JOTO LA MOTO
JF-Expert Member
- Apr 11, 2018
- 758
- 555
SIMULIZI: DUNIA DUARA.
KUTOKA KWA JOTO LA MOTO.
SEHEMU YA KWANZA.
KIJENGE JUU ARUSHA-MSURURU WA VYUMBA VYA KUPANGA-NJE-ASUBUHI.
Rose, Mwanadada mrembo wa miaka 20, yupo nje ya nyumba anapiga mswaki, anakuja Mlela, kijana wa miaka 21, huku akiwa mkononi ameshikilia fulana kuu kuu, “mimi ngoja niwahi maji kabla hakujawa na foleni” anasema Mlela huku akiwa anaivaa ile fulana aliyoibeba, “jitahidi basi maana pale sina maji kabisa” anasema Rose, Mlela anabaki amesimama akimuangalia Rose, “nini tena?” anauliza Rose baada ya kuona Mlela bado ameduwaa, “tairi moja haina upepo na mfukoni sina hata sumni” anasema Mlela, Rose anashusha pumzi, “hivi pesa zako huwa unapeleka wapi?” anauliza Rose, “ni pesa gani ile ninayoipata Rose?” anasema Mlela, “chukua elfu tano pale ndani kwenye ile pochi kubwa nyeupe” anasema Rose na kumfanya Mlela kuondoka na kuelekea ndani ya chumba, Rose anaendelea kuswaki.
MTAANI-CHUMBA CHA MAMALISHE-NDANI.
Rose amesimama kwenye kona akimimina chai kwenye kikombe kutoka kwenye thermos, kisha anachukua kikombe kile na sahani yenye chapati mbili na kupeleka kwa mmoja wa Wateja kadhaa waliopo pale ndani. Nje anafika Mlela, akiwa ameloa jasho sehemu ya kifuani na makwapani huku mkononi ana kitambaa akijifuta jasho usoni, anasimama mlangoni akimuangalia Rose anayeweka kikombe na sahani ya chapati mezani kwa Mteja na kisha anapokea pesa, Rose anainua kichwa na kumuona Mlela akiwa amesimama pale nje, anamfuata “vipi..mbona umechelewa hivyo tena jamani?” anasema Rose huku akifika pale alipo Mlela, “tairi la mkokoteni limesumbua tena”, “maji nimeleta jaba tano” anasema Mlela, “afadhali..nikuwekee chakula?” anauliza Rose, “nadhani nikimbie kwanza kwa Mama mwenye nyumba” anasema Mlela na kumfanya Rose kushtuka na kuingiza mkono kwenye mkoba wake aliouvaa kiunoni na kutoa pesa kadhaa, “hebu kweli mpelekee hela yake yule Mama..maana tangu amesikia tumeanza kujenga ni visa juu ya visa” anasema Rose huku akihesabu pesa zile, “uchukue na elfu ishirini pale ndani juu ya meza” anasema Rose huku akimpatia Mlela zile pesa, Mlela anapokea na kuziweka mfukoni, “ukirudi pitia basi mkaa kwa Abuu” anasema Rose, “naenda kwanza shuleni wamenipigia wanahitaji maji” anasema Mlela, “sawa basi ukimaliza hiyo kazi ya shule upite kwa Abuu” anasema Rose, “poa” anajibu Mlela huku akiondoka, “na naomba leo ukipata hela huko ulipe deni la Mukulu..sipendi anavyokuja kusumbua pale nyumbani” anasema Rose na kumfanya Mlela kusita kwa muda, “kama ticha atalipa vizuri nitamlipa Mukulu” anasema Mlela na kuondoka,“dada ongeza maharage” inasikika sauti kali ya Mteja kutoka ndani inayomshtua Rose na kumfanya kuingia ndani kwa haraka.
MIAKA NANE BAADAE.
NYUMBANI KWA ROSE NA MLELA-NJE.
Gari zuri aina ya Toyota Harrier nyeupe imesimama nje ya geti, mbele ya nyumba moja nzuri ya kuvutia, Mlela yupo ndani ya gari ametulia huku akionekana kufurahia muziki laini wa bongo fleva unaotoka redioni, geti linafunguka anatoka Rose akiwa amevalia kitenge maridadi na kupendeza, mkononi amebeba pochi nzuri, anafunga geti lile na kuingia kwenye gari, “nilikuacha umeshavaa lakini bado umetumia zaidi ya dakika ishirini” anasema Mlela huku akiwasha gari na kuweka gia na kuondoa, “nilikuwa kwenye maombi” anasema Rose, kinapita kimya kifupi, “naona wewe siku hizi maombi kwako si muhimu tena?” anasema Rose, “maombi ni popote Rose..mimi nimeomba nikiwa huku kwenye gari” anasema Mlela, Rose anamkata Mlela jicho, “tangu lini?” anauliza Rose, Mlela anabaki kimya, “miaka yote mpaka tumefika hapa tulipo ulikuwa ukiheshimu sana maombi Mlela” anasema Rose, “sijasema siheshimu maombi..usiniwekee maneno mdomoni Rose” anasema Mlela kwa sauti ya chini lakini inayoashiria kughafilika, wanakuwa kimya kwa muda, “alafu nikisema siku hizi umebadilika sana unakuwa mkali” anasema Rose kwa sauti ya chini kama Mtu anayenung’unika, kisha anashusha pumzi nyepesi na kutulia, huku Mlela akimkata jicho bila kujibu neno.
