Simuliza: Jestina

Simuliza: Jestina

RIWAYA: JESTINA
MTUNZI: Tariq Haji
CONTACT: 0624065911

SEHEMU YA 11

"unajua mke wangu Alwin kabadilika sana siku hizi" aliongea Mr Kelvin kumwambia mkewe, "kivipi mbona mi namuona yupo kawaida tu. "hapana mke wangu mi nakwambia tena Alwin kabadilika sana tokea atoke hospitali ya vichaa" alisitiza Mr Kelvin. "mhh haya lakini mi namuona kawaida tu isipokuwa siku hizi kachangamka sana tafauti na zamani" aliongea mama Alwin huku akiachia tabasamu akionesha kufurahishwa na mabadiliko ya Alwin. Wakati wakiendelea kuongea Alwin aliingia na kuwasalimia, waliitika kwa pamoja na baadae Alwin akaenda zake chumbani kwake.


Kwa upande wa inspecta Hans baada ya kutoka kwenye kikao alikwenda nje na kutulia huku akili ikitafakari mengi sana, akiwa dimbwi hilo la mawazo aliskia akiitwa na alipogeuka alikutana na mkuu wake wa kituo inspecta Brandon. "nifuate ofisini" aliongea na kuondoka, bila kusita aliinuka nae akamfuata nyuma mpaka walipofika ofisini. "bwana mdogo chunga kauli zako" hayo ni maneno ya kwanza yaliotoka kinywani mwa inspecta Brandon, "wewe hapa kituoni unaongea vile kama nani" aliendelea kuongea kwa hasira. "samahani mkuu, ule ndio ukweli we unadhani dunia bila haki ipo sawa. Hata waliokufa nao wanataka haki zao, we ulielewa fika kama Matt na wenzake wako hatiani lakini ukaibaitilisha kesi na kumuuzia Alwin. Natamani huo mzimu siku moja ukutembelee na wewe uone machungu ya kudhulumiwa" alijibu inspecta Hans bila woga wowote ule. "sasa unaonekana umeota mapembe si ndio" aliongea inspecta Brandon, "kama ndivyo unavofikiri sawa tena makubwa sana" alijib inspecta Hans na hakusubiri neno jingine kutoka kwa mkuu wake aliondoka maana hata yeye hasira zilishaanza kumpanda. Alimuacha mkuu wake akiwa ni mwenye mawazo tele lakini akaona bora apotezee tu.


Kifo cha Jesca kiliwachanganya wengi miongoni ya waliotenda kosa lile, wapo walioomba usiku usiingie maana walijua Jestina hufanya mauaji yake usiku. Lakini kwa vile hatuwezi kuzuia masaa basi muda uliyoyoma na hatimae kiza kikaana kutanda angani, hatiame usiku uliingia lakini kulikua na mvua kali sana iliondamana na ngurumo pamoja na radi. Usiku huo ulivo ulitosha kuwatisha wengi sana, Mark ndo alikuwa akitoka zake mihangaikononi kwake kuelekea nyumbani kwao ghafla akiwa njiani umeme ukazima.


Hali hiyoilimshtua kidogo Mark lakini akajipa moyo kuwa ameshaakaribia nyumbani kwao, hivyo basi alianza kukazana huku akiangalia pande zote kama kuna kitu ama mtu anamfuata. Nyumba yao ilikuwa imejitenga kidogo kutoka katika makazi ya wtu wengine, aliacha njia kubwa na kuingia njia ndogo ambayo ilikuwa nampeleka mpaka kwao. Wakati akikazana kwa mbali mbele yake akaona kama mtu kapita mbio. Moyo ulianza kumuenda mbio maana alishaanza kuziona dalili za mauzauza, akiwa anatetemeka ghafla alihisi kama kitu kimepita nyuma yake. Aligeuka kwa kasi lakini hakuona kitu, alipogeuka tena mbele kwa mbali akaona mtu akiwa anakuja upande wake taratibu . Kidogo alipata matumaini na kuanza kukazana kumfata yule mtu. Lakini alivomkaribia mwili ulimsisimka na kuhisi kama hakuwa mtu wa kawaida lakini alipiga moyo konde na kunyongea kwa mendo wa haraka. Ghafla tochi yake ilizima, na ilivowaka alikutana sura ya ajabu sana mbele yake. Aliruka na kuiangusa tochi pembeni, japo kulikuwa na baridi lakini kijasho kilianza kumtoka kwa wingi. "maumivu...." alisikia sauti ikitamka neno hilo kwa sauti a kuning'ona, "leo utahisi maumivu nilioyapata" sauti hiyo iliendelea kuongea huku ikizidi kuwa kali. "unataka nini lakini" aliuliza Mark kwa woga, "nataka roho yako" alijibiwa na wakati huu sauti aliifahamu vizuri sana kama ilikuwa sauti ya Jestina.


Aliokota tochi yake na kuanza kukimbia, lakini hakufika mbali alishtukia akichezea kofi zito la uso lililomfanya aanze kuona mawenge kidogo na kuanguka chini. Mark alijua kuwa huo ndio ulikuwa mwisho wake, "nisamehe Jestina" alianza kuomba msamaha kwa kilio huku damu zikimoka mdomoni. "leo unalia mshenzi mkubwa wewe, siku ile ulikuwa ukicheka" Jestina aliongea na kumnyanyua Mark. Sasa alifanikiwa kumuona uso kwa uso, macho yalimtoka Mark asijue nini la kufanya. Wakati akiendelea kutumbua macho alirushwa kwa nguvu, kabla hajakaa sawa alichezea makucha kadhaa ya mgongo na kumfanya apige kelele za maumivu. "nimekoma naomba unisamehe" aliongea huku akisimama, "nikusamehe kweli, hivi unajua ni maumivu kiasi gani niliyapata siku ile" Jestina alijibu na kumtokea Mark mbele na kumkaba, kisha sura yake ilianza kubadilika na kuwa ya kutisha sana huku damu nyingi zikichuruzika kutoka machoni mwake kama machozi. Mabadiliko hayo yaliambatana na harufu kali sana ya kuoza, kwa nguvu alimpiga Mark na chini kiasi cha kushndwa kuinuka. "leo utakiona cha moto mpumbavu mkubwa wewe" aliongea Jestina na kisha akamfungua mdomo Mark na kumtia funza. Yeye alikaa pembeni akimuangalia kwa jinsi funza wanavomteketeza Mark. Hawakuwa funza wa kawaida kwani punde baada ya kutiwa mdomoni walianza kutoboa sehemu mbalimbali za mwili wa Mark na kusababisha maumivu makali sana. Mark alipiga sana kelele lakini hakuna msaada wowote alioupata mpaka mwisho alitulia tuli na kuaga dunia. Jestina alipotea eneo hilo akiacha ujumbe wake wa kawaida.


Asubuhi taarifa ya kwanza ilikuwa ni kifo cha Mark, huku ikisema bado mauaji hayo hajulikani yanasababishwa na nani. Lakini kilichowashtua watu ni kwamba wote waliokufa walikuwa ni marafiki tokea zamani sana, hivo kukaibua maswali mengi sana. Kituo kimoja cha televisheni kiliomba kufanya mahojiano na mwalimu mkuu wa shule ambayo inaaminika kuwa wote waliokufa wamesoma pale.

"habari yako mwalimu"
"nzuri nashkuru"
"kwa jina naitwa Anita ni mwandishi wa habari kutoka J76 news chanel"
"mimi naitwa Anthon Dickson, ni mwalimu mkuu hapa"
"naam mwalim unazungumziaje matukio haya ya mauaji yanayoendelea hapa mjini hasa ukizingatia wote walipoteza maisha mpaka sasa ni wananfunzi wako"
"kwa kweli ni vigumu kueleza"
"kivipi mwalimu"
"unajua ndugu Anita hapa kulitokea kesi kubwa sana ya ubakaji kama utakuwa unakumbuka, ni takriban miaka kumi sasa imepita na inavosemekana kuna wananfunzi wamehusika na tukio hilo"
"unaweza kuwataja"
"hapana siruhusiwi kufanya hivo"
"na kwanini hasa ukawa unahisi kama mauaji yanayofanyika sasa ya uhusiano wowote na kilichotokea miaka kumi nyuma"
"Unajua tulivokuwa wadogo, tulikuwa tukisimuliwa mambo mengi sana ambayo wengi wetu hatuyaamini"
"kama yapi"
"kwa mfano najua utakuwa umesimuliwa kuhusu ulimwengu wa watu waliodhulumiwa"
"ndio lakini hizo ni hadithi za kufikirika tu"
"hapo ndio kwenye utata sasa na hilo ndilo linalotokea saa hivi, baada kufanyika tukio lile kesi ilipelekwa mahakamani lakini cha ajabu ilizimwa haraka na watuhumiwa wakaacha huru, kwa sababu haki haikupatikana, sasa aliedhulumiwa amerudi kuja kuitafuta haki kwa mikono yake kama tunavojua HAKI ISIPOPATIKANA KWA AMANI BASI ITAPATIKANA KWA VITA. Na hii ni vita ambayo hakuna mtu yoyote kati yetu anaeweza kuizua na kama huamini kama mizimu ipo heebu jaribu siku moja kuuwa halafu uachiwe huru uone kama hutokipata walichokipata hawa vijana walikufa"


Mwalimu mkuu alimaliza kuongea na kuomba kuondoka akaendelee na majukumu mengine ya kawaida. Na kwa sababu kipindi hicho kilikuwa hewani live kila mtu alishuhudia, "ni bora wafe tu ili watu wajue kama haki ya mtu ni mali", "pumbavu nani atakaa aamini upumbavu ule". "mmmh makubwa mi nlijua ni hadithi tu za kufikirika", hayo ni baadhi ya maneno yaliokuwa yakisemwa na baadhi ya watu kila pahali. Kwa kweli story ilikuwa ni hiyo tu kila kona unayopita, Alwin ni miongoni mwa watu waliokiona kipindi hicho na kufurahia sana majibu ya mwalimu, yalitosha kupeleke ujumbe kwa wote ambao wanacheza na haki za watu.


"jamani hali imezidi kuwa mbaya sasa" Jay aliongea katika kikao kifupi cha dahrura kilichoitisha baada ya kifo cha Mark. "sasa tunafanyaje" aliuliza Monica, "ah hatuna la kufanya, sisi tulitenda uovu huku tukifurahia bila kufikiria ni kiasi gani tulichowaumiza wengine" Jay aliongea akionekana kujuta sasa. "akah! we vipi sasa unajuta nini, mi nasema hapa cha msingi ni kumuua Alwin maana nahisi yeye ndie anetufanyia mchezo huu" alifoka Alex kwa hasira. "sasa umeona ulivokuwa huna akili unataka kurekebisha kosa moja kwa kutenda jingine" Jay alimjibu akionekana kuchukizwa na maneno ya Alex. "mi nlikwambieni huyo boya ni mtoto wa mama" aliongea Alex na kumkejeli Jay, "sawa mi ni mtoto wa mama, lakini mi naona bora tujiandae kufa tu maana hatujui anefuata ni nani" Jay aliongea na kuinuka kisha akaanza kutoka nje, "nenda huko na leo utakufa wewe, Jestina kama unanisikia leo Jay amejianda ukamuue sawa" aliongea Alex na kufanya mzaha.


Jay hakujibu kitu,wakati anatoka aliingia unyonge wa ghafla na kupatwa na homa kali sana iliomfanya aanguke barabarani. Wasamaria wema walipiga simu hospitali na punde gari ya kubebea wagonjwa ilifika na kumuawahisha hospitali. Alipofika tu alipatiwa huduma ya kwanza na kupelekwa chumba cha wagonjwa mahututi kutokana na hali yake kuwa mbaya sana. Familia yake ilifka akiwemo mkewe na mwanae wa kike mwenye umri wa miaka minne, lakini hawakuruhuisiwa kumuona kutokana na kuwa hali yake haikuwa nzuri. Hali hiyo ilimtia simanzi mkewe kumuona mumewe yupo katika hali mbaya sana lakini angefanyaje na alitakiwa kusubiri.


Walisubiri mpaka jioni lakini hali yake haikuchanganya hico wakaambiwa waondoke na warudi kesho kwa ajili ya kumuangalia walikubaliana na daktaru na kuondoka. Kiza kilianza kuingia lakini bado hali ya Jay haikutengemaa kabisa "kwa kweli tumejaribu kadri ya uwezo wetu sasa ni muda wa kumuachia Mungu atende muujiza" aliongea daktari mmoja na wenzake wakamuunga mkono. Walizima vifaa vyote na kumuhamisha chumba, huko walimuunganisha na mashine ya kupumulia kwa ajili ya msaada maana hata pumzi ilikuwa ni ngumu kuvuta. Baada ya hapo walitoka wote na kumuacha chini ya uangalizi wa manesi.

ITAENDELEA.
 
RIWAYA: JESTINA
MTUNZI: Tariq Haji
CONTACT: 0624065911

SEHEMU YA 12.

Walisubiri mpaka jioni lakini hali yake haikuchanganya hico wakaambiwa waondoke na warudi kesho kwa ajili ya kumuangalia walikubaliana na daktaru na kuondoka. Kiza kilianza kuingia lakini bado hali ya Jay haikutengemaa kabisa "kwa kweli tumejaribu kadri ya uwezo wetu sasa ni muda wa kumuachia Mungu atende muujiza" aliongea daktari mmoja na wenzake wakamuunga mkono. Walizima vifaa vyote na kumuhamisha chumba, huko walimuunganisha na mashine ya kupumulia kwa ajili ya msaada maana hata pumzi ilikuwa ni ngumu kuvuta. Baada ya hapo walitoka wote na kumuacha chini ya uangalizi wa manesi.


"Jay.....amka" alisikia sauti ikimuamsha huku akitingishwa, kwa uvivu alifungua macho na mbele yake alikuwa Jestina amesimama akiwa na sura yake ya kawaida, sio ile ya kutisha. "najua umekuja kulipiza" aliongea Jay huku akiitoa mashine ya kupumulia, "lakini nina ombi moja tu kwako, naomba uniache mpaka kesho angalau nimuone mwanangu kwa mara ya mwisho kabla ya kuaga dunia" aliongea Jay kwa masikitiko makubwa. "kwanini ulikubali kushuhudia unyama ule" aliuliza Jestina huku uso wake ukianza kubadilika na kuwa wa kutisha. "kwa kweli siku ile sikutegemea kama kungetokea tukio kama lile" alijibu Jay kiunyonge, "lakini wakati linafanyika ulikuwa na uwezo wa kuzuia lisifanyika" aliongea Jestina akizidi kutisha. "hilo ndio linalonijutisha mpaka leo" aliongea Jay huku machozi yakianza kumtoka, "najua kama nimekukosea na niko tayari kulipa kwa nilolitenda, lakini naomba unipe siku moja tu japo nimuone mwanangu na mke wangu kisha njoo unimalize" Aliendelea kuongea Jay huku kilio kikipamba moto, alijaribu kujifuta lakini aliposusha mkono Jestina alikuwa kashaatoweka. "asante kwa kunikubalia ombi langu" aliongea huku akijiweka vizuri kitandani na kuendelea kulala.


Asubuhi mapema familia yake ilifika kumuona, "nini kimekusibu baba Sophia" aliongea mkewe huku akimuangalia kwa huruma, "hata mimi mwenyewe sijui, homa tu ilinishika ghafla" alijibu huku akilazimisha kutabasamu. "pole mume wangu" aliongea mkewe kumpiga busu katika paji la uso, "pole dady utapona" sauti ya Sophia iliskika huku akimpa pipi baba yake. Sophia alikuwa kafanana sana na baba yake, na alimpenda sana. "Sophia baby njoo nkwambie kitu" Jay alimuita mwanae na kumnong'oneza kitu, Sophia alitabasamu na kumrukia baba yake kisha akasema " wewe ni baba mzuri kuliko wote". Muda wa kutizama wagonjwa uliisha na familia yake iliaga na kuondoka huku wakiahidi kurudi kesho yake kwa ajili ya taratibu za kwenda nae nyumbani. Aliagana nao huku machozi yakimtoka maana alielewa hiyo ilikuwa ni siku yake ya mwisho duniani. Kutokana na hali yake kuimarika mashine za msaada wa kupumua ziliondolewa na kupelekwa chumba cha wagonjwa wa kawaida tu. Aliendelea kupata matibabu madogomadogo, lakini akilini mwake alikuwa akiwaona kama madaktari wanatwangaa maji kwenye kinu maana usiku wa siku hiyo ni usiku wa kifo chake.


Usiku hatimae ulifika na Jay alikuwa tayari kwaajili ya kufa tu maana alielewa kabisa ni aina gani ya mauaji anayofanya Jestina. "Jay, naona uko tayari kwa adhabu yako" alimsikia Jestina akimwambia wakati akiwa amepumzika. "ndio niko tayari kwa chochote" alijibu Jay huku akitetemeka, "Kwa vile umelitambua kosa lako na kulijutia, mimi sikuja hapa kukuuwa maana kwanza una mke anaekuthamini sana na pili una mtoto ambae bado anahitaji malezi yako na upendo wako kama baba yake" aliongea Jestina na kujitokeza mbele ya Jay akiwa katika umbile la kibinaadamu "lakini nataka ufanye kitu kimoja, usijaribu kutoa ushahidi kokote pale na pia nakupa siku tatu uondoke Mashvile na familia yako yote, nenda mbali sana na uwe baba mwema kwa mwanao na pia mume mwema kwa mkeo. Na jengine asijue hata mmoja miongoni mwa marafiki zako waliohusika na kifo changu. Mimi nimekusamehe na nakutakia maisha mema na yenye amani tele lakini kumbuka ukitovukwa adabu nitakurudia" alimaliza kuongea Jestina na kuoweka. Jay hakuamini kama kasamehewa maana alielewa kabisa kuwa Jestina alikuwa hataki masihara, alilala usingizi mzuri huku akijiapiza kufanya yote aliyoambiwa.
*******************
Mapema siku ya iliyofuata familia yake ilifika na taratibu za kutoka hospitali zikafanyika, baada ya kufika kwake alimueleza mkewe kuwa anataka kuhama Mashvile kwani amepata kazi nzuri nchini Italy. Aliwaeleza pia wazazi wake swala hilo na kwa vile yeye ndie aliekuwa analisha familia hakuna aliempinga, maandalizi ya safari yalifanyika kimya kimya bila hata rafiki yake mmoja kujua. Jioni yalikuwa yamekamilika na wote waliondoka mjini Mashvile "nakuahidi Jestina nitatekeleza yote ualionambia" aliongea maneno hayo kimoyomoyo wakati analipita bango liliandikwa KWA HERI MASHVILE.


"Oya Alex mtu wangu mbona tokea jana sijamsikia Jay" Patrick alimuuliza Alex ambae alikuwa bize akijaribu kumchora mwanadada mmoja ambe alionekana kudance vizuri sana, "ah mara mwisho niliskia kalazawa hospitali, lakini nahisi Jestina atakua kashampitia tayari" alijibu Alex na kuinuka kulekea katika ulingo wa kudance lakini nia na madhumuni yake ilikuwa ni kwa ajili ya yule mschana. "habari yako mrembo"
"safi tu"
"Mimi naitwa Alex sijui mwenzangu"
"ahaa mimi naitwa Jessie"
"jina lako zuri, tunaweza tukasogea pembeni tukaongea mawili matatu"

"hamna shida"
basi walisogea mpaka counter na Alex akaagiza vinywaji kisha wakaanza kuongea, waliongea sana mwisho walionekana kukubaliana "oya Patrick wacha mi nitoke na shemeji yako" Alex alimuita Patrick na kumwambia, "oya mwanangu mtoto huyo mkali, kama vipi tupige tungo" Patrick alimnong'oneza Alex. "tulia mtu wangu mi naenda nae geto nikimaliza kula asali na kutwangia na wewe uje kuonja mtu wangu" aliongea na wakakubaliana.


Patrick alirudi kwenye dance floor huku Alex akiondoka na Jessie, "tunaenda wapi sasa" aliuliza Jessie, "ah nyumbani kwangu si mbali na hapa" alijibu Alex na kuzungusha mkono wake kwenye nyonga ya binti huyo. Mwendo ulikwa wa dakika tano tu hatimae walifika geto na kumkaribisha ndani. "kaa kitandani hapo nakuja" aliongea Alex na kuingia chooni, kumbe alikwenda kutega camera ili ajirikodi anavomkuna mrembo huyo. Alirudi na kumkuta tayari ameshavua nguo na kubakia mtupu, tamaa ya ngono ilimpanda Alex kujikuta anamvamia lakini kabla hajafikisha mdomo wake kwenye midomo ya mrembo huyo alijikuta akirushwa kwa nguvu.


Ghafla mrembo huyo alianza kubadilika, naam hakuwa mwengine isipokuwa Jestina. "wewe hujabadilika hata kidogo" aliongea kwa nguvu sana, "yaani bado wewe na yule mshenzi mwenzako mlikuwa mnafikiri kupiga mtungo" aliendele kuongea huku akimsogelea. "Jestina nisamehe" alianza kuomba msamaha, "umechelewa sana" alijibu Jestina na kupiga kofi la uso akimwachia alama za kucha. Alex aliweweseka lakini alipofungua macho hakumuona ila ghafla akamtokea kwa nyuma na kumchana mgongoni. Alex alipiga yowe la kuomba msaada lakini wapi hakuna lolote lilisikilikana nje ya chumba hicho. Jestina akatoweka tena na kumtokea mbel yake ila hakumgusa alimuangalia tu usoni na Alex mwenyewe akaokota kipande cha kioo na kunaza kujichana. Alipiga kelele kwa maumivu lakini alishindwa kujizuia mwisho alianguka chini, hapo Jestina alimsogelea na kumpiga kucha za shingo na kulitoa koromeo, aliacha ujumbe na kutoweka huku Alex akiwa chini akijaribu kuvuta pumzi ambayo haikua na pakupita mpaka mwisho akakata roho. Patrick baada kuona Alex hapigi simu aliamu kutoka na kumfata geto.


Kwa mwendo wa haraka Patrick alifka geto kwa Alex na kukuta mlango umefungwa lakini kila alipojaribu kugonga haukufunguliwa. Alisubiri kama dakika kumi kumi hivi ila bado kulikuwa kimya, mwisho alikumbuka kuwa ana ufunguo mwengine wa mlango huo lakinialipojaribu kuingiza kwenye kitasa uligoma hiyo ilikuwa ni ishara kuwa kulikua na ufunguo mwingine kwa ndani. Baada kuona jitihada zake zimegonga mwamba aliamua kutoa simu yake na kuandika ujmbe "poa mshkaji wangu tumekubaliana vipi na wewe unafanya nini, mbona mimi nikipata kama hivo tunapiga mtungo safi ila haina noma" aliutuma na kuondoka. Aliondoka na kuelekea nyumbani kwao, baada kufika alivua nguo zake na kwenda kujimwagia maji. Alimaliza na kutoka kurudi chumbani na hapo ndipo aliposhtuka kidogo maana suruali yake chini ilikuwa imeganda damu. Alitahidi kutafuta ni sehemu gani ameumia lakini hakuiona ndipo machale yakamcheza lakini akapotezea na kuingia kitandani.


Asubuhi mapema aliwahi kuamka nakwenda geto kwa Alex, alipofika alishtuka sana baada kuona michirizi ya damu ikitokea ndani ya chumba hicho. Alipiga kelele na watu wakaja kwa pamoja walisaidiana kuvunjia mlango na hapo ndipo wakakutana na mwili wa Alex umelela sakafuni huku ukiwa umetapakaa damu. Bila kuchelewa walipiga simu polisi na kutoa taarifa, ila alichokifanya Patrick ni kuchukua simu ya Alex na kuufuta ujumbe aliomtumia ili asije akaonekana yupo hatiani. Haukupita muda polisi walifika eneo la tukio na kuanza kufanya uchunguzi na katik tafuta yao walifanikiwa kuipata camera alioitega Alex na kuichukua kama sehemu moja ya ushahidi wao. Walimaliza kufanya uchunguzi na taratibu nyingine zikafuata ikiwa ni pamoja na kuupeleka mwili wa Alex hospitali kwa ajili ya uchunguzi zaidi.


"tumefanikiwa kupata camera sehemu ya tukio" aliongea polisi mmoja na kumkabidhi Inspector Hans ile camera. Na yeye bila kuchelewa aliunganisha na computer yake na kuanza kuangalia, ilionyesha Alex akitoka chooni na alipofika kitandani alijirusha lakini hakuonekana mtu mwengine katika kitanda hicho. Lakini ghafla alichomoka kitandani na kujigonga ukutani kisha akaonekana kama akiomba msamaha lakini ghafla alipiga kelele na damu kuanza kumtoka. Waliendelea kuangalia video hiyo mpaka walipoona anachukua kioo na kuanza kujikata wenyewe mpaka akaanguka chini na ghafla akaanza kutoka damu shingoni kama ishara kuwa amekachinjwa, yakatokea maandishi ukutani "AMELIPA". Hapo camera ikaingia chenga na kuzima kabisa,askari wengi waliotizama ile video walishtuka sana hasa pale yalipotokea maandshi ukutani.

ITAENDELEA
 
RIWAYA: JESTINA
MTUNZI: Tariq Haji
CONTACT: 0624065911

SEHEMU YA 13.

tumefanikiwa kupata camera sehemu ya tukio" aliongea polisi mmoja na kumkabidhi Inspector Hans ile camera. Na yeye bila kuchelewa aliunganisha na computer yake na kuanza kuangalia, ilionyesha Alex akitoka chooni na alipofika kitandani alijirusha lakini hakuonekana mtu mwengine katika kitanda hicho. Lakini ghafla alichomoka kitandani na kujigonga ukutani kisha akaonekana kama akiomba msamaha lakini ghafla alipiga kelele na damu kuanza kumtoka. Waliendelea kuangalia video hiyo mpaka walipoona anachukua kioo na kuanza kujikata wenyewe mpaka akaanguka chini na ghafla akaanza kutoka damu shingoni kama ishara kuwa amekachinjwa, yakatokea maandishi ukutani

"AMELIPA". Hapo camera ikaingia chenga na kuzima kabisa,askari wengi waliotizama ile video walishtuka sana hasa pale yalipotokea maandshi ukutani.


"mi si niliwaambia kama mauaji haya hayafanywi na mtu wa kawaida" aliongea Inspecta Hans na kuwaangalia wenzake "sasa mmeamini kama kuna mizimu duniani" aliendelea kuongea lakini alionesha kama kushtuka kidogo na kuamua kurudia kuingalia tena kwa mara ya pili lakini kwa makini zaidi, ndipo akagundua kama shape ya mschana kama iliokuwa inaakisi mwanga. Wenzake walimshangaa na kumuuliza mbona anaangalia tena. "hebu angalieni kwa makini hiyo video kwa mbali sana utaona kama shape ya mschana" aliwaambia na wote wakaikodolea macho ndipo wengi wakagundua kile alichokisema Inspecta Hans.


