Simu kutoka kwa baba mkwe

Kajuni

JF-Expert Member
May 27, 2009
486
186
Wana JF kwanza kabisa shalom. Ni jumamosi tulivu pande za hapa Dar na hali ya hewa ni manyunyu manyunyu! Nikiwa katika harakati za kumalizia vipolo vya kazini mara napokea simu kutoka kwa baba mkwe. Namsalimia kwa heshima na tahadhima kwani ndiye mzaa chema (mke wangu). Ama baada ya salamu baba mkwe ana anza kunishutumu kwamba sisi pamoja na binti yake hatuwaheshimu na hatuwajali kwa sababu jana tulishindwa kupeleka japo ua kwa mama mkwe kama zawadi ya kuadhimisha sikukuu ya kuzaliwa. Baba mkwe aliendelea kutiririka kwamba sisisi tumekuwa na mkono wa birika! Na hata siku moja hatujawahi kuwapa zawadi japokuwa wao wamekuwa mstari wa mbele katika hilo.
Kikubwa ni kwamba mimi nimezaliwa na kuishi na kusomea kwenye hizi shule zetu za kayumba! Uaratibu huu wa kushelekea siku za kuzaliwa nilianza kukuana nao nikiwa chuo kikuu. Sikuwahi kushelekea katika kukua kwangu wala sikumuona baba na mama yangu wakitunulia zawadi wakati wa hii siku nyeti. Sina nia mbaya ya kutopeleka zawadi kwa mama mzaa chema lakini mazingira niliyokulia yanachangia sana mimi kutokuwa sensitive na hizi ishu!
Sasa wandugu nifanyeje kwani Jumamosi leo nimeambulia lawama na shutuma.
 
inabidi mke wako akaongee na wazazi wake, mambo ya kubebeshana nyani ukubwani kweli haifai.

Hizi mila za kukopi na kupaste wala hazina mashiko kihivyo, je siku akilazwa ukashindwa kwenda muona si utanyang'anywa mke?

Kukwazana bure tu kwa kweli, ila ningekuwa mie nisingemkopesha hata kidogo.
 
Pole sana,subiri siku zipite kidogo,then kamuone na ukaongee naye kwa maneno ya utararibu na heshima..nadhani hapo utakuwa umerekebisha mambo..
 
inabidi mke wako akaongee na wazazi wake, mambo ya kubebeshana nyani ukubwani kweli haifai.

Hizi mila za kukopi na kupaste wala hazina mashiko kihivyo, je siku akilazwa ukashindwa kwenda muona si utanyang'anywa mke?

Kukwazana bure tu kwa kweli, ila ningekuwa mie nisingemkopesha hata kidogo.

Kabisa my dear, umenena vyema mdada
 
Wana JF kwanza kabisa
shalom. Ni jumamosi tulivu pande za hapa Dar na hali ya hewa ni manyunyu
manyunyu! Nikiwa katika harakati za kumalizia vipolo vya kazini mara
napokea simu kutoka kwa baba mkwe. Namsalimia kwa heshima na tahadhima
kwani ndiye mzaa chema (mke wangu). Ama baada ya salamu baba mkwe ana
anza kunishutumu kwamba sisi pamoja na binti yake hatuwaheshimu na
hatuwajali kwa sababu jana tulishindwa kupeleka japo ua kwa mama mkwe
kama zawadi ya kuadhimisha sikukuu ya kuzaliwa. Baba mkwe aliendelea
kutiririka kwamba sisisi tumekuwa na mkono wa birika! Na hata siku moja
hatujawahi kuwapa zawadi japokuwa wao wamekuwa mstari wa mbele katika
hilo.
Kikubwa ni kwamba mimi nimezaliwa na kuishi na kusomea kwenye hizi shule
zetu za kayumba! Uaratibu huu wa kushelekea siku za kuzaliwa nilianza
kukuana nao nikiwa chuo kikuu. Sikuwahi kushelekea katika kukua kwangu
wala sikumuona baba na mama yangu wakitunulia zawadi wakati wa hii siku
nyeti. Sina nia mbaya ya kutopeleka zawadi kwa mama mzaa chema lakini
mazingira niliyokulia yanachangia sana mimi kutokuwa sensitive na hizi
ishu!
Sasa wandugu nifanyeje kwani Jumamosi leo nimeambulia lawama na
shutuma.

