneo hilo ilikuwa imetimia saa 10:15 jioni, mpaka tunaingia ndani ya gari letu tayari kwa kuondoka bado walikuwepo watu waliokuwa wanamfuata Olivia ili kutaka mawasiliano yake ikiwemo barua pepe na namba ya simu.

“Pole kwa vikao vizito,” nilimwambia Olivia wakati akiliondoa gari lake taratibu kutoka kwenye viunga vya magari vya hoteli ile.

“Nimeshavizowea. Pole wewe kwa usumbufu niliokusababishia maana leo nimekuharibia ratiba zako,” Olivia alisema huku akinitazama na kuachia tabasamu.

“Wala hujaharibu ratiba zangu zozote, kwani umesahau kuwa siku ya leo niliitenga maalumu kwa ajili yako?” nilimwambia huku nikitabasamu.

“Hata hivyo, nami nikushukuru sana kwa kukutana nawe kwa sabahu umenifanya kwa siku hizi mbili tulizofahamiana niwe mtu mwenye furaha sana na kusahau masaibu yote yaliyonipata,” niliongeza na hapo Olivia alinitupia jicho mara moja na kutabasamu pasipo kusema chochote.

Muda huo Olivia alikuwa anakata kona kuingia katika barabara kuu ya lami inayotoka katika nchi za Rwanda, Uganda na Burundi. Safari ya kurudi mjini ikaanza.

“Nakiri kwamba wewe ni mwanamke wa pekee sana, Olivia… mwanamume atakayekuoa atakuwa na bahati kubwa mno,” niliongeza katika namna ya kumchokoza Olivia ili nisikie angesema nini.

Olivia alicheka sana. “Jason, mbona kila mara unaongelea kuhusu mwanamume. Elewa tu kwamba nayafurahia maisha yangu bila mwanamume…”

“Na hufikirii kuja kuwa na watoto siku moja?” nilimuuliza tena Olivia. Olivia alikaa kimya kwa muda akionekana kufikiria.

“Vipi kuhusu watoto?” nilimuuliza tena na kumfanya ageuze shingo yake kunitazama. Macho yetu yalipogongana Olivia aliyaondosha haraka macho yake na kutazama mbele kwa aibu huku akiachia tabasamu la aibu. Alijitahidi sana kutabasamu lakini uso wake haukuonesha furaha na wala haukuwa na tashwishwi yoyote, alionekana kuwa alikuwa na jambo zito lililokuwa likimtatiza sana moyoni. Alikuwa na huzuni moyoni na niliweza kuiona waziwazi kwenye macho yake ingawa alijitahidi sana kuificha hali ile.

“Nakumbuka jana nilikujibu… ningepeda sana kuwa na watoto wawili…” Olivia alisema na kushusha pumzi za ndani kwa ndani. Nilimtazama usoni kwa kitambo, nilikuwa najaribu kuyasoma mawazo yake.

“Kama ni hivyo unadhani utawapataje hao watoto wawili bila kuwa na mume?” nilizidi kumsaili huku lengo langu likiwa kutaka kufahamu undani wake kuhusu maisha yake ya kimahusiano. Tangu nilipokutana naye alikuwa mgumu sana kunieleza kuhusu maisha yake ya kimapenzi.

“Jason, please let’s talk of something else…” Olivia aliomba tubadilshe maongezi huku akionesha wazi kulikwepa swali langu.

“Olivia, ingawa umekiri kuwa una furaha ya kutosha maishani lakini ukweli ni kwamba huna furaha ya moyo. Kuwa mkweli tu maana hauutendei haki moyo wako… unahitaji upate mwenza aliye sahihi na hivyo kuufanya moyo uwe na furaha…” nilimwambia Olivia.

I know you are a great woman. You deserve to be loved and be happy, unahitaji mtu wa kuikamilisha furaha yako. Usilisahau hilo,” niliongeza baada ya kumwona Olivia akiwa kimya.

“Nashukuru sana kwa ushauri wako, Jason. Nitaufanyia kazi ingawa kwa sasa namwachia Mungu kwani ndiye anayejua hatma ya maisha yangu,” Olivia alisema huku akipunguza mwendo kulipisha lori la mchanga lililokuwa linakuja mbele yetu huku likionesha taa iliyoashiria kuingia upande wetu wa kushoto, kwenye Chuo cha Maendeleo ya Wananchi cha Mwanva.

Kisha kilizuka kitambo kirefu cha ukimya kila mmoja akizama kwenye tafakuri. Sikujua Olivia alikuwa anawaza nini lakini mawazo yangu hayakwenda mbali, nilikuwa namfikiria Olivia. Nilimtafakari sana nikajiambia kuwa huenda ni Mungu aliyekuwa amemleta Olivia kwenye maisha yangu ili awe mbadala wa Rehema. Moyo wangu ulikuwa rahisi mno kumkubali Olivia na kumpa nafasi kubwa ndani ya moyo wangu.

Sikuwa na shaka na moyo wangu kwa kuwa niliamini kuwa safari hii nilikuwa nimenasa kwenye penzi lake na moyo wangu haukunidanganya. Kila nilipomtupia jicho Olivia nilijihisi furaha kubwa, sikuliona tena pengo la Rehema. Nikaapa kuwa kama nilimpoteza Rehema basi safari hii sikutakiwa kufanya makosa ya kumpoteza Olivia. Na hivyo nilipanga nimwambie ukweli wote siku hiyo. Sikuona sababu ya kusubiri kwa sababu tayari tulishakuwa marafiki wakubwa na alionesha kuniamini…

* * *

Endelea...
 
fungate.jpeg

140

Saa 10:45 jioni.

“Mbona uko kimya sana, Jason?” Olivia alinishtua kwa swali lake huku akinitazama kwa umakini.

Niligeuza shingo yangu kumtazama Olivia, na hapo nikamwona akiachia tabasamu pana huku akionekana kuyasoma mawazo yangu.

“Kawaida tu,” nilisema na kushusha pumzi ndefu za ndani kwa ndani.

Olivia aliendelea kunitazama kwa kitambo na kunifanya niyahamishe macho yangu kutoka kwenye uso wake na kutazama nje, na hapo nikagundua kuwa tayari tulifika Hotel Latitude na Olivia alikuwa ameliegesha gari lake kwenye viunga vya maegesho ya magari vya hoteli hiyo.

Hotel Latitude ilikuwa hoteli kubwa yenye mandhari tulivu ya kupendeza na jengo lake lilikuwa limejengwa kwa ufanisi wa hali ya juu. Ilikuwa hotel ya hadhi ya nyota 4 iliyokuwa katika eneo tulivu la Nyahanga mjini Kahama. Hoteli ile ilikuwa na eneo kubwa la mbele la maegesho ya magari lililokuwa limepandwa miti mirefu ya kivuli iliyozungukwa na bustani ya maua ya kupendeza yenye hewa safi ya upepo wa asili baina ya sehemu moja ya maegesho ya magari na sehemu nyingine.

Muda huo kulikuwa na magari machache madogo yaliyokuwa yameegeshwa katika eneo lile.

Niliyatupa macho yangu kutazama upande mwingine wa eneo lile, niliiona bustani ya nyasi laini zilizokatwa vizuri na kupendeza na katika bustani ile kulikuwa na sehemu za kupumzika zenye viti na meza chini ya miamvuli mikubwa yenye rangi za kupendeza.

