Sikumteua Lowassa kirafiki - Kikwete

Sikumteua Lowassa kirafiki - Kikwete

nngu007

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2010
Posts
15,860
Reaction score
5,803
RAIS Jakaya Kikwete amesema hakumteua Edward Lowassa kuwa Waziri Mkuu kwa sababu ya urafiki wao bali kwa sababu ya ufanisi wake.

Kikwete ameyasema hayo kupitia kitabu chake cha
JK: A Political Biography, kitabu kinachoeleza kuhusu maisha yake ambacho sasa kinapatikana hapa nchini.

Kikwete ameelezwa kutoa maelezo haya mwaka mmoja baada ya tukio la kujiuzulu kwa Lowassa kufuatia kashfa ya Richmond ambayo ililazimu baraza lote la mawaziri kuvunjwa.

"Sikiliza. Ni kweli kwamba Lowassa ni rafiki yangu na nimemfahamu kwa muda mrefu. Lakini pia ninawafahamu watu wengi zaidi kwa muda mrefu, wanasiasa na wasiokuwa wanasiasa na sikuwachagua kuwa Waziri Mkuu.

"Nilikuwa natafuta mtu ambaye atafanya kazi kwa ufanisi na kutekeleza sera zangu. Lowassa alijitokeza vizuri kama mtu anayeweza kutokana na uzoefu wake," kitabu hicho kinamnukuu Kikwete.

Hii ni mara ya kwanza ambapo Kikwete anaeleza wazi wazi mahusiano yake pamoja na tathmini ya utendaji wa Lowassa, tangu kuibuka kwa kashfa ya Richmond.

Sentensi moja katika maelezo ya Kikwete inaonyesha mtazamo wake kwa waziri mkuu huyo aliyejiuzulu; "Lowassa alikuwa mmoja wa mawaziri wakuu wenye ufanisi mkubwa kabisa nchini."

Tafsiri ya maelezo haya ya Kikwete inaonyesha kwamba mwaka mmoja baada ya kashfa ya Richmond, rais bado alikuwa na imani na Lowassa.

Wakati Kikwete alipochaguliwa kuwa rais mwaka 2005, majina mengi yalitajwa kuchukua nafasi ya uwaziri mkuu ingawa la Lowassa lilitajwa zaidi kutokana na ukaribu waliokuwa nao viongozi hao.

Lowassa pia hakuchukua fomu kuwania urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2005, jambo lililotajwa kama kuonyesha azma yake ya kumuunga mkono mgombea huyo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Baadhi ya wachambuzi wa masuala ya kisiasa, walidai kwamba uamuzi wa Kikwete kumteua Lowassa ungekuwa na athari kubwa kwake kwa vile ukaribu wake ungeweza kuingia kwenye kazi.

Mara baada ya uteuzi huo, ndipo ilipoibuka dhana ya ‘serikali ya kishkaji' kutokana na baadhi ya watu waliotajwa kuwa maswahiba wa Kikwete, akiwamo Lowassa, kupata nafasi katika baraza lake la kwanza la mawaziri.

Kikwete na Lowassa walikutana kwa mara ya kwanza mwaka 1974 wakiwa wanafunzi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, wote wakiwa wanachama wa Umoja wa Vijana wa chama cha TANU ingawa Jakaya alikuwa katika mwaka wake wa mwisho wa masomo huku Edward akiwa mwaka wa kwanza.

Wote kwa pamoja walifanya maamuzi ya kujiunga na ajira katika chama cha TANU (sasa CCM) wakati huo mara baada ya kumaliza masomo yao, na wote walichukua fomu kuwania urais kupitia CCM mwaka 1995 wakiwa na umri chini ya miaka 50.


Source
: Raia Mwema
 
Nyota ya Lowassa yazidi kung'ara, mkuu wa kaya azidi kuuhusudu hadharani utendaji wake.

Safari njema ya urais mheshimiwa EL.
 
Hii pia ni sehemu ya kampeni kwaajili ya 2015.
Naona kuanzia sasa kila gazeti limelipwa limtaje japo kila siku, hata kama kaenda kunyoa.

Hii story ya urafiki wa hawa watu wawili iko way too old, na monotonous.
 
Nyota ya Lowassa yazidi kung'ara, mkuu wa kaya azidi kuuhusudu hadharani utendaji wake.

Safari njema ya urais mheshimiwa EL.
Mkuu Rock City Angelikuwa Mh Lowasa Kiongozi Mzuri kwanini alijiuzulu? Kwa kashfa za Serikali? angalisafisha machafu waliyokuwa wanafanya hao Mafisadi. Mh Lowasa na Marehemu Aliyekuwa Waziri Mkuu ndugu Edward Moringe Sokoine nani zaidi?
 
Kwanini hukusema sababu ya kumteua kwako 2005 unakuja kuisema 2013!??????.....Haituhuuuuuuu!!!!....Fisadi huyu hafai kabisa kugombea ULAIS 2015.
 
Lowasa hasafishiki hata kwa jiki...lowasa ni mchafu hafai hata kidogo..huyu kikwete naye ajinyamazie tuu...amalize muda wake asepe zake...hatuna mpango naye wala nini hafai hata kidogo inabidi tumpuuze tuu huyu baba ajiondokee zake.
 
Kwenye demokrasia za kibepari ili upate uongozi wa juu kabisa wa nchi lazima uwe na kimoja kati ya vitu vitatu ambavyo ni PRESTIGE, POWER AND MONEY.

Kitu kinachomfanya Edward Lowassa kuwa UNIQUE kwenye siasa za Tanzania ni kuwa na vyote vitatu badala ya kimoja au viwili.

Kuna watu kwa fikra za itikadi zao za kisiasa au kutopenda ukweli wata brush aside lakini ukweli unabakia pale pale. He can sustain Tanzania subterfuge political fight and the guy is doing pretty well.

Kwa mtu aliye makini na anayeziangalia nyendo za mh. Lowassa lazima atakuwa makini pia kujua Lowassa next step ikichukuliwa katiba ijayo kuna uwezekano mkubwa ikaruhusu wagombea binafsi ambao mara nyingi huwa ni wavurugaji kwenye taasisi za kisiasa zenye dictatorial candidate selection na pia wagawa kura kwenye chaguzi mbali mbali.

Watch out Lowassa political space.
 
Political Biography? Bado mapema - asubiri kutoka madarakani atoe hiyo habari maana bado ana kazi kubwa hadi 2015
 
bila kumung'unya maneno lowassa is one and the only fit and suitable for presidency 2015.

Endapo CCM itakataa kumsimamisha then the downfall of CCM is much more obvious and accelerated than now.

Mark my words
 
Tuacheni chuki na ukasuku. Hivi ukiambiwaa ueleze ufisadi wa Lowasa, utauelezea upi? Na kwa ushahidi upi? avoid dogmatic..
 
Im not being political judgemental but being frank Im ahundred % sure tht we need a president ambaye ni mzalendo wa kweli.... n for sure this maasai is purely mzalendo... He will tek us forward, his spirit is the best.
Big up mh. L!!
 
Nyota ya Lowassa yazidi kung'ara, mkuu wa kaya azidi kuuhusudu hadharani utendaji wake.

Safari njema ya urais mheshimiwa EL.
[MENTION][JFMP3][/JFMP3][/MENTION]

Rock city yani mimi tangu kipindi hicho EL ajiuzulu na kukawa na maneno yakupishana na mkulu lakini sikuamini kabisa kwamba eti siokitu kimoja tena, hawa jamaa ni wasanii nawasikitikia wale ambo ndani ya chama chao waliamini hivyo na wakaanza kumponda el wanawakati mugumu sana, yani kitu ambacho pia kimenishangaza ni El kuvalishwa kilemba na maustadhi tena wamejipanga pembeni na kutandika zulia mzee apite aiseeeee!
 
Nyota ya Lowassa yazidi kung'ara, mkuu wa kaya azidi kuuhusudu hadharani utendaji wake.

Safari njema ya urais mheshimiwa EL.

Acha kujidanganya mkuu Lowassa hakubaliki hata nyumbani kwake Arusha.Monduli kwenyewe chupu chupu ahadhirike kama sio uhuni wa Green Guard dhidi ya Mawakala wa Chadema kata ya Makuyu ingekuwa Upinzani.Lowassa ni mwepesi mno.Pale mtu makini CCM ni Dr Salim Ahmed Salim peke yake.Labda na Mwakyembe kidogo waliobakia wote ni wehu.
 
Kwenye demokrasia za kibepari ili upate uongozi wa juu kabisa wa nchi lazima uwe na kimoja kati ya vitu vitatu ambavyo ni PRESTIGE, POWER AND MONEY.

Kitu kinachomfanya Edward Lowassa kuwa UNIQUE kwenye siasa za Tanzania ni kuwa na vyote vitatu badala ya kimoja au viwili.

Kuna watu kwa fikra za itikadi zao za kisiasa au kutopenda ukweli wata brush aside lakini ukweli unabakia pale pale. He can sustain Tanzania subterfuge political fight and the guy is doing pretty well.

Kwa mtu aliye makini na anayeziangalia nyendo za mh. Lowassa lazima atakuwa makini pia kujua Lowassa next step ikichukuliwa katiba ijayo kuna uwezekano mkubwa ikaruhusu wagombea binafsi ambao mara nyingi huwa ni wavurugaji kwenye taasisi za kisiasa zenye dictatorial candidate selection na pia wagawa kura kwenye chaguzi mbali mbali.

Watch out Lowassa political space.

Hamna kitu pale Lowassa mweupe tu hivi uchaguzi wa Arusha bado haujawapa somo tu kuhusu Lowassa ama kweli mna roho za paka.
 
bila kumung'unya maneno lowassa is one and the only fit and suitable for presidency 2015.

Endapo CCM itakataa kumsimamisha then the downfall of CCM is much more obvious and accelerated than now.

Mark my words

CCM ikimsimamisha ndio itakufa rasmi Lowassa ni mchafu mno lakini la Ukabila ambalo alilificha kwa muda mrefu kabla ya kulifichua hivi karibuni kupitia mshirika wake wa karibu wa kisiasa Ole Medeye ndio limekuwa kaburi lake rasmi la kisiasa.Lowassa asahau Urais wa Tanzania,Watanzania hawatamchagua Rais Mkabila na Fisadi kamwe
 
Back
Top Bottom