Sasa kama mkeo amekulia kwenye familia ya kubofya kwa nini asikuelekeze? Angalia mkuu usije ukanyang'anywa mke bure
 
wazazi wanapoanza kuiga mambo ya ughaibuni ni shida mnoo...ila kama ni ishu ya upande wa pili na weye unataka kushiriki ni bora ukajificha nyuma ya mkeo ili usihusike moja kwa moja...kwani utakua ni mchezo kila siku ...leo mama mkwe kesho dingi. kesho kutwa kipaimara..wiki ijayo harusi...THE LIST GOES ON
 
Wana JF kwanza kabisa shalom. Ni jumamosi tulivu pande za hapa Dar na hali ya hewa ni manyunyu manyunyu! Nikiwa katika harakati za kumalizia vipolo vya kazini mara napokea simu kutoka kwa baba mkwe. Namsalimia kwa heshima na tahadhima kwani ndiye mzaa chema (mke wangu). Ama baada ya salamu baba mkwe ana anza kunishutumu kwamba sisi pamoja na binti yake hatuwaheshimu na hatuwajali kwa sababu jana tulishindwa kupeleka japo ua kwa mama mkwe kama zawadi ya kuadhimisha sikukuu ya kuzaliwa. Baba mkwe aliendelea kutiririka kwamba sisisi tumekuwa na mkono wa birika! Na hata siku moja hatujawahi kuwapa zawadi japokuwa wao wamekuwa mstari wa mbele katika hilo.
Kikubwa ni kwamba mimi nimezaliwa na kuishi na kusomea kwenye hizi shule zetu za kayumba! Uaratibu huu wa kushelekea siku za kuzaliwa nilianza kukuana nao nikiwa chuo kikuu. Sikuwahi kushelekea katika kukua kwangu wala sikumuona baba na mama yangu wakitunulia zawadi wakati wa hii siku nyeti. Sina nia mbaya ya kutopeleka zawadi kwa mama mzaa chema lakini mazingira niliyokulia yanachangia sana mimi kutokuwa sensitive na hizi ishu!
Sasa wandugu nifanyeje kwani Jumamosi leo nimeambulia lawama na shutuma.
Zipokee tuu,lawama kaumbiwa mwanadamu!!!
 
Duh! Hatupishani sana mkuu, binafsi hata siku yangu ya kuzaliwa mara nyingi nakumbushwa na mail za JF, hapa nitakumbukaje d'day za mama au baba mzaa chema . Pole mkuu:sad:
 
Sasa kama mkeo amekulia kwenye familia ya kubofya kwa nini asikuelekeze? Angalia mkuu usije ukanyang'anywa mke bure

Sio rahisi kunyang'anywa mke. Walitoa kwa hiyo maji yalishamwagika! Hapa ni kuhifadhi tu heshima na mahusiano mazuri. Hakuna hoja ya kisheria hapo.
 
inabidi mke wako akaongee na wazazi wake, mambo ya kubebeshana nyani ukubwani kweli haifai.

Hizi mila za kukopi na kupaste wala hazina mashiko kihivyo, je siku akilazwa ukashindwa kwenda muona si utanyang'anywa mke?

Kukwazana bure tu kwa kweli, ila ningekuwa mie nisingemkopesha hata kidogo.

Asante sana mkuu kwa kweli nimebaki mdomo wazi na ikizingatia mie naishi Ukonga na wakwe wanaishi Mbezi mbichi na kazi ni posta sasa fikiria mziki wa foleni eti kuwaisha ua kwa mama mkwe?
 
Duh! Hatupishani sana mkuu, binafsi hata siku yangu ya kuzaliwa mara nyingi nakumbushwa na mail za JF, hapa nitakumbukaje d'day za mama au baba mzaa chema . Pole mkuu:sad:

Mkuu hata ya kwangu mie huwa nakumbushwa na hii mitandao... hata wazazi wangu wenyewe sikuzao za kuzaliwa huwa nasahau
 
Wakuu inaonekana kwamba ukipewa kitu lazima urudishe!!!
 
wazazi wanapoanza kuiga mambo ya ughaibuni ni shida mnoo...ila kama ni ishu ya upande wa pili na weye unataka kushiriki ni bora ukajificha nyuma ya mkeo ili usihusike moja kwa moja...kwani utakua ni mchezo kila siku ...leo mama mkwe kesho dingi. kesho kutwa kipaimara..wiki ijayo harusi...THE LIST GOES ON

Mkuu hii mambo imenisubua sana sana huu uzungu naona unakuwa shida juu ya shida
 
Kajuni sikubaliani na majibu ya Kongosho rafiki yangu wa moyoni. Kwanza kabisa nafikiri mkeo naijua vyema hali halis ya nyumbani kwao na utaratibu mzima. Kama na yeye anauona hauna mantiki kama wengi wetu hasa huu wa kusheherekea bday ni sawa pia. ila tusione kwamba ulipaswa kumjibu ama ukajipange kumrushia makombora mkweo kama alivyoonyesha Kongosho na namshukuru Mungu sana kwamba asiyo yeye manake angenitia aibu huyu.

ushauri wangu kwako, kwanza kabisa tulia kimya upepo huu upite kabisa na hali iwe shwari kabisa. kisha siku weye na mkeo mjipange mwende kuwaona wakwezo mkiwa mmejifungasha hata kwa kajisukari tu. siku mtakayokwenda mtaongea nao kwa upole na heshima juu ya kughafilika kwenu kuhusu tarehe ya mama ya kuzaliwa. Naamini kwa wazazi wastaarabu watawasamehe na mambo yataendelea kama kawaida.
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: BAK
Zawadi haiombwi wala kulazimishwa, ila pia kukosa fadhila si maungwana.

Ungepeleleza familia ikoje na wakwe wanataka nini kabla ya kuoa.

Inaonekana wakwe zako wanaweza kuwa na lao zaidi ya hili la zawadi.Haiyumkiniki mtu mzima kulilia zawadi kama mtoto anayelilia peremende.
 
Mkuu Bak kwa jinsi tunavyoishi na wakwe zangu hatuna matatizo na tumekuwa tunashirikiana katika shida na raha. Natumekuwa pale tunapokumbuka isipokuwa nimepata picha moja kwamba kumbe ukiona mtu anakupatia zawadi jua na wewe unatakiwa urudishe kwa kile kiwango.. am wondering ndo maana watu wakati wa harusi ubwaga machozi wakijua fika zile zawadi lazima zilipwe... je ni sahii kukataaa zawadi kama unajua hutaweza kuzilipa?
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Zawadi haiombwi wala kulazimishwa, ila pia kukosa fadhila si maungwana.

Ungepeleleza familia ikoje na wakwe wanataka nini kabla ya kuoa.

Inaonekana wakwe zako wanaweza kuwa na lao zaidi ya hili la zawadi.Haiyumkiniki mtu mzima kulilia zawadi kama mtoto anayelilia peremende.
Mkuu kiranga hapo ndo pana nishangaza kwani inaonekana kwamba kuna jambo nyuma ya pazia...
 
Mkuu Bak kwa jinsi tunavyoishi na wakwe zangu hatuna matatizo na tumekuwa tunashirikiana katika shida na raha. Natumekuwa pale tunapokumbuka isipokuwa nimepata picha moja kwamba kumbe ukiona mtu anakupatia zawadi jua na wewe unatakiwa urudishe kwa kile kiwango.. am wondering ndo maana watu wakati wa harusi ubwaga machozi wakijua fika zile zawadi lazima zilipwe... je ni sahii kukataaa zawadi kama unajua hutaweza kuzilipa?

Mkuu Kajuni hakuna ubaya wowote wa kubadilishana zawadi kati ya wanandoa na in laws wapande zote mbili. Kama alivyosema gfsonwin mkeo anajua hali halisi ya kwao inapokuja kwenye mambo ya kusherehekea Birthday kwa hiyo ni vizuri kuendelea kulipa uzito jambo hilo hata kama nyie wenyewe hamlifagilii. Swali kama mmejaliwa watoto je nao birthday zao zinapita kimya kimya bila hata card au kasherehe kadogo?

Sidhani kama ukipewa zawadi ya shilingi laki moja nawe inabidi urudishe zawadi ya kiasi hicho kwani waswahili walisema mtu hujikuna pale mkono wake unafika...Hivyo wakwe zako bila shaka wanafahamu financial position yenu kama uwezo wenu ni zawadi ya shilingi 50,000 basi hawataona tatizo lakini kama kweli mna mkono wa birika pamoja na kuwa mna vipato vikubwa basi hapo pia inabidi mbadilike na kunyoosha mikono yenu ili iwe mirefu zaidi.



 
Mkuu hata ya kwangu mie huwa nakumbushwa na hii mitandao... hata wazazi wangu wenyewe sikuzao za kuzaliwa huwa nasahau

Kajuni haya mambo ya ku-copy na ku-paste yanatusumbua wengi. Mi na wife wangu tumejitahidi kuwa tunawafanyia besdei angalau watoto wetu, cha ajabu huwa tunajikuta wote tumesahau mpaka tunakumbushwa na marafiki zetu wa nje kwa emails! watoto bado wadogo hawawezi kukumbuka ili watushtue. Kwa asili ni utamaduni ambao si wetu so unaleta shida sometimes
 
Back
Top Bottom