Siku moja na Sir Andy Chande

Siku moja na Sir Andy Chande

Amir Jamal ni mmoja wa Wazalendo wa nchi yetu.

Ametumikia nafasi mbali mbali na aliaminiwa sana na Mwalimu

Baada ya kustaafu alihamia Canada ambako umri wake uliishia hapo

Mwalimu Nyerere na Benjamin Mkapa walikutana chuo cha IFM katika kuomboleza na ndiyeo siku Mwalimu alianza kumshawishi Ben kuhusu Urais

Kuhamia Canada si kwasababu ya kuiba kama watu wanavyozusha. Si kweli hata kidogo

Pumzika kwa Amani Amir Jamal, Mzalendo na Mwananchi

JokaKuu
Nguruvi3,
Safari ya pili ya Mwalimu Nyerere UNO 1957 Amir Jamal akakutana na
Nyerere kwa bahati mbaya tu Ring Street (Sasa Jamuhuri Street).

Jamal akamwambia Nyerere kuwa alikuwa anamtafuta sana lakini
hajampata.

Pale pale Jamal akaingiza mkono mfukoni akatoa fedha kumpa Nyerere
zisaidie safari yake.
 
Sijaelewa hii story maudhui yake nini ?
Mimi nadhani stori tu. Anzia pale "kijana mdogo" Mohamed apewe kukaimu ukurugenzi. Siri ni kuwa Dau na Saidi wana "club" yao ya "islamic fundamentalism" kwa hiyo hapa tunanogeshwa na mapambano ya Club hii na Club ile. Chande nimefanya naye kazi Unga Limited wala hayuko hivi.

Siku pekee Mwenyekiti kukataza posho alikywa Professor Mmari UDSM akisema "tumeidhinisha leo, posho zianze kikao kijacho" ambayo ilieleweka. Halafu bahati mbaya (nzuri?) si Mmanyema, ni Mnyamwezi wa Nzega, la sivyo wangekuwa marafiki.
 
Amir Jamal ni mmoja wa Wazalendo wa nchi yetu.

Ametumikia nafasi mbali mbali na aliaminiwa sana na Mwalimu

Baada ya kustaafu alihamia Canada ambako umri wake uliishia hapo

Mwalimu Nyerere na Benjamin Mkapa walikutana chuo cha IFM katika kuomboleza na ndiyeo siku Mwalimu alianza kumshawishi Ben kuhusu Urais

Kuhamia Canada si kwasababu ya kuiba kama watu wanavyozusha. Si kweli hata kidogo

Pumzika kwa Amani Amir Jamal, Mzalendo na Mwananchi

JokaKuu
Muhindi mzalendo?,,haya mkuu....
 
Leo ndio siri imefichuka, ni wazi Dr Dau amewabeba sana ndugu zake katika imaani hasa huyu Mzee Mohammed Said, karani ambaye alikuwa na access ya kuingia hadi board meeting.
Matola,
Hapana sijabebwa wala sikuwa karani nilikuwa ni ''officer.''

Nimeeleza vizuri vipi ilikuwa si jambo la kawaida kwangu mimi ''junior officer,''
kuingia bodi.

Wako waliokuwa wanabebwa lakini si Mohamed Said.
Lakini hapana haja ya haya hii ni taazia tunaomboleza tusilete mambo mengine.
 
Mimi nadhani stori tu. Anzia pale "kijana mdogo" Mohamed apewe kukaimu ukurugenzi. Siri ni kuwa Dau na Saidi wana "club" yao ya "islamic fundamentalism" kwa hiyo hapa tunanogeshwa na mapambano ya Club hii na Club ile. Chande nimefanya naye kazi Unga Limited wala hayuko hivi.

Siku pekee Mwenyekiti kukataza posho alikywa Professor Mmari UDSM akisema "tumeidhinisha leo, posho zianze kikao kijacho" ambayo ilieleweka. Halafu bahati mbaya (nzuri?) si Mmanyema, ni Mnyamwezi wa Nzega, la sivyo wangekuwa marafiki.
William...
Hapana haifai kuleta hayo kwenye taazia si uungwana.
Mimi nimemweleza Chande kwa ile siku moja.

Bado unayo nafasi na wewe ukamweleza vyema kupita mie kwa kuwa
ulifanyanae kazi Unga Limited.
 
Mkuu Oscar Kambona..alivyorudi kutoka UK,alitwambia pale Jangwani kuhusu Amir Jamal,JK Nyerere na Mfaume Kawawa ..
kwamba wana fedha nyingi nje ya nchi!..Huyu muhindi ndiye alitumiwa sana..
Baada ya Kambona kuwajaza watu kwamba atataja wapi Mwalimu alificha pesa; je alifanya hivyo?! Yaani unashindwa kufahamu kwamba zilikuwa ni siasa tu zile?! Hivi kabisa kwa maisha yale wanayoishi familia ya Mwalimu bado unaamini alichokuwa amesema Kambona?!
 
Baada ya Kambona kuwajaza watu kwamba atataja wapi Mwalimu alificha pesa; je alifanya hivyo?! Yaani unashindwa kufahamu kwamba zilikuwa ni siasa tu zile?! Hivi kabisa kwa maisha yale wanayoishi familia ya Mwalimu bado unaamini alichokuwa amesema Kambona?!
Ha ha ha hakuna kiongozi wa hivyo Afrika...endelea kuamini hivyohivyo.
 
