Siku ambayo sitaisahau

Siku ambayo sitaisahau

Bianca joseph

Member
Joined
Jan 20, 2015
Posts
35
Reaction score
25
Ilikuwa ni siku ya Alhamisi, mpenzi wangu alinipia simu kwamba anahitaji tuonane. Kwa kweli alinishtua sana, nilijua labda amepatwa na tatizo. Nilipofika kwake aliniambia kwamba anahitaji kutoka na mimi kwenye sikukuu ya pasaka. Kwasababu ya upendo wangu kwake nilimkubalia ombi lake.

Ilipofika siku ya Jumapili asubuhi alinipigia simu kwamba anajisikia vibaya (anaumwa), kwahiyo hawezi kwenda sehemu yoyote siku hiyo. Kwa kweli nilimuhurumia sana, nakumuahidi nitaenda kumuona siku hiyo. Japo kuwa alinikatalia kwenda kumuona, sikukata tamaa jioni nilienda kumuona, cha kushangaza sikumkuta na mlango ulikuwa umefungwa.

Nikaanza kuwauliza majirani zake, walinijibu kwamba aliwaaga anakuja kwangu, nilipojaribu kupigia simu hakupatikana. Nikaamua kurudi nyumbani, wakati nipo njiani nikapigiwa simu na rafiki yangu kwamba amemuona mpenzi wangu akiwa na msichana mwingine wakiwa kwenye Bar fulani.

Nikachukua bodaboda hadi eneo husika na nilichokishuhudia ni Mungu mwenyewe anajua. Jamani nimevurugwa sana. Nilikuwa nahitaji marafiki wa kunifariji. Sichagui Dini, kabila wala jinsia. Wote kwangu ni marafiki tu.
 
Pole mayo...

Uamuz ni wako EITHER kumfikiria mpenz wako na kuumia AU kumshukuru Mungu kwa kukuonesha tabia ya mpenzi wako na kuendelea na maisha kama kawaida....

Think positive#
 
Ilikuwa ni siku ya alhamisi, mpenzi wangu alinipia simu kwamba anaitaji tuonane. Kwa kweli alinishtua sana, nilijua labda amepatwa na tatizo. Nilipofika kwake aliniambia kwamba anaitaji kutoka na mimi kwenye sikukuu ya pasaka. Kwa7bu ya upendo wangu kwake nilimkubalia ombi lake. Ilipofika siku ya jumapili asubuhi alinipigia simu kwamba anajisikia vibaya (anaumwa), kwahiyo hawezi kwenda sehemu yoyote siku hiyo. Kwa kweli nilimuhurumia sana, nakumuahidi nitaenda kumuona siku hiyo. Japo kuwa alinikatalia kwenda kumuona, sikukata tamaa jioni nilienda kumuona, cha kushangaza sikumkuta na mlango ulikuwa umefungwa. Nikaanza kuwauliza majirani zake, walinijibu kwamba aliwahaga anakuja kwangu, nalipojaribu kupigia simu hakupatikana. Nikaamua kurudi nyumbani, wakat nipo njiani nikapigiwa simu na rafiki yangu kwamba amemuona mpenzi wangu akiwa na msichana mwingine wakiwa kwenye Bar fulani. Nakachukua bodaboda hadi eneo husika na nilichokishuhudia ni Mungu mwenyewe anajua . Jamani nimevurugwa sana. Nilikuwa naitaji marafiki wa kunifariji. Sichagui Dini, kabila wala jinsia. Wote kwangu ni marafiki tu.

Ulichokikuta....... Hapo umeacha doti doti nyingi mkuu,hebu jazia nyama uzi wako, nini haswa ulicho kiona
 
Mbona hii kawaida sana bi dada? Halafu una bahati umegundua mapema, ni rahisi kwako kuchukua hatua! Kuliko ingetokea hivyo upo ndani ya ndoa!! Nahisi ungeumia zaidi!
 
Tuliza mtima kwanza,husikimbilia kutafuta marafiki kwa haraka utazidi kuumia zaidi,jifariji mwenyewe kwanza..
 
Huu mtego ni wakung'olea vijana wa JF?umeshawapata ila lazima utaombwa kipochi
 
Pole sana usikate tamaa hivyo usieke furaha yako juu ya watu au mtu maana utaumizwa tu
 
Hahahah! Manufaa ya michepuko huja siku kama hizi za disappointments !!!
 
Nawashukuru sana kwa wale wote walionipa ushauri na wale walionipa pole.
 
Inauma,but good thing about maumivu hukufanya uwe imara zaidi. Pole,and take it easy
 
Back
Top Bottom