Silinde alipua juu ya ndovu

Hana akili,mbunge unategemea kutafuta cha kuongea bungeni kwenye online forum?

Unatuaminisha kwamba yaliyomo kwenye forum ni hadithi za sungura na fisi? unashangaza wewe kumshangaa silinde, kwani forums si chombo cha habari kama ilivyo TBC, kwani kuna tofauti ya habari iliyotolewa kwenye luninga na iliyotolewa on line? Kwa nini wewe umeamini hapa ni mahali sahihi pa kumtetea huyo membe kama umeona its just forum?
 
wakati wa epa ishue ilianzia kwenye mitandao, lakini ilibaki kuwa ukweli, viva silinde
 

Huyu ndo anataka kuwa raisi! Mimi natafuta uraia wa somalia.

Hii nchi hakuna kiongozi. Bunge limekuwa kama lango la jiji, taarab. Du!
 

Ukishinda sana kwenye mitandao ya kijamii ndo madhara yaje haya
 

habari zipi ni sahihi Kwa mbunge kufanyia kazi au za magazeti ya Uhuru na mzalendo.
 
Hana akili,mbunge unategemea kutafuta cha kuongea bungeni kwenye online forum?
Wabunge wengi hasa wa CHADEMA hushinda online,kwenye magazeti na TV hawashindi na wapiga kura kupata hoja za kupeleka bungeni .Mbozi kwenye jimbo la Silinde kulivyojaa matatizo kibao, ndio akae anapoteza muda kuulizia habari za tembo wa Arusha kwani Arusha hakuna mbunge wa kuuliza hilo? Nawapenda wabunge wa Kenya ukiuliza swali la kwenye eneo lisilokuhusu yule mwenye jimbo lake anainuka saa hiyo hiyo na kuja kukutwaga mingumi na miteke kuwa unamwingilia kwenye jimbo lake.

Lakini hii ni tabia ya wabunge wa CHADEMA huwezi wasikia wakiulizia habari za majimbo yao mara nyingi. Kutwa Utawasikia wanaongelea IPTL,EPA,DOWANS,RICHMOND au hoja hewa hewa za hivyo wanavyoita vibomu vya nchi .Mimi huwa sielewi wamefata nini bungeni na ni wabunge wanaomwakilisha mwananchi wa wapi?
 
Hii nchi ina raia wa ajabu yan kuna watu kabisaa wanatetea uozo wa serikali eti kwa sababu tu ya maslahi ya kisiasa
 

kumbe nawe ni walewale misukule ya Lumumba.
 

tunachoangalia ni whether ahadi wanatekeleza au lah

kuhusu za jimboni nadhani huwa wanaiziainisha kwenye mapendekezo yao ya bajeti

wabunge wa upinzani wanafanya kazi ngumu sana

wanatimiza wajibu wao wa kuisimamia serikali

tofaut na wabunge wa chama tawala ambao kutwa wanatetea hoja serikali.. Huu ni usaliti
 

Mh! Wanaowawakilisha watanzania ni wale wezi,wabadhirifu wa mali za umma,mafisadi,wala rushwa,wahujumu uchumu ambao ni wale wale wa CHAMA CHA MAFISADI.Pole sana kwa kutumia za kuambiwa tu.Nakuone huruma mpaka basi.
 
Huyu ndo anataka kuwa raisi! Mimi natafuta uraia wa somalia.

Hii nchi hakuna kiongozi. Bunge limekuwa kama lango la jiji, taarab. Du!

Halafu hakuna kitu kinaudhi pale anaposimama anayejiita Mheshimiwa eti hili "BUNGE LAKO TUKUFU"Wakati mle ndani wamejaa wahalifu,wezi,wauji,amajangili yaani sipati kueleza.
 
.

Taarifa zote zote za kashfa na mengine, Zinatoka kwenye vyombo vya habari ikiwepo mitandao, We ulitaka Xi Ji Ping aongee ndiyo iwe habari? Walioathiriwa na pepo la CCM siku zao zimefika, JK huyo kaenda meza Panadol Marekani
 

Dada Tiba nimepata wazo kuwa hawa siyo BUKU SABA,hawa ni either WATOTO wa hawa MAFISADI,MARAFIKI ,JAMAA au WAHUSIKA wakuu wakupenyeza dili za kuliua TAIFA.

Leo nimepata simuliza ya TANAPA imebidi nipate mshtuko wa moyo.Ni matatizo kweli kweli.Waache waendelee kujigamba ila wajue kuwa chenye mwanzo kina mwisho.
 
Kamanda Silinde amehoji juu ya utoroshwaji wa pembe za ndovu na Mchina wa JK,ameomba muongozo kwa spika.Membe ameanza kwa kumfagilia mchina na kusema ni uzushi.Amesema kuwa taarifa ni ya kuunga-unga kwa ajili ya kuichafua nchi

Huwa inaanzia hapo halafu baadaye inatoka.Ni rais huyu huyu wa China aliyesema anajua watu wake ni corrupt na ni wafanya biashara wazuri wa meno ya tembo sababu kule kwao ni deal la maana sana.
 
Naomba kujuzwa kabla ya jana ni lini Membe alifanya uchunguzi kama Mchina hakuondoka na ndovu.hili nadhani Mh.Silinde angelihoji pia.Maana waliotoa kashfa wamefanya uchunguzi.
 

Wewe tunakujua Ni Punda wa Riziwani tunakujua, kila ikitokea ishu ya Sembe na pembe vifunza vinakuwasha
 
Hili dili kweli linawahusu viongozi Wa ccm Kwa nin wakanushe wangesema wanalifanyia kazi Kwa sababu ni uchunguzi umefanywa kimataifa sio kujibu majibu ya kanga wanatuonea wivu wivu gani Wa k uionea Tanzania hivi wanaokusaidia watakuonea wivu
 
Hivi wewe hauna cha kuandika? yaani mbunge anahoji kashifa ya meno ya tembo wewe unaleta storry za
kushost achana na hao wanaokutuma tuongelee maslahi ya nchi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…