Simba imejipiga shoti kwa Jonathan Sowah na itawagharimu

Simba imejipiga shoti kwa Jonathan Sowah na itawagharimu

DELETED ACCOUNT

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
9,805
Reaction score
15,470
Ngoja leo niongelee kidogo timu yangu ya zamani ya Simba SC.

Hapo nyuma niliwahi kusema Jonathan Sowah siyo chaguo sahihi kwa Simba na nitakupa sababu kubwa tatu.

1. Sowah ni mzee na hajawahi kuonyesha uwezo wowote kimataifa. Huyu jamaa hata ukiangalia tu maumbile yake utagundua anachezea miaka 32-35. Kwa levo za Simba na kile wanacholenga kufanya, huyu alitakiwa kuwa chaguo la pili au tatu na siyo la kwanza.

2. Wachezaji wa Ghana wana masikhara mengi na viburi. Ghana ya miaka hii siyo ile ya kina Abedi Pele au Anthony Yeboah. Ndiyo maana wachezaji wao hata wa kimataifa wakirudi kuchezea timu ya taifa unasikia migomo na drama kibao. Ni watu wanaojiamini sana na wenye viburi.

3. Uhusiano wake na Hersi haiwezi kufutika kwa kumwambia achane picha yake. Tusidanganyane, Hersi anajenga mahusiano ya karibu mno na wachezaji. Ndiyo maana pale Yanga, Simba haina uwezo wa kumchomoa mchezaji yoyote yule hata wamuahidi mara tatu ya mshahara anaolipwa sasa. Sowah amesema Hersi alimfanyia jambo kubwa ila hajawahi kulitaja hilo jambo. Sowah kuja Simba ni kwa sababu Hersi amempa baraka za kufanya hivyo, tusisahau hilo.

ZIADA: Kitendo cha kuchana picha ya Hersi kumempa pressure itakayomfanya asiende kufanikiwa. Juzi nimetoka kusema Simba haijui kujifunza, inapenda kurudia makosa yake. Ateba aliongea maneno ya shombo dhidi ya Yanga kabla ya derby na anaondoka Tanzania bila kuifunga Yanga hata goli la mkono tena akiwa amepotea kabisa na haeleweki.

Kitendo cha viongozi wa Simba kumfanya achane picha ya Hersi ni utoto na kujikosha tu kwa mashabiki kama ambavyo walitengeneza drama za Feisal. Kiufupi, viongozi wa Simba wanacheza tu na hisia za mashabiki wao.

Simba mkumbuke ubingwa wa ligi ya Tanzania unaamuliwa kwa mechi zisizozidi mbili. Simba ilikosa ubingwa si kwa kufungwa na Yanga mara mbili bali kwa kutoa sare za kizembe dhidi ya Coastal Union na Fountain Gate.

Sowah atachoma mechi kama mbili zitakazowahakikishia ubingwa Yanga. Jiandaeni kisaikolojia.
 
Hizi mambo za kusajili mchezaji kwa kukuona siku mmecheza naye ndo tunakuja kupata kina Mutale.

Sehemu nzuri ya kupata wachezaji ni CHAN ila naona hata huwa hatuzingatii huko.
^^^^^^^^^^^^^

Niliwahi kusema CHAN ni sehemu nzuri sana ya kupata wachezaji cheap lakini wenye potential siyo unaenda kuwaokoteza hawa vichomi kina Sowah. Tatizo Simba siku hizi inasajili wachezaji ili ionekane imejaribu.
 
Itakuwa furaha kuiona Simba nusu fainali club bingwa au fainali hata kwa gharama ya Yanga kuchukua ligi msimu huu na msimu ujao.
 
Ngoja leo niongelee kidogo timu yangu ya zamani ya Simba SC.

Hapo nyuma niliwahi kusema Jonathan Sowah siyo chaguo sahihi kwa Simba na nitakupa sababu kubwa tatu.

1. Sowah ni mzee na hajawahi kuonyesha uwezo wowote kimataifa. Huyu jamaa hata ukiangalia tu maumbile yake utagundua anachezea miaka 32-35. Kwa levo za Simba na kile wanacholenga kufanya, huyu alitakiwa kuwa chaguo la pili au tatu na siyo la kwanza.

2. Wachezaji wa Ghana wana masikhara mengi na viburi. Ghana ya miaka hii siyo ile ya kina Abedi Pele au Antony Yeboah. Ndiyo maana wachezaji wao hata wa kimataifa wakirudi kuchezea timu ya taifa unasikia migomo na drama kibao. Ni watu wanaojiamini sana na wenye viburi.

3. Uhusiano wake na Hersi haiwezi kufutika kwa kumwambia achane picha yake. Tusidanganyane, Hersi anajenga mahusiano ya karibu mno na wachezaji. Ndiyo maana pale Yanga, Simba haina uwezo wa kumchomoa mchezaji yoyote yule hata wamuahidi mara tatu ya mshahara anaolipwa sasa. Sowah amesema Hersi alimfanyia jambo kubwa ila hajawahi kulitaja hilo jambo. Sowah kuja Simba ni kwa sababu Hersi amempa baraka za kufanya hivyo, tusisahau hilo.

ZIADA: Kitendo cha kuchana picha ya Hersi kumempa pressure itakayomfanya asiende kufanikiwa. Juzi nimetoka kusema Simba haijui kujifunza, inapenda kurudia makosa yake. Ateba aliongea maneno ya shombo dhidi ya Yanga kabla ya derby na anaondoka Tanzania bila kuifunga Yanga hata goli la mkono tena akiwa amepotea kabisa na haeleweki.

Kitendo cha viongozi wa Simba kumfanya achane picha ya Hersi ni utoto na kujikosha tu kwa mashabiki kama ambavyo walitengeneza drama za Feisal. Kiufupi, viongozi wa Simba wanacheza tu na hisia za mashabiki wao.

Simba mkumbuke ubingwa wa ligi ya Tanzania unaamuliwa kwa mechi zisizozidi mbili. Simba ilikosa ubingwa si kwa kufungwa na Yanga mara mbili bali kwa kutoa sare dhidi ya Coastal Union na Fountain Gate.

Sowah atachoma mechi kama mbili zitakazowahakikishia ubingwa Yanga. Jiandaeni kisaikolojia.

WANAWAKE MKIPENDA MMEPENDA. KAUNGANISHE PICHA ALIYOCHANA BASI
 
Eeeeh hakuna jema aiseee 😃🙌
Kwa hiyo watu wote walie sana!?
Kwa hiyo tukusaidieje?
Kumbe uchungu wako na ghadhabu ni kuhusu picha ya Hersi kuchanwa 🤣🤣

Ukikua utaacha kuandika nyuzi za kitoto
WANAWAKE MKIPENDA MMEPENDA. KAUNGANISHE PICHA ALIYOCHANA BASI
Sawa mtume na nabii 😃
😂😂🤣 Ameumia picha ya mumewe kuchanwa.
Yaani kuchana picha ya mtu mwenye kichwa kama amevaa helmet ndo kusababishe nyuzi nyingi hivi?
Siku hizi mashabiki wa Simba mmekuwa kama wa Yanga tu, mnadanganyika na kuchezewa akili zenu. Vingozi wenu hawawaheshimu.
 
Itakuwa furaha kuiona Simba nusu fainali club bingwa au fainali hata kwa gharama ya Yanga kuchukua ligi msimu huu na msimu ujao.
Sikupingi ila ila.....niseme tu kuna shida kubwa pale Simba kuliko mnavyodhania
 
  • Kicheko
Reactions: Tsh
"Sowah amesema Hersi alimfanyia jambo kubwa ila hajawahi kulitaja hilo jambo. Sowah kuja Simba ni kwa sababu Hersi amempa baraka za kufanya hivyo, tusisahau hilo."

Mkuu unaelewa maana ya professional footballer?
 
Back
Top Bottom