Mzee MS navutiwa sana na maandiko yako mbali mbali naomba uzidi kutuhabarisha mambo ya zamani kwa kadiri utakavyojaliwa
 
Ahsante Mwalimu wetu mzee MS ..simulizi yako imenipa picha kidogo kuhusu marehemu
 
Mkuu Oscar Kambona..alivyorudi kutoka UK,alitwambia pale Jangwani kuhusu Amir Jamal,JK Nyerere na Mfaume Kawawa ..
kwamba wana fedha nyingi nje ya nchi!..Huyu muhindi ndiye alitumiwa sana..
Akutukanaye hakuchagulii tusi. Pesa ya mwalimu Nyerere kama alikuwa nazo ughaibuni kwa nini isihudumie watoto na Mke wake? Huoni ulikuwa ni uzushi?
 
Ha ha ha hakuna kiongozi wa hivyo Afrika...endelea kuamini hivyohivyo.
Muhamakilo,
Unajua inawezekana kuwa mimi ndiyo mtu wa kwanza kuandika
maisha ya Nyerere katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Wakati wa utafiti na baada ya kutoka kitabu kile cha Abdul Sykes
watu wengi sana walinijia kwa mazungumzo ya kawaida tu na
baadhi ya watu hawa walikuwa na Mwalimu Nyerere kwa karibu
sana.

Wote wanasema Mwalimu Nyerere alikuwa na uadilifu wa hali ya juu
katika sauala fedha na hii toka enzi za TANU 1954.

Utajiri haukumshughulisha.
 
Mkuu Oscar Kambona..alivyorudi kutoka UK,alitwambia pale Jangwani kuhusu Amir Jamal,JK Nyerere na Mfaume Kawawa ..
kwamba wana fedha nyingi nje ya nchi!..Huyu muhindi ndiye alitumiwa sana..
Hivi wewe na wale si Mange kasema? Mna tofauti gani? Umesahau Kambona kwamba ni mwanasiasa?

Umesahau fix tuliyopigwa eti Kambona kashinda bahati nasibu ya dunia anarudi Tanzania na Land cruiser 300? Hivi unadhani ni kwa nini watu wengi walijiunga na Tadea?

Wabongo ni poor IQ hata kuutafuta ukweli ni shida Kambona amerudi Tanzania hana lolote na tumshukuru Mzee Mwinyi uchaguzi wa mwaka 1995 ruzuku kwa wagombea wa vyama vyote ngazi zote na mawakala wote pesa zilitolewa na serikali ya Mwinyi.

Ukiniuliza leo nitamkumbuka Mwinyi kwa lipi hakika kwa hili hata mimi kwa mara ya kwanza na ya mwisho nilikula pesa ya serikali burebure kabisa.

Uchaguzi ule ndio ulisababisha kuzaliwa vyama holela na wagombea holela wakidhani pesa za bure kama zile za mwaka 1995 zitarudi tena.

Mtu anachukuwa fomu kwenye chama kama cha Dovutwa kugombea ubunge serikali inampa ruzuku cash money millioni 5 mtu anatokomea hakuna cha kufanya kampeni wala nini.

Utaratibu ule ungeendelezwa hadi leo ingekuwa tuna vyama 1000 mpaka sasa.
 
Matola,
Hapana sijabebwa wala sikuwa karani nilikuwa ni ''officer.''

Nimeeleza vizuri vipi ilikuwa si jambo la kawaida kwangu mimi ''junior officer,''
kuingia bodi.

Wako waliokuwa wanabebwa lakini si Mohamed Said.
Lakini hapana haja ya haya hii ni taazia tunaomboleza tusilete mambo mengine.
Manshkhofu Sheikh wangu tusonge mbele.
 
Mkuu Oscar Kambona..alivyorudi kutoka UK,alitwambia pale Jangwani kuhusu Amir Jamal,JK Nyerere na Mfaume Kawawa ..
kwamba wana fedha nyingi nje ya nchi!..Huyu muhindi ndiye alitumiwa sana..
Narudia tena, hakuna , hakuna! aliyewahi kuthibitisha pesa za Kawawa, Nyerere au Amir Jamal nje ya nchi.

Kumsikia Kambona akisema hakufanyi kuwa ukweli
Nani alitegemea Kambona ataongea jambo zuri kuhusu Nyerere kwa ugomvi wao?

Hadi anafariki, hakuna aliyewahi kuthibitisha madai akiwemo Kambona mwenyewe

Vijana wa leo wanasikia tu na kuamini, walioishi zama hizo wanajua ukweli

Kuna Anour Kassum,alikuwa waziri na moja ya wizara alizodumu ni Madini na Nishati. Leo kama angekuwa sawa na 'fisi' tulio nao, tusingekuta hata mchanga wa kujaza katroli. Nani alikuwa na ufahamu wakati huo?

Tuwape heshima waliotumikia Taifa tukalikuta lilipo, tuache hadithi za kuzusha tu

JokaKuu
 
Narudia tena, hakuna , hakuna! aliyewahi kuthibitisha pesa za Kawawa, Nyerere au Amir Jamal nje ya nchi.

Kumsikia Kambona akisema hakufanyi kuwa ukweli
Nani alitegemea Kambona ataongea jambo zuri kuhusu Nyerere kwa ugomvi wao?

Hadi anafariki, hakuna aliyewahi kuthibitisha madai akiwemo Kambona mwenyewe

Vijana wa leo wanasikia tu na kuamini, walioishi zama hizo wanajua ukweli

Kuna Anour Kassum,alikuwa waziri na moja ya wizara alizodumu ni Madini na Nishati. Leo kama angekuwa sawa na 'fisi' tulio nao, tusingekuta hata mchanga wa kujaza katroli. Nani alikuwa na ufahamu wakati huo?

Tuwape heshima waliotumikia Taifa tukalikuta lilipo, tuache hadithi za kuzusha tu

JokaKuu
Nakumbuka sana zamani tuliaminishwa Saab Scania ni investment ya Nyerere pia.

I don't buy this nonsense.
 
Back
Top Bottom