Simu na decoder zinafanana?

Simu na decoder zinafanana?

JAYJAY

JF-Expert Member
Joined
Oct 31, 2008
Posts
8,902
Reaction score
9,338
Nimekuwa nikijiuliza sana kuhusu ufanyaji kazi wa hivi vitu naona kama zinafanana.kwamba kila kimojawapo inawezekana kinatumiwa mawasiliano ya kipekee na provider wa huduma tofauti na matangazo ya redio na tv ambazo ni za free.mfano mtumiaji A ambaye hajalipa hapati huduma wakati huohuo mtumiaji B aliyelipa anapata huduma.mwenye ufahamu naomba anijibu 1. inawekana vipi kumnyima huduma mmoja na kumuhudumia mwingine, na 2. kuna tofauti gani kati ya mawimbi ya decoder na yale ya simu na 3. Je kuna uwezekano wa minara ya simu kutumika kurusha matangazo ya tv hasa hizi za decoder jambo ambalo litawezesha maeneo mengi kufikiwa kirahisi au kuna ugumu hapo na kama upo ni upi?ngoja niishie hapa .
 
Mkuu mimi sio mtaalamu wa hii maneno lakini in simple logic hivi vitu vipo tofauti.
Simu inauwezo wa kupokea na kurusha mawimbi wakati decorder inapokea tu.
Swala la mnara ni kuwa mnara kama mnara sio issue, issue ni kuwa mnara ukisimamishwa je juu yake umefungwa kitu gani kufanya kitu gani.
Tofauti na radio hizi huduma kama simu, decorder nk ili imfikie mteja kunakuwa na njia yake kwa kila mteja, mfano kwa simu ni sim card ndio njia kati ya mteja na provider so kama hujalipa inafungwa njia yako tu ya mwingine inakuwa wazi.
 
Habarini wanawane.

Simu:
Ni kifaa kinachotumika kufanya mawasiliano kati ya sehemu mbili yaani mpigaji na mpokeaji. Mawasiliano haya yanaweza kuwa katika mawimbi kama ni wireless au katika signal kama ni wired. Kila mwenye simu anayo akaunti yake ambapo katika hii akaunti kuna baadhi ya vigezo inabidi awenavyo ili aweze kupiga au kupokea simu. Kigezo kimojawapo ni kuwa na salio ili uweze kupiga simu. Na salio hilo hupungua kulingana na vigezo vilivyowekwa na mtoa huduma (Service Provider).


Decoder:

Ni chombo kinachotumika ku-encode coded information. Yaani ni chombo kinachotumika ku-reverse transmitted information in order to obtain its original form.

Lakini mimi nadhani hapa wewe umetumia neno decoder kumaanisha kile chombo kinachoungwa ili kupata aina fulani ya stesheni za television. Hata kama ni hicho, kazi yake ndio hiyohiyo. Na kinavyofanya kazi pia kinatumia "user account" ambayo ni sawa na namba yako ya simu. Kwenye hiyo akaunti kunazo habari za mtumiaji pamoja na vigezo vingine ili uweze kuendelea kupata huduma.


Decoder inaweza kupokea na kutuma mawimbi kama imekuwa enabled kufanya hivyo na mtoa huduma. Ndio maana unakuta kuna vipindi ambavyo ni "interactive" kwenye baadhi ya stesheni za televisheni.

Kwa hiyo basi ufanyaji kazi wake kwa urahisi ni kuwa vyote yaani, decoder na simu, vinafanya kazi kwa kutumia vigezo vilivyowekwa kwenye "user account - attributes"

Nawasilisha
 
yaaah @JF umetumia lugha rahisi sana,nadhani hakuna lugha rahisi kama hiyo,mimi ni mdau wa mawasiliano lakini nilikuwa nashindwa kupata lugha lahisi kuwasilisha ,Nadhani JAY umeridhika, big up JF
 
Technicaly unaweza sema kwamba decoder ni kifaa kinachoweza badili x input chanels to maximum of 2^x chanels. Yan wakat wa kutuma informations unatuma informations nyng katika hzo x channel na decoder kaz yake ni kurudisha hzo x chanels kwenda kwenye <= 2^x chanels. Nadhan umenpata. Kwa upande wa simu kama simu cdhan kama kuna decoder ndan yake, kwan inapokea decoded information kutoka ktk base tranceiver station (BTS) ya karibu nayo. Kitu spesho ambacho cmu inayo ni modulator na demodulator (modem). Kwa upande wa decoder za tz n kwamba chanel nyng znatumwa katika say x comunictn chanels na decoder inaznyambua kwenda ktk chanel nyng zaid. Wanafanya hivi kusave bandwidth during transmision. Nadhan umenipata. Kuhusu masuala ya security ni mangezeko yanayofanywa na kampun husika lyk dstv does. Na hapo tutakuwa tunahamia ktk masuala ya cryptography.
 
Back
Top Bottom