Simuelewi mwanaume huyu

Simuelewi mwanaume huyu

Umechunguza kweli hajaoa? Asije akawa anajenga kwa mke mwingine kupitia jasho lako. Hata kama kuolewa unataka lakini asikufanye zuzu, cha. Mwambie ukweli
 
Kama kweli unataka ushauri kutoka kwetu, USIKUBALI KUOLEWA NA HUYO MWANAUME, Duh! hata hivyo una kipaji mpaka sasa kuwa nae. yani ni bora utilize akili utafute Mume bora kuliko bora Mume, kiufupi huyo si MWANAUME, Kusaidiana ni sawa ila iwe mara moja n.k. lakini huyo kila siku shida hana mana.
 
teeeena akikuoa utalisha mpk nyumbani kwao.. atakwambia anamjukumu ya kwao hela haitoshi.. ukija kushtuka mwenzio anajenga kwao kama sio biashara.... kimbia faastaaa!!!!
 
Jaribu na wewe siku moja kumuomba hela usikie atakujibu nini.
 
Bora uishi maisha ya ukapera kuliko maradhi hayo,kimbia
 
Dada uyo jamaa hakufai achana nae yupo kwako kimaslahi sio kukupenda na usikute ana mke alaf baba zima kuwa matonya ata haipendezi
 
Aisee una kipaji maalumu, kwa maisha haya unaweza kumtunza huyo bahili(tetemeko)?? Ameshajua unahitaji ndoa ndo maana anakufanyia hivyo. Wala hakupendi kabisaaa, zee zima linaomba hela ya vocha
 
Huenda anakujaribu tu,uvumilivu wako na kujitoa kwako kwake,labda ukivumilia unaweza faulu na kupata hiyo ndoa
 
Mjini hapa hujui kuna wanaune wapiga mizinga??????

Kama upo tayari kubeba majukumu ya mume kubali akuoe....

Kama haupo tayari kataa maana akikuoa utakuwa unaibukaje na nyuzi hapa

Ila mwanaume anakosa 20-30 ya umeme na ana kipato kimbia shosti...kitamani ndoa kutakuponza

Anyway

Zungumza nae
 
Habarini za leo wana Jukwaa hili. nipo hapa leo munishauri ndugu zangu, mimi ni mdada wa miaka 33 niliolewaga zamani ila ndoa ikaota mabawa miaka 6 iliopita. lakini pamoja na hayo bado nina hamu sana ya kuolewa cause naona mara ya kwanza hata sikuinjoy maisha ya ndoa. sasa naomba ushauri wenu kuna mwanaume nimekutana nae kama miezi sita hivi imepita, ni mtu mzima miaka 38 yeye hajaoa bado, so anataka tuoane baada ya kufahamiana vizuri lakini kinachonichosha ni kwamba tangu nijuane nae kila siku analia shida, anasema hana hela ananiambia matatizo yake kila kukicha na kuniomba hela mara hana ela ya kula, mara umeme umeisha nimnunulie luku nk. mwanzo nilijua ni kusaidiana tu labda anapitia kipindi kigumu kifedha, lakini imekuwa ni zoezi endelevu, wakati yeye anafanya kazi na mimi nafanya kazi. amekuwa ni mtu wa kulalamika kwamba kazi anayofanya haina maslahi nk. sasa kwa kweli nachoka sana nashindwa kuelewa hii tabia yake, hela anapeleka wapi? na kama hatujaoana tu ndio hivi ikifika ndani si ndio itakkuwa balaa wakati mimi natagemea tusaidiane maisha badala yake imekuwa mimi ndio wa kumsaidia yeye kila siku. kashakula hela zangu nyingi wakati mimi sijawahi kumuomba hela yoyote ile. nahisi kama nimemchoka jamani, naomba ushauri wenu. sihitaji wale wenye lugha chafu za kejeli, nipo serious jamani nahitaji ushauri wenu. Asante
Nafikiri ana tatizo la negativity unahitaji kumfungua aone fursa...Mpeleka kwenye semina za ujasiriamali akili yake ibadilike
 
Habarini za leo wana Jukwaa hili. nipo hapa leo munishauri ndugu zangu, mimi ni mdada wa miaka 33 niliolewaga zamani ila ndoa ikaota mabawa miaka 6 iliopita. lakini pamoja na hayo bado nina hamu sana ya kuolewa cause naona mara ya kwanza hata sikuinjoy maisha ya ndoa. sasa naomba ushauri wenu kuna mwanaume nimekutana nae kama miezi sita hivi imepita, ni mtu mzima miaka 38 yeye hajaoa bado, so anataka tuoane baada ya kufahamiana vizuri lakini kinachonichosha ni kwamba tangu nijuane nae kila siku analia shida, anasema hana hela ananiambia matatizo yake kila kukicha na kuniomba hela mara hana ela ya kula, mara umeme umeisha nimnunulie luku nk. mwanzo nilijua ni kusaidiana tu labda anapitia kipindi kigumu kifedha, lakini imekuwa ni zoezi endelevu, wakati yeye anafanya kazi na mimi nafanya kazi. amekuwa ni mtu wa kulalamika kwamba kazi anayofanya haina maslahi nk. sasa kwa kweli nachoka sana nashindwa kuelewa hii tabia yake, hela anapeleka wapi? na kama hatujaoana tu ndio hivi ikifika ndani si ndio itakkuwa balaa wakati mimi natagemea tusaidiane maisha badala yake imekuwa mimi ndio wa kumsaidia yeye kila siku. kashakula hela zangu nyingi wakati mimi sijawahi kumuomba hela yoyote ile. nahisi kama nimemchoka jamani, naomba ushauri wenu. sihitaji wale wenye lugha chafu za kejeli, nipo serious jamani nahitaji ushauri wenu. Asante
Kumbe wanawake wa dizaini yenu wapo...hongera sana...mjue hata wanaume nao huchoka vizinga kama nyie...cha kufanya zungumza naye kwa utaratibu...mwambie na yeye akupe pesa..mwambie unashida..pesa kupeana.
 
Tupa kule huyo Mario, sio kawaida mwanaume Kukosa aibu na kuwa anakuomba kila kitu hivyo, You ain't his mama.!
Inawezekana anaona una shida ya kuolewa so anatumia hiyo chance kujifaidisha
Wanawake na nyinyi hampendi kupigwa vizinga...sasa mbona sisi tukiwaambia kupiga vizinga sio vizuri...mnasema ss mabahili..jina la wanaume wapiga vizinga wanaitwa Mario...wanawake wapiga vizinga wanaitwaje??
 
lugha za kejeli ndo uwaga mnazielewa vzr nyie....kakuona zezeta au anakupima.....kura yangu ipo kwenye kukuona ww zezeta wa kupita tu ila ww muulize ana malengo gan...km luku inamshinda kulea familia ataweza?kumbuka tyr una gundu la ndoa ya kwanza sasa tumia mihisia yko ya kike na uache kutumia akili yako vzr aje akutie gundu jingine
 
Wanawake na nyinyi hampendi kupigwa vizinga...sasa mbona sisi tukiwaambia kupiga vizinga sio vizuri...mnasema ss mabahili..jina la wanaume wapiga vizinga wanaitwa Mario...wanawake wapiga vizinga wanaitwaje??
Imeandikwa, mwanaume atakula kwa jasho sio mwanamke atakula kwa jasho... Ni maandiko .mwanaume wa kulia njaa kumwomba omba mwanamke ni Mario tu tena mzigo. Sio Ile kusaidiana Mara moja moja , kila siku anaomba.

Mbona mwanamke akiwa na wanaume wengi anaitwa Malaya wakati wanaume hamtaki kuitwa hivyo...
 
Imeandikwa, mwanaume atakula kwa jasho sio mwanamke atakula kwa jasho... Ni maandiko .mwanaume wa kulia njaa kumwomba omba mwanamke ni Mario tu tena mzigo. Sio Ile kusaidiana Mara moja moja , kila siku anaomba.

Mbona mwanamke akiwa na wanaume wengi anaitwa Malaya wakati wanaume hamtaki kuitwa hivyo...
Mwanaume naye huitwa malaya..sasa hv haki sawa...zamani mambo ya haki sawa hayakuwepo.
 
Back
Top Bottom