Deva
JF-Expert Member
- May 29, 2018
- 1,238
- 1,801
Habari za asubuhi wakuu.
Kwanza nianze na mtiririko wa matukio.
Asubuhi nimeenda kwenye shughuli zangu,nikawasiliana naye vizuri tukaagana kama ilivyo kawaida ya wapenzi wengi, jioni nimetoka kwenye shughuli, nikampigia simu tukawasiliana vizuri nikamuambia kuwa nimechoka sana ngoja nijipumzishe lisaa limoja hiyo ilikuwa saa 12:30 jioni, akasema haya basi tutawasiliana kesho, nikamuuliza kesho? Kwanini iwe kesho na ninajipumzisha lisaa limoja tu? Hakujibu akakata simu, nikamtumia sms kwamba nalala lisaa limoja, akanijibu usiku mwema, hiyo ilikuwa saa 12:30 jioni, sikuijibu.
Nimeamka lisaa limoja baadae sikumtumia sms tena maana niliona kama ananizuia nisiwasiliane naye, hapo hatuna ugomvi wowote, nikawa namuona tu online whatsapp, ila sikumtafuta maana alinionesha dalili za kunikwepa kwa siku hiyo, nikajiongeza labda ana mood mbaya, nikampa uhuru kidogo, sikutaka kulazimisha mawasiliano, mida ya saa tano usiku akanitumia sms ya usiku mwema nikamjibu asante, siku ikawa imeisha hivyo.
Kesho yake asubuhi nikampigia sinu kumjulia hali hakupokea na sms hakujibu, basi nikaenda kwenye shughuli zangu, niliporudi nikamtafuta tena, nikakuta simu ipo busy nikamtumia sms kuwa akimaliza anitafute, ila hakunitafuta, muda ulipopita mwingi nikamtafuta mimi, nikazungumza nae kidogo akasema nikate, anataka kuzungumza na mtu kwenye simu, nikasema sawa ukimaliza nitafute, hakufanya hivyo, na mimi nikakaa kimya mpaka pale alipokuja kunitumia usiku mwema, nikaijibu asante, siku ya pili ikawa imeisha, tatizo halijulikani ni nini.
Kesho yake akaamka akihitaji tuachane, nikauliza sababu ni nini, akasema mimi namdharau, simuheshimu wala simthamini namchukulia wa ziada tu, tulivutana kwa muda nikijaribu kumuelezea mahali anapokosea, hakukubali, nilimueleza dalili zote na yote aliyokuwa anafanya, mimi siwezi kulazimisha mawasiliano, pale aliponikwepa nilikaa kimya.
Matokeo yake ni tumeachana, kwa yeye kunilaumu mimi, mimi nimeshafanya kinachonipasa kufanya, maana sidhani kama ningeweza kuendelea kumsumbua mtu anayenitakia usiku mwema saa 12 jioni, na story yetu ya mahusiano ikaishia hapo.
Kwanza nianze na mtiririko wa matukio.
Asubuhi nimeenda kwenye shughuli zangu,nikawasiliana naye vizuri tukaagana kama ilivyo kawaida ya wapenzi wengi, jioni nimetoka kwenye shughuli, nikampigia simu tukawasiliana vizuri nikamuambia kuwa nimechoka sana ngoja nijipumzishe lisaa limoja hiyo ilikuwa saa 12:30 jioni, akasema haya basi tutawasiliana kesho, nikamuuliza kesho? Kwanini iwe kesho na ninajipumzisha lisaa limoja tu? Hakujibu akakata simu, nikamtumia sms kwamba nalala lisaa limoja, akanijibu usiku mwema, hiyo ilikuwa saa 12:30 jioni, sikuijibu.
Nimeamka lisaa limoja baadae sikumtumia sms tena maana niliona kama ananizuia nisiwasiliane naye, hapo hatuna ugomvi wowote, nikawa namuona tu online whatsapp, ila sikumtafuta maana alinionesha dalili za kunikwepa kwa siku hiyo, nikajiongeza labda ana mood mbaya, nikampa uhuru kidogo, sikutaka kulazimisha mawasiliano, mida ya saa tano usiku akanitumia sms ya usiku mwema nikamjibu asante, siku ikawa imeisha hivyo.
Kesho yake asubuhi nikampigia sinu kumjulia hali hakupokea na sms hakujibu, basi nikaenda kwenye shughuli zangu, niliporudi nikamtafuta tena, nikakuta simu ipo busy nikamtumia sms kuwa akimaliza anitafute, ila hakunitafuta, muda ulipopita mwingi nikamtafuta mimi, nikazungumza nae kidogo akasema nikate, anataka kuzungumza na mtu kwenye simu, nikasema sawa ukimaliza nitafute, hakufanya hivyo, na mimi nikakaa kimya mpaka pale alipokuja kunitumia usiku mwema, nikaijibu asante, siku ya pili ikawa imeisha, tatizo halijulikani ni nini.
Kesho yake akaamka akihitaji tuachane, nikauliza sababu ni nini, akasema mimi namdharau, simuheshimu wala simthamini namchukulia wa ziada tu, tulivutana kwa muda nikijaribu kumuelezea mahali anapokosea, hakukubali, nilimueleza dalili zote na yote aliyokuwa anafanya, mimi siwezi kulazimisha mawasiliano, pale aliponikwepa nilikaa kimya.
Matokeo yake ni tumeachana, kwa yeye kunilaumu mimi, mimi nimeshafanya kinachonipasa kufanya, maana sidhani kama ningeweza kuendelea kumsumbua mtu anayenitakia usiku mwema saa 12 jioni, na story yetu ya mahusiano ikaishia hapo.