Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,983
- 10,804
- Thread starter
- #61
SEHEMU YA 43 YA 50
“Lakini nina wazo mume wangu,” mama yake Mariam akamwambia mumewe.
“Wazo gani mama Mariam?”
“Tunahangaika na tutahangaika sana, lakini ipo njia moja tu tunayopaswa kuitumia!”
“Ipi?”
“Tumesahau kumuomba Mungu, nakuhakikishia kama tukimshirikisha yeye kila kitu kitakuwa sawa, ni lazima tuwe karibu na Mungu baba Mariam.”
“Ni kweli, tumefanya kosa kubwa sana mke wangu, hatuna haja ya kupoteza muda, tunatakiwa kuanza kusali sasa hivi.”
“Haya simama tuombe mume wangu.” Wote wakasimama, kisha wakashikana mikono, mama Marim akaongoza sala.
Walianza na nyimbo za kuabudu, ambazo waliimba kwa robo saa kabla ya kuingia kwenye maombi yaliyowachukua saa nzima! Kila mmoja alikuwa akimuomba Mungu wake, amuepushie Mariam kwenye mateso na shida zote na hata kama alikuwa na mawazo mabaya ambayo yalikuwa yanateka akili yake, yashindwe!
“Katika jina la Yesu Kristo wa Nazareth tumeomba na kushukuru...”
“Aaamen...” baba Mariam akaitikia.
“Mungu ndiyo kila kitu mume wangu, nakuhakikishia tutaona majibu yake, Mungu wetu siyo mwongo, maana yeye mwenyewe tumuombe naye atatujibu, hawezi kutoa ahadi ya uongo, lazima atatujibu tu, lazima.”
“Ni kweli mke wangu, twende chumbani tukalale.”
Wakaongozana hadi chumbani kulala, angalau sasa mioyo yao ilikuwa na amani baada ya kufanya maombi.
*******
“Acha!” Mariam alisikia sauti hiyo ambayo hakuelewa ilitokea wapi.
Alihisi alikuwa ndotoni, hivyo akapuuza, akaamua kuipandisha glasi yake hadi kinywani, akiwa anataka kuanza kunywa, ghafla akahisi mkono wake ukitetemeka kwa kasi, ukazidisha kasi hadi glasi ikaanguka chini.
Mariam hakuelewa kilichotokea, chumba kizima kikawa kinanuka harufu ya sumu ya panya. Ilikuwa harufu mbaya sana, Mariam alichanganyikiwa, hakujua kwanini jambo lile lilitokea, alichoamua kwa muda huo, ilikuwa ni kurudi tena dukani na kununua sumu nyingine ili aweze kuendelea na zoezi lake.
Akiwa ndiyo anataka kufungua mlango ili atoke nje, akashangaa miguu yake inakuwa mizito, sauti nyingine tena ikasisika, tena kwa sauti ya juu na ya msisitizo zaidi; “Wewe ni msichana mzuri sana, unayevutia na ambaye una mpenzi mzuri sana, siyo kweli kwamba baada ya kufa utakuwa umekimbia matatizo, achana na mawazo hayo.
“Unachotakiwa kufanya sasa ni kwenda kwa wazazi wako, uwaangukie na kuwaomba radhi, bado una nafasi ya kuendelea kuishi. Mariam badili uamuzi wako...” Mariam alizidi kuchanganyikiwa, hakuweza kuelewa ilikuwa sauti ya nani na wapi ilipotokea.
Katika hali ambayo hata yeye mwenyewe hakuitegemea, alijikuta akiahirisha kujiua, moyo wake ukawa umekunjamana na kuhisi uhitaji wa radhi za wazazi wake.
“Lazima nirudi nyumbani, lazima tena usiku huu huu wa leo,” Mariam akawaza na kuchukua begi lake dogo lililokuwa na nguo zake chache kisha akafunga chumba na kushuka hadi chini ambapo aliingia kwenye taxi.
“Wapi sister?”
“Jeti, Lumo!”
“Poa.” Dereva akawasha gari na safari ya kwenda nyumbani kwa wazazi wake ikaanza.
Kwa kuwa hakukuwa na foleni, dakika ishirini zilitosha kabisa kutoka Magomeni Mapipa katika hoteli aliyokuwa akiishi hadi Jeti, Lumo. Tayari ilikuwa imeshafika saa saba kasoro za usiku. Kwa bahati nzuri, nyumba yao ilikuwa barabarani, hivyo alimlipa dereva akashuka na kuanza kugonga geti.
Muda mfupi baadaye baba yake akafika getini.
“Nani usiku wote huu?”
“Ni mimi baba!”
“Mariam!”
“Ndiyo!”
“Karibu mwanangu, ngoja nikufungulie!” Mlango ukafunguliwa na Mariam akaingia.
Mapokezi aliyokutana nayo hakuyategemea kabisa, baba yake akampokea begi na kuingia naye hadi ndani ambapo alimwita mama Mariam ambaye hakuamini kilichokuwa mbele yake.
“Mariam ni wewe mwanangu? Karibu nyumbani mama...” mama yake alisema huku machozi yakianza kumlengalenga.
“Ahsante sana mama, nawaombeni msamaha wazazi wangu, najua ni kiasi gani nimewavunjia heshima, nimewakosea adabu na hata kuwadhalilisha mbele ya jamii. Nawaahidi nitakuwa mtoto mwema kwenu, naachana na mambo yote ya kale na sasa naanza upya maisha yangu.
“Kama siyo Mungu, kesho mngepata taarifa za kifo changu, tayari nilikuwa na sumu ambayo niliitayarisha kwa ajili ya kujiua, nikasikia sauti ya ajabu ikiniambia niache, hapo ndipo nilipoamua kurudi kwenu wazazi wangu.
“Naamini mkinisamehe na kunibariki nitaishi maisha mapya,” Mariam alikuwa akisema huku akilia. Mama yake naye alikuwa akilia sana, maneno ya mwanaye yalikuwa makali sana na hakuamini kuwa mwanaye alipitia mateso makali kiasi kile.
“Mwanangu, sisi tumekwishakusamehe siku nyingi sana, huna haja ya kuwa na wasiwasi juu ya hilo,” baba yake Mariam akasema.
“Nashukuru kusikia hivyo wazazi wangu, lakini nilikuwa na ombi moja ambalo nawaomba sana mnikubalie!”
“Ombi gani mwanangu, we sema tu!”
“Naomba mniahidi kwanza kuwa mtanikubalia!”
“Sema tu!”
“Au basi, tuache tu...” Mariam akasema akionekana kuwa na wasiwasi sana.
“Akha! Kwanini tena.”
“Basi tu!” Mariam akaanza kulia, tena kwa sauti ya juu kama ambaye alikuwa amefiwa.
Wazazi wake walishindwa kuelewa alikuwa na tatizo gani kubwa kiasi cha kushindwa kusema. Vichwa vyao vikawaka moto, mwenye siri hiyo alikuwa ni Mariam mwenyewe.
Furaha waliyokuwa nayo wazazi wa Mariam ilikuwa haielezeki, lakini sasa ilianza kuyeyuka taratibu. Kutokuwa na mwanao kwa muda mrefu kiasi kile tena wakiwa hawafahamu mahali alipo lilikuwa pigo kubwa sana kwao, lakini kilichowachanganya zaidi vichwa vyao ni Mariam kusema ana jambo alilotaka kuwaomba wazazi wake lakini ghafla anakataa.
“Lakini nina wazo mume wangu,” mama yake Mariam akamwambia mumewe.
“Wazo gani mama Mariam?”
“Tunahangaika na tutahangaika sana, lakini ipo njia moja tu tunayopaswa kuitumia!”
“Ipi?”
“Tumesahau kumuomba Mungu, nakuhakikishia kama tukimshirikisha yeye kila kitu kitakuwa sawa, ni lazima tuwe karibu na Mungu baba Mariam.”
“Ni kweli, tumefanya kosa kubwa sana mke wangu, hatuna haja ya kupoteza muda, tunatakiwa kuanza kusali sasa hivi.”
“Haya simama tuombe mume wangu.” Wote wakasimama, kisha wakashikana mikono, mama Marim akaongoza sala.
Walianza na nyimbo za kuabudu, ambazo waliimba kwa robo saa kabla ya kuingia kwenye maombi yaliyowachukua saa nzima! Kila mmoja alikuwa akimuomba Mungu wake, amuepushie Mariam kwenye mateso na shida zote na hata kama alikuwa na mawazo mabaya ambayo yalikuwa yanateka akili yake, yashindwe!
“Katika jina la Yesu Kristo wa Nazareth tumeomba na kushukuru...”
“Aaamen...” baba Mariam akaitikia.
“Mungu ndiyo kila kitu mume wangu, nakuhakikishia tutaona majibu yake, Mungu wetu siyo mwongo, maana yeye mwenyewe tumuombe naye atatujibu, hawezi kutoa ahadi ya uongo, lazima atatujibu tu, lazima.”
“Ni kweli mke wangu, twende chumbani tukalale.”
Wakaongozana hadi chumbani kulala, angalau sasa mioyo yao ilikuwa na amani baada ya kufanya maombi.
*******
“Acha!” Mariam alisikia sauti hiyo ambayo hakuelewa ilitokea wapi.
Alihisi alikuwa ndotoni, hivyo akapuuza, akaamua kuipandisha glasi yake hadi kinywani, akiwa anataka kuanza kunywa, ghafla akahisi mkono wake ukitetemeka kwa kasi, ukazidisha kasi hadi glasi ikaanguka chini.
Mariam hakuelewa kilichotokea, chumba kizima kikawa kinanuka harufu ya sumu ya panya. Ilikuwa harufu mbaya sana, Mariam alichanganyikiwa, hakujua kwanini jambo lile lilitokea, alichoamua kwa muda huo, ilikuwa ni kurudi tena dukani na kununua sumu nyingine ili aweze kuendelea na zoezi lake.
Akiwa ndiyo anataka kufungua mlango ili atoke nje, akashangaa miguu yake inakuwa mizito, sauti nyingine tena ikasisika, tena kwa sauti ya juu na ya msisitizo zaidi; “Wewe ni msichana mzuri sana, unayevutia na ambaye una mpenzi mzuri sana, siyo kweli kwamba baada ya kufa utakuwa umekimbia matatizo, achana na mawazo hayo.
“Unachotakiwa kufanya sasa ni kwenda kwa wazazi wako, uwaangukie na kuwaomba radhi, bado una nafasi ya kuendelea kuishi. Mariam badili uamuzi wako...” Mariam alizidi kuchanganyikiwa, hakuweza kuelewa ilikuwa sauti ya nani na wapi ilipotokea.
Katika hali ambayo hata yeye mwenyewe hakuitegemea, alijikuta akiahirisha kujiua, moyo wake ukawa umekunjamana na kuhisi uhitaji wa radhi za wazazi wake.
“Lazima nirudi nyumbani, lazima tena usiku huu huu wa leo,” Mariam akawaza na kuchukua begi lake dogo lililokuwa na nguo zake chache kisha akafunga chumba na kushuka hadi chini ambapo aliingia kwenye taxi.
“Wapi sister?”
“Jeti, Lumo!”
“Poa.” Dereva akawasha gari na safari ya kwenda nyumbani kwa wazazi wake ikaanza.
Kwa kuwa hakukuwa na foleni, dakika ishirini zilitosha kabisa kutoka Magomeni Mapipa katika hoteli aliyokuwa akiishi hadi Jeti, Lumo. Tayari ilikuwa imeshafika saa saba kasoro za usiku. Kwa bahati nzuri, nyumba yao ilikuwa barabarani, hivyo alimlipa dereva akashuka na kuanza kugonga geti.
Muda mfupi baadaye baba yake akafika getini.
“Nani usiku wote huu?”
“Ni mimi baba!”
“Mariam!”
“Ndiyo!”
“Karibu mwanangu, ngoja nikufungulie!” Mlango ukafunguliwa na Mariam akaingia.
Mapokezi aliyokutana nayo hakuyategemea kabisa, baba yake akampokea begi na kuingia naye hadi ndani ambapo alimwita mama Mariam ambaye hakuamini kilichokuwa mbele yake.
“Mariam ni wewe mwanangu? Karibu nyumbani mama...” mama yake alisema huku machozi yakianza kumlengalenga.
“Ahsante sana mama, nawaombeni msamaha wazazi wangu, najua ni kiasi gani nimewavunjia heshima, nimewakosea adabu na hata kuwadhalilisha mbele ya jamii. Nawaahidi nitakuwa mtoto mwema kwenu, naachana na mambo yote ya kale na sasa naanza upya maisha yangu.
“Kama siyo Mungu, kesho mngepata taarifa za kifo changu, tayari nilikuwa na sumu ambayo niliitayarisha kwa ajili ya kujiua, nikasikia sauti ya ajabu ikiniambia niache, hapo ndipo nilipoamua kurudi kwenu wazazi wangu.
“Naamini mkinisamehe na kunibariki nitaishi maisha mapya,” Mariam alikuwa akisema huku akilia. Mama yake naye alikuwa akilia sana, maneno ya mwanaye yalikuwa makali sana na hakuamini kuwa mwanaye alipitia mateso makali kiasi kile.
“Mwanangu, sisi tumekwishakusamehe siku nyingi sana, huna haja ya kuwa na wasiwasi juu ya hilo,” baba yake Mariam akasema.
“Nashukuru kusikia hivyo wazazi wangu, lakini nilikuwa na ombi moja ambalo nawaomba sana mnikubalie!”
“Ombi gani mwanangu, we sema tu!”
“Naomba mniahidi kwanza kuwa mtanikubalia!”
“Sema tu!”
“Au basi, tuache tu...” Mariam akasema akionekana kuwa na wasiwasi sana.
“Akha! Kwanini tena.”
“Basi tu!” Mariam akaanza kulia, tena kwa sauti ya juu kama ambaye alikuwa amefiwa.
Wazazi wake walishindwa kuelewa alikuwa na tatizo gani kubwa kiasi cha kushindwa kusema. Vichwa vyao vikawaka moto, mwenye siri hiyo alikuwa ni Mariam mwenyewe.
Furaha waliyokuwa nayo wazazi wa Mariam ilikuwa haielezeki, lakini sasa ilianza kuyeyuka taratibu. Kutokuwa na mwanao kwa muda mrefu kiasi kile tena wakiwa hawafahamu mahali alipo lilikuwa pigo kubwa sana kwao, lakini kilichowachanganya zaidi vichwa vyao ni Mariam kusema ana jambo alilotaka kuwaomba wazazi wake lakini ghafla anakataa.