Simuelewi my X anataka nini!!!!!

Simuelewi my X anataka nini!!!!!

Kaka jaribu kuwa na subira njia ya mwongo huwa ni fupi. Wewe waache waendelee kuchat jifanye kama there is nothing happened , Ila kuwa mwangalifu usidisclose mambo yako na mipango yako kwa mdogo wako maana inaonekana huyo dada anamtumia mdogo wako kukufuatilia. Wapotezee!
 
Huwa wanasema watu wakiachana ushemeji haufi lakini bado dogo anatakiwa atumie busara kwamba yule alikuwa awe shemejie lakini kakake ameshaachana nae so nionavo mimi dogo anatakiwa kupunguza mawasiliano na huyo dada, wanaweza kuendelea kuwasiliana lakini si kihiiiivyo. Lakini upande wa pili naona huyo dada anazidisha mawasiliano na dogo ili tu akurushe roho hana lolote.

Sasa wewe unatakiwa umrushe roho kwelikweli kwa kufanya kweli (kumuoa huyo dada ambaye umeshampata)
 
Usifanye makosa ya kumrudisha mdogo wako Bongo...Ni aje wewe? :rant:
 
Unajua kuna jambo moja amblo ulikosea toka mwanzo,wewe ndiye ulimuintroduce huyo mwanamke kwa mdogo wako,wakawa wanawasiliana,tayari waliishajenga "Bond" ambyo wewe kuivunja ni ngumu, vilevile ujue wao hawajagombana ,ila wewe ndio umegombana na yule.sasa unapokua unampiga bit dogo unamuonea.Wanawake huwa ndipo wanapotuweza ukiisha mtambulisha kwa ndugu zako huwa wana wawin kwanza ndugu.Siku wewe utakapokuja na mawazo tofauti hautaeleweka.Ulikosea kumtambulisha kwa mdogo wako wakati hukuwa na uhakika wa kuendelea nae.Na hiyo ni kwa wengine wajifunze kuwa unapofikia hatua ya kumtambulishamme/mke kwa ndugu zako lazima uwe na uhakika uhusiano wenu umefika mbali.Sio mtu umelala nae siku moja mbili,tayari ushamtambulisha ,kesho unatambulisha mwingine ,hata ndugu zako watakuona unamatatizo.
Kwa ushauri wangu kama uliamua kumsaidia mdogo wako ,endelea kumsaidia lakini sio kwa sababu anachat na x wako ndio umrudishe home.Maisha ya mapeni huwa hayana formuala,pengine ndio Mungu alipanga wakutane kupitia wewe.wakipendana hiyo haikuhusu,kumbuka dogo anafeelings tofauti na wewe hata kama mmetoka tumbo moja.unaweza ukawa unafanya hivyo kumsaidia lakini kumbuka mwisho wa siku mko tofauti.
Imetokea mara nyingi,mtu anaenda kuoa familia fulani,akashindwana na dada mtu akaoa mdogo mtu na maisha yakaendelea.
Usije ukajaribu kumrudisha mdogo wako sababu tu ya huyo demu,nakuhakikishia huyo dogo hiyo kitu haitamtoka maishani mwake,kwani tayari ameishakua na matarajio fulani ya kimaisha, utakapoikatisha ndoto yake maishani na wewe siku mambo yakikuendea kombo utakuja juta.
 
Ahsanteni sana member wenzangu kuna vitu nimejifunza hapa nashkuru woote kwa jumla'
 
Mpaka hapo mimi nakuona wewe ndio mbinafsi tena ni hatari sana,

Yani umemuacha kisha dogo anajipigia ndefundefu we roho inakutoka?

Tena ukimrudisha dogo tz kisa huyo demu na mungu atakutandika adhabu ya milele mkuu, wewe kuwa mpole kubali kuwa shemeji tu na mpe moyo dogo afanikishe malengo yake kama wewe ulishindwa!


Yericko nimekupata mkuu'wala usijali maisha yanasonga'lakini ipo siku naamini kama tutakuwa hai nitaleta uzi wa huyo bint na dogo watapofikia,kwa sbb mm naamini anataka kumtumia dogo kwa faida yake,ambacho hata mimi nimeshampa warning dogo'
 
pole sana ndugu yangu jaribu kuongea na x wako vizuri ili umwambie aachane na mdogo wako afanye maisha yake hy sio tabia nzuri anayofanya huyo mdada hata kidogo
 
acheni kumlaumu jamani.huyo msichana ni hana heshima.afunuliwe na kaka,halafu afunuliwe na mdogo mtu.kuchati 8 za usiku some times ni sexy chat tu.either ananajaribu kumkomoa kaka mtu mtu kwa ku m use huyo mdogo mtu,au u never know maybe kuna mapenzi.maybe hizo tabia za huyo dada,kwa kuwa mdogo mtu ameshapenda,anazikubali.na wewe kwa kuwa umeshamuonya,muachie,yakimshinda na yeye ataachia ngazi
nakubaliana na wewe. kama kweli hawa wawili wamependana basi wasingepoteza muda wa kumponda huyu bwana mkubwa ktk mazungumzo yao. wote huwa tunabadilisha mahusiano , lakini ktk mauhsuiano mapya tunapeana upendo kwa kuwaponda waliopita? wanaomwita huyu mkubwa mbinafsi wamwite , ni maoni yao. ila mimi ninamkosoa tu kwa kusema amtudishe dogo, kumrudisha si sawa, bali ampe muda dogo atafute makazi yake. lakini hili la huyu mwanamke anania mbaya na hawa ndugu ninaweza kulikubali kwa kiasi fulani.
 
Habari zenu wadau wa MMU

Kwa mara ya kwanza naingia jukwaa hili kuomba ushauri juu ya kile kilinikuta;

Mnamo mwaka mmoja na kitu umepita nilikuwa home tz kwa bahati mbaya au nzuri nikagongana na mrembo flani mitaa ya hapo kati'kwa kweli nilivutiwa nae sana na kwa sababu nilikuwa katika mchakato wakutafuta jiko nikaona si vibaya nikifungua nae ukurasa mpya wa mapenzi,kwa kweli kwa muda mfupi tulizoeana kwa sababu likizo yangu haikuwa ndefu nikaondoka, lakini nilishamueleza dukuduku langu lote kama nahitaji mke.

Basi kadri siku zinakwenda tuliendelea na mapenzi yetu, Huyu bint hakuwa natabia ya umalaya laa,ila alikuwa Selfish'anapenda afanyiwe kila kitu kizuri yeye. Basi mwaka huu mwezi april nilikuja tena likizo tz ya miezi 2 na kitu,basi kadri nilivyokaa nae huyu ndio nikagundua kuwa kweli Selfish,mbinafsi sana hakupenda mimi nikae na ndugu yeyote kama ingetokea nikamuowa,yeye alitaka tuishi wawili tu,kwakweli hilo lilinishinda ikabidi nimwambie ukweli kuwa sitaweza kuishi nae,nikaamua kuvunja ule uhusiano wote kila mmoja akashika njia yake.

Sasa hapa swala limejitokeza kama wiki 2 zimepita mimi huku ng'ambo naishi na mtoto wa baba yangu mdogo anafanya kazi,na yule my X anamfahamu hata kipindi niko nae walikuwa wakiwasiliana kwa kuchat,Sasa hapa kuna swala moja limetokea huyu mdogo wangu na huyo my X wanachat sana sana'mpaka saa 8 usiku,yule bint anamtumia mdogo wangu mapicha kibao,hapa nashindwa kufaham nini kinaendelea,ila mdogo wangu nimeshampa warning juu ya huyo bint kwa sababu she was my gf anajua,lakini nahisi hanielewi.

Khofu yangu nahisi kutokea mgogoro mkubwa kati yangu na mdogo wangu,kwa sababu mimi ndio nilimleta hapa na kazi nikampa nafikiria nimrudishe tu home tz ili wakutane vizuri huko,hebu niishie hapa naombeni ushauri wenu,maana nina mengi yakuandika naona ntawachosha kusoma.
NGOSWE Penzi "Kitovu Cha Uzembe" aftrol tupo kwenye mwezi mtukufu...tupa kule tafta mwingine
 
kaka presha ya nini. just sit back and watch the show between those two......kaa kimya, usimrudishe hom mdogo wako, muache tu aendelee na huyo dada, yakimshinda si utajua tu?ukimrudisha hom kisa huyo dada utaonesha udhaifu wako sasa! kama ulimwaga totally, kauka kimya acha dogo ajiachie, ila kama ni partially, kazi unayo mkuu!
Paka hiyo sio bahati'kwa sisi wafrica huo si utamaduni wetu kuchukua mwanamke m1 family nzima,na faham kuwa huyu alikuwa ni mchumba wangu'
Na huyu ni mdogo wangu,
 
Umrudishe Mdogo wako kisa X wako?
Kwanza sababu ya kumuacha haikuwa na nguvu sana, wewe ulitaka mkioana muishi na ukoo?

Pia yaonekana bado unampenda huyo X, kama hayuko moyoni muache hata akiwa na mdogo wako ni dhamira zao si zako. Umesusa waachie wengine wale!



Ama kweli WAHENGA WALISEMA: Mwalimu wa wanawake ni Kipofu......ndo haya sasa unayoyaongea yamethibitisha: Naomba unijibu swalihili Kaunga Please:- " INA MAANA KUWA WEWE MUME WAKO AKIKUPIGA CHINI/ AU BOYFRIEND WAKO AKIKUMWAGA .....MAZIMA.....UPO TAYARI.....KUMDOWNLODIA HIYO PANTS/kufuli shemeji yako wakiume na ale mzigo kama kawa kisa eti wewe umeachwa na bro wake??? Tell us ili tujue jinsi wanawake mlivyochanganyikiwa na mapenzi ili wote tuone mpo sawa tu!
 
Huna hoja iliyokomaa ya kumrudisha dogo hme zaid jipange
 
Ama kweli WAHENGA WALISEMA: Mwalimu wa wanawake ni Kipofu......ndo haya sasa unayoyaongea yamethibitisha: Naomba unijibu swalihili Kaunga Please:- " INA MAANA KUWA WEWE MUME WAKO AKIKUPIGA CHINI/ AU BOYFRIEND WAKO AKIKUMWAGA .....MAZIMA.....UPO TAYARI.....KUMDOWNLODIA HIYO PANTS/kufuli shemeji yako wakiume na ale mzigo kama kawa kisa eti wewe umeachwa na bro wake??? Tell us ili tujue jinsi wanawake mlivyochanganyikiwa na mapenzi ili wote tuone mpo sawa tu!


Ni kweli binadamu tunatofautina tabia,utashi,na hata haiba,ila kwenye wengi hakiharibiki kitu,nashkuru kwa ushauri wa wana jamvi'
 
Kitendo anachofanya huyo mwanamke ni ishara tosha kuwa ulifanya uamuzi sahihi wa kumwacha. Inaonekana hana maadili mema na hata kama huyo dogo atamchukua ataishia kupata shida tu kwani mila na desturi za kiafrika haziruhusu.
 
Dogo hana adabu hata kidogo yaani anataka X wako awe shemeji kweli kizazi hiki kimelaaniwa
 
ningukuwa wewe ningemuambia dogo ukweli kwamba akiendelea kuwasiliana na huyo x nitamrudisha bongo ili waendelee naye,then kama ataendelea kuwasiliana naye atajua kifuatacho ni kurudishwa bongo
 
We si ushafanya yako,km vipi mwache dogo nae afanye yake ila usijekubali huyo mwanamke awakosanishe nyie ndugu
 
Kwa mtazamo wangu huyo mwanamke anamtumia Mdogo wako ili awe karibu na wewe(kwa mfano taarifa kuhusu maendeleo yako Huko uliko)
Kama Dogo ataamua kuwa Nae kimapenz basi ni dhahir Hana adabu kabisa,ushauri wangu mueleweshe Mdogo wako unavyojisikia vibaya kwa Kitendo cha yeye kuwa na mawasiliano ya karibu na x wako..asipokusikia muache atajifunza.
 
Back
Top Bottom