Olivia aliniomba nimsindikize ndani, sikujivunga, nilifungua mlango na kushuka. Kisha tukaongozana kuelekea ndani ya lile jengo. Pale kwenye mlango mkubwa wa kuingilia tulipishana na mhudumu mmoja aliyetusalimia kwa bashasha zote huku akionesha tabasamu la kirafiki kwenye uso wake. Tuliitikia salamu yake na kumpita huku tukitembea taratibu kupita juu ya zulia nene la rangi nyekundu, tukatokea katika eneo la mapokezi.

Eneo lile la mapokezi lilikuwa pana lenye mazingira yaliyoashiria ustaarabu, na mandhari yake yalikuwa ya kuvutia sana na yalitoa liwazo kwa mgeni yeyote aliyeingia. Kulikuwa na meza nzuri ya kaunta yenye umbo la nusu duara iliyotengenezwa kwa mbao za mninga, na ilikuwa ikitazamana na makochi mawili makubwa ya ngozi laini ya sofa.

Nyuma ya ile meza kubwa ya mapokezi kulikuwa na mhudumu mmoja wa kike aliyekuwa katika sare nadhifu za kazi. Kwa mtazamo wa haraka haraka niligundua kuwa alikuwa msichana mrefu wa wastani, mweupe kwa rangi na mwenye umbo kubwa na zuri la namba nane lililovutia mno lenye kiuno chembamba na hakuwa amezidi miaka ishirini na tano.

Japokuwa alikuwa amevaa sare za kazi lakini bado uzuri wake haukujificha kabisa. Alikuwa na macho mazuri malegevu. Nilijikuta nikivutiwa sana kumtazama yule msichana, nilijiuliza kama niliwahi kumwona mahali kwani sura yake haikuwa ngeni kabisa machoni mwangu.

Yule msichana alipomwona Olivia uso wake ulichanua kwa tabasamu pana lenye bashasha lililovifanya vishimo vidogo mashavuni kwake vichomoze haraka. Kisha macho yake yakahama toka kwa Olivia hadi kwenye uso wangu, macho yetu yalipogongana nikamtambua. Na hapo nikajikuta nikinywea sana kwani sikutegemea kabisa kukutana naye mahali hapo na kwa wakati kama huo.

Hata yeye baada ya kuniona alionesha mshtuko wa wazi. Nadhani hakuwa ametegemea kukutana na mimi katika mazingira yale ingawa nilikuwa na uhakika kuwa alikuwa anafahamu kuwa nilikuwa naishi katika mji wa Kahama. Haraka Zakia aliinamisha uso wake chini kuyakwepa macho yangu na kumfanya Olivia kumshtukia baada ya kumwona alivyobadilika ghafla. Olivia aligeuza shingo yake kunitazama, alikuwa akiniangalia kwa umakini sana, nikayakwepa macho yake huku nikivunga kuyastaajabia mandhari ya eneo lile la mapokezi.

Msichana huyo wa mapokezi aliitwa Zakia, mpenzi wangu wa zamani niliyemtoa usichana wake na kumwingiza kwenye ulimwengu wa mapenzi wakati huo nikiishi katika Manispaa ya Tabora. Nilimfahamu Zakia wakati akiishi kwa wazazi wake eneo la Kiloleni Tabora, jirani na nyumbani kwa mjomba wangu, Japheti Ngelela.

Mapenzi yetu yalidumu muda mfupi kwani aliolewa na mwanamume mmoja aliyeitwa Msabaha Jumanne na kisha walihamia kwenye nyumba niliyokuwa naishi eneo la Ng’ambo. Hata hivyo miezi miwili baadaye uliibuka mzozo mkubwa kuhusu ujauzito wake jambo lililomfanya kunywa sumu na kuponea tundu la sindano huku ujauzito huo ukitoka.

Kwa kweli moyoni nilikuwa nimepatwa na mshtuko mkubwa kwani sikuwa nimetarajia kukutana na Zakia na sikujua kama alikuwa amehamia mjini Kahama ingawa nilisikia kuwa alikuwa ameachana na Msabaha. Hivyo mshtuko ulionipata uliiondoa kabisa amani moyoni mwangu lakini sikuwa na namna nyingine ya kufanya isipokuwa kujikausha kwani sikutaka kuiharibu furaha ya Olivia, msichana aliyeweza kunitoa katika ukiwa kwa muda mfupi tu.

Ni kama alikuwa akiyasoma mawazo yangu, Olivia aliminya midomo yake na kushusha pumzi za ndani kwa ndani kisha alionekana kupuuzia na kunyoosha mkono wake kwa Zakia kuomba ufunguo wa chumba chake. Zakia alichukua ufunguo na kumpa Olivia huku akinitupia jicho la wizi. Macho yake yalionesha kuwa mshtuko ulikuwa bado haujamtoka.

Sikujali, nilimfuata Olivia tukaelekea zilipokuwa ngazi za lile jengo la hoteli za kuelekea juu na kuzikwea hadi chumba namba 23 orofa ya kwanza. Olivia alinikaribisha ndani, sikujivunga nikaingia ndani na kuketi kwenye sofa dogo. Kilikuwa chumba kikubwa cha sebule ya kisasa chenye vitu vyote muhimu ikiwa ni pamoja na seti moja ya runinga bapa aina ya LG, jokofu aina ya LG, simu ya mezani, kiyoyozi, seti ya makochi ya sofa na meza ndogo.

Now, wait me here and I’ll be back in a second,” (Sasa, nisubiri hapa nitarudi baada ya sekunde chache) Olivia aliniambia huku akifungua mlango na kuingia katika chumba cha kulala.

Baada ya kama dakika kadhaa alirudi pale sebuleni akiwa amevaa kaptula nyekundu yenye maua meupe ya kitambaa chepesi iliyoishia sentimeta chache juu ya magoti pamoja na fulana nyekundu iliyoyahifadhi matiti yake yenye mvuto. Kisha alilifungua jokofu na kutoa chupa kubwa ya mvinyo aina ya Dompo na bilauri mbili, akainama kwa utulivu akizipanga juu ya meza mbele yangu, na kitendo kile cha kuinama kidogo mbele yangu kikanifanya niyaone matiti yake yenye mvuto wa kipekee.

Olivia alipogundua kuwa nilikuwa nikiyatazama matiti yake kwa matamanio aliachia tabasamu dogo la aibu huku akiyakwepesha macho yake pembeni yasikutane na yangu kisha akaitengeneza vizuri blauzi yake.

“Nina furaha ya ajabu sana leo, Jason. Kwa mara ya kwanza baada ya miaka mitatu nimeamua ninywe mvinyo… naomba tunywe na tufurahie ushindi,” Olivia alisema na kufungua chupa ya mvinyo kisha akamimina kwenye bilauri na kunipa moja. Kisha aliinua bilauri yake tukagonganisha.

Cheers!” tulisema kwa pamoja na kuanza kunywa. Olivia aliketi kwenye sofa lililokuwa linatazamana na lile nililokalia.

Nilijikuta nikiwa katika wakati mugumu sana kwani muda wote tulipokuwa tunakunywa nilikuwa kimya, nilikuwa natamani niinuke na kumkumbatia Olivia kisha nimporomoshee mabusu motomoto, nilihisi kuwa nilikuwa nalihitaji sana penzi lake, lakini sikuwa na ujasiri huo kwa hofu kuwa ningeonekana nina papara.

Endelea...
 
fungate.jpeg

141

Niliamini kuwa Olivia alikuwa ameigundua hali yangu na muda mwingi alijitahidi sana kunichangamsha kwa kunipigisha stori hizi na zile huku akicheka, baada ya kugundua nilikuwa nimepoteza uchangamfu wangu. Hatimaye nilionekana kufikia mwisho wa subira, nikapiga moyo konde, “Liwalo na liwe leo namwambia,” niliwaza.