Alwin akiwa kwao alifutwa na askari kuombwa aende kituoni kwa ajili ya majadiliano, alikubali bila kinyongo na kuondoka nao. walifika kituoni na kuanza mazungumzo.
"kijana hebu tueleze kuhusiana na Jestina"
"mimi sina la kueleza"
"tunaomba msaada wako maana mauaji yamezidi na yantupa sifa mbaya kama kitengo cha polisi"
"sasa mimi niwaambie nini wakati kesi yake ilifikishwa kwenu miaka kumi iliopita lakini mkajifanya wababe kuipindisha sheria, kwa kupewa pesa mkanibambikia mimi"
"tusaidie basi tuweze kumdhibiti"
"hahaha mna kichaa kweli nyinyi, kiufupi mumechelewa sana amerudi mwenyewe kuja kuiweka sawa sheria na nyinyi hakuna mnaloweza kufanya kilichobaki nyie kaeni tu musubiri kukusanya miili ya atakao waua"
"kijana unajifanya jeuri si ndio" inpecta Brandon alifoka
"tena wewe haswaa umo katika list yangu" Alwin aliongea maneno hayo na ghafla alianza kubadilika na kupotea katika mazingira ya kutatanisha. Naam walilipata jibu kumbe hakuwa Alwin bali alikuwa ni mwenyewe Jestina na aliamua kufanya hivo kumpa onyo Inspecta Brandon na polisi wengine juu ya mpango wa kupenda pesa na kupindisha sheria. Kushuhudia hivo Inspecta Brandon alianguka chini na kupoteza fahamu.


"mimi niliwaambia mkaniona namtetea Alwin, sikusema tu ila yalishaanikuta ndio maana nikawaambia haitasaidia hata kama mtamkamata Alwin kwa sababu Jestina ndie anaejibu ukimwita Alwin" aliongea Inspecta Hans, "unamaanisha nini kusema hivyo" aliuliza askari mwingine. "namaanisha kuwa Jestina anatumia sura ya Alwin, hivyo basi hata ukimhoji utaishia kukipata kama kilichompta Inspecta Brandon muda mfupi uliopita" aliposema hivo ndio wakakumbuka kama mkuu wao ameanguka, haraka walimbeba na kumuwahisha hosptali.
******************************
Ndege ilitua uwanja wa Mashvile, miongon mwa abiria walioshuka alikuwemo binti mmoja mrembo sana. Hakuwa mwengine isipokuwa ni mtoto wa Profesa Alexander Harison, Miryam. Baada ya miaka mingi sasa ndio anarudi nyumbani akitoka kuchukua masters katika udaktari akiwa kama daktari bingwa saikolojia. Alitoka nje ya uwanja na kuonana na baba yake mzazi "karibu nyumbani mwanangu" profesa aliongea huku akitanua mikono kama ishara ya kutaka kumkumbatia mwanae. Miryam kwa furaha aliruka na kumkumbatia baba yake.

"umekuwa mkubwa mwanangu" aliongea profesa, "ah kawaida tu baba" Miryam alijibu na kuachia tabasamu na kuufanya uzuri wake uonekane vilivyo. "mie ningapata mtoto kama yule pia nisingefikiria kuoa mke mwengine", "dah yule mtoto ni mkali kupindukia kiasi profesa ampe kila anachotak", "sasa wewe unadhani acheze zawadi kama ile kutoka kwa muumba, kama angekuwa mwanangu angetaka hata dunia ningempa". Hayo ni maneo yalikuwa yakisemwa na walinzi walipokuwa wakimpokea mtoto wa bosi wao.


Waliingia kwenye gari na safari ikaanza, msafara huo ulikuwa ni zaidi ya ule wa raisi, ulikuwa na gari kumi zote aina Rolls royce nyeusi zikisindikizwa na pikipiki tatu mbele na tatu nyuma. Kwa kweli profesa alimpenda sana mwanae kiasi kwamba hakujali anatumia kiasi gani cha fedha kumhudumia tu. Alimpa kila alichotaka na hakusita kumwambia "WEWE NI LULU YA MAISHA YANGU". Mapenzi yake kwa mtoto wake hayakuwa na hayakufanana na chochote. Ila alijua ipo siku itabidi amkabidhi kwa mtu mwengine ili amlee, akimaanisha kuwa ipo siku mwanae pekee ataolewa na kuondoka nyumbani. Na kila alipoifikiria siku hiyo alihisi kama nusu na robo ya maisha yake atakua kayatoa, kuna baadhi ya wakati alijikuta akibubujikwa na machozi lakini angefanyaje na ndio mfumo wa maisha ulivo.


Walifika nyumbani na kupokewa kwa shangwe kubwa hasa ukizingatia anapokuwepo Miryam katika nyumba hio kila siku ni skukuu. Maana binti huyo kajaaliwa upendo wa hali ya juu sana kiasi kwamba wafanyakazi wote walikuwa wawazi katika kuongea nae, Ni mschana ambae hakujiona kwa uzuri wake na utajiri aliokuwa nao bali aliishi na watu wote kama sehemu ya familia yake. "Afadhali amerudi", "nakwambia huyu mtoto ni baraka ndani ya nyumba hii", "hata leo profesa aseme hana mshahara wa kutulipa basi mie nitafanya kazi bure ilimradi niwe karibu tu na Miryam". wafanyakazi wa kike hawakuwa nyuma katika kummwagia sifa binti huyo wa profesa maana aliuteka moyo wa kila mtu alikuwa ndani ya nyumba yao.


Kutokana na machofu ya safari, Miryam alioga na kupumzika. Upande wa Alwin alikuwa hafahamu chochote kuhusiana na ujio wa Miryam na hata profesa alikubaliana na mwanae kuwa asimwambie chochote.


Sasa kutokana na kilichoonekana kwenye kamera askari wote waliamini kama kuzuia mauaji hayo ni sawa na kuzuia mawimbi baharini. Kila asakri aliamua kushughulika na mambo yake pasi na kuwaza tena njia za kumkamata muuaji, walijisemea "muache auwe tutakwena kukusanya mizoga". Jestina akiwa chumbani kwa Alwin ghafla hali ya hewa ilibadilika ghafla na kutoweka bila yeye mwenyewe kutaka, funga fungua alijikuta yupo kule katika ulimwengu wa waliodhulumiwa. "karibu tena Jestina" aliongea yule malkia, "mbona umenirudisha huku wakati sijamaliza kazi yangu" aliongea akionekana kuchukia kidogo. "kuna jambo nataka nikueleze kwanza ndio utarudi tena katika ulimwengu wa kibinaadamu" baada kusikia hivo kidogo akapoa. "Muda wako wa kukaa huko unakaribia kuisha" aliongea malikia na kumshtuwa kidogo Jestina, "si umenambia muda wangu utakwisha mpaka pale nitakapo wamaliza wote" aliongea Jestina kwa sintofahamu. "ndio, ilikuwa iwe hivyo lakini muda si mrefu utaanza kukutana na kikwazo" alijibu malikia, "na hicho kikwazo kitakufanya upumgukiwe nguvu za kuishi katika ulimwengu wa kibinaadamu", "nambie ni kikwazo gani hicho nikakiondoe mapema" aliaongea Jestina huku akianza kubadilika kwa hasira. "hutoweza kukiondoa hata uwe na nguvu kiasi gani hata mimi pia sikuweza kukiondoa wakati wangu" alijibu malikia akionesha ugumu wa kukiondoa kikwazo hicho. "basi nambie kikwazo chenyewe ni kipi" aliomba sasa Jestina, "MIRYAM" malikia alijibu huku akitetemeka.


"ah kumbe huyo tu" aliongea Jestina kwa dharau kidogo, "hiyo ni kutokana na mapenzi mazito aliokuwa nayo juu ya Alwin na jambo ambalo wewe hulijui ni kwamba Alwin anampenda sana Miryam japo hajawahi kumuona tokea azinduke, ila kwa sasa Miryam amerudi kutoka masomoni na akianza tu kuwasiliana na Alwin mapenzi yao yatamea tena jambo ambalo litamfanya Alwin aanze kusahau mambo mengine ikiwemo kisasi anachokusaidia kukikamilisha" aliongea malikia na hapo Jestina aliishiwa ujanja.