SUPER MARKET-NJE.
Gari la Mlela linafika na kusimama nje ya jengo moja zuri lenye bango juu yake linalosomeka “M and R SUPERMARKET”, wanateremka Mlela na Rose na kupokelewa na vijana wawili, Donii na Riki waliokuwa wameketi pale nje ya jengo lile, Mlela anampatia Riki ufunguo, Riki na Donii wanaanza kufungua kofuli za milango ya pale Supermarket.
SUPER MARKET-NDANI-BAADAE.
Wateja kadhaa wakipita huku na kule ndani pale wakichagua bidhaa, Mlela yupo kaunta, mbele yake yupo Mimi Mars, binti mrembo, 26, wanaonekana wakiongea huku kila mmoja akiwa na tabasamu pevu usoni, Rose yupo amesimama mita kadhaa kwenye kona akiwaangalia Mimi Mars na Mlela, huku Riki(kijana wa kazi) akiweka bidhaa mbalimbali kwenye mifuko, kisha Riki anachukua mifuko ile na kutoka akifuatana na Mimi Mars, Rose anakuja kwa Mlela pale kaunta, “mbona sijaona huyo dada akilipia hivyo vitu?” anauliza Rose, “amesema amesahau pesa ataleta kesho” anasema Mlela, “hii ni mara ya pili nashuhudia huyu dada anaondoka na vitu bila kulipa Mlela” anasema Rose, "tatizo lako ni kumuhudumia Mteja huku nimetabasamu au nini Rose?“ anasema Mlea, "tatizo ni kuwa unachofanya ni kutoa zawadi badala ya kufanya biashara Mlela", "Rose please” anasema Mlela kwa sauti ya chini akimkatiza Rose, “hebu naomba nihudumie Wateja” anasema Mlela kisha anamgeukia Bwana mmoja wa makamo anayefika pale kaunta akiwa amebeba chupa kubwa ya maji, Mlela anapokea pesa kutoka kwa Bwana yule, Rose anabaki pale pembeni akimuangalia Mlela huku akishusha pumzi inayoashiria hasira imemkaba kifuani kwake, “karibu tena” Mlela anamwambia Mteja yule huku akimpatia chenji na risiti na yule bwana anaondoka, “naomba baadae tuwe na mazungumzo Mlela” anasema Rose kwa sauti inayoashiria amechukizwa na kisha anandoka pale.
NYUMBANI KWA ROSE NA MLELA-NJE-JIONI
Gari la Mlela linafika getini na kusimama, ndani yupo Mlela na Rose “kuna mahali nafika mara moja nitarudi sasa hivi” anasema Mlela mara baada ya kuvuta hand break, “naomba tuingie ndani tukazungumze kwanza Mlela ndio uende unapoenda”, anasema Rose, “nimesema narudi sasa hivi Rose” anasema Mlela kwa sauti ya kusisitiza, Rose anafungua mlango na kuteremka, Mlela anaondoa hand break, anaweka gia kurudisha gari nyuma na kisha kuondoka, Rose anaenda getini na kubofya kitufe cha kengele, muda kidogo geti linafunguliwa na Nandi, binti mrembo, 20. Rose anaingia na kufunga geti.
NYUMBANI KWA ROSE NA MLELA-NDANI-USIKU.