Jason, are you ok?” (Jason, uko sawa?) Olivia aliniuliza huku akinitazama kwa udadisi.

Yeah, I’m okay,” nilimjibu Olivia kuwa nipo sasa huku nikiachia tabasamu. Olivia alinitazama kwa umakini na kushusha pumzi za ndani kwa ndani kisha alinyanyua juu mabega yake juu.

“Sasa mbona huongei? Na unaonekana umenywea!” Olivia alisema huku akiendelea kunitazama kwa tuo.

“Nilikuwa nakufikiria… natumaini leo unaweza kuniokoa maana nateketea ndani kwa ndani, Olivia,” nilisema kwa sauti ya unyonge.

“Unateketea! Kivipi?” Olivia alihoji huku akinikazia macho.

Ilinichukua dakika nzima nikiwa kimya bila ya kulijibu swali lake, muda huo nilikuwa natafakari namna ya kulijibu swali hilo, majibu nilikuwa nayo lakini nilihofu juu ya mapokezi ya jibu langu kabla sijalitoa. Sikuweza kujua kwa haraka ni kwa vipi litapokelewa. Hata hivyo nilijikaza na kuamua kwamba lolote na liwe, maji nilishayavulia nguo sikuwa na budi kuyaoga.

“Ni penzi lako Olivia… nakuhitaji sana kwenye maisha yangu na huu ndiyo wakati ambao nalihitaji penzi lako kuliko kitu kingine chochote,” nilisema na kuinuka pasipo hata kufikiria mara mbili kisha nikamsogelea na kuketi kando yake, nikauzungusha mkono wangu na kukishika kiuno chake huku nikihisi msisimko wa ajabu kwa kugusana na mrembo huyo. Kitendo hicho kilimfanya Olivia ashtuke sana na kuanza kuhema kwa nguvu.

What do you want from me?” (Unataka nini kwangu?) Olivia aniuliza kwa sauti laini iliyoonesha wazi kuwa alikuwa anatetemeka.

I just want a wonderful evening with you…” (Nataka hii iwe jioni ya kupendeza nikiwa nawe) nilisema huku nikiupeleka mdomo wangu mdomoni kwake lakini alinikwepa na kuinuka haraka toka kwenye lile sofa huku akijitoa kwenye mikono yangu. Alionekana kutahayari sana.

“Olivia, naomba nikiri kwamba umeniteka sana. Sikutegemea kama ingetokea siku nikapenda tena baada ya masaibu yaliyonipata. Naomba usinielewe vibaya kwani toka nimekutana na wewe nimejikuta nikiwa tofauti sana na nilivyokuwa awali. Nimejikuta nikiwa na furaha ya ajabu kitu ambacho hakijawahi kunitokea hapo kabla,” nilisema huku nikiinuka kumfuata Olivia, nikasimama mbele yake na kumshika mikono.

Olivia alibaki kimya akiwa ananitumbulia macho, alikuwa amepigwa na butwaa asijue lipi la kusema au la kufanya.

“Umeniambia huna boyfriend baada ya kutendwa na umeahidi utaufanyia kazi ushauri wangu, siyo?” nilimuuliza Olivia.

“Ndiyo,” alinijibu huku akinitazama machoni. Kimya cha sekunde kadhaa kikajiunda baina yetu huku tukitazamana.

“Kama ilivyo kwako, nami pia nimetendwa na kwa sasa nipo single…” nilisema kisha nikasita kidogo, nikamtazama Olivia ili kumsaili umakini wake. Naam, alikuwa makini sana akinisikiliza. Usikivu wa Olivia lilikuwa ni jambo lililonitia matumaini.

“Maisha haya yananiwia vigumu, unaonaje kama tutakuwa wachumba, uchumba ambao utadumu kwa muda mfupi kabla hatujafunga ndoa?” nilimuuliza Olivia huku macho yangu nikiwa nimeyatuliza kwenye uso wake.

Nilimwona Olivia akishusha pumzi ndefu kisha akajitoa tena toka kwenye mikono yangu na kupiga hatua mbili huku akiwa ameinamisha uso wake chini, hali hiyo ilidumu kwa sekunde chache kisha aliinua tena uso wake kunitazama huku macho yake yakiwa yametawaliwa na aibu ambayo ilimnyima kabisa ujasiri, kiasi cha kumfanya ashindwe kukabiliana na macho yangu ambayo yalikuwa yamesheheni ujasiri.

Alinitazama kwa kitambo fulani akataka kusema neno lakini akashindwa na kuniashiria niketi kwenye sofa. Nilikaa kwenye sofa alilokuwa amekalia mwanzo huku naye akiketi kwenye sofa nililokuwa nimekalia mwanzo, kisha kikatokea kitambo kifupi cha ukimya.

“Jason Sizya!” Olivia aliniita na kunishtua sana, ilikuwa ni mara ya kwanza tangu tulipofahamiana kwa Olivia kuliita jina langu kwa ukamilifu wake. “Imekuwa ghafla sana, huoni kama…”

“Najua kwako inaweza kuonekana ni ghafla lakini tambua kuwa moyo wenye kupenda hauna subira…” nilimkatisha Olivia kabla hajamalizia sentensi yake.

“Nimejikuta nikitoka nje ya msimamo wangu kwa mara ya kwanza na kuhisi kwamba ninahitaji kuwa na mtu wa kunifanya niendelee kuipata furaha hii ya ajabu niipatayo sasa. Olivia, sihitaji kuwa mbali nawe tena kuanzia sasa,” niliongeza huku nikiinuka na kwenda kupiga magoti mbele ya Olivia.

“Ninathubutu kupiga magoti na kuomba nafasi ndani ya moyo wako. Olivia tafadhali naomba unipe nafasi ndani ya moyo wako. Sitakuumiza kama alivyokufanya mwanamume mwenzangu. Nitakupenda na kuwa nawe daima kwa sababu you are so special, Olivia!” nilisema na kushusha pumzi.

“Naelewa, Jason, lakini…” Olivia alisema kauli iliyobaki ikielea na kuzusha maswali ambayo nilijaribu kubashiri majibu yake lakini sikuweza.

“Najua huniamini na pengine naonekana tapeli wa mapenzi… labda unataka muda zaidi wa kufikiri juu ya hili, ila ukweli ni huo; nakupenda sana Olivia,” nilimwambia kisha nikainuka na kurudi kwenye sofa nikaketi na kuinua bilauri yangu ya mvinyo, nikaitazama kwa umakini na kupeleka mdomoni huku macho yangu nikiyaelekeza kwa Olivia ambaye alikuwa ananitazama kwa jicho la udadisi.

Nilihisi kuutua mzigo uliokuwa kifuani kwangu na hivyo niliugida kama maji ule mvinyo wote uliokuwemo kwenye bilauri yangu kisha nikajimiminia mvinyo mwingine na kuugida wote. Hata hivyo nilianza kutamani kupata pombe kali zaidi kwa sababu mvinyo huo ulikuwa na kiwango kidogo cha kilevi. Nilipoitupia jicho saa yangu nikagundua kuwa ilishatimu saa 12:45 jioni.

Muda wote Olivia alikuwa akinitazama kwa jicho la udadisi kama aliyekuwa akijaribu kuyasoma mawazo yangu, nami nikamtazama, tukawa tunatazamana.

