Hata iweje siwezi kuacha kukagua simu ya bebi mimi...Hbr yenu wakuu
Nawaalika tujadili kwa pamoja kama ni vyema Mke na mume kukaguana simu.
Nijuavyo Mimi simu ya kiganjani ni Mali binafsi kwa matumizi binafsi na haipaswi kutazamwa na mtu asiye mmliki pasi ya ruhusa ya mmiliki.
Wewe unasemaje?
Aaaaah wapi wewe hiyo ni suprise, hajui ni lini wala sa ngapi nitaishikaOmba ruhusa kabla ya zoezi. Ndio maana hata polisi huwa na search warrant kwa kazi km hiyoo
Sio wanawake hat wanaume pia na kumbuka baba ndo kichwa cha familia
Ndoa siku hizi nyingi ni jina tuu kila mtu ana yake na usiri wake
Kikubwa kama unaona mwenzio anafanya Yale majukumu yake hakuna dalili za michepuko mshukuru Mungu na usipekue simu yake cos unaweza haribu furaha yako ya maisha
Na kama ni hawara au mchepuko usijaribu kupekua kabisa utaweza kupoteza maisha
mkifutliiana mpaka kwenye cm hakika hata kama mnapendana hamwezi kudumu ktk uhusiano kwanza ni wivu wa kijinga utaishia kuumizwa tuu
Ukiendekeza sana upekuzi utakufa kwa pressure by the way kila mmoja ana privacy zake
Sijambo jema kukagua simu ya mtu/mpenzi/mume. lakini mara nyingi mtu anajengewa dhamira ya kukagua hata kama alikuwa hapendi. unakuta mume/mke/mpenzi simu ikiita anakimbia kuongelea nje,au akiongelea ndani anagugumia kama amebanwa na kitu,simu imejaa password kila eneo, usiku simu zake zote zimezimwa.lazima mwenza atataka kujua kuna nini kwenye simu maana mwenye simu amejenga mazingira. binafsi bora nipate presha lakini nijue naishi na mtu wa aina gani. Siwezi jifanya namuamini hali dalili za kutokuwepo uaminifu zinaonekana wazi.
Ukiomba unapewa baada ya sms zote kufutwa na calls kufutwa. ukiweza kufanya timing nzuri ukaingia unakutana na madudu mengi ya kutisha, kwangu mimi ni heri maana nitakuwa nimemjua mwenza wangu yupoje na niishi nae vipi.Omba ruhusa ya kukagua please. Omba password
Ukiomba unapewa baada ya sms zote kufutwa na calls kufutwa. ukiweza kufanya timing nzuri ukaingia unakutana na madudu mengi ya kutisha, kwangu mimi ni heri maana nitakuwa nimemjua mwenza wangu yupoje na niishi nae vipi.
watu wanabadilika hasa wanaume, anapokuwa hana pesa na anapokuwa nazo ni tofauti sana.Kwanini uolewe nae humjui? Akifuta kabla hujaona anakujali. Hataki kukuumiza