Mlango unafunguka, anaingia Mlela, anabofya switch pale ukutani kuwasha taa, anashtuka kumuona Rose ameketi kochini ametulia kimya, “upo gizani?” anauliza Mlela, “ndio nipo gizani ndio maana nataka leo nijue ni nini kinaendelea kwa sasa Mlela maana mwenzangu sikuelewi” anasema Rose kwa sauti tulivu, “alafu saa hizi ni saa tano..na ulisema ungerudi mapema?” anauliza Rose, “nilipata kikao cha dharura” anasema Mlela huku akiketi kochini, mezani kuna hotpoti mbili, sahani na vijiko, Rose anachukua sahani na kijiko na kufungua hot poti, “mimi sitakula” anasema Mlela, Rose anabaki anamuangalia Mlela na kisha anashusha pumzi na kuifunga ile hotipoti, Mlela anachukua remote control ya TV iliyopo pale mezani na kuwasha TV, “kama huli basi naomba twende chumbani tukazungumze” anasema Rose, “naaangalia mechi kwanza” anasema Mlela huku akibofya remote mara kadhaa kabla ya kukutana na mechi ya mpira, anaiweka remote mezani, Rose anaangalia kwenye TV, “jamani hiyo mechi si ni marudio?” anasema Rose, “ndio..nataka nirudie kuangalia”, anasema Mlela, Rose anabakia akimuangalia Mlela kwa jicho kali, kisha anainuka na kuondoka, zinapita sekunde kadhaa, Mlela anainuka na kwenda meza iliyo pembeni na kuchukua chupa ya whisky na glasi, anamimina whisky kwenye glasi nusu na kurudi kuketi pale kochini, zinapita sekunde kadhaa huku akipiga funda kadhaa. Anapita Nandi na kumfanya Mlela kushtuka na kugeuka, kisha Mlela anainuka na kwenda alipoelekea Nandi.
NYUMBANI KWA ROSE NA MLELA-JIKONI-USIKU.
Nandi anafika pale jikoni kwenye sinki na kuanza kuosha vyombo, anakuja Mlela na kusimama mlangoni akiwa na ile glasi ya whisky mkononi, “mpaka saa hizi bado hujalala?” anauliza Mlela na kumfanya Nandi kushtuka na kugeuka kumuangalia Mlela, huku Mlela akiendelea kupiga funda ya whisky, “nilikuwa naangalia tamthilia” anasema Nandi, kisha Nandi anageuka na kuja mlangoni akitaka kutoka, Mlela anaziba mlango kumzuia, Nandi anamuona Rose akiwa amesimama nyuma ya Mlela, Nandi anajaribu kumpa Mlela ishara ageuke nyuma, Mlela anageuka nyuma na kumuona Rose, kisha anasogea kumpisha Nandi kutoka, Mlela na Rose wanabaki wanaangaliana kwa muda, kisha Rose anaondoka, Mlela anarudi na kuketi kochini na kuendelea kuangalia TV.
NYUMBANI KWA MLELA-CHUMBANI KWA NANDI-USIKU.
Nandi ameketi kitandani, Rose anaingia na kuketi pembeni ya Nandi pale kwenye kitanda, akiwa amejiinamia na macho yake yakiwa yamejaa machozi, “Nandi mdogo wangu” anasema Rose na kumfanya Nandi kushtuka na kubaki makini kumsikiliza Rose, “kuna nini kinaendelea kati yako na Mlela?” anauliza Rose, “hakuna chochote Dada” anasema Nandi, wanabaki kimya kwa muda, “mimi sio Mtoto Nandi..na kama kuna chochote nitajua tu Nandi...kwa hiyo usipoteze muda kunificha” anasema Rose kwa sauti tulivu lakini ya kusisitiza, “kweli Dada Rose hakuna chochote kinaendelea” anasema Nandi, Rose anashusha pumzi ndefu kisha anapanda kitandani pale na kujilaza, huku Nandi akibaki ameketi pale kitandani.
NYUMBANI KWA ROSE NA MLELA-SEBULENI-ASUBUHI.
Rose na Nandi wameketi kwenye meza ya chakula, Rose akiwa na simu mkononi akiibofya mara kadhaa huku Nandi akimuangalia kwa makini, “kwa nini hakuna kumbukumbu ya simu ulizowahi kupiga au kupigiwa?” Rose anauliza, “huwa sipendi tu kuzihifadhi”, anasema Nandi huku akiangalia chini na kumuacha Rose akibaki anamkodolea macho, wanabaki kimya kwa muda wa sekunde kadhaa, mara wanashtushwa na mlio wa ile simu kuita, Rose anaiangalia simu na kuonyesha mshtuko mkubwa usoni kwake, “Mungu hamfichi mnafiki Nandi” anasema Rose huku akimuonyesha namba inayoonekana kwenye simu, Nandi anabaki anaangalia huku akibaki kimya ameduwaa, “naomba upokee” anasema Rose huku akimpatia Nandi simu, Nandi anapokea na kutaka kuiweka sikioni, Rose anamshika mkono na kumzuia, anaichukua simu na kubofya kitufe na kuifanya simu kuwa kwenye mfumo wa loud speaker kisha anaiweka mezani, “hallow” inasikika sauti ya Mlela, “hallow” anajibu Nandi huku akionekana kuwa na uoga, “uko sawa?” sauti ya Mlela inauliza, “nipo sawa tu” anajibu Nandi, “huyo Kipepe ameshaondoka?” anauliza Mlela, Nandi anamuangalia Rose, Rose anampa ishara aseme ndio, “ameshaondoka” anasema Nandi, “ok nakuja unipe stori za nini kiliendelea jana” inasema sauti ya Mlela na kisha simu inakatika, Rose anabaki anamuangalia Nandi ambaye ameinamisha kichwa huku kaweka mkono shavuni, “kwa nini mnaniita Kipepe?” anauliza Rose, Nandi anabaki kimya kwa muda, “anasema zamani ulikuwa unapenda kufunga nywele zako kwa nyuma kama yule kipepe wa gazetini” anasema Nandi na kumfanya Rose kubaki ameduwaa kwa sekunde kadhaa machozi yakimlenga, anashusha pumzi “Nandi kweli mdogo wangu?” anasema Rose kwa sauti ya chini inayotetema kwa majonzi na jazba, “ulikuja na heshima zote..huna hili wala lile” anaendelea Rose, “Watu nje hata hawajui kama wewe ni dada wa kazi humu ndani kwa jinsi ninavyoishi na wewe kwa upendo?” anaendelea Rose huku akilengwa na machozi, “kweli haya ndio malipo yako?” anaendelea Rose huku Nandi bado amejiinamia, wanabaki kimya kwa muda, mara Nandi anainuka kwa haraka, Rose anashtuka na kumuangalia, Nandi anaondoka huku akionyesha dalili za kutaka kutapika.
