Simbachawene, vyeo vya Michongo havipo Halmashauri. Umesahau nini?

Mizega

Senior Member
Feb 10, 2021
143
304
Habari za leo wana jamvi,

Tarehe 7.7.2023 Gazeti la Mwananchi lilichapisha nukuu ya hotuba ya Mhe. Waziri Simbachawene ambaye ni Waziri wa Mashauri ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora hapa Nchini.

Katika habari hiyo, Mhe Waziri amewatuhumu Maafisa Utumishi kwamba wanagawa vyeo kwa michongo ya rushwa kuanzia milioni 5 hadi 10 katika Mamlaka za Serikali za Mitaa. Katika hotuba hiyo Mhe. Simbachawene alikemea na kuonya Maafisa Utumishi kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa.

Binafsi nimeshangazwa na taarifa hii, na kwa pekee nilijiuliza kwamba Mhe. Simbachawene amesahau nini?
1. Mamlaka za uteuzi katika Halmashauri nchini si Afisa Utumishi. Mkurugenzi wa Halmashauri ndiye Katibu wa mamlaka ya ajira.
2. Baraza la Madiwani ndilo linalopendekeza na kuthibitisha uteuzi wa mkuu wa idara.
3. Vibali vya kukaimu vinatoka kwenye ofisi ya Simbachawene.
4. Vetting hufanya na taasisi yetu ya usalama.

Sasa kwa muktadha huu ni wapi Afisa utumishi atachukua mchongo wa milioni 5 au 10? Lakini tuseme ukweli, kati ya Halmashauri na Pale kwa Mhe Simbachawene, wapi ndiko kwenye Michongo?

1. Vipo vyeo vya uteuzi vyenye miongozo yake, mfano nafasi ya DAS anayeteuliwa kwa mujibu wa PMG ni Afisa utumishi au afisa tawala aliye mwandamizi. Je mhe. Simbachawene hawa ma DAS ambao umewatoa UVCCM, walio kuwa wafanyabiashara nje ya utumishi, hawa walio makada walimu hao ni Maafisa utumishi/tawala waandamizi? Huo siyo mchongo?

2. Kwa mujibu wa nyaraka zilizopo mtu mwenye Sifa za kuteuliwa kuwa mkurugenzi wa Halmashauri anapaswa kuwa Afisa Mwandamizi tena mkuu wa Idara kwa miaka isiyopungua 8 katika utumishi wa Serikali za Mitaa. Je, hawa ma DED uliowachukua mtaani na kuwapatia halmashauri zetu ndiyo mchongo unaouzungumzia? Ama kweli umeongea kwa mafumbo.

3. Katibu Tawala wa Mkoa anapaswa kuwa Afisa mwandamizi Serikalini, anaweza kuwa DED, DAS, ambaye ametumika kwa miaka zaidi ya 14 katika uandamizi serikalini. Hawa baadhi uliochukua hapa na pale ndiyo tuaminini kwamba ni Michongo uliyosema?

4. Utumishi wa umma una miongozo lukuki, upo mpango wa kurithishana madaraka ambao ofisi yako imeutupa chini, ipo PMG ya Sekretarieti za Mikoa ambayo pia umeikanyaga, mathalan zipo Kanuni za uendeshaji wa Serikali za Mitaa zinazoonesha nafasi za uteuzi na taratibu zake ambazo pia umezikanyaga. Hapa ndipo kwenye michongo.

5. Si ofisi yako inayoshusha watu moja kwa moja na kuwaacha watumishi waliokuwa wanakaimu nafasi za uongozi katika Mikoa na Halmashauri. Ofisi yako inatoa vibali vya kukaimu madaraka halafu wakati wa uteuzi mtu huyo uliyempa kibari unamwacha unaleta mtu wa kuokota hapa na pale, tuamini ndiyo michongo yenyewe?

6. Utumishi wa umma hauna ladha, watu wanajiendeea bila kuwa na matumaini ya kuwa viongozi, ndiyo maana CAG hataacha kubaini madudu..eat and run, the future is not guaranteed.

