Simba SSC- Uongozi unacheza na akili zenu

Simba SSC- Uongozi unacheza na akili zenu

Megawatt B

JF-Expert Member
Joined
Aug 23, 2011
Posts
259
Reaction score
69
Miezi kadhaa nilileta thread hapa kuwaulikiza wanachama na wapenzi wa simba, nani kaona eneo au kiwanja Rage na uongozi wa simba wanasema watajenga uwanja. sikupata jibu. Uongozi wa Rage umebakiza muda mfupi tu hata uwanja wa mazoezi hakuna na alijinasibu kuwa uwanja utajengwa katika kipindi hiki, hakuna. alianza kuwapa moyo wanaSimba kuwa anamakubaliano na waturuki hadi leo imebaki hadithi tu.
Akasoma alama za nyakati kwenye mkutano wa juzi, akatafuta mbinu ya kuwapumbaza wanasimba na kuwa aambia kuwa fedha za Okwi zitaanzia ujenzi, mbona habari ya waturuki haikusemwa? anawaambia fedha za Okwi huku akijua Okwi hakufaulu na hakuna hata kashilingi, watu wameshangilia jamaa anapeta tu. Akwapumbaza tena, eti wamelipia Tsh. 50 milioni bado 30. watu wakachanga zaidi ya hizo, hivi kweli simba inashindwa kukusanya milion 80 kwa miaka minne kweli? kama milion 30 zilichangwa chap chap pale kwenye mkutano wameshindwaje kuchanga hata milioni mia mbili kwa miaka mitatu iliyopita ya uongozi huu wa Rage? mbona wachezaji wananunuliwa kwa mamilioni ya shilingi kila mwaka? Hebu tujiulize..
1 .Kiwanja cha Bunju kibo Bunju ipi - A au B?
2. Miaka miaka 70 ya klabu, hata heka mbili tu za mazoezi?
3. Wale waturuki wapo wapi
4. Fedha za Okwi, zinakuja lini, ujenzi uanze
5. Zile zilizochangwa pale kwenye mkutano zimelipwa? risiti ipo wapi
6. Rambi rambi za Mafisanago maelezo yake yakoje? mbona hata hitima ishapita
7.

Hakika Simba ni shamba la bibi. Jiulize:
 
Tatizo ni uwepo wa huyu msomali kuwa kiongozi wa simba.
 
umeanza mapema sana kampeni, kwa nn hukuuliza ktk mkutano mkuu wa club? hukumuona Rage kwenye mkutano? unategemea ni nani anaye weza kukupa majibu kama si Rage na makamu wake?
 
Leo nimeamka na wazo jipya,nafikiri iko haja ya mimi kwenda kugombea 1 ya nafasi za juu kabisa za uongozi wa team ya Simba,labda (nasema tena,labda) kosa langu ni kujipambanua mapema hapa JF kuwa moyo wangu umelalia wapi lkn No....nitakwenda, wengi (naomba nieleweke vizuri hapa,wengi) wa Wanachama na Mashabiki wa Simba ni s hapanio waelevu shaka watanichagua tu.
Waliambiwa Mwenyekiti amekamilisha kazi ya Twite na angetambulishwa kwenye Mkutano mkuu,siku ya mkutano inafika hola...wakaambiwa tena angekipiga siku ya Simba day,siku ya Simba Day ikafika hola,sasa imethibitishwa kuwa atakipiga Jangwani lkn bado Wapenzi na Wanachama wa Simba despite longolongo zote za Viongozi wao wanawaona TFF na kuongeza muda wa usajili kuwa ndo Mchawi wa kumtorosha Twite wao.
Haya kwenye Simba day pale Mh Rage akawahakikishia Wana Simba(kama ambavyo amewahi kuwahakikishia hapo nyuma kumsajili Asamoah,Nizar na Yondani kutochezea Yanga Kagame) kuwanYondani huyohuyo hatacheza Ligi kuu na kama Yanga watataka imtumie mchezaji huyu basi watatakiwa watoe Mill 60 fedha za kitanzania,Wanachama wa Simba wakashangillllliaa,wakiamini kuwa hivi karibuni team yao itavuna mahela mengine kwa kuuza mchezaji,eh.....
Kuna nini huko Simba?, unajua hali hii ya kuchezewa akili mchana kweupee inanifanya nianze kuamini kuwa inawezekana katika Dunia hii ushirikina upo kweli,naanza kuhisi siyo bure......

Wapenzi na wanachama wa Simba tafakarini na kuchukua hatua,hao viongozi wenu wameshawaona "MABOYA"
 
Jamani hebu waacheni hawa jamaa naona wanapita tu kuchungulia bila kuacha comments zozote kwa aibu .,mhurumien maha rage
 
Rambi rambi ya patrick mutesa mafisango mtatuma lini?
 
Leo nimeamka na wazo jipya,nafikiri iko haja ya mimi kwenda kugombea 1 ya nafasi za juu kabisa za uongozi wa team ya Simba,labda (nasema tena,labda) kosa langu ni kujipambanua mapema hapa JF kuwa moyo wangu umelalia wapi lkn No....nitakwenda, wengi (naomba nieleweke vizuri hapa,wengi) wa Wanachama na Mashabiki wa Simba ni Mazuzu hapana shaka watanichagua tu.
Waliambiwa Mwenyekiti amekamilisha kazi ya Twite na angetambulishwa kwenye Mkutano mkuu,siku ya mkutano inafika hola...wakaambiwa tena angekipiga siku ya Simba day,siku ya Simba Day ikafika hola,sasa imethibitishwa kuwa atakipiga Jangwani lkn bado Wapenzi na Wanachama wa Simba despite longolongo zote za Viongozi wao wanawaona TFF na kuongeza muda wa usajili kuwa ndo Mchawi wa kumtorosha Twite wao.
Haya kwenye Simba day pale Mh MahaRage akawahakikishia Wana Simba(kama ambavyo amewahi kuwahakikishia hapo nyuma kumsajili Asamoah,Nizar na Yondani kutochezea Yanga Kagame) kuwanYondani huyohuyo hatacheza Ligi kuu na kama Yanga watataka imtumie mchezaji huyu basi watatakiwa watoe Mill 60 fedha za kitanzania,Wanachama wa Simba wakashangillllliaa,wakiamini kuwa hivi karibuni team yao itavuna mahela mengine kwa kuuza mchezaji,eh.....
Kuna nini huko Simba?, unajua hali hii ya kuchezewa akili mchana kweupee inanifanya nianze kuamini kuwa inawezekana katika Dunia hii ushirikina upo kweli,naanza kuhisi siyo bure......

Wapenzi na wanachama wa Simba tafakarini na kuchukua hatua,hao viongozi wenu wameshawaona "MABOYA"

simba nguvu moja tutakutana kwenye ligi hapo wajumbe wengine watachia nafasi zao ndani ya club yenu
 
Back
Top Bottom