NYUMBANI KWA ROSE NA MLELA-CHOONI.
Nandi anaingia chooni kwa kasi na kuinama kwenye sinki la choo na kuanza kutapika, Rose naye anafika na kusimama nyuma ya Nandi, “ni nini?” anauliza Rose huku akijaribu kumsaidia kwa kumshika mabegani, Nandi anaendelea kutapika kwa mara kadhaa kisha anatulia kwa sekunde kadhaa, “bado unajisikia vibaya?” anauliza Rose kisha anamuinua na kutoka naye nje.
NYUMBANI KWA ROSE NA MLELA-SEBULENI.
Nandi ameketi kochini, Rose anakuja na glasi ya maji na kumpatia, “bado unajisikia kichefuchefu?” anauliza Rose huku akimpatia Nandi ile glasi, “sasa nasikia afadhali” anajibu Nandi kwa sauti ya kichovu huku anapokea glasi na kupiga funda mara kadhaa, Nandi anashusha pumzi nzito huku akiiweka glasi mezani, wanabaki kimya kwa muda, “haya ngoja mimi niende umsubiri huyo mgeni wako” anasema Rose na kisha anaelekea mlangoni na kutoka.
SAKINA-MGAHAWANI-NJE.
Rose na Mai, dada wa makamo, 34, wameketi wote wakiwa na vikombe vya chai mbele yao, kimya kinatawala kwa muda, “au ananifanyia hivi kwa kuwa sijajaliwa kuzaa” anasema Rose kwa sauti ya kinyonge, “hakuna lolote Rose” anang’aka Mai akimkatiza Rose, “wangapi hawajapata Watoto na bado wanaheshimiana bana” anaongeza Mai, “anachofanya huyu Pimbi ni dharau za kipimbi tu” anasema Mai kwa sauti iliyojaa shari, wanabaki kimya kwa muda, “umedharau mwiba sasa mguu umeota tende Rose..nilikwambia umtoe yule binti pale kwako hukusikia” anasema Mai”, Rose anabaki kimya, “na yule Malaya atatoka pale ndani” anasema Mai na kumfanya Rose kuinua kichwa kumuangalia Mai, “kwa kosa lipi Mai?” anasema Rose na kumfanya Mai kugeuka na kumkata jicho kali, “mwenye kosa ni Mlela sio Nandi” anaongeza Rose, “hapo tu ndio huwa unanichefua Rose” anasema Mai, “jitu mpaka limebeba mimba ndani kwako bado huoni kosa lake?..tunaanza na yule Malaya kisha tunahamia kwa huyo Pimbi wako” anaendelea Mai, “Mai naomba mimi sitaki vurugu zisizo na maana” anasema Rose na kumfanya Mai abaki anamkata Rose jicho kali, “Pale mlipofika ni juhudi zako Rose” anasema Mai, “mchango wa yule Pimbi ni mdogo sana..wakuachie nyumba yako wakatafute kwa kuishi na huyo Malaya wake”anang'aka Mai kwa sauti kali huku anainuka “tena twende sasa hivi kwa huyo Malaya” anasema Mai na kumfanya Rose bado ameduwaa, “nyumba sio yangu naenda kumtoa” anasema Mai huku akichukua mkoba wake na funguo za gari pale mezani, “twende” Mai anamuamrisha Rose, “tukafanye nini haswa Dada Mai” anauliza Rose, “we twende” Mai anaamrisha huku akimshika Rose mkono na kumuinua na kumkokota kuelekea lilipo gari la Mai, Mai anafungua mlango wa gari na kuingia, Rose naye pole pole anaelekea upande mwingine wa gari na kuingia, Gari linaondoka.
KUTOKA KWA JOTO LA MOTO.
SEHEMU YA KWANZA.
KIJENGE JUU ARUSHA-MSURURU WA VYUMBA VYA KUPANGA-NJE-ASUBUHI.
Rose, Mwanadada mrembo wa miaka 20, yupo nje ya nyumba anapiga mswaki, anakuja Mlela, kijana wa miaka 21, huku akiwa mkononi ameshikilia fulana kuu kuu, “mimi ngoja niwahi maji kabla hakujawa na foleni” anasema Mlela huku akiwa anaivaa ile fulana aliyoibeba, “jitahidi basi maana pale sina maji kabisa” anasema Rose, Mlela anabaki amesimama akimuangalia Rose, “nini tena?” anauliza Rose baada ya kuona Mlela bado ameduwaa, “tairi moja haina upepo na mfukoni sina hata sumni” anasema Mlela, Rose anashusha pumzi, “hivi pesa zako huwa unapeleka wapi?” anauliza Rose, “ni pesa gani ile ninayoipata Rose?” anasema Mlela, “chukua elfu tano pale ndani kwenye ile pochi kubwa nyeupe” anasema Rose na kumfanya Mlela kuondoka na kuelekea ndani ya chumba, Rose anaendelea kuswaki.
MTAANI-CHUMBA CHA MAMALISHE-NDANI.
Rose amesimama kwenye kona akimimina chai kwenye kikombe kutoka kwenye thermos, kisha anachukua kikombe kile na sahani yenye chapati mbili na kupeleka kwa mmoja wa Wateja kadhaa waliopo pale ndani. Nje anafika Mlela, akiwa ameloa jasho sehemu ya kifuani na makwapani huku mkononi ana kitambaa akijifuta jasho usoni, anasimama mlangoni akimuangalia Rose anayeweka kikombe na sahani ya chapati mezani kwa Mteja na kisha anapokea pesa, Rose anainua kichwa na kumuona Mlela akiwa amesimama pale nje, anamfuata “vipi..mbona umechelewa hivyo tena jamani?” anasema Rose huku akifika pale alipo Mlela, “tairi la mkokoteni limesumbua tena”, “maji nimeleta jaba tano” anasema Mlela, “afadhali..nikuwekee chakula?” anauliza Rose, “nadhani nikimbie kwanza kwa Mama mwenye nyumba” anasema Mlela na kumfanya Rose kushtuka na kuingiza mkono kwenye mkoba wake aliouvaa kiunoni na kutoa pesa kadhaa, “hebu kweli mpelekee hela yake yule Mama..maana tangu amesikia tumeanza kujenga ni visa juu ya visa” anasema Rose huku akihesabu pesa zile, “uchukue na elfu ishirini pale ndani juu ya meza” anasema Rose huku akimpatia Mlela zile pesa, Mlela anapokea na kuziweka mfukoni, “ukirudi pitia basi mkaa kwa Abuu” anasema Rose, “naenda kwanza shuleni wamenipigia wanahitaji maji” anasema Mlela, “sawa basi ukimaliza hiyo kazi ya shule upite kwa Abuu” anasema Rose, “poa” anajibu Mlela huku akiondoka, “na naomba leo ukipata hela huko ulipe deni la Mukulu..sipendi anavyokuja kusumbua pale nyumbani” anasema Rose na kumfanya Mlela kusita kwa muda, “kama ticha atalipa vizuri nitamlipa Mukulu” anasema Mlela na kuondoka,“dada ongeza maharage” inasikika sauti kali ya Mteja kutoka ndani inayomshtua Rose na kumfanya kuingia ndani kwa haraka.
MIAKA NANE BAADAE.
NYUMBANI KWA ROSE NA MLELA-NJE.
Gari zuri aina ya Toyota Harrier nyeupe imesimama nje ya geti, mbele ya nyumba moja nzuri ya kuvutia, Mlela yupo ndani ya gari ametulia huku akionekana kufurahia muziki laini wa bongo fleva unaotoka redioni, geti linafunguka anatoka Rose akiwa amevalia kitenge maridadi na kupendeza, mkononi amebeba pochi nzuri, anafunga geti lile na kuingia kwenye gari, “nilikuacha umeshavaa lakini bado umetumia zaidi ya dakika ishirini” anasema Mlela huku akiwasha gari na kuweka gia na kuondoa, “nilikuwa kwenye maombi” anasema Rose, kinapita kimya kifupi, “naona wewe siku hizi maombi kwako si muhimu tena?” anasema Rose, “maombi ni popote Rose..mimi nimeomba nikiwa huku kwenye gari” anasema Mlela, Rose anamkata Mlela jicho, “tangu lini?” anauliza Rose, Mlela anabaki kimya, “miaka yote mpaka tumefika hapa tulipo ulikuwa ukiheshimu sana maombi Mlela” anasema Rose, “sijasema siheshimu maombi..usiniwekee maneno mdomoni Rose” anasema Mlela kwa sauti ya chini lakini inayoashiria kughafilika, wanakuwa kimya kwa muda, “alafu nikisema siku hizi umebadilika sana unakuwa mkali” anasema Rose kwa sauti ya chini kama Mtu anayenung’unika, kisha anashusha pumzi nyepesi na kutulia, huku Mlela akimkata jicho bila kujibu neno.
SUPER MARKET-NJE.
Gari la Mlela linafika na kusimama nje ya jengo moja zuri lenye bango juu yake linalosomeka “M and R SUPERMARKET”, wanateremka Mlela na Rose na kupokelewa na vijana wawili, Donii na Riki waliokuwa wameketi pale nje ya jengo lile, Mlela anampatia Riki ufunguo, Riki na Donii wanaanza kufungua kofuli za milango ya pale Supermarket.
SUPER MARKET-NDANI-BAADAE.
Wateja kadhaa wakipita huku na kule ndani pale wakichagua bidhaa, Mlela yupo kaunta, mbele yake yupo Mimi Mars, binti mrembo, 26, wanaonekana wakiongea huku kila mmoja akiwa na tabasamu pevu usoni, Rose yupo amesimama mita kadhaa kwenye kona akiwaangalia Mimi Mars na Mlela, huku Riki(kijana wa kazi) akiweka bidhaa mbalimbali kwenye mifuko, kisha Riki anachukua mifuko ile na kutoka akifuatana na Mimi Mars, Rose anakuja kwa Mlela pale kaunta, “mbona sijaona huyo dada akilipia hivyo vitu?” anauliza Rose, “amesema amesahau pesa ataleta kesho” anasema Mlela, “hii ni mara ya pili nashuhudia huyu dada anaondoka na vitu bila kulipa Mlela” anasema Rose, "tatizo lako ni kumuhudumia Mteja huku nimetabasamu au nini Rose?“ anasema Mlea, "tatizo ni kuwa unachofanya ni kutoa zawadi badala ya kufanya biashara Mlela", "Rose please” anasema Mlela kwa sauti ya chini akimkatiza Rose, “hebu naomba nihudumie Wateja” anasema Mlela kisha anamgeukia Bwana mmoja wa makamo anayefika pale kaunta akiwa amebeba chupa kubwa ya maji, Mlela anapokea pesa kutoka kwa Bwana yule, Rose anabaki pale pembeni akimuangalia Mlela huku akishusha pumzi inayoashiria hasira imemkaba kifuani kwake, “karibu tena” Mlela anamwambia Mteja yule huku akimpatia chenji na risiti na yule bwana anaondoka, “naomba baadae tuwe na mazungumzo Mlela” anasema Rose kwa sauti inayoashiria amechukizwa na kisha anandoka pale.
NYUMBANI KWA ROSE NA MLELA-NJE-JIONI
Gari la Mlela linafika getini na kusimama, ndani yupo Mlela na Rose “kuna mahali nafika mara moja nitarudi sasa hivi” anasema Mlela mara baada ya kuvuta hand break, “naomba tuingie ndani tukazungumze kwanza Mlela ndio uende unapoenda”, anasema Rose, “nimesema narudi sasa hivi Rose” anasema Mlela kwa sauti ya kusisitiza, Rose anafungua mlango na kuteremka, Mlela anaondoa hand break, anaweka gia kurudisha gari nyuma na kisha kuondoka, Rose anaenda getini na kubofya kitufe cha kengele, muda kidogo geti linafunguliwa na Nandi, binti mrembo, 20. Rose anaingia na kufunga geti.
NYUMBANI KWA ROSE NA MLELA-NDANI-USIKU.
Mlango unafunguka, anaingia Mlela, anabofya switch pale ukutani kuwasha taa, anashtuka kumuona Rose ameketi kochini ametulia kimya, “upo gizani?” anauliza Mlela, “ndio nipo gizani ndio maana nataka leo nijue ni nini kinaendelea kwa sasa Mlela maana mwenzangu sikuelewi” anasema Rose kwa sauti tulivu, “alafu saa hizi ni saa tano..na ulisema ungerudi mapema?” anauliza Rose, “nilipata kikao cha dharura” anasema Mlela huku akiketi kochini, mezani kuna hotpoti mbili, sahani na vijiko, Rose anachukua sahani na kijiko na kufungua hot poti, “mimi sitakula” anasema Mlela, Rose anabaki anamuangalia Mlela na kisha anashusha pumzi na kuifunga ile hotipoti, Mlela anachukua remote control ya TV iliyopo pale mezani na kuwasha TV, “kama huli basi naomba twende chumbani tukazungumze” anasema Rose, “naaangalia mechi kwanza” anasema Mlela huku akibofya remote mara kadhaa kabla ya kukutana na mechi ya mpira, anaiweka remote mezani, Rose anaangalia kwenye TV, “jamani hiyo mechi si ni marudio?” anasema Rose, “ndio..nataka nirudie kuangalia”, anasema Mlela, Rose anabakia akimuangalia Mlela kwa jicho kali, kisha anainuka na kuondoka, zinapita sekunde kadhaa, Mlela anainuka na kwenda meza iliyo pembeni na kuchukua chupa ya whisky na glasi, anamimina whisky kwenye glasi nusu na kurudi kuketi pale kochini, zinapita sekunde kadhaa huku akipiga funda kadhaa. Anapita Nandi na kumfanya Mlela kushtuka na kugeuka, kisha Mlela anainuka na kwenda alipoelekea Nandi.
NYUMBANI KWA ROSE NA MLELA-JIKONI-USIKU.
Nandi anafika pale jikoni kwenye sinki na kuanza kuosha vyombo, anakuja Mlela na kusimama mlangoni akiwa na ile glasi ya whisky mkononi, “mpaka saa hizi bado hujalala?” anauliza Mlela na kumfanya Nandi kushtuka na kugeuka kumuangalia Mlela, huku Mlela akiendelea kupiga funda ya whisky, “nilikuwa naangalia tamthilia” anasema Nandi, kisha Nandi anageuka na kuja mlangoni akitaka kutoka, Mlela anaziba mlango kumzuia, Nandi anamuona Rose akiwa amesimama nyuma ya Mlela, Nandi anajaribu kumpa Mlela ishara ageuke nyuma, Mlela anageuka nyuma na kumuona Rose, kisha anasogea kumpisha Nandi kutoka, Mlela na Rose wanabaki wanaangaliana kwa muda, kisha Rose anaondoka, Mlela anarudi na kuketi kochini na kuendelea kuangalia TV.
NYUMBANI KWA MLELA-CHUMBANI KWA NANDI-USIKU.
Nandi ameketi kitandani, Rose anaingia na kuketi pembeni ya Nandi pale kwenye kitanda, akiwa amejiinamia na macho yake yakiwa yamejaa machozi, “Nandi mdogo wangu” anasema Rose na kumfanya Nandi kushtuka na kubaki makini kumsikiliza Rose, “kuna nini kinaendelea kati yako na Mlela?” anauliza Rose, “hakuna chochote Dada” anasema Nandi, wanabaki kimya kwa muda, “mimi sio Mtoto Nandi..na kama kuna chochote nitajua tu Nandi...kwa hiyo usipoteze muda kunificha” anasema Rose kwa sauti tulivu lakini ya kusisitiza, “kweli Dada Rose hakuna chochote kinaendelea” anasema Nandi, Rose anashusha pumzi ndefu kisha anapanda kitandani pale na kujilaza, huku Nandi akibaki ameketi pale kitandani.
NYUMBANI KWA ROSE NA MLELA-SEBULENI-ASUBUHI.
Rose na Nandi wameketi kwenye meza ya chakula, Rose akiwa na simu mkononi akiibofya mara kadhaa huku Nandi akimuangalia kwa makini, “kwa nini hakuna kumbukumbu ya simu ulizowahi kupiga au kupigiwa?” Rose anauliza, “huwa sipendi tu kuzihifadhi”, anasema Nandi huku akiangalia chini na kumuacha Rose akibaki anamkodolea macho, wanabaki kimya kwa muda wa sekunde kadhaa, mara wanashtushwa na mlio wa ile simu kuita, Rose anaiangalia simu na kuonyesha mshtuko mkubwa usoni kwake, “Mungu hamfichi mnafiki Nandi” anasema Rose huku akimuonyesha namba inayoonekana kwenye simu, Nandi anabaki anaangalia huku akibaki kimya ameduwaa, “naomba upokee” anasema Rose huku akimpatia Nandi simu, Nandi anapokea na kutaka kuiweka sikioni, Rose anamshika mkono na kumzuia, anaichukua simu na kubofya kitufe na kuifanya simu kuwa kwenye mfumo wa loud speaker kisha anaiweka mezani, “hallow” inasikika sauti ya Mlela, “hallow” anajibu Nandi huku akionekana kuwa na uoga, “uko sawa?” sauti ya Mlela inauliza, “nipo sawa tu” anajibu Nandi, “huyo Kipepe ameshaondoka?” anauliza Mlela, Nandi anamuangalia Rose, Rose anampa ishara aseme ndio, “ameshaondoka” anasema Nandi, “ok nakuja unipe stori za nini kiliendelea jana” inasema sauti ya Mlela na kisha simu inakatika, Rose anabaki anamuangalia Nandi ambaye ameinamisha kichwa huku kaweka mkono shavuni, “kwa nini mnaniita Kipepe?” anauliza Rose, Nandi anabaki kimya kwa muda, “anasema zamani ulikuwa unapenda kufunga nywele zako kwa nyuma kama yule kipepe wa gazetini” anasema Nandi na kumfanya Rose kubaki ameduwaa kwa sekunde kadhaa machozi yakimlenga, anashusha pumzi “Nandi kweli mdogo wangu?” anasema Rose kwa sauti ya chini inayotetema kwa majonzi na jazba, “ulikuja na heshima zote..huna hili wala lile” anaendelea Rose, “Watu nje hata hawajui kama wewe ni dada wa kazi humu ndani kwa jinsi ninavyoishi na wewe kwa upendo?” anaendelea Rose huku akilengwa na machozi, “kweli haya ndio malipo yako?” anaendelea Rose huku Nandi bado amejiinamia, wanabaki kimya kwa muda, mara Nandi anainuka kwa haraka, Rose anashtuka na kumuangalia, Nandi anaondoka huku akionyesha dalili za kutaka kutapika.
NYUMBANI KWA ROSE NA MLELA-CHOONI.
Nandi anaingia chooni kwa kasi na kuinama kwenye sinki la choo na kuanza kutapika, Rose naye anafika na kusimama nyuma ya Nandi, “ni nini?” anauliza Rose huku akijaribu kumsaidia kwa kumshika mabegani, Nandi anaendelea kutapika kwa mara kadhaa kisha anatulia kwa sekunde kadhaa, “bado unajisikia vibaya?” anauliza Rose kisha anamuinua na kutoka naye nje.
NYUMBANI KWA ROSE NA MLELA-SEBULENI.
Nandi ameketi kochini, Rose anakuja na glasi ya maji na kumpatia, “bado unajisikia kichefuchefu?” anauliza Rose huku akimpatia Nandi ile glasi, “sasa nasikia afadhali” anajibu Nandi kwa sauti ya kichovu huku anapokea glasi na kupiga funda mara kadhaa, Nandi anashusha pumzi nzito huku akiiweka glasi mezani, wanabaki kimya kwa muda, “haya ngoja mimi niende umsubiri huyo mgeni wako” anasema Rose na kisha anaelekea mlangoni na kutoka.
SAKINA-MGAHAWANI-NJE.
Rose na Mai, dada wa makamo, 34, wameketi wote wakiwa na vikombe vya chai mbele yao, kimya kinatawala kwa muda, “au ananifanyia hivi kwa kuwa sijajaliwa kuzaa” anasema Rose kwa sauti ya kinyonge, “hakuna lolote Rose” anang’aka Mai akimkatiza Rose, “wangapi hawajapata Watoto na bado wanaheshimiana bana” anaongeza Mai, “anachofanya huyu Pimbi ni dharau za kipimbi tu” anasema Mai kwa sauti iliyojaa shari, wanabaki kimya kwa muda, “umedharau mwiba sasa mguu umeota tende Rose..nilikwambia umtoe yule binti pale kwako hukusikia” anasema Mai”, Rose anabaki kimya, “na yule Malaya atatoka pale ndani” anasema Mai na kumfanya Rose kuinua kichwa kumuangalia Mai, “kwa kosa lipi Mai?” anasema Rose na kumfanya Mai kugeuka na kumkata jicho kali, “mwenye kosa ni Mlela sio Nandi” anaongeza Rose, “hapo tu ndio huwa unanichefua Rose” anasema Mai, “jitu mpaka limebeba mimba ndani kwako bado huoni kosa lake?..tunaanza na yule Malaya kisha tunahamia kwa huyo Pimbi wako” anaendelea Mai, “Mai naomba mimi sitaki vurugu zisizo na maana” anasema Rose na kumfanya Mai abaki anamkata Rose jicho kali, “Pale mlipofika ni juhudi zako Rose” anasema Mai, “mchango wa yule Pimbi ni mdogo sana..wakuachie nyumba yako wakatafute kwa kuishi na huyo Malaya wake”anang'aka Mai kwa sauti kali huku anainuka “tena twende sasa hivi kwa huyo Malaya” anasema Mai na kumfanya Rose bado ameduwaa, “nyumba sio yangu naenda kumtoa” anasema Mai huku akichukua mkoba wake na funguo za gari pale mezani, “twende” Mai anamuamrisha Rose, “tukafanye nini haswa Dada Mai” anauliza Rose, “we twende” Mai anaamrisha huku akimshika Rose mkono na kumuinua na kumkokota kuelekea lilipo gari la Mai, Mai anafungua mlango wa gari na kuingia, Rose naye pole pole anaelekea upande mwingine wa gari na kuingia, Gari linaondoka.