“Sijui utapendelea nikupe kinywaji kingine kwa sasa?” Olivia aliniuliza huku akiendelea kunitazama kwa umakini. Ni kama alikuwa ameyasoma mawazo yangu.

“Ndiyo, nadhani whisky au pombe yoyote kali itanifaa,” nilisema kwa sauti dhaifu kabisa.

Olivia hakuonekana kushtushwa na kauli yangu nadhani kwa sababu aliitarajia jibu kama hilo, alinitazama kwa muda kidogo kisha akageuka kulitazama jokofu.

“Mi’ nafikiri badala ya whisky nikuletee Konyagi ambayo ni pombe ya Kitanzania au vipi?” Olivia aliniuliza lakini safari hii sikujibu kitu, nilikaa kimya huku nikimtazama kana kwamba sikusikia alichosema. Nilihisi kwamba alikuwa ananifanyia dhihaka.

“Nadhani Konyagi ni nzuri zaidi,” Olivia aliongeza.

Endelea...
 
fungate.jpeg

142

“Sawa, itapendeza kama nitapata na kipande cha limao,” nilisema na kumfanya Olivia atabasamu.

“Lakini kabla sijakuletea Konyagi nahitaji kujua jambo…” Olivia alisema na kuendelea, “do you real love me?

I love you more than what you think,” (Nakupenda zaidi ya unavyoweza kudhani) nilimjibu kwa sauti tulivu huku nikiyatuliza macho yangu kwenye uso wake.

“Ok, sasa naomba unijibu swali hili…” Olivia alisema kwa sauti tulivu na kuinamisha kichwa chake chini kidogo, akatafakari kabla hajainua uso wake kunitazama.

“Mimi na Rehema ni nani aliye na nafasi kubwa kwenye moyo wako? Tell me the truth, Jason,” Olivia aliniuliza huku akiwa amenikazia macho.

“Aah… suala lililopo hapa halimhusu Rehema… let’s talk about us,” nilimwambia Olivia huku nikionesha kubabaika kidogo.

“Usinidanganye Jason, najua Rehema bado yumo moyoni mwako. Bado unampenda Rehema ila unachofanya hapa ni kujaribu kuingia kwenye uhusiano na mimi kwa sababu unadhani itakusaidia kumsahau jambo ambalo litakuja kunitesa baadaye endapo nitaingia kichwa kichwa,” Olivia alisema kwa huzuni.

“Lakini…” nilitaka kusema ila Olivia akanikatisha.

“Nikwambie tu ukweli, naogopa sana kuufungua moyo wangu na kuuruhusu upende tena, kwa hiyo siwezi kurudi nyuma. Kwangu utaendelea kuwa rafiki na mtu muhimu sana…” Olivia alisema kwa sauti tulivu ya kirafiki.

“Aah… usinifanyie hivyo Olivia! Naomba uruhusu penzi langu ndani ya moyo wako, nakuhakikishia nitakuwa mwanamume mwema sana kwako. Nitahakikisha unakuwa mwenye furaha siku zote. Narudia kukwambia tena, nakupenda sana hadi nahisi kuchanganyikiwa,” nilisema na kumfanya Olivia acheke.

“Ahsante kwa kunipenda lakini…” Olivia alisema lakini nikamkatiza.

“Tafadhali Olivia, naomba usinifanyie hivyo…” nilimwambia kisha nikaendelea, “Nadhani siku nitakayokupoteza nitakuwa nimepoteza kitu cha thamani kuliko chochote nilichowahi kuwa nacho, sitaweza kuishi kwa furaha wala amani moyoni mwangu,” nilisema kwa hisia kali za kimapenzi huku nikimtazama Olivia kwa macho yaliyojaa ubembe wa huba.

“Jason, kama rafiki hutakuja kunipoteza. Nimekuwepo na nitaendelea kuwa rafiki yako…” Olivia alisema na kuonekana kusita.

“Hayo mambo ya kuniita rafiki yananikera sana, basi tu…” nililalamika na kumfanya Olivia acheke tena.

“Naomba niwe mkweli, sitaweza kuwa mpenzi wako ila niko tayari kusimama na wewe katika kuhakikisha unakuwa na furaha, na Rehema anarudi kwenye himaya yako,” Olivia alisema akionesha kumaanisha. Nilibaki kimya nikimtumbulia macho.

“Jason, naomba nikiri tu kuwa hata mimi nimetokea kukupenda sana na sitaki kukuacha katika hali hii lakini sitaweza kuingia kwenye uhusiano wowote wa kimapenzi na wewe kwa sababu ya ukweli ulio wazi kwamba Rehema anakuhitaji sana, na wewe pia unamhitaji. Kwa kifupi mnahitajiana. Acha niendelee kuishi maisha yangu niliyoyazoea, maisha ya kuwa peke yangu. Sitegemei kama nitaingia katika uhusiano kwa sasa kwa sababu nikijaribu kuufungua moyo wangu kupenda tena kuna uwezekano mkubwa wa kutokewa na kitu kile kile nilichokuwa nakikwepa, yaani maumivu ya moyo…” Olivia alisema kwa hisia kali huku akilengwa lengwa na machozi.

Nilijikuta nikikosa ujasiri nikabaki kimya huku nikiyatafakari maneno yake, na hapo nikajikuta nikimwonea huruma. Alionekana kuwa na upendo wa dhati kwangu lakini uwepo wa Rehema ulikuwa unamfanya kuumia moyo. Alikuwa akiteseka kupita kiasi!

“Olivia, naomba usiwe mwepesi wa kuhukumu jambo. Nadhani bado ipo nafasi ya kuweza kuyaweka sawa mambo haya ili mimi na wewe tuweze kutimiza lengo na kuishi kwa amani katika maisha yetu. Sikatai, ni kweli Rehema bado yupo akilini mwangu lakini kwa sasa wewe ndiye uliyeutawala moyo wangu kwa kiasi kikubwa. tafadhali nipe nafasi nikuoneshe,” nilimsihi.

Olivia alitingisha kichwa chake taratibu na kusema, “Kukupa nafasi ni kujitafutia matatizo! Tutaweza kujidanganya kuwa tuna furaha lakini ukweli sitakuwa na amani moyoni.”

Kwa dakika kadhaa nilijaribu sana kumshawishi anikubalie lakini ilikuwa kazi ngumu sana. Msimamo wake haukutetereka. Kwa mara nyingine tena nilihisi maumivu makali sana yakipenya kwenye moyo wangu tofauti na hata pale mwanzo. Ilikuwa ni kama pigo la kisu ambalo lilipenya mwilini na kuujeruhi moyo wangu.

Muda mfupi uliokuwa umepita nilikuwa nimeingia hapo hotelini nikiwa mwenye furaha kubwa na matumaini kibao lakini sasa sikujua nifanye nini baada ya Olivia kunikatalia katakata.

Nilimtazama Olivia kwa uchungu mkubwa, yeye alikuwa ametulia tuli kwenye kiti chake, bila shaka hakuwa na habari na kile kilichokuwa kinaendelea akilini kwangu. Shingo yake ndefu aliilaza upande kidogo, macho yake malegevu yalikuwa makini kunitazama kwa namna ambayo sikuweza kupata tafsiri ya haraka.

Ilikuwa picha ya kusisimua, picha ya kuvutia, picha ya kusikitisha, picha ambayo, kwa muda ilifanya fikra zangu zichukue likizo na nafasi yake kuchukuliwa na hisia za ajabu, hisia za kimaumbile zilizonifanya niwaze kumkumbatia kwa nguvu akiwa kama alivyozaliwa! Fahari iliyoje kumkumbatia mikononi mwangu msichana mrembo kama Olivia! Hadhi iliyoje kuserebuka na mrembo kama huyo!