Kwa ujumla hebu turejee nyaraka za akina Rugumyamheto tuujenge upya utumishi wa umma. Kwa sasa ni kumbakumba ilimradi watu waende.
Mhe. Simbachawene, achana na Maafisa utumishi na utawala wa Halmashauri.

Michongo ipo ofisini kwako baada ya wewe mwenyewe kukubali kukanyaga Nyaraka, Kanuni, Taratibu na Miongozo ambayo ofisi yako ndiyo inayosimamia.

Wasalaam.
 
Habari za leo wana jamvi,
Tarehe 7.7.2023 Gazeti la Mwananchi lilichapisha nukuu ya hotuba ya Mhe. Waziri Simbachawene ambaye ni Waziri wa Mashauri ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora hapa Nchini.
Katika habari hiyo, Mhe Waziri amewatuhumu Maafisa Utumishi kwamba wanagawa vyeo kwa michongo ya rushwa kuanzia milioni 5 hadi 10 katika Mamlaka za Serikali za Mitaa. Katika hotuba hiyo Mhe. Simbachawene alikemea na kuonya Maafisa Utumishi kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa.
Binafsi nimeshangazwa na taarifa hii, na kwa pekee nilijiuliza kwamba Mhe. Simbachawene amesahau nini?
1. Mamlaka za uteuzi katika Halmashauri nchini si Afisa Utumishi. Mkurugenzi wa Halmashauri ndiye Katibu wa mamlaka ya ajira .
2. Baraza la Madiwani ndilo linalopendekeza na kuthibitisha uteuzi wa mkuu wa idara
3. Vibali vya kukaimu vinatoka kwenye ofisi ya Simbachawene
4. Vetting hufanya na taasisi yetu ya usalama
Sasa kwa muktadha huu ni wapi Afisa utumishi atachukua mchongo wa milioni 5 au 10?
Lakini tuseme ukweli, kati ya Halmashauri na Pale kwa Mhe Simbachawene, wapi ndiko kwenye Michongo?

1. Vipo vyeo vya uteuzi vyenye miongozo yake, mfano nafasi ya DAS anayeteuliwa kwa mujibu wa PMG ni Afisa utumishi au afisa tawala aliye mwandamizi. Je mhe. Simbachawene hawa ma DAS ambao umewatoa UVCCM, walio kuwa wafanyabiashara nje ya utumishi, hawa walio makada walimu hao ni Maafisa utumishi/tawala waandamizi? Huo siyo mchongo?
2. Kwa mujibu wa nyaraka zilizopo mtu mwenye Sifa za kuteuliwa kuwa mkurugenzi wa Halmashauri anapaswa kuwa Afisa Mwandamizi tena mkuu wa Idara kwa miaka isiyopungua 8 katika utumishi wa Serikali za Mitaa. Je, hawa ma DED uliowachukua mtaani na kuwapatia halmashauri zetu ndiyo mchongo unaouzungumzia? Ama kweli umeongea kwa mafumbo.
3. Katibu Tawala wa Mkoa anapaswa kuwa Afisa mwandamizi Serikalini, anaweza kuwa DED,DAS, ambaye ametumika kwa miaka zaidi ya 14 katika uandamizi serikalini. Hawa baadhi uliochukua hapa na pale ndiyo tuaminini kwamba ni Michongo uliyosema?
4. Utumishi wa umma una miongozo lukuki, upo mpango wa kurithishana madaraka ambao ofisi yako imeutupa chini, ipo PMG ya Sekretarieti za Mikoa ambayo pia umeikanyaga, mathalan zipo Kanuni za uendeshaji wa Serikali za Mitaa zinazoonesha nafasi za uteuzi na taratibu zake ambazo pia umezikanyaga. Hapa ndipo kwenye michongo
5. Si ofisi yako inayoshusha watu moja kwa moja na kuwaacha watumishi waliokuwa wanakaimu nafasi za uongozi katika Mikoa na Halmashauri. Ofisi yako inatoa vibali vya kukaimu madaraka halafu wakati wa uteuzi mtu huyo uliyempa kibari unamwacha unaleta mtu wa kuokota hapa na pale, tuamini ndiyo michongo yenyewe?
6. Utumishi wa umma hauna ladha, watu wanajiendeea bila kuwa na matumaini ya kuwa viongozi, ndiyo maana CAG hataacha kubaini madudu..eat and run, the future is not guaranteed.

Kwa ujumla hebu turejee nyaraka za akina Rugumyamheto tuujenge upya utumishi wa umma. Kwa sasa ni kumbakumba ilimradi watu waende.
Mhe. Simbachawene, achana na Maafisa utumishi na utawala wa Halmashauri. Michongo ipo ofisini kwako baada ya wewe mwenyewe kukubali kukanyaga Nyaraka,Kanuni,Taratibu na Miongozo ambayo ofisi yako ndiyo inayosimamia.

Wasalaam.
Pamoja na hayo hamuwezi kukwepa lawama za rushwa na unyanyasaji wa watumishi wa umma.

Nina mifano hai mingi ya maafisa utumishi kuvunja ndoa za watumishi wao kwa kutembea na wake za watu watumishi,nina ushuhuda wa mwalimu aliyeambukizwa ukimwi na Afisa utumishimara tu baada ya kuripoti kazini kutokana na kuwekewa mazingira magumu ya kupata stahiki zake huku afisa akiomba rushwa ya ngono.

Wapo watumishi ambao hawapandi madaraja hadi watoe pesa kwanza.

Ni mambo mengi sana ya hovyo yanayokatisha tamaa kazini.Huwa nikisikia wananchi wanalalamikia watumishi wa umma kwa utendaji wao,nabaki nawaonea huruma tu watumishi hao maana wao wanapata maumivu makubwa sana ya manyanyaso na hawana pa kulilia.Maana hata wakilia kwenye forum kama hizi,wataishia kutukanwa na kubezwa tu na vijana wasaka ajira wenye uchungu( nongwa) waliojazana humu.

Kitendo cha waziri kuwatuhumu na kuwaonya,ingawa ilikuwa ni siasa tu,angalau kinaonesha kumbe madudu yenu viongozi wanajua ila ni kwa vile tu wameamua kuwalinda,ndio maana hayaishi.
 
Pamoja na hayo hamuwezi kukwepa lawama za rushwa na unyanyasaji wa watumishi wa umma.

Nina mifano hai mingi ya maafisa utumishi kuvunja ndoa za watumishi wao kwa kutembea na wake za watu watumishi,nina ushuhuda wa mwalimu aliyeambukizwa ukimwi na Afisa utumishimara tu baada ya kuripoti kazini kutokana na kuwekewa mazingira magumu ya kupata stahiki zake huku afisa akiomba rushwa ya ngono.

Wapo watumishi ambao hawapandi madaraja hadi watoe pesa kwanza.

Ni mambo mengi sana ya hovyo yanayokatisha tamaa kazini.Huwa nikisikia wananchi wanalalamikia watumishi wa umma kwa utendaji wao,nabaki nawaonea huruma tu watumishi hao maana wao wanapata maumivu makubwa sana ya manyanyaso na hawana pa kulilia.Maana hata wakilia kwenye forum kama hizi,wataishia kutukanwa na kubezwa tu na vijana wasaka ajira wenye uchungu( nongwa) waliojazana humu.

Kitendo cha waziri kuwatuhumu na kuwaonya,ingawa ilikuwa ni siasa tu,angalau kinaonesha kumbe madudu yenu viongozi wanajua ila ni kwa vile tu wameamua kuwalinda,ndio maana hayaishi.
Ni kweli, suala la uzinzi si la Afisa utumishi, ni human nature. Ni kweli Maafisa Utumishi wana udhaifu ila si katika suala la uteuzi. Mhe. Simbachawene angezungumzia tuhuma hizo ulizosema ningemwelewa lakini suala la vyeo vya michongo ofisi yake ndiyo yenye michongo
 
Back
Top Bottom