Sikubaliani na jinsi Rais Samia anavyofanya Teuzi, na zitakuja kumfanya kujuta baadaye

britanicca

JF-Expert Member
May 20, 2015
15,636
30,004
Bila kupepesa macho na kupindisha maneno

Mimi ni CCM damu damu ambaye nimeanza kuwa Mwana chama wengi wenu hamjazaliwa, tokea Niko Pugu Mwaka 1979 na baadae tukasoma kupewa kadi ya CCM siyo zinazogawiwa Kama njugu!

Baada ya hapo nina machache tu ya kusema

1. Vetting ni ama haipo au inampotosha mama, hawa vijana ambao walipaswa kuwa ama Segerea au Butimba gerezani ndo wanahamishwa na kufanya mtaani watanzania wajue kuna mtu zaidi ya Mama SAMIA anayeongeza SERIKALI Huku Mama akiwa kivuli.

Mpaka watu wa kawaida tu mtaani wanaelewa kwamba kuna Tatizo mahali, sikutegemea watu Kama Maharage Chande, January na wenzake wangeendelea kuwa kwenye uteuzi wake

Pamoja na kashfa ambazo tukiziweka hapa watu watakimbiana. Wizara hii hii ya nishati Taarifa ya Migodi 336 kupelekewa umeme na Wakala wa Nishati Vijijini lakin katika migodi hiyo kuna migodi hewa imeorodheswa na kuonekana pesa inayotakiwa kupelekwa ni kwa migodi 307 tu wala si 336 kama tunavyo ambiwa na wizara hapa kuna. upigaji mkubwa sana, katika billion 300 iliyotengwa basi kuna 42,168,000,000 Yaan Bilion 42 zimeshaelekea Kibra asubuhi na mapema, si hapo tu kuna Taarifa za Ku repair Vipuli kila siku invoice ni za maeneo yale yale na hakuna kinachorekebishwa ila zinasainiwa pesa tu wanaondoka Takriban Miezi minne mfululizo kuanzia mwezi wa 2-6 mwaka huu zimeshenda pesa hewa zaidi ya 546,000,000 Kwa matengenezo hewa ambayo hayafanyiki nakuambia siku moja kuna mtu atakuja kujilipua live kwenye Tv kusema haya.

👉🏻👉🏻Wizara kiujanja ili tangaza mnada wa hadhara wa vifaa chakavu. Mnada huo ulifanyika siku ya Ijumaa tarehe 23 Novemba, 2021 kuanzia saa 4 :00 asubuhi kwenye eneo la Ofisi za Wizara ya Nishati Mtaa wa Samora Jengo la TANESCO. (karibu na Jengo la British Council)

Vifaa vilivyouzwa kiini Macho ni pamoja na Viti, Meza, Steel Cabinets, Microwave, Air Condition, fax Mchine, Telephone receivers, Printers, Scanners, Computers, na UPS. Hivi hakukuwa na kifaa chakavu ilikuwa ni dili la mkubwa kumpa mwenzake wa kariakoo tenda ili waongeze ten percent kwenye vifaa vingine watakavyonunua, na mbaya Zaidi vifaa si vyote viliuzwa na ikatumika pesa kubwa ya wizara kufanya kwamba wameagiza vifaa vingine, Takriban million 700, yaan vifaa vyenyewe havifiki hata million 80, anyway sisi kanyaboya tulikaa kimya,
lakini nje yah apo kuna gari jipya la wizara likawekwa plate number binafsi mara moja nalo eti kapata kwa mnada wakati hata kwenye orodha halikuwapo kauziwa mwenzao kiujanja Kama chakavu na tenda ikaandikwa Upya kupata gari jingine haraka Kwa bei ya juu 420M

Ishu ya kutuhumiwa tu ilipaswa imuache Makamba na Maharage nje ya teuzi Ila Mama akawakumbatia hii ni nini?

Najua makamba ni rafiki wa mwenye forum Hii Uzi huu hautamaliza muda,

Ila ishu ya msingi ni kumfahamisha Rais haya

Ukizingatia aliyemchangua Maharage ni January na amekiri mwenyewe Pamoja na barua kusema aliyemchagua ni Rais, Ila kwa clip ya Maneno ya Makamba ni Makamba mwenyewe na jiulize

Hapo zamani kuna vijana wangu wa kazi walifanya kazi na Maharage taasisi moja kubwa, yeye akiwa kijana sana kuaminiwa nafasi ya pili kwa ukubwa katika taasisi hiyo. Kiukweli kabisa ni kati ya watu wachache sanaa wamebarikiwa kuwa na akili nyingi mnoo yaan mnoo... Na ambao kimtazamo wangu anazitumia kufikiri/kufanyia tofauti.

Kama mtakumbuka nilijiuliza sana anawezaje kuacha mshahara wa Multichoice, Ukurugenzi wa kanda ya Afrika Mashariki na kati na akiwa anakaimu kanda ya Afrika Magharibi ambapo kimsingi mshahara wake ulikuwa haupungui TZS 80Mio kwa mwezi kisha aende Tanesco ambako mshahara wake na marupurupu hauzidi TZS 15Mio? Hapa kulikuwa na fumbo kubwa sana na niliutazama kama mpango wa uchafu kati ya wote waliompendekeza na yeye pia.

Anyway hili ni tatizo letu kamaTaifa, kuamini kuwa wanaoteua/ wanapendekeza wanakuwa na akili sana kuliko watanzania wengine wote na hivyo hawana Muda wa kusikiliza.

Maharage ni kama wengi wana kashfa nyingi sana sana hawafai kuwa hata balozi wa nyumba kumi ila kwa sababu ni kashfa zilizoifanya Serikali kuendelea kuwepo nyakati fulani ngumu basi bado kama Taifa/Chama tunaendelea kuoneana aibu anapewa nafasi zingine.

Britanicca Encyclopaedia
 
Bila kupepesa macho na kupindisha maneno

Mimi ni CCM damu damu ambaye nimeanza kuwa Mwana chama wengi wenu hamjazaliwa, tokea Niko Pugu Mwaka 1979 na baadae tukasoma kupewa kadi ya CCM siyo zinazogawiwa Kama njugu...
Tuliposema ccm ina wenyewe wewe ulikuwa miongoni mwa waliotupinga , sasa leo unalia nini ?

Nani alikudanganya kwamba Memo zina Vetting ?
 
Kwa hali ilivyo ni dhahiri kuwa mama amezongwa na wahuni....na bahati mbaya sana ni kwamba mama amechagua kuwaamini wahuni na wameamua kumfanyia uhuni mbele ya macho yake........

Kwa kweli mama kadri Siku zinavyokwenda anazidi kuudhalilisha urais.....
Mimi niko kinyume kidogo na ninyi.

Mimi ninamlaani Mbowe.

Chadema imeaminiwa na Watanzania wengi, ilitosha kumpa sauti kubwa kukemea au hata kuita maandamano lkn badala yake aneungana na watesi wetu.

Upinzani imara huifanya serikali kuwajibika
 
Bila kupepesa macho na kupindisha maneno

Mimi ni CCM damu damu ambaye nimeanza kuwa Mwana chama wengi wenu hamjazaliwa, tokea Niko Pugu Mwaka 1979 na baadae tukasoma kupewa kadi ya CCM siyo zinazogawiwa Kama njugu...
CEO wa posta yuko masomoni kazi yake anapewa maharage. Badala ya kutemwa mtu mwenye record yake nzuri anaondolewa kwa sababu ya mpiga dili. Januari pia alitakiwa kurudi back bencher bungeni.
 
Back
Top Bottom