Simba inapodanganya Watanzania

Simba inapodanganya Watanzania

akili akili

JF-Expert Member
Joined
May 5, 2014
Posts
1,767
Reaction score
1,155
Wana jamii forum, nikiwa kama mwanamichezo nashangazwa kuona report kwamba Simba imecheza na Orando Pirates ya Africa Kusini. Bila kupepesa macho, Orando Pirates imecheza na Black Ace siku ya 11/10/2014 na kushinda bao 1 kwa 0. Hivi wahusika hawajui kama dunia ni kama kijiji?, nn malengo ya kuwanganga wapenzi wao juu ya hili?

attachment.php

 
Rage akukosea alipowaita mbu3
 

Attachments

  • 1413060295031.jpg
    1413060295031.jpg
    80.5 KB · Views: 6,044
na ninyi tarhe 18 mmtuletee Yanga nyengine
 
Na hivi vyombo vya habar ambavyo huripoti hizi taarifa huwa hawafanyi uchunguz kwanza kabla ya kutoa habari!!! na nyinyi viongoz wa simba kwann mnafanya hivi, kuna kipindi watu wa simba watamkumbuka rage.
 
Mimi naamini kuna udhaifu ndani ya uongozi wa vilabu vyetu na kwa waandishi wetu wa habari.

Lakini siamini kwamba Aveva & Co. ni washenzi kiasi cha kuthubutu kutudanganya kama inavyofikiriwa.

Ninahisi:

1. Ni kweli Simba ilicheza na Orlando Pirates ya Afrika ya Kusini na kutoka 0-0, lakini si hii Orlando ya Premeir. Hata hapa Tanzania kuna Simba (na Small Simba) nyingi tu huko mitaani, au

2. Inawezekana wamecheza na Orlando Pirates yenyewe na kutoka nayo 0-0, lakini ni Orlando ya wachezaji wa akiba na wa akademia, huku wa kikosi cha kwanza wakiwa mashindanoni. Ndio maana Malinzi anasisitiza kuanzisha akademia kwa 5%, au

3. Inawezekana walicheza na timu waliyoamini kwamba ni Orlando Pirates, kwenye uwanja walioamini kuwa ni wa Orlando Pirates, lakini kumbe walicheza na kundi la wajanja fulani hivi walioona wasipoteze fursa ya kula mshiko wa nje nje. Nani kasema wenye bongo za kutapelia wako Bongo tu?, au

4. Simba hawajacheza wala hawajamwambia yeyote kwamba wamecheza na Orlando Pirates, ila wanaudaku (wanahabri?) wetu wakajua tu kimahesabu kwamba kwa sababu Simba huwa inatoa sare kila mechi, na kwa sababu awali ilisemwa kwamba wangecheza na Orlando Pirates, na kwa sababu sare pekee ambayo Simba haijatoa kwenye mfululizo huu ni hiyo ya 0-0, basi mkokotoo (calculation) rahisi ni kuwa hiyo ndiyo sare iliyopatikana. Hivyo ndivyo udaku unavyokokotolewa, au

5. Hatuwezi kujua, labda 'Kamati ya Ufundi' iliagiza kwamba ili ishinde mechi ya 18/10, Simba lazima itoe sare nyengine kabla ya hapo, hata kama ni ya kubuni, au

6. Jinsi Simba inavyoendeshwa Kisayansi, wameona wawazuge watani wao kwamba wametoka sare nyengine, watani hao wazidi kubweteka ili Mnyama awashtukize hiyo siku ya siku, au..........
 
Mkuu nimekukubali , umetisha sana au...!

Mimi naamini kuna udhaifu ndani ya uongozi wa vilabu vyetu na kwa waandishi wetu wa habari.

Lakini siamini kwamba Aveva & Co. ni washenzi kiasi cha kuthubutu kutudanganya kama inavyofikiriwa.

Ninahisi:

1. Ni kweli Simba ilicheza na Orlando Pirates ya Afrika ya Kusini na kutoka 0-0, lakini si hii Orlando ya Premeir. Hata hapa Tanzania kuna Simba (na Small Simba) nyingi tu huko mitaani, au

2. Inawezekana wamecheza na Orlando Pirates yenyewe na kutoka nayo 0-0, lakini ni Orlando ya wachezaji wa akiba na wa akademia, huku wa kikosi cha kwanza wakiwa mashindanoni. Ndio maana Malinzi anasisitiza kuanzisha akademia kwa 5%, au

3. Inawezekana walicheza na timu waliyoamini kwamba ni Orlando Pirates, kwenye uwanja walioamini kuwa ni wa Orlando Pirates, lakini kumbe walicheza na kundi la wajanja fulani hivi walioona wasipoteze fursa ya kula mshiko wa nje nje. Nani kasema wenye bongo za kutapelia wako Bongo tu?, au

4. Simba hawajacheza wala hawajamwambia yeyote kwamba wamecheza na Orlando Pirates, ila wanaudaku (wanahabri?) wetu wakajua tu kimahesabu kwamba kwa sababu Simba huwa inatoa sare kila mechi, na kwa sababu awali ilisemwa kwamba wangecheza na Orlando Pirates, na kwa sababu sare pekee ambayo Simba haijatoa kwenye mfululizo huu ni hiyo ya 0-0, basi mkokotoo (calculation) rahisi ni kuwa hiyo ndiyo sare iliyopatikana. Hivyo ndivyo udaku unavyokokotolewa, au

5. Hatuwezi kujua, labda 'Kamati ya Ufundi' iliagiza kwamba ili ishinde mechi ya 18/10, Simba lazima itoe sare nyengine kabla ya hapo, hata kama ni ya kubuni, au

6. Jinsi Simba inavyoendeshwa Kisayansi, wameona wawazuge watani wao kwamba wametoka sare nyengine, watani hao wazidi kubweteka ili Mnyama awashtukize hiyo siku ya siku, au..........
 
Hivi ligi yao inaendelea na timu ya taifa lao jana imecheza??
 
hapa bujibuji tunatengana?

hivi kila timu ina wachezaji wangapi? Wanaoingia kwenye mechi huwa 18. Je wanaosalia hawawezi kucheza. Je yanga nao walipokuwa antalya si walifanya vivi hivi
 
Kweli lugha ya kiingereza ni ngumu sana.Aliyeleta habari hii atuambie kwani ni
 
Aliyeleta habari hii kutaka tuamini kwamba mechi hiyo anayodai Orlando imecheza jana kwanini mwandishi asiandike played today aandike last Saturday.Pili aliyeposti habari hii aliposti saa nane na dakika 27 mchana.Je mechi ilianza saa 5 asubuhi ?Tuache kurukia kutoa conclusions bila lugs nya u tagit.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom