Nakapanya
JF-Expert Member
- May 22, 2012
- 2,096
- 708
Siku moja kulikuwa na bendi moja ya taarabu wanatumbuiza eneo fulani,mimi si mpenzi wa taarabu ila kwa kuwa siku nyingi sijaenda mziki kutokana na mazingira nikaamua kwenda kuburudika.Katika usiku ule nilianza kucheza peke yangu kwa mbali nikamuona DADA mmoja ambaye huwa namuona mtaani kwetu lakini hatuna mazoea ya karibu hivyo nikampotezea.Wakati nikiendelea kuburudika ghafla yule dada akaja kwangu na kuanza kunichombeza pale mara ooh....huwa nakuona mtaani so naomba tucheze pamoja,bila hiyana nikaamua kucheza naye.Mwanzoni tulianza kucheza vizuri ila kadiri muda ulivyokuwa unaenda ndivyo vurugu zilipoongezeka,alianza kunishika hata sehemu mabazo hazihusiki tena mbele ya hadhara,nikawa muwazi na nikamwambia sipendi anavyofany,kweli akacha ila akaanza kuning'ang'ania nimnunulie bia;nikamnunulia kama bia tatu bila kinyongo.Wakati muziki ukielekea mwishoni nilishtushwa na kauli kutoka kwa yule dada,aliniambia hivi:"KAMA UNATAKA MWANAMKE UWE UNANIAMBIA NIKUTONGOZEE",Kauli ile ilinifanya nimuanglie mara mbilimbili bila kummaliza,hapohapo nikaamua kumkwepa kabisa.Siku iliyofuata nikawasimulia washkaji zangu wa kitaa na wote hawakuonyesha kushangaa kwani waliniambia hiyo ndio TABIA yake yule dada na shughuli hizo huzifanya yeye pamoja na wenzake ambao hufanya kazi katika SALUNI MOJA YA KIKE,kweli tangu siku ile sikupenda kabisa kukutana na yule dada kutokana na ile TABIA aliyonionyesha usiku ule.loooh UKUWADI kumbe nayo kazi.....?