Mara nikainuka. Olivia akanitazama kwa mshangao kama aliyezinduka toka usingizini, “Vipi, mbona umeinuka?” aliniuliza kwa mshangao.

“Sina sababu ya kuendelea kukaa hapa, nadhani ni wakati muafaka wa kuondoka zangu,” nilimwambia Olivia huku donge la hasira za kunyimwa penzi likinikabaa kooni.

“Kwa nini? Nilidhani bado tunapiga stori, na vipi kuhusu Konyagi uliyoitaka?” Olivia aliniuliza kwa sauti tulivu ya kirafiki.

“Hata mimi ningependa iwe hivyo,” nilimjibu. Kisha nikaongeza, “Kwa bahati mbaya haitawezekana tena.”

“Kwa nini?” Olivia aliniuliza huku akinitazama kwa umakini usoni, huenda alijaribu kuyasoma mawazo yangu.

“Naogopa yasije kunitokea ya bondia Mike Tyson,” nilisema huku nikiwa nimekunja sura yangu.

“Yepi?” Olivia aliniuliza huku mshangao ukijitokeza usoni kwake.

“Hujui kama aliwahi kufungwa?” nilimuuliza huku nikimkazia macho.

“Nafahamu. Si alibaka!” Olivia alijibu kwa haya kidogo.

“Nani ana uhakika kuwa alibaka? Alimkaribisha msichana mrembo chumbani kwake na baadaye msichana huyo alidai kuwa amebakwa. Tyson akatupwa jela,” nilisema kwa uchungu.

“Sijakuelewa, Jason. Unamaanisha kuwa naweza kukugeuka na kusema kuwa ume…” Olivia alisema lakini akasita kumalizia sentensi yake na kubaki akinitumbulia macho ya hasira na mshangao, hata hivyo sauti yake ilikuwa ile ile ya urafiki.

“Usijali… mimi ni mtu wa utani kila wakati. Hata hivyo nadhani ni wakati wa kurudi nyumbani kwangu,” nilimwambia Olivia kwa sauti tulivu.

“Mbona haraka namna hii?” Olivia aliniuliza. “Una haraka ya nini? Mi’ nilidhani tutakaa, tuongee, tunywe na tufurahi kisha tule chakula pamoja usiku kisha nikusindikize!”

Nilimtumbulia macho ya mshangao huku nikibaki mdomo wazi. Taratibu mshangao wangu ulianza kutoweka na nafasi yake kuchukuliwa na hasira, hasira za mwanamume aliyeumizwa, hasira ambazo kama nisingekuwa makini ningempa jibu ambalo lingemfanya asitamani tena kuongea na mimi.

Hata hivyo niliishia kumtazama kwa mshangao. Sikujua kama alikuwa akimaanisha alichokisema au ilikuwa ni dhihaka nyingine ya kutaka kuniumiza kiakili. Sikuelekea kuelewa.

“Mbona hukai?” Olivia aliniuliza kwa mshangao.

Nilitabasamu, “Usijali… nitakuja kukaa siku nyingine hadi unichoke,” alisema kwa utani.

Kauli hiyo ilimfanya Olivia aangue kicheko. “Wala siwezi kukuchoka, rafiki yangu,” alisema na kuongeza, “Nisubiri.”

Kisha nilimwona akiinuka na kuelekea chumbani. Punde tu, alirudi pale sebuleni akiwa ameshika kitabu ambacho sikuchelewa kukitambua kuwa ni cha mtaalamu wa afya ya akili na mwanasaikolojia mashuhuri duniani, Sigmund Freud cha ‘Introduction to Psychoanalysis’.

* * *

Endelea kufuatilia...
 
Baada ya hekaheka nyingi Jason utulizane sasa na uende ukatubu kwa Mungu wako
View attachment 2237749
138

Una furaha?


Saa 8:35 mchana.

SIKUWA nimetegemea kitu kama kile kutokea katika kipindi hicho. Tangu nikuitane na Olivia mambo makubwa yalikuwa yanatokea kwa haraka sana kwenye maisha yangu. Niliona ni kama ndoto. Kikao kile kilikuwa kimenijengea heshima kubwa mno kwa wale wawakilishi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika, heshima ambayo sikuwa nimetarajia kuipata. Kwa kweli Olivia alikuwa ameniheshimisha mno mbele ya wale watu.

You did great… sikutegemea kabisa kama ungeweza kuwa msaada mkubwa kwenye kikao cha leo. Jason you are amazing!” Olivia alininong’oneza sikioni wakati tukiinuka toka kwenye viti vyetu baada ya kikao cha kibiashara kati yetu na wawakilishi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika kumalizika.

Sikujibu kitu bali niliachia tabasamu tu, kisha nilitoa kitambaa na kujifuta jasho jepesi lililokuwa likinitoka usoni licha ya hewa safi yenye ubaridi mkali iliyosambazwa mle ukumbini na kiyoyozi kikubwa. Mambo yaliyokuwa yametokea mle ukumbini yalikuwa kama ndoto kwangu. Sikuwa nimetarajia kabisa kuwa mambo yangekwenda kama vile.

Nisingeweza hata kuelezea ni jinsi gani nilivyokuwa nimefurahi moyoni kukutana na wawakilishi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika jambo lililokuwa limeniongezea mtandao wa marafiki.

Wale wawakilishi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika walinifuata na kunipa mkono wa pongezi kwa jinsi nilivyoonekana kujua mambo mengi kwa kuwa nilikuwa na taarifa nyingi kutokana na utaalamu wangu adimu wa kukaa nyuma ya tarakilishi na kubofya kicharazio ili kuifanya dunia kuwa sawa na kijiji. Huo ulikuwa mchana wa kipekee sana kwangu. Nilifurahia sana kwa namna ambayo Olivia alivyonifanya niyasahau masaibu yote yaliyokuwa yamenikumba. Kila nilipomtazama Olivia usoni nilishindwa kuamini kama ni yeye kweli ndiye aliyeweza kunifanya nikawa na furaha kubwa namna ile!

“Nina furaha ya ajabu sana leo Jason. Umenifanya nione kuwa sikuwa nimekosea kukuamini na kukushirikisha kwenye mipango yangu kwa jinsi ulivyoonesha kuwa una akili nyingi na uwezo mkubwa wa kupambanua mambo magumu,” Olivia alinong’ona tena huku akishindwa kuificha furaha yake.

Kisha Olivia aliwaalika wale wawakilishi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika ukumbi wa chakula kwa ajili ya chakula cha mchana huku alinishika mkono, tukaanza kutoka nje ya ule ukumbi na kuelekea kwenye vyumba vya lifti za kushuka chini.

“Hata hivyo, naomba nichukue nafasi hii kukuomba sana samahani kwa kukushtukiza kuhusu jambo hili,” Olivia alisema huku akinitazama usoni.

“Usijali, Olivia… cha msingi ni kwamba kila kitu kimekwenda sawa,” nilisema katika namna ya kumtoa shaka. Wakati huo tulikuwa tumefika kwenye lifti na Olivia alibonyeza kitufe cha kuita lifti ili itupeleke chini, na mara mlango wa chumba cha lifti ukafungua na kuturuhusu kujitoma ndani.

“Najua utasema nisijali lakini nilikushirikisha kwenye mazungumzo ya kibiashara pasipo kwanza kukueleza kinagaubaga kuhusu mchakato wenyewe ulivyo. Haukuwa umejiandaa…”

“Nimekwambia usijali kwa yote,” nilimkatisha Olivia kabla hajamaliza sentensi yake. “Uliponiomba niambatane nawe kwenye kikao kati yako na wawakilishi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika nilikwisha jiandaa kisaikolojia. Na kuhusu kunishtukiza, yeah… I was a bit nervous lakini kuwa karibu nawe ilinipa ujasiri mkubwa hata nikaweza kutoa mchango wangu kwa kadiri nilivyoweza,” nilisema kwa msisitizo na kumfanya Olivia atabasamu.

Olivia alinitazama usoni kwa sekunde kadhaa kisha akasema, “Jason, you are amazing. Nilifanya makusudi kukuomba uje kushiriki kikao hiki lengo langu lilikuwa kuona kama nimepata rafiki mwerevu na mwenye kufahamu mambo mengi. Though you were nervous but what you did was wonderful…” Olivia alisema huku akinishika mkono, tukatoka nje ya kile chumba cha lifti baada ya kufika chini.

Kisha tuliongozana kuelekea kwenye ukumbi wa mgahawa wa Utulivu Grill ambao ulikuwa kwa ajili ya chakula cha Kitanzania na cha kimataifa. Niligundua kuwa ulikuwa mgahawa mzuri wa kisasa wenye huduma zote muhimu kama aina ya vyakula mbalimbali vya watu wa mataifa tofauti na utulivu wa kutosha.

Hatimaye tukatafuta meza moja iliyojitenga kwenye kona moja ya mgahawa ule na kuketi huku tukijitenga na watu wengine. Sehemu ile tuliyoketi ilituwezesha kuongea mengi ya kibinafsi yaliyotuhusu pasipo wasiwasi wowote. Mhudumu mmoja wa mgahawa ule alifika haraka kutusikiliza nikamwagiza wali kuku, maharage na saladi nyingi ya mboga za majani. Olivia yeye aliagiza biriani ya kuku na saladi ya mboga za majani.

Vyakula vile vilipoletwa na mhudumu tukaanza kuvishambulia huku kila mmoja akionekana kuwa na njaa, na wakati tukielekea kumaliza chakula Olivia alianzisha tena maongezi huku akishindwa kuificha furaha yake.

“Nimefurahi sana Jason kwa sababu hukuweza kuniangusha. Umeweza kuziteka akili za watu wa ADB. Sijawahi kuwa na furaha kama siku ya leo. Na furaha yote hii imechangiwa na wewe. You really made my day.” Olivia alisema huku akiinua bilauri ya maji na kuyanywa maji yote yote.

Kwa sifa alizokuwa akinipa Olivia nilihisi kama vile dunia yote ilikuwa kwenye himaya yangu, kitu kimoja tu sikuwa na uwezo nacho, uwezo wa kusimamisha muda uliokuwa ukienda kwa kasi ya ajabu. Nilitaka niendelee kuwa na mrembo yule asiyechosha kuwa naye. Nilihisi kuipata furaha ya ajabu ambayo sikuwa nimeipata kwa kitambo tangu ule mkasa ulionifanya kufarakana na Rehema.

“Jason mbona uko kimya sana? Unawaza nini?” Olivia aliniuliza baada ya kuniona nikiwa kimya nikimtazama.

“Nilikuwa nafikiria…” nilisema na kusita kidogo huku nikishusha pumzi za ndani kwa ndani. “Ningependa sasa kusikia the story about your affairs with your handsome ex-boyfriend,” niliongeza na kumfanya Olivia agune mara tu nilipomaliza sentensi yangu.

Ex-boyfriend!” Olivia aliniuliza kisha akaachia kicheko.

Yap! someone you loved, someone whom your heart belonged to him. Na kama uko tayari kumsamehe ili muwe kama zamani!” nilisema huku nikimtazama Olivia kwa tuo.

“Eti kumsamehe!” Olivia alisema na kucheka tena. Sikushangaa kwa sababu toka nilipomfahamu Olivia niligundua kwamba alikuwa anapenda mno kucheka.

“Usinifurahishe Jason, after what I got from him, I don’t think I will ever love again. Kwa sasa ninaishi maisha yangu ya furaha and I have lots of friends and lots to do… so what do I need a man for?” Olivia alisema huku akitingisha kichwa chake taratibu.

Endelea...
 
View attachment 2237753
141

Niliamini kuwa Olivia alikuwa ameigundua hali yangu na muda mwingi alijitahidi sana kunichangamsha kwa kunipigisha stori hizi na zile huku akicheka, baada ya kugundua nilikuwa nimepoteza uchangamfu wangu. Hatimaye nilionekana kufikia mwisho wa subira, nikapiga moyo konde, “Liwalo na liwe leo namwambia,” niliwaza.

Jason, are you ok?” (Jason, uko sawa?) Olivia aliniuliza huku akinitazama kwa udadisi.

Yeah, I’m okay,” nilimjibu Olivia kuwa nipo sasa huku nikiachia tabasamu. Olivia alinitazama kwa umakini na kushusha pumzi za ndani kwa ndani kisha alinyanyua juu mabega yake juu.

“Sasa mbona huongei? Na unaonekana umenywea!” Olivia alisema huku akiendelea kunitazama kwa tuo.

“Nilikuwa nakufikiria… natumaini leo unaweza kuniokoa maana nateketea ndani kwa ndani, Olivia,” nilisema kwa sauti ya unyonge.

“Unateketea! Kivipi?” Olivia alihoji huku akinikazia macho.

Ilinichukua dakika nzima nikiwa kimya bila ya kulijibu swali lake, muda huo nilikuwa natafakari namna ya kulijibu swali hilo, majibu nilikuwa nayo lakini nilihofu juu ya mapokezi ya jibu langu kabla sijalitoa. Sikuweza kujua kwa haraka ni kwa vipi litapokelewa. Hata hivyo nilijikaza na kuamua kwamba lolote na liwe, maji nilishayavulia nguo sikuwa na budi kuyaoga.

“Ni penzi lako Olivia… nakuhitaji sana kwenye maisha yangu na huu ndiyo wakati ambao nalihitaji penzi lako kuliko kitu kingine chochote,” nilisema na kuinuka pasipo hata kufikiria mara mbili kisha nikamsogelea na kuketi kando yake, nikauzungusha mkono wangu na kukishika kiuno chake huku nikihisi msisimko wa ajabu kwa kugusana na mrembo huyo. Kitendo hicho kilimfanya Olivia ashtuke sana na kuanza kuhema kwa nguvu.

What do you want from me?” (Unataka nini kwangu?) Olivia aniuliza kwa sauti laini iliyoonesha wazi kuwa alikuwa anatetemeka.

I just want a wonderful evening with you…” (Nataka hii iwe jioni ya kupendeza nikiwa nawe) nilisema huku nikiupeleka mdomo wangu mdomoni kwake lakini alinikwepa na kuinuka haraka toka kwenye lile sofa huku akijitoa kwenye mikono yangu. Alionekana kutahayari sana.

“Olivia, naomba nikiri kwamba umeniteka sana. Sikutegemea kama ingetokea siku nikapenda tena baada ya masaibu yaliyonipata. Naomba usinielewe vibaya kwani toka nimekutana na wewe nimejikuta nikiwa tofauti sana na nilivyokuwa awali. Nimejikuta nikiwa na furaha ya ajabu kitu ambacho hakijawahi kunitokea hapo kabla,” nilisema huku nikiinuka kumfuata Olivia, nikasimama mbele yake na kumshika mikono.

