Simuelewi mwanaume huyu

Simuelewi mwanaume huyu

Princessor

Member
Joined
Aug 30, 2015
Posts
9
Reaction score
7
Habarini za leo wana Jukwaa hili. nipo hapa leo munishauri ndugu zangu, mimi ni mdada wa miaka 33 niliolewaga zamani ila ndoa ikaota mabawa miaka 6 iliopita. lakini pamoja na hayo bado nina hamu sana ya kuolewa cause naona mara ya kwanza hata sikuinjoy maisha ya ndoa.

sasa naomba ushauri wenu kuna mwanaume nimekutana nae kama miezi sita hivi imepita, ni mtu mzima miaka 38 yeye hajaoa bado, so anataka tuoane baada ya kufahamiana vizuri lakini kinachonichosha ni kwamba tangu nijuane nae kila siku analia shida, anasema hana hela ananiambia matatizo yake kila kukicha na kuniomba hela mara hana ela ya kula, mara umeme umeisha nimnunulie luku nk. mwanzo nilijua ni kusaidiana tu labda anapitia kipindi kigumu kifedha, lakini imekuwa ni zoezi endelevu, wakati yeye anafanya kazi na mimi nafanya kazi.

Amekuwa ni mtu wa kulalamika kwamba kazi anayofanya haina maslahi nk. sasa kwa kweli nachoka sana nashindwa kuelewa hii tabia yake, hela anapeleka wapi? na kama hatujaoana tu ndio hivi ikifika ndani si ndio itakkuwa balaa wakati mimi natagemea tusaidiane maisha badala yake imekuwa mimi ndio wa kumsaidia yeye kila siku. kashakula hela zangu nyingi wakati mimi sijawahi kumuomba hela yoyote ile. nahisi kama nimemchoka jamani, naomba ushauri wenu.

Sihitaji wale wenye lugha chafu za kejeli, nipo serious jamani nahitaji ushauri wenu.

Asante
 
pole mnaweza kaa na kuzungumza kwa umri wako sitaki kukuambia uachane naye hasa ukizingatia unahitaji ndoa.
 
Dada uko vizuri nakupongeza na ukipata mtu muhitaji kweli wa ndoa nahisi kila Siku ushuzi utakuwa pafumu nzuri sana..
kwa Huyo kaka embe anza kumbania na umwambie aanze kuweka mahali maana hautamsaidia
 
Zungumza nae uso kwa macho..Majibu yake ndio yata determine kama uendelee kuwa kitega uchumi wake au la
 
Nafikir mkioana itakuwa poa maana hz bili za umeme na maji na vyakula itakuwa sehem ya bajeti yenu kuliko sasa kila mtu na bajeti yakr mimi nakushauli mioane tu
 
True story: Jamaa mmoja aliopoa demu mzuri kweli wakafunga ndoa ila jamaa akawa analia shida sana kuwa kazi yake ya u-Dr haina maslahi sana, kwahio bibie akawa anabeba sehemu kubwa ya huo mzigo. siku ya siku Mama kapata tatizo kaenda pale hospitalini kajitambulisha Mimi ni Mke wa Dr fulani, kila mtu akawa anashangaa! Kumbe jamaa ni mzibua vyoo (kizibua vyoo si kazi mbaya ila alipaswa kusema ukweli). Kilichoteka ni Mama kupoteza fahamu.

Jitahidi umfahamu vizuri, usikimbilie ndoa, ukiona hujaridhika njoo inbox
 
Habarini za leo wana Jukwaa hili. nipo hapa leo munishauri ndugu zangu, mimi ni mdada wa miaka 33 niliolewaga zamani ila ndoa ikaota mabawa miaka 6 iliopita. lakini pamoja na hayo bado nina hamu sana ya kuolewa cause naona mara ya kwanza hata sikuinjoy maisha ya ndoa. sasa naomba ushauri wenu kuna mwanaume nimekutana nae kama miezi sita hivi imepita, ni mtu mzima miaka 38 yeye hajaoa bado, so anataka tuoane baada ya kufahamiana vizuri lakini kinachonichosha ni kwamba tangu nijuane nae kila siku analia shida, anasema hana hela ananiambia matatizo yake kila kukicha na kuniomba hela mara hana ela ya kula, mara umeme umeisha nimnunulie luku nk. mwanzo nilijua ni kusaidiana tu labda anapitia kipindi kigumu kifedha, lakini imekuwa ni zoezi endelevu, wakati yeye anafanya kazi na mimi nafanya kazi. amekuwa ni mtu wa kulalamika kwamba kazi anayofanya haina maslahi nk. sasa kwa kweli nachoka sana nashindwa kuelewa hii tabia yake, hela anapeleka wapi? na kama hatujaoana tu ndio hivi ikifika ndani si ndio itakkuwa balaa wakati mimi natagemea tusaidiane maisha badala yake imekuwa mimi ndio wa kumsaidia yeye kila siku. kashakula hela zangu nyingi wakati mimi sijawahi kumuomba hela yoyote ile. nahisi kama nimemchoka jamani, naomba ushauri wenu. sihitaji wale wenye lugha chafu za kejeli, nipo serious jamani nahitaji ushauri wenu. Asante
Tupa kule huyo Mario, sio kawaida mwanaume Kukosa aibu na kuwa anakuomba kila kitu hivyo, You ain't his mama.!
Inawezekana anaona una shida ya kuolewa so anatumia hiyo chance kujifaidisha
 
Mara ya kwanza huku enjoy maisha ya ndoa?
na huyu wa sasa hadi hapo unaona uta enjoy?

mbona kama majibu unayo tayari?
inawezekana ana mke tayari ndo maana hela yake inaishia huko

wewe kakusoma kakuona uko 'desperate ' na ndoa ndo maana anakuingiza mjini
 
Huyo jamaa piga chini inawezekana ana mke mwingine. Wanaume hatuna sehemu za kupeleka fedha zaidi ya wazazi, wake na miradi yetu. Maana hatujirembi..huyu pesa anapeleka wapi kama anafanya kazi na hajaoa?

Sasa yeye anafanya kazi halafu analia shida means kuna mke anamhudumia pembeni na kachukulia weakness yako kukunyonya.

Stuka hapa tauni
 
kaa nae uzungumze nae direct au ukiona vp pima kwanza upendo wake kwa kujifanya na wew shida zimekuandama na huna hela ili uone je atakuwa katka hali ipi kwako juu ya hilo.
 
Hakuna mwanaume wa aina hiyo, huyo ni tapeli wa mjini tu hawezi kukuoa. Mpotezee kabisa na epuka kujilazimisha kuolewa, utaolewa na viruka njia utajuta. Mwombe Mungu na jipe matumaini.
 
Kuna wanaume wa kabila fulani wengi wao wanatabia hizo! huyu wa kwako kabila gani?
 
Back
Top Bottom