Siku nilipolala na nyoka SUA

Mdakuzi mkuu

JF-Expert Member
Dec 27, 2016
212
720
Hatari sana.

Mwaka 2008 nikiwa nasoma Chuo Kikuu cha Sokoine (SUA) kampasi ya Mazimbu,na wakati huo nilikuwa nakaa chumba Na. 04 Hostel 5 kitanda cha chini.

Siku moja kipindi cha mvua nikiwa nimelala na umeme ukawa unasumbua sana (unakatika mpk siku 3 hadi 4), usingizi ukakatika usiku wa manane nikasema nijigeuze kitandani (nilikuwa nimelala chali).

Ghafla nikaona mkono wangu wa kulia umekuwa mzito, mkono ambao ndo nilitaka kuvuta blanketi nijifunike vzr. Nilipoushika kwa kutumia mkono wangu wa kushoto, nikahisi kitu laini kipo juu ya mkono wangu.

Akili ya haraka ikaja, nikalabua chini hicho kitu kilichokuwa kimenilalia mkononi.La hasha!!! Alikuwa nyoka (wa wastani),ambaye alijibanza kupata joto kipindi hicho cha baridi.

Nilipomrusha tu,nikasikia kishindo "puu..".Dah.

Nikawaamsha wenzangu.Shida ikawa kushuka kitandani na kunyata mpk switch ilipo, na wakati huohuo nyoka akawa amepaniki,anatoa sauti km ya mawimbi baharini.

Rafk yangu aliyekuwa juu akafanikiwa kuiwasha taa aisee!!!bonge ya joka jeusi.

Tukamsurubu,Mungu mkubwa.

SUA-Mazimbu na majoka meusi,akuu!
 
Mazimbu bwana manyoka na makenge yalikuwa mengi sana miaka ya 1990's hadi miaka ya 2000's,sikuhizi kiukweli wamepungua sana zama hizo kukutana na kenge jalalani au nyoka ilikuwa kawaida na maeneo yaliyokuwa yanaongoza ni clip town kule kepa,farm na tabora then kuanzia unit one hadi unit six huko kwenye mabweni napo ilikuwa balaa hadi pande za grave napo palikuwa hapatoshi hadi pale hospitali napo ni the same
 
1994 Nikiwa kama dereva wa gari la kubeba pamba tulifuata pamba vijijini sengerema huko baada ya kuondoka kilomita chache gari liliharibika tukaomba hifadhi kwa watu tukasitiriwa tu kwenye kibada kimoja tukachukua baadhi ya magunia tukalalia aisee asubuhi naambuka kubeba gunia zangu kidogo nichomokee dirishani nyoka mweusi kajikunja katikati nilipokuwa nimelala tunawaeleza wenyeji wanasema ni kawaida tu
 
Hatari sana.

Mwaka 2008 nikiwa nasoma Chuo Kikuu cha Sokoine (SUA) kampasi ya Mazimbu,na wakati huo nilikuwa nakaa chumba Na. 04 Hostel 5 kitanda cha chini.

Siku moja kipindi cha mvua nikiwa nimelala na umeme ukawa unasumbua sana (unakatika mpk siku 3 hadi 4), usingizi ukakatika usiku wa manane nikasema nijigeuze kitandani (nilikuwa nimelala chali).

Ghafla nikaona mkono wangu wa kulia umekuwa mzito, mkono ambao ndo nilitaka kuvuta blanketi nijifunike vzr. Nilipoushika kwa kutumia mkono wangu wa kushoto, nikahisi kitu laini kipo juu ya mkono wangu.

Akili ya haraka ikaja, nikalabua chini hicho kitu kilichokuwa kimenilalia mkononi.La hasha!!! Alikuwa nyoka (wa wastani),ambaye alijibanza kupata joto kipindi hicho cha baridi.

Nilipomrusha tu,nikasikia kishindo "puu..".Dah.

Nikawaamsha wenzangu.Shida ikawa kushuka kitandani na kunyata mpk switch ilipo, na wakati huohuo nyoka akawa amepaniki,anatoa sauti km ya mawimbi baharini.

Rafk yangu aliyekuwa juu akafanikiwa kuiwasha taa aisee!!!bonge ya joka jeusi.

Tukamsurubu,Mungu mkubwa.

SUA-Mazimbu na majoka meusi,akuu!
tuwekee ka picha, BTW: ulivaa pichu?
 
Wakat wale watu wa SA walikua wakiishi pale walikua wametenga mahali kwa ajili ya kufugia nyoka.
So nyoka Mazimbu Campus bado wapo particularly MTAA WA TABORWW
plain lie, mazimbu wakati wa ANC palipandikizwa sisimizi wakubwa ili kufukuza nyoka
 
Shyeeeh...!!! Ulikumbuka kutumia kinga lakini? usijekuwa ulimfanya nyoka wa SUA singo maza bure.
 
Back
Top Bottom