Mzito Kabwela
JF-Expert Member
- Nov 28, 2009
- 18,857
- 7,617
Simu huwa inapata joto hasa wakati processor nafanya kazi sana na hii huendeshwa na shughuli ambazo unafanya na simu.
Kuna app ambazo huwa zinatumia sana nguvu ya simu kama GPS, mwanga wa flash ya simu, display ya simu.
1. Ili simu yako ipunguze joto angalia kama GPS iko on. Ama iko on weka off. Natumia tu wakati unatumia map (Google map)
2. Pia punguza mwanga wa simu yako au weka auto.
3. Uwe unamtindo wa kuzima na kuwasha simu angalau kila siku mara moja.
4. Wakati wa kucharge simu, izime kabisa, hii huondoa joto la processor na battery.
5. Tumia charger original ya simu siku zote.
Umejibu kitaalam sana mkuu. Ubarikiwe