"lakini kuna kitu unaweza kukifanya ili kuendelea kubakia ulimwengu wa kibinaadamu" aliongea malikia, "kitu gani hicho". "usiwaingilia katika mapenzi yao wala usijaribu kumsogelea Miryam kwa ubaya maana katika ulimwengu hakuna vita kubwa kama ya mapenzi, pia hayohayo mapenzi ni amani ya kutosha" aliongea malikia. "sasa umesema wakianza kukutana mimi nitapoteza nguvu zangu" aliuliza Jestina, "utaweza kuwa nazo ikiwa Alwin atamueleza Miryam juu ya uwepo wa mzimu wako na kama atakubali bila kinyongo na kuamini kama ni kweli basi hapo utakuwa umeshinda maana hata nguvu zako zitaongezeka kwa sababu utakuwa na watu wawili ambao walikupenda sana kipindi cha uhai wako japo mwenyewe hukulifahamu hilo" alimaliza kuongea Malikia na kabla Jestina hajajibu chochote alitoweka na kurudi katika ulimwengu wa binaadamu. Alimkuta Alwin kalala fofofo, alisogea mpaka pembeni yake na kukaa. Alimuangalia kwa muda sana kisha akajilaumu kwa kumpa wakati mgumu sana kipindi cha uhai wake japo alimuonyesha ni kiasi alimpenda na kumjali, lakini kutokana na wivu wake wakimasomo hakutaka kumkubalia bali aliamua kumtesa kwa kutoka na mwanaume mwengine ambae baadae aliamua kumfanyi ukatili wa hali ya juu sana. Machozi yalianza kumtoka na kujikuta ni mwanamke asie na shukurania hata kidogo. Pia alikumbuka kipindi akiwa na urafiki na Miryam mschana ambae walitokea kupendana sana kutoka na tabia zao kuendana sana japo kiakili hakuwa na akili kama yeye "ama kweli kuwa na akili nyingi si kuwa na maarifa" alijisemea moyoni huku akihisi maumivu makali ya usaliti aliowatendea wawili hao pasi na kumthamini sana. Ila angefanyaje na ndio mambo yashaatokea hata kama angetaka kuyarekebisha isingewezekana maana tayari alishaaga dunia.
*****************************
Usiku uliingia huku maandalizi ya sherehe kubwa ya yakifanyika, ilikuwa ni sherehe ya kumkaribisha Miryam. Alwin akiwa kwao aliskia akiitwa na mama yake na aliposhuka alikutana na mtu asie mfahamu. Alikuwa na briefcase mkononi, "Mr Alwin huu ni mzigo wako" aliongea na kumkabidhi kisha bila kuongea kitu yeye aliondoka. Alwin alirudi chumbani kuufungua mzigo huo, alishangaa kuona kuna suti ya rangi ya maziwa au crem, viatu, tai nyekundu pamoja na funguo ya usafir. Pembeni kulikuwa na barua ndogo iliosema hivi.

ITAENDELEA
 
MTUNZI: Tariq Haji
CONTACT: 0624065911

SEHEMU YA 14

Usiku uliingia huku maandalizi ya sherehe kubwa ya yakifanyika, ilikuwa ni sherehe ya kumkaribisha Miryam. Alwin akiwa kwao aliskia akiitwa na mama yake na aliposhuka alikutana na mtu asie mfahamu. Alikuwa na briefcase mkononi, "Mr Alwin huu ni mzigo wako" aliongea na kumkabidhi kisha bila kuongea kitu yeye aliondoka. Alwin alirudi chumbani kuufungua mzigo huo, alishangaa kuona kuna suti ya rangi ya maziwa au crem, viatu, tai nyekundu pamoja na funguo ya usafir. Pembeni kulikuwa na barua ndogo iliosema hivi.


"jiandae uje nyumbani kwangu by Profesa", yeye akiitwa na profesa huwa hafikirii mara mbili, aliingia chooni na kujimwagia maji. Alipomaliza alitinga suti alioletewa na kuning'iniza tai shingoni, alivaa viatu na kuchukua funguo lakini alipaongalia vizuri aliona saa moja matata sana na yeye bila kuchelewa aliitia mkononi na kuhakikisha kuwa amechukua kila kilicho ndani ya briefcase hilo. Alipojiridhisha yuko sawa alitoka chumbani kwake na kuelekea nje, aliwaaga wazazi wake na kutoka. Nje huko alikutana na gari moja ya bei mbaya aina ya Buggtti supersport vitesse ya rangi ya maziwa. Hakuuliza alibonyeza kitufe na kutoa loki, aliingia kwenye gari na safari ya kuelekea kwa profesa ilianza, kwa mwendo wa umakini zaidi alitumia dakika kama saba hivi kufika mjengoni kwa profesa.


Alishuka gari na kumkabidhi funguo mlinzi aende akaiweke maegesho, "na sasa anaingia mgeni rasmi wa kwanza Mr Alwin Kelvin" MC alitangaza na ukumbi mzima ulilipuka kwa shangwe. "mmh jamani huyu kapendezaje", "wee jifanye mwendawazimu tu mali ya watu hiyo shosti". "sasa kwani mimi jiwe" hayo ni maneno waliokuwa wakiongea waschana wawili ambao walivutiwa sana ujio wa Alwin.


Basi aliekezwa meza kuu na kuambiwa akae kwenye kiti, "profesa kuna nini mbona unafanya sherehe" aliuliza Alwin "mambo matamu hayataki haraka" alijibu Profesa na hapo Alwin alielewa kuwa anatakiwa asiulize tena maswali. "na sasa tumkairbishe mgeni rasmi mwengine ambae pia ndie mlengwa mkuu wa sherehe hii Ms Miryam Alexander Harison" MC alitangaza tena na kuwafanya watu wachizike kwa makelele. Alwin alijikuta akitumbua macho kama mjusi aliebanwa na mlango huku akihisi hata moyo wake ulipunguza kasi ya mapigo, bila kujitmbua alijikuta akisemama na kuelekea kwenye ngazi ambapo Miryam alikuwa anashuka, hakuna aliemuuliza watu wote walitengeza njia ili apite bila kikwazo. "kwa kweli umependeza sana" alisema maneno hayo huku akimpa mkono Miryam, "asante hata wewe umependeza pia" alijibu Miryam. walitembea wawili hao huku wameshikana mikono utadhani ni mfalme na malkia wake mpaka kwenye meza.
**************************


Kimbembe kilikuwa kwa Patrick amabe alikuwa anapambana kutetea maisha yake, "Jestina najua nimekukosea naomba unisamehe", "ulikuwa na muda mwingi wa kutubu lakini hukufikiria hilo" Jestina aliongea kwa hasira mpaka radi zikawa zinapiga. Lakini ghafla alianza kupotea bila mpango, Patrick alipoona adui yake anapoteza muelekeo akaamua kutoka nduki. "Alwin nakuomba subiri japo kidogo nimalizane na huyu kwanza" aliongea katika moyo wake, na papo hapo akatoweka na kumtokea Patrick kwa mbele, bila kuchelewa alimpiga kucha za koromeo na kumuulia mbali. Alimpa kifo cha haraka makusudi ili asije akapoteza nguvu kabisa, Patrick alianguka chini kama mzigo huku damu nyingi zikimtoka shingoni. Taratibu Jestina alianza kutoweka kama vile unavofuta mchoro wa penseli kwa ufutio, nguvu zilinza kumuisha na kuanza kusikia maumivu makali sana. Aliona njia peke ya kujinusuru na kutoweka kabisa ni kwenda alipo Alwin na kumueleza yanayomkuta. Kwa nguvu zake kidogo zilizobakia alifanikiwa kutoweka na kutokea nyumbani kwa profesa. Na moja kwa moja alitokea mbele ya Alwin lakini alishangaa na kuona hata Alwin alikuwa hamuoni tena.


Alijaribu sana kumtokea mbele yake lakini hali ilikuwa ileile, kwa wakati ule Alwin alisahau kila kitu kiasi cha kuwa akili yake ilikuwa ikiutathmini uzuri wa Miryam tu. Baada kuona haonekani mbele ya Alwin, akaona njia pekee ya kuongea na Alwin ni kwa kutumia mwili wa mtu mwengine, alizunguka ndani ya ukumbi huo mpaka alipopata mtu wa kumtumia. Hapo aliuingia mwili huo na kuelekea alipo Alwin, "Alwin tunaweza kuongea kidogo" aliongea na kumfanya Alwin kugeuka lakini hakushughulika sana kwa sababu mwanamke aliemuita wala yeye hamjui. Alijaribu kumuita tena lakini haliilikuwa ni ile ile ndipo akaamua kumgusa mkononi, hapo Alwin alizinduka na kumgeukia kwasababu mwili wake ulikuwa wa baridi haswaa.


"Jestina unafanya nini hapa" aliuliza kwa sauti ya chini, "Alwin nakuomba nisikilize kwa makini sana" Jestina aliongea na kumvuta pembeni na kumueleza kila kitu. Alwin alishtuka kidogo baada kusikia vile, "subiri nikamwite Miryam" aliongea na kuondoka. "Miryam tunaweza kwenda kuongea varanda" nae Miryam hakukataa waliongozana mpaka varanda na kuanza kumueleza kila kitu, mwanzo Miryam alionekana kusita. "najua utakuwa huamini, subiri ni nimwite lakini nakuomba usipige kelele" aliongea Alwin baada kuona Miryam anakuwa mgumu kumuelewa. "Jestina jitokeze mbele yake ili akuone". Ghafla Jestina akatokea mbele ya Miryam "Mungu wangu, hivi ni kweli au nasinzia" yaliomtoka maneno hayo bila kujitambua. "Miryam nakuomba unisamehe kwa yale yote nlokukosea kwa sasa naomba unikubali kama rafiki yako kwa mara nyingine tena" aliongea Jestina huku akijitahidi asibadilike.


"Jestina mimi nilishaasahau hasa kama tuligombana mimi na wewe, siku ile nilitaka ufahamu tu kama ulikuwa ukiwaumiza watu wasio na hatia" Aliongea Miryam huku akimsogelea, "kama alivyoniambia Alwin kuwa umerudi kuja kuwalipisha waliokutenda basi mim niko pamoja na wewe" aliongea na hapo alikuwa karibu yake sana, aliamua kumshika mkono ili ajiridhishe kama kweli aliokuwa mbele yake. Alpomshika tu Jestina alitoweka na kumfanya Miryam ashangae kidogo "wow! Alwin its fantastic" aliongea huku akimkubatia Alwin kwa nguvu, "kama sheria ilishindwa kumpatia rafiki yangu haki yake basi mimi niko pamoja na nyinyi katika kuwateketeza wale wote waliohusika na kifo chake" Miryam aliongea lakini sauti yake ilikuwa imebadilika kidogo, Alwin alijitoa na kumwangalia "mbona unalia sasa" aliuliza kwa mshangao. "Alwin najua ulikuwa ukidhani namchukia sana Jestina, ukweli ni kwamba nilikuwa nampenda sana na ndio maana sikutaka apotee" aliongea Miryam kwa kwikwi. "usijali mpenzi wale wote waliohusika na kifo chake watalipa kwa maisha yao" Aliongea Alwin na kwa mara ya kwanza alimvuta Miryam na kukutanisha midomo yao au kama wanavyosema wengine "ROMANCE".


Kwa upande wa Jestina huo ulikuwa ni msimu mpya, maana alihisi mwili wake umepata uhai tena. Nguvu zake ziliongezeka mara dufu, wakati alizidi kutisha kiasi kwamba akikutokea tu kama unariho nyepesi basi unaweza kuaga dunia. Mvua ilianza kunyesha na radi zikawa zinapiga kwa nguvu sana hadi umeme ukazimika, "hahaha mlobakia jiandaeni" aliongea na kutoweka kisha hali ikarudi kuwa kawaida na umeme ukarudi.


Alwin na Miryam walirudi uwanjani huku wakiwa wameshikana viunoni, moja kwa moja mpaka meza kuu. "Profesa" Alwin aliita kwa sauti ya chini, "sema Alwin" alijibu profesa huku akimuangalia. "nataka kukuibia kitu"

"wewe mtoto we, kitu gani hicho"

"ni kitu unachokipenda sana katika maisha yako" Profesa aliposikia hivyo akaelewa Alwin anamaanisha nini. Alisimama na kuelekea kwa MC kisha akachukua kipaza sauti na kuomba watu wamsikilize. "mabibi na mabwana naomba muniazime masikio yenu kwa dakika chache, ule muda niliokuwa nikiusubiria kwa hamu umefika, hatimae Mungu ameitika maombi yangu. Nawaomba wageni rasmi wasogee hapa jukwaani" aliongea na Alwin na Miryam wakainuka na kuelekea jukwaani. "napenda kumtambulisha kwenu rasmi Mr Alwin Kelvin ni mkwe wangu wangu kuanzia sasa" aliongea na ukumbi mzima ulilipuka kwa shangwe "hongera kijana na karibu katika familia" aliongea tena na kukumbatiana na Alwin kisha akairudisha mike kwa MC na kumwambia aendelee na ratiba.


Wakati wakiendelea na sherehe, aliingia mwanamke mwengine aliekuwa mzuri kupita maelezo. Vidume vyote vilianza kutokwa na mate ya kumtamani mwanamke huyo ambae alivaa nguo iliong'ara sana. Alitembea taratibu mpaka alipo Alwin na Miryam "hongereani sana" aliongea na hapo Alwin akashtuka baada kusikia sauti hiyo maana aliifahamu vilivyo kama ilikuwa ni sauti ya Jestina. "duh umebadilika" alikuta akiongea, "Jestina" Miryam aliita. "ndio mwenyewe" Jestina alijibu, Miryam alishindwa kujizuia na kumkumbatia bila kujali kama ule ni mzimu. Marafiki hao watatu waliongea na kufurahi sana, waliongea kama walivyokuwa wakiongea kipindi kabla hawajagombana. "Jestina nina ombi moja kwako" alikuwa Miryam, "lipo tena" aliuliza Jestina "ombi langu ni Matt, naomba umpe kifo chechenye maumivu makali sana" aliongea Miryam na kumfanya Jestina atabasamu kisha akajibu "usijali maana huyo dawa yako ipo kuzimu naipika".


"na mimi nina ombi moja" mara Alwin aliingilia, "haya lipi hilo" aliuliza Jestina. "nikipata mtoto wa kike nitamwita Jestina" aliongea na kutabasamu, "ah hilo si umwambie Miryam" alijibu Jestina, "mimi nimekubali" Miryam alijibu kisha wote wakacheka. "jamani muda wangu wa kuondoka umefika kwa hio tutaonana kesho" aliongea Jestina na wote walikubaliana. Alipiga hatua tatu ghafla umeme ukazima na uliporudi hakuonekana tena.
**************************************


Veronica akiwa kwenye gari yake anarudi kwao, alikuwa amefungulia mziki mzito hiyo ni kwa sababu alikuwa anatoka club kujirusha. Alipoangalia kwenye kioo aliona kama mtu amekaa siti ya nyuma, lakini alipogeuka hakuona kitu. "ah pombe bwana" alijsemea huku akitoa simu yake kwenye begi ili apige, ghafla alihisi kama kagonga kitu. Alisimamisha gari, kwa uoga akashuka kuangalia ni kitu gani. "toba nimegonga mtu" alijisemea baada kugunduwa kuwa aliemgonga ni mtu. Wakati anajishauri afanye nini mara akaanza kumuona akisimama huku akionekana kuvunjikavunjika viuongo, lakini ajabu vilianza kukaa sawa. Baada kuona hivo aliamua kukimbilila kwenye gari, lakini alipojaribu kufungua mlango ulikuwa na loki. Alijaribu milango mingine lakini hali ilikuwa hiyohiyo, "huwezi kunikimbia" alimsikia akiongea, Alipogeuka uso kwa uso na Jestina. "wewe si ushakufa" alijikuta akiropoka, "ndio" alijibu Jestina na kumtandika kofi la uso Veronica. Kisha akaanza kubadilika na kuanza kutisha sana macho yalikuwa meusi yote huku mwili wake ukitanuka na kutoa harufu mbaya sana. Veronica kuona hivo alianza kukimbia hovyo bila kujua wapi anaelekea, "huwezi kunitoroka" Jestina aliongea kwa hasira na kutoweka.

ITAENDELEA.
 
RIWAYA: JESTINA
MTUNZI: Tariq Haji
CONTACT: 0624065911

SEHEMU YA MWISHO 1.

Veronica akiwa kwenye gari yake anarudi kwao, alikuwa amefungulia mziki mzito hiyo ni kwa sababu alikuwa anatoka club kujirusha. Alipoangalia kwenye kioo aliona kama mtu amekaa siti ya nyuma, lakini alipogeuka hakuona kitu. "ah pombe bwana" alijsemea huku akitoa simu yake kwenye begi ili apige, ghafla alihisi kama kagonga kitu. Alisimamisha gari, kwa uoga akashuka kuangalia ni kitu gani. "toba nimegonga mtu" alijisemea baada kugunduwa kuwa aliemgonga ni mtu. Wakati anajishauri afanye nini mara akaanza kumuona akisimama huku akionekana kuvunjikavunjika viuongo, lakini ajabu vilianza kukaa sawa. Baada kuona hivo aliamua kukimbilila kwenye gari, lakini alipojaribu kufungua mlango ulikuwa na loki. Alijaribu milango mingine lakini hali ilikuwa hiyohiyo, "huwezi kunikimbia" alimsikia akiongea, Alipogeuka uso kwa uso na Jestina. "wewe si ushakufa" alijikuta akiropoka, "ndio" alijibu Jestina na kumtandika kofi la uso Veronica. Kisha akaanza kubadilika na kuanza kutisha sana macho yalikuwa meusi yote huku mwili wake ukitanuka na kutoa harufu mbaya sana. Veronica kuona hivo alianza kukimbia hovyo bila kujua wapi anaelekea, "huwezi kunitoroka" Jestina aliongea kwa hasira na kutoweka.


Wakati Veronoca anakimbia ghafla alijikuta akirushwa na kujipigiza katika mti, alitoa yowe la maumivu makali sana huku akijishika mbavuni. "nisamehe Jestina" alianza kulia huku akiomba msamaha, "wewe huna haja ya kusamehewa, wewe ulikuwa unashangilia wakati mwanamke mwenzako anadhalilishwa pumbavu mkubwa wee" alijibu Jestina na kumsigelea na kumtia vidole vya macho kisha akaanza kumpiga makucha. Alimnyanyua na kumpigiza na chini kisha akamnyanyua tena na kumrusha kwa nguvu, moja kwa moja alikwenda kutua kwenye gogo lenye ncha kali lilipenya mgongoni na kutokea mbele na hapo mia zake zikawa zimefika ukingoni, kama kawaida aliacha ujumbe na kutoweka eneo hilo.
Uwezo aliokuwa nao sasa ulimuwezeshe kuwatokea maadui zake mpaka mchana, lakini hakutaka kutembeza kichapo mchana hivyo aliamua kuendelea na kazi yake nyakati za usiku. Wazazi wa vijana waliouwa waliamua kufanya maandamano na kuitaka serekali iwajibike na vifo vya watoto wao. Walonekana ni wenye hasira sana, "sasa jamani hasira za nini" aliongea waziri mkuu wakati akijaribu kuwapoza. "wewe na serekali yako ni wapuuzi, watoto wetu kila siku wanakufa vifo vya kutatanisha halafu wewe unatuuliza hasira za nini" aliongea mzazi mmoja, macho yake yalikuwa mekundu sana. "au kwa sababu wako wewe hayupo ndio maana unatuona sisi wajinga" mwengine alifoka, "eh yamekuwa hayo tena, basi msijali nawaahidi kuwa muuaji tutamkamata na tutamleta mbele yenu mumuhukumu" aliongea waziri mkuu na kuondoka bila kutaka swali lolote.


"dah mnajua leo nimedhalilika sana" aliongea waziri mkuu katika kikao maalum cha dharura, "mwiteni mkuu wa kituo" alitoa agizo. "hilo haliwezekani" alijibu Inspecta Hans nae pia alikuwepo kenye kikao hicho. "kwanini isiwezekane" alifoka waziri mkuu, "kwa sababu Inspecta Brandon yupo hospitaly kalazwa" alijibu inspecta Hans. "unasemaje wewe, sasa yule aliekuwa anakuja nyumbani kwangu tokea juzi ni nani" aliongea waziri mkuu huku akionyesha kuchanganyikiwa, "ndio muheshimiwa, tokea majuzi Inspecta Brandon amelazwa hospitali kuu akiwa amepooza" alijibu inspecta Hans, "na umesema alikuwa anakuja kwako" aliuliza Inspecta Hans. "ndio kwanini atakuwa nani yule" alijibu na kuuliza kwa wakati mmoja, "huyo ndio muuaji mwenyewe" alijibu inspecta Hans na kumfanya waziri ashtuke kidogo na kijasho chembamba kikaanza kumtoka. Bila kuongea jambo aliinuka na kuondoka huku kichwani mwake akiwa na mawazo mengi sana kwa sababu amemueleza mambo mengi sana ambaya alitka kuyafanya kabla ya kumaliza wakati wake kama waziri mkuu.


Kwa upande wa Alwin na Miryam mapenzi yalinoga sana, muda mwingi walikuwa pamoja huku wakibadilishana mawazo na hasa wakipanga maisha yao ya ndoa yatakuwaje. Jestina hasira ziliongezeka na kujikuta akitamani kuuwa hata mchana. Alipoona hali imezidi kuwa mbaya aliamua kufunga safari na ya kurudi katika ulimwengu wa watu waliodhulumiwa. "nilitarajia utarudi tu" aliongea malikia baada kumuona Jestina, "tokea nguvu ziongezeka huwa napata hamu ya kuuwa sana" aliongea Jestina. "hio ni dalili ya kuwa muda wako kukaa duniani unakwenda ukingoni" aliongea malikia na kumshangaza Jestina. "unasema nini" aliuliza Jestina, "ndio, mpaka sasa umebakia na siku tano tu" alijibu malikia. "hauwezi kuongezeka muda" aliuliza tena, "haiwezekani hata kidogo, kwa sababu muda wako wakuwepo katika ulmwengu huu pia umekwisha, unatakiwa kuondoka na urudi kwa muumba wako" aliongea malikia na alionekana kama hatanii hata kidogo. Baada ya kusikia hivo aliaga na kuondoka zake. Alirudi duniani hukua akitafakari jinsi ya kuwamaliza waliobakia hasa Matt ambae yupo nje ya mji. Na ukizingatia yeye hawezi kutoka nje mji huo, alihisi kama mpaka ataondoka hatokamilisha kazi yake. Kilichomuuma zaidi ni pale alipokumbuka kuwa Adui yake mkubwa alikuwa hayupo katika mji huo.
**********************************************
Siku mbili zilipita na mauaji yalizidi sasa, kwa siku aliuwa watu zaidi ya wanne, Watu walizidi kulalamika kutokana na mauaji hayo lakini kumkamata ni jambo ambalo lilkuwa haliwezekani. Alipoona zimebakia siku tatu ndipo likamjia wazo, aliamua kwenda kwa waziri na kumuingia mwilini na kumtia kama ugonjwa hivi. Hali ya waziri ilikuwa mbaya sana, aliwahishwa hospitali kwaajili ya matibabu lakini haikusaidia, Alipoona anakaribia mwisho wake akaamuru Matt apigiwe simu na kupewa taarifa hizo jambo ambalo lilitekelezwa haraka sana. Ndani ya masaa kumi baada kupigiwa simu Matt aliwasili Mashvile na moja kwa moja alikwenda hospitali kwaajili ya kumjulia hali baba yake. Masikini hakujua kama amerudi kuja kukifata kifo chake "vipi hali yako baba" aliuliza "ndio kama unavyoiyona mwanangu" alijibu kwa tabu sana. Mwili wake ulivimba na kupata vidonda vingi sana ambavo vilitoa harufu na damu. Jestiina baada kuona windo lake limerudi alisubiri mpaka usiku na kutoka katika mwili wa waziri mkuu, usiku huo alikwenda kuwamaliza waliobakia ili abakie na Matt tu.


Siku iliofuata Matt alikwenda hospitali kumuona baba yake, lakini alipofika alishangaa kuona vidonda vimeanza kupungua na akaambiwa kuwa hali ya mheshimiwa inazidi kuwa nzuri na huenda muda si mrefu akeuhusiwa kurudi nyumbani. Mapenzi yalizidi kunoga kati ya Alwin na Miryam na kutokana na kuwa walikuwa ni watoto wa familia zenye uwezo mkubwa kifedha. Walinunua jumba moja kubwa sana na la kisasa, taratibu walianza kuweka vitu huku wakionekana ni wenye furaha sana. Mtu yeyote aliewaona aliweza kuiona furaha hiyo kupitia macho ya wawili hao. Jestina alikuwa kaishuhudia yote hayo na alionekana kufurahi sana, jioni ya siku hiyo aliwatokea kina Alwin na kuomba kuongea nao.

"najua mupo katika kipindi cha maandalizi ya ndoa lakini naomba dakika kadhaa tu mnisikilize" aliongea Jestina.
"sawa hakuna shida" Alijibu Alwin
"muda wangu wa kukaa katika dunia umekwisha"
"unamaanisha nini" aliuliza Miryam
"namaanisha kuwa muda si mrefu nitawaacha niende nnapostahiki kuwepo
"mbona mapema" aliongea tena Miryam kwa unyonge zaidi
"na vipi kuhusu Matt" aliuliza Alwin
"Matt siku yake ishafika" alijibu Jestina akionekana kupandwa na hasira
"Dah sawa ila tunatamani ungeendelea kuwepo" aliongea Alwin
"Hata mimi pia natamani ingekuwa hivyo lakini ni jambo ambalo haliwezi kutokea kumbuka mimi nilishaakufa muda mrefu sana" aliongea Jestina na kuwaaga "nakwenda kutimiza kilichonileta duniani" aliongea na kutoweka.


Kwa bahati nzuri usiku huohuo waziri mkuu aliruhusiwa na kurudi nyumbani, ama kweli siku hiyo illikuwa ni ya furaha sana kwa Matt baada kumuona baba yake akiingia nyumbani. "karibu baba" aliongea Matt na kumkumbatia mzee wake. Walifanya kasherehe kadogo cha kushukuru, usiku huo waliongea mengi sana mpaka waliporidhika kila mtu aliingia chumbani kwake kwaajili ya kupimzika.


Matt alikwenda chooni na kujimwagia maji na kurudi chumbani, "home sweet home" alijisemea na kuachia tabasamu. Alipanda kitandani kwaajili ya mapumziko, ghafla hali ya hewa chumbani ikaana kubadilika. Alianza kuhisi kama kuna mtu ndani ya chumba hicho lakini kila alipoangaza huku na kule hakuona mtu akajipa moyo "labda ni mawazo tu". "Matt" aliskia jina likiitwa, alishtuka na kuwasha taa lakini hakuona mtu yoyote, "Matt kwanini" aliskia tena sauti na kwa wakati mshale wa hatari ukagonga kichwani mwake. "mbona hii" sauti kama naijua hivi", "ndio unaijua" yeye alijisemea moyoni lakini lishangaa kujibiwa. "hahaha Matt mpenzi wangu" alisikia kicheko na maneno hayo, alianza kuhisi kuchanganyikiwa. Alikurupuka kitandani na kukimbilia mlangoni lakini cha ajabu hakuona mlango, "unakwenda wapi unadhani" alisikia tena na wakati huu moja kwa moja akaitambua sauti hiyo kuwa ni ya Jestina. "haiwezekani hata kidogo" alisema kwa nguvu kidogo, "kwanini isiwezekane we ulidhani utanifanyiwa unyama ule halafu uendelee kuponda raha za dunia bila kuadhibiwa" alijiu Jestina na kumpitia Matt kwa nyuma,Matt aligeuka lakini hakuona kitu.
 
RIWAYA: JESTINA
MTUNZI: Tariq Haji
CONTACT: 0624065911

SEHEMU YA MWISHO 2.

Matt alikwenda chooni na kujimwagia maji na kurudi chumbani, "home sweet home" alijisemea na kuachia tabasamu. Alipanda kitandani kwaajili ya mapumziko, ghafla hali ya hewa chumbani ikaana kubadilika. Alianza kuhisi kama kuna mtu ndani ya chumba hicho lakini kila alipoangaza huku na kule hakuona mtu akajipa moyo "labda ni mawazo tu". "Matt" aliskia jina likiitwa, alishtuka na kuwasha taa lakini hakuona mtu yoyote, "Matt kwanini" aliskia tena sauti na kwa wakati mshale wa hatari ukagonga kichwani mwake. "mbona hii" sauti kama naijua hivi", "ndio unaijua" yeye alijisemea moyoni lakini lishangaa kujibiwa. "hahaha Matt mpenzi wangu" alisikia kicheko na maneno hayo, alianza kuhisi kuchanganyikiwa. Alikurupuka kitandani na kukimbilia mlangoni lakini cha ajabu hakuona mlango, "unakwenda wapi unadhani" alisikia tena na wakati huu moja kwa moja akaitambua sauti hiyo kuwa ni ya Jestina. "haiwezekani hata kidogo" alisema kwa nguvu kidogo, "kwanini isiwezekane we ulidhani utanifanyiwa unyama ule halafu uendelee kuponda raha za dunia bila kuadhibiwa" alijiu Jestina na kumpitia Matt kwa nyuma,Matt aligeuka lakini hakuona kitu.


Alijaribu kila njia kutoka ndani ya chuma chake lakini juhudi zake ziligonga mwamba, alianza kupiga kelele kwa nguvu "hazitakusaidia hizo" aliongea Jestina na kumpitia mbele kwa kasi ya ajabu sana na kupiga kikumbo kilichomtupa huko. "Jestina tafadahali nisamehe" aliongea Matt huku akijifuta damu zilizokuwa zikitoka puani, "wewe mbona hukuniachia nilipokwambia uniache" aliongea Jestina na kupiga kofi zito la mgongo. "nakufaa, Jestina nisamehe mpenzi wangu" yalimtoka maneno hayo Matt bila kutarajia. "nyooo nani mpenzi wako, kweli mtu anaweza kumbaka mpenzi wake na kisha kuwaambia marafiki zake wajisevie" aliongea Jestina na kumtokea mbele katika umbile la kutisha sana. "nakubali nimekosa nisamehe maana hata mungu anasamehe" aliongea Matt huku akipiga magoti akionyesha kuomba msamaha, "leo unamkumbuka mungu wakati unanibaka ulikuwa hujui kama kuna mungu wa kuogopa" alijibu Jestina na kumkaba kooni ghafla akatoweka nae na kutokea katika kaburi lake. "siku ile si ulinifanya kwa nguvu bila mimi kutaka, sasa leo nataka tufanye tena kwa ridhaa yangu" aliongea Jestina na papo hapo nguo zake zikachonyoka mwilini na kumuacha akiwa uchi. Kwa kweli mwili wake ulitisha sana, ulipambwa na vidonda vilivokuwa vinatoka damu na usaha mwingi sana. Pia ulitawaliwa na funza wengi sana kiasi cha kumfanya aonekana kama kaota nyasi mwilini, "sasa ole wako ushindwe kufanya ulichokifanya siku ile" aliongea Jestina huku akimfata Matt ambae wakati huo alikuwa akijaribu kutafuta njia ya kukimbia lakini kutokana na kiza hakufanikiwa. "Jestina nisamehe......nisamehe sitarudia tena" aliendelea kuongea Matt ambae alikuwa akiishika suruali yake ili isivuke lakini wapi ilichojoka katika mazingira ya kutatanisha. "siku ile si uliona raha kunidhalilisha tena kwa kujifanya kidume na kuwaalika wenzako wanifanyie uchafu" alizidi kuongea Jestina wakati huu tayari alikuwa kashamlaza Matt chini. Kila damu zilipomdondokea Matt alipiga kelele kuashiria kuwa alikuwa akipata maumivu makali sana, na kila ilipondokea damu palifoka moshi. Katika hali ya kawaida hata uwe rijali vipi lakini katika hali kama hio uume hauwezi simama.


Jestina aliuangalia uume wa Matt na papo hapo ulisimama na bila kupoteza muda aliukalia. Matt alianza kupiga kelele kwa nguvu huku akijaribu kumtoa lakini wapi ilikuwa ni sawa na kutaka kuuhamisha ukuta. Jestina alinyanyuka huku uume wa Matt ukionekana kuungua sana, alimnyanyua kwa nguvu na kumrusha katika mti. Kabla hajakaa sawa alimnyanyua na kumning'niza katika mti. "nataka uyahisi maumivu nilioyapata mimi wakati ule na pengine utayapata zaidi ya yale" zilitoka kucha ndefu mkononi, zilikuwa zimechongeka sana na zilikuwa ngumu mithili ya chum. Taratibu alizunguka nyuma na kumchoma chini shingo na kuanza kuteremsha mkono chini kama vile anachuna ngozi ya mnyama. Maumivu yalikuwa makali sana kiasi cha kama ingekuwa anafanyiwa na mu wa kawaida angekuwa kashaazimia tayari lakini halikutokea hilo. Matt alipiga kelele sana akiomba msaada lakini wapi hakukuwa na yoyote wa kumsaidia. Jestina aliendelea kumchanja mgongoni mpaka mgongo wote ulirowa damu, baada ya hapo alimgeukia mbele na sura yake ilizidi kuwa mbaya. "kama ungenisikiliza siku ile tusingefika hapa leo" aliongea Jestina huku machozi ya damu yakimtoka. Alimshika kichwa na kumfungua mdomo kisha akamtemea kitu kama makohoo hivi na kumfunga mdomo na pua jambo ambalo lilimfanya ameze bila kutaka. "tutakutana kuzimu huko" aliongea Jestina kutoweka eneo hilo, ghafla Matt alianza kutapika damu nzito ikiamatana usaha pamoja na funza.


"Alwin nimekuja hapa kukuaga kwani muda wangu wa kuwepo hapa umekwisha" aliongea Jestina baada kumtokea Alwin, "tutakumis sana kwa kweli" aliongea Alwin huku machozi yakimtoka. "utanisahau tu, nina imani Miryam atakufanya uwe mume bora kabisa" aliongea Jestina huku akianza kutoweka taratibu, "utarudi kama mwanangu" aliongea Alwin huku akipunga mkono. Mwisho kabisa Jestina alitoweka kabisa, "nenda kwa amani Jestina" aliongea Alwin huku akitabasamu. Asubuhi mapema televisheni zote zilitangaza kifo cha Matt ambae alikutwa ametapika mpaka utumbo, habari hiyo ilipelekea waziri mkuu kupata shimikizo la damu lilisababisha kifo chake.
*************************************


Mwezi mmoja sasa umepita na hakukuripotiwa mauaji yoyote yale, na hali ya amani ilirudi katika mji wa Mashvile. Harusi ya Alwin na Miryam ndio iliopmba vichwa vya magazeti huku kila mtu akialikwa kuhudguria harusi hiyo.
"bwana Alwin umekubali kuishi na Ms Miryam kama mke wako halali wa ndoa katika dhiki na faraja"
"nimekubali"
"Ms Miryam Alexander umekubali kumpokea bwana Alwin Kelvin kama mume wako halali wa ndoa katika dhiki na faraja"
"nimekubali"
"unaweza kumbusu bibi harusi"
Hapo Alwin alimsogelea Miryam na kumbusu, ukumbi mzima ulisimama na kuashangilia. Jioni yake ilifanyika sherehe kubwa sana huku watu kadhaa wakuwa wakuhudhuria ghafla hiyo.

"Alwin mwanangu akirudi nyumbani na kipele tu utawajibika" aliongea Profesa na kugonga glass na Alwin. "ah usijali, hata mbu akimgusa mke wangu atawajibika kama walivowajibika wengine" alijibu Alwin na kutabasamu kidogo. Sherehe ilimalizika na maharusu hao wakapelekwa nyumbani kwao, usiku huo ulikuwa ni usiku wa pekee kwa wapenda nao hao. Ulikuwa ni kihistoria katika mapenzi yao, mapenzi yalinoga kupita maelezo, baada ya muda walikwenda hospitali na majibu yalikuwa mazuri sana. Tayari Miryam alishaabeba mimba, ilikuwa furaha kubwa sana kwa familia hiyo ya wazazi vijana. Miezi ilikatika na hatimae mwezi wa kijufungua ulifika, na Mungu aliitika kilio chao. Mtoto wao wa kwanza alikuwa ni mwanamke na kama walivyokubaliana walimpa Jina la JESTINA. Baada kuruhusiwa kutoka hospitali, moja kwa moja walikwenda wazazi wa Jestina kwa ajili ya utambulisho rasmi wa Jestina mdogo.


Wazee hao ambao tabasamu lao lilipotea baada kuondokewa na mtoto wao wa pekee lilirudi baada kupewa mtot huyo wambebe. Walishindwa kujizuia, machozi yaliana kuwatiririka kwa furaha, "ama kweli Mungu ndie mjua kila kitu, na hakutokei kitu isipokuwa kuna sababu nyuma yake. Umeona mke wangu Mungu kamchukua Jestina wetu ili amlinde aibu kwa walimwengu lakini angalia sasa ametupa watoto wengine wawili na mjukuu juu" Aliongea Mr Hendrix huku akimwangalia mkewe ambae sura yake baada muda mrefu kupoteza tabasamu sasa limerudi upya. "wanangu mukihitaji msaada wowote ule iwe ni ushauri au jambo lolote lile msisite kutuambia, na msiache kutulea mjukuu wetu tumuone" Aliingea mke wa Mr Hendrix.
******************************************

IN GOD WE TRUST
MWISHO
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom