Sikukuu ya Leo imepooza sana kulikoni?

Sikukuu ya Leo imepooza sana kulikoni?

kimsboy

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2016
Posts
11,185
Reaction score
24,565
Ukiambiwa leo kuna sikukuu utakataa!!

Kumepooza kama futari ya magimbi ya juzi

Yaani hamna vibe wala nini

Hamna cha kuchoma nyama wala nini

Siku imekaakaa tu haieleweki
 
Ukiambiwa leo kuna sikukuu utakataa!!

Kumepooza kama futari ya magimbi ya juzi

Yaani hamna vibe wala nini

Hamna cha kuchoma nyama wala nini

Siku imekaakaa tu haieleweki
Tunawaogopa HAMAS mkuu ndio maana sikukuu imepoa.
 
IMG-20240617-WA0466.jpg
 
Watanzania wana hali mbaya ya uchumi kuliko wakati wowote ule, afadhali hata wakati wa vita vya Idd Amin
Wewe mpumbavu ulikuwa una umri gani wakati huo?
Maduka yalikuwa hayana bidhaa.Watu walikuwa wanatumia pipi nyeupe na sukari guru kupikia chai.Vibali vya sukari vilikuwa vinatolewa kwa RDD wakati huo.Ukipatikana na sabuni ya Imperial au dawa ya kupigia mswaki ya Colgate kutoka Kenya unafunguliwa kesi ya uhujumu uchumi.
Watanzania walikuwa hawana hata nguo za maana za kuvaa.Ukivaa jeans unatumbuliwa macho umeipata wapi?
Kulinganisha hali ile na sasa ni uendawazimu wa kipimo cha juu.
 
Ikifika jioni sogea maeneo ya Bar na wanapouza kitimoto na sehemu zenye dada poa utaona jinsi hao wenye sikukuu yao wanavyosheherekea.
 
Zamani ulikua unakuta baba mmoja ana watoto wanne.
Lakini skuizi unakuta baba wanne wana mtoto mmoja....🤣labda ndio mabadiliko ya tabia ya nchi...teh😜
 
Wewe mpumbavu ulikuwa una umri gani wakati huo?
Maduka yalikuwa hayana bidhaa.Watu walikuwa wanatumia pipi nyeupe na sukari guru kupikia chai.Vibali vya sukari vilikuwa vinatolewa kwa RDD wakati huo.Ukipatikana na sabuni ya Imperial au dawa ya kupigia mswaki ya Colgate kutoka Kenya unafunguliwa kesi ya uhujumu uchumi.
Watanzania walikuwa hawana hata nguo za maana za kuvaa.Ukivaa jeans unatumbuliwa macho umeipata wapi?
Kulinganisha hali ile na sasa ni uendawazimu wa kipimo cha juu.
angalia hii

Screenshot_2024-06-17-15-29-10-1.png
 
Imeangukia siku mbaya kwanza katikati ya mwezi ambapo salio la mshahara wa mwezi uliopita sio rafiki, pili mshahara wa mwezi wa 6 ndio wa kulipa ada za watoto, tatu jumatatu sio siku nzuri ya kula bata maana kesho watu wanaamkia makazini. By the way, ukipita maeneo ya kumwagilia moyo shamrashamra zishaanza.
 
Back
Top Bottom