Olivia alibaki kimya akiwa ananitumbulia macho, alikuwa amepigwa na butwaa asijue lipi la kusema au la kufanya.

“Umeniambia huna boyfriend baada ya kutendwa na umeahidi utaufanyia kazi ushauri wangu, siyo?” nilimuuliza Olivia.

“Ndiyo,” alinijibu huku akinitazama machoni. Kimya cha sekunde kadhaa kikajiunda baina yetu huku tukitazamana.

“Kama ilivyo kwako, nami pia nimetendwa na kwa sasa nipo single…” nilisema kisha nikasita kidogo, nikamtazama Olivia ili kumsaili umakini wake. Naam, alikuwa makini sana akinisikiliza. Usikivu wa Olivia lilikuwa ni jambo lililonitia matumaini.

“Maisha haya yananiwia vigumu, unaonaje kama tutakuwa wachumba, uchumba ambao utadumu kwa muda mfupi kabla hatujafunga ndoa?” nilimuuliza Olivia huku macho yangu nikiwa nimeyatuliza kwenye uso wake.

Nilimwona Olivia akishusha pumzi ndefu kisha akajitoa tena toka kwenye mikono yangu na kupiga hatua mbili huku akiwa ameinamisha uso wake chini, hali hiyo ilidumu kwa sekunde chache kisha aliinua tena uso wake kunitazama huku macho yake yakiwa yametawaliwa na aibu ambayo ilimnyima kabisa ujasiri, kiasi cha kumfanya ashindwe kukabiliana na macho yangu ambayo yalikuwa yamesheheni ujasiri.

Alinitazama kwa kitambo fulani akataka kusema neno lakini akashindwa na kuniashiria niketi kwenye sofa. Nilikaa kwenye sofa alilokuwa amekalia mwanzo huku naye akiketi kwenye sofa nililokuwa nimekalia mwanzo, kisha kikatokea kitambo kifupi cha ukimya.

“Jason Sizya!” Olivia aliniita na kunishtua sana, ilikuwa ni mara ya kwanza tangu tulipofahamiana kwa Olivia kuliita jina langu kwa ukamilifu wake. “Imekuwa ghafla sana, huoni kama…”

“Najua kwako inaweza kuonekana ni ghafla lakini tambua kuwa moyo wenye kupenda hauna subira…” nilimkatisha Olivia kabla hajamalizia sentensi yake.

“Nimejikuta nikitoka nje ya msimamo wangu kwa mara ya kwanza na kuhisi kwamba ninahitaji kuwa na mtu wa kunifanya niendelee kuipata furaha hii ya ajabu niipatayo sasa. Olivia, sihitaji kuwa mbali nawe tena kuanzia sasa,” niliongeza huku nikiinuka na kwenda kupiga magoti mbele ya Olivia.

“Ninathubutu kupiga magoti na kuomba nafasi ndani ya moyo wako. Olivia tafadhali naomba unipe nafasi ndani ya moyo wako. Sitakuumiza kama alivyokufanya mwanamume mwenzangu. Nitakupenda na kuwa nawe daima kwa sababu you are so special, Olivia!” nilisema na kushusha pumzi.

“Naelewa, Jason, lakini…” Olivia alisema kauli iliyobaki ikielea na kuzusha maswali ambayo nilijaribu kubashiri majibu yake lakini sikuweza.

“Najua huniamini na pengine naonekana tapeli wa mapenzi… labda unataka muda zaidi wa kufikiri juu ya hili, ila ukweli ni huo; nakupenda sana Olivia,” nilimwambia kisha nikainuka na kurudi kwenye sofa nikaketi na kuinua bilauri yangu ya mvinyo, nikaitazama kwa umakini na kupeleka mdomoni huku macho yangu nikiyaelekeza kwa Olivia ambaye alikuwa ananitazama kwa jicho la udadisi.

Nilihisi kuutua mzigo uliokuwa kifuani kwangu na hivyo niliugida kama maji ule mvinyo wote uliokuwemo kwenye bilauri yangu kisha nikajimiminia mvinyo mwingine na kuugida wote. Hata hivyo nilianza kutamani kupata pombe kali zaidi kwa sababu mvinyo huo ulikuwa na kiwango kidogo cha kilevi. Nilipoitupia jicho saa yangu nikagundua kuwa ilishatimu saa 12:45 jioni.

Muda wote Olivia alikuwa akinitazama kwa jicho la udadisi kama aliyekuwa akijaribu kuyasoma mawazo yangu, nami nikamtazama, tukawa tunatazamana.

“Sijui utapendelea nikupe kinywaji kingine kwa sasa?” Olivia aliniuliza huku akiendelea kunitazama kwa umakini. Ni kama alikuwa ameyasoma mawazo yangu.

“Ndiyo, nadhani whisky au pombe yoyote kali itanifaa,” nilisema kwa sauti dhaifu kabisa.

Olivia hakuonekana kushtushwa na kauli yangu nadhani kwa sababu aliitarajia jibu kama hilo, alinitazama kwa muda kidogo kisha akageuka kulitazama jokofu.

“Mi’ nafikiri badala ya whisky nikuletee Konyagi ambayo ni pombe ya Kitanzania au vipi?” Olivia aliniuliza lakini safari hii sikujibu kitu, nilikaa kimya huku nikimtazama kana kwamba sikusikia alichosema. Nilihisi kwamba alikuwa ananifanyia dhihaka.

“Nadhani Konyagi ni nzuri zaidi,” Olivia aliongeza.

Endelea...
Jason uvumilivu zero, unawaza ngono tu hapa umejipunguzia credit kwa Olivia
 
fungate.jpeg

143

Sasa funga macho.


Saa 11:15 alfajiri.

KULIKUWA kumeanza kupambazuka, sauti za majogoo waliokuwa wakishindana kuwika kwenye mabanda, na kwa mbali, sauti za ndege angani walioshindana kuimba nyimbo nzuri na kuruka huku na kule kwenye vilele vya miti mikubwa ziliashiria ujio wa siku mpya.

Hadi muda huo, ikiwa imeingia siku nyingine, nilikuwa sijaambua japo lepe la usingizi. Nilikuwa bado nimeketi sebuleni kwangu kwenye sofa kwa kuegemea huku mawazo mchanganyiko yakiendelea kuzunguka kichwani kwangu. Muda wote tangu niliporejea nyumbani kwangu majira ya saa 1:30 usiku wa siku iliyokuwa imetangulia, nilikuwa nasoma maandishi yahusuyo saikolojia na ushauri. Ulikuwa usiku mrefu mno kwangu.

Hadi muda huo nilikuwa nimemaliza chupa nzima ya wisky, jambo ambalo niliamini kuwa lilitokana na hisia za upweke wa pekee ambao sikupata kuujua huko nyuma, upweke ulioongezeka baada ya kutoka hotelini kwa Olivia. Hivyo, kichwa changu nilikiona chepesi huku macho yangu yakiwa makini kiasi. Hali hilo ilinifanya nizidi kutafakari hili na lile.

Ni kipindi cha siku mbili tu zilizokuwa zimetangulia nilikuwa mtu mwenye furaha kubwa, mambo mazuri yalikuwa yamenitokea hasa tangu nilipofahamiana na mwanadada Olivia. Ilianza kama tamthiliya, tena tamthiliya yenyewe ya kusisimua sana, tamthiliya ya mapenzi.

Kama waigizaji katika tamthiliya hiyo; mimi kwa upande mmoja na Olivia kwa upande mwingine, hatukupata angalau kuhisi tu kuwa mwanzo wa tamthiliya hiyo ulikuwa sawa na kuanza kwa mkasa mwingine mzito wa kusisimua. Mkasa ambao ungeishia kunipa maumivu mengine makali ya moyo wangu.

Maumivu hayo yalianza baada ya kuathiriwa na tamati ya mambo katika mkasa ulioandikiwa hadithi inayoitwa ‘Narudi Buzwagi’, kwa mara nyingine tena almanusra nijikute nikichanganyikiwa.

Ni Olivia aliyekuwa amenirejesha kwenye hali ya kawaida kutoka kwenye msongo wa mawazo ambao ilibaki kidogo tu unisababishie uchizi kwa sababu ya sintofahamu iliyotokea na kusababisha nifarakane na Rehema. Na sasa, ni Olivia huyo huyo aliyetaka kunipa msongo mwingine wa mawazo kwa maumivu yaliyonijia katika picha fulani akili kwangu mfano wa tamthiliya ya kusisimua ya mapenzi.

Japo mji wa Kahama ulikuwa umefurika wasichana warembo kupindukia, wengi wao wakiwa wameuongeza urembo wao wa asili maradufu kwa vipodozi lukuki vilivyokuwa vimefurika madukani, lakini Olivia, huenda ni kama ilivyokuwa kwa ‘pacha wake’ Rehema, alikuwa na ziada kubwa juu ya uzuri wake. Alikuwa na kila kitu kilichonifanya nipagawe!

Niliendelea kutulia kwenye sofa tangu nilipowasili nyumbani. Lakini safari hii niliamua kuachana kabisa na kuwaza habari za mapenzi, japo halikuwa jambo rahisi. Niliamua nianze maisha mapya bila kufikiria hisia za upweke, bila Rehema au Olivia, kwa lengo la kuendeleza mipango yangu ya kimaisha ambayo ilikuwa imesimama kwa sababu ya matatizo ya kiakili yaliyokuwa yakinikabili.

Miongoni mwa mambo niliyopanga kuyashughulikia ni kuwasiliana na watu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika walioahidi kunisaidia ili niweze kuanzisha kampuni kubwa ya teknolojia ya mawasiliano hasa kwa kuanzisha programu maalumu ambazo zingetumika katika vifaa vya mawasiliano kama simu, tarakilishi na runinga. Kampuni hii ingekuwa mshindani mkubwa wa kampuni zingine kubwa zinazojihusisha na mawasiliano.

Niliamini kuwa ingekuwa rahisi kutekeleza kwa sababu nilikuwa mjuzi wa mambo ya tehama, pia miundombinu yote ya uendeshaji wa kazi hiyo ilikuwepo.

Pale kwenye sofa nilipoketi nilijizuia sana kuwaza chochote juu ya Rehema, na pengine juu ya Olivia, japokuwa hisia kali za mapenzi kwa watu hao zilikuwa zinanisukuma kufanya hivyo, hisia ambazo zilianza kujiunda upya akilini mwangu na kutuama kwenye vilindi vya moyo wangu baada ya kuhisi upweke. Rehema ambaye alianza kusahaulika akilini mwangu baada ya ujio wa Olivia, sasa alianza kurejea taratibu!

Hadi muda huo wa alfajiri sikuwa nimepata usingizi, si kwa sababu ya mawazo juu ya Rehema na wala si kwa sababu ya fikra juu ya Olivia, bali nilikuwa natafakari kuhusu hali yangu, hasa baada ya kujisomea maandishi yahusuyo saikolojia na ushauri toka kwenye kitabu cha Psychoanalysis cha Sigmund Freud nilichopewa na Olivia, na kukutana na nadharia yake ya ‘Psychoanalysis’ ambayo tunaweza kuiita ‘Udodosi Nafsi’ kwa Kiswahili.

Maandishi hayo yalikuwa yameifungua akili yangu na sasa nilihisi kupata tiba ya tatizo langu la kiakili lililotokana na ule mkasa ambao uliandikiwa hadithi ya ‘Narudi Buzwagi’.

Katika kuyasoma maandishi ya Sigmund Freud na nadharia yake nilijikuta kama vile nazungumza na mwananadharia huyo ana kwa ana!

Kwenye nadharia hiyo niliweza kujua kuwa: binadamu ana nafsi tatu ambazo hana utambuzi nazo. Nafsi hizo ambazo humkamilisha mtu ni; ‘Idi’ ambayo ni nafsi ya kibaiolojia, inayotawaliwa na tabia za ubinafsi na hamasa ya kupunguza au kuondoa maumivu.

Katika nafsi hii huwa hakuna mjadala wala nafasi ya kufikiri. Hapa mtu hutenda anayotenda kwa sababu ya msukumo wa ubinafsi uliomo ndani yake. Nafsi hii ndiyo humsukuma mtu kutenda matendo ya ajabu kama vile kubaka, kuua na kadhalika.

Nafsi ya pili ni ‘Ego’, ambayo ni nafsi ya kisaikolojia inayojaribu kuhusianisha ‘Idi’ na uhalisia. Katika nafsi hii angalau kuna chembechembe za fikra na mjadala. Hivyo mtu anapoamua kutenda jambo hujaribu kufikiri kabla ya kutenda.

Na nafsi ya tatu ni ‘Super-ego’, hii ni nafsi ya kijamii ambayo ni nafsi amuzi. Huamua kati ya Idi na Ego kwa kuzingatia maadili, utamaduni na misingi ya jamii. Nafsi hii ndiyo humfanya mtu kuwa na aibu au kutofanya jambo fulani kwa sababu ni kinyume na kanuni na taratibu za jamii fulani.

Nafsi hizi tatu hufanya kazi ndani ya mtu bila ya mtu mwenyewe kujitambua, ila mtu mwingine anayemwona mtendaji ndiye hujua ni nafsi ipi inamsukuma mtu kufanya afanyayo.

Muda wote wakati nikiisoma kwa umakini nadharia hii sikuhisi usingizi, nilisoma na kutafakari, nikaelewa namna inavyofanya kazi katika kushauri na hatua ninazopaswa kuzifuata katika kuondokana na tatizo la kiakili lililonikumba, na pengine kuja kuwa mshauri kwa wengine hasa pale nitakapohitajika kuitumia nadharia hii.

Kwa kuhusianisha hali yangu nilitambua fika kuwa, yawezekana nilikuwa sijui nilitendalo kwa sababu nafsi iliyokuwa ikiniongoza wakati wote ilikuwa ‘Idi’, na nilikuwa nimepoteza maana ya maisha yangu ndiyo maana nilikuwa jinsi nilivyokuwa.

_____

Sikuweza kufahamu ni wakati gani lepe hafifu la usingizi lilikuwa limefanikiwa kuziteka fikra zangu pale pale kwenye sofa wakati nilipokuwa nikiendelea kuwaza hili na lile juu ya hali yangu, hadi pale niliposhtushwa na sauti ya kengele ya getini iliyoanza kuita kwa fujo.

Niliyatega masikio yangu vizuri kusikilizia huku nikiwaza mgongaji angekuwa nani. Niliitupia macho saa yangu ya mkononi nikashtuka kuwa ilikuwa ikielekea kutimia saa tatu ya asubuhi. Muda huo miale ya jua la asubuhi ilikuwa imepenya dirishani na kutuama pale kwenye sofa nilipoketi tangu kulipopambazuka.

Endelea...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom