Simbachawene: Job Ndugai atakumbukwa kwa usimamizi wa sheria na Mageuzi makubwa katika jimbo lake la Kongwa

Simbachawene: Job Ndugai atakumbukwa kwa usimamizi wa sheria na Mageuzi makubwa katika jimbo lake la Kongwa

Just Pray

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
2,142
Reaction score
4,777
Aliyekuwa mbunge wa Jimbo la Kibakwe mkoani Dodoma, George Simbachawene, amesema kuwa Spika mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Job Ndugai, atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa katika kusimamia utungwaji wa sheria ya Makao Makuu ya nchi yaliyopo Dodoma.

Akizungumza katika mahojiano kwenye kipindi cha Jambo Wikendi cha TBC1 leo Agosti 10, 2025, Simbachawene ameongeza kuwa katika kipindi cha uongozi wake, Hayati Job Ndugai alitoa mchango mkubwa katika utengenezaji wa sheria na kanuni za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

 
Uzalendo ndio tatizo kubwa kweli.
Magonjwa ya taifa hili,gonjwa baya kabisa ni ubinafsi.
 
Aliyekuwa mbunge wa Jimbo la Kibakwe mkoani Dodoma, George Simbachawene, amesema kuwa Spika mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Job Ndugai, atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa katika kusimamia utungwaji wa sheria ya Makao Makuu ya nchi yaliyopo Dodoma.

Akizungumza katika mahojiano kwenye kipindi cha Jambo Wikendi cha TBC1 leo Agosti 10, 2025, Simbachawene ameongeza kuwa katika kipindi cha uongozi wake, Hayati Job Ndugai alitoa mchango mkubwa katika utengenezaji wa sheria na kanuni za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
tunasubiri sifa za uwongo hapo kesho
 
Majimbo ya Dodoma yana umasikini wa hali ya juu.

Hapo Kongwa kwa Ndugai panatia huruma ukienda sio barabara sio maji ni kakijiji fulani tu cha masikini

Kwa Simbachawene jimbo la Kibakwe ufukara umerindima hatari

Na wana miaka zaidi ya 15 bungeni barabara za majimbo yao hazipitiki
 
Wagogo wengi ni wajinga sn, pamoja na uzee wangu sijawahi kuona mgogo tajiri zaidi ya ombaomba, Dodoma mjini kukuta biashara kubwa ya mgogo ni ngumu sn matokeo yake ni kuwa na watu wajinga kama huyu mpuuzi.
 
Majimbo ya Dodoma yana umasikini wa hali ya juu.

Hapo Kongwa kwa Ndugai panatia huruma ukienda sio barabara sio maji ni kajiji fulani tu cha masikini

Kwa Simbachawene jimbo la Kibakwe umasikini umerindima hatari

Na wana miaka zaidi ya 15 bungeni barabara za majimbo yao hazipitiki
Ni aibu tupu mkuu, ukitoka Dodoma mjini nayo sababu ya kuwa ofisi nyingi za serikali zipo hapo ni pana mafukara wa kutosha.
 
